Friday, 28 August 2026

DG NEMC ATUNUKIWA TUZO YA HESHIMA–USIMAMIZI WA MAZINGIRA


-Ni katika hitimisho la Kongamano la FARViBE 2026,lililofanyika Jijini Dar es salaam

Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt.Immaculate Sware Semesi ametunukiwa tuzo ya heshima na Naibu Waziri Wizara ya Uvuvi na Uchumi wa Buluu - Zanzibar, Mhe. Mboja Ramadhan Mshenga katika Kongamano la kimataifa la Kisayansi la Utafiti wa Uvuvi na Ufugaji wa Samaki kwa Uchumi wa Buluu Endelevu (FARViBE 2026), lililofanyika kuanzia tarehe 24 hadi 27 Agosti 2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa JNICC Jijini Dar es Salaam.

Tuzo hiyo iliyopokelewa na Meneja wa NEMC Kanda ya Mashariki Kaskazini Bi. Glory Kombe kwa niaba yake imelenga kutambua mchango alionao katika Sekta ya Mazingira hasa ikizingatiwa suala la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira nchini ndio msingi wa Maendeleo endelevu kufikia Dira ya Maendeleo ya Taifa ya 2050.

Akizungumza wakati wa kukabidhi tuzo hiyo, Naibu Waziri Mhe. Mboja Mshenga amesisitiza umuhimu wa kuendelea kuimarisha juhudi za Uhifadhi na Usimamizi wa mazingira ya bahari, kwani ndio msingi wa maendeleo katika sekta ya uvuvi na uchumi wa buluu huku akisistiza maendeleo ya kiuchumi ili kuhakikisha rasilimali za bahari zinalindwa na kutumika kwa manufaa ya kizazi cha sasa na baadae

NEMC imeshiriki kongamano hilo kwa lengo la kuwasilisha na kujadili masuala ya Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira hususani Bahari kwa ustawi wa uvuvi na uchumi wa buluu endelevu.

Kongamano hilo lililowakutanisha wataalamu na wadau wa masuala ya bahari kutoka ndani na nje ya Tanzania, lililenga kujadili tafiti, ubunifu na teknolojia zinazoweza kuchangia maendeleo endelevu ya sekta ya uvuvi na uchumi wa buluu.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA AGOSTI 28, 2026

Share:

Thursday, 27 August 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI AGOSTI 27,2026






Magazeti ya leo

 



Share:

Wednesday, 26 August 2026

NILE BLUES PROJECT KUWAFIKIA SHULE 10 ARUSHA KWA ELIMU YA MUZIKI, SANAA NA UTAMADUNI

Na Bora Mustafa, Arusha

 Mradi wa Nile Blues Project umeendelea kuwafikia wanafunzi wa shule mbalimbali jijini Arusha kupitia warsha za muziki, sanaa, ubunifu na utamaduni, ukiwa na lengo la kuwajengea vijana ujuzi na kuwapa nafasi ya kugundua na kukuza vipaji vyao.

Mradi huo ambao unalenga kufikia jumla ya shule 10 jijini Arusha, umeendelea na mafunzo yake katika Sekei Secondary School, ambapo wanafunzi wamepata nafasi ya kujifunza kwa vitendo pamoja na kushiriki katika shughuli za ubunifu.

Akizungumza Leo Agosti 26,2026 wakati wa programu hiyo, Lwanda Magere,Meneja wa Mradi wa Nile Blues Project, amesema mafunzo hayo yamekuwa na matokeo mazuri kutokana na mwitikio wa wanafunzi ambao wameweza kutumia maarifa waliyopata kutengeneza na kuonesha ubunifu wao wenyewe.

Pia amesema furaha kubwa kwa timu ya mradi huo ni kuona wanafunzi wakipata ujuzi ambao unaweza kuwasaidia kutambua uwezo wao na kuutumia katika maisha ya sasa na baadaye.

Kwa upande wake, Renalda Masawe, Mratibu wa Programu, amesema Sekei Secondary ni miongoni mwa shule ambazo mradi umefikia katika utekelezaji wa programu hiyo, baada ya awali kutembelea St. Patrick School.

Amesema baada ya Sekei, mpango huo utaendelea katika Kaloleni Primary School na baadaye Arusha Meru, huku lengo likiwa ni kufikisha mafunzo hayo katika shule 10 za Arusha.

Masawe amesema mpango huo utaendelea pia wiki ijayo katika shule nyingine, huku akieleza kuwa baadhi ya shule zimeonesha nia ya kushiriki katika programu hiyo kutokana na umuhimu wake kwa wanafunzi.

Amesema timu ya mradi iko tayari kushirikiana na shule zitakazohitaji programu hiyo ili kuhakikisha wanafunzi wengi zaidi wanapata fursa ya kujifunza na kukuza vipaji vyao.

Aidha, amesema lengo si kuwafundisha wanafunzi maarifa ya darasani pekee, bali pia kuwawezesha kutumia ubunifu, sanaa na utamaduni kama sehemu ya kujenga uwezo wao.

Kwa upande wake, Sir Patrick, Mwalimu wa Michezo wa Sekei Secondary School, amesema programu kama hiyo ina umuhimu mkubwa katika kuboresha elimu kwa wanafunzi kwa kuwa inawapa nafasi ya kujifunza kupitia michezo, sanaa na utamaduni.

Amesema ni muhimu shule kuendelea kutoa nafasi kwa shughuli za nje ya darasa ambazo zinaweza kuwasaidia wanafunzi kugundua vipaji na uwezo wao katika maeneo mbalimbali.

Amesema ushirikiano kati ya shule na programu zinazolenga kukuza vipaji unaweza kuwa chachu ya kuwajenga wanafunzi wenye uwezo mpana zaidi, sambamba na masomo yao ya kawaida.

Naye Rose Frank, mwanafunzi wa Kidato cha Tatu katika Sekei Secondary School, amesema mafunzo hayo yamewapa wanafunzi fursa ya kujifunza mambo mapya ambayo awali hawakuwa na uelewa nayo.

Pia amesema kupitia mafunzo hayo wanafunzi wameweza kupata maarifa mapya na kujifunza kwa vitendo, jambo ambalo limewapa hamasa ya kuendelea kutumia vipaji na ubunifu wao.

Nile Blues Project inaendelea na mpango huo katika shule mbalimbali za Arusha, huku ikilenga kuwafikia wanafunzi wengi zaidi na kuwapa ujuzi unaohusisha muziki, sanaa, ubunifu na utamaduni.

Programu hiyo pia inaendana na umuhimu wa kuwapa vijana nafasi ya kujifunza kuhusu sanaa na utamaduni wao, huku shughuli za vitendo zikiwasaidia kugeuza maarifa wanayopata kuwa ujuzi unaoweza kutumika katika maisha yao.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger