Tuesday, 13 August 2019

Acacia yaruhusiwa kuendelea kusafirisha Dhahabu kutoka mgodi wa North Mara

...
Kampuni ya Acacia imeruhusiwa kuendelea na utaratibu wa kusafirisha dhahabu baada ya kuzuiliwa kwa takribani mwezi mmoja na Tume ya Madini Tanzania

Taarifa iliyotolewa na Acacia inaeleza sasa wataanza kusafirisha madini kutoka North Mara baada ya kutimiza masharti

Hata hivyo, Tume ya Madini imesema inaamini baadhi ya vipengele vya kanuni ya madini ya mwaka 2010 vilikiukwa na imewataka kuwasilisha mpango wa uchimbaji na ripoti ya upembuzi yakinifu ifikapo Ijumaa ya wiki hii

Acacia imekuwa kwenye mvutano wa muda mrefu na Serikali baada ya kuzuiwa kusafirisha Makinikia nje ya nchi kwa madai ya kutolipa mrabaha stahiki


Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger