Monday, 11 May 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU MEI 11,2026



Magazeti leo





Share:

Sunday, 10 May 2026

MAGAMBO AGUSA SEKTA YA ELIMU NYAMATARE,AMUUNGA MKONO RAIS SAMIA KWA KUJENGA VYUMBA VITANO VYA MADARASA

MKURUGENZI Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), Fortunatus Magambo ameandika historia mpya katika Kata ya Nyamatare baada ya kujitolea kujenga vyumba vitano vya madarasa katika Shule ya Msingi Ring’wani, hatua inayotajwa kuwa mkombozi kwa wanafunzi wa shule hiyo.

Bw. Magambo alifikia uamuzi huo baada ya kutembelea shule hiyo mwaka 2024 na kushuhudia hali ya uchakavu wa miundombinu pamoja na upungufu mkubwa wa madarasa uliokuwa ukiathiri mazingira ya kujifunzia kwa wanafunzi.

“Nilipofika hapa niliguswa kuona watoto wakisomea katika mazingira magumu kutokana na uhaba wa vyumba vya madarasa. Nimeamua kushiriki kuboresha mazingira haya ili watoto wetu wapate sehemu bora ya kujifunzia,” amesema Bw. Magambo.

Tayari kazi ya uchimbaji wa msingi pamoja na hatua za awali za ujenzi wa vyumba hivyo vitano imeanza, huku lengo likiwa ni kuhakikisha mradi huo unakamilika kabla ya Julai 2026 kuisha.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Nyamatare, Mgaya Maheke amemshukuru Bw. Magambo kwa moyo wake wa kujitoa kusaidia maendeleo ya elimu katika kata hiyo.

“Tunawapongeza wadau wetu wa maendeleo wanaoendelea kushirikiana nasi kuinua sekta mbalimbali za kijamii. Ushirikiano huu ni faraja kubwa kwa wananchi wetu,” amesema Mheshimiwa Maheke.

Ameongeza kuwa ataendelea kutoa ushirikiano wa kutosha kwa wadau wote wanaojitokeza kusaidia jamii kupitia miradi mbalimbali ya maendeleo.

Kutokana na Elimu kuwa nguzo muhimu katika jamii na ndio ufunguo wa maisha, jamii imeendelee kuhimizwa kuleta maendeleo katika maeneo yao wao wenyewe na siyo tu kuiachia serikali peke yake.












Share:

SALOME: NYUMBA 2,512 ZIMEUNGANISHWA NA MIUNDOMBINU YA GESI ASILIA


Na Mwandishi Wetu

Naibu Waziri wa Nishati, Salome Makamba amesema hadi Aprili 2026, jumla ya nyumba 2,512 zimeunganishwa na miundombinu ya gesi asilia katika mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani na Dar es Salaam.

Mhe. Salome ametoa taarifa hiyo Mei 8, 2026 bungeni jijini Dodoma alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Asha Omar Rashid, aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kuboresha upatikanaji wa nishati ya gesi vijijini.

Akijibu swali hilo, Mhe.Salome amesema Serikali kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) inaendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya usambazaji wa gesi asilia, ambapo hadi Aprili 2026 nyumba 425 zimeunganishwa katika Mkoa wa Mtwara, 677 Mkoa wa Lindi, 530 Mkoa wa Pwani na 880 Mkoa wa Dar es Salaam.

Aidha, amesema katika kuhakikisha nishati ya gesi inawafikia Watanzania wengi zaidi, Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unaendelea kutekeleza mradi wa kusambaza mitungi 452,445 ya Gesi Oevu ya Petroli (LPG) yenye ujazo wa kilogramu sita kwa ruzuku ya asilimia 50 ili kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia katika maeneo ya vijijini na vijiji-miji.

Vilevile, Serikali inaendelea kuhamasisha sekta binafsi kuwekeza katika miundombinu ya usambazaji wa gesi ya LPG katika maeneo ya vijijini na vijiji-miji.

Mhe. Salome amesema Serikali pia inaendelea kufanya tafiti katika maeneo ya mijini na vijijini ili kubaini aina sahihi ya miundombinu inayohitajika kwa ajili ya kufikisha na kusambaza gesi asilia kwa ufanisi zaidi.

Amefafanua kuwa matokeo ya tafiti hizo yatawezesha kubainisha njia bora za usambazaji wa gesi asilia kulingana na mahitaji ya maeneo husika, sambamba na kuibua fursa za kuanzishwa kwa miradi mingine ya usambazaji wa gesi asilia itakayotekelezwa kwa ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi ili kuhakikisha wananchi wengi zaidi mijini na vijijini wananufaika na nishati hiyo safi.




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger