Wednesday, 10 April 2019

Rais Magufuli Aibua Kashfa ya Stampu Hewa za Bilioni 10 TRA

...
Rais Magufuli amesema Wahujumu uchumi wamewahi kushirikiana na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kutengeneza stampu hewa za Bilioni 10.

Amesema stampu hizo baada ya kutengenezwa zilisambazwa katika viwanda nchini kupitia ushirikiano wa baadhi ya wafanyakazi wa TRA.

Kauli hiyo ameitoa jana Jumanne Aprili 9, 2019 akifungua kiwanda cha majani ya Chai katika kijiji cha Kabambe mkoani Njombe, ikiwa ni sehemu ya ziara yake kwenye mikoa mbalimbali nchini.


“Kwenye suala hili la kodi hasa kwenye vinywaji kama vile bia, konyagi na spirit (vinywaji vikali) nyingine hili kidogo ni very complex (linachanganya) ndio maana Mwenyekiti hakuzungumza tulikuwa tunakusanya kiasi gani, angezungumza hilo tungekuwa tunagonga stampu tungekuwa tunakusanya ngapi, tungepata jibu vizuri.

“Hatukusanyi kitu katika eneo ambalo tumepigwa sana ni hilo la vinywaji, kwa hiyo Serikali inakosa pesa hakuna mahali tulipata pesa, lazima sasa tutafute utaratibu mzuri ili hawa wenye viwanda vya vinywaji tusipoteze pesa zaidi” Alisema Rais Magufuli


Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger