Friday 28 June 2019

ATCL yazindua safari za Tanzania kwenda Afrika Kusini

...
Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), leo limeanza rasmi safari yake ya kwanza kuelekea Johannesburg, Afrika Kusini kwa kutumia ndege aina ya Airbus. 

Mkurugenzi wa Shirika hilo Mhandisi Ladslaus Matindi amesema kwa wiki kutakuwa na safari nne. 

Ndege hiyo  aina ya Airbus 220-300 imeondoka Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam Tanzania (JNIA)  saa 4:30 asubuhi ikitarajia kutua katika Uwanja wa Kimataifa wa OR Tambo, Afrika Kusini saa 6:45 mchana.


Share:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger