Wednesday, 16 October 2019

Malawi Yakanusha Kuwa Na Mgonjwa Wa Ebola

...
Malawi imekanusha ripoti zilizoenea kwamba mtu mmoja amegunduliwa kuwa na Ebola kwenye eneo la Karonga linalopakana na Tanzania.

Hofu hiyo ilitokea Jumapili wakati wafanyakazi wa afya kwenye eneo hilo waligundua mwanamume mwenye umri wa miaka 37 kuwa na dalili za Ebola.

Afisa wa afya katika eneo hilo,  Louis Tukula amesema mtu huyo alikuwa na maambukizi ya bakteria na si Ebola.

Amesema eneo hilo limekuwa katika hali ya tahadhari tokea ugonjwa wa Ebola uripotiwe katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger