
Sunday, 26 April 2026
WATANZANIA WATAKIWA KUENZI MISINGI YA MUUNGANO

TAIFA GESI YATOA ELIMU YA MATUMIZI SALAMA YA GESI NJOMBE

Na Mwandishi Wetu
Kampuni ya Taifa Gesi imeendelea kutoa elimu kwa wananchi kuhusu matumizi sahihi na salama ya gesi, sambamba na kuhamasisha usalama mahali pa kazi katika maadhimisho ya Wiki ya Usalama na Afya Mahali pa Kazi Duniani.
Akizungumza katika viwanja vya Shule ya Msingi Mji Mwema, Njombe, Mtaalamu wa Masuala ya Afya, Mazingira, Usalama na Ulinzi Mahali pa Kazi kutoka Taifa Gesi, Aurelius Marcus Mdemu, alisema kampuni hiyo imeshiriki maadhimisho hayo yanayoanza Aprili 24 hadi 29, 2026 kwa lengo la kutoa elimu kwa wateja na jamii kwa ujumla.

Alisema kupitia banda lao, wanaonesha vifaa mbalimbali vinavyotumika kazini ili kuimarisha usalama wa wafanyakazi, pamoja na kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya gesi na faida zake. Aidha, alieleza kuwa wanajitahidi kuondoa hofu na dhana potofu zilizopo miongoni mwa watumiaji wa gesi.
“Tunawaonesha wananchi namna Taifa Gesi inavyoweka kipaumbele kwenye usalama wa wafanyakazi, ikiwa ni pamoja na matumizi ya vifaa kinga vinavyotakiwa kutumika muda wote wakiwa kazini,” alisema Mdemu.


Kwa upande wake, Afisa Masoko wa Chapa wa Taifa Gesi, Santina Ngaponda, alisema maonyesho hayo yameandaliwa na OSHA, yalianza Aprili 24 na yanatarajiwa kufikia kilele chake Aprili 29 mwaka huu.
Ngaponda aliwahimiza wakazi wa Njombe na maeneo ya jirani kutembelea banda la Taifa Gesi ili kupata elimu kutoka kwa wataalamu wa usalama, kujifunza matumizi sahihi ya gesi, pamoja na kuona vifaa vya usalama vinavyotumika kazini na umuhimu wake.

Aidha, aliongeza kuwa kampuni hiyo inatoa punguzo maalum la bei ya gesi na vifaa vyake, pamoja na zawadi mbalimbali kwa wateja watakaotembelea banda hilo.

Naye Meneja Mauzo wa Kanda ya Nyasa wa Taifa Gesi, Arnold Salewa, alisema wanaendelea kutumia maonyesho hayo kutoa elimu kuhusu matumizi sahihi ya nishati safi pamoja na kuuza bidhaa zao kwa bei ya promosheni.
Alisema kanda hiyo inajumuisha mikoa ya Njombe, Iringa na Ruvuma, na kwamba pia wanatoa fursa kwa wananchi wanaotaka kuwa mawakala wao, kwa kuwapatia elimu ya biashara na usimamizi salama wa mitungi ya gesi.

Salewa alisisitiza kuwa Taifa Gesi ipo mstari wa mbele kuhakikisha kaya, migahawa na taasisi mbalimbali zinaanza kutumia nishati safi ya kupikia kwa gharama nafuu, ili kupunguza athari za matumizi ya mkaa na kuni kwa mazingira na afya za Watanzania.
Aliongeza kuwa mwitikio wa wananchi umekuwa mkubwa, huku Taifa Gesi ikiendelea kuwa chaguo sahihi kwa watumiaji wengi nchini.
WANANCHI SHINYANGA WAPOKEA RIPOTI YA JAJI CHANDE KWA MATUMAINI YA MARIDHIANO
Wananchi hao wamesema wanaamini kuwa utekelezaji wa mapendekezo yaliyomo kwenye ripoti hiyo utasaidia kurejesha mshikamano wa kitaifa na kuzuia kujirudia kwa matukio ya uvunjifu wa amani siku zijazo.
Akizungumza kuhusu ripoti hiyo iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa Tume, Mohamed Chande Othman, mmoja wa wakazi wa Shinyanga Mjini, Chief Abdallah Sube, amesema ameipokea vizuri kwa kuwa inalenga kuponya majeraha yaliyosababishwa na matukio ya uvunjifu wa amani.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, sababu kuu zilizochangia ghasia hizo ni pamoja na mchanganyiko wa malalamiko ya kisiasa, changamoto za kiuchumi pamoja na utendaji usioridhisha wa baadhi ya watumishi wa umma.
Ripoti hiyo imekabidhiwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, katika hafla iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 23 Aprili 2026, ikiwa ni sehemu ya jitihada za Serikali kutafuta suluhu ya kudumu na kuimarisha amani nchini.
Saturday, 25 April 2026
WAFANYABIASHARA SOKO LA NAMANGA KAHAMA WALALAMIKIA TOZO NA UKOSEFU WA UWAZI, DC NKINDA AAGIZA TAKUKURU KUCHUNGUZA
Magazeti




















