Monday, 19 August 2019

Mwandishi Erick Kabendera Arudishwa Rumande Hadi Agosti 30

...
Wakili Mwandamizi wa Serikali, Wankyo Simon ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa upelelezi wa kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili Mwandishi wa Kujitegemea wa Habari za uchunguzi, Erick Kabendera bado haujakamilika.

Simon ameeleza hayo leo Jumatatu Agosti 19, 2019 mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Agustina Mmbando

Mbali na upelelezi kutokamilika, Pia, hakimu anayesikiliza kesi hiyo, Augustine Rwizile amepata udhuru.

Kabendera anashtakiwa kwa Makosa matatu ikiwemo kukwepa Kodi kiasi cha Tsh. Milioni 173,247,047.02, Utakatishaji Fedha na kujihusisha na genge la uhalifu Makosa ambayo  hayana dhamana
 
Kesi imeahirishwa hadi Agosti 30, 2019 itakapotajwa tena.


Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger