Thursday 28 May 2020

Riwaya Kali ya Kusisimua....SIN- Sehemu Ya Tano (05)

...
Mwandishi- EDDAZARIA G.MSULWA
Age-18+
Simu-0657072588(whatsapp) au 0768516188


ILIPOISHIA
“Kwa nini kaka?”
“Kuna watu wana wateka watu na wanavishwa jina.... Yaani nashindwa hata kuelewa, tunaelekea wapi?”
“Nani mwengine ametekwa?”
“Si yule nabii Sanga wa kanisa la Heaven light ministry”
Mapigo ya moyo wa Magreth, yakasimama kwa sekunde kadhaa, kisha yakaanza kumuenda kasi, mwili mzima ukaanza kumtetemeka na jasho likimtiririka usoni mwake, hadi muendesha bajaji akabaki akiwa ameshikwa na butwaa kwa nini hali ya abiria wake imebadilika gafla mara ya kusikia taarifa hiyo.


ENDELEA   
“Dada upo salama?”
Dereva wa bajaji aliuliza huku akimtazama Magreth kwa macho ya kuiba iba kwani anahitajika kuwa makini katika barabara hiyo yenye magari mengi sana.
“Dada”
“Beee”
“Upo salama?”
“Umesema wamemteka nani?”
“Nabii Sanga, “
“Wamemuaa?”
“Hapana, hakuna taarifa kama hiyo, ila polisi wana dai kwamba gari lake kwenye kioo cha mbele kilipigwa kwa risasi moja”
Magreth akazidi kutetemeka kwa woga huku hali ya kukata tamaa ikiendelea kumtawala. Akataka kupiga namba ya nabii Sanga na kujikuta nafsi yake ikiendelea kusita na kushindwa kabisa kufanya hivyo. Akafikishwa hospitalini, akamlipa muendesha bajaji kiasi cha pesa anacho kihitaji, kisha akashuka kwenye bajaji hiyo, huku mwili mzima ukiwa umeishiwa na nguvu. Akaanza kutembea kwa mwendo wa taratibu, huku akihisi kukata tamaa, ndoto zake zote ambazo kwa siku hiyo zilikuwa zinakwenda kutimia, zote zimepotea. Akaingia ndani ya chumba alicho lazwa Evans. Wakatazamana na Evans kwa sekunde kadhaa kisha akaanza kuangua kilio kizito, kilicho mfanya Evans kushangazwa.
“Hei Mage kwa nini unalia?”
“Mchungaji?”
“Mchungaji amefanya nini?”
“Ametekwa na watu wasio julikana”
Habari hii hakika haikuwa nzuri kwa Evans.
“Mchungaji gani lakini, au yule uliye kuja naye hapa jana usiku?”
“Huyo huyo, ohoo Mungu wangu. Ni kina nani wamemfanyia mambo hayo jamani”
Magreth alizungumza huku akiendelea kulia kwa uchungu sana, hadi ikamlazimu, Evans kuanza kumbembeleza.
                                                                                                                                ***
    Majira ya saa mbili asubuhi, watekaji wawili wakaingia kwenye chumba walicho muhifadhi nabii Sanga. Wakamfungua kamba walizo mfunga na kumkalisha kwenye kiti. Wakamfungua kitambaa usoni mwake. Nabii Sanga akakutana na wanaume hao ambao wameendelea kufunika sura zao. Mbele yake kuna meza iliyo wekwa kikombe cha chai ya maziwa pamoja na vipande vinne vya mkate ulio pakwa blueband vizuri.
“Pata kifungua kinywa”
Mtekaji mmoja alizungumza huku mkononi mwake akiwa na bastola.
“Vijana, ninaomba tuweze kuzungumza. Kama ni pesa ambayo mumelipwa kwa ajili ya kuniteka. Tafadhali, nipo tayari kuhakikisha kwamba nina walipa mara mbili ya pesa hiyo ambayo mume pangiwa kunilipa”
“Mzee acha siasa, unahitaji kula au unahitaji kufa?”
Mtekaji wa pili alizungumza kwa ukali sana, mwezake akamnyooshea mkono kwa ishara ya kumuomba aweze kutulia.
“Una weza kutupatia ofa gani?”
“Mkuu unakosea?”
“Hapa, tuna fanya kazi hii kwa pesa. Upo tayari kutupa ofa gani?”
Mtekaji huyo alizugumza huku akisimama mbele ya nabii Sanga.
“Semeni aliye wapa hii kazi amewalipa kiasi gani?”
“Milioni ishirini”
“Nipo tayari kuwapa milioni hamsini by cash”
“By cash, unazo hapo ili uweze kutupatia?”
“Mukikubali na mukiniamini basi nita hakikisha kwamba nina wapatia hicho kiasi. Ila kabla sijafanya hivyo, nina waomba muweze kunisaidia jambo moja”
“Jambo gani?”
“Ninahitaji kumfahamu mtu aliye weza kutoa kazi hii”
“Siku zote huwa tuna linda siri za wateja wetu. Hatuto weza kukuambia ni nani ambaye ametupatia kazi hiyo.”
“Milioni sabini nawapatia”
“Hatuwezi kutoa siri”
“Milioni themani”
“Mzee hatuto weza kukuambia siri kwa ajili ya pesa”
“Milioni mia moja cashe munazipata katika siku hii hii ya leo”
Watekaji hawa wakatazamana usoni. Hapakuwa na kazi kubwa walio ifanya kwenye maisha yao, ambayo walihi kulipwa milioni mia moja. Uchu wa pesa ukawajaa mioyoni mwao, wakavutana pembeni ya chumba hicho na kuanza kunong’onezana.
“Mkuu tukubali hiyo ofa, milioni mia moja ni kubwa sana”
“Kawaite wezako”
“Sawa”
Mtekaji huyo akatoka na baada ya dakika moja akarudi akiwa ameongozana na wezake ambao nao sura zao wamezifunika. Mkuu wao akawaeleza ofa iliyo wekwa mezani na nabii Sanga.
“Mkuu ni pesa nyingi, kama ana uhakika wa kutupatia hicho kiasi hakuna haja ya sisi kuendelea kumshikilia. Yaani hapo ni sawa una ambiwa uchague Vitz na Hammer”
Hapakuwa na mtekaji yoyote ambaye aliweza kukataa ofa hiyo.
“Natambua kwamba muna fanya kazi hii kwa ajili ya kukidhi mahitaji ya maisha yenu, ikiwemo familia zenu. Nipo tayari kuwalipa kiasi hicho cha pesa na nyinyi mkawa ni watu wa mkono wangu wa kushoto”
Nabii Sanga aliendelea kuwashawishi watekaji hawa.
“Una maanisha nini kusema tuwe watu wa mkono wako wa kushoto?”
“Haya ni maisha, kesho na kesho kutwa nami nitakuwa na kazi ya kuwapatia, je mtashindwa kuifanya?”
Watekaji hawa wakatazamana huku sura zao wakiwa wamezifunika na kubakisha macho tu.
“Tutafanya”
“Basi kwa leo nipatieni hiyo nafasi ya kuwalipa na muweze kuniambia ni nani ambaye ameifanya kazi hiyo.”
Ushawishi wa nabii Sanga ukazidi kuwapagawisha watekaji hawa.
“Sawa tupo tayari ila kwa sharti moja”
“Niambieni”
“Pesa tuna ihitaji iweze kuletwa hapa”
“Ndio iletwe hapa, hatuwezi kurudi mjini. Polisi wapo makini kukutafuta nchi nzima. Changanua akili yako kisha hakikisha kwamba hiyo pesa ina letwa hapa na huyo atakaye ileta hapa awe ni mtu ambaye una muamini na asije akafanya kosa lolote la kipumbavu, kuwaeleza polisi. Akifanya hivyo nina apia kwa MUNGU. Nitakuchinja kama kuku”
Mkuu wa kikosi hicho cha watekaji alizungumza huku akimtazama nabii Sanga usoni mwake. Nabii Sanga akaanza kuchanganua akilini mwake ni nani ambaye ata muamini. Akili ikatua kwa mke wake, ila akajikuta akipata ukinzani mkubwa sana moyoni mwake.
‘Kwa nini nafsi yangu ina kataa kwa mke wangu. Kuna nini?’
Nabii Sanga alizungumza kimoo moyo huku akiendelea kutafuta ni nani ambaye anaweza kumuamini na kumkabidhi kazi hiyo. Akafikiria baadhi ya wachungaji wa kanisani kwake, ila hapo napo hakuweza kupata mtu wa uhakika wa kuwaamini.
“Mzee una dakika moja ya kutujulisha ni nani utakaye muamini”
Mtekaji huyo alizungumza na kumfanya nabii Sanga kuongeza umakini wa kuwachanganua watu wake wa karibu na kujua ni nani anaweza kuwaamini. Akili ikaangukia kwa Magreth, mwanamke aliye tokea kumpenda na kumjali kwa kipindi cha hivi karibuni. Moyo wake katika kumuamini Magreth haukuwa na wasiwasi hata kidogo.
“Nimempata”
“Nani?”
“Ahaa ni muumini wangu wa karibu ana itwa Magreth”
“Muumini, hato weza kutoboa siri kwa askari?”
“Hapana. Nina muamini sana.”
Watekaji hawa wakatazamana kisha mkuu wao akamsogelea nabii Sanga. Akamtazama machoni mwake kwa sekunde kadhaa kisha akatoa simu yake na kuiweka mezani.
“Endapo utafanya kosa lolote, nitakufumua ubongo wako. Mpigie na uweke loud speaker”
“Sawa sawa”
Nabii Sanga akaichukua simu hiyo, akafumba macho yake kwa sekunde kadhaa, huku akijaribu kuikumbuka namba ya Magreth na kwa bahati nzuri akafanikiwa kuikumbuka, akaiingiza katika simu hiyo kisha akaipiga na kwa bahati nzuri akakuta ina patikana hewani.
                                ***
    Mlio wa taratibu unao ita katika simu yake, ukamfanya Magreth kuitazama simu yake. Evans aliye lala pembeni yake, naye akamtazama Magreth kwa sekunde kadhaa anaye endelea kuitazama simu yake inayo ita.
“Mbona hupokei simu?”
“Hii namba yangu ni mpya na hakuna mtu yoyote anye ifahamu”
“Mmmm sasa inakuwaje watu wameifahamu?”
Evans aliuliza, taratibu Magreth akaipokea simu hiyo na kuiweka sikioni mwake.
“Haloo”
Magreth alizungumza kwa umakini sana huku akisubiria kusikilizia ni nani huyo aliye mpigia.
“Ni mimi Magreth, usijaribu kutaja jina langu wala kuonyesha dalili yoyote ya kuweza kunifahamu, kwa maana nina hisi upo na watu”
Sauti ya nabii Sanga ikamfanya Magreth macho kumtoka. Akasimama huku akiwa amejawa na tabasamu.
“Nisikilize kwa umakini mkubwa sana, kwanza upo wapi?”
“Hospitali”
“Simama sehemu ambayo hakuna mtu anaye weza kusikiliza mazungumzo yetu”
Magreth kwa haraka akatoka ndani humo pasipo hata kumuaga Evans. Akatafuta eneo lisilo na mtu na akasimama.
“Unaweza kuendelea”
“Nipo chini ya watekaji, wanahitaji kiasi cha milioni mia moja.”
“Mungu wangu!!”
“Nisikilize, wewe ndio mtu wa pekee ambaye ninakuamini na unaye weza kunisaidia mimi kutoka katika kifungo hichi”
Nabii Sanga alizungumza kwa msisitizo mkubwa sana.
“Ehee”
“Nenda pale kanisani, password ya mlango wa ofisini kwangu ni tisa, moja, moja tisa moja, sifuri. Fungua mlango wa ofisini kwangu, kuna shelf kubwa imo mule ofisini, fungua hiyo shelf kwa kutumia password hizo hizo nilizo kutajia. Kuna pesa za kimarekani. Chukua dola alfu sitini, weka kwenye begi, ukifanikisha kufanya hivyo hakikisha kwamba una piga namba hii, kwa ajili ya maelekezo zaidi. Ninakuomba Magreth usimuambie mtu wa aina yoyote. Ukifungua kinywa chako, basi tambua mimi huku nina kufa”
Magreth mwili mzima ukamtetemeka, akashusha pumzi huku akifikiria ni wapi anapo weza kuanzia.
“Baba mchungaji lakini upo salama”
“Ndio yupo salama na endapo utafungua kinywa chako kwa askari. Tutamuua na wewe tutakutafuta na kukuua”
Sauti hiyo nzito ya mwanaume, ikamstua sana Magreth. Mwili mzima ukazidi kutawaliwa kwa woga. Simu ikakatwa na kumfanya aishiwe hata nguvu za kusimama. Akakaa chini kwa sekunde kadhaa huku akitafakari ni wapi kwa kuanzia.
‘Lazima nimsaidie, ndio lazima nimsaidie’
Magreth alizungumza kimoyo moyo huku akinyanyuka eneo hilo. Wazo la kurudi chumbabini kwa Evans wala hakuweza kuwa nalo kabisa. Akakodisha pikipiki na akarudi nyumbani kwake, akatoa nguo zilizomo kwenye begi lake la mgongoni. Alipo hakikisha begi hilo halina nguo akalivaa na kutoka ndani humu. Akapanda pikipiki nyingine na kufikishwa kanisani. Kutokana mlinzi wa kanisa hilo wana fahamiana, hapakuwa na tatizo la yeye kufunguliwa geti.
“Mage una habari yoyote ya kupatikana kwa nabii?”
Mlinzi aliuliza huku akiwa amejawa na unyonge mkubwa sana.
“Hapana kaka. Nimekuja kumuomba MUNGU japo aweze kulete rehema yake”
“Sawa Mage ila huko hakuna mtu yoyote”
“Hakuna shaka”
Magreth akamuongopea mlinzi huyo. Akaingia kwa mlango wa mbele wa kanisa hilo, ili kumdanganya mlinzi asiweze kufahamu kwamba lengo na nia iliyo mleta hapo kanisani ni kuingia katika ofisi ya nabii Sanga. Magreth akatoke katika mlango mwingine wa kanisa hilo na kuelekea ilipo ofisi ya mchungaji. Akasimama mlangoni hapo na kuchunguza eneo hilo kwa umakini. Alipo hakikisha hakuna mtu wa aina yoyote akaingiza namba hizo za siri alizo tajiwa na mchungaji. Mlango ukafunguka na kuzama ndani na huku nyuma mlango ukajifunga.
Magreth akaanza kuangaza macho yake huku na huku na kufanikiwa kuona shelf kubwa iliyomo ofisini hapo, akaisogelea na akaingiza namba hizo za siri. Mlango mzito wa shelf hiyo ukafunguka. Magreth macho yakamtoka mara baada ya kukuta vibunda vya pesa za kimarekani(USD DOLLARS) vikiwa vimepangwa vizuri. Akaanza kuvihesabu kwa haraka haraka. Alipo hakikisha kwamba ni dola elfu stini, akaziingiza kwenye begi lake na kulivaa mgongoni. Akaanza kutembea kuelekea mlangoni, ila kabla hajaufungua mlango, akasikia hatua za miguu ya watu zikija katika mlango huo. Akatazama eneo hilo na kwa haraka akakimbilia kwenye moja ya sofa iliyomo ndani humo. Akajificha nyuma ya sofa ambapo sio rahisi kwa mtu kuweza kumuona.
“Yaani mpenzi wangu, nimewakimbia maaskari nyumbani kwa ajili yako. Nimeona tusikutanie kwako kwa maana una weza kufaatiliwa na ukakamatwa bure”
Sauti ya mama chungaji ikamstua sana Magreth aliye jibanza nyuma ya sofa hilo.
“Usijali mpenzi wangu, acha nikupe chap chap tuondoke kwa maana nina hamu na wewe sasa”
Sauti ya Tomas haikuwa ngeni kabisa masikoni mwa Magreth, kwani mtu huyo ni jana tu ametoka kuonana naye uso kwa uso.
“Ila vijana wako walio mteka huyo mpuuzi, una waamini au ni watu wa ajabu ajabu?”
Magreth akazidi kujawa na mshangao ulio sababisha mapigo yake ya moyo kuanza kumuenda kasi sana. Siri ya Mrs Sanga na Tomas, imevuja masikioni mwake.
“Nina waamini sana, tena hakuna ambaye ana weza kuenenda kinyume na mimi. Unacho paswa ni wewe kunipatia milioni arobaini za kuwalipa tu”
“Usijali pesa sio tatizo kwangu, jambo la msingi ni kuhakikisha kwamba wana mshikilia hadi wiki ijayo, na akiondoka kuelekea nchini Nigeria, yule kimada wake aliye panga kumnunulia nyumba na kumfungulia mgahawa nitamuua kwa mikono yangu mimi mwenyewe.”
Maneno hayo ya Mrs Sanga yakamfanya Magreth kuhisi haja ndogo ikianza kumtoka. Kama mwana mama huyo amefanya maamuzi ya kumteka mume wake bila ya huruma na yeye ndio anaye faatia kuuwawa, je itakuwaje endapo wata muona nyuma ya sofa hilo.
                                                                                                   ITAENDELEA
Haya sasa Magreth ametambua siri ambayo hakuna mtu mwingine ameweza kuifahamu huku akiwa na mzigo mkubwa sana wa kumsaidia nabii Sanga.Je ataweza kumsaidia nabii huyo?. Nini kitatokea? Endelea kufatilia kisa hiki cha kusisimua, usikose sehemu ya 06

 


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger