Wednesday, 25 February 2026

PROF. SHEMDOE AONGOZA UJUMBE KUMWAKILISHA RAIS SAMIA MKUTANO WA KILIMO, ARDHI NA MAENDELEO VIJIJINI, COLOMBIA


Na OWM - TAMISEMI, Colombia

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu -TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa nchi zinazoshughulika  na masuala Kilimo, Ardhi na Maendeleo vijijini,  ulioanza  Februari 24, 2026 nchini Colombia kwenye jiji la Cartegina.

Prof. Shemdoe amemuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mkutano huo, baada ya Mhe. Rais kupokea mwaliko wa kuudhuria mkutano huo kutoka kwa Rais Gustavo Petro Urrego wa Colombia. 

Lengo kuu la mkutano huo uliohudhuriwa na nchi zaidi 100 duniani, ni kutoka na mwafaka wa namna gani matumizi bora ya ardhi katika kilimo yanaweza kupunguza migogoro ya ardhi na kuharakisha maendeleo vijijini.

Aidha nchi hizo zaidi ya 100 zilizoshiriki mkutano huo, ambazo zinashughulika na masuala ya Kilimo, Ardhi na Maendeleo ya Vijijini, zimepata fursa ya kubadilishana uzoefu katika masuala ya kilimo, Ardhi na Maendeleo Vijijini pamoja na matumizi ya teknolojia katika shughuli hizo, ambapo wananchi katika mataifa hayo watanufaika.

Katika Mkutano huo wa siku tano unaotarajiwa kufikia tamati Februari 28, 2026 Prof. Shemdoe ameambatana na Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. David Silinde, wataalam kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI na  Wizara ya Kilimo, lengo likiwa ni kutimiza ndoto za  Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuleta mapinduzi ya kilimo nchini ili kuwanufaisha watanzania na kuwapatia tabasamu la kudumu.

Share:

WANANCHI PERAMIHO , SHIWINGA KUPIGA KURA KESHO KUCHAGUA MBUNGE, DIWANI



Na Mwandishi wetu, Ruvuma

Wapiga Kura 127,632 walioandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura watashiriki katika uchaguzi wa kuchagua Mbunge katika Jimbo la Peramiho lililopo Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mkoa wa Ruvuma na Kata ya Shiwinga iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi Mkoa wa Songwe.

Mwenyekiti wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji wa Rufaa Mhe. Jacobs Mwambegele ameyasema hayo leo Februari 25, 2026 mjini Songea Mkoani Ruvuma wakati akisoma risala maalum kuhusu uchaguzi katika jimbo na kata husika utakao fanyika kesho Februari 26, 2026 na kusema kuwa jumla ya vituo 373 vya Kupigia Kura vitatumika.

“Kati yao wapiga kura 120,780 ni wa Jimbo la Peramiho na wapiga kura 6,852 wapo katika kata ya shiwinga na jumla ya vituo 373 vya Kupigia Kura vitatumika, ambapo vituo 354 vipo Jimbo la Peramiho na vituo 19 vipo katika Kata ya Shiwinga Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi,”amesema Jaji Mwambegele.

Aidha, amesema kwa uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Peramiho vyama vya siasa 15 vimesimamisha wagombea na kwa upande wa uchaguzi mdogo wa udiwani katika Kata ya Shiwinga vyama vya siasa nane (08) vimesimamisha wagombea.

“Natumia fursa hii kuvikumbusha Vyama vya Siasa vinavyoshiriki uchaguzi kesho Februari 26, 2026 kuzingatia wajibu wao wa kuweka mawakala katika vituo vyote vya zoezi la kupiga, kuhesabu na kujumlishia kura. Wasimamizi wa uchaguzi katika Jimbo na Kata husika, wamekamilisha taratibu zinazoweka mazingira yanayowawezesha mawakala wa vyama vya siasa kufuatilia mchakato mzima wa uchaguzi,”alisema Jaji Mwambegele.

Amesema, mawakala hao, wanawajibika katika kulinda maslahi ya vyama na wagombea wao. Hivyo, wanapaswa kuzingatia Sheria, Kanuni, taratibu za Uchaguzi na maelekezo ya Tume katika utekelezaji wa majukumu yao vituoni.

Jaji Mwambegele amesema vituo vitafunguliwa saa 01:00 asubuhi na kufungwa saa 10:00 jioni na kwamba ifikapo muda wa kufunga kituo saa 10:00 kamili jioni, kama wapiga kura bado wapo kwenye mistari, mlinzi wa kituo atasimama nyuma ya mtu wa mwisho na zoezi la upigaji kura litaendelea hadi wapiga kura walio kwenye mstari watakapomalizika.

“Baada ya kumaliza kupiga kura, mpiga kura anatakiwa kuondoka eneo la kituo cha kupigia kura; na Mpiga kura awapo kituoni, anatakiwa kufuata maelekezo yote atakayopewa na karani mwongozaji wapiga kura,”amesema Jaji Mwambegele.

Kwa mpiga kura ambaye ameandikishwa katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura na taarifa zake zipo katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura lililopo katika kituo husika, lakini amepoteza kadi yake au kadi yake imeharibika, ataruhusiwa kupiga Kura kwa kutumia moja wapo ya vitambulisho cha Taifa NIDA, Leseni ya udereva au Pasi ya kusafiria (Passport).




Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO FEBRUARI 25,2026



Magazeti




















Share:

Tuesday, 24 February 2026

DC ILALA AAHIDI KUSHIRIKIANA NA FCC KUDHIBITI BIDHAA BANDIA


Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo Akizungumza wakati wa semina ya wahariri iliyoandaliwa na FCC jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu - Dar es salaam.

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo, amesema ataimarisha ushirikiano kati ya ofisi yake na Tume ya Ushindani (FCC) katika mapambano dhidi ya bidhaa bandia na viwanda bubu ndani ya Jiji la Dar es Salaam. Amesema hatua kali zitachukuliwa kwa wote watakaobainika kuvuruga uchumi wa soko.

Amesema hayo wakati wa semina ya wahariri iliyoandaliwa na FCC jijini Dar es Salaam, akisisitiza kuwa ofisi yake kwa kushirikiana na halmashauri zote itaongeza udhibiti wa uzalishaji na biashara. Amesema lengo ni kuwabaini na kuwachukulia hatua wanaojihusisha na usambazaji wa bidhaa zisizo halali.

Amesema kumekuwepo na ongezeko la viwanda bubu vinavyozalisha bidhaa feki, hali inayochangia kuvuruga ushindani wa soko, kupunguza mapato ya Serikali na kuhatarisha afya za wananchi. Amesema Ilala ni lango la biashara, hivyo usimamizi wake unapaswa kuwa makini zaidi.

Aidha, amesema FCC inapaswa kuongeza idadi ya watumishi kutokana na majukumu yake kuwa makubwa, hususan katika mipaka na bandarini. Amesema kuongezeka kwa shehena katika Bandari ya Dar es Salaam kunahitaji nguvu kazi ya kutosha kudhibiti bidhaa zinazoingia nchini.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Khadija Ngasongwa, akizungumza na wahariri wakati wa semina ya wahariri



Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Khadija Ngasongwa, amesema taasisi hiyo inaendelea kutekeleza maono ya Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha mazingira ya ushindani na kuvutia wawekezaji. Amesema sheria ya ushindani ni kigezo muhimu kwa mwekezaji kabla ya kuamua kuwekeza.

Amesema semina hiyo imelenga kuwajengea uwezo wahariri kuhusu Sheria ya Ushindani ya mwaka 2003 na mabadiliko yanayotarajiwa kupelekwa bungeni. Amesema FCC haiko tayari kuona soko linapangwa kwa namna inayowaumiza wananchi.

Naye Mwakilishi wa Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Bakari Kimwanga, amesema ushirikiano kati ya FCC na wahariri ni muhimu katika kutoa elimu kwa umma. Amesema hatua hiyo itasaidia kulinda ushindani wa soko na maslahi ya watumiaji nchini.



Picha za matukio mbalimbali wakati wa semina ya wahariri iliyoandalia na Fcc.
Share:

Monday, 23 February 2026

MFANYABIASHARA ATOA SIRI YA KUREJESHEWA MALI YAKE ILIYOIBIWA NDANI YA SAA 24

Kwa miaka mingi, baba wa watoto watatu huko Kiambu, Kenya, aliishi katika nyumba iliyojaa mabishano yasiyoisha na mvutano wa kihisia. Kile kilichoanza kama kutokubaliana kidogo kati yake na mkewe kiliongezeka polepole na kuwa makabiliano ya kila siku. Watoto walinyamaza na kujitenga, mara nyingi wakirudi vyumbani mwao ili kuepuka kelele. Ukarimu ambao hapo awali uliwakilisha maisha ya familia yao ulitoweka polepole, na kubadilishwa na tuhuma, hasira, na ukimya baridi.

Anaelezea kwamba hata masuala madogo yangeibuka na kuwa migogoro mikubwa. Mawasiliano yalivunjika kabisa, na kila mazungumzo yalionekana kugeuka kuwa lawama na kuchanganyikiwa. Jamaa walijaribu kuingilia kati na kupatanisha amani, lakini utulivu ungedumu kwa siku chache tu kabla ya mzunguko wa migogoro kuanza tena. Msongo wa kifedha na shinikizo la nje vilifanya hali kuwa mbaya zaidi, lakini ndani kabisa, alihisi kulikuwa na kitu zaidi ya kutokubaliana kwa kawaida tu kulikoathiri nyumba yao.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU FEBRUARI 23,2026

Magazeti ya leo
 





Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger