Saturday, 4 July 2026

JAB YATAKIWA KUONGEZA KASI YA UTOAJI ELIMU NA HUDUMA KWA WAANDISHI WA HABARI




Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam

Mkurugenzi wa Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Bi. Savera Salvatory, ameielekeza Bodi ya Ithibati ya Waandishi wa Habari (JAB) kuongeza juhudi katika kutangaza huduma zake zinazotolewa kwenye Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba), ili kuwafikia waandishi wengi zaidi na kuwahamasisha kupata huduma kwa wakati.

Bi. Savera amesema hatua hiyo pia itasaidia kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu majukumu ya JAB pamoja na umuhimu wa waandishi wa habari kuwa na ithibati kwa mujibu wa sheria na miongozo inayosimamia taaluma hiyo.

Ameyasema hayo leo, Julai 4, 2026, alipofanya ziara katika Kijiji cha Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kinachoshirikisha taasisi mbalimbali zilizo chini ya wizara hiyo, ambapo alijionea huduma na elimu inayotolewa kwa wananchi na wadau wanaotembelea maonesho hayo.

Katika ziara hiyo, Bi. Savera alipata fursa ya kutembelea banda la JAB na kujionea namna huduma za ithibati, usajili pamoja na utoaji wa elimu kuhusu taaluma ya uandishi wa habari zinavyotolewa kwa waandishi na wananchi.

Aidha, aliambatana na Mkurugenzi Msaidizi wa Utawala, Bi. Zahra Guga, ambaye alimpongeza Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa JAB, Wakili Patrick Kipangula, kwa usimamizi wake wa karibu wa shughuli za banda hilo kupitia ziara za mara kwa mara wakati wa maonesho.

Bi. Guga alisema uwepo wa viongozi katika banda la JAB unachochea uwajibikaji, huongeza ufanisi wa utoaji wa huduma na kuimarisha utoaji wa elimu kwa wadau wanaotembelea maonesho ya Sabasaba.






Share:

JWTZ YATOA TAHADHARI DHIDI YA VURUGU, YASISITIZA HATUA ZA KISHERIA KWA WATAKAOVUNJA AMANI



Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limetoa tahadhari kwa wananchi dhidi ya kushiriki au kuhamasishwa kushiriki katika vitendo vya vurugu na uvunjifu wa amani, likisisitiza kuwa litachukua hatua kali za kisheria dhidi ya yeyote atakayejihusisha na vitendo vinavyohatarisha usalama wa nchi.

Katika taarifa kwa umma iliyotolewa Julai 4, 2026 na Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa JWTZ, Luteni Kanali Sylvester Mangure, Jeshi limesema hali ya mipaka ya Tanzania na usalama wa ndani ya nchi ni shwari kutokana na ushirikiano uliopo kati ya wananchi na vyombo vya ulinzi na usalama katika kulinda amani na utulivu.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa mazingira ya amani yaliyopo yamewawezesha wananchi kuendelea na shughuli zao za uzalishaji na maendeleo, huku ikibainisha kuwa kuna watu wanaoendelea kutumia njia za uchochezi na upotoshaji kuwashawishi wananchi kushiriki katika vitendo vya vurugu vinavyolenga kuvuruga utulivu wa nchi.

JWTZ limeonya kuwa vitendo hivyo vinaweza kusababisha madhara makubwa, ikiwemo kuhatarisha maisha ya wananchi, kuharibu mali, kusimamisha shughuli za uzalishaji na kudhoofisha uchumi wa Taifa.

Kutokana na hali hiyo, Jeshi limewataka wananchi kupuuza wito wowote unaohamasisha vurugu na kuendelea na shughuli zao za kila siku bila hofu, huku likisisitiza kuwa lina mamlaka ya kuchukua hatua stahiki kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 pamoja na Sheria ya Ulinzi wa Taifa dhidi ya wote watakaobainika kujihusisha na vitendo hivyo.

Aidha, JWTZ limewahimiza wananchi kutoa taarifa kwa viongozi wa vijiji, mitaa na vyombo vya ulinzi na usalama kuhusu viashiria vyovyote vya uchochezi au uvunjifu wa amani ili hatua zichukuliwe mapema.

Jeshi pia limewahakikishia wananchi kuwa litaendelea kutekeleza majukumu yake ya kulinda nchi, Katiba na wananchi, pamoja na kushirikiana na vyombo vingine vya ulinzi na usalama katika kuhakikisha amani, utulivu na umoja vinaendelea kudumishwa kwa maslahi ya Taifa.
Share:

JUKWAA LA BIASHARA NA UWEKEZAJI TANZANIA–KOREA LATANGAZA FURSA ZA DODOMA


Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Dkt. Richard Muyungi amevutiwa na Kijiji cha Mazingira katika Maonesho ya Kimataifa ya Biashara ya Dar es Salaam (Sabasaba).

Dkt. Muyungi amesema kilichomvutia zaidi ni kuona namna ambavyo vijana wabunifu wamepewa nafasi ya kuonesha ujuzi wao katika kutumia fursa zinazopatikana kwenye Mazingira kupitia kampeni ya Taka ni Fursa.

Dkt. Muyungi amesema kuna haja ya kuwawezesha vijana wenye mitaji midogo ili waweze kufanya mambo makubwa kupitia ubunifu wao kwenye kutumia fursa mbalimbali za urejelezaji na uchakataji taka ili kujipatia kipato na kusafisha Mazingira.

Dkt. Muyungi aliambatana na Mkurugenzi Mkuu wa NEMC Dkt. Immaculate Sware Semesi alipotembelea Kijiji cha Mazingira mara baada ya kushiriki hafla ya ufunguzi waaonesho hayo Julai 3,2026.
Share:

Friday, 3 July 2026

USHIRIKIANO WA WANANCHI NA POLISI SHINYANGA WATAJWA KUWA NGUZO YA USALAMA WA JAMII


Na Elizabeth Cosmas - Shinyanga

Wananchi wa Mkoa wa Shinyanga wameendelea kutambua umuhimu wa ushirikiano wao na Jeshi la Polisi, wakieleza kuwa hatua hiyo imeongeza uhuru wa kutoa taarifa za kiusalama na kuchangia kwa kiasi kikubwa kupunguza vitendo vya uhalifu katika maeneo mbalimbali ya mkoa huo.

Baadhi ya wakazi wa Shinyanga wamesema ushirikiano uliopo kati ya wananchi na Jeshi la Polisi umeimarisha hali ya usalama na utulivu, huku ukiwawezesha wananchi kushiriki kikamilifu katika kufichua na kuzuia vitendo vya uhalifu.

Mmoja wa wananchi hao, Tiffany Mswahili, mkazi wa Shinyanga, amesema hali ya kiusalama imeimarika tofauti na ilivyokuwa hapo awali, ambapo kwa sasa wananchi wamejengewa mazingira rafiki ya kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama bila hofu.

"Tunaweza kutoa taarifa za matukio ya kihalifu kwa uhuru zaidi kuliko zamani. Hii imeongeza imani kati ya wananchi na Jeshi la Polisi na imechangia kudhibiti uhalifu katika jamii," amesema Tiffany.

Akizungumza na Malunde Blog leo Julai 3, 2026, Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Magomi, amesema ushirikiano wa wananchi ndiyo msingi wa mafanikio katika mapambano dhidi ya uhalifu, kwani huwezesha upatikanaji wa taarifa kwa wakati na kuchochea hatua za haraka pindi matukio yanapotokea.

Amesema Jeshi la Polisi limeendelea kuimarisha uhusiano wake na wananchi kupitia mikakati mbalimbali inayolenga kujenga imani, jambo ambalo limeongeza ufanisi katika kudhibiti uhalifu na kulinda usalama wa raia na mali zao.

Kamanda Magomi amesema mfumo wa Polisi Kata umeendelea kuleta matokeo chanya kwa kuwawezesha askari kuwa karibu zaidi na wananchi, huku wakishirikiana na viongozi wa maeneo husika, wakiwemo madiwani, wenyeviti wa mitaa na vijiji pamoja na watendaji wa kata, kutatua changamoto mbalimbali za kiusalama.

Aidha, amesema Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga linaendelea kutoa elimu kwa umma kupitia njia mbalimbali ikiwemo semina mashuleni, mikutano ya hadhara, vijiwe vya bodaboda na majukwaa mengine ya kijamii, ili kuhamasisha wananchi kushiriki kikamilifu katika kudumisha amani na usalama.

"Lengo letu kuu ni kulinda raia na mali zao. Hili haliwezi kufanikiwa bila ushirikiano wa wananchi wenyewe. Ndiyo maana tunaendelea kuweka mkazo katika utoaji wa elimu na kujenga ukaribu na jamii," amesema Kamanda Magomi.

Ametoa wito kwa wananchi wa Mkoa wa Shinyanga kuendelea kuimarisha ushirikiano na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa za uhalifu na vitendo vyote vinavyoweza kuhatarisha usalama wa jamii, akisisitiza kuwa usalama ni jukumu la kila mwananchi.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga linaendelea kusisitiza kuwa ushirikiano kati ya wananchi na vyombo vya ulinzi na usalama ni nguzo muhimu ya kudumisha amani, utulivu na maendeleo ya Mkoa wa Shinyanga na taifa kwa ujumla.
Share:

YOGE URGES CLEAN ENERGY AND LIVESTOCK CONTROL IN RUVUMA



Authorities in the Ruvuma Region have been urged to accelerate the promotion of clean and affordable alternative energy—including coal‑based technologies—and to support community‑driven waste management enterprises as part of efforts to reduce deforestation and curb pollution.


The call was made by the Youth Environmental Justice and Gender Equality (YOGE) during the Regional Policy Summit in Songea, held under its Voices for Water Project, which focuses on inclusive water governance in the Ruvuma Basin. YOGE also recommended a complete prohibition and tighter control of large livestock herds entering the region, warning that unchecked influx threatens national food security given Ruvuma’s critical role in agricultural production.

Advocate Philomena Mwalongo, YOGE Executive Director, presented an overview of the project, noting that it has been implemented in Ruvuma for the past eight months with support from the IUCN BRIDGE Programme. She explained that a baseline survey revealed limited awareness among women and youth regarding water resource conservation, which the project has sought to address through training, dialogues, and community engagement.

Stakeholder voices added urgency:
👉Fatuma Gawaza of Matogoro Ward urged support for women and youth to access capital for pumps and irrigation ponds, enabling farming outside the 60‑meter buffer zone.

👉Acting Administrative Secretary Louis Chomboko pledged government commitment to awareness creation and clean energy initiatives.

👉Bishop John Ndimbo of Mbinga Diocese called for environmental education to be integrated into school curricula to instill conservation values early.

Plenary discussions highlighted persistent challenges in water resource management, including weak enforcement of environmental laws, political interference, buffer zone violations, and deforestation.

The initiative forms part of the Inclusive Freshwater Governance for Sustainable Communities in the Ruvuma Basin – Voices for Water Project, supported by IUCN through its BRIDGE Programme. Key implementing partners include Tanzania Media for Community Development (TAMCODE), YOGE, the Ruvuma Southern and Coastal Water Basin Board, the Office of the Regional Commissioner of Ruvuma, Mbinga Town Council, and Songea Municipal Council.

The summit brought together district authorities, regional leaders, water agencies, religious institutions, forest reserve representatives, water users, and the press—demonstrating collective resolve to strengthen inclusive water governance and environmental conservation across the Ruvuma Basin.
















Share:

Thursday, 2 July 2026

WAZIRI SANGU: TAASISI ZA DINI NI NGUZO YA AMANI, MAADILI NA MALEZI BORA


Na: OWM (KAM), Manyoni - Singida

Serikali imesema inatambua mchango mkubwa wa taasisi za dini katika kuimarisha huduma za kijamii kudumisha amani na kukuza maadili nchini huku ikizitaka viongozi wa dini kuendelea kushirikiana na Serikali katika kukuza malezi bora kwa watoto na vijana ili kujenga taifa lenye ustawi na mshikamano.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu Amesema hayo leo tarehe 2 Julai, 2026 alipomwakilisha Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba katika Kumbukizi ya Miaka 60 ya Uwepo wa Wamisionari wa Damu Azizi ya Yesu (C.PP.S) Provinsi ya Tanzania iliyofanyika katika viwanja vya Parokia ya Kupaa Bwana, Manyoni, Mkoani Singida.

Amesema, maendeleo ya taifa hayawezi kupatikana kwa juhudi za Serikali pekee bali yanahitaji ushirikiano wa wadau wote wakiwemo taasisi za dini sekta binafsi na wananchi hivyo alibainisha kuwa maadhimisho hayo ya miaka 60 Uwepo wa Wamisionari wa Damu Azizi ya Yesu (C.PP.S) Provinsi ya Tanzania ni ishara ya urafiki, mshikamano na dhamira ya pamoja ya kujenga Tanzania yenye amani na matumaini.

“Ushirikiano kati ya Serikali na taasisi za dini umeendelea kuwa nguzo muhimu ya maendeleo ya taifa kwa kusaidia utoaji wa huduma za kijamii, kuimarisha maadili na kujenga jamii yenye amani,” amesema

Kwa upande wake, Mhe. Sangu ametoa wito kwa viongozi wa dini kuendelea kuwa sauti ya matumaini kwa waliokata tamaa, chanzo cha upatanisho katika jamii na daraja la kuunganisha wananchi pale panapojitokeza migawanyiko. Ameongeza kuwa kuwa amani ndiyo msingi wa maendeleo na kwamba Watanzania wanapaswa kuendelea kuilinda na kuirithisha kwa vizazi vijavyo.

Vilevile, Alisisitiza kuwa vijana wanapaswa kutumia vipaji na maarifa yao bila kuacha misingi ya imani, akieleza kuwa maendeleo ya kweli yanahitaji kizazi kinachounganisha elimu maadili na hofu ya Mungu.

Naye Mkuu wa Mkoa wa Singida Halima Dendego amesema Serikali itaendelea kuzifanyia kazi changamoto zilizowasilishwa na viongozi wa Shirika la Wamisionari wa Damu Azizi ya Yesu (C.PP.S) Provinsi ya Tanzania, ikiwemo ushirikiano katika sekta ya afya na huduma za kijamii ili shirika hilo liendelea kutoa huduma kwa wananchi.

Kwa upande wake Kiongozi wa Shirika la Wamisionari wa Damu Azizi ya Yesu Padre Vedasto Ngowi waliishukuru Serikali kwa ushirikiano uliopo na kueleza matumaini yao ya kuendelea kushirikiana katika kuwaletea Watanzania maendeleo ya kiroho na kijamii.

Shirika la Wamisionari wa Damu Azizi ya Yesu limesajiliwa na Serikali ya Tanzania kama (The Society of the Precius Blood) ambapo linajishughulisha na kazi za kitume kwa Mapadre na Mabruda kwa lengo la kueneza upendo wa Kristo aliouonesha alipomwaga Damu yake msalabani kwa ajili ya ukombozi wa mwanadamu.
Share:

WAFANYAKAZI WA STANDARD CHARTERED WAADHIMISHA MIAKA 20 YA KUJITOLEA KWA JAMII KWA KUSAFISHA FUKWE






Standard Chartered Tanzania kwa kushirikiana na Nipe Fagio imeadhimisha miaka 20 ya programu ya kujitolea kwa jamii ya Standard Chartered duniani kwa kufanya zoezi la kila mwaka la usafi wa fukwe katika Ufukwe wa Silversand, Kunduchi.

Jumla ya washiriki 74, wakiwemo watoto 20, walishiriki katika zoezi hilo lililolenga kuchangia uhifadhi wa mazingira na kuhamasisha ushiriki wa wafanyakazi katika shughuli za maendeleo ya jamii.

Akizungumza kuhusu shughuli hiyo, Afisa Mtendaji Mkuu na Mkuu wa Kitengo cha Coverage wa Standard Chartered Bank Tanzania, Geofrey Mchangila, alisema:

"Zoezi la mwaka huu lina umuhimu wa pekee kwetu kwani linafanyika wakati Standard Chartered inaadhimisha miaka 20 ya kujitolea kwa jamii duniani kote. Tunaamini kuwa mabadiliko ya kweli huanza pale watu wanapounganisha nguvu zao.


Kupitia ushirikiano wetu na wafanyakazi, familia zao pamoja na Nipe Fagio, tunaendelea kuchangia kulinda ukanda wa pwani wa Tanzania na kujenga jamii zenye afya bora na mazingira endelevu kwa vizazi vijavyo."

Katika zoezi hilo, washiriki walisafisha eneo lenye ukubwa wa takribani mita za mraba 4,000 za ufukwe na kukusanya kilo 506 za taka zilizohifadhiwa katika mifuko 55.


Uchambuzi wa taka zilizokusanywa ulionyesha kuwa plastiki, hususan povu la polystyrene na chupa za plastiki za vinywaji, ndizo zilikuwa taka zilizopatikana kwa wingi, hali inayodhihirisha umuhimu wa kuendelea kuchukua hatua za kudhibiti uchafuzi wa mazingira ya bahari.

Kwa kipindi cha miaka mitatu iliyopita, kupitia ushirikiano wake na Nipe Fagio, Standard Chartered Tanzania imefanikisha jumla ya kampeni tano za usafi wa fukwe, ikihusisha washiriki 594, kusafisha zaidi ya mita za mraba 32,000 za ukanda wa pwani na kukusanya karibu tani tano za taka.

Mpango huu ni sehemu ya mkakati mpana wa Standard Chartered wa kuendeleza uhimilivu wa mazingira na maendeleo endelevu, huku ukiunga mkono Malengo ya Maendeleo Endelevu ya Umoja wa Mataifa (SDGs), hususan Lengo la 13 la Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Lengo la 14 la Kuhifadhi Maisha ya Chini ya Maji na Lengo la 17 la Kuimarisha Ushirikiano kwa Ajili ya Kufanikisha Malengo.

Standard Chartered inapoendelea kuadhimisha miaka 20 ya programu yake ya kujitolea kwa jamii, inaendelea kuwahamasisha wafanyakazi wake kutumia muda, ujuzi na utaalamu wao kuleta mabadiliko chanya na endelevu katika jamii na mazingira.








Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger