Friday, 14 June 2019

KIGOGO WA CHADEMA AUAWA MOROGORO

...
Uongozi wa Chadema mkoa wa Morogoro umeeleza kusikitishwa na kifo cha katibu mwenezi wa jimbo la Malinyi, Lucas Lihambalimu baada ya kudaiwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana nyumbani usiku wa manane.

Akizungumza na Mwananchi jana, katibu wa Chadema mkoa wa Morogoro, Barnabas Okola alisema kwa mujibu wa taarifa walizopata watu wasiojulikana walifika nyumbani kwa Lucas saa 8:00 usiku na kumgongea.

Okola alisema alipofungua mlango ghafla alipigwa na kushambuliwa na watu hao kwa kumpiga risasi shingoni.

“Kihistoria Lucas hakuwa na ugomvi na mtu au watu alikuwa mpole na mchapa kazi ndani ya chama, tuliposikia ameuawa kila mtu alipigwa butwaa,” alisema.

Via Mwananchi
Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger