Saturday, 6 June 2026

NEMC YAMTUZA JACKLINE KWA UFAFANUZI BORA WA UCHUMI MZUNGUKO


Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) limemtambua mwanafunzi wa Darasa la Sita, Jackline Eliabi wa Shule ya Msingi Manyinga, Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro, kwa uwasilishaji wake bora wa dhana ya Uchumi Mzunguko katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani.

Jackline alipata pongezi na kutunukiwa zawadi baada ya kuwasilisha kwa umahiri dhana hiyo muhimu inayohamasisha matumizi endelevu ya rasilimali, upunguzaji wa taka na uhifadhi wa mazingira.

Uwasilishaji wake ulionesha uelewa mkubwa wa masuala ya mazingira na mchango wa wanafunzi katika kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kutunza mazingira kwa maendeleo endelevu.

Zawadi hiyo ilitolewa na Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Dkt. Immaculate Sware Semesi, ikiwa ni kutambua mchango wa wanafunzi katika kusukuma gurudumu la uhifadhi na usimamizi wa mazingira nchini.

Dkt. Semesi alieleza kuwa wanafunzi ni wadau muhimu katika juhudi za kulinda mazingira na kwamba wao ndio mabalozi wa baadaye wa mazingira watakaosaidia kuendeleza agenda ya maendeleo endelevu kwa manufaa ya taifa na vizazi vijavyo.
Share:

Video Mpya : LUPEMBE LIMBU - NSIYA

 

Share:

MRADI WA VISIMA VYA GESI MNAZI BAY WAONGEZA UZALISHAJI, WANANCHI WANUFAIKA


Mradi wa uchorongaji wa visima vitatu vya gesi asilia unaoendelea katika Kitalu cha Mnazi Bay kilichopo Mkoani Mtwara umeleta manufaa makubwa kwa wananchi na Taifa kwa ujumla kufuatia utekelezaji wenye mafanikio.

Mradi huo unaohusisha uchorongaji wa visima viwili vya uzalishaji na kimoja cha utafutaji ulianza kutekelezwa Februari 06, 2026 ambapo hadi kufikia Juni 05, 2026, uchorongaji wa visima viwili vya uzalishaji vilivyopewa majina ya MB5 na MS2 ulikuwa umekamilika na uchorongaji wa kisima cha tatu kilichopewa jina la KASA-1X ulikuwa unaendelea.

Miongoni mwa manufaa yaliyopatikana kufuatia utekelezaji huo ni pamoja na kuongezeka kwa uzalishaji wa gesi asilia kutoka katika Kitalu cha Mnazi Bay ambapo kisima cha MB5 kimeongeza uzalishaji kwa wastani wa futi za ujazo milioni 40 kwa siku na kisima cha MS2 ambacho bado kinafanyiwa majaribio kinatarajiwa kuongeza ujazo mwingine zaidi wa uzalishaji wa gesi asilia.

Ongezeko hili la uzalishaji wa gesi asilia umewezesha uwepo wa gesi zaidi kwa matumizi ya uzalishaji umeme, viwandani, kwenye vyombo vya usafiri (magari na bajaji) na majumbani.

Kwa wananchi, mradi umeleta fursa za ajira na utoaji wa huduma na bidhaa zinazohitajika ambapo zaidi ya watanzania 320 wameajiriwa katika nafasi mbalimbali na kandarasi zanye thamani ya zaidi ya bilioni 20 za kitanzania zimeenda kwa watoa huduma wakitanzania.

Kwa upande wa uwekezaji, utekelezaji wa mradi huu pamoja na miradi mingine ya utafutaji wa mafuta na gesi asilia inayoendelea umeongeza imani kwa wawekezaji ndani na nje ya nchi kuhusu uhai wa sekta ndogo ya mafuta na gesi asilia nchini

Kukamilika kwa mradi huu wa uchorongaji wa visima vitatu kutaifanya Tanzania kuwa na idadi ya visima 99 vilivyochorongwa tangu kuanza kwa shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi asilia nchini kutoka visima 96 vilivyokuwepo awali.
Share:

SERIKALI KUENDELEA UBORESHA NA KUJENGA MIUNDOMBINU YA UVUVI






NA MWANDISHI WETU – SONGEA

Serikali inaendelea kuboresha na kujenga Miundombinu ya uvuvi ikiwemo masoko ,maghala ya kuhifadhia mazao ya uvuvi, vichanja vya kukaushia samaki maghala ya kuhifadhia mazao ya uvuvi na viwanda vya kuchakata mazao ya uvuvi na teknolojia rafiki za ukaushaji ili kubadilisha sekta hiyo kutoka ufugaji na ukulima mdogo kuelekea katika kuimarisha lishe na uchumi wa wakulima wadogo wanaojikita katika uzalishaji na ukuzaji wa viumbe maji nchini ambapo matokeo hayo yanatarajia kuchochea uchumi wa wananchi na taifa kwa ujumla.



Hayo yameelezwa na Bw. Jumanne Mwankoo Kaimu katibu Tawala Mkoa wa Ruvuma wakati wa tukio la kuhakiki taarifa ya matokeo ya mwisho ya mradi wa kuimarisha lishe kwa wakuzaji wadogo wa viumbe maji (ARNSA) uliokuwa ukiratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge Uratibu wenye Ulemavu kwa msaada wa Shirika la NORAD kupitia Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo Duniani IFAD tarehe 5 Juni 2026.Bw. Mwankoo alisema kuwa Mradi huo wa kikanda uliokuwa katika Nchi za Tanzania, Kenya na Msumbiji na kutekelezeka katika Mikoa ya Lindi Mtwara na Ruvuma nchini,



Ambao umetoa mchango mkubwa katika sekta ya uvuvi ambayo imechangia takribani asilimia 69% ya protini katika lishe bora, uzalishaji wa mazao ya viumbe maji sambamba na ongezeko la ajira kwa vijana na wanawake na kuimarisha lishe kwa wakuzaji wadogo wa viumbe maji, hususan wakulima wa mwani na wafugaji wa samaki katika Halmashauri za Mtama, Ruangwa Songea na Mbinga



Akiongea wakati wa kufunga mradi huo wa Lishe, Mratibu wa Programu ya Kuendeleza Kilimo na Uvuvi (AFDP) kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu Bw. Salimu Mwinjaka Alisema kuwa, mradi huo wa miaka miwili ulijikita zaidi katika katika kilimo cha mwani na uzalishaji wa viumbe maji ulifanikiwa kwa kiasi kikubwa kwani wanufaika wa mdari huo bado wanaendelea na shughuli hizo za uzalishaji kwa kutumia teknolojia za kisasa na ubunifu waliojijengea.








Kwa pande wake Mkurugenzi wa Ukuzaji viumbemaji toka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dkt Nazaeli Madala alieleza kuwa, Serikali imeweka msisistizo katika kukuza uchumi na mikoa iliyotekeleza mradi huo imeweza kukuza uchumi.








‘Mkoa hiyo imebahatika kupata ardhi nzuri na imekuwa fursa ya kuweza kufuga na kupata chakula na kuwauzia wengine chakula, kupata uzalishaji ulio na tija pamoja na uzalishaji Ajira na huu ndo msukomo wa Serikali.” Alibainisha Dkt Madala.
Aidha Aliwaasa wanufaika wa Mradi huo kuwapatia wengine ujuzi walioupata na kuwa waaminifu wanapopata mikopo kupitia Bank ya Kilimo nchini TADB kwa kuirejesha kwa wakati kwa amendeleo ya Taifa.Afisa Uvuvi kutoka Cameroon Bi Audrely Tchoundi aliwapongeza wafugaji wa Tanzani kwa kuwa wabunifu katika eneo la ufungaji viumbemaji na ukulima wa mwani kwa kutumia mbinu mbadala akitolea mfano wakulima wa Mwani wa Kijiji cha Shuka Mkoani Lindi, pamoja na usimamizi mzuri wa mabwawa ya samaki.



Mmoja wa wanufaika wa Mradi huo mwakilishi wa vijana Bw. Innocent Kikiwa Amesema kuwa mradi huo umemuwezesha yeye kama kijana kuweza kupata uzoefu katika eneo la Ufugaji Viumbemaji na kilimo cha mwani, kuweza kujiajiri kukuza mnyororo wa thamani kwa kuuza mazao yatokanayo na zao la mwani, kuuza samaki anaowafuga pamoja na kutafuta masoko.
Share:

Friday, 5 June 2026

TANZANIA: BELGRADE MEETINGS SEAL ARUSHA PREPARATIONS FOR 153RD IPU ASSEMBLY


#Tanzanian delegation confirms readiness after key meetings with IPU leadership and Serbian hosts in Belgrade

By Prosper Makene

Tanzania’s Deputy Permanent Representative to the United Nations in Geneva, Ambassador Dr. Hoyce Temu, joined Tanzanian MPs in Belgrade to engage with the IPU leadership and Serbian parliamentary hosts. In meetings with the heads of the Preparatory Committee from the Parliament of Serbia — Mr. Vladimir and Ms. Vesna — the Tanzanian team exchanged critical lessons on logistics, protocol, and conference management.  

Dr. Temu who also manages the IPU in Geneva, said the engagement was crucial for aligning Arusha’s hosting plans with global standards.  

“After attending five IPU meetings around the world, I can confirm that we are now ready. Arusha is ready and Tanzania is ready,” Dr. Temu posted after the Belgrade sessions. “We have learned a lot about the preparations. Arusha is ready to receive parliamentarians from around the world.”  

On her part, IPU President Hon. Dr. Tulia Ackson, addressed delegates at the IPU Global Conference of Women Parliamentarians in Belgrade, Serbia. She said:

“Today is not a day to talk about anything you haven’t been good in, but for anything good that you have seen in Tanzania, you will get it in abundance,” Dr. Tulia told the assembly.  

She announced that the 153rd IPU Assembly will be held from 5th to 9th October 2026 in Arusha, and assured delegates that Tanzania is ready to host:  

“So I would like to take this opportunity to specially invite all of you, dear women and men parliamentarians of the world, to come to Arusha, to come to Tanzania and enjoy the hospitality of this country.”  

Dr. Tulia further confirmed that President Dr. Samia Suluhu Hassan is ready to receive the global delegation, and that Tanzania has put comprehensive measures in place for safety and health:  

“Her Excellency Dr. Samia Suluhu Hassan is ready to receive you, the President of Tanzania, but also Tanzania is ready to receive you. Tanzania is prepared to serve you. We have put in place everything needed to make sure you arrive safely and healthy, and you leave safely and healthy too.”  

In a separate engagement in Belgrade, Dr. Temu assured Dr. Tulia and outgoing Secretary General Martin Chungong that Tanzania has completed its groundwork.  

Arusha to Host 2,000+ Global Delegates  

The 153rd IPU Assembly in Arusha is expected to bring together over 2,000 delegates, parliamentarians, and observers from across the globe, making it one of the largest diplomatic gatherings ever hosted by Tanzania.  

In this context, it is particularly noteworthy that Tanzania will host the 153rd Assembly of the Inter-Parliamentary Union (IPU) in Arusha this October 2026. The announcement has raised expectations as the country positions Arusha — already known as Africa’s diplomatic capital — as a center for parliamentary dialogue, peacebuilding, and multilateral cooperation.  

Tanzania’s Parliament is making final preparations to welcome the world. A high-level delegation of Members of Parliament confirmed the country’s readiness during the World Conference of Women Parliamentarians in Belgrade, Serbia. The delegation, representing the Parliament of Tanzania at the IPU event, met with key IPU officials to ensure the Arusha assembly will be a success.  

The message was echoed by fellow MPs  in Belgrade, including Hon. Rashid Shangazi, Hon. Pindi Chana, Hon. Dr. Zeyana Hamid, and Hon. Kiza Mayeye. The group used the platform to showcase Tanzania’s capacity to host high-level global forums.  

From Geneva to Arusha: A Decade of Parliamentary Diplomacy 
 
Dr. Temu’s role is particularly significant. Based in Geneva where the IPU headquarters is located, she has coordinated Tanzania’s participation in multiple IPU assemblies. Her presence in Belgrade alongside the MPs signals a whole-of-government approach to ensuring Arusha 2026 delivers on diplomacy, organization, and impact.  

With lessons from Belgrade now integrated into the plan, all eyes turn to Arusha. The blueprint is set. The Tanzania Parliament Under the leadership of the House Speaker Mussa Azzan Zungu is Confident and Ready As Dr. Temu said, we are now ready for the IPU meeting in Arusha, the city which is popularly known as the Geneva of Africa.




Share:

TPDC YAKABIDHI KARAKANA YA KISASA YA CNG KWA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM.


Dar es Salaam, Juni 5, 2026

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) limekabidhi rasmi Karakana ya kuongeza mfumo wa matumizi ya gesi asilia Iliyoshindiliwa kwenye vyombo vya usafiri (CNG Conversion Workshop) kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), hatua inayotarajiwa kuimarisha matumizi ya nishati safi nchini pamoja na kukuza ujuzi wa kitaalamu katika teknolojia ya gesi asilia.

Makabidhiano hayo yamefanyika leo katika eneo jijini Dar es Salaam, ambapo TPDC iliwakilishwa na Mkurugenzi wa Idara ya Mipango na Uwekezaji, Bw.Derick Moshi, kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa TPDC. Kwa upande wa UDSM, karakana hiyo ilipokelewa na Naibu Mkuu wa Chuo Prof. Bernadeta Kilian.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Bw. Derick Moshi alisema kuwa ujenzi wa karakana hiyo ni sehemu ya jitihada za TPDC katika kuunga mkono mkakati wa Serikali wa kuhamasisha matumizi ya nishati safi na nafuu kwa wananchi.

“Kukamilika na kukabidhiwa kwa karakana hii ni hatua muhimu katika kukuza matumizi ya gesi asilia Iliyoshindiliwa (CNG) nchini. Mbali na kutoa huduma za kuongeza mifumo ya CNG kwenye magari, karakana hii itatumika kujenga wataalamu wazalendo kupitia mafunzo ya vitendo kwa wanafunzi wa uhandisi wa UDSM,” alisema Bw. Moshi.

Aliongeza kuwa mradi huo umegharimu shilingi bilioni 1.52 za Kitanzania na ni sehemu ya utekelezaji wa makubaliano ya ushirikiano kati ya TPDC na UDSM yaliyowekwa kupitia Mkataba wa Upangishwaji Ardhi uliosainiwa mwaka 2022.

Kwa mujibu wa Bw. Moshi, karakana hiyo ina vifaa vya kisasa vinavyowezesha ufungaji wa mifumo ya CNG kwenye vyombo vya usafiri, ukaguzi wa usalama wa mifumo hiyo pamoja na matengenezo yake, hatua itakayochangia kupunguza gharama za matumizi ya nishati kwa watumiaji wa magari nchini.

Kwa upande wake, Prof. Bernadeta Kilian aliishukuru TPDC kwa kutekeleza ahadi yake ya kujenga na kukabidhi karakana hiyo, akieleza kuwa miundombinu hiyo itakuwa kichocheo muhimu katika maendeleo ya elimu, utafiti na ubunifu wa teknolojia za nishati nchini.

“Kupokea karakana hii ni hatua kubwa kwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Miundombinu hii itawapa wanafunzi wetu nafasi ya kupata mafunzo ya vitendo yanayokidhi mahitaji ya soko la ajira na wakati huo huo kusaidia maendeleo ya sekta ya nishati nchini,” alisema Prof. Kilian

Alisisitiza kuwa UDSM itaendelea kushirikiana na TPDC katika tafiti, ubunifu na maendeleo ya teknolojia zinazochangia matumizi bora ya rasilimali za gesi asilia kwa manufaa ya Taifa.

Karakana hiyo imejengwa ndani ya eneo la Kituo Mama cha kujaza gesi asilia (CNG Mother Station) kilichopo UDSM na inatarajiwa kuwa kituo muhimu cha utoaji huduma za CNG pamoja na mafunzo ya kitaalamu kwa wanafunzi na wadau wa sekta ya usafiri.

Kupitia uwekezaji huo, TPDC inaendelea kutekeleza dhamira ya Serikali ya kuhamasisha matumizi ya Nishati Safi, salama na nafuu, sambamba na kuongeza ushiriki wa taasisi za elimu ya juu katika maendeleo ya sekta ya nishati nchini.
Share:

DKT. KIJAJI: NYUMBA ZA IBADA ZIWE CHANZO CHA MSHIKAMANO NA AMANI KWA TAIFA




KONDOA, DODOMA

Mbunge wa Jimbo la Kondoa ambaye pia ni Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji (Mb), amesisitiza kuwa nyumba za ibada zinapaswa kuwa sehemu ya kuimarisha mshikamano, umoja na amani miongoni mwa wananchi na si kuwa chanzo cha migawanyiko katika jamii.

Dkt. Kijaji ametoa kauli hiyo leo alipokuwa akifungua rasmi Msikiti wa Filimo uliopo Kata ya Mnenia, Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma.



Akizungumza katika hafla hiyo, Dkt. Kijaji amesema kuwa nyumba za ibada zina nafasi kubwa katika kujenga maadili mema, kuimarisha upendo na kukuza mshikamano wa kijamii, hivyo zinapaswa kutumika kwa malengo hayo kwa manufaa ya Taifa.

“Msikiti huu uwe chachu ya mshikamano ndani ya jamii yetu. Nawapongeza viongozi wa dini kwa kusimama katika haki na kuendelea kuhubiri amani na umoja miongoni mwa wananchi,” alisema Dkt. Kijaji.


Aidha, aliongeza kuwa kila mtu ana wajibu wa kutekeleza majukumu yake kwa uadilifu katika jamii na mbele za Mungu, akibainisha kuwa maendeleo yanayopatikana katika Jimbo la Kondoa yanalenga kuwanufaisha wananchi wote bila ubaguzi.

"Ninachokifanya ndani ya jimbo letu ni kwa ajili ya maendeleo ya Wakondoa wote. Tunapaswa kuendelea kushirikiana na kuishi kwa upendo ili kuleta maendeleo endelevu,” alisisitiza.



Vilevile , Dkt. Kijaji alitumia fursa hiyo kuwahamasisha waumini na wananchi wa eneo hilo kuendelea kujenga na kuendeleza nyumba za ibada ili zitumike katika kukuza maadili mema na kuimarisha imani katika jamii.

Katika hatua nyingine, amewataka vijana kujiepusha na matumizi ya dawa za kulevya na vitendo vingine vinavyohatarisha mustakabali wao, huku akiwataka viongozi wa dini kuendelea kuliombea Taifa pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.


Pia amesisitiza umuhimu wa malezi bora kwa watoto na vijana, akiwataka wazazi na walezi kuwajenga katika misingi ya maadili mema ili kuwa raia wema na wenye mchango chanya kwa maendeleo ya Taifa.


Share:

Thursday, 4 June 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JUNI 5, 2026

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger