Thursday, 19 March 2026

KAMATI YA BUNGE YATOA WITO WA KUFUATILIA TAARIFA ZA HALI YA HEWA, YAIOMBA SERIKALI KUHARAKISHA MIRADI TMA

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Selemani Kakoso, Akizungumza jijini Dar es Salaam wakati wa ziara ya kamati hiyo TMA.

********

Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, Selemani Kakoso, ametoa wito kwa Watanzania kufuatilia na kuzingatia taarifa za hali ya hewa zinazotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) ili kusaidia kupanga shughuli za kiuchumi na kijamii kwa usahihi.

Akizungumza jijini Dar es Salaam wakati wa ziara ya kamati hiyo TMA, Kakoso alisema mamlaka hiyo imekuwa ikitoa taarifa sahihi na za kuaminika kila siku kupitia vyombo mbalimbali vya habari, hivyo wananchi wanapaswa kuacha kupuuza taarifa hizo muhimu.

Alisisitiza kuwa sekta kama kilimo, biashara na maji zinategemea kwa kiasi kikubwa taarifa za hali ya hewa, na kuongeza kuwa uwekezaji uliofanywa na Serikali umewezesha upatikanaji wa teknolojia za kisasa za utabiri.

Katika ziara hiyo, kamati ilikagua miradi mbalimbali ikiwemo ujenzi wa Ofisi ya Kanda ya Mashariki, Kituo cha Tahadhari ya Matukio ya Tsunami pamoja na Kituo cha Taifa cha Uhakiki wa vifaa vya hali ya hewa, ambapo imeelezwa kuwa baadhi ya miradi hiyo inasuasua.

Kutokana na hali hiyo, kamati imeiomba Serikali kuingilia kati ili kuongeza kasi ya usimamizi na kuhakikisha miradi hiyo ya kimkakati inakamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa.

Kwa upande wake, Waziri wa Uchukuzi, Makame Mbarawa, alisema Serikali ya Awamu ya Sita itaendelea kuwekeza katika sekta ya hali ya hewa na kuhakikisha fedha za kukamilisha miradi hiyo zinapatikana kwa wakati.



Naye Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Ladislaus Chang'a, ameishukuru Serikali kwa uwekezaji mkubwa uliofanywa, akieleza kuwa mitambo ya kisasa ikiwemo rada imeongeza uwezo wa utoaji wa tahadhari na kuvutia mataifa mengine kuja kujifunza nchini.
Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Ladislaus Chang'a,Akizungumza jijini Dar es Salaam wakati wa ziara ya kamati hiyo TMA.














Share:

Wednesday, 18 March 2026

ADEM ITAENDELEA KUTOA FURSA ZA MAFUNZO ENDELEVU YA UONGOZI WA ELIMU KUIMARISHA UONGOZI NA USIAMAMIZI WA SHULE


NA EMMANUEL MBATILO, BAGAMOYO

WIZARA ya Elimu, Sayansi na Teknolojia kupitia Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM) itaendelea kutoa fursa za mafunzo endelevu ya viongozi wa elimu wa ngazi mbalimbali na wadau wengine wa elimu ili waweze kuimarisha uongozi, usimamizi na uendeshaji wa shule kwa ajili ya utoaji wa elimu bora nchini.

Ameyasema hayo Mkurugenzi wa Elimu msingi, Abdul Maulid wakati akimwakilisha Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Wanu Hafidh Ameir katika ufungaji mafunzo ya uongozi, usimamizi na utawala bora wa elimu kwa Maafisa Elimu Kata Tanzania Bara yaliyofanyika katika Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), katika Halmashauri ya Bagamoyo, mkoani Pwani.

Amesema mafunzo hayo yamekusudiwa kuwajengea uwezo viongozi na wasimamizi wa taasisi za elimu ili waweze kusimamia ipasavyo rasilimali na michakato ya utoaji wa elimu, huku wakizingatia misingi ya uongozi bora, uwazi na uwajibikaji.

"Ni matumaini yetu kuwa, ADEM mtaendelea kutoa mafunzo yanayoelenga kuimarisha uongozi, usimamizi na uendeshaji wa elimu kwa njia endelevu na yenye mafanikio pamoja na kufanya tafiti mbalimbali zakielimu na kutoa ushauri wa kitaalam katika masuala ya uongozi. Ninawasihi muendelee kufanya kazi kwa weledi ili kutimiza malengo ya kuanzishwa kwa ADEM". Amesema

Ameongeza kuwa ushirikishwaji wa jamii, matumizi sahihi ya takwimu za elimu na utoaji wa fursa za mafunzo endelevu kwa walimu ni mambo muhimu katika kuimarisha ubora wa elimu.

Ametoa wito kwa washiriki wa mafunzo hayo kutumia maarifa waliyoyapata kuboresha utendaji wao, akisisitiza umuhimu wa kufanya kazi kwa weledi, ubunifu, kujituma na uzalendo ili kufanikisha malengo ya sekta ya elimu nchini.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM), Dkt. Maulid J. Maulid amesema kuwa mafunzo hayo yametekelezwa kama sehemu ya utekelezaji wa dhamira ya Serikali ya kuimarisha mifumo ya usimamizi wa elimu kwa kuzingatia misingi ya uongozi bora, uwajibikaji na ufanisi katika utoaji wa huduma za elimu.

"Mpango huu ulianza kwa kutoa mafunzo ya kuwajengea uwezo Walimu Wakuu wa shule za msingi kuhusu Uongozi, Usimamizi na Utawala Bora wa Elimu, yaliyowahusisha Walimu Wakuu 17,817 kutoka Mikoa yote 26 ya Tanzania Bara". Amesema

Amesema kuwa mafunzo hayo yamelenga kuwaimarisha Walimu Wakuu katika kusimamia shule kwa kutumia mbinu stahiki za uongozi pamoja na kuzingatia sera, miongozo na viwango vya kitaifa ili kuhakikisha kuwa shughuli za ufundishaji na ujifunzaji zinafanyika kwa ubora, ufanisi na kwa kuzingatia viwango vinavyokubalika kitaifa na kimataifa.

Pamoja na hayo Dkt. Maulid amesema kuwa tathmini inaonyesha kiwango kikubwa cha mabadiliko ya kiutendaji kwa walimu wakuu katika kuongoza na kusimamia shule zao baada ya kupatiwa mafunzo hayo.

`
Share:

ALIYEKUWA AKITUHUMIWA KUOLEWA NA ‘JINI’ KISA KUTOSHIKA MIMBA, SASA NI MAMA WA WATOTO WANNE!




Naitwa Brenda, mkazi wa mkoa wa Arusha. Mimi ni mwanamke mjasiriamali ninayemiliki maduka kadhaa ya utalii, lakini mafanikio yangu ya kifedha yalikuwa chungu kwangu. Kwa miaka kumi na moja ya ndoa, sikuwa nimefanikiwa kubeba hata ujauzito mmoja uliotoka (miscarriage), achilia mbali wa kuzaliwa.

Majirani na hata baadhi ya wafanyakazi wangu walianza kunisema kwa siri kuwa huenda niliolewa na “jini la mali” ambalo linazuia mimi nisizae ili nishindwe kuacha mrithi.

Share:

Tuesday, 17 March 2026

🌙✨ EID SPECIAL , NGARA, PENDEZA NA MADERA FASHION, KITUO CHA ABAYA

✨🌙

Pendeza Zaidi Msimu Huu wa Eid

 MADÊRA FASHION IPO KWA AJILI YAKO!

Eid hii, chagua muonekano wa kipekee utakaoacha watu wakikuangalia mara mbili! 😍

MADÊRA FASHION tumekuletea mitindo mipya, maridadi na yenye heshima – inayokufanya uangaze siku ya Eid na kila siku.

📍 Tupo Shinyanga Mjini
👉 Mkabala na Benki ya TCB “Posta” (utaona duka moja kwa moja ukiwa langoni)
👉 Pia tupo jirani na Katamba Lodge, karibu na Daraja la Upongoji Ndala

🛍 EID COLLECTION IMEWASILI!
✨ Abaya & Madera za kisasa na za heshima
✨ Magauni ya kuvutia kwa ajili ya Eid
✨ Vijora, Mikoba & Vipochi vya kupendeza
✨ Nguo za Watoto – wapendeze siku ya Sikukuu
✨ Suruali, Tisheti & Mashati ya Wanaume

💎 Ubora wa Kimataifa – Bei Nafuu!
Mitindo kutoka Oman, China, India, Uganda na Tanzania – kwa muonekano wa kisasa na wa kujiamini.

🎉 Ofa Maalum za Eid Zipo!
Usikose punguzo na mitindo mipya ya msimu huu!

📲 Wasiliana nasi: 0652 882 061

🌟 Eid hii – Pendeza, Jiamini, Ng’ara na MADÊRA FASHION!🌟



 
@malundeblog

🌸MADÊRA FASHION – Pendeza kwa Ubora wa Kipekee! 🌸 Karibu katika duka jipya la Madera Fashion – Shinyanga Mjini, mkabala na Benki ya TCB “Posta” (utaona duka moja kwa moja ukiwa langoni). Pia tupo jirani na Katamba Lodge, karibu na Daraja la Upongoji Ndala. 🛍 Tunauza: ✔ Abaya, Madera & Vijora ✔ Magauni, Mikoba & Vipochi ✔ Nguo za Watoto ✔ Suruali, Tisheti & Mashati ya Wanaume 💎 Mitindo ya kisasa kutoka Oman, China, India, Uganda na Tanzania – kwa bei nafuu na ubora wa uhakika. 📞 0652 882 061 Njoo upendeze na Madera Fashion!

♬ Give it to me like - Official Sound Studio



















mama

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger