Waziri wa Uchukuzi Mheshimiwa Profesa Makame Mbarawa wa pili kutoka kulia akiwa pamoja na mwenyeji wake mkuu wa mkoa wa Ruvuma Brigedia Jenerali Ahmed Abbas Ahmed baada ya kuzindua jengo la mapumziko ya muda mfupi kwa abiria katika uwanja wa ndege wa Songea unatarajiwa kuwa chachu ya maendeleo ya kiuchumi katika ukanda wa kusini Na Regina Ndumbaro
Songea-Ruvuma
Uwekezaji wa Serikali wa shilingi milioni 842 katika upanuzi wa jengo la mapumziko ya muda mfupi kwa abiria katika uwanja wa ndege wa Songea unatarajiwa kuwa chachu ya ukuaji wa biashara, uwekezaji na utalii, baada ya kuongeza uwezo wa uwanja huo kuhudumia abiria 300 kwa wakati mmoja.










































