Thursday, 22 January 2026

WANANCHI WA UKONGA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA KUDUMISHA AMANI NA USALAMA





Na Mwandishi wetu, Dar

Wananchi wa Ukonga Mkoani Dar Es Salaam wametoa pongezi na Shukrani kwa Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuimarisha amani, utulivu na usalama katika Jimbo lao la Ukonga, suala ambalo limewezesha shughuli za kiuchumi na kijamii kuendelea.

Kwaniaba ya wananchi wengine wa Jimbo hilo wakati akizungumza na Chombo chetu cha habari, Bw. Salum Issa Salum, Mkazi wa Kata ya Buyuni ameeleza kuwa licha ya kupitia baadhi ya changamoto mwishoni mwa mwaka jana, hali kwasasa ni shwari na hatua za maendeleo zimeendelea kushuhudiwa katika Kata hiyo na maeneo mengine kote Tanzania.

"Nisemee zaidi katika miundombinu, Mama amesikia kilio chetu na sasa barabara nyingi zimejengwa kwa kiwango cha lami kupitia miradi mbalimbali ikiwemo mradi wa DMDP kutoka hapa kwetu kwenda Kivule." Amesema Bw. Salum.

Katika maelezo yake, Mwananchi huyo amemuombea uhai zaidi na afya njema Rais Samia, akisisitiza pia umuhimu wa kila mwananchi kushiriki kikamilifu katika kuilinda amani ya Tanzania ili kutoa fursa ya Taifa na kila mwananchi kupiga hatua za kimaendeleo.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI JANUARI 22,2026

Share:

Wednesday, 21 January 2026

Tanzia : MUASISI NA MWENYEKITI WA KWANZA WA CHADEMA EDWIN MTEI AFARIKI DUNIA







Mwasisi na Mwenyekiti wa kwanza wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Edwin Mtei amefariki Dunia usiku wa Januari 19, 2026.




Share:

Tuesday, 20 January 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JANUARI 21, 2026

Share:

KANISA LA MLIMA WA MOTO LAZINDUA MAOMBEZI YA KUIOMBEA TANZANIA


Kanisa la Mlima wa Moto Tanzania limesema linatarajia kufanya maombezi maalum ya kuliombea Taifa la Tanzania kupitia Kongamano la Neno la Mungu lililopewa jina la Anza Mwaka na Bwana.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Kanisa la Mlima wa Moto lililopo Mikocheni B jijini Dar es Salaam, Mchungaji Samwel Hillary, ambaye ni mjumbe wa Kamati ya Maandalizi ya kongamano hilo, alisema lengo lao ni kuhakikisha Taifa linaanza mwaka likiwa karibu na Mungu, jambo lililowasukuma kuandaa kongamano hilo.
Mjumbe wa kamati ya Maandalizi ya Kongamano Mchungaji Samwel Hillary akizungumza na Waandishi wa habari katika Kanisa la Mlima wa Moto lililopo Mikocheni B jijini Dar es Salaam.

Alisema kongamano hilo litafanyika kuanzia Januari 25 hadi Februari 1, 2026, na linatarajiwa kuongozwa na Askofu Dastani Maboya, Rose Mgeta, Mchungaji Madoshi pamoja na mchungaji kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kwa lengo la kuhubiri Neno la Mungu na kuliombea Taifa ili lipate amani ya kweli pamoja na uponyaji katika maeneo mbalimbali.

Kwa upande wake, Katibu wa Kamati ya Maandalizi ya kongamano hilo, Godfrey Kazinja, alisema wameamua kuliombea Taifa ili kulinusuru na kulirejesha kwa Mungu, pamoja na kuyahamasisha vizazi na jamii kwa ujumla kuishi katika misingi ya kumpendeza Mungu.

Katibu wa kamati ya Maandalizi ya Kongamano Godfrey Kazinja akizungumza na Waandishi wa habari katika Kanisa la Mlima wa Moto lililopo Mikocheni B jijini Dar es Salaam.

Aidha, Kazinja alisema kutakuwepo na usafiri wa kuwachukua waumini kuanzia eneo la Mwenge hadi kanisani hapo, huku akiwahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi ili kupata Neno la Mungu na uponyaji.

Naye Sarah Daniel, mjumbe wa Kamati ya Maandalizi ya kongamano hilo, alisema waimbaji mbalimbali wanatarajiwa kushiriki katika tukio hilo, akiwemo John Lissu, Mchungaji Epa, Ashery na wengine wengi, huku akiwaomba Watanzania kuendelea kufuatilia taarifa kupitia vyombo mbalimbali vya habari nchini.
Mjumbe wa kamati ya Maandalizi ya Kongamano Sarah Danielakizungumza na Waandishi wa habari katika Kanisa la Mlima wa Moto lililopo Mikocheni B jijini Dar es Salaam.

Kongamano hilo ni sehemu ya jitihada za kudumisha amani na upendo miongoni mwa Watanzania, hususan mwanzoni mwa mwaka huu, kwa lengo la kuimarisha mshikamano na maadili ya upendo katika jamii.
PICHA ZOTE NA JAMES SALVATORY - TORCH MEDIA
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger