Tuesday, 30 June 2026

NAIBU WAZIRI MAHUNDI AHIMIZA WANAWAKE KUTUMIA MIKOPO KUINUA UCHUMI



Na Jackline Minja, Mtwara

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe. Maryprisca Mahundi, amezindua rasmi Mfuko wa Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi katika Jimbo la Mtwara Mjini (UWEZO Program) na kusema Serikali itaendelea kuunga mkono jitihada za uwezeshaji wa wanawake.

Akizungumza katika hafla hiyo Juni 30, 2026, Naibu Waziri Mahundi amesema Serikali inaamini kuwa maendeleo ya Taifa hayawezi kupatikana bila kuyawezeaha makundi maalum wakiwemo wanawake na vijana.

Amesema ushiriki wa makundi maalum katika shughuli za kiuchumi ni hatua ya kujivunia na kuongeza kuwa mafanikio yatapatikana kwa makundi hayo kupatiwa mafunzo stahiki.

"Serikali inaamini kuwa maendeleo ya Taifa hayawezi kupatikana bila wananchi wake kuwa na uwezo wa kushiriki kikamilifu katika shughuli za uzalishaji mali na hii ndiyo sababu kuwndelea kuweka mazingira wezeshi kwa wanawake na vijana kupata fursa za kiuchumi kupitia sera na programu mbalimbali," alisema Naibu Waziri Mahundi.

Aidha, ameeleza kuvutiwa kwake na Programu ya UWEZO kwa kuanza kutoa mikopo na kuwajengea wanawake uwezo kupitia mafunzo ya ujasiriamali, usimamizi wa fedha, utunzaji wa kumbukumbu za biashara na uundaji wa vikundi, akieleza kuwa msingi huo utasaidia kuhakikisha mikopo inazalisha matokeo chanya na kuongeza maendeleo ya wanawake pamoja na familia zao.

Awali akitoa maelezo kuhusu Programu ya UWEZO, Mbunge wa Jimbo la Mtwara Mjini na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Mhe. Joel Nanauka, amesema wazo la kuanzisha mfuko huo limetokana na ahadi aliyoitoa kwa wananchi wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ya kuwawezesha wananchi kiuchumi.

Amesema kupitia mfuko huo wenye mtaji wa shilingi milioni 150, wanawake zaidi ya 5,000 walitambuliwa kutoka kata zote 18 za jimbo hilo, wanawake 300 walipatiwa mafunzo ya ujasiriamali na wanawake 81 wamekabidhiwa mikopo katika awamu ya kwanza.

"Mikopo hiii haina riba kutokana na ushirikiano kati ya Joel Nanauka Foundation na Benki ya Ushirika (Coop Bank), sababu lengo la programu hii si kutoa fedha pekee bali kujenga wanawake wajasiriamali wenye uwezo wa kujitegemea, kuongeza ajira na kuchangia ukuaji wa uchumi wa Mtwara Mjini na Taifa kwa ujumla". alisema

Nao baadhi ya wanufaika wa Mkopo huo wameipongeza Serikali na kumpongeza Waziri Nanauka kwa maono na kutekeleza ahadi aliyoitoa wakati wa kampeni zake ambapo kwa sasa wataweza kujiendesha kiuchumi na kupunguza makali ya ugumu wa maisha na kuingizia taifa mapato.






Share:

WALIMU DODOMA WAELEKEA KOREA KUSINI KWA ZIARA YA KIMASOMO


Na Mwandishi Wetu

UJUMBE wa walimu na viongozi wa elimu kutoka Mkoa wa Dodoma wapatao 40 umeondoka kwenda Korea Kusini kujifunza, namna ya kufundisha, kusimamia shule na kutumia teknolojia katika elimu.

Ujumbe huo unatarajiwa kushiriki programu ya mafunzo na ziara ya kielimu ya siku nne kamili nchini Korea Kusini, ikiwa ni sehemu ya kutambua mchango wa walimu walioonesha utendaji bora na kufanikisha ongezeko la ufaulu wa wanafunzi katika Mkoa wa Dodoma.

Mratibu wa safari hiyo ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Global Education Link, Abdulmalik Molle alisema walimu hao waliondoka juzi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam, Juni 27, 2026, kuelekea Seoul, Korea Kusini, kupitia Doha, Qatar.

Alisema ziara hiyo ya kimasomo itafanyika kwa siku nne, ambapo walimu na viongozi wa elimu wanatarajiwa kushiriki katika mafunzo, kubadilishana uzoefu na kujifunza kuhusu matumizi ya teknolojia, ubunifu, uongozi wa shule na mbinu za kisasa za ufundishaji.

Alisema katika ziara hiyo ya siku nne, ujumbe unatarajiwa kujifunza namna Korea Kusini inavyotumia teknolojia, ubunifu, nidhamu na usimamizi bora katika kuimarisha ufundishaji na ujifunzaji.

Alisema walimu wanatarajiwa kupata uzoefu kuhusu matumizi ya vifaa na mifumo ya kidijitali darasani, maandalizi ya masomo, ushirikishwaji wa wanafunzi na ufuatiliaji wa maendeleo yao ya kitaaluma.

Alisema kabla ya safari hiyo, walimu na viongozi wa elimu waliomo katika ujumbe walipatiwa mafunzo maalumu ya maandalizi ambapo walielezwa kuhusu mazingira ya Korea Kusini, utamaduni wa nchi hiyo, nidhamu, utunzaji wa muda na wajibu wao kama wawakilishi wa Mkoa wa Dodoma na Tanzania.

Alisema mbali na kushiriki katika udhamini, taasisi ya Global Education Link imeratibu maandalizi mbalimbali ya ujumbe na kutoa mwongozo muhimu kwa washiriki kabla ya kuondoka nchini.

Akizungumza wakati wa mafunzo hayo, Mollel aliwataka washiriki kutumia safari hiyo kama fursa ya kujifunza na kurejea na maarifa yatakayoweza kuleta mabadiliko yanayoonekana katika shule za Mkoa wa Dodoma.

Alisisitiza kuwa lengo la safari si kufika na kutembelea Korea Kusini pekee, bali kupata uzoefu wa kimataifa kuhusu matumizi ya teknolojia katika elimu, mbinu za kisasa za ufundishaji, usimamizi wa shule na mikakati ya kuongeza ufaulu wa wanafunzi.

Katika mafunzo hayo, washiriki walipatiwa maelezo kuhusu jiografia, uchumi, maendeleo ya teknolojia, hali ya hewa, utamaduni, mila na mfumo wa elimu wa Korea Kusini.

Pia walielekezwa kujiandaa kisaikolojia na kimwili, kuheshimu muda, kufuata ratiba rasmi na kuzingatia sheria na utamaduni wa nchi watakayotembelea.

Mollel alisema safari hiyo ni matokeo ya jitihada za Mkoa wa Dodoma za kutambua, kuthamini na kuwapa motisha walimu walioonesha utendaji mzuri katika kutekeleza majukumu yao na kuwasaidia wanafunzi kupata matokeo bora.

Alisema mpango huo ulitokana na Mkutano wa Wadau wa Elimu wa Mkoa wa Dodoma uliofanyika jijini Dodoma na kuongozwa na Waziri mwenye dhamana ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.

Mollel alisema mkutano huo uliwakutanisha viongozi wa Serikali, walimu, maofisa elimu, viongozi wa shule, taasisi za umma, sekta binafsi na wadau wengine wa maendeleo ya elimu.

Molle alisema katika mkutano huo, walimu, wanafunzi na shule zilizofanya vizuri katika matokeo ya kitaaluma zilitambuliwa na kupongezwa kutokana na mchango wao katika kuinua kiwango cha elimu mkoani Dodoma.

Alisema mpango wa kuwapeleka walimu Korea Kusini ulianzishwa kama sehemu ya kutoa motisha kwa walimu walioonesha kujituma, nidhamu, uwajibikaji na mafanikio katika kufundisha na kuwawezesha wanafunzi kufanya vizuri.

Alisema safari hiyo imefanikishwa kupitia ushirikiano wa Serikali ya Mkoa wa Dodoma na wadau mbalimbali wa elimu, wakiwamo Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, Benki ya NMB na Global Education Link.

Alisema ushirikiano huo unaonesha namna Serikali na wadau wanavyoweza kuunganisha nguvu katika kutambua utendaji bora na kutoa fursa za maendeleo ya kitaaluma kwa walimu.


Share:

DMG NAMED BEST MARITIME COMPANY AT MOROGORO AWARDS 2026

By Staff Writer

Morogoro, Tanzania – June 27, 2026_ — Dar es Salaam Merchant Group (DMG) has clinched the coveted _Best Maritime Technology Company of the Year_ award at the 2026 Morogoro Business Awards, cementing its position as a leader in Tanzania’s technological transformation of the blue economy.

The win comes just weeks after DMG was recognized by Forbes Africa as one of the few class one maritime companies in building ships in Africa, citing its pioneering work in port digitalization, shipbuilding, and smart logistics.

The prestigious award was presented by Hon. Adam Kigoma Malima, Morogoro Regional Commissioner, during a gala ceremony held on June 27, 2026. The event brought together top CEOs, innovators, and government officials to celebrate enterprises driving Tanzania’s economic growth through technology and innovation.

The award recognizes DMG’s commitment to _Building Dreams with Lasting Quality_ through a unified service ecosystem that spans the entire project lifecycle. Backed by international standards and deep regional expertise, the company delivers end-to-end maritime technology solutions — from initial feasibility studies through to final delivery and post-implementation support.

Speaking after receiving the award, Dar es Salaam Merchant Group Managing Director Rayton Kwembe said the honor reflects years of relentless innovation and teamwork.

“This award is not just for DMG — it is for every Tanzanian who believes our maritime sector can compete with the best in the world,” said Kwembe. “Three years ago, we set out with a simple vision: use technology to unlock the full potential of Tanzania’s maritime sector. Today, that vision is reality. From Dar es Salaam, Kigoma to Zanzibar and Mtwara, our shipyards are facilitating trade by making sure ships are running smoothly to transport goods and people across borders.”

Kwembe emphasized that the win is a call to do more: “Maritime technology is the backbone of our blue economy. We cannot industrialize without digitizing our gateways to the world. This award challenges us to innovate further. We dedicate this to our engineers, developers, and port partners who work 24/7 to keep Tanzania moving.”

Hon. Adam Kigoma Malima praised DMG’s impact during the handover, noting that “companies like Dar es Salaam Merchant Group are proving that Tanzanian firms can lead Africa in technology. Your work aligns directly with the government’s agenda to modernize trade infrastructure and attract global investment.”

The Morogoro Business Awards, now in its 6th year, evaluates companies on innovation, impact, scalability, and contribution to national development.

DMG’s technology suite is now deployed across strategic installations and is being eyed for regional expansion into East Africa. The company also runs a flagship “Maritime Tech Academy” in partnership with local universities to build homegrown skills.

“This is just the beginning,” Kwembe added. “Our next frontier is connecting Tanzania’s maritime ecosystem to the global digital supply chain. With support from government and the private sector, we will continue achieving the best.”

He concludes by saying that the award solidifies DMG’s reputation as the go-to partner for governments and corporations seeking to modernize maritime operations.

Industry analysts and economists say the win positions Tanzania as an emerging hub for maritime technology innovation on the continent. Leading maritime technology consultant Dr. Amina Shaban noted that “DMG’s award signals a shift — East Africa is no longer just adopting foreign maritime systems, but exporting homegrown solutions. Their integrated approach from feasibility to final delivery sets a new benchmark for quality excellence in the region.”

Morogoro-based economist Nicholas Gilliard added: “Every shilling invested in maritime tech returns 3-4x in trade value. This award is recognition that DMG can continue to support Tanzania’s blue economy in driving the Vision 2050.”


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JUNI 30, 2026

Magazetini Leo































Share:

Monday, 29 June 2026

WAZIRI SANGU: MAHUSIANO, AMANI NA UMOJA NI MSINGI WA MAENDELEO YA TAIFA

 

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Mhe. Deus Sangu amesema kuwa uamuzi wa Serikali ya Awamu ya Sita wa kuanzisha Wizara maalum yenye dhamana ya kushughulikia masuala ya Mahusiano inaakisi maono ya Mheshimiwa Rais, Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuimarisha Umoja, Mshikamano na Amani nchini.

“Dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa taifa lenye amani, mshikamano na maendeleo kupitia mazungumzo, maridhiano na ushirikiano wa wadau wote,” amesema.

Mhe. Sangu amesema hayo Juni 28, 2026 katika Ibada maalumu ya kilele cha harambee iliyofanyika kwenye ushirika wa Amani wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kati, mjini Singida ambapo alieleza kuwa Serikali imeendelea kujenga mazingira ya mazungumzo na ushirikiano kati yake na taasisi za dini ili kuimarisha mshikamano wa kitaifa.

Alisema Ofisi ya Waziri Mkuu kuratibu Mahusiano ni utekelezaji wa maelekezo ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan pamoja na kutimiza wito wa kibiblia wa kuwaleta watu pamoja bila kujali tofauti za kisiasa, kidini au kikabila.

Vile vile, Waziri Sangu amempongeza Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba kwa kusimamia karibu agenda ya mahusiano nchini, jambo ambalo limewezesha viongozi wa dini kupata fursa ya kuwasilisha hoja zao serikalini kupitia wizara hiyo, hatua ambayo imeongeza ushirikiano na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi.

Aidha, alisema jukumu la kuwasikiliza wananchi, hususan wanyonge na wenye mahitaji, ni sehemu ya wajibu wa Serikali na linaendana na mafundisho ya dini yanayohimiza kuwajali wahitaji na kujenga jamii yenye haki na mshikamano.

Kwa upande mwengine, Waziri Sangu aliwashukuru viongozi wa dini kwa kuendelea kuliombea Taifa na viongozi wake, na kusema maombi yao yamekuwa nguzo muhimu katika kudumisha amani, utulivu na maendeleo ya nchini.

Kadhalika, Mhe. Sangu amesema Serikali itaendelea kushirikiana kwa karibu na taasisi za dini pamoja na wadau wengine katika kuimarisha mahusiano ya kijamii na kisiasa, ikiwa ni pamoja na kuendelea kufanya mazungumzo na vyama vya siasa kwa lengo la kuimarisha umoja wa Watanzania.

Share:

PROF. SHEMDOE AWAASA WANAFUNZI KUENDELEZA VIPAJI VYAO VYA MICHEZO, SANAA


•Awataka kuwa na nidhamu na kusoma kwa bidii

Na OWM - TAMISEMI, Iringa

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amewaasa wanafunzi walioshiriki mashindano ya UMISSETA mwaka 2026 kuendeleza vipaji vya michezo na Sanaa walivyonavyo kwani vitawasaidia katika maisha yao ya baadaye, huku akiwataka kuzingatia nidhamu na kusoma kwa bidii ili  kufikia ndoto zao na kutoa mchango katika maendeleo ya taifa.

Prof. Shemdoe ametoa wito huo kwa wanafunzi leo Juni 28, 2026 mjini Iringa katika Viwanja vya Shule ya Sekondari Lugalo, wakati akifunga mashindano ya UMISSETA kwa mwaka wa 2026.

“Nina wasihi muendelee kuwa na nidhamu, kujituma katika masomo yenu na kuendeleza vipaji vyenu vya michezo na sanaa, msiviache vipaji vyenu kwani hata mimi juzi tulipokuwa tunapokea Mwenge wa Uhuru Lushoto nilijikuta nikikumbushia kipaji changu cha kupiga ngoma za utamaduni na kuimba kwa umahiri,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe amewahakikishia wanafunzi hao kuwa, Serikali itaendelea kuweka mazingira bora ya kuhakikisha vipaji vya wanafunzi vinaibuliwa, vinatambuliwa, vinakuzwa ili kuwanufaisha na kulinufaisha taifa kupitia ushiriki wao katika kuliwakilisha taifa kwenye mashindano ya michezo na Sanaa ndani na nje ya nchi.

Aidha, Prof. Shemdoe ametumia fursa hiyo kumpongeza Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kuipa kipaumbele sekta ya elimu, michezo, sanaa na maendeleo ya vijana kwenye ajenda kuu ya taifa na kuongeza kuwa, uwekezaji huo unaendelea kuweka msingi imara wa kuibua na kuendeleza vipaji vya watoto na vijana wa Tanzania.

 Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI anayeshughulikia Elimu Bw. Atupele Mwambene amesema kuwa, ushiriki wa wanafunzi katika michezo mbalimbali ya UMITASHUMTA na UMISSETA umeendelea kuwa jukwaa muhimu la kitaifa la kuibua vipaji, kuimarisha afya, kujenga urafiki na kuendeleza umoja wa kitaifa miongoni mwa wanafunzi. 

Naye Mwakilishi wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Bi. Leah Kihimbi amemuhakikishia Prof. Shemdoe kuwa wizara yake itatekeleza ipasavyo jukumu la kuibua kuendeleza vipaji na vipawa vinavyotokana na mashindano hayo ya sanaa na michezo shuleni. 

Mwakilishi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar ambaye ni Afisa Mdhamini Bw. Mohamed Nassoro Salimu amesema Zanzibar inakwenda kujipanga ili kuleta ushindani mkubwa katika mashindano ya mwakani, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi ya kufanya mageuzi katika sekta ya michezo.

Akitoa neno la shukrani, Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI Bw. Adolf Ndunguru amewashukuru maafisa elimu, wakuu wa shule, walimu, waratibu wa michezo na walezi wa wanafunzi, kwa kazi kubwa walioifanya ya kuwaandaa na kuwaleta wanafunzi katika mashindano ambayo yamewawezesha kujifunza thamani ya nidhamu, ushindani wa haki, uvumilivu, uzalendo na mshikamano wa kitaifa.











Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger