Tuesday 15 October 2024

WAZIRI MKUU AWATAKA VIJANA KUJIUNGA NA VETA


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa amewahamasisha vijana kujiunga na mafunzo ya ufundi stadi katika vyuo vya VETA, ili waweze kuajiriwa au kujiajiri kwa urahisi.

Waziri Mkuu ameyasema hayo juzi, tarehe 11 Oktoba 2024 alipokuwa akizindua Wiki ya Vijana Kitaifa katika uwanja wa Furahisha, jijini Mwanza.

Amesema Serikali imewekeza nguvu kubwa kwa vijana kupitia ujenzi wa vyuo vya VETA ambapo vyuo vipya 25 vimekamilika na vingine 65 vinajengwa katika kila wilaya na kwamba jukumu lililobaki ni la vijana kujiunga na mafunzo katika vyuo hivyo ili kujipatia ujuzi utakaowawezesha kuajiriwa au kujiajiri.

Naye, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Patrobas P. Katambi (MB) ameipongeza VETA kwa juhudi za kusaidia kukuza na kuendeleza ubunifu wa vijana.

Katambi ameyasema hayo alipotembelea banda la VETA kwenye maonesho hayo, tarehe 10 Oktoba 2024 na kujionea ubunifu mbalimbali wa wahitimu kutoka vyuo vya VETA nchini.

Kipekee, Mhe. Katambi amevutiwa zaidi na ubunifu wa mhitimu wa chuo cha VETA Mwanza, Benjamin Samweli ambaye ametengeneza gari linalotumia injini ya pikipiki lenye uwezo wa kubeba nusu tani, kutembea Kilometa 80 kwa saa, kutumia lita moja kwa Kilometa zaidi ya 20.

“Serikali katika Sera yake ya maendeleo ya vijana imeongelea kuwezesha vijana wenye uwezo na vipaji kuhusiana na ubunifu na uvumbuzi. VETA fuatilieni COSTECH kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu kumsaidia mhitimu huyu kukuza na kuendeleza kipaji chake kwa kupatiwa mkopo nafuu ili aweze kuendeleza kipaji chake,” amesema.

Aidha ametoa wito kwa vijana kujiunga na Mafunzo na Elimu ya Ufundi Stadi ili kukuza uchumi wao kupitia ajira rasmi na zisizo rasmi.
Share:

SERIKALI KUANZA MAHOJIANO RASMI NA WAKIMBIZI


Serikali ya Tanzania inatarajia kuanza mahojiano ya kina na wakimbizi wa Burundi wanaoishi nchini ifikapo 2025. Mahojiano haya yatashirikisha wadau mbalimbali, ikiwa ni pamoja na Shirika la Umoja wa Mataifa linalohudumia Wakimbizi (UNHCR). Lengo kuu ni kubaini changamoto wanazokabiliana nazo wakimbizi na kutafuta suluhisho la kudumu kulingana na maoni yatakayokusanywa katika mahojiano.

Hayo yameelezwa na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Daniel Sillo, alipowasilisha ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 75 wa Kamati Tendaji ya UNHCR nchini Uswisi, tarehe 15 Oktoba 2024.

Mhe. Sillo alibainisha kwamba Tanzania inahifadhi wakimbizi zaidi ya 240,000, wengi wao wakiwa kutoka Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Alisema serikali imefanikiwa kutafuta suluhisho la kudumu kwa wakimbizi 17,283 kwa mwaka huu, ambapo wakimbizi 12,717 walirudi kwa hiari katika nchi zao za asili, na 4,566 walipatiwa makazi mapya katika mataifa mengine.
Aidha Mhe. Sillo katika Ujumbe wake alieleza kuwa licha ya Mafanikio hayo, Operesheni za Kuhudumia Wakimbizi nchini Tanzania inakabiliwa na changamoto kubwa za kifedha, hasa katika sekta za afya na elimu katika kutoa huduma bora kwa Wakimbizi

Kwa upande wake, Kamishna Mkuu wa UNHCR, Filippo Grandi, ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa juhudi zake katika kuhifadhi wakimbizi kwa miaka mingi na sasa kujikitika katika kutafuta suluhisho la kudumu kwa Wakimbizi hao. Aidha alitoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuungana ili kusaidia wahanga wa migogoro na kuhakikisha wanapata misaada inayohitajika.


Share:

MKATABA WA BILIONI 13.5 WASAINIWA KWA UJENZI WA JENGO LA TIA SINGIDA

Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo (kulia) pamoja na Mwakilishi wa Salem Construction, Charles Casmir (kushoto) wakionesha mkataba waliosaini kwaajili ya ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.

************************

TAASISI ya Uhasibu Tanzania (TIA), imesaini mkataba na kampuni ya Salem Construction kwaajili ujenzi wa jengo la kampasi yake mkoani Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5.

Mkataba huo utachukua miezi 24 hadi kukamilika kwa ujenzi jengo hilo mkoani Singida.

Akizungumza leo Oktoba 15,2024 katika hafla hiyo iliyofanyika kwenye ofisi za taasisi hiyo Jijini Dar es Salaam, Mtendaji Mkuu wa TIA, Prof. William Pallangyo amesema fedha za ujenzi wa kampasi hiyo zimetolewa chini ya Mradi wa Mageuzi ya Kiuchumi kwa Vyuo Vikuu nchini (HEET) unaofadhiliwa na Benki ya Dunia (WB).

Aidha amemtaka mkandarasi kuhakikisha anajenga jengo lenye ubora na kufanyakazi kwa karibu na wananchi wa Singida ili wawe walinzi wa mradi huo mpaka utakapokamilika kwa muda ambao umewekwa.

“Tumemtaka mkandarasi azingatie kanuni za ujenzi ili kuhakikisha wafanyakazi wanakuwa salama wakati wote tunataka mpaka mradi unapokamilika watu wawe salama kusitokee kifo hata kimoja wala majeruhi,” amesema Prof. Pallangyo.

Amesema watajitahidi kufanyakazi kwa karibu na benki ya dunia ambayo ndiyo inayofadhili mradi huo kuhakikisha kila mkandarasi anapoomba malipo analipwa kwa wakati ili mradi usisimame.

Kwa upande wake Mratibu wa HEET Kitaifa, Dkt. Kenedy Hossea, ameipongeza TIA na menejimenti yake kwa kupata mkandarasi mapema kwaajili ya ujenzi wa jengo katika Kampasi ya Singida

“Nawapongeza Mtendaji Mkuu wa TIA kwasababu kuna watu walianza muda mrefu hawajapata mkandarasi mpaka sasa wanalumbana tu zabuni inatangazwa inafutwa wanashindwa kufikia muafaka,” amesema

Pamoja na hayo, Dkt. Hossea amemtaka mkandarasi wa jengo hilo kuzingatia ubora na kuahidi kuwa wataalamu wanaosimamia mradi huo kutoka wizarani watakuwa wakipita mara kwa mara kuhakikisha ubora unazingatiwa.

Nae Mwakilishi wa Salem Construction, Charles Casmir, amesema mkataba huo ni wa miezi 24 lakini kwa namna walivyojipanga watakamilisha mradi huo ndani ya miezi 18.

Amesema wanatarajia kuwa jengo hilo litakuwa la mfano na kwamba watahakikisha wanazingatia usalama wa wafanyakazi na jamii inayozunguka mradi huo katika Mkoa wa Singida.

Mratibu wa mradi wa huo TIA , Oyombe Simba, aliishukuru serikali kwa kukubali fedha hizo kupelekwa kwenye taasisi hiyo kwaajili ya kuboresha mazingira ya wanafunzi kujisomea.

Amesema TIA imepokea jumla ya shilingi bilioni 27.6 ambazo zinakwenda kuboresha kampasi za taasisi hiyo ambapo mbali na ujenzi wa jengo la Singida pia watajenga majengo kwenye kampasi ya Mwanza.

Hata hivyo amesema jengo la bweni litakalojengwa Mwanza litagharimu shilingi bilioni 7.2 na litakuwa na uwezo wa kuchukua wanafunzi 306 kwa wakati mmoja.

“Mbali na ujenzi wa majengo mradi huu umelenga kuboresha mitaala na kuwajengea uwezo wakufunzi kwenye taasisi yetu kwa hiyo tunapoanza kutekeleza mradi huu ni fahari kubwa sana kwetu,” amesema
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo (kulia) pamoja na Mwakilishi wa Salem Construction, Charles Casmir (kushoto) wakisaini mkataba wa ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo (kulia) pamoja na Mwakilishi wa Salem Construction, Charles Casmir (kushoto) wakisaini mkataba wa ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo (kulia) pamoja na Mwakilishi wa Salem Construction, Charles Casmir (kushoto) wakisaini mkataba wa ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo (kulia) pamoja na Mwakilishi wa Salem Construction, Charles Casmir (kushoto) wakionesha mkataba waliosaini kwaajili ya ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo (kulia) pamoja na Mwakilishi wa Salem Construction, Charles Casmir (kushoto) wakipongezana huku wakionesha mkataba waliosaini kwaajili ya ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo (kulia) pamoja na Mwakilishi wa Salem Construction, Charles Casmir (kushoto) wakipongezana huku wakionesha mkataba waliosaini kwaajili ya ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo (kulia) pamoja na Mwakilishi wa Salem Construction, Charles Casmir (kushoto) wakionesha mkataba waliosaini kwaajili ya ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mratibu wa HEET Kitaifa, Dkt. Kenedy Hossea akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa jengo la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mratibu wa HEET Kitaifa, Dkt. Kenedy Hossea akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa jengo la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mratibu wa HEET Kitaifa, Dkt. Kenedy Hossea akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa jengo la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Makamu Mkuu wa Chuo- Taaluma, Utafiti na Ushauri wa kitaalamu TIA, Dkt. Momole Kasambala akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa jengo la TIA kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Watumishi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) wakiwa katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa  jengo la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Watumishi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) wakiwa katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa  jengo la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Watumishi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) wakiwa katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa  jengo la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Watumishi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) wakiwa katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa  jengo la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Watumishi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) wakiwa katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa  jengo la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Watumishi wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) wakiwa katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa  jengo la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.
Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA), Prof. William Pallangyo, Mratibu wa HEET Kitaifa, Dkt. Kenedy Hossea, Mratibu wa mradi wa HEET katika taasisi ya (TIA), Oyombe Simba pamoja na wadau wengine wakiwa kwenye picha ya pamoja katika hafla ya utiaji saini wa mkataba wa ujenzi wa  jengo la Taasisi ya Uhasibu Tanzania (TIA) kampasi ya Singida ambapo mkataba huo utagharimu kiasi cha shilingi bilioni 13.5. Hafla hiyo imefanyika leo Oktoba 15,2024 kwenye Ofisi za TIA Jijini Dar es Salaam.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)
Share:

MAFIA BOXING PROMOTION WAUNGA MKONO KAMPENI YA RAIS DKT SAMIA SULUHU YA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA

 




Na Oscar Assenga,TANGA

KAMPUNI ya Mafia Promotion Boxing imetoa msaada wa majiko ya Gesi kwa wanawake wanaojishughuli na uuzaji wa vyakula katika masoko ya Mgandini, Makorora na Mlango wa Chuma yaliyoko jijini Tanga ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Rais Dkt Samia Suluhu ya matumizi ya Nishati Safi ya kupikia.

Licha ya kugawa mitungi hiyo ya gesi lakini wametoa msaada mwengine wa vitu mbalimbali katika kituo cha kulea watoto yatimacha Green Cresent Ophanege Foundation cha Jijini humo .

Hatua ya kampuni hiyo kuunga mkono juhudi hizo inatokana na ushindi walioupata mabondia mbalimbali wanaodhaminiwa na kampuni hiyo ambao walipata ushindi katika mapambano yao walipopanda hivi mwanzoni mwa mwezi 0ctoba mwaka huu Jijini Dar es Salaam.
Akizungumza Mkurugenzi wa Matangazo na Uzalishaji kutoka Kampuni ya Mafia Promotion Omari Clayton alisema pambano hilo lilichagizwa na Technical Knock Out ‘KO’ ya Rais Dkt. Samia Suluhu.

Alisema baada ya ushindi huo wapewa fedha taslimu kama zawadi kwa mabondia hao ambayo imewatia hamasa kuhakikisha wanazidi kuijengea heshima Tanzania kupitia mchezo wa ngumi.

Alisema kwamba jambo ambalo wameifanya kwa kugawa majiko hayo ya gesi ni kama sehemu ya kurudisha kwa jamii ikiwa ni utaraibu wao na wanaungana na watanzania kupitia Kampeni ya Rais Dkt. Samia ya kuhamasisha juu ya matumizi ya nishati safi na kuachana na matumizi ya mkaa na kuni katika kupikia na shughuli nyingine hali ambayo inasababisha mabadiliko ya tabianchi na uzalishaji wa hewa ukaa.
Alisema kwamba kampuni hiyo ya Mafia wanaunga mkono juhudi za Rais Dkt Samia Suluhu Hassan katika kupambana na kuhamasisha watanzania kuhama kutoka kwenye matumizi ya mkaa na kuni kupikia na kwenda kwenye matumizi ya nishati safi.

“ Ndio maana leo tumegawa majiko ya gesi kwa mama zetu wanapika vyakula katika masoko yaliyopo katika jiji la Tanga” Alisema Clayton.
“Tumehamasika na tunampongeza sana Rais wetu Dkt. Samia kuja na ‘KO ya Mama’ na kuwazawadia mabodia wetu ambao walipambana kuhakikisha wanabakisha mikanda hapa Tanzania na walifanikiwa na tunamuahidi kwamba mama kupitia Mafia Boxing tutazidi kuiheshimisha Tanzania”Alisema .

Akizungumza kwa niaba ya mabondi wenzanke Ibrahim Mafia alisema kwamba haikuwa rahisi kupamba ulingoni kutokana na mpinzani wake kuwa imara lakini kupitia maombi ya watanzania alipambana kuhakikisha anawapa furaha kwa kupata ushindi .

“Ule ushindi ni ushindi ni ushindi wetu lakini pia ni ushindi wa watanzania walikuwa wakituombea tumepokea zawadi kutoka kwa Rais wetu mama Samia tukaona hatuwezi kuitumia peke yetu bali tushirikiane kile ambacho tumepata kwa kuwapa majiko ya gesi na kutoa msaada kwa kituo cha watoto yatima tunaomba mzidi kutuombea dua ili wakati mwingine tuweze kutoa kikubwa zaidi. Alisema Mafia”

Bondia Ibrahim Mafia alipanda ulingoni kuzichapa na mpinzani wake Enoch Tettey raia wa Ghana kuwania mkanda wa dunia ‘World Boxing Council Bantamweight’ wenye uzito wa Kg 53 katika ukumbi wa City Center Hall Magomeni Sokoni na hatimaye kufanikiwa kubwaga chini mpinzani wake kwa KO.
Hata hivyo wakina mama mntilie ambao walipata majiko hayo waliwapongeza mabondia wote kwa ushindi walioupata pamoja na kuishukuru Kampuni ya Mafia Boxing Promotion kwa kuwapatia mitungi ya gesi ambayo itawasaidia katika shughuli zao.
Tunawashukuru kwa zawadi zenu na sisi tunaendelea kuwaombea kwa Mungu hakika atawalipa tulikuwa na changamoto ya kupata mkaa kwa ajili ya kupikia lakini sasa kupitia majiko haya yatatusaidia kurahisisha shughuli zetu za kupika kila siku .
Share:

Monday 14 October 2024

DAWA YA KUMZUIA MUME ASIENDE KULALA NJE YA NDOA

Ukweli ni kwamba katika ndoa wanawake wengi hupitia changamoto mbalimbali kutokana na tabia za wanaume wao kuwa na mapango wa kando, hilo kufanya kushindwa kuhudumia familia vizuri.

Nasema hivyo kwa sababu hilo lilishawahi kunipata maishani mwangu, mume wangu hakuijali familia yake kwa lolote lile licha ya kuwa alikuwa na kazi na anapokea mshahara kila mwezi.

Sikujua tatizo lilikuwa ni nini hasa, kila ambapo ningemuuliza ni wapi fedha zake zinakwenda, basi angekuwa mkali kiasi cha kuibuka mgomvi mkubwa ndani ya nyuma yetu.

Hali hiyo ilikuwa inaniumiza sana mimi kama mwanamke, maana mimi nimeolewa tena kwa ndoa halali kabisa, ni lazima yeye kama mume anihudumie mimi mkwe, lakini hakufanya hivyo.

Baada ya kuchunguza simu yake kwa muda mrefu, nikaja kugundua kuwa alikuwa na mahusiano na wanawake wengi, hao ndio hasa walikuwa wanachukua fedha zake na yeye kuisahau familia yake.

Niliumia sana baada ya kubaini hilo, nilijiona sina thamani tena kwake, niliona ni bora nirudi kwa wazazi wangu, lakini kila ambapo nilipokuwa nawafikiria watoto wangu wataishije, nilikuwa naishiwa nguvu ya kufanya.

Wazo lilinijia kuwa nitafute watu wa mitishamba wanaweza kunisaidia kumtuliza huyo mwanaume, ndipo nikakutana na Dr Bokko ambao ndio waliokuja kuiponya ndoa yangu.

Baada ya kuwaeleza tabia ya mume wangu jinsi ilivyokuwa, waliniambia wanaweza kumfunga, hivyo hatoweza tena kuwa na mpango wa kando maisha yake yote.

Niliwaambia basi wamfunge tu, na kweli tangu wakati huo naona ametulia nyumbani na kuzidisha mapenzi kwangu, na sasa anahudumia familia yake vizuri na fedha zinaonekana ndani ya nyumba tofauti na hapo awali.

Ninatoa wito kwa wenye shida au magonjwa, kusumbuliwa na mapenzi, ndoa, biashara, kukosa ujauzito n.k, basi wasisite kuwatembelea Dr Bokko, sio lazima usafiri hadi ofisini kwao, unaweza kuongea nao kwa njia ya simu na utasaidiwa kwa haraka. Piga kwa namba; +255618536050.

Mwisho.


Share:

RAIS SAMIA ATETA NA ZUHURA YUNUS


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongea na Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Zuhura Yunus, jijini Mwanza leo Oktoba 14,2024 kwenye maadhimisho ya kilele cha mbio za Mwenge wa Uhuru. Katikati ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu) Kazi,Vijana, Ajira na Watu Wenye Ulemavu), Patrobas Katambi.
Share:

RAIS SAMIA AELEKEZA MAKAMPUNI YA MADINI KUCHANGIA NA KUSHIRIKIANA NA CHUO CHA VETA GEITA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameyaelekeza makampuni ya madini kuchangia na kushirikiana na chuo cha VETA Geita katika utoaji wa mafunzo ya ufundi stadi.

Mhe. Rais Samia ametoa maelekezo hayo alipotembelea wakati akifunga Maonyesho ya Saba ya Teknolojia na Uwekezaji katika Sekta ya Madini, jana, tarehe 13 Oktoba, 2024.

Mhe. Rais amesema ushirikiano huo pia uwawezeshe vijana kujifunza na baada ya kuhitimu wafanye kazi kwenye makampuni ya madini yaliyopo ndani ya mkoa wa Geita.

Amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mheshimiwa Martin Shigella kuratibu suala hilo na kuhakikisha linatekelezwa.

Chuo cha VETA Geita ni chuo cha hadhi ya mkoa ambacho kimeanza mafunzo mwaka 2024 na kina uwezo wa kudahili wanafunzi 720 kwa kozi ndefu na kozi fupi 1500 kwa mwaka na kwa sasa chuo kinatoa mafunzo katika fani za Umeme na Bomba, na chuo kinatarajia kutoa zaidi ya fani 13 katika maeneo mbalimbali.
Share:

WAZIRI DKT. SELEMANI JAFO APOKEA TUZO YA TANTRADE URATIBU BORA WA MAONESHO YA MADINI GEITA

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akikabidhi Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Selemani Jafo tuzo kwa niaba ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania ( TanTrade) kwa kutambua usimamizi bora na uratibu wa Maonesho ya biashara ndani na nje ya nchi na kutoa huduma ya kliniki ya biashara kipindi cha Maonesho ya 7 ya kitaifa ya Teknolojia ya Madini yaliyofanyika Viwanja vya EPZA Bombambili mjini Geita, maonesho hayo yamefungwa Leo Oktoba 13, 2024 ,

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan akikabidhi Waziri wa Viwanda na Biashara Dkt. Selemani Jafo tuzo kwa niaba ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania ( TanTrade) kwa kutambua usimamizi bora na uratibu wa Maonesho ya biashara ndani na nje ya nchi na kutoa huduma ya kliniki ya biashara kipindi cha Maonesho ya 7 ya kitaifa ya Teknolojia ya Madini yaliyofanyika Viwanja vya EPZA Bombambili mjini Geita, maonesho hayo yamefingwa Leo Oktoba 13, 2024 , Kushoto ni Waziri wa Madini Anthony Mavunde.

Share:

Sunday 13 October 2024

DKT. SHEKALAGHE AHIMIZA SHIUMA KUWA KITU KIMOJA KWA MAENDELEO YA WAFANYABIASHARA NDOGONDOGO


Na WMJJWM, Dodoma

Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Seif Shekalaghe amewataka viongozi wa Shirikisho la Umoja wa Machinga Tanzania (SHIUMA) ngazi ya Taifa na mikoa kuwa kitu kimoja na kushiriki kikamilifu kwenye shughuli zinazosimamiwa na Serikali kwa maendelea ya wafanyabiashara ndogondogo nchini.

Hayo ameyasema Oktoba 11, 2024 jijini Dodoma wakati akifungua mafunzo ya siku moja ya kuwajengea uwezo na uelewa kuhusu miongozo ya uratibu wa utoaji mikopo kwa viongozi wa SHIUMA, ili waweze kushirikiana na Serikali katika kutoa hamasa na elimu kwa ŵafanyabiashara ndogondogo kuendelea kujitokeza kujisajili kwenye Mfumo wa Kidigitali wa Kusajili Wafanyabiashara Ndogondogo (WFB).

"Baada ya mafunzo haya, ni matarajio yangu kuwa, juhudi zenu za kutoa hamasa kwa wafanyabiashara ndogondogo litazaa matunda tunapoelekea kwenye uzinduzi wa Vitambulisho na Mikopo yenye mashart nafuu itakayoanza kutolewa na Serikali kupitia Benki ya NMB na kitambulisho cha kidigitali kitakuwa moja ya dhamana yako", amesema Dkt. Shekalaghe.

Ameongeza kuwa, Wafanyabiashara ndogondogo wana mchango mkubwa katika uchumi wa nchi, akisisitiza kwamba, Dhamira ya Serikali ya kutoa vitambulisho hivyo imeambatana na faida nyingi zikiwemo kutambulika na taasisi mbalimbali, kuunganishwa na mifumo ya NIDA, NAPA na Huduma nyingine za kijamii.

Aidha, Dkt. Shekilaghe amewaasa viongozi wa SHIUMA kuendelea kuwa wazalendo na kuwa mfano mzuri na watakaporejea watoe mrejesho kwa wafanyabiashara ndogondogo, pamoja na kuwahamasisha kushiriki kikamilifu katika zoezi la uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Kwa upande wa mwenyekiti wa SHIUMA mkoa wa Pwani Filemon Maliga , amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kupitia Wizara ya Maendeleo Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kwa kuwatambuwa, kuboresha mazingira ya wao kufanya kazi kwa umoja pamoja na kuwapambania kuwaunganisha na taasisi za kifedha kwa ajili ya kupata mikopo yenye masharti nafuu.

Uzinduzi wa utambuzi na usajili wa vitambulisho vya kidijitali unatarajiwa kufanyika Otoba 17, 2024 jijini Arusha.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger