Wednesday, 11 March 2026

SAUTI ZA DHAHABU: RAIS SAMIA AFUNGUA UKURASA MPYA WA UTU KWA MAGWIJI BITCHUKA NA ZAHIR ZORRO



Katika ulimwengu wa muziki wa dansi nchini Tanzania, majina ya Hassan Bitchuka na Zahir Zorro si majina ya kawaida. Hizi ni tunu za taifa; ni sauti zilizobeba huzuni, furaha, na mafundisho ya jamii ya Kitanzania kwa zaidi ya miongo minne.

Wiki hii, tasnia ya sanaa imeshuhudia mguso wa kipekee wa kibinadamu kutoka kwa Rais Samia Suluhu Hassan, ambaye kupitia kwa Naibu Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwinjuma ‘Mwana FA’, amemfikia Hassan Bitchuka nyumbani kwake Sinza Mori, Dar es Salaam.

Hassan Bitchuka, fundi wa mashairi na mwimbaji aliyepata kutamba na bendi za DDC Mlimani Park Orchestra ‘Sikinde’, Msondo Ngoma, na OSS, kwa sasa anapambana na maradhi. Rais Samia amemtumia kiasi cha Shilingi milioni 10 kama mkono wa pole na msaada wa matibabu.

"Rais anathamini mchango usiopimika ambao Bitchuka ametoa kuijenga sanaa ya Tanzania," alisema Mwana FA wakati akikabidhi msaada huo. Hili si jambo dogo; ni ishara kuwa serikali sasa inahamia kwenye falsafa ya "Kazi na Utu"—kutambua kuwa msanii ni binadamu anayehitaji kuthitimiwa wakati wa uhai wake.

Ukitaja Sikinde huwezi kumuacha Bitchuka. Ukitaja darasa la uimbaji lenye weledi, huwezi kumuacha mzee Zahir Zorro. Hawa ni watu walioweka misingi ya muziki wa dansi (Tanzania Rumba) ambao leo hii unarithishwa kwa vizazi vipya.

Bitchuka anajulikana kwa uwezo wake wa kutunga mashairi yenye falsafa nzito na sauti iliyokaa kimamlaka jukwaani wakati Zahir Zorro ni gwiji aliyebobea katika uimbaji wa sauti za juu na uandishi wa nyimbo zinazogusa hisia, huku akiwa ameacha mrithi kama Banana Zorro anayeendeleza kipaji hicho.

Hatua ya Rais kuwakumbuka magwiji hawa, inarejesha heshima ya taaluma ya sanaa ambayo kwa muda mrefu ilionekana kusahaulika pindi wasanii wanapostaafu au kuugua.

Katika mwendelezo huo huo wa kuthamini alama za wasanii, Rais Samia alitumia maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani kumzawadia mama mzazi wa marehemu Steven Kanumba, Bibi Flora Mtegoa, gari jipya aina ya Harrier (New Model).

Hii ni ujumbe tosha kwa jamii kwamba hata kama msanii ametangulia mbele za haki, alama aliyoiacha (Legacy) bado inatambulika na serikali yake, na familia yake haitaachwa pweke.

Tunapongeza hatua hii ya Rais Samia. Kuwajali magwiji wetu wakati bado wapo nasi ni kitendo cha kishujaa. Inatuma ujumbe kwa wasanii vijana kuwa ukifanya kazi kwa uaminifu na uzalendo, taifa lako litakukumbuka.

Tunamtakia Hassan Bitchuka nafuu ya haraka na tunazidi kuwaombea magwiji wetu wote maisha marefu yenye amani.
Share:

KANISA KATOLIKI LAJITENGA NA UOVU WA KISIASA


Na mwandishi wetu, Mara

Askofu wa Jimbo Katoliki la Musoma Mkoani Mara Michael Msonganzila amesema Kanisa hilo haliruhusu kikundi chochote kuingia Kanisani kikiwa kimevalia sare za Chama cha siasa kwani Kanisa hilo halifungamani na upande wowote wa kisiasa isipokuwa lina waumini ambao ni wanasiasa na wanachama wa Vyama mbalimbali vya siasa nchini.

Askofu Msonganzila ametoa kauli hiyo mara baada ya Wanawake wanachama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema (BAWACHA) kuingia kwenye ibada ya Jumapili ya Machi 08, 2026 katika Kanisa Kuu la Jimbo la Musoma Mjini wakiwa wamevalia sare zao na baadae kutaka kufanya Mkutano na waandishi wa habari ndani ya eneo la Kanisa, suala ambalo lilisababisha mvutano kati yao na Jeshi la Polisi Mkoani Mara.

"Jumapili imefika hawa BAWACHA, bila sisi kufahamu kikanisa kama wamekuja pale Kanisani kwangu, wakaingia Kanisani na nadhani walibaini kuwa wanafuatiliwa na ninaambiwa hawakuingia getini na mavazi ya Kanisa, waliingia kawaida na wakaenda mafichoni ndani ya Kanisa wakavaa mavazi ya Chadema na baadae wakaingia kanisani na wameshiriki ibada."

"Kanisa tuna kanuni moja, haturuhusu mambo ya siasa yafanyike Kanisani lakini wakati mwingine tunaongozwa na busara na hekima ya hali ya juu na ndio maana aliyeongoza ibada hakusema ninyi mliovaa hivi ondokeni. 

Alishangaa baada ya misa wametoka halafu ghafla wanataka kufanya mahojiano na waandishi wa habari, kitu ambacho baadhi ya walei waliona si kitu cha kawaida." Amekaririwa akisema Baba Askofu Msonganzila.

Wakati akizungumza na waandishi wa habari Jumanne Machi 10, 2026, Askofu Msonganzila amesema binafsi anaamini kuwa masuala au malalamiko ya kisiasa yalipaswa kutolewa ndani ya Ofisi ya Chadema tofauti na awali walivyokuwa wakitaka kufanyia Mkutano wao wa wanahabari ndani ya Viunga vya kanisa, akihoji kupatikana kwa Mwandishi huyo wa habari ikiwa aliandaliwa ama lah na ni kwanini aende kufanyia kazi zake ndani ya Kanisa Katoliki.

Akizungumzia kuhusu Kanisa kuruhusu Wanawake wa Chadema kufanya Kongamano lao katika Viwanja vya Matumaini kwa Vijana, uwanja unaomilikiwa na Kanisa hilo, Askofu Msonganzila amesema awali waliruhusu uwanja huo kutumika kwani hawakuwa wakifahamu kuhusu zuio la serikali kutokana na maamuzi ya Mahakama.
Share:

MWAJUMA AMLIPUA KWA PETROLI MMEWE MADAI YA KUGAWA PESA KWA MCHEPUKO SHINYANGA



Na Mapuli Kitina Misalaba

Mwanamke mmoja anayefahamika kwa jina Mwajuma Shaban anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kwa tuhuma za kumwagia mafuta ya petroli na kumchoma moto mume wake kufuatia mgogoro wa wivu wa mapenzi uliotokea katika Mtaa wa Mageuzi, Kata ya Ngokolo, Manispaa ya Shinyanga.

 Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP), amesema tukio hilo lilitokea Machi 5, 2026 majira ya saa sita usiku.

Amesema majeruhi ametambulika kwa jina la David Mollis mwenye umri wa Miaka 34, dereva wa bodaboda na mkazi wa Mtaa wa Mageuzi ambapo inadaiwa kuwa wakati akiwa amekaa sebuleni nyumbani kwake, alijeruhiwa baada ya kumwagiwa mafuta ya petroli na kuwashiwa moto na mke wake na kusababisha kupata majeraha katika sehemu mbalimbali za mwili ikiwemo kifuani na mkononi.

Kwa mujibu wa Kamanda huyo, mwanamke anayehusishwa na tukio hilo ni Mwajuma Shaban Mwenye umri wa Miaka 24 ambaye pia ni mkazi wa mtaa huo na alikuwa akiishi pamoja na David kama mke na mume.

Amesema chanzo cha tukio hilo kinadaiwa kuwa ni wivu wa mapenzi, ambapo mwanamke huyo alidai kuwa alimkopesha mume wake kiasi cha shilingi 80,000 na baadaye kuhisi kuwa fedha hizo ameenda kuzigawa kwa wanawake wengine.

Kamanda Magomi amesema kuwa majeruhi anaendelea kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Manispaa ya Shinyanga huku uchunguzi ukiendelea ili mtuhumiwa aweze kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.

Kamanda huyo amelaani kitendo hicho na kutoa wito kwa wanandoa na jamii kwa ujumla kuepuka vitendo vya ukatili na badala yake kutatua migogoro kwa kufuata taratibu za kisheria.

Amesema Jeshi la Polisi lina madawati maalum yanayoshughulikia ukatili wa kijinsia na kusisitiza kuwa ukatili unaweza kuwakumba wanawake, watoto pamoja na wanaume.

Wakati huo huo, Mwandishi wetu amefika katika eneo la tukio na kuzungumza na baadhi ya majirani wakiwemo wapangaji wenzake Cesilia John, Lucy Shija pamoja na jirani Bi. Rosemary Mboje, ambao wamethibitisha kutokea kwa tukio hilo majira ya saa sita usiku.

Majirani hao wamesema hawakuwa na taarifa ya mgogoro wowote kati ya wanandoa hao kabla ya tukio hilo kutokea, ambapo wameeleza kuwa baada ya tukio hilo walifanikiwa kumzuia mwanamke huyo ili asikimbie hadi jeshi la Polisi lilipofika.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Wasafirishaji Bodaboda Mitumbani Kata ya Ngokolo, Jacobo Msimbang’ombe, amesema amesikitishwa na tukio hilo lililompata mwanachama wao na kuwataka madereva wa bodaboda kushirikishana changamoto wanazokutana nazo ili kupata suluhisho kabla ya madhara makubwa kutokea.

Naye Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mageuzi, Vitalis Mugisha, amesema alipigiwa simu na mmiliki wa nyumba aliyopanga David na kufika katika eneo la tukio kabla ya kutoa taarifa kwa viongozi mbalimbali ikiwemo Jeshi la Polisi ili hatua zaidi zichukuliwe.

Ametoa wito kwa wananchi kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi na badala yake kutumia njia za kisheria kutatua migogoro.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO MACHI 11,2026


Magazeti











Share:

Tuesday, 10 March 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE MACHI 10, 2026

Share:

Monday, 9 March 2026

DAWA ZA UHAKIKA ZA ULINZI WA MWILI NA NYUMBA 'ZINDIKO ZITO'


Je, unahisi kuna nguvu zisizoeleweka zinakufuata?

Je, nyumba yako inakosa amani au biashara haikui?

Dr. Sudai “Ng’wana Gama” anatoa dawa za kienyeji zenye nguvu za ulinzi wa mwili na nyumba, kupitia zindiko la asili lenye nguvu kubwa za kiroho.

Huduma zinazopatikana:
✔ Ulinzi wa mwili dhidi ya nguvu hasi
✔ Kufunga njia za wachawi na majambazi
✔ Kuweka kinga ya kiroho kwenye nyumba au biashara
✔ Kuondoa mikosi na mapepo
✔ Kuvutia mafanikio na baraka

📍 Huduma zinapatikana Maswa – Simiyu
📞 Wasiliana: +255 676 444 408 au 0624333380

Share:

WANAZUONI WAHIMIZA WAISLAMU KUTOA ZAKA KUPAMBANA NA UMASKINI


Mwenyekiti wa Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu, Sheikh Abdallah Swallehe Ndauga.

***
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu, Sheikh Abdallah Swallehe Ndauga, amewahimiza Waislamu kutekeleza ipasavyo ibada ya Zaka ili kusaidia kupunguza umasikini katika jamii.

Akizungumza katika kongamano la wanazuoni wa Kiislamu lililofanyika katika ukumbi wa Dar es Salaam Youth Centre (DYCC) jijini Dar es Salaam, Sheikh Ndauga alisema Zaka ni moja ya ibada muhimu inayolenga kuwasaidia watu wenye uhitaji katika jamii.
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu, Sheikh Abdallah Swallehe Ndauga.


Alisema kwa mujibu wa mafundisho ya dini ya Kiislamu, Zaka imewekwa mahsusi ili kuwainua watu wasiojiweza pamoja na kuimarisha mshikamano wa kijamii miongoni mwa waumini wa dini hiyo.


Sheikh Ndauga alieleza kuwa Waislamu wakitekeleza ibada hiyo kwa uaminifu na kwa kuzingatia maelekezo ya dini, inaweza kuwa nyenzo muhimu ya kupunguza umasikini na kuboresha maisha ya watu wengi.


Kwa upande wake, Sheikh Ally Zuberi akichangia mada katika kongamano hilo, alisema kumekuwepo na dhana potofu miongoni mwa baadhi ya Waislamu kuhusu walengwa wa Zaka.

Alisema baadhi ya watu wamekuwa wakidai kuwa Zaka inapaswa kutolewa kwa yatima pekee bila kuzingatia mafundisho sahihi ya Kiislamu kuhusu makundi yanayostahili kupewa Zaka.


Sheikh Zuberi alifafanua kuwa katika mafundisho ya Kiislamu, yatima hawakutajwa moja kwa moja miongoni mwa makundi ya wanaostahili kupewa Zaka isipokuwa pale wanapokuwa katika hali ya umasikini.


Wanazuoni hao walisisitiza umuhimu kwa Waislamu kujifunza na kuelewa kwa usahihi mafundisho ya dini kuhusu utoaji wa Zaka ili kuhakikisha ibada hiyo inatekelezwa kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa.















Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger