Wednesday 31 July 2019

MKUU WA WILAYA YA MISSENYI KANALI MWILA AONYA WANANCHI KUHIFADHI WAHAMIAJIA HARAMU

...
Mkuu wa wilaya ya Missenyi Kanali Denice Mwila  

Na Lydia Lugakila - Malunde1 blog Bukoba
Mkuu wa wilaya ya Missenyi  mkoani Kagera Kanali Denice Mwila  amewataka wananchi wilayani Missenyi kuacha tabia za kuwapokea na kuwahifadhi wahamiaji haramu kutoka nchi jirani kwani tabia hizo zinaweza kuhatarisha usalama wa nchi.


Akizungumza na Malunde 1 blog leo Julai 31,2019 Kanali Mwila ametoa amesema vitendo hivyo vimekuwa vikisababisha wahamiaji haramu kuongezeka wilayani missenyi mkoani hapa  hivyo kupelekea watanzania kukosa ardhi ya kulima na kufanya shughuli za ufugaji.

Kanali Mwila amewataka Watanzania katika maeneo ya mipakani hususani kata za Mtukula,Kakunyu na Minziro waepuke kupokea rushwa kutoka kwa wahamiaji ili wawape hifadhi.

Ameonya kuwa serikali wilayani humo haitawafumbia macho wananchi watakaobainika kujihusisha na vitendo hivyo.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger