Monday, 19 August 2019

Waliofariki Ajali ya Lori la Mafuta Morogoro Wafika 97

...
Idadi ya waliofariki katika ajali ya Lori iliyotokea mkoani Morogoro imezidi kuongezeka na kufikia 97 baada ya majeruhi wawili kati ya 20 waliokuwa wamelazwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), Dar es Salaam kufarikii dunia.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano MNH, Aminiel Aligaesha amesema majeruhi waliobaki hospitalini hapo ni 18 ambao wote wapo kwenye chumba cha uangalizi maalum (ICU).

Amewataja waliofariki ni Rosijo Mollel (35) aliyefariki jana Jumapili mchana na Neema Chakachaka ambaye amefariki alfajiri ya leo Jumatatu.


Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger