Friday, 3 April 2026

BAGAMOYO YAVUTA WAWEKEZAJI, MAOMBI 48 YAPOKELEWA



Mkurugenzi wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA), Gilead Teri, akizungumza leo Aprili 2, 2026 jijini Dar es Salaam

***

DAR ES SALAAM:

Kongani ya Bagamoyo imeendelea kuwa kitovu cha uwekezaji nchini baada ya kupokea maombi 48 kati ya maombi 86 yaliyowasilishwa TISEZA hadi kufikia Aprili Mosi mwaka huu.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa TISEZA, Gilead Teri, amesema mwitikio huo unaonyesha imani kubwa ya wawekezaji katika eneo hilo.

Amesema mbali na Bagamoyo, kongani ya Kwale imepokea miradi 20, huku Nala na Buzwagi zikibaki na miradi miwili kila moja.

Kwa mujibu wa Teri, mafanikio hayo yanachangiwa na uwepo wa miundombinu bora pamoja na sera rafiki za uwekezaji zinazotekelezwa na Serikali.




Amebainisha kuwa mradi wa Bagamoyo Eco Maritime City umeendelea kuvutia wawekezaji wengi zaidi wanaotaka kuwekeza katika sekta mbalimbali za uzalishaji.




Katika hatua nyingine, TISEZA imesaini mikataba na kampuni tisa zitakazowekeza zaidi ya Shilingi bilioni 177 katika miradi ya viwanda na huduma.





Amesema uwekezaji huo unatarajiwa kuongeza ajira pamoja na kuchochea ukuaji wa uchumi wa viwanda nchini.

Aidha, Teri ametoa wito kwa wawekezaji wa ndani kutumia fursa zilizopo kwa kusajili miradi yao kupitia TISEZA ili kunufaika na vivutio vya Serikali.




Share:

DKT. GWAJIMA ATOA WITO KWA JAMII NA WAZAZI KUSHIRIKI MALEZI YA WATOTO KIKAMILIFU


Na Saidi Saidi WMJJWM - Dodoma

Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Mhe.Dkt. Dorothy Gwajima, ametoa wito kwa jamii na wazazi kushiriki kikamilifu katika malezi na ulinzi wa watoto, ili kuzuia ongezeko la watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani.

Akizungumza na waandishi wa habari Aprili 01, 2026 jijini Dodoma kuelekea Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Mtoto anayeishi na kufanya kazi mtaani, yatakayofanyika Aprili 12, 2026 Jijini Dar Es Salaam yakiwa na Kaulimbiu isemayo “Malezi na Ulinzi wa Mtoto, Wajibu wetu Sote”.

Amesema ushiriki wa pamoja ni muhimu ili kuhakikisha watoto wanakua katika mazingira salama na yenye maadili mema huku akisisitiza jukumu la malezi si la wazazi pekee, bali ni la jamii nzima.

Aidha, Waziri Gwajima ameeleza kuwa changamoto kama umasikini, migogoro ya kifamilia, na ukatili dhidi ya watoto zimekuwa zikichangia watoto wengi kukimbilia mitaani.

Ameibainisha pia mafanikio ya juhudi za Serikali katika kuwaokoa watoto wa mitaani kuwa zaidi ya watoto 5,000 wameunganishwa na familia zao tangu kuanza kwa kampeni ya kuwaokoa watoto wa mitaani mwaka 2025.

Vilevile, Serikali imeanzisha mifumo mbalimbali, ikiwemo madawati ya ustawi wa jamii katika vituo vya usafiri na makao ya watoto, ili kuhakikisha watoto waliookolewa wanapata huduma muhimu kama elimu, afya, na malezi bora.

Waziri Gwajima ametoa wito kwa Watanzania kushirikiana na Serikali kwa kutoa taarifa za ukatili dhidi ya watoto na kuhakikisha wanapata malezi bora. Amesisitiza kuwa watoto wa mitaani wanapaswa kulindwa na kupewa fursa sawa za maendeleo, akihitimisha kwa kusema kuwa ni jukumu la kila mmoja kuhakikisha hakuna mtoto anayelazimika kuishi au kufanya kazi mitaani.

Waziri Gwajima ametumia nafasi hiyo pia kuwashukuru wadau wote wanaoshirikiana na Serikali katika kuhakikisha malezi ya watoto yanaimarishwa hususani shirika SoS Village na Railway Children.

Akizungumza kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Dodoma, mkuu wa wilaya ya Dodoma Jabir Shekimweri, amesisitiza umuhimu wa ushirikiano wa wadau wote katika kukabiliana na changamoto ya watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani, akieleza hatua mbalimbali zilizofikiwa na mkoa wa Dodoma.

Shekimweri amesema mwaka 2024 hadi 2026 Serikali ya mkoa imewaunganisha watoto 293 na familia zao.

Share:

Thursday, 2 April 2026

Video Mpya : JINASA MADEBE - MAJIVUNO

 

Share:

SERIKALI YAPANUA WIGO WA MAFUNZO NA FURSA ZA AJIRA KUINUA USHINDANI WA NGUVUKAZI YA WATANZANIA KATIKA SOKO LA KIMATAIFA


Katika jitihada za kukabiliana na mabadiliko ya kasi ya kiuchumi na kiteknolojia duniani, Serikali imeweka mkazo wa kipekee katika kuimarisha ujuzi wa nguvukazi ya ndani na kupanua wigo wa fursa za ajira ili kuwajengea Watanzania uwezo wa kushindana vyema katika soko la ndani na nje ya nchi. 

Akisoma Mapitio na Mwelekeo wa Kazi za Serikali pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha kwa mwaka 2026/2027 jijini Dodoma, Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba amebainisha kuwa juhudi hizi ni sehemu ya utekelezaji wa mikakati ya vitendo inayolenga kuzalisha ajira zenye tija na kuinua viwango vya utaalamu kwa wananchi wote. 

Serikali imekuwa ikiratibu kwa karibu utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo ili kubaini na kuzalisha nafasi mpya za kazi, huku ikijenga mazingira rafiki kwa wawekezaji na kuimarisha ushirikiano na sekta binafsi, hatua inayolenga kuhakikisha kunakuwepo na ajira zenye staha na endelevu kwa vijana.

Katika kuelekea kilele cha mafanikio ya kuimarisha ujuzi, Serikali imefanikisha mafunzo ya uanagenzi kwa vijana 5,746 kupitia vyuo na taasisi 46 katika kipindi cha mwaka 2025/2026, sambamba na kutoa mafunzo maalum kwa wakulima na wasindikaji wadogo 1,065 ili kuongeza thamani ya mazao na kupunguza upotevu wa malighafi. 

Taarifa ya Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba inaonesha kuwa hadi kufikia Februari 2026, jumla ya ajira 625,273 zilikuwa zimezalishwa nchini, huku  kukiwa na mnyororo wa thamani ambapo uwepo wa wataalamu wa kigeni kupitia vibali 12,549 umesaidia kuzalisha ajira nyingine 242,656 kwa wazawa, hali inayothibitisha kuimarika kwa ushirikishwaji wa Watanzania katika shughuli kubwa za uzalishaji na uhamishaji wa teknolojia.

Vilevile, milango ya ajira nje ya nchi imeendelea kufunguka ambapo Watanzania 6,367 wamefanikiwa kupata nafasi za kazi katika mataifa mbalimbali ikiwemo Saudi Arabia, Qatar, Oman na Umoja wa Falme za Kiarabu, huku Serikali ikiendelea kupanua diplomasia ya ajira katika nchi nyingine zaidi. 

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii, Mhe. Hawa Mchafu, amesisitiza kuwa programu zinazoratibiwa na Ofisi ya Waziri Mkuu zinalenga kuwajengea vijana misingi imara ya ubunifu itakayowawezesha kujiajiri na kushindana kikamilifu. 

Kamati hiyo imejionea mafanikio ya mafunzo katika fani za uchomeleaji, umeme, mabomba, ushonaji na ufundi wa magari katika vyuo mbalimbali ikiwemo Chuo cha Maendeleo ya Wananchi Kigamboni, huku ikishauri kukamilishwa kwa utoaji wa fedha zilizosalia za uanagenzi ili kuhakikisha malengo ya kuwafikia vijana wengi zaidi yanafikiwa kwa wakati.


Share:

POLISI YAJIDHATITI KUHAKIKISHA USALAMA NA UTULIVU WAKATI WOTE WA SIKUKUU ZA PASAKA


Na mwandishi wetu

Jeshi la Polisi nchini Tanzania limesema limejipanga vyema kuanzia ngazi ya Kata na kwa kushirikiana na Kamati za ulinzi na usalama kuhakikisha kuwa usalama na utulivu unadumishwa wakati wote wa kipindi cha kuhitimisha mfungo wa Kwaresma na sikukuu za pasaka kwa waumini wa dini ya Kikristo wakati wote wa ibada Kanisani na majumbani mwao.

Taarifa ya Msemaji wa Jeshi la Polisi Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) David Misime kuhusu kuimarishwa kwa hali ya usalama kuelekea sikukuu za Pasaka iliyotolewa leo Alhamisi Machi 02, 2026 kwa Vyombo vya habari, imetoa wito pia kwa kila mmoja wakati wa ibada na sherehe za pasaka kuhakikisha makazi yanakuwa chini ya uangalizi badala ya kuacha makazi yao bila ya usimamizi.

"Aidha kama tutaruhusu watoto wetu kutoka kwaajili ya kwenda kusherehekea sikukuu hizi katika maeneo stahiki na salama, kila mmoja ahakikishe wanakuwa na uangalizi wa mtu mzima na mwenye akili timamu. Pia tunatoa wito kwa kila mmoja kuzingatia sheria, kanuni na ishara za usalama barabarani ili kuepuka ajali zinazotokana au zinazosababishwa na uzembe pamoja na kuendesha chombo cha moto katika hali ya ulevi."amesema Kamanda Misime.

Polisi pia katika taarifa yake imesisitiza umuhimu wa kila mmoja kuendelea kuchukua tahadhari katika kipindi hiki ambacho mvua zinaendelea kunyesha, wakisisitiza kuacha na kujiepusha na tabia za kupita sehemu ambazo maji mengi yametuama au yanayotiririka suala ambalo si salama kwa binadamu.

"Tunarudia tena kutoa tahadhari hii kwasababu tumeshuhudia baadhi ya watanzania wenzetu wanaopoteza maisha walipojaribu kuvuka sehemu hatarishi ambazo zimejaa maji, tumeshuhudia pia watoto waliopoteza maisha kutokana na kusombwa na maji na wengine kutumbukia kwenye mashimo yaliyochimbwa na kuachwa wazi,

Wazazi/walezi tuwalinde watoto wetu dhidi ya madhara hayo na kwa wale waliochimba mashimo na kuyaacha wazi wayafunike au kuyafukia." Amekaririwa Kamanda Misime katika taarifa yake.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI APRILI 2,2026



Magazeti

















Share:

Wednesday, 1 April 2026

Wimbo Mpya : MALIGANYA MADIRISHA - YAKALE


Share:

PROF. SHEMDOE AWASILISHA RANDAMA YA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI OFISI YA WAZIRI MKUU 2026/2027

 Machi 31, 2026, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI), Mhe. Prof. Riziki Shemdoe, amewasilisha randama ya makadirio ya mapato na matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2026/27.

Mhe. Prof. Shemdoe amewasilisha randama hiyo yenye mafungu 37 kwa niaba ya Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba ambaye anatarajia kusoma rasmi makadirio hayo kesho tarehe 01 Aprili, 2026 katika kikao cha pili cha mkutano wa tatu wa Bunge la Bajeti, ambapo Wabunge watapata fursa ya kujadili mipango na matumizi ya fedha ya ofisi hiyo.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO APRILI 1,2026

 

Magazeti

                                

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger