Sunday, 14 June 2026

WANANCHI MSIKUBALI MANENO YA USHAWISHI; WAKOMALIENI WACHOCHEZI - KIHONGOSI



Wananchi na vijana kote nchini wanahimizwa kuwa macho na kutokubali kabisa kuyasikiliza maneno ya ushawishi yanayohubiri chuki na uharibifu.Badala yake, jamii inatakiwa kushikamana na "kuwakomalia" kikamilifu watu wote wanaojaribu kupandikiza mbegu za machafuko, iwe ni mitaani au kwenye mitandao ya kijamii.

Katibu wa NEC, Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, Kenani Laban Kihongosi, alisisitiza kuwa kulinda amani ni wajibu wa kila mmoja:

"Ni wajibu wa kila mmoja wetu kuhakikisha Tanzania inaendelea kuwa salama, yenye amani na utulivu kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kijacho."

Aidha wananchi wametakiwa kuwa na Kumbukumbu za matukio ya nyuma, hususan Oktoba 29, ambayo yanasalia kuwa funzo kubwa na la kudumu kwa Watanzania wote.

Historia inatufundisha kuwa ghasia, vurugu, na uharibifu wa mali wakati wa harakati za kisiasa haujawahi kuleta tija, bali huacha makovu yasiyofutika, vifo, ulemavu, na kuporomoka kwa uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.

Wananchi wanatakiwa kukumbuka machungu ya nyuma na kukataa katakata kutumika kama kuni za kuwasha moto utakaoteketeza nchi yao wenyewe.

Kauli hioyo imetolewa huku upande wa upinzani kupitia kwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Bara, John Heche, ukilalamikia misukosuko ya kisheria na kiutawala


Wadau wa amani wanasisitiza kuwa madai yoyote ya kisiasa lazima yafuate njia za kisheria na amani, bila kuingiza nchi kwenye dimbwi la damu na moto.


Siri nzito imevuja kuhusu uwepo wa mikakati ya kisiri inayoratibiwa na baadhi ya watu wenye nia ovu, inayolenga kutumia mwavuli wa maandamano na mikutano kufanya uharibifu mkubwa wa miundombinu ya umma, ikiwemo kuchoma moto shule na vyuo.


Taarifa za kiintelijensia na vyanzo vya kuaminika vinabainisha kuwa, baadhi ya vikundi na akaunti za mitandao ya kijamii zinazoendeshwa na watu wenye msimamo mkali—akiwemo mchochezi anayejulikana zimekuwa zikisuka mipango hiyo hatari kwa lengo la kuleta taharuki, kuvuruga usalama, na kuifanya nchi isitawalike.


Wachambuzi wa masuala ya usalama na maendeleo wameonya vikali dhidi ya fikra hizi za kiharifu. Swali kubwa linaloulizwa na kila Mtanzania mzalendo ni: "Ukishachoma nchi moto, ukaharibu shule na vyuo vinavyolelea watoto wetu, unatarajia kupata nini?"


Kuchoma shule na vyuo siyo kupigania demokrasia, bali ni kuharibu mustakabali wa elimu ya vizazi vya sasa na vijavyo. Kitendo cha kuharibu miundombinu ambayo imejengwa kwa kodi za Watanzania maskini ni kujirudisha nyuma kimaendeleo na kuongeza umaskini. Maisha ya wananchi yakishaharibika na amani ikitoweka, hakuna mshindi—sote tutakuwa waathirika.


"Maendeleo ya haraka yaliyopatikana Tanzania Bara na Zanzibar yametokana na kuwepo kwa amani na utulivu. Vijana wa Kitanzania msikubali kuiweka nchi yenu rehani," alikaririwa Katibu wa Kamati Maalum ya NEC Zanzibar (Itikadi na Uenezi), Khamisi Mbeto Khamis, akionya dhidi ya maandamano haramu.


Amewataka watanzania kulinda shule yako, linda chuo chako, na kemea kila sauti inayohamasisha uharibifu. Tanzania ni yetu sote, na kuichoma moto ni kujiteketeza wenyewe.
Share:

FILAMU YA KIFURUSHI YAZINDULIWA KUPAMBANA NA USAFIRISHAJI WA DAWA ZA KULEVYA


Dar es Salaam

Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) imezindua rasmi filamu ya Kifurushi, ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kuelimisha wananchi kuhusu hatari za kubeba mizigo au vifurushi wasivyovifahamu na kushiriki kwa namna yoyote katika usafirishaji wa dawa za kulevya.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo uliofanyika katika Kituo Kikuu cha Mabasi cha Magufuli, Kamishna Jenerali wa DCEA, Aretas Lyimo, alisema tatizo la dawa za kulevya linaendelea kuwa tishio kwa maendeleo ya taifa kutokana na athari zake kwa afya, uchumi na ustawi wa jamii.

Alisema uchunguzi wa mamlaka hiyo umebaini kuwa baadhi ya wahalifu wamekuwa wakitumia mbinu mbalimbali za kuficha dawa za kulevya katika mizigo na vifurushi vinavyoonekana kuwa vya kawaida, hali inayowafanya baadhi ya wananchi kujikuta wakikabiliwa na mkono wa sheria bila kufahamu.

"Filamu hii imeandaliwa kuonesha uhalisia wa namna mtu anavyoweza kuingia kwenye mtego wa wahalifu kwa kubeba kifurushi au mzigo usiofahamika. Tunataka wananchi watambue kuwa mzigo unaoonekana wa kawaida unaweza kubeba dawa za kulevya na kubadilisha maisha yao kwa namna hasi," alisema Lyimo.

Aliongeza kuwa DCEA itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuimarisha mapambano dhidi ya dawa za kulevya kupitia operesheni, uchunguzi, tiba kwa waathirika na kampeni za elimu kwa umma.

Kwa upande wake, Mchungaji Richard Hananja alisisitiza umuhimu wa jamii kushiriki katika kuwasaidia waraibu wa dawa za kulevya kurejea katika maisha ya kawaida badala ya kuwanyanyapaa.

"Waraibu wanahitaji kusaidiwa na kupewa nafasi ya kubadilika. Viongozi wa dini, wazazi na jamii kwa ujumla wanapaswa kushiriki katika kuwaongoza na kuwatia matumaini," alisema.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Udhibiti Usafiri wa Barabara wa LATRA, Halima Lutabi, alisema sekta ya usafiri ni miongoni mwa maeneo ambayo wahalifu wamekuwa wakiyatumia kusafirisha dawa za kulevya, jambo linalohatarisha usalama wa abiria na taswira ya sekta hiyo.

Alisema LATRA itaendelea kushirikiana na vyombo vya dola na wadau wa usafirishaji kuhakikisha sheria, kanuni na taratibu zinazodhibiti matumizi ya vyombo vya usafiri katika shughuli haramu zinasimamiwa kikamilifu.

Kwa upande wa sekta binafsi, Naibu Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania (TABOA), Abdallah Kiongozi, alisema chama hicho kiko tayari kushirikiana na Serikali katika kuzuia usafirishaji wa dawa za kulevya kupitia vyombo vya usafiri wa umma.

"Tunapokea filamu hii kwa mikono miwili na tuko tayari kuisambaza kwa wanachama wetu ili kuongeza uelewa kuhusu hatari za dawa za kulevya," alisema.

Katibu Mtendaji wa Bodi ya Filamu Tanzania, Dkt. Gervas Kasiga, alisema filamu ni nyenzo muhimu ya kuelimisha jamii na kuhamasisha mabadiliko ya kitabia, akieleza kuwa kazi hiyo itasaidia wananchi kutambua hatari za kubeba mizigo au vifurushi wasivyovifahamu.

Filamu ya Kifurushi inatarajiwa kuoneshwa katika mabasi yanayofanya safari za mikoani kote nchini kupitia ushirikiano kati ya DCEA, LATRA na Bodi ya Filamu Tanzania.

Ujumbe mkuu wa filamu hiyo ni kuwataka wananchi kutokubali kubeba mizigo, vifurushi au bidhaa za watu wengine bila kufahamu kilichomo, kwani kufanya hivyo kunaweza kuwahusisha na makosa ya jinai yenye madhara makubwa kwa maisha yao, familia na jamii kwa ujumla.

Kaulimbiu ya kampeni hiyo ni "Usafiri Salama Bila Dawa za Kulevya."
h="2560" src="https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgutC7u41v6T0K_e1paCUYtjnWplohfAX2frzzitmYZm6RPOLVf3MwuB52RY2ewq0-CF0svFitzHj8nBGAb8iKETFLoKcJn9iT2fQv_1WQAX8UB-8bQ5dpPSQzN-yXowOZSpVJVLWT6lioFThKiPV9Ht7NPK9U-3KR7lqcraBROaAe0t7v8rMTPkzwl9sM/s600/4330696.jpg"/>
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger