Wednesday, 8 April 2026

SERIKALI YAINUA UTALII WA TIBA: WAGONJWA WA NJE WAFIKIA 3,018



Na Shaban Juma, WAF – Dodoma

Serikali ya Tanzania inaendelea kuchukua hatua madhubuti za kukuza utalii wa tiba, ikiwa ni sehemu ya mikakati ya kuongeza uchumi wa sekta ya afya na mchango wake wa pato la Taifa.

Hayo yamesemwa leo Aprili 08, 2026, na Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Florence Samizi, bungeni jijini Dodoma, akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Dkt. Catherine Canute Joachim, katika Bunge la Kumi na Tatu, Mkutano wa Tatu, Kikao cha Nne.

Akijibu swali kwa niaba ya Waziri wa Afya,.Mhe. Mohamed Mchengerwa, Dkt. Samizi amesema Serikali chini ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, imewekeza zaidi kwenye uboreshaji wa miundombinu ya hospitali, ikiwemo kujenga majengo mapya na kukarabati yale yaliyochakaa.

Aidha, amesema Serikali inaendeleza upatikanaji wa vifaa tiba vya kisasa kama PET/CT Scan, Angio Suite, Cathlab, na CT Scan, sambamba na kuendeleza mafunzo ya kitaaluma kwa wataalamu wa afya ili kuhakikisha huduma zinakuwa za ubora wa kimataifa.

“Serikali pia inaanzisha huduma mpya za ubingwa bobezi na kuhakikisha hospitali zinapata ithibati za kimataifa, na kuzitangaza katika masoko ya kimataifa ili kuvutia wagonjwa kutoka nje ya nchi,” amesema Dkt. Samizi.

Takwimu zinaonyesha ukuaji wa utalii wa tiba: katika kipindi cha Julai 2025 hadi Februari 2026, wagonjwa 3,018 kutoka nje ya nchi walipatiwa huduma za ubingwa bobezi katika hospitali za rufaa za mikoa, kanda, maalum na taifa.

Aidha, Dkt. Samizi ameongeza kuwa Serikali inaendelea kuwekeza katika rasilimali watu kupitia Samia Health Super-specialization Program, ambapo wataalamu 1,483 wanafadhiliwa kusomea fani za ubingwa na ubingwa bobezi ndani na nje ya nchi, hatua inayolenga kuongeza ubora na uwezo wa hospitali zetu.
Share:

Tuesday, 7 April 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRILI 8,2026

Magazeti






Share:

BARRICK NORTH MARA YAWEZESHA VIJANA TARIME KUANZISHA MIRADI YA KIUCHUMI


Vijana wakiwezeshwa kuendesha miradi mbalimbali ikiwemo ya kilimo wataweza kujikwamua kiuchumi kama wanavyoonekana vijana wakiwa shambani kwenye mradi wa kilimo cha mboga wa Matongo unaofadhiliwa na Barrick North Mara (Picha kutoka maktaba)
Mgodi wa Barrick North Mara uliopo wilayani Tarime katika mkoa wa Mara umeendelea kutekeleza moja ya sera ya mkakati endelevu wa kampuni ya kuwezesha wananchi wanaoishi jirani na migodi yake kuwa na maisha bora ambapo kupitia fedha za uwajibikaji kwa jamii (CSR) umetoa shilingi milioni 220 kwa vikundi 13 vya vijana ili kuanzisha miradi ya kiuchumi katika vijiji vyote 11 vinavyozunguka mgodi huo.

Hatua hii ni mwendelezo wa mgodi wa Barrick North Mara kuwezesha kiuchumi makundi mbalimbali katika jamii hususani vijana ambapo mwaka jana iliunga mkono jitihada za Serikali za kuwapatia leseni za uchimbaji ambapo mgodi ulitoa leseni zake na kufadhili mafunzo ya vijana hao zaidi ya 1700 wanaojiandaa kuingia katika uchimbaji wa madini chini ya programu ya Mining For a Brighter Tomorrow (MBT) inayolenga kuboresha usalama, kuongeza tija na kuondoa uvamizi wa mgodi kwa kuwapatia rasmi maeneo ya uchimbaji.

Tayari vikundi hivyo vimepokea fedha hizo, ikiwa ni ruzuku ya (CSR) ya mwaka uliopita kutoka kwa mgodi huo ambao unaendeshwa kwa ubia na serikali kupitia kampuni ya Twiga Minerals.

Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jami wa Halmashauri hiyo, Anthony George Nyange amesema kuwa fedha hizo zimesaidia vijana takriban 100 wanachama wa vikundi hiyo kuanzisha miradi ya mbalimbali ya kiuchumi.
Anthony George Nyange

“Nawashukuru sana Barrick North Mara hususan idara ya mahusiano ya jamii kwa ushirikiano ambao wamekuwa wakitoa katika kufanikisha mpango huu wa ruzuku ya uwajibikaji kwa jamii kwa vijana,” amesema Nyange.

Nyange amesema miradi hiyo imesaidia kutatua changamoto mbalimbali zilizokuwa katika vijiji hivyo kwa ajili ya ustawi wa jamii vinavyouzunguka mgodi huo.

“Wanufaika wengi ni vijana na wamejielekeza kwenye miradi ambayo siyo tu kwa ajili ya kujipatia kipato bali pia kutatua changamoto zilizokuwepo,” amesema.

Ametaja vikundi ambavyo vimenufaika na mpango huo kuwa ni Mokarambe Agribusiness, Hope and Revolution of Economy for Youth, Tunza Mazingira Nyamongo, Amshana Nyamongo na REMHOCHI.

Vingine ni Kazi ni Moyo, Konna Nne, Kiumanya, Ibuka Umoja, Tunaweza Kerende, Nyasa Group, Mtazamo Youth na Kikundi cha Keryoba.

Amesema baadhi ya vikundi hivyo vimeanzisha miradi ya usafi wa mazingira jambo ambalo limesaidia kuweka mji mdogo wa Nyamongo katika hali nzuri ya usafi na mazingira.

“Kwa mfano, kulikuwa na changomoto ya usafi katika mji wa Nyamongo, sasa hali ya usafi ni nzuri kwa sababu kuna kikundi cha mazingira ambacho kinafanya vizuri sana kwenye usafi wa mazingira,” amesema Nyange.

Nyange amesema Halmashauri ya Wilaya ya Tarime itaendelea kutenga sehemu ya fedha za Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) zinazotolewa na mgodi wa Barrick North Mara kwa ajili ya kuwawezesha vijana kuanzisha na kuendeleza miradi ya kiuchumi.

“Tunategemea na mwaka huu pia tutatenga sehemu ya CSR kwenda kuwezesha vijana kwenye miradi ya kiuchumi. Sasa hivi, vijana wengi kule Nyamongo wana shughuli za kufanya kujipatia kipato na hata vitendo vya kihalifu vimepungua,” amesema Nyange.

Amesema mbali na mpango wa Uwajibikaji kwa Jamii (CSR), vijana hao pia wamenufaika na mikopo kupitia asilimia 10 ya mapato ya ndani inayotolewa na halmshauri hiyo kuwezesha wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

“Wanufaika wakubwa ni vijana, na mbali ya kunufaika na mikopo yetu ya halmashauri ya asilimia 10, pia wamenufaika na mpango wa ruzuku ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) kwa vijana,” amefafanua Nyange.

Taarifa zinaonesha Halmashauri ya Wilaya ya Tarime inaongoza kwa kutoa kiasi kikubwa cha mikopo ya asilimia 10 kwa vijana, wanawake na watu wenye ulemavu katika Mkoa wa Mara.

Mgodi wa Barrick North Mara pamoja na kutekeleza sera ya Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) pia utoaji wa leseni za uchimbaji kwa vijana uliwezesha na mafunzo ya siku 14 yaliyofanywa kwa kushirikiana na serikali.

Lengo la mafunzo hayo ni kuhakikisha sekta ya madini iankuwa na tija zaidi kwa kuzingatia usalama mahali pa kazi na utunzaji wa mazingira , usimamizi wa biashara za madini na kufuata sheria za nchini na usimamizi wa vikundi pamoja na elimu ya masuala ya fedha.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE APRILI 7,2026

Magazeti



 













Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger