Monday, 20 April 2026

UVCCM BUKOBA YATOA VIFAA VYA MICHEZO KUELEKEA MASHINDANO YA “BUKOBA CUP 2026”


Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi UVCCM Bukoba Bw. James MichaelNyamanza (kulia) akimkabidhi zawadi za washindi wa mashindano ya UVCCM BUKOBA CUP 2026 Katibu wa Chama cha Mpira Wilaya ya Bukoba Bw. Mwinyi Mohamed Mwinyi (kushoto) na katikati ni Katibu wa chama cha mpira Mkoa wa Kagera Bw. Ali Amini Abdul

**

Na Mbuke Shilagi Kagera. 

Mwenyekiti wa UVCCM Manispaa ya Bukoba, James Michael Nyamanza, amekabidhi jezi na mipira kwa wawakilishi wa Kata zote 14 za manispaa hiyo ikiwa ni maandalizi ya mashindano ya UVCCM Bukoba Cup 2026 yanayotarajiwa kuanza rasmi Ijumaa, tarehe 24 Aprili 2026.

Katika hafla hiyo, mwenyekiti huyo pia amekabidhi zawadi zitakazotolewa kwa washindi kwa Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Bukoba, akisisitiza kuwa lengo la mashindano hayo ni kuwakutanisha vijana, kujenga mahusiano, kuibua na kuendeleza vipaji pamoja na kuchochea ukuaji wa uchumi kupitia michezo.

Ameeleza kuwa kupitia mashindano hayo, vijana watapata fursa ya kuonesha uwezo wao huku wakijenga nidhamu na mshikamano, mambo ambayo ni muhimu katika maendeleo ya jamii.

Kwa upande wake, Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Bukoba, Mwinyi Mohamed Mwinyi, amesisitiza umuhimu wa kufuata taratibu zote za michezo, akieleza kuwa shughuli yoyote ya michezo katika ngazi ya wilaya lazima ipitie kwa viongozi husika na kupata kibali kinachotolewa hadi ngazi ya Mkoa kwa kuzingatia kanuni na sheria za michezo.

Amefafanua kuwa mashindano hayo yataendeshwa kwa kuzingatia Sheria 17 za mpira wa miguu, huku kila Kata ikicheza mechi za nyumbani na ugenini, pamoja na kuzingatia mfumo wa bao la ugenini.

Naye Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Kagera, Ali Amin Abdul, amempongeza Mwenyekiti wa UVCCM Bukoba kwa kuanzisha mashindano hayo pamoja na kudhamini vifaa na zawadi kwa washindi. 

Huku akibainisha kuwa kuanzia hatua ya robo fainali na nusu fainali, mechi zitachezwa kwa dakika 90 na endapo sare itatokea, mshindi atapatikana kwa njia ya mikwaju ya penalti, huku fainali ikichezwa kwa dakika 90 pamoja na dakika 30 za nyongeza kabla ya penalti iwapo sare itaendelea.

Ikumbukwe kuwa, mashindano ya UVCCM Bukoba Cup 2026 yanatarajiwa kuanza rasmi Ijumaa, tarehe 24 Aprili 2026, ambapo mchezo wa ufunguzi utazikutanisha timu za Kashai na Bilele katika Uwanja wa Kaitaba stadium.

Share:

Sunday, 19 April 2026

TUMUOMBEE RAIS, TULIOMBEE TAIFA-MASHILI



Na Mwandishi wetu,Tabora

Watanzania wamehamasishwa kuendelea kumuombea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe Dkt. Samia Suluhu Hassan ili aweze kupata utulivu wa kuliongoza Taifa la Tanzania kwa amani, upendo na mshikamano.

Rai hiyo imetolewa leo Aprili 19, 2026 na Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya MASHILI COMPANY LIMITED ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Mradi wa Uchenjuaji Dhahabu wa (Matinje Mining, Msilale Mining na Igurubi Mining) Ndg Peter Andrea Mashili aliposhiriki tamasha la Inland Festival lililoandaliwa na kanisa la Africa Inland Church Tanzania - AIC Wilayani Nzega katika mkoani Tabora.

Mashili amesema kuwa Mhe Rais Dkt. Samia anafanya kazi kubwa ya kuifungua nchi na kuleta maendeleo hivyo ni jukumu la wananchi kuhakikisha wanamuombea ili aweze kuongoza kwa busara na mshikamano wa kitaifa.

Pia Mashili amewataka viongozi wa dini na wananchi wote wa wilaya ya Nzega kumuombea Mbunge wa jimbo la Nzega Mjini Mhe Hussein Bashe ili aweze kuitumikia nafasi yake kwa uaminifu na weledi katika bunge la Tanzania.

Amesisitiza umuhimu wa kuwaombea viongozi wote katika nchi itasaidia kutangaza na kuhubiri amani jambo ambalo litalifanya Taifa la Tanzania kuwa na utulivu.

"Maombi ni silaha hivyo naendelea kusisitiza kuwaombea viongozi wetu kwani jambo hilo litarahisisha uenezaji wa injili na kuwafanya watanzania kuendelea kuwa na mshikamano wa kudumu" Amekaririwa Mshili

Katika tamasha hilo Peter Mashili amechangia jumla ya shilingi 3,200,000 kwa ajili ya kuunga mkono maboresho ya studio ya Inland Tv na ununuzi wa vifaa vya kurushia matangazo ya televisheni na redio ya kanisa hilo.








Share:

DIWANI WA KATA YA KILIMANI JIJINI DODOMA AANZA ZIARA YA MTAA KWA MTAA KUSIKILIZA CHANGAMOTO MBALIMBALI KWA WANANCHI



Na Barnabas Kisengi Dodoma

Wananchi wa Mtaa wa image kata ya kilimani Jijini Dodoma wamelalamikia mamlaka ya Maji safi na usafi wa mazingira (Duwasa) pamoja na kampuni inayokusanya takataka katika mtaa wa Image pamoja na wakala wa barabara za Mjini na vijijini (Tarura) kwa ubovu wa miundombinu ya barabara za Mtaa wa Image.

Wakizungumza katika mkutano wa hadhara wa Mhe Diwani wa kata ya kilimani Jijini Dodoma wamesema kuwa wamekuwa na kero kubwa ya kupasuka kwa Bomba kubwa ambalo limekuwa likivujisha maji ambayo yamekuwa yakimwagika na kuleta hasara katika makazi yao licha ya pia kuwa ni upotevu wa maji katika eneo hilo ambayo ni hasara kwa mamlaka hiyo pia wamezungumzia changamoto nyingine ni ubovu wa miundombinu ya barabara za mitaa huo pamoja na kuwekewa Taa za barabarani katika Mtaa huku wakilalamikia miundombinu ya barabara za mtaa huo kuwa ni mbovu jambo linalowapelekea wakishindwa kupita na vyombo vya usafiri kama magari na bajaji mtaani hapo.

"Hili swala la bomba kupasuka limekuwa kero kubwa kwetu licha ya kutoa taarifa kwenye mamlaka husika pamoja na wataalamu wa Duwasa kufika lakini hatujaona hatua zozote zilizo chukuliwa hadi Sasa jambo ambalo tunalihofia kuwa bomba hili likizudi kupasuka litaleta athari kubwa katika makazi pamoja na hizo changamoto bado tunachangamoto nyingine ya miundombinu ya barabara za mtaa wetu sio rafiki jambo ambalo wakazi wenye vyombo vya usafiri kama magari na bajaji kushindwa kuingia katika baadhi ya maeneo yetu kwenye mtaa hata tunapo kuwa na mgonjwa huwa ni shida kuingia katika maeneo yetu ya mtaa wetu amesema moja wa wananchi akiwawakikisha Wananchi wenzake katika mkutano wa hadhara wa Mhe Diwani wa kata hiyo hivyo tunaomba sana Mhe Diwani na wataalamu wako tena tumeona viongozi wa chama hapo mtusaidie kutatua changamoto hizi kwetu imekuwa kero ya muda mrefu licha ya kuripoti kwa viongozi wetu wa mtaa sasa tunaamini kuwa viongozi wa CCM kata na wataalamu kutoka kata sasa tunaamini kuwa tutapata ufumbuzi wa changamoto zetu za Mtaa kushulikiwa Ipasavyo.amesema moja wa wananchi akiwawakikisha Wananchi wengine Mzee Sebastian Chambasi

Aidha wananchi hao wakatoa changamoto nyingine za uwepo wa takataka kwa muda mrefu ambazo hazijachukuliwa kwa muda mrefu licha ya wao kuchangia pesa jambo ambalo ni hatari linaloweza kusababisha magonjwa ya mlipuko kama kipindupindu na kulalamikia kuwepo kwa mtaro ambao umekuwa na Mamba ambao wamekuwa wakionekana mara kwa mara huku watoto wakiwa wanapita kwenye mtaro huo ambao ni hatari kwa maisha ya watu wanao pita kwenye mtaro huo hivyo wameomba wahusika wafuatilie swala hilo kwa uharaka.

Akijibu changamoto hizo Diwani wa kata ya kilimani Jijini Dodoma Mhe Mussa Mkunda amesema kuwa changamoto zote hizo amezichukuwa na wanakwenda kuzifanyia kazi kwa haraka ili kuleta tija kwa wananchi wa Mtaa wa image huku akimwelekeza afisa mifugo wa kata Bi Tabia Shani kuwasiliana haraka na watu wa maliasi ili kuweza kutatua changamoto hiyo kwa haraka ili isije ikasababisha maafa katika mtaa huo kutokana na wananchi wanao vuka katika korongo hilo.

"Ndugu zangu wananchi wa mtaa wa image niwapongeze sana kwa kuweza kuelezea changamoto za mtaa wenu niwahakikishie Mimi kama Diwani wenu hapa zimefika na tunakwenda kuzifanyia kazi kwa haraka nitahakikisha Mimi na wataalamu wangu tulio ongozana nao na viongozi wa Chama cha mapinduzi ambao ndio tunatekeleza ilani tunazifanyia kazi ikiwemo kuwafukia wahuusika wote kwa haraka ili kuhakikisha changamoto zote mlizo sema zinafanyiwa kazi kwa haraka na kuleta tija kwenye Mtaa huu niwaahidi kwakuwa nimeongozana na wataalamu na viongozi wa chama tutahakikisha tumemaliza hizi changamoto zote za Mtaa naomba muendelee kuniamini Mimi ni Diwani niliyotokana na chama cha mapinduzi hivyo kwenu lazima niwe msikivu na kwakuwa tunatekeleza ilani ya chama cha mapinduzi ndio maana nimeongoza na viongozi wa CCM hapa pamoja na wataalamu"amesema Diwani wa kata ya kilimani Mhe Mussa Mkunda

Kwa upande Wake katibu wa chama cha mapinduzi CCM kata kilimani Ramadhani Ramadhani amesema kuwa kama chama ndicho chenye ilani inayotekelezwa kwa kipindi Cha 2025/2030 wao kwa kushirikiana na serikali watahakikisha changamoto zote zilizojitokeza kwenye mkutano huo zinafanyiwa kazi kwa haraka ili kuweza kuhakikisha wananchi wanakuwa katika mazingira mazuri na salama kwenye Mtaa huo.

Ziara hiyo ya Mhe Diwani wa kata ya kilimani ya Mtaa kwa mtaa imeanza katika mtaa wa Image na itaendele katika Mtaa wa kilimani, Nyerere na itamalizika katika Mtaa wa Chinyoyo ikiwa na lengo kuu la kuongea na Wananchi wa Mtaa husika kusikiliza changamoto mbalimbali zilizop kwenye mitaa minne ya kata ya kilimani Jijini Dodoma.

Ziara hiyo ya Mhe Diwani imewashirikisha viongozi wa chama cha mapinduzi CCM kata ya kilimani wakimbatana na wataalamu kutoka ofisi ya Mtendaji wa kata ya kilimani ikiongozwa na Mtendaji wa kata ya kilimani akiongozana na wataalamu wake afisa afya ,afisa maendeleo ya jamii,afisa mifugo,Police kata na watendaji wa mitaa yote minne ya kata ya kilimani pamoja na viongozi wa chama cha mapinduzi kata ya kilimani Jijini Dodoma.





Share:

BARRICK BULYANHULU YAKABIDHI TREKTA WILAYA NYANG’WALE KUFANIKISHA USAFI WA MAZINGIRA


Afisa Mwandamizi wa Idara ya Mahusiano kwa Jamii katika Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Zuwena Senkondo (kulia) akipeana mkono wa shukrani na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'wale John Isack wakati wa hafla ya makabidhiano ya Trekta kwa ajili ya kusomba taka na kufanya usafi kwenye halmashauri ya Wilaya ya Nyang'wale.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'wale John Isack (kushoto) wakipongezana na Afisa Mwandamizi wa Idara ya Mahusiano kwa Jamii katika Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Zuwena Senkondo (kulia) wakati wa hafla ya makabidhiano ya Trekta kwa ajili ya usafi kwenye halmashauri ya Wilaya ya Nyang'wale.
  Muonekano wa Trekta iliyotolewa na Mgodi wa Barrick Bulyanhulu kwa ajili ya kusomba taka na kufanya usafi kwenye halmashauri ya Wilaya ya Nyang'wale.
Viongozi wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na wa halmashauri ya wilaya ya Nyang’wale wakipeana vifaa kwa ajili ya usafi kwenye halmashauri hiyo.
Afisa Mwandamizi wa Idara ya Mahusiano kwa Jamii katika Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Zuwena akizungumza kwenye halfa hiyo ya makabidhiano ya trekta kwa halmashauri ya Nyang’wale
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang'wale John Isack (Katikati) na kulia kwake ni Senkondo Afisa Mwandamizi wa Idara ya Mahusiano kwa Jamii katika Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Zuwena wakiwa kwenye utiaji wa saini katika halfa ya makabidhiano ya trekta kwa ajli ya kusomba taka na ufanyaji wa usafi kwenye halmashauri hiyo
Wafanyakazi wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu na wa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’wale wakiwa kwenye picha ya pamoja
***

Mgodi wa Barrick Bulyanhulu umeendelea kutekeleza sera yake ya mkakati endelevu wa kusaidia jamii baada ya kukabidhi trekta ya kusomba taka yenye thamani ya shilingi  milioni 66 pamoja na vifaa vya kufanyia usafi kwa Halmashauri ya Wilaya ya Nyang’wale kupitia fedha za Uwajibikaji kwa Jamii (CSR) katika juhudi zake za kutunza mazingira nchini.

Akiongea katika hafla ya makabidhiano ya trekta hiyo, kwa niaba ya Mkurugenzi wa Halmshauri ya Wilaya ya Nyang'wale , Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, John Isack alisema msaada huo umekuja kwa wakati katika juhudi za kulinda na kutunza mazingira kwa maslahi ya wakazi wa wilaya hiyo na vitongoji vyake.

“Tunashukuru Barrick Bulyanhulu kwa msaada huu wa trekta , tunaamini sasa hali ya usafi katika Wilaya yetu itakuwa nzuri kwa kiasi kikubwa kwani hii ni trekta ya pili wametupatia, matarajio yetu ni kuongeza kasi ya kuondoa taka kutoka hapo awali ya kutoa mara mbili kwa wiki, awali tulikuwa tunazoa taka katika siku za Alhamisi na Jumatatu hivyo tutaongeza siku pia tunatarajia kuongeza huduma kwa maeneo ya miji inayokuwa kwa kasi kibiashara kama vile Bosolwa, Nyijundu, Bukwimba na maeneo ya migodini",alisema.

Isack aliongeza kuwa kampuni ya Barrick Bulyanhulu kupitia uwekezaji wake imefanikisha miradi mingi ya kijamii na utunzaji wa mazingira wilayani humo kupitia fedha za uwajibikaji kwa jamii ambayo inazidi kuboresha maisha ya wananchi.

“Leo tumepokea Trekta ambalo limenunuliwa na kampuni ya Barrick Bulyanhulu kwa gharama ya Shilingi Milioni 66 , Trekta hili ni maalum kwa kazi ya kuzoa uchafu na kupeleka dampo kwa kweli ni msaada mkubwa kwa wilaya yetu kwani kwa miaka mingi sana tumekuwa na changamoto juu ya uzoaji wa taka katika mitaa yetu ukichukulia kwamba mji wetu unakua kwa kasi na kupelekea uzalishaji wa taka kuongezeka kwa kasi, na ni matarajio yangu sasa mazingira ya Wilaya yetu yatakuwa safi, nichukue fursa hii kuwaomba wananchi kufanya usafi kila siku kwani tayari kwa sasa tunalo trekta ambalo litakuwa linasomba taka mara kwa mara”, alisema.

Kwa upande wake Afisa Mwandamizi wa Idara ya Mahusiano kwa Jamii katika Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Zuwena Senkondo alitoa shukrani kwa viongozi wa serikali na wananchi kwa kuwa na uhusiano mzuri na Kampuni hiyo na kuongeza kuwa msaada wa trekta lililokabidhiwa ni kwa ajili ya kufanya usafi na utunzaji wa mazingira.

“Niwaombe ndugu zangu usafi ni jukumu letu sote,trekta hili tulitunze ili liweze kuboresha mazingira yetu ipasavyo ,milioni 66 ni pesa nyingi hivyo naamini tutakuwa tumefungua njia ya kuboresha mazingira ya usafi wilayani Nyang’hwale, haswa ikizingatia kampuni ya Barrick Bulyanhulu ni wadau wakubwa wa utunzaji wa mazingira”, alisisitiza Zuwena.







Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI APRILI 19,2026




Magazeti
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger