Friday, 11 September 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI SEPTEMBA 12, 2026

Share:

TANZANIA-CHINA KUIMARISHA USHIRIKIANO KWENYE SEKTA YA MADINI



▪️Waziri Mavunde na Waziri Dkt. Dachun waongoza majadiliano ya ushirikiano

▪️Watanzania kujengewa uwezo wa Kijiolojia na Tafsiri ya taarifa za utafiti madini

▪️China-Tanzania kushirikiana kwenye utafiti wa Madini Tabora,Singida,Shinyanga na Dodoma

▪️Matumizi ya Teklonojia ya kisasa ya uchimbaji yatawala majadiliano


TIANJIN, CHINA

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China zakubaliana kuimarisha ushirikiano katika sekta ya madini ili kuinua uchumi wa wananchi wa mataifa yote.

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 11 Septemba, 2026 na Waziri wa Madini, *Mheshimiwa Anthony Mavunde (Mb)* alipokutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Maliasili wa China, Mheshimiwa Dkt. Xu Dachun katika ukumbi wa mikutano wa Serikali Jijini Tianjin, China.

Katika mazungumzo hayo, Waziri Mavunde alibainisha kuwa Serikali ya China kupitia Taasisi ya Jiolojia ya China imekubali kujenga uwezo wa wataalam wa Tanzania kijiolojia na namna ya kutafsiri kwa usahihi taarifa za utafiti wa madini.

"Dhamira ya Rais wetu  Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuona sekta ya madini inakua na kuongeza mchango wake kwenye uchumi wa nchi yetu. Ndiyo maana, Mhe. Rais ameipa sekta ya madini kipaumbele cha juu hususan katika utafiti wa kijiolojia ili kuongeza tija ya uchimbaji na manufaa kwa wananchi wa Taifa letu na uchumi kwa ujumla"

Aidha, Mhe. Mavunde alieleza kuwa China kupitia fedha za msaada (Grants) ipo mbioni kushirikiana na Tanzania katika kufanya utafiti wa kina wa madini wa kurusha ndege (High resolution airborne geophisical survey) katika bloku ya Kati inayojumuisha Mikoa ya Dodoma, Tabora, Singida na Shinyanga.

Pamoja na masuala mengine, mazungumzo hayo pia yalijikita kwenye majadiliano ya namna ya kubadilishana uzoefu na utaalam katika matumizi ya teknolojia kwenye uendelezaji wa shughuli za madini ikiwa ni pamoja na uimarishaji wa mfumo wa utolewaji wa leseni.

Kwa upande wake, Dkt. Xu Dachun Naibu Waziri wa Maliasili wa China ambaye pia ndiye Rais wa Taasisi ya Utafiti wa Jiolojia ya China (CGS) alishukuru kwa Tanzania kushiriki mkutano wa Madini China na kusisitiza kwamba yupo tayari kuendelea kutoa ushirikiano kwa Serikali ya Tanzania katika kubadilishana uzoefu utakaosaidia kuendeleza sekta zetu za madini.

Pia, Dkt. Dachun alisisitiza kuwa ushirikiano baina ya Tanzania ni China una maana kubwa na manufaa kwa pande zote mbili za Nchi kwani Tanzania ina fursa nyingi za uwekezaji wakati China ina teknolojia na mitaji, hivyo ushirikiano wa Nchi hizi ni wazi utaleta manufaa yenye tija kwa wananchi wa Nchi zote mbili.







Share:

SHEIKH WA DODOMA ATOA AGIZO LA DUA MAALUMU MISIKITINI



Na Mwandishi wetu, Dodoma

Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) Mkoa wa Dodoma limewaagiza Masheikh na Maimamu wote wa misikiti mkoani humo kufanya dua maalumu kwa ajili ya kuombea taifa na kuendelea kuomba mvua, kutokana na changamoto ya mabadiliko ya hali ya hewa yanayotarajiwa.

Agizo hilo limetolewa leo Septemba 11,2026 na Sheikh wa Mkoa wa Dodoma, Alhaji Dkt. Mustafa Rajabu Shabani, ambaye amewataka Masheikh na Maimamu wote wa misikiti mkoani Dodoma kutekeleza dua hizo kuanzia Ijumaa, Septemba 11, 2026, baada ya Swala ya Ijumaa na kuendelea.

Sheikh Dkt. Shabani,amesema dua hiyo ina mambo mawili muhimu, ikiwemo kumuombea Marehemu Mzee Hafidh Ameir Mume, aliyekuwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Amesema ni muhimu kwa viongozi na waumini wa dini ya Kiislamu kumuombea marehemu huyo, huku akiwataka Masheikh na Maimamu kuhakikisha dua hiyo inafanyika katika misikiti mbalimbali mkoani Dodoma.

Aidha, Sheikh Dkt. Shabani ametoa agizo la kufanyika kwa dua endelevu ya kuliombea taifa kupukana na janga la mvua za El-Nino, ambazo zinatajwa kuwa na uwezekano wa kuleta athari kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa.

Amesema dua hiyo inapaswa kuendelea kufanyika kwa mujibu wa mamlaka za hali ya hewa na taarifa zinazotolewa kuhusu mwenendo wa hali ya hewa nchini.




Share:

TANZANIA, MAREKANI KUENDELEZA USHIRIKIANO KATIKA SEKTA ZA MAENDELEO

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb) akisalimiana na Naibu Katibu wa Hazina ya Marekani anayeshughulikia Masuala ya Kimataifa, Bi. Erin Browne, mjini Nairobi, Kenya, kando ya Jukwaa la Mazungumzo ya Ngazi za Juu la Mawaziri wa Fedha kuhusu kuimarisha uwekezaji wa pamoja katika sekta ya afya.


***************

Na. Peter Haule, WF, Nairobi, Kenya

Tanzania na Marekani zimeeleza dhamira ya kuendelea kuimarisha ushirikiano katika sekta mbalimbali za maendeleo, ikiwemo afya, kilimo, nishati, madini, miundombinu, elimu na utalii.

Dhamira hiyo imeelezwa wakati Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb), alipokutana na kufanya mazungumzo na Naibu Katibu wa Hazina ya Marekani anayeshughulikia Masuala ya Kimataifa, Bi. Erin Browne, mjini Nairobi, Kenya, kando ya Jukwaa la Mazungumzo ya Ngazi za Juu la Mawaziri wa Fedha kuhusu kuimarisha uwekezaji wa pamoja katika sekta ya afya.

Katika mazungumzo hayo, Mhe. Luswetula amezialika kampuni na wawekezaji kutoka Marekani kutumia fursa mbalimbali za uwekezaji zinazopatikana Tanzania, akitaja maeneo ya kilimo, nishati, madini, miundombinu, afya, elimu na utalii.

Aidha, Mhe. Luswetula ameishukuru Serikali ya Marekani kwa kuendelea kushirikiana na Tanzania pamoja na mchango wake katika maeneo mbalimbali ya maendeleo tangu kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya nchi hizo mwaka 1968.

Amesema ushirikiano huo umekuwa na mchango katika juhudi za Tanzania za kukuza maendeleo ya kijamii na kiuchumi na kupunguza umaskini.

Kwa upande wake, Naibu Katibu wa Hazina ya Marekani anayeshughulikia Masuala ya Kimataifa, Bi. Erin Browne, amesema Marekani itaendelea kushirikiana na Tanzania katika maeneo mbalimbali ya maendeleo, pamoja na kuimarisha na kukuza ushirikiano uliopo baina ya nchi hizo.

Mazungumzo hayo yameangazia pia umuhimu wa kuendelea kujenga ushirikiano wa kiuchumi na uwekezaji kati ya Tanzania na Marekani kwa manufaa ya wananchi wa nchi hizo mbili.
Naibu Katibu wa Hazina ya Marekani anayeshughulikia Masuala ya Kimataifa, Bi. Erin Browne, mjini Nairobi, Kenya, akizungumza kuhusu ushirikiano wa maendeleo wakati wa mkutano na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb), kando ya Jukwaa la Mazungumzo ya Ngazi za Juu la Mawaziri wa Fedha kuhusu kuimarisha uwekezaji wa pamoja katika sekta ya afya.
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb) (katikati), akieleza fursa za uwekezaji wakati wa mkutano na Naibu Katibu wa Hazina ya Marekani anayeshughulikia Masuala ya Kimataifa, Bi. Erin Browne kando ya Jukwaa la Mazungumzo ya Ngazi za Juu la Mawaziri wa Fedha Afrika, kuhusu kuimarisha uwekezaji wa pamoja katika sekta ya afya, wengine ni wajumbe walioambatana nae kutoka Tanzania.
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb) (wa pili kushoto) na Naibu Katibu wa Hazina ya Marekani anayeshughulikia Masuala ya Kimataifa, Bi. Erin Browne (wa pili kulia) wakiwa katika mkutano kati yao, kando ya Jukwaa la Mazungumzo ya Ngazi za Juu la Mawaziri wa Fedha Afrika, kuhusu kuimarisha uwekezaji wa pamoja katika sekta ya afya.
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb) na Naibu Katibu wa Hazina ya Marekani anayeshughulikia Masuala ya Kimataifa, Bi. Erin Browne wakiteta jambo, kando ya Jukwaa la Mazungumzo ya Ngazi za Juu la Mawaziri wa Fedha Afrika, kuhusu kuimarisha uwekezaji wa pamoja katika sekta ya afya.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha)

Share:

Thursday, 10 September 2026

MATUNDA YA AWAMU YA SITA: VETA KUZINDUA SIMU YA ‘UJUZI Pro’


Uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan katika sekta ya elimu na mafunzo ya ufundi stadi umeanza kuzaa matunda yanayoonekana kupitia Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), ikiongozwa na mafanikio makubwa katika uvumbuzi wa kiteknolojia, uzalishaji, na kukuza ujuzi kwa nguvukazi ya taifa.

Akizungumza jijini Dodoma, Mkurugenzi Mkuu wa Veta, Anthony Kasore, alieleza kuwa mamlaka hiyo iko katika hatua za mwisho kabisa za kuingiza rasmi sokoni simu ya mkononi ya kwanza ya kizalendo iitwayo Ujuzi Pro, hatua iliyofikiwa baada ya kukamilisha taratibu zote muhimu na kupata kibali rasmi kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), jambo ambalo ni kielelezo tosha cha uwezo wa wataalamu wa ndani unaochochewa na mazingira wezeshi ya serikali.

Sambamba na hilo, mafanikio hayo yameonekana katika kukuza ujuzi viwandani kupitia ushirikiano na viwanda 16 uliowezesha kutoa mafunzo maalum kwa wafanyakazi 600 na kuongeza tija mahali pa kazi, pamoja na kuwawezesha wananchi 4,465 wakiwemo wajasiriamali wa sekta ya uvuvi kupitia mafunzo yaliyogharamiwa na serikali.

Veta pia imeendelea kuboresha mitaala yake kwa kuandaa mitaala mipya 29 inayokidhi mahitaji ya soko la ajira, ikiwemo ya sekta ya vioo na alumini pamoja na usimamizi na urejelezaji wa taka.

Katika kukuza ubunifu na teknolojia, mamlaka imeratibu bunifu zaidi ya 120 kutoka kwa wanafunzi na wakufunzi, ambapo bunifu 17 zimeshaboreshwa na kuingizwa sokoni kwa ajili ya kuzalishwa kwa wingi, huku mfumo wa kidijiti wa Fundi Connect ukianzishwa ili kuwasajili mafundi rasmi na kuwaunganisha na wateja.

Mafanikio haya yanathibitisha kwa vitendo dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kujenga uchumi unaotegemea maarifa, teknolojia na viwanda.


Share:

Wednesday, 9 September 2026

WAANDISHI WA HABARI WAPEWA MAFUNZO YA UBUNIFU UNAOMLENGA MTUMIAJI (HCD) KUKABILIANA NA HABARI POTOFU

Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya teknolojia na habari ya Nukta Africa, Nuzulack Dausen akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya teknolojia na habari ya Nukta Africa, Nuzulack Dausen, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Programu Meneja wa International Media Support (IMS), Fausta Musokwa, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Mwezeshaji wa mafunzo hayo kuhusu Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD), Dkt. Hellen Maziku, Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mwanzilishi wa HCD Services Tanzania, akizungumza wakati wa mafunzo hayo.


Na Waandishi wetu - Malunde 1 blog

 Waandishi wa habari, wahariri na wataalamu wa masoko na biashara kutoka taasisi 10 za habari nchini Tanzania wamejengewa uwezo wa kukabiliana na taarifa potofu na za upotoshaji kupitia mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (Human-Centred Design - HCD), yanayolenga kuwasaidia kutambua changamoto zinazohusiana na taarifa potofu na kubuni suluhisho zinazozingatia mahitaji, uzoefu na tabia za watumiaji wa taarifa.

Mafunzo hayo ya siku tatu yanafanyika jijini Arusha kuanzia Septemba 9 hadi 11, 2026, yakiendeshwa na Shirika la International Media Support (IMS) kwa kushirikiana na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), JamiiAfrica na Nukta Africa.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Nukta Africa, Nuzulack Dausen, amesema taarifa sahihi ni jambo nyeti katika jamii kwa kuwa zina nafasi kubwa katika kusaidia wananchi na taasisi kufanya maamuzi sahihi kwa ajili ya maendeleo.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya teknolojia na habari ya Nukta Africa, Nuzulack Dausen, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu.

Dausen ameeleza kuwa, kuenea kwa taarifa potofu kunaweza kuathiri sekta mbalimbali na kuhatarisha ustawi wa jamii, hivyo ni muhimu kwa waandishi wa habari kuwa na ujuzi na mbinu za kisasa za kubaini na kukabiliana na taarifa hizo.

Ameongeza kuwa, mafunzo hayo yanatoa fursa kwa wadau wa habari kujengeana uwezo na kubadilishana uzoefu kuhusu mbinu za kisasa za kukabiliana na habari potofu katika vyombo vya habari, kwa lengo la kusaidia jamii kupata taarifa sahihi na kufanya maamuzi yenye tija kwa maendeleo yao.

Amesema Mafunzo hayo ni sehemu ya programu ya Maabara ya Fikra Bunifu na Uvumbuzi (Design Thinking and Innovation Lab) inayosimamiwa na IMS na washirika wake, ikiwa na lengo la kuwajengea washiriki uelewa na uwezo wa kutumia kanuni, hatua na mbinu za HCD katika kutambua na kutatua changamoto zinazohusiana na taarifa potofu.

Kwa upande wake, Programu Meneja wa International Media Support (IMS), Fausta Musokwa, amesema taasisi hiyo inashirikiana na wadau wa habari nchini Tanzania katika kutekeleza mradi unaolenga kukabiliana na misinformation na disinformation, ili kusaidia vyombo vya habari kuwa na mbinu sahihi za kuelimisha jamii na kukabiliana na taarifa zinazoweza kupotosha umma.
Programu Meneja wa International Media Support (IMS), Fausta Musokwa.

Musokwa amesema juhudi hizo ni muhimu katika kuongeza uwezo wa vyombo vya habari kukabiliana na changamoto ya taarifa potofu, hasa katika kipindi ambacho teknolojia za mawasiliano zimefanya taarifa kusambaa kwa kasi kubwa.

Musokwa amesema kuenea kwa taarifa potofu na maudhui ya chuki ni miongoni mwa changamoto zinazozidi kujitokeza duniani, huku ukuaji wa matumizi ya simu janja na upatikanaji mpana wa intaneti, sambamba na viwango vya chini vya uelewa wa mfumo wa taarifa, ukiongeza uwezekano wa kusambaa kwa taarifa zisizo sahihi na zinazopotosha hivyo ni wajibu wa vyombo vya habari kuwa mstari wa mbele kulinda jamii ipate taarifa sahihi ili ifanye maamuzi sahihi.

Amebainisha kuwa, hali hiyo inaweza kuleta madhara kwa watu binafsi na jamii kwa ujumla, ikiwemo kuathiri namna wananchi wanavyofanya maamuzi kuhusu masuala mbalimbali yanayogusa maisha yao.

Naye Mwezeshaji wa mafunzo hayo, Dkt. Hellen Maziku, Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mwanzilishi wa HCD Services Tanzania, amesema mafunzo hayo yanasisitiza umuhimu wa kutumia mtazamo unaomlenga mtumiaji katika kutafuta suluhisho la changamoto ya taarifa potofu.

Amesema mtazamo huo unazingatia mahitaji, matarajio, uzoefu na tabia za wananchi wanaokumbwa na changamoto ya taarifa potofu, hatua inayolenga kuhakikisha suluhisho zinazobuniwa zinakidhi mahitaji halisi ya watumiaji wa taarifa.

Kwa upande wao, washiriki wa mafunzo hayo wamesema yatawasaidia kupata uelewa na mbinu mbalimbali zitakazowasaidia kutambua, kuchambua na kukabiliana na habari potofu na taarifa za upotoshaji katika kazi zao za kila siku.


Wamesema mafunzo hayo yatawasaidia kuongeza umakini katika kuchakata taarifa kabla ya kuzifikisha kwa wananchi, hatua ambayo itachangia kuimarisha uaminifu wa jamii kwa vyombo vya habari na kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi na zenye manufaa kwa maisha yao.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya teknolojia na habari ya Nukta Africa, Nuzulack Dausen, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya teknolojia na habari ya Nukta Africa, Nuzulack Dausen akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya teknolojia na habari ya Nukta Africa, Nuzulack Dausen, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya teknolojia na habari ya Nukta Africa, Nuzulack Dausen, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya teknolojia na habari ya Nukta Africa, Nuzulack Dausen, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya teknolojia na habari ya Nukta Africa, Nuzulack Dausen, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya teknolojia na habari ya Nukta Africa, Nuzulack Dausen akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Programu Meneja wa International Media Support (IMS), Fausta Musokwa, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Programu Meneja wa International Media Support (IMS), Fausta Musokwa, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Programu Meneja wa International Media Support (IMS), Fausta Musokwa, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Programu Meneja wa International Media Support (IMS), Fausta Musokwa, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Programu Meneja wa International Media Support (IMS), Fausta Musokwa, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Mwezeshaji wa mafunzo hayo kuhusu Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD), Dkt. Hellen Maziku, Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mwanzilishi wa HCD Services Tanzania, akizungumza wakati wa mafunzo hayo.
Mwezeshaji wa mafunzo hayo kuhusu Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD), Dkt. Hellen Maziku, Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mwanzilishi wa HCD Services Tanzania, akizungumza wakati wa mafunzo hayo.
Mkurugenzi wa Malunde Media, Kadama Malunde, akichangia hoja wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger