Sunday, 13 September 2026

BARRICK NORTH MARA, JUMUIYA YA WATUMIA MAJI WAFANIKISHA UPANDAJI MITI 47,200 KUHIFADHI MTO TIGHITE


Sehemu ya viongozi na wafanyakazi wa Barrick North Mara (kulia), viongozi wa Jumuiya ya Watumia Maji Mto Tighite Chini na Kijiji cha Matongo wakikagua maendeleo ya mradi huo Siku ya Mazingira Duniani 2026. (Picha za Maktaba)
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watumia Maji Mto Tighite Chini, Mwita Seri, akiwa kwenye kitalu cha miche ya asili inayooteshwa kwa ajili ya kupandwa kandokando ya Mto Tighite.
Ushirikiano wa Jumuiya ya Watumia Maji Mto Tighite (JWMT) na Kampuni ya Barrick kupitia Mgodi wake wa dhahabu wa North Mara umefanikisha upandaji wa miti ya asili 47,2000 kati ya 50,000 ambao utasaidia kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na kulinda chanzo hicho cha maji kinachotegemewa katika shughuli mbalimbali za ustawi wa jamii na utunzaji wa mazingira.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Watumiaji maji wa Mto Tighite, Bw. Mwita Seri amesema mradi huo unaotekelezwa kwa ufadhili wa Barrick North Mara unalenga kurejesha uoto wa asili na kuimarisha uhifadhi wa mto huo uliopo Nyamongo, Wilaya ya Tarime.

Amesema Tanzania kama zilivyo nchi nyingine duniani inakabiliwa na tishio la majanga yanayotokana na mabadiliko ya tabia nchi kutokana na uharibifu wa mazingira hususani kupitia kukata miti ovyo, shughuli za kilimo na kiuchumi.

Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Bw. Seri, mradi huo unalenga kurejesha uoto wa asili na kuimarisha uhifadhi wa mto huo uliopo Nyamongo, wilaya ya Tarime, mkoani Mara.

“Miti hiyo imepandwa katika eneo lenye ukubwa wa takriban ekari 40,” Seri amewaambia waandishi wa habari wilayani Tarime.

Amebainisha kuwa eneo lililopandwa miti hiyo ni sehemu ya ekari 100 za kingo za Mto Tighite zinazotakiwa kurejeshewa uoto wa asili kutokana na uharibifu wa mazingira.

Hivyo, upandaji wa miti 47,200 kwenye ekari 40 ni hatua ya awali katika safari ndefu ya kurejesha uoto wa asili wa Mto Tighite uliopo jirani na Mgodi wa North Mara.

Seri ameongeza mradi huo unatarajiwa kuchangia katika kulinda kingo za mto huo kwa kuzuia mmomonyoko wa udongo na kurejesha mazingira ya asili yaliyoharibiwa.

Mwenyekiti huyo wa Jumuia ya Watumia Maji, alitumia nafasi hiyo pia kuishukuru Barrick North Mara kwa kutoa shilingi milioni 36.7 kuwezesha uanzishaji na utekelezaji wa awali wa mradi huo.

“Barrick wamesaidia sana kufanikisha mradi huu, kwani fedha hizo ziligharamia uoteshaji wa miche ya miti ya asili, upandaji, ulinzi wa awali wa miti hiyo na uwekaji wa nguzo za chuma za uzio wa mradi huo,” amesema Seri.

Aidha, Seri ametoa wito kwa jamii zinazozunguka mto huo kuunga mkono mradi huo kwa kuhakikisha kuwa unafanikiwa bila kuhujumiwa kwa namna yoyote ile.

“Jamii inayozunguka Mto Tighite nayo ina wajibu wa kuonesha ushirikiano na juhudi za kulinda miti iliyopandwa ili iweze kukua na kutimiza lengo la kurejesha uoto wa asili wa mto wetu,” ameeleza.

Pia, amesisitiza umuhimu wa kuendelea kuwezesha mradi huo kifedha na kitaalamu ili kuhakikisha mafanikio yaliyoanza kuonekana yanaendelea kudumu na kuleta matokeo chanya ya muda mrefu kwa mazingira na jamii.

Mradi wa kurejesha uoto wa asili wa Mto Tighite unatajwa kuwa na umuhimu mkubwa wa kimazingira kutokana na nafasi ya chanzo hicho cha maji katika mfumo wa ikolojia ya eneo hilo.

Ulizinduliwa wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani mwaka jana kwa lengo la kurejesha uoto wa asili wa mto huo unaotegemewa na maelfu ya watu kwa ajili ya maji ya matumizi ya nyumbani, kunywesha mifugo na shughuli za kilimo.

Hivi karibuni Mgodi wa North Mara uliungana na Jumuiya ya Watumia Maji Tighite Chini na wakazi wa kijiji cha Matongo kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani, kwa kutembelea na kukagua maendeleo ya mradi huo.

Wadau hao, wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kijiji cha Matongo, Charles Ryoba, walieleza kuridhishwa na ukuaji wa miti iliyopandwa na hatua zinazochukuliwa kurejesha uoto wa asili wa mto huo baada ya kuathiriwa na ukataji wa miti ovyo.

Ushirikiano wa Barrick North Mara na jumuiya hiyo unaweka msingi wa hatua zaidi za kuhusisha jamii, taasisi na wadau wengine katika kukamilisha upandaji wa miti ya asili kwenye ekari 100 za kingo za Mto Tighite.

Mto Tighite ni miongoni mwa vyanzo muhimu vinavyochangia maji katika Mto Mara ambao unamwaga maji yake katika Ziwa la kimataifa - Ziwa Victoria upande wa Tanzania.

Mbali na uwezeshaji wa kupanda miti maeneo yam to Tigheti , Barrick North Mara imekuwa mstari wa mbele kutekeleza sera ya kulinda mazingira kwa kuhakikisha inatumia uzalishaji kwa kutumia mifumo isiyoharibu mazingira sambamba na kushiriki kutoa elimu ya kulinda mazingira na vyanzo vya maji.

Vilevile wafanyakazi wake wamekuwa mstari wa mbele kushiriki katika miradi mbalimbali ya utunzaji wa mazingira.


Share:

UCHAGUZI VIONGOZI WAPYA BURUNGE WMA WAANZA

Mkuu wa idara Ulinzi na mahusiano Chem chem Charles Sylivester akimkabidhi kadi ya gari Mkurugenzi wa halmshauri ya Babati vijijini ,Anna Mbogo kwa ajili ya kazi za uhifadhi Burunge WMA
Mkurugenzi halmashauri Babati vijijini Anna Mbogo



Mwandishi wetu, Babati

Halmashauri ya Babati vijijini, imetangaza kuanza  kwa uchaguzi wa viongozi wapya katika eneo la Hifadhi ya  Jamii ya  Wanyamapori ya Burunge,baada ya kukamilika maboresho ya Katiba ili kuifanya hifadhi hiyo kuwa bora barani Afrika.

Burunge WMA ipo kati kati ya hifadhi ya Taifa ya Tarangire na Hifadhi ya Taifa ya Manyara , mkoa wa Manyara  chini ya usimamizi wa halmashauri ya Babati na Mamlaka ya usimamizi wanyamapori ( TAWA).          

Uchaguzi huo unafanyika baada ya kusimamishwa viongozi waliokuwepo madarakani kwa tuhuma kadhaa na baadae kumaliza muda wao.

Akizungumza na waandishi wa habari za Utalii na Uhifadhi wilayani Babati, Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Babati vijijini,Anna Mbogo  jana amesema, chaguzi  maboresho hayo yanafanyika pia kuendana na dhamira ya Rais, Dkt.Samia Suluhu Hassan, kuongeza mapato ya Taifa kupitia Utalii.

Mbogo anasema tayari  maboresho ya Katiba na mfumo wa uendeshaji Burunge WMA umekamilika na sasa chaguzi  za viongozi wa jumuiya hiyo, zimeanza katika vijiji 10 vinavyounda jumuiya hiyo.

Anasema vijiji hivyo ni, Mwada.Sangaiwe,Vilima Vitatu,Ngoley,Kakoi,Olasiti ,Manyara,Magara,Maweni
na Minjingu.

"Chaguzi zimeanza tunatarajia zikikamilika tutapa viongozi bora ambao wataweza kuja kusimama Uhifadhi, Utalii na kubwa kuongeza mapato ya Utalii kwa manufaa ya vijiji na serikali kwa ujumla",anasema.

Anasema Rais wa Jamuhuri ya Muungano, Dkt Samia Suluhu Hassan, tayari ilikamilisha kazi ya kuitangaza Tanzania kupitia filamu ya Royal Tour hivyo, sasa kazi iliyopo ni kuweka mazingira mazuri ya kuvutia watalii katika maene yote yaliyohifadhiwa.

Mkurugenzi huyo anasema, katika eneo la Burunge WMA tayari matunda ya uhifadhi yameanza kuonekana baada ya hivi karibuni, hoteli ya Chem chem iliyopo  ndani ya hifadhi hiyo, kushinda tuzo ya Safari Luxury lodge Afrika na Tanzania tuzo zilizotolewa na shirika la Utalii duniani la WTA.

"Tuzo hii inaendelea kuitangaza Burunge WMA vizuri na itavutia watalii zaidi na tunaomba na wawekezaji wengine katika eneo hili kuboresha huduma zao ili kuendelea kuvutia watalii",anasema.       

Mbogo amewataka wananchi wenye sifa na nia ya dhati kuendeleza uhifadhi na Utalii katika vijiji hivyo kujitokeza kugombea nafasi mbali mbali.

Kwa upande wake, Meneja Mkuu wa Chem chem, Clever Zulu anasema, lengo lao ni kuifanya WMA ya burunge kuwa bora barani  Afrika, kwa kuwa na vivutio vingi vya utalii, huduma bora ya malazi na kubwa kuhifadhiwa vizuri.

"Hili ndio lengo kubwa la wakurugenzi wa chem chem Nicolaus Negri na Fabia Bausch kuifanya Burunge WMA kuwa bora na ushindi wa tuzo ni sehemu ya mikakati lakini pia sasa tumeanza kupokea maafisa wa uhifadhi maeneo kadhaa Afrika kuja kujifunza hapa",anasema.

Anasema hifadhi hiyo, kwa sasa wanyama wameongezeka, ujangili umedhibitiwa na wananchi wananufaika sana na uhifadhi kupitia fedha zinazokusanywa.

Spika wa Burunge WMA, Erick Lilayoni ambaye anamaliza muda wake, anasema mapato ya Burunge WMA yamekuwa yakiongezeka hadi kufikia takriban billion 4 kwa mwaka na vijiji vimekuwa vikipata mgao zaidi ya millioni 200 kwa mwaka.

"Binafsi sitarajii kugombea tena uongozi lakini naamini eneo hili tukilitunza vizuri, manufaa makubwa yataendelea kupatikana kwa wananchi wa vijiji 10 na serikali kwa ujumla",anasema.

Share:

Saturday, 12 September 2026

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA ATEMBELEA KIWANJA CHA UJENZI WA VIWANGO HOUSE ARUSHA


Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Denis Londo (Mb), ametembelea kiwanja kinachotarajiwa kujengwa Viwango House eneo la Mateves, Mkoani Arusha.
Ziara hiyo imelenga kujionea eneo lililotengwa kwa ajili ya ujenzi wa ofisi hizo, pamoja na kufahamu hatua zinazofikiwa katika maandalizi ya utekelezaji wa mradi huo.

Ujenzi wa Ofisi za TBS Mateves unatarajiwa kuimarisha upatikanaji wa huduma za viwango na uhakiki wa ubora kwa wananchi, wafanyabiashara na wazalishaji wa bidhaa katika Mkoa wa Arusha na maeneo jirani.

Aidha, uwepo wa ofisi katika eneo hilo utasaidia kusogeza huduma za TBS karibu zaidi na wadau, kuongeza ufanisi wa utoaji wa huduma na kuimarisha utekelezaji wa majukumu ya Shirika katika kuhakikisha bidhaa na huduma zinazotumika nchini zinakidhi matakwa ya viwango.
Share:

WIZARA , TAASISI ZATAKIWA KUCHUKUA HATUA KUKABILIANA NA MVUA ZA EL NIÑO


OWM –TAMISEMI, Dar es Salaam  

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Deogratius Ndejembi leo Septemba 11, 2026 amezitaka Wizara, Mamlaka na Taasisi zinazohusika na majanga kuchukua hatua za haraka kujiandaa ili kuzuia na kupunguza athari zinazoweza kusababishwa na mvua za El Niño zinazotarajiwa kuanza mwezi Oktoba hadi Desemba 2026. 
 
Makamu wa Rais ametoa maagizo hayo kwa taasisi hizo katika kikao kilichofanyika Ofisi ya Makamu wa Rais Jijini Dar es Salaam, ambapo kwa upande wa Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI yamepokelewa na Waziri Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, mara baada ya ofisi yake na taasisi zinazohusika kuchukua hatua za haraka, kuwasilisha taarifa ya utayari na maandalizi ya Serikali katika kukabiliana na madhara ya mvua hizo, kufuatia tahadhari iliyotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania.

Katika kikao kazi hicho, Makamu wa Rais, Mhe. Ndejembi ameagiza wataalamu kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Wizara ya Ujenzi pamoja na Taasisi zilizo chini ya Wizara hizo kuhakikisha zinafanya kampeni maalum ya usafi katika miundombinu ya barabara na mifereji ya maji.

“Ifanyike kampeni ya haraka, mikondo na mifereji ya maji izibuliwe, na barabara ziandaliwe,” amesisitiza Makamu wa Rais.
 
Aidha, Makamu wa Rais Mhe.  Ndejembi, ameelekeza taka, tope na udongo unaotolewa baada ya kuzibua mitaro na mifereji katika maeneo mbalimbali kuondolewa mara moja na kutupwa katika maeneo yaliyotengwa, badala ya kuachwa kandokando ya barabara ambako taka, tope na udongo huo zinaweza kurejea kwenye mifereji wakati mvua zinapoanza.
 
Makamu wa Rais pia amezitaka Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI, Wizara ya Ujenzi pamoja na Taasisi zilizo chini ya Wizara hizo, kufanya kazi kwa pamoja ya kujiandaa ili kuzuia na kupunguza athari zinazoweza kusababishwa na mvua za El Niño.


Akipokea maagizo hayo kwa ajili ya utekelezaji, Waziri wa Nchi, OWM – TAMISEMI Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amemueleza Mhe. Makamu wa Rais kuwa ofisi yake imeshaanza kutekeleza maelekezo ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuboresha usafi wa mazingira katika majiji aliyoyatoa Septemba 02, 2026 wakati akiwaapishwa Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala aliowateua Agosti 27, 2026.

Prof. Shemdoe amemtaarifu Makamu wa Rais Mhe. Ndejembi kuwa, Septemba 07, 2026 alifanya kikao kazi na Wakuu wa Mikoa yenye majiji, viongozi wa majiji na manispaa za Mkoa wa Dar es Salaam na kuwataka kuhakikisha  wanatekeleza  kampeni maalum ya wiki mbili ya usafi wa mazingira  katika majiji ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ya Mheshimiwa Rais.

Akianisha namna ofisi yake itakavyotekeleza maelekezo ya Makamu wa Rais ya kujiandaa na kukabiliana na athari za mvua za El Niño, Prof. Shemdoe amewasilisha kwa Makamu wa Rais Mhe.  Ndejembi, mkakati wa ofisi yake kupitia TARURA ulioandaliwa kwa ajili ya kujiaanda, kuzuia na kupambana na madhara ya uharibifu wa miundombinu ya barabara unaoweza kutokana na mvua za El Niño, ambao umeanisha namna utakavyotekelezwa.









Share:

Friday, 11 September 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI SEPTEMBA 12, 2026

Share:

TANZANIA-CHINA KUIMARISHA USHIRIKIANO KWENYE SEKTA YA MADINI



▪️Waziri Mavunde na Waziri Dkt. Dachun waongoza majadiliano ya ushirikiano

▪️Watanzania kujengewa uwezo wa Kijiolojia na Tafsiri ya taarifa za utafiti madini

▪️China-Tanzania kushirikiana kwenye utafiti wa Madini Tabora,Singida,Shinyanga na Dodoma

▪️Matumizi ya Teklonojia ya kisasa ya uchimbaji yatawala majadiliano


TIANJIN, CHINA

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa China zakubaliana kuimarisha ushirikiano katika sekta ya madini ili kuinua uchumi wa wananchi wa mataifa yote.

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 11 Septemba, 2026 na Waziri wa Madini, *Mheshimiwa Anthony Mavunde (Mb)* alipokutana na kufanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Maliasili wa China, Mheshimiwa Dkt. Xu Dachun katika ukumbi wa mikutano wa Serikali Jijini Tianjin, China.

Katika mazungumzo hayo, Waziri Mavunde alibainisha kuwa Serikali ya China kupitia Taasisi ya Jiolojia ya China imekubali kujenga uwezo wa wataalam wa Tanzania kijiolojia na namna ya kutafsiri kwa usahihi taarifa za utafiti wa madini.

"Dhamira ya Rais wetu  Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuona sekta ya madini inakua na kuongeza mchango wake kwenye uchumi wa nchi yetu. Ndiyo maana, Mhe. Rais ameipa sekta ya madini kipaumbele cha juu hususan katika utafiti wa kijiolojia ili kuongeza tija ya uchimbaji na manufaa kwa wananchi wa Taifa letu na uchumi kwa ujumla"

Aidha, Mhe. Mavunde alieleza kuwa China kupitia fedha za msaada (Grants) ipo mbioni kushirikiana na Tanzania katika kufanya utafiti wa kina wa madini wa kurusha ndege (High resolution airborne geophisical survey) katika bloku ya Kati inayojumuisha Mikoa ya Dodoma, Tabora, Singida na Shinyanga.

Pamoja na masuala mengine, mazungumzo hayo pia yalijikita kwenye majadiliano ya namna ya kubadilishana uzoefu na utaalam katika matumizi ya teknolojia kwenye uendelezaji wa shughuli za madini ikiwa ni pamoja na uimarishaji wa mfumo wa utolewaji wa leseni.

Kwa upande wake, Dkt. Xu Dachun Naibu Waziri wa Maliasili wa China ambaye pia ndiye Rais wa Taasisi ya Utafiti wa Jiolojia ya China (CGS) alishukuru kwa Tanzania kushiriki mkutano wa Madini China na kusisitiza kwamba yupo tayari kuendelea kutoa ushirikiano kwa Serikali ya Tanzania katika kubadilishana uzoefu utakaosaidia kuendeleza sekta zetu za madini.

Pia, Dkt. Dachun alisisitiza kuwa ushirikiano baina ya Tanzania ni China una maana kubwa na manufaa kwa pande zote mbili za Nchi kwani Tanzania ina fursa nyingi za uwekezaji wakati China ina teknolojia na mitaji, hivyo ushirikiano wa Nchi hizi ni wazi utaleta manufaa yenye tija kwa wananchi wa Nchi zote mbili.







Share:

SHEIKH WA DODOMA ATOA AGIZO LA DUA MAALUMU MISIKITINI



Na Mwandishi wetu, Dodoma

Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) Mkoa wa Dodoma limewaagiza Masheikh na Maimamu wote wa misikiti mkoani humo kufanya dua maalumu kwa ajili ya kuombea taifa na kuendelea kuomba mvua, kutokana na changamoto ya mabadiliko ya hali ya hewa yanayotarajiwa.

Agizo hilo limetolewa leo Septemba 11,2026 na Sheikh wa Mkoa wa Dodoma, Alhaji Dkt. Mustafa Rajabu Shabani, ambaye amewataka Masheikh na Maimamu wote wa misikiti mkoani Dodoma kutekeleza dua hizo kuanzia Ijumaa, Septemba 11, 2026, baada ya Swala ya Ijumaa na kuendelea.

Sheikh Dkt. Shabani,amesema dua hiyo ina mambo mawili muhimu, ikiwemo kumuombea Marehemu Mzee Hafidh Ameir Mume, aliyekuwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Amesema ni muhimu kwa viongozi na waumini wa dini ya Kiislamu kumuombea marehemu huyo, huku akiwataka Masheikh na Maimamu kuhakikisha dua hiyo inafanyika katika misikiti mbalimbali mkoani Dodoma.

Aidha, Sheikh Dkt. Shabani ametoa agizo la kufanyika kwa dua endelevu ya kuliombea taifa kupukana na janga la mvua za El-Nino, ambazo zinatajwa kuwa na uwezekano wa kuleta athari kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa.

Amesema dua hiyo inapaswa kuendelea kufanyika kwa mujibu wa mamlaka za hali ya hewa na taarifa zinazotolewa kuhusu mwenendo wa hali ya hewa nchini.




Share:

TANZANIA, MAREKANI KUENDELEZA USHIRIKIANO KATIKA SEKTA ZA MAENDELEO

Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb) akisalimiana na Naibu Katibu wa Hazina ya Marekani anayeshughulikia Masuala ya Kimataifa, Bi. Erin Browne, mjini Nairobi, Kenya, kando ya Jukwaa la Mazungumzo ya Ngazi za Juu la Mawaziri wa Fedha kuhusu kuimarisha uwekezaji wa pamoja katika sekta ya afya.


***************

Na. Peter Haule, WF, Nairobi, Kenya

Tanzania na Marekani zimeeleza dhamira ya kuendelea kuimarisha ushirikiano katika sekta mbalimbali za maendeleo, ikiwemo afya, kilimo, nishati, madini, miundombinu, elimu na utalii.

Dhamira hiyo imeelezwa wakati Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb), alipokutana na kufanya mazungumzo na Naibu Katibu wa Hazina ya Marekani anayeshughulikia Masuala ya Kimataifa, Bi. Erin Browne, mjini Nairobi, Kenya, kando ya Jukwaa la Mazungumzo ya Ngazi za Juu la Mawaziri wa Fedha kuhusu kuimarisha uwekezaji wa pamoja katika sekta ya afya.

Katika mazungumzo hayo, Mhe. Luswetula amezialika kampuni na wawekezaji kutoka Marekani kutumia fursa mbalimbali za uwekezaji zinazopatikana Tanzania, akitaja maeneo ya kilimo, nishati, madini, miundombinu, afya, elimu na utalii.

Aidha, Mhe. Luswetula ameishukuru Serikali ya Marekani kwa kuendelea kushirikiana na Tanzania pamoja na mchango wake katika maeneo mbalimbali ya maendeleo tangu kuanzishwa kwa uhusiano wa kidiplomasia kati ya nchi hizo mwaka 1968.

Amesema ushirikiano huo umekuwa na mchango katika juhudi za Tanzania za kukuza maendeleo ya kijamii na kiuchumi na kupunguza umaskini.

Kwa upande wake, Naibu Katibu wa Hazina ya Marekani anayeshughulikia Masuala ya Kimataifa, Bi. Erin Browne, amesema Marekani itaendelea kushirikiana na Tanzania katika maeneo mbalimbali ya maendeleo, pamoja na kuimarisha na kukuza ushirikiano uliopo baina ya nchi hizo.

Mazungumzo hayo yameangazia pia umuhimu wa kuendelea kujenga ushirikiano wa kiuchumi na uwekezaji kati ya Tanzania na Marekani kwa manufaa ya wananchi wa nchi hizo mbili.
Naibu Katibu wa Hazina ya Marekani anayeshughulikia Masuala ya Kimataifa, Bi. Erin Browne, mjini Nairobi, Kenya, akizungumza kuhusu ushirikiano wa maendeleo wakati wa mkutano na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb), kando ya Jukwaa la Mazungumzo ya Ngazi za Juu la Mawaziri wa Fedha kuhusu kuimarisha uwekezaji wa pamoja katika sekta ya afya.
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb) (katikati), akieleza fursa za uwekezaji wakati wa mkutano na Naibu Katibu wa Hazina ya Marekani anayeshughulikia Masuala ya Kimataifa, Bi. Erin Browne kando ya Jukwaa la Mazungumzo ya Ngazi za Juu la Mawaziri wa Fedha Afrika, kuhusu kuimarisha uwekezaji wa pamoja katika sekta ya afya, wengine ni wajumbe walioambatana nae kutoka Tanzania.
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb) (wa pili kushoto) na Naibu Katibu wa Hazina ya Marekani anayeshughulikia Masuala ya Kimataifa, Bi. Erin Browne (wa pili kulia) wakiwa katika mkutano kati yao, kando ya Jukwaa la Mazungumzo ya Ngazi za Juu la Mawaziri wa Fedha Afrika, kuhusu kuimarisha uwekezaji wa pamoja katika sekta ya afya.
Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula (Mb) na Naibu Katibu wa Hazina ya Marekani anayeshughulikia Masuala ya Kimataifa, Bi. Erin Browne wakiteta jambo, kando ya Jukwaa la Mazungumzo ya Ngazi za Juu la Mawaziri wa Fedha Afrika, kuhusu kuimarisha uwekezaji wa pamoja katika sekta ya afya.

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Fedha)

Share:

Thursday, 10 September 2026

MATUNDA YA AWAMU YA SITA: VETA KUZINDUA SIMU YA ‘UJUZI Pro’


Uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan katika sekta ya elimu na mafunzo ya ufundi stadi umeanza kuzaa matunda yanayoonekana kupitia Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA), ikiongozwa na mafanikio makubwa katika uvumbuzi wa kiteknolojia, uzalishaji, na kukuza ujuzi kwa nguvukazi ya taifa.

Akizungumza jijini Dodoma, Mkurugenzi Mkuu wa Veta, Anthony Kasore, alieleza kuwa mamlaka hiyo iko katika hatua za mwisho kabisa za kuingiza rasmi sokoni simu ya mkononi ya kwanza ya kizalendo iitwayo Ujuzi Pro, hatua iliyofikiwa baada ya kukamilisha taratibu zote muhimu na kupata kibali rasmi kutoka Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), jambo ambalo ni kielelezo tosha cha uwezo wa wataalamu wa ndani unaochochewa na mazingira wezeshi ya serikali.

Sambamba na hilo, mafanikio hayo yameonekana katika kukuza ujuzi viwandani kupitia ushirikiano na viwanda 16 uliowezesha kutoa mafunzo maalum kwa wafanyakazi 600 na kuongeza tija mahali pa kazi, pamoja na kuwawezesha wananchi 4,465 wakiwemo wajasiriamali wa sekta ya uvuvi kupitia mafunzo yaliyogharamiwa na serikali.

Veta pia imeendelea kuboresha mitaala yake kwa kuandaa mitaala mipya 29 inayokidhi mahitaji ya soko la ajira, ikiwemo ya sekta ya vioo na alumini pamoja na usimamizi na urejelezaji wa taka.

Katika kukuza ubunifu na teknolojia, mamlaka imeratibu bunifu zaidi ya 120 kutoka kwa wanafunzi na wakufunzi, ambapo bunifu 17 zimeshaboreshwa na kuingizwa sokoni kwa ajili ya kuzalishwa kwa wingi, huku mfumo wa kidijiti wa Fundi Connect ukianzishwa ili kuwasajili mafundi rasmi na kuwaunganisha na wateja.

Mafanikio haya yanathibitisha kwa vitendo dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kujenga uchumi unaotegemea maarifa, teknolojia na viwanda.


Share:

Wednesday, 9 September 2026

WAANDISHI WA HABARI WAPEWA MAFUNZO YA UBUNIFU UNAOMLENGA MTUMIAJI (HCD) KUKABILIANA NA HABARI POTOFU

Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya teknolojia na habari ya Nukta Africa, Nuzulack Dausen akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya teknolojia na habari ya Nukta Africa, Nuzulack Dausen, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Programu Meneja wa International Media Support (IMS), Fausta Musokwa, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Mwezeshaji wa mafunzo hayo kuhusu Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD), Dkt. Hellen Maziku, Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mwanzilishi wa HCD Services Tanzania, akizungumza wakati wa mafunzo hayo.


Na Waandishi wetu - Malunde 1 blog

 Waandishi wa habari, wahariri na wataalamu wa masoko na biashara kutoka taasisi 10 za habari nchini Tanzania wamejengewa uwezo wa kukabiliana na taarifa potofu na za upotoshaji kupitia mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (Human-Centred Design - HCD), yanayolenga kuwasaidia kutambua changamoto zinazohusiana na taarifa potofu na kubuni suluhisho zinazozingatia mahitaji, uzoefu na tabia za watumiaji wa taarifa.

Mafunzo hayo ya siku tatu yanafanyika jijini Arusha kuanzia Septemba 9 hadi 11, 2026, yakiendeshwa na Shirika la International Media Support (IMS) kwa kushirikiana na Umoja wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania (UTPC), JamiiAfrica na Nukta Africa.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Afisa Mtendaji Mkuu wa Nukta Africa, Nuzulack Dausen, amesema taarifa sahihi ni jambo nyeti katika jamii kwa kuwa zina nafasi kubwa katika kusaidia wananchi na taasisi kufanya maamuzi sahihi kwa ajili ya maendeleo.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya teknolojia na habari ya Nukta Africa, Nuzulack Dausen, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu.

Dausen ameeleza kuwa, kuenea kwa taarifa potofu kunaweza kuathiri sekta mbalimbali na kuhatarisha ustawi wa jamii, hivyo ni muhimu kwa waandishi wa habari kuwa na ujuzi na mbinu za kisasa za kubaini na kukabiliana na taarifa hizo.

Ameongeza kuwa, mafunzo hayo yanatoa fursa kwa wadau wa habari kujengeana uwezo na kubadilishana uzoefu kuhusu mbinu za kisasa za kukabiliana na habari potofu katika vyombo vya habari, kwa lengo la kusaidia jamii kupata taarifa sahihi na kufanya maamuzi yenye tija kwa maendeleo yao.

Amesema Mafunzo hayo ni sehemu ya programu ya Maabara ya Fikra Bunifu na Uvumbuzi (Design Thinking and Innovation Lab) inayosimamiwa na IMS na washirika wake, ikiwa na lengo la kuwajengea washiriki uelewa na uwezo wa kutumia kanuni, hatua na mbinu za HCD katika kutambua na kutatua changamoto zinazohusiana na taarifa potofu.

Kwa upande wake, Programu Meneja wa International Media Support (IMS), Fausta Musokwa, amesema taasisi hiyo inashirikiana na wadau wa habari nchini Tanzania katika kutekeleza mradi unaolenga kukabiliana na misinformation na disinformation, ili kusaidia vyombo vya habari kuwa na mbinu sahihi za kuelimisha jamii na kukabiliana na taarifa zinazoweza kupotosha umma.
Programu Meneja wa International Media Support (IMS), Fausta Musokwa.

Musokwa amesema juhudi hizo ni muhimu katika kuongeza uwezo wa vyombo vya habari kukabiliana na changamoto ya taarifa potofu, hasa katika kipindi ambacho teknolojia za mawasiliano zimefanya taarifa kusambaa kwa kasi kubwa.

Musokwa amesema kuenea kwa taarifa potofu na maudhui ya chuki ni miongoni mwa changamoto zinazozidi kujitokeza duniani, huku ukuaji wa matumizi ya simu janja na upatikanaji mpana wa intaneti, sambamba na viwango vya chini vya uelewa wa mfumo wa taarifa, ukiongeza uwezekano wa kusambaa kwa taarifa zisizo sahihi na zinazopotosha hivyo ni wajibu wa vyombo vya habari kuwa mstari wa mbele kulinda jamii ipate taarifa sahihi ili ifanye maamuzi sahihi.

Amebainisha kuwa, hali hiyo inaweza kuleta madhara kwa watu binafsi na jamii kwa ujumla, ikiwemo kuathiri namna wananchi wanavyofanya maamuzi kuhusu masuala mbalimbali yanayogusa maisha yao.

Naye Mwezeshaji wa mafunzo hayo, Dkt. Hellen Maziku, Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mwanzilishi wa HCD Services Tanzania, amesema mafunzo hayo yanasisitiza umuhimu wa kutumia mtazamo unaomlenga mtumiaji katika kutafuta suluhisho la changamoto ya taarifa potofu.

Amesema mtazamo huo unazingatia mahitaji, matarajio, uzoefu na tabia za wananchi wanaokumbwa na changamoto ya taarifa potofu, hatua inayolenga kuhakikisha suluhisho zinazobuniwa zinakidhi mahitaji halisi ya watumiaji wa taarifa.

Kwa upande wao, washiriki wa mafunzo hayo wamesema yatawasaidia kupata uelewa na mbinu mbalimbali zitakazowasaidia kutambua, kuchambua na kukabiliana na habari potofu na taarifa za upotoshaji katika kazi zao za kila siku.


Wamesema mafunzo hayo yatawasaidia kuongeza umakini katika kuchakata taarifa kabla ya kuzifikisha kwa wananchi, hatua ambayo itachangia kuimarisha uaminifu wa jamii kwa vyombo vya habari na kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi na zenye manufaa kwa maisha yao.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya teknolojia na habari ya Nukta Africa, Nuzulack Dausen, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya teknolojia na habari ya Nukta Africa, Nuzulack Dausen akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya teknolojia na habari ya Nukta Africa, Nuzulack Dausen, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya teknolojia na habari ya Nukta Africa, Nuzulack Dausen, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya teknolojia na habari ya Nukta Africa, Nuzulack Dausen, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya teknolojia na habari ya Nukta Africa, Nuzulack Dausen, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Afisa Mtendaji Mkuu wa kampuni ya teknolojia na habari ya Nukta Africa, Nuzulack Dausen akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Programu Meneja wa International Media Support (IMS), Fausta Musokwa, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Programu Meneja wa International Media Support (IMS), Fausta Musokwa, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Programu Meneja wa International Media Support (IMS), Fausta Musokwa, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Programu Meneja wa International Media Support (IMS), Fausta Musokwa, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Programu Meneja wa International Media Support (IMS), Fausta Musokwa, akizungumza wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.
Mwezeshaji wa mafunzo hayo kuhusu Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD), Dkt. Hellen Maziku, Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mwanzilishi wa HCD Services Tanzania, akizungumza wakati wa mafunzo hayo.
Mwezeshaji wa mafunzo hayo kuhusu Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD), Dkt. Hellen Maziku, Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na Mwanzilishi wa HCD Services Tanzania, akizungumza wakati wa mafunzo hayo.
Mkurugenzi wa Malunde Media, Kadama Malunde, akichangia hoja wakati wa mafunzo ya Ubunifu Unaomlenga Mtumiaji (HCD) yanayolenga kuwajengea uwezo wadau wa habari kukabiliana na taarifa potofu, jijini Arusha.




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger