Saturday, 4 May 2019

MAITI YACHOMOKA KWENYE JENEZA WAKATI WA MAZISHI

...
Familia chini Ghana huwapa mkono wa buriani wapendwa wao waliofariki dunia kwa mtindo wa aina yake huku wengi wao hata wakiwaajiri kwa muda wasakata densi kushiriki majira ya mwisho ya kumpa buriani marehemu.

 Mtindo huu wa kuwaajiri watakaolibeba sanduku la maiti huku wakisakata densi kwa nyimbo umeonekana kushika kasi mno na ni bayana kuwa utakuwepo kwa muda mrefu zaidi. 

Hata hivyo, kwenye tukio moja mambo yameonekana kwenda mrama katika hafla ya mazishi.

 Katika video moja iliyosambaa kwa kasi mitandaoni, jamaa wa marehemu wameachwa na mshtuko baada ya maiti ya mpendwa wao kuteleza na kuanguka kutoka katika sanduku lililombeba.

 Hii ni baada ya wanadensi waliokuwa wamelibeba sanduku hilo kupoteza mwelekeo wakila uhondo na kupelekea maiti kuchomoka kwa bahati mbaya na kuanguka. 

Familia ya mwendazake na waombolezaji walisika wakimaka kwa mshangao kufuatia kihoja hicho huku jamaa hao wakiwa katika harakati ya kuufunika mwili wa marehemu.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger