Saturday, 13 April 2019

ANUSURIKA KUFA BAADA YA KUDUNGWA VISU MARA 17 NA MMEWE

...

 Mwanamke aitwaye Peninnah Wangechi mwenye umri wa miaka 30 anauguza majeraha mabaya aliyoyapata baada ya mume wake kumvamia na kumdunga visu mara 17  kisha kutoroka baada ya kuufanya unyama huo.

 Mama huyo wa watoto watatu alipata majeraha mgongoni, usoni na kifuani.

 Peninnah Wangeci ambaye amelazwa katika hospitali ya Kaunti ndogo ya Karatina alinusurika kifo baada ya kudungwa kisu mara kumi na saba kufuatia mgogoro wa kinyumbani.

Kwa mujibu wa Citizen Digital, kisa hicho kilitokea Jumanne, Aprili 9,2019 ambapo mumewe, Samuel Ndirangu alimtishia kabla ya kumtendea unyama huo na kisha kutoroka. 

Wangeci, alisema ndoa yake imekuwa ikikabiliwa na migogoro ya mara kwa mara na kwamba siku hiyo haikuwa ya kwanza kwa mumewe kumtishia.

Mkurugenzi wa hospitali hiyo Benson Ngari alisema, mgonjwa yupo katika hali nzuri ijapokuwa alipoteza damu nyingi.

Chanzo - Tuko
Share:

Related Posts:

0 comments:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © 2025 MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger