Monday, 13 July 2026

UZINGATIAJI WA SHERIA NDIO MSINGI WA KULINDA HAKI ZA BINADAMU NA UTULIVU NCHINI



Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora imewataka wananchi kote nchini kuendelea kuheshimu sheria za nchi kwani kufanya hivyo ndio msingi mkuu wa wao kuweza kufurahia haki zao kikamilifu katika jamii.

Akizungumza wakati wa Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, maarufu kama Sabasaba, Katibu Mtendaji wa tume hiyo, Patience Ntwina aliwakumbusha wananchi kwa msisitizo kuwa utekelezaji wa haki za binadamu daima unaenda sambamba na wajibu wa kila mmoja wa kudumisha amani, utulivu pamoja na utaratibu katika jamii na nchini kwa ujumla.

Alifafanua kuwa uzingatiaji wa sheria na kanuni zilizopo kwa upande wa wananchi wote unaifanya tume hiyo iweze kutekeleza kwa ufanisi mkubwa jukumu lake la kikatiba la kuhamasisha na kulinda haki za binadamu.

Ntwina alieleza kuwa iwapo Watanzania wote wataendelea kudumisha utamaduni wao wa muda mrefu wa kuheshimu sheria na kanuni za nchi, watakuwa wamechangia kwa kiwango kikubwa sana juhudi zinazochukuliwa na tume hiyo katika kuhamasisha na kulinda haki za binadamu nchini.

Aliongeza kuwa ukiukwaji wa sheria na kanuni huleta athari kwani husababisha vyombo vya dharura na sheria, likiwemo Jeshi la Polisi, kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria zilizowekwa ili kurejesha utaratibu.

Kwa mujibu wa maelezo yake, ushiriki wa tume hiyo katika maonesho hayo ya biashara umeiwezesha kupeleka elimu ya uraia karibu zaidi na wananchi, hatua ambayo imesaidia kwa kiasi kikubwa kuwasaidia kuelewa kwa kina haki zao za kimsingi pamoja na wajibu wao kwa taifa.

Alisisitiza kuwa ni muhimu sana kila mtu afurahie haki zake lakini afanye hivyo bila kukiuka au kuingilia haki za watu wengine.

Katika kuweka uzito kwenye hoja hiyo, alitolea mfano wa baadhi ya sehemu za starehe zinazopiga muziki kwa sauti kubwa katika maeneo ya makazi, akisema hali hiyo huifanya upande mmoja kudai kuwa unatekeleza haki zake za kibiashara au burudani, huku kwa upande mwingine ukivunja haki za wananchi wengine za kuishi katika mazingira tulivu.


Akizungumzia hali ya utawala bora nchini, Ntwina alisema kuwa binafsi ameridhishwa kwa kiwango kikubwa na kiwango cha amani na utulivu kinachoendelea kuwepo nchini kote. Alibainisha kuwa utulivu huo wa sasa umeendelea kuwezesha shughuli mbalimbali za kijamii na kiuchumi kufanyika kwa ufanisi wa hali ya juu na hivyo kuchochea maendeleo ya taifa kwa ujumla.
Share:

WIZARA YA ELIMU YAANZA MAGEUZI MAKUBWA KUJIBU MAHITAJI YA SOKO LA AJIRA




Na Dotto Kwilasa,Dodoma

WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeanza utekelezaji wa mkakati mpya unaolenga kuifanya sekta ya elimu izalishe wahitimu wenye ujuzi, ubunifu na uwezo wa kushindana katika soko la ajira la ndani na kimataifa, sambamba na utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Mkakati huo unajumuisha maboresho ya mitaala, matumizi makubwa ya teknolojia ya habari na mawasiliano, ushirikishwaji wa sekta binafsi katika uwekezaji wa elimu pamoja na kuimarisha mifumo ya ukusanyaji wa takwimu kwa ajili ya kupanga na kufanya maamuzi.

Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Profesa Caroline Nombo,amesema mafanikio yaliyofikiwa katika sekta ya elimu yanapaswa kuwa chachu ya kuharakisha mageuzi yanayolenga kuandaa rasilimali watu itakayokidhi mahitaji ya uchumi wa kisasa.

Akizungumza leo July 13,2026 kwenye Kikao cha mwaka cha Menejimenti ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya wizara hiyo kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda,Prof.Nombo amesema sekta ya elimu ndiyo msingi wa utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, hivyo ni muhimu mipango yote ya wizara ikaendana na matarajio ya taifa ya kujenga uchumi unaotegemea maarifa, sayansi na teknolojia.

“Tumekutana kufanya tathmini ya tulikotoka, tulipo na tunapokwenda. Ni wajibu wetu kuhakikisha sekta ya elimu inatoa mchango mkubwa katika kufanikisha Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050,” amesema.

Profesa Nombo amesema moja ya maeneo yatakayopatiwa kipaumbele ni kupitia upya kozi na programu za elimu ili ziweze kujibu mahitaji halisi ya jamii na soko la ajira.

Amesema mjadala unaoendelea katika mitandao ya kijamii kuhusu kozi zinazofaa kusomwa na wahitimu wa kidato cha sita unaonyesha wazi kuwa jamii inahitaji mfumo wa elimu unaobadilika kulingana na mahitaji ya wakati.

“Mrejesho tunaoupata unatufanya tujitathmini na kuangalia aina ya kozi tunazotoa,tunahitaji kuongeza ubunifu na unyumbufu katika kuwapa wanafunzi fursa ya kusoma taaluma zinazojibu mahitaji ya maendeleo ya taifa,” amesema.

Aidha, ameagiza taasisi zote zilizo chini ya wizara kuhakikisha mifumo yao ya TEHAMA inaunganishwa na Mfumo wa Taarifa za Usimamizi wa Elimu (ESMIS) ili kuongeza ufanisi wa ukusanyaji wa takwimu na kurahisisha maamuzi ya kisera.

Amesema hatua hiyo pia inatekeleza maelekezo ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuhakikisha mifumo ya Serikali inasomana na kufanya kazi kwa pamoja.

Katibu Mkuu huyo pia amesisitiza umuhimu wa kushirikisha sekta binafsi katika uwekezaji wa elimu ili kuongeza ubora wa huduma, kuimarisha miundombinu na kupanua fursa za kujifunza kwa Watanzania wengi zaidi.

Amesema pamoja na kuendelea kuboresha mitaala, wizara itaweka mkazo katika kuboresha mazingira ya kujifunzia na kufundishia ili wahitimu wawe na maarifa na ujuzi unaokidhi mahitaji ya taifa na dunia.

Kwa upande wake, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Profesa Daniel Mushi, amewataka viongozi wa taasisi mbalimbali kuendelea kutoa taarifa kwa wananchi kuhusu mafanikio yanayopatikana kupitia utekelezaji wa miradi na programu za Serikali katika sekta ya elimu.

Katika kikao hicho, viongozi wa wizara, wakurugenzi, wakuu wa vitengo na wakuu wa taasisi waejadili nafasi ya elimu katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050, matumizi ya TEHAMA katika utoaji wa huduma, mfumo wa ESMIS, Mpango Mkakati wa Wizara wa mwaka 2026/27 hadi 2030/31 pamoja na utekelezaji wa bajeti ya mwaka wa fedha 2026/27.





Share:

ELIMU YA UTOAJI WA MIKOPO KWA MAKUNDI MAALUM IONGEZEKE - RABIA





Viongozi wa Serikali wameshauriwa kuongeza Elimu ya utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10, ambayo katika bajeti ya mwaka 2026/2027 itakuwa asilimia 15.

Hayo yameelezwa leo Julai 12,2026 na Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa Ndg Rabia Abdalla Hamid katika muendelezo wa ziara yake ya Kusikiliza na kutatua changamoto za Makundi mbalimbali ya kijamii mkoani Rukwa.

“Nitoe rai kwa Viongozi wa serikali kuhakikisha Elimu ya utoaji na urejeshaji wa mikopo ya asilimia 10,ambayo katika bajeti ya mwaka 2026/2027 itakuwa asilimia 15 inatolewa kwa kasi ili wananchi wawe na uelewa mpana katika masuala ya fedha na walengwa waendelee kunufaika ”,amesema Ndugu Rabia.

































Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU JULAI 13,2026



Magazeti





Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger