Monday, 4 May 2026

POLISI WATOA ONYO KALI DHIDI YA MATUMIZI MABAYA YA MITANDAO YA KIJAMII



Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Wakati matumizi ya mitandao ya kijamii yakiendelea kukua kwa kasi na kuwa sehemu muhimu ya mawasiliano ya kijamii na kiuchumi, changamoto ya matumizi mabaya ya majukwaa hayo imeanza kuibua wasiwasi kwa jamii huku Jeshi la Polisi likionya na kuanza kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya wahusika.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi, Makao Makuu ya Polisi, Dodoma,pamoja na mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kudhibiti uhalifu kupitia ushirikiano na wananchi, bado kuna baadhi ya watu wanaotumia mitandao ya kijamii kufanya vitendo vinavyokiuka maadili na sheria, ikiwemo utapeli, matusi, udhalilishaji na uchochezi.

Jeshi hilo limeeleza kuwa hali ya usalama nchini inaendelea kuwa shwari, huku matukio machache ya kihalifu yakishughulikiwa kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa.

Akizungumzia hatua zinazochukuliwa, Msemaji huyo anebainisha kuwa wahusika wa makosa ya mtandaoni wanachukuliwa hatua kwa mujibu wa Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015, ambayo imeendelea kuwa nyenzo muhimu katika kudhibiti uhalifu wa kidijitali nchini.

Amefafanua kuwa Katika operesheni za hivi karibuni, Jeshi la Polisi limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa watatu katika mikoa ya Arusha, Iringa na Mbeya kwa tuhuma za kutumia vibaya mitandao ya kijamii, ikiwemo kutoa lugha za matusi dhidi ya watu mbalimbali wakiwemo wajumbe wa Tume ya Uchunguzi wa matukio ya vurugu za Oktoba 29, 2025.

Aidha, Jeshi hilo limeeleza kuwa msako dhidi ya watuhumiwa wengine unaendelea, hasa wale wanaohusika katika kusambaza maudhui ya kashfa, chuki na upotoshaji wa taarifa, hata kama si waanzilishi wa maudhui hayo.

Katika hatua nyingine,jeshi hilo limewataka wananchi kuendelea kushirikiana na vyombo vya dola kwa kutoa taarifa sahihi zitakazosaidia kudhibiti uhalifu huo, huku wakihimizwa kutumia mitandao ya kijamii kwa uwajibikaji na kuzingatia sheria za nchi.

Aidha jeshi la Polisi limesisitiza kuwa halitasita kuchukua hatua kali dhidi ya mtu yeyote atakayekiuka sheria, bila kujali nafasi au hadhi yake katika jamii.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU MEI 4,2026



Magazeti





















Share:

Sunday, 3 May 2026

ZOEZI LA UFUNGAJI KAMBI LIMEKIDHI VIGEZO KISHERIA - KATAMBI



Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mhe. Patrobas Katambi ametoa ufafanuzi juu ya zoezi nzima la Urejeshaji na Ufungaji wa Kambi ya Wakimbizi wa Burundi nchini ambao walikua wanahifadhiwa katika Kambi ya Nduta iliyoko mkoani Kigoma.

Waziri Katambi ametoa ufafanuzi huo wakati wa Mahojiano na Mwandishi wa Habari ambapo alielezea utaratibu wote ulivyofuatwa ikiwemo vikao kadhaa vya pande tatu ikiwemo Serikali ya Tanzania,Serikali ya Burundi na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR).

“Tumekaa vikao vya pamoja na makubaliano kulingana na sheria zinavyoelekeza,kunakua na uratibu wa hatua kwa hatua na kuna zile sababu zilizofanya wakimbie zisiwepo tena na moja ya sababu ni kutokuwepo kwa vita katika nchi husika lakini pia kusiwe na matishio ya kiusalama ambayo yanapelekea matishio ya vifo au mateso makali.” amesema Waziri Katambi.

“Sisi Serikali ya Tanzania tumehakikisha mazingira hatarishi katika nchi yao wanayorudi yako Salama,Rais wa Burundi Mheshimiwa Evariste Ndayishimiye pamoja na Balozi wa Burundi hapa nchini wamethibitisha kwamba nchi yao iko salama na tayari maeneo ya kufikia yameandaliwa na huduma zao muhimu ikiwemo afya,elimu,maji na ustawi wao kwenye nchi hiyo.” aliongeza Waziri Katambi

Ni takribani miaka 10 Serikali ya Tanzania imehifadhi Wakimbizi hao wa Burundi katika Kambi ya Nduta ambayo hadi kufungwa kwake rasmi tarehe 30 Aprili, 2026 ilikua na jumla ya Wakimbizi 165,394 ambapo katika Mkutano wa 26 wa Pande Tatu; Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Serikali ya Burundi na Shirika la Kuhudumia Wakimbizi Duniani (UNHCR) uliofanyika tarehe 28 Novemba, 2025 jijini Dar es Salaam uliazimia na pande zote tatu kutiliana saini makubaliano ya kuanza Urejeshaji wa Wakimbizi hao ambapo hatua iliyofuatia ni kufungwa kwa kambi hiyo.
Share:

MIGODI YA BARRICK YASHINDA TUZO 11 ZA OSHA 2026


Naibu Katibu Mkuu-Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi,Ajira na Mahusiano, Zuhura Yunus (kushoto) akimkabidhi tuzo ya ushindi wa kwanza katika kipengele cha usambazaji maji na udhibiti wa Maji taka na shughuli za urekebishaji, Afisa Rasilimali Mwandamizi wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Renatus Malawa wakati wa hafla ya tuzo za OSHA 2026 zilizofanyika mjini Njombe. Migodi ya Barrick nchini ilishinda tuzo 11.
Naibu Katibu Mkuu-Ofisi ya Waziri Mkuu - Kazi, Ajira na Mahusiano, Zuhura Yunus (kushoto) akimkabidhi tuzo ua ushindi ,Mrakibu Mwandamizi wa Usalama kutoka Mgodi wa Barrick North Mara, Meshack Issack wakati wa hafla ya tuzo za OSHA 2026 zilizofanyika mjini Njombe. Migodi ya Barrick nchini ilishinda tuzo 11.
Wafanyakazi wa Barrick Bulyanhulu wakisherekea ushindi wakati wa hafla hiyo iliyofanyika mjini Njombe.
Wafanyakazi wa Barrick Bulyanhulu wakisherekea ushindi wakati wa hafla hiyo iliyofanyika mjini Njombe.

***

Migodi ya Bulyanhulu na North Mara inayomilikiwa na kampuni ya Barrick nchini yenye ubia na Serikali kupitia kampuni ya Twiga imeendelea kudhihirisha kuwa ni mahiri katika kutekeleza kwa vitendo kanuni za Afya na Usalama Mahali pa Kazi ambapo imenyakua tuzo 11 katika hafla ya utoaji wa Tuzo za Afya na Usalama Mahali pa Kazi (OSHA) kwa mwaka 2026 iliyofanyika mjini Njombe.
Share:

RIPOTI YA JAJI CHANDE IMETOA MWANGA MPYA WA MATUMAINI KWA WATANZANIA- DKT. NDILITO



Ripoti ya Tume iliyoongozwa na Jaji Mohamed Chande Othman ya kuchunguza matukio ya uvunjifu wa amani wakati na baada ya uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, 2025 imeendelea kuzua mjadala mkubwa nchini, huku mchambuzi wa masuala ya uongozi, uchumi na siasa Tanzania, Dk Netho Ndilito (PhD), akiitaja kama nyaraka muhimu iliyofichua mambo makubwa matano yenye maslahi kwa taifa.

Akizungumza kuhusu ripoti hiyo, Dk Ndilito amesema baada ya kupitia maoni ya Watanzania, wanamitandao na wachambuzi mbalimbali, amebaini kuwa taarifa hiyo imeleta mwanga mpya kuhusu hali halisi ya taifa na changamoto zilizokuwa zikijadiliwa kwa muda mrefu.

Kwa mujibu wa Dk Ndilito, jambo la kwanza ni kwamba ripoti hiyo imeliponya taifa kwa kueleza ukweli ambao kwa muda mrefu haukupata nafasi ya kujadiliwa waziwazi, ikifichuliwa pia kwa nia na dhamira ovu za baadhi ya watu waliotamani vurugu kabla, wakati na baada ya uchaguzi, jambo ambalo sasa limewekwa wazi kupitia uchunguzi huo.

Aidha, ameeleza kuwa ripoti hiyo imeweka bayana upotoshaji na taarifa zisizo sahihi zilizokuwa zikisambazwa na baadhi ya watu wasiolitakia mema taifa, huku wakitamani kuona nchi ikiingia kwenye machafuko.

Katika hoja ya nne, Dk Ndilito amesema ripoti hiyo imeonesha namna Watanzania wengi wanavyoipenda nchi yao, kuiamini serikali yao na kutokuwa tayari kushawishika kuivuruga amani, umoja na mshikamano wa taifa, huku pia ripoti hiyo ikionesha uimara wa serikali pamoja na ukomavu wa vyombo vya ulinzi na usalama katika kushughulikia masuala ya ndani kwa weledi na utulivu.

Dk Ndilito alitumia nafasi hiyo kuwapongeza Watanzania kwa kuendelea kudumisha umoja, upendo, mshikamano na amani, akisisitiza kuwa huo ndiyo utamaduni uliojenga heshima ya taifa kwa miaka mingi.

“Watanzania wameendelea kuonesha ukomavu mkubwa wa kisiasa na uzalendo. Hii ndiyo desturi yetu kama taifa,” alisema.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI MEI 3,2026


Magazeti




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger