Tuesday, 23 June 2026

MWENYEKITI MPYA WA BODI YA USHAURI ADEM AONGOZA KIKAO CHAKE CHA KWANZA


📍Bagamoyo, Tanzania

Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Ushauri ya ADEM, Dkt. Hillary A. Dachi, amewasili rasmi chuoni hapo na kuongoza kikao chake cha kwanza tangu alipoteuliwa kushika nafasi hiyo, ambapo Bodi ilikutana kujadili masuala mbalimbali ya kimkakati yanayolenga kuimarisha utendaji wa taasisi na kuchangia maendeleo ya sekta ya elimu nchini.

Kikao hicho, ambacho ni Kikao cha 62 cha Bodi ya Ushauri ya ADEM, kilifanyika katika Kampasi ya Bagamoyo na kuhudhuriwa na wajumbe wa bodi pamoja na menejimenti ya taasisi wakiongozwa na Mtendaji Mkuu wa ADEM, Dkt. Maulid J. Maulid.

Akizungumza katika kikao hicho, Dkt. Dachi alieleza dhamira yake ya kushirikiana kwa karibu na wajumbe wa bodi pamoja na menejimenti ya ADEM ili kuhakikisha taasisi inaendelea kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi, ubunifu na weledi mkubwa katika kuandaa na kuendeleza viongozi wa elimu wenye uwezo wa kukabiliana na changamoto za wakati.

Kwa upande wake, Mtendaji Mkuu wa ADEM, Dkt. Maulid J. Maulid, alimkaribisha rasmi Mwenyekiti huyo mpya na kumhakikishia ushirikiano wa karibu kutoka kwa menejimenti na watumishi wa taasisi katika kutekeleza maamuzi na maelekezo yatakayosaidia kuifikisha ADEM katika viwango vya juu zaidi vya utoaji huduma.

Katika kikao hicho, wajumbe wa bodi walipata fursa ya kujadili na kutoa maelekezo kuhusu masuala mbalimbali ya maendeleo ya taasisi, ikiwemo utekelezaji wa mipango ya kimkakati, ubora wa mafunzo, uendelevu wa programu za kitaaluma pamoja na fursa za kukuza mchango wa ADEM katika maendeleo ya sekta ya elimu na Taifa kwa ujumla.

Kikao cha 62 cha Bodi ya Ushauri ya ADEM kinaashiria mwanzo wa hatua mpya ya kuimarisha usimamizi na uongozi wa taasisi hiyo, huku kikidhihirisha dhamira ya viongozi wake kuendelea kuifanya ADEM kuwa kitovu cha ubora katika maendeleo ya uongozi na usimamizi wa elimu nchini Tanzania.

Share:

Monday, 22 June 2026

PROF. SHEMDOE AELEKEZA BILIONI 5.2 ZA MRADI WA LoCAL ZITUMIKE KWA MALENGO YALIYOKUSUDIWA


Na OWM - TAMISEMI, Dodoma

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe amazielekeza Halmashauri za wilaya ya Mkinga, Mafia, Mpwapwa, Kondoa, Chamwino, Mtwara, Mtama na Manispaa ya Kigamboni kutumia Bilioni 5.2 za programu ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi (Local Climate Adaptive Facility-LoCAL) kwa malengo yaliyokusudiwa ili kuwanufaisha wananchi.

Prof. Shemdoe ametoa maelekezo hayo leo Juni 22, 2026 jijini Dodoma katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Waziri Mkuu –TAMISEMI, mara baada ya kukabidhiwa hundi yenye thamani ya Bilioni 5.2 za kitanzania na Katibu Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo ya Mitaji (UNCDF) Bw. Pradeep Kurukulasuriya, ambalo linafadhili utelelezaji wa programu ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi (LoCAL).

“Katumieni fedha hizi kama zilivyoanishwa kwenye maelekezo ya mradi huu, kama ambavyo tumefanya vizuri katika utekelezaji wa awamu ya kwanza kwenye halmashauri za Chamwino, Kondoa na Mpwapwa,” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe ameeleza kuwa, utekelezaji mzuri wa awamu ya kwanza ya mradi wa LoCAL katika Halmashauri hizo umewezesha kupatikana kwa mradi mpya wa SCALE wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi ambao unaotekelezwa katika halmashauri 54 nchini.

Katika kuongeza ufanisi wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, Prof. Shemdoe ametoa wito kwa wadau mbalimbali wa maendeleo  kujitokeza ili kuunga mkono jitihada za Serikali za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, na kuongeza kuwa milango ya Ofisi ya Waziri Mkuu - TAMISEMI ipo wazi kwa mdau yeyote mwenye nia ya kuwasaidia wananchi kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Prof. Shemdoe amefafanua kuwa, Diplomasia ya Uchumi ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ndio inayofungua milango ya wadau mbalimbali kuja kushirikiana na Serikali katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Mratibu wa Mradi wa LoCAL Wilaya ya Kondoa Bw. Laurence Robert Mogela amesema Halmashauri ya Kondoa imepokea dola za kimarekani 149,043 kwa ajili utekelezaji wa awamu ya pili ya mradi huo, utakaotekelezwa kwenye Kata ya Bumbuta kupitia kilimo cha kisasa kitakachoimarisha usalama wa chakula.

Kwa upande wake, Afisa Mazingira wa Wilaya ya Chamwino Bi. Elizabeth Solwa amesema wananchi wengi wa Wilaya ya Chamwino watanufaika na fedha za mradi wa LoCAL kwani wilaya itapokea milioni 500 kwa ajili ya kutekeleza awamu ya pili ya mradi huo katika kata mbili za Mtamalo na Mvumi Makulu.

Naye, Mratibu wa Mradi wa LoCAL Wilaya ya Mpwapwa Bw. Issa Abdallah Sepanja, amesema wilaya ya Mpwapwa imepokea Shilingi Milioni 491 kwa ajili ya kutekeleza awamu ya pili ya mradi wa LoCAL ambazo zitatumika katika vijiji vya Godegode na Kitati kuchimba visima vya umwagiliaji na kujenga mfereji wa umwagiliaji wenye urefu wa mita 1200.











Share:

Wimbo Mpya : PILI NZALIA - MAMA MKWE

 

Share:

TARURA WATOA ELIMU KWA WANANCHI 300 KUPITIA MAADHIMISHO YA UTUMISHI WA UMMA DODOMA.


Na Mwandishi Wetu, Dodoma

Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) wametoa Elimu ya miundombinu ya barabara kwa wananchi 300 waliotembelea kwenye banda lao kupitia Maadhimisho ya Utumishi wa Umma Mkoani Dodoma ambapo wananchi hao wamepatiwa ufafanuzi wa miradi mbalimbali ya barabara katika maeneo yao

Hayo yamesemwa Mkoani  na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano na Mawasiliano kwa Umma TARURA Catherine Sungura, amesema wananchi waliotembelea kwenye banda letu tumewahudumia na kusikiliza changamoto zao ambapo tunaenda kuzitatua kupitia mameneja waliopo maeneo husika.

Aidha sungura ameongeza kuwa Tarura inaendelea na ujenzi wa barabara ya zege kimara King'ong'o Dar es salaam hivyo unaendelea vizuri, na Meneja wa TARURA amewahakikishia wananchi kuwa kilomita 1.6 pekee ndizo zimebaki kukamilishwa, huku mita 800 zikitarajiwa kujengwa mwanzoni mwa mwaka mpya wa fedha kuanzia Julai na sehemu iliyobaki kukamilishwa katika awamu inayofuata.

"Nitoe wito kwa wananchi kuwa tarura itaendelea kuhakikisha miundombinu ya barabara inaboreshwa ili kurahisisha mawasiliano na usafiri kwa wananchi kwani barabara hizo zinachochea Upatikanaji wa Maendeleo ya uchumi nchini "Amesema Afisa sungura"

Hata hivyo sungura amewataka wananchi wote waendelee kutembelea kwenye banda la tarura waweze kujipatia elimu ya Miundombinu ya barabara zinazoendelea kujengwa nchini.







Share:

Wimbo Mpya : PILI NZALIA - MAMA MKWE

 

Share:

Sunday, 21 June 2026

WAZIRI SANGU: SERIKALI INATHAMINI MCHANGO WA TAASISI ZA DINI KATIKA KUJENGA AMANI NA MAENDELEO YA TAIFA


SERIKALI imeendelea kuthamini mchango mkubwa unaotolewa na taasisi za kidini nchini katika kuimarisha amani, mshikamano na maendeleo ya taifa.

Amesema hayo Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu leo Juni 19,2026 alipomwakilisha Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba, katika ibada maalum ya kuliombea Taifa la Tanzania katika kanisa la KKKT Dayosisi ya Mashariki ya Ziwa Victoria Jijini Mwanza.

Akizungumza katika ibada hiyo, Waziri Sangu amesema Serikali inatambua mchango muhimu wa taasisi za kidini katika kujenga jamii yenye maadili mema, umoja na mshikamano, mambo ambayo ni msingi wa maendeleo endelevu ya nchi.

Amesema kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wote ikiwemo makundi mbalimbali ya kijamii yenye nia njema ya kuijenga Tanzania yetu.

“Tunatambua kuwa maendeleo ya kweli hayawezi kupatikana bila amani, utulivu, umoja na mshikamano wa wananchi wake”

Katika hatua nyingine Waziri Sangu amewahasa viongozi wa dini kuendelea kuhubiri amani, upendo, uvumilivu na maadili mema kwa jamii yetu, hasa kwa vijana ambao ndio nguvu kazi ya Taifa letu.

Vilevile, amewapongeza Umoja wa Unity of Christian International (UCI) kwa kuweka malengo mazuri yanayoendana na Dira ya Taifa 2050 yenye lengo la kujenga jamii yenye mshikamano, upendo, utu na maendeleo.

Kwa upande wake, Askofu Profesa Wilson George Munguza, Askofu kiongozi Unity Christian International Dar es Salaam, ameipongeza Serikali kwa kuendelea kushirikiana na taasisi za kidini katika kuimarisha umoja na maendeleo ya Taifa.

Ibada hiyo maalum ya kuliombea Taifa viongozi wa dini, waumini na wadau mbalimbali wameshiriki ikiwa ni sehemu ya kuendelea kuhamasisha amani, umoja na maendeleo ya Tanzania.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JUNI 21,2026

Magazetini Leo




Share:

Saturday, 20 June 2026

TBS YATIMIZA MIAKA 50, YAWEKEWA MKAKATI WA KUONGOZA UBORA AFRIKA



Na mwandishi wetu, Dodoma

Shirika la Viwango Tanzania (TBS) limepongezwa kwa mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kipindi cha miaka 50 tangu kuanzishwa kwake, huku likitakiwa kuendelea kwenda sambamba na maendeleo ya teknolojia na mabadiliko ya soko la dunia ili kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania kimataifa.

Pongezi hizo zimetolewa na Waziri wa Viwanda na Biashara, Judith Kapinga,wakati wa maadhimisho ya kilele cha miaka 50 ya shirika hilo yaliyofanyika katika ofisi zake zilizopo Njedengwa jijini Dodoma, sambamba na uzinduzi wa kitabu kinachoelezea historia, mafanikio na mchango wa taasisi hiyo katika kukuza ubora wa bidhaa na huduma nchini.

Waziri Kapinga amesema TBS imekuwa nguzo muhimu katika kulinda afya na usalama wa wananchi kupitia usimamizi wa viwango vya bidhaa mbalimbali, huku ikichangia kwa kiasi kikubwa ukuaji wa sekta za uzalishaji, biashara na viwanda nchini.

Ameeleza kuwa katika kipindi hiki ambacho dunia inaendelea kubadilika kwa kasi kupitia teknolojia na ubunifu, TBS inapaswa kuwa na dhana ya kujitegemea zaidi kwa kuimarisha mifumo ya kisasa ya utoaji huduma na kuongeza uwezo wake wa kitaalamu ili kukidhi mahitaji ya soko la ndani na nje ya nchi.

"Tunapoadhimisha miaka 50 ya TBS, tunashuhudia mchango mkubwa wa taasisi hii katika kujenga imani ya bidhaa za Tanzania. Hata hivyo, ni muhimu kuendelea kuwekeza katika teknolojia, ubunifu na ushirikiano na sekta binafsi ili kuhakikisha bidhaa zetu zinakidhi viwango vya kimataifa," amesema Kapinga.

Aidha, Waziri huyo amesisitiza umuhimu wa TBS kuendelea kufanya kazi kwa karibu na sekta binafsi ili kuongeza ubora wa bidhaa zinazozalishwa nchini na kusaidia kutafsiri kwa vitendo maono ya Tanzania ya kuwa taifa lenye uchumi wa viwanda unaozalisha bidhaa zenye ushindani mkubwa katika masoko ya kikanda na kimataifa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Dkt. Ashura Katunzi,amesema maadhimisho hayo ni fursa ya kutathmini mafanikio yaliyofikiwa na kuweka mikakati mipya ya kuifanya taasisi hiyo kuwa ya kisasa zaidi na yenye uwezo mkubwa wa kukabiliana na changamoto za karne ya 21.

Dkt. Katunzi amesema TBS itaendelea kuimarisha maabara za kisasa, kuongeza matumizi ya teknolojia za kidijitali na kuwekeza katika rasilimali watu ili kuhakikisha huduma za viwango zinakuwa bora zaidi, za haraka na zenye kuaminika.

"TBS inatambua kuwa dunia inabadilika kwa kasi kubwa, huku teknolojia na mazingira ya biashara vikibadilika, hivyo shirika hilo linapaswa kuendelea kuwa imara, bunifu na lenye uwezo wa kujibu changamoto mpya zinazoibuka."aamesema Dkt. Katunzi

Amebainisha kuwa kwa kipindi cha nusu karne, TBS imekuwa mhimili muhimu wa maendeleo ya viwanda na biashara nchini kwa kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa na kuuzwa zinazingatia viwango vinavyotakiwa, jambo ambalo limeongeza imani ya walaji na kufungua fursa za biashara katika masoko mbalimbali duniani.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara, Kilimo na Mifugo, Mariam Ditopile Mzuzuri, amesema TBS imekuwa mhimili muhimu katika kulinda maslahi ya walaji, kuimarisha ushindani wa bidhaa za Tanzania na kuchochea ukuaji wa sekta za uzalishaji nchini.

Ditopile amesema ipo haja ya kufanyika kwa mapitio ya kina ya Sera ya Ubora wa Bidhaa ili iweze kuakisi mabadiliko makubwa yaliyotokea katika nyanja za sayansi, teknolojia, biashara na uzalishaji tangu sera hiyo ilipoanzishwa.

"Tunapoipongeza TBS kwa mafanikio ya miaka 50, ni muhimu pia kuangalia mbele na kufanya maboresho yatakayoiwezesha taasisi hii kuendelea kuwa nguzo ya maendeleo ya viwanda, biashara na kilimo katika mazingira ya sasa ya kiteknolojia," amesema Ditopile.

Ditopile amesema imejijengea rekodi ya kuwa taasisi muhimu katika kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa, kuuzwa na kutumiwa nchini zinakidhi viwango vinavyotakiwa kwa ajili ya kulinda afya, usalama na maslahi ya watumiaji.

Naye Katibu Mkuu wa Shirikisho la Viwango Afrika (ARSO), Dkt. Hermogene Nsengimana, amesema Julai 2026 Tanzania itakuwa nchi ya saba barani Afrika kupata Alama ya Ubora ya Afrika (Africa Quality Mark) kwenye bidhaa zake.

Amesema kwa hatua hiyo, Tanzania itaungana na Rwanda, Togo, Senegal, Ethiopia, Nigeria na Zimbabwe katika nchi zinazotumia alama hiyo ya ubora inayolenga kuimarisha viwango vya bidhaa barani Afrika.

Amesema Shirikisho la Viwango Afrika limekwisharatibu na kuoanisha takribani viwango 2,600 vinavyolenga sekta za kipaumbele ikiwemo usindikaji wa mazao ya kilimo, sekta ya magari, dawa na bidhaa za afya, usafirishaji na ugavi, pamoja na nguo na bidhaa za ngozi.

Ameeleza kuwa kwa sasa takribani bidhaa 500 katika ngazi ya Afrika zinapitiwa ili kupata Alama ya Ubora ya Afrika, hatua itakayosaidia kurahisisha biashara ndani ya Eneo Huru la Biashara la Afrika (AfCFTA).

Amesema bidhaa za Tanzania ambazo kwa sasa zinabeba alama ya TBS, zitapata fursa ya kuwekewa alama ya ubora ya Afrika, jambo litakaloongeza ushindani na upatikanaji wa masoko katika nchi mbalimbali za bara hilo.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger