Saturday, 25 April 2026

WAFANYABIASHARA SOKO LA NAMANGA KAHAMA WALALAMIKIA TOZO NA UKOSEFU WA UWAZI, DC NKINDA AAGIZA TAKUKURU KUCHUNGUZA

 


Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Frank Nkinda akizungumza na wafanyabiashara wasoko la Namanga lililopo Manispaa ya kahama mara baada ya kusikiliza kezo zao


Na Neema Nkumbi, Kahama


Wafanyabiashara wa Soko la Namanga lililopo Manispaa ya Kahama mkoani Shinyanga wameeleza kutoridhishwa na mfumo wa ukusanyaji wa ushuru wakidai kuwepo kwa tozo wanazoziita zisizo rasmi pamoja na ukosefu wa uwazi katika matumizi ya mapato yanayokusanywa sokoni hapo.


Wakizungumza katika mkutano wa kusikiliza na kutatua kero ulioandaliwa na ofisi ya Mkuu wa Wilaya katika soko hilo, wafanyabiashara wamesema wamekuwa wakikumbwa na mzigo mkubwa wa ushuru unaowadhoofisha kiuchumi, huku wakidai kuwa hakuna mrejesho wa wazi kuhusu matumizi ya fedha hizo.
Mfanyabiashara samaki katika soko hilo Irene Thomas amesema kumekuwepo kwa vikundi vinavyohusika na ukusanyaji wa mapato ambavyo havitoi taarifa za kutosha kwa wafanyabiashara, hali inayozua sintofahamu sokoni hapo.


"sisi tunalipa ushuru zaidi ya maduka makubwa wanaolipa TRA, mimi mtaji wangu laki nne mpaka tano lakini kwa mwezi ushuru nalipa laki tatu na elfu tisini nikiwa na kijana na bado sijamlipa kijana, mimi nabakiwa na nini?", amesema Irene.


ameongeza kuwa "halafu hiyo hela ni bora ningejua inaenda serikalini, inaenda kufanya maendeleo ambapo itatengeneza barabara nami nitapita, kuliko kwenda kwenye kikundi ambacho kinakula hela ya mwananchi, kikundi hiki sidhani kama kinalipa TRA maana kinatoa risiti za makaratasi na kikundi kinaingiza zaidi ya milioni nne kwa mwezi na halmashauri inalipwa laki tano na arobaini tu".
Mfanyabiashara mwingine wa samaki amesema " sisi kwenye kikundi hicho hatumo na hatufaidiki kwa chochote mapato yao wanafaidika wenyewe ikifika mwisho wa mwaka wanapeana bahasha wenyewe sasa mimi ninachotakiwa nikilipe ni mapato ya serikali yaliyonyooka na si kulipa vikundi".


Hata hivyo, Mwenyekiti wa Soko la Namanga, Juma Jumeju, amekanusha tuhuma hizo akisema mfumo wa sasa ulianzishwa ili kurahisisha ukusanyaji wa mapato baada ya soko kukumbwa na changamoto za utulivu katika kipindi cha nyuma.


Jumeju amesema uongozi uliingia ubia na baadhi ya wafanyabiashara kuunda kikundi kilichosajiliwa kisheria kwa lengo la kuboresha mfumo wa ukusanyaji wa mapato, akibainisha kuwa kuna mkanganyiko wa uelewa kuhusu majukumu ya kikundi hicho.


“Kwa kipindi cha nyuma soko halikuwa na utulivu, ndipo tukaunda kikundi kilichosajiliwa kisheria ili kurahisisha ukusanyaji wa mapato,” amesema.


Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Frank Nkinda, ameeleza kuwa ni muhimu kupata uhalisia wa suala hilo kabla ya kuchukua hatua, akisema kuna haja ya kusikiliza pande zote ili kuhakikisha haki inatendeka.


Aidha, ameiagiza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) kufuatilia kwa kina malalamiko hayo ili kubaini iwapo kuna mianya ya udanganyifu au ukiukwaji wa taratibu katika ukusanyaji wa mapato sokoni hapo.


“Ninaigiza TAKUKURU kufuatilia suala hili kwa haraka ili tupate uhalisia na tufanye maamuzi sahihi ya kumaliza mgogoro huu,” amesema Nkinda.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRILI 25,2026


Magazeti
Share:

Friday, 24 April 2026

MKUTANO WA KIKANDA WAJADILI USALAMA NA BIASHARA YA SILAHA HARAMU



Na Mwandishi Wetu,DAR ES SALAAM

Makamu Mwenyekiti wa RECSA na ‎Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Paschal Katambi Patrobass (Mb), ameshiriki Mkutano kwa njia ya Mtandao wa Kamati Ndogo ya Mawaziri ya Kikanda, unaoshughulikia Udhibiti wa Silaha ndogo na nyepesi katika Ukanda wa Maziwa Makuu na Pembe ya Afrika (RESCA).

‎Kikao hicho, kimewakutanisha Mawaziri wa Usalama kutoka nchi wanachama, kikiwa na lengo la kujadili Hali ya Usalama katika ukanda huo pamoja na changamoto zinazoendelea kujitokeza, hususani Usambazaji na Matumizi Haramu ya Silaha ndogo na nyepesi.

Ametoa kauli hiyo baada ya Kikao cha Saba cha nchi wanachama wa Kituo cha Kikanda Kinachoshughulika na Udhibiti wa Silaha katika Nchi za Maziwa Makuu na Pembe ya Afrika (RECSA),ngazi ya mawaziri kinachojumuisha nchi ya Tanzania,Burundi,Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC), Rwanda,Uganda,Kenya,Somalia,Sudan,Sudan Kusini, Ethiopia, Eritrea, Djibouti, Jamhuri ya Kongo na Jamhuri ya Kati, kilichofanyika kwa njia ya mtandao ambapo masuala mbalimbali yalijadiliwa ikiwemo udhibiti wa silaha na kupambana na biashara haramu ya silaha.

Amesema sambamba na hilo, Serikali kupitia Wizara ya mambo ya ndani ya Nchi imejipanga kimkakati kuimarisha ulinzi na usalama wa Mifumo ya Uthibiti katika Uingizaji Silaha,Kuangalia Dhana nzima ya Umiliki na Wajibu wa Mmiliki, Tathmini ya Matumizi sahihi ya Silaha,Ukaguliwaji wa Silaha,Lengo na Dhamira ya Muombaji na Mmiliki wa Silaha, Tabia na mienendo hatarishi ya mmiliki wa Silaha na kuimarisha mifumo ya kiteknolojia na Kidigitali katika kudhibiti Silaha.

“Nchi yetu ni nchi ya Muungano Kikatiba, yenye misingi ya kisheria, sera madhubuti, zinazochochea Amani, Mshikamano na Utulivu,Tanzania ni Nchi mwanachama wa RECSA, tumeendelea kuwahakikishia wanachama wenzetu kuwa nguzo ya amani na utulivu ndani na nje ya mipaka yetu.

 Tunashirikiana pamoja katika doria ili kudhibiti na kupunguza silaha ndogondogo na nyepesi zinazozunguka kinyume na sheria. Katika dhana nzima ya udhibiti wa silaha, serikali tumedhamiria kuimarisha mifumo ya uingizaji wa silaha,utambuzi wa mifumo ya uingizaji,umiliki na wajibu wa mmiliki,ukaguliwaji wa silaha,pamoja na tathmini ya matumizi sahihi ya silaha kuondoa matishio ya amani ndani na nje ya kanda ya pembe ya Afrika.” Amesema Mheshimiwa Katambi

Mhe. Katambi pia amewataka wamiliki wa silaha hapa nchini, kuzingatia kikamilifu masharti ya umiliki wa silaha zao pamoja na kulipia leseni za silaha wanazomiliki ikiwa ni takwa la kisheria ambapo kwa mujibu wa kifungu cha 20 cha Kanuni za Udhibiti wa Silaha na Risasi za mwaka 2016 linalomtaka kila mmiliki wa silaha nchini kulipia Leseni za Bastola, Shotgun na Rifle na ada hiyo ya Leseni hulipwa kuanzia tarehe 1 Julai hadi 30 Septemba kila mwaka.

Ametoa agizo kwa wale wanaomiliki au kukaa na Silaha kinyume cha Sheria iwe kwa kupewa, kuokota, kurithishwa, kupora au kwa namna yoyote isivyo kisheria kuzisalimisha haraka katika Kituo cha Polisi au kutoa taarifa za siri kufichua umiliki wa kinyemera kwa ajili ya Usalama wa Raia na Mali zao pia Amani ya Nchi yetu.


Share:

Video Mpya : SHINJE ORIGINAL - YA MOTO BALAA

 

Share:

TAMCU YAIMARISHA UCHUMI WA WAKULIMA TUNDURU KWA UNUNUZI WA MALORI MAPYA MATANO

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Mhe.  Denis Masanja watatu kutoka kulia akiwa anakata utepe wakati wa kukabidhi magari hayo mapya matano ya chama cha Ushirika Tunduru (TAMCU) limited Mwenyekiti wa Chama kikuu cha ushirika wilaya ya Tunduru (Tamcu) Musa Manjaule kushoto na meneja masoko wa Benki ya Crdb kanda ya kusini  Emanuel Bigailo wakisaini hati ya makabidhiano ya malori matano mapya yaliyonunuliwa na Tamcu baada ya kupata mkopo kutoka Crdb,nayeshuhudia katikati Mkuu wa Wilaya ya Tunduru Deni Masanja.

Na Regina Ndumbaro Tunduru-Ruvuma 

Chama Kikuu cha Ushirika Wilaya ya Tunduru (TAMCU) kimechukua hatua kubwa ya kuongeza ufanisi katika sekta ya kilimo kwa kununua malori matano mapya ya kubebea mazao, hatua inayolenga kurahisisha usafirishaji na kuongeza mapato ya chama pamoja na wanachama wake. 

Uamuzi huo umepokelewa kwa furaha na wakulima wa wilaya hiyo ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakikumbwa na changamoto ya ucheleweshaji wa mazao kufika sokoni kutokana na uhaba wa vyombo vya usafiri.

Akizungumza kwa niaba ya wakulima, Rashid Chibwana amesema kuwa malori hayo yatasaidia kuwafikia wakulima mashambani na kusafirisha mazao yao kwa wakati hadi maghala na hatimaye kwenye minada. 

Amebainisha kuwa hapo awali walitegemea chanzo kimoja cha mapato, lakini uwekezaji huo mpya utaongeza mapato ya chama huku ukipunguza gharama na usumbufu wa usafirishaji.

Mwenyekiti wa TAMCU, Mussa Manjaule, amesema ununuzi wa malori hayo umetokana na maombi ya wanachama waliotaka kuboreshwa kwa huduma za usafirishaji pamoja na kuongeza vyanzo vya mapato. 

Ameeleza kuwa awali walikuwa wanapata changamoto hata katika kusafirisha pembejeo kama viuatilifu kutoka mikoa jirani, lakini sasa hali hiyo itaboreshwa kwa kiasi kikubwa.

Kwa upande wake, Meneja wa Benki ya CRDB Tawi la Tunduru, Emanuel Mwasuka, amesema benki hiyo imechangia sehemu kubwa ya fedha zilizotumika kununua malori hayo yenye thamani ya shilingi bilioni 1.5. 

Ameahidi kuendelea kushirikiana na vyama vya ushirika kwa kutoa mikopo, huku akisisitiza umuhimu wa kuyatunza malori hayo ili yadumu na kuleta tija inayokusudiwa.

Mkuu wa Wilaya ya Tunduru, Denis Masanja, ameipongeza TAMCU kwa hatua hiyo akieleza kuwa ni mfano bora wa maendeleo katika sekta ya ushirika. 

Amesema uwekezaji huo utachochea biashara ya mazao kama korosho, ufuta na mbaazi, kupunguza gharama za usafirishaji na kuongeza kipato kwa wakulima, huku akitoa wito kwa wanachama kushirikiana na viongozi wao ili kufanikisha malengo ya chama.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA APRILI 24,2026


Magazeti
 
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger