Leo Asubuhi Jumatano April 22, 2020 Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema, hadi jana Aprili 21, 2020 jumla ya Wagonjwa 284 wamethibitika kuwa na Virusi vya Corona. Wagonjwa 256 wanaendelea vizuri, 7 wako kwenye uangalizi maalum, 11 wamepona na 10 wamefariki.
Kutokana na taarifa hiyo wa Waziri Mkuu, Waziri wa Afya Ummy Mwalimu kupitia ukurasa wake wa Twitter ametoa mchanganuo wa Ongezeko hilo la Wagonjwa kimkoa.
Ameandika;Jumla ya watu waliopata maambukizi ya #COVID19 nchini sasa ni 284 kutoka 254 tuliowatolea Taarifa tar 20 April 2020. Mchanganuo wa wagonjwa wapya 30 ni kama ifuatavyo: Dar es salaam (10), Zanzibar (9), Mwanza (4), Pwani (2), Kagera (1), Dodoma (2), Manyara (1) na Morogoro (1)


0 comments:
Post a Comment