Sunday, 12 July 2026

MYCOELY BALOZI MPYA WA MAZINGIRA NCHINI

Msanii wa Mziki wa Bongo fleva nchini Michael Muganda (Mycoely) amesaini hati ya makubaliano na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) ya kuwa Balozi wa Mazingira nchini.

Hati hiyo ya makubaliano imesainiwa Julai 11, 2026 kwenye Maadhimisho ya Siku ya Mazingira kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba).

Akizungumza mara baada ya zoezi hilo, Mycoely amesema amepokea kwa furaha kubwa na jukumu lake ni moja tu kuhakikisha anafikisha ujumbe wa umuhimu wa kutunza Mazingira kwa Watanzania.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JULAI 12, 2026



Magazetini Leo


Share:

Saturday, 11 July 2026

JAB YAZINDUA MWONGOZO WA ITHIBATI YA MAISHA KWA WAANDISHI WA HABARI WAKONGWE








Na Mwandishi Wetu.


Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) imezindua rasmi Mwongozo wa Kisheria wa Utoaji wa Ithibati ya Maisha kwa Waandishi wa Habari Wakongwe, hatua inayolenga kutambua na kuthamini mchango wa waandishi wa habari waliolitumikia Taifa kwa muda mrefu na kwa utumishi uliotukuka katika maendeleo ya sekta ya habari nchini.


Uzinduzi huo umefanyika leo, Julai 11, 2026, wakati wa maadhimisho ya JAB Day yaliyofanyika katika Banda la Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba).


Kupitia hotuba yake iliyosomwa na Dkt. Egbert Mkoko, Mwenyekiti wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari, Bw. Tido Mhando, alisema mwongozo huo umeandaliwa kwa kuzingatia mamlaka iliyopewa Bodi chini ya Sheria ya Huduma za Habari, Sura ya 229 pamoja na Kanuni zake, ili kuweka utaratibu wa utoaji wa Ithibati ya Maisha kwa waandishi wa habari wakongwe waliotoa mchango wa kipekee katika maendeleo ya taaluma hiyo.


Alisema mwongozo huo unawahusu waandishi wa habari ambao wakati Sheria ya Huduma za Habari ilipoanza kutumika mwaka 2016 walikuwa na umri wa miaka 50 au zaidi na walikuwa tayari wametoa mchango mkubwa katika sekta ya habari, lakini hawakupata fursa ya kujiendeleza hadi kufikia sifa za kitaaluma zinazohitajika kwa mujibu wa sheria.


"Mwongozo huu unalenga kuhifadhi historia ya tasnia ya habari, kuthamini mchango wa waandishi wa habari wakongwe na kuhakikisha uzoefu wao unaendelea kuwa sehemu ya urithi wa taaluma ya uandishi wa habari nchini," ilieleza sehemu ya hotuba ya Mwenyekiti.




Bw. Mhando alisisitiza kuwa mwongozo huo hauondoi wala haupunguzi masharti ya msingi yaliyowekwa na Sheria ya Huduma za Habari kuhusu sifa za kupata ithibati kwa waandishi wa habari, bali unaweka utaratibu wa kutekeleza mamlaka ambayo sheria imeipa Bodi kuhusu utoaji wa Ithibati ya Maisha kwa watu wenye utumishi uliotukuka na waliotoa mchango wa kipekee katika maendeleo ya sekta ya habari.


Aidha, aliipongeza Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kwa kuendelea kuiwezesha Bodi kutekeleza majukumu yake na kuimarisha ushirikiano unaolenga kukuza weledi, uwajibikaji na maadili katika taaluma ya uandishi wa habari.


Kwa upande wake, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari, Wakili Patrick Kipangula, alisema uzinduzi wa mwongozo huo ni hatua muhimu katika utekelezaji wa Sheria ya Huduma za Habari na unaonesha dhamira ya Bodi ya kuimarisha viwango vya taaluma huku ikitambua na kuthamini mchango wa waandishi wa habari wakongwe waliolitumikia Taifa kwa uaminifu, uzalendo na weledi.


Sambamba na uzinduzi huo, JAB iliendesha mdahalo uliowakutanisha wadau mbalimbali wa sekta ya habari kujadili maendeleo ya sekta ya habari nchini, utekelezaji wa Sheria ya Huduma za Habari pamoja na mafanikio na changamoto zilizojitokeza katika mwaka mmoja wa utekelezaji wa mfumo wa utoaji wa ithibati kwa waandishi wa habari waliokidhi vigezo vya sheria.

Share:

UWEKEZAJI WA SERIKALI WAFUNGUA FURSA ZA UCHUMI RUVUMA

Waziri wa Uchukuzi Mheshimiwa Profesa Makame Mbarawa wa pili kutoka kulia akiwa pamoja na mwenyeji wake mkuu wa mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Ahmed Abbas Ahmed baada ya kuzindua jengo la mapumziko ya muda mfupi kwa abiria katika uwanja wa ndege wa Songea unatarajiwa kuwa chachu ya maendeleo ya kiuchumi katika ukanda wa kusini 
Baadhi ya wafanyakazi wa uwanja wa ndege Songea wakiwa katika uzinduzi huo wa jengo la mapumziko ya muda mfupi kwa abiria katika uwanja wa ndege Songea uliozinduliwa na Mheshimiwa Waziri wa Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa leo tarehe 10 julai 2026

Na Regina Ndumbaro

Songea-Ruvuma 

Uwekezaji wa Serikali wa shilingi milioni 842 katika upanuzi wa jengo la mapumziko ya muda mfupi kwa abiria katika uwanja wa ndege wa Songea unatarajiwa kuwa chachu ya ukuaji wa biashara, uwekezaji na utalii, baada ya kuongeza uwezo wa uwanja huo kuhudumia abiria 300 kwa wakati mmoja.

Share:

Friday, 10 July 2026

HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JULAI 11, 2026


 


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger