Monday, 6 April 2026

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU APRILI 6,2026

         
 Magazeti
   


Share:

Sunday, 5 April 2026

UKOMAVU WA KISIASA: RAIS SAMIA AZIBA MAKOVU YA UCHAGUZI, AKUTANA NA WAGOMBEA URAIS 16 IKULU

 

Katika hatua inayotajwa kama kielelezo cha juu cha ukomavu wa demokrasia na uongozi wenye busara, Rais Samia Suluhu Hassan amekutana na kufanya mazungumzo na waliokuwa wagombea urais 16 alioteuliwa nao katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu. 0755844215 

Mkutano huo wa kihistoria uliofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam tarehe 31 Machi 2026, umelenga kuimarisha maridhiano ya kitaifa na mshikamano baada ya kipindi cha ushindani wa kisiasa.

Wadau mbalimbali wa siasa, wasomi, na wachambuzi wamemwagia sifa Rais Samia kwa hatua hiyo, wakibainisha kuwa imesaidia "kuziba makovu" yaliyotokana na joto la uchaguzi. 

Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa, Juma Ally Khatib, amepongeza kitendo hicho akisema kinaleta tafsiri njema ya demokrasia na kukuza siasa za staha. 

Amesema kuwa washindani kukaa meza moja na mshindi ni ishara kuwa maslahi ya Tanzania ni makubwa kuliko itikadi za vyama.

Mwanasiasa mkongwe, Hamad Rashid, amebainisha kuwa mkutano huo ni utekelezaji wa vitendo wa falsafa ya Rais Samia ya 4R (Maridhiano, Ustahimilivu, Mageuzi na Kujenga Upya). 

Rashid ameshauri utaratibu huu uwe wa kudumu na hata kuingizwa kwenye mfumo wa maandishi kama kanuni ya nchi, huku akitoa mwito kwa upande wa Zanzibar kuiga mfano huo ili kuunganisha wananchi.

Uchambuzi wa wasomi, akiwemo Dk. Paul Loisulie wa UDOM na Goodluck Ng’ingo, unaonesha kuwa Rais amefanya jambo la msingi kwani amani na utulivu ndivyo vinavyotoa nafasi kwa serikali kutekeleza majukumu ya maendeleo kwa wananchi.

 Wamesisitiza kuwa siasa za kuheshimiana hupunguza taharuki, hasa katika zama hizi ambapo mitandao ya kijamii hutumika vibaya kuchochea migogoro.

Kwa upande wake, Rais Samia kwa kuitikia wito huo wa wagombea wenzake, amethibitisha kuwa milango yake iko wazi kwa majadiliano yenye tija. 

Viongozi hao wa vyama 16 walipata fursa ya kuwasilisha maoni yao kuhusu hali ya nchi, amani, na mshikamano, jambo linalotuma ujumbe mzito kwa ulimwengu kuwa Tanzania ni taifa linalotatua tofauti zake kupitia mazungumzo ya kistaarabu badala ya mivutano. 

Share:

MALUNDE 1 BLOG INAKUTAKIA SIKUKUU NJEMA YA PASAKA!

 


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI APRILI 5,2026

magazeti






Share:

Saturday, 4 April 2026

MWANAMKE AUAWA KWA KUKATWA SHINGO SHINYANGA


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Janeth Magomi akizungumza na vyombo vya habari mjini Shinyanga Jumamosi Aprili 4, 2026.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Janeth Magomi akizungumza na vyombo vya habari mjini Shinyanga Jumamosi Aprili 4, 2026.

Na mwandishi wetu - Malunde 1 blog

Jeshi la Polisi linawashikilia watuhumiwa wawili kuhusiana na mauaji ya kikatili ya mwanamke Hollo Ruchanganya (60), mkazi wa kijiji cha Bunambiyu wilayani Kishapu mkoani Shinyanga, huku uchunguzi wa awali ukihusisha imani za kishirikina.

Akizungumza na vyombo vya habari mjini Shinyanga leo Jumamosi Aprili 4, 2026, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, ACP Janeth Magomi, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa watuhumiwa hao wanahojiwa ili kubaini ukweli wa tukio hilo.

Katika tukio hilo, marehemu Hollo Ruchanganya aliuawa kikatili kwa kukatwa shingoni na mtu asiyejulikana, kabla ya mwili wake kutupwa katika shamba la mahindi jirani na makazi yake.

Kwa mujibu wa taarifa za awali, mtuhumiwa wa mauaji hayo anadaiwa kuwa mgeni aliyefika nyumbani kwa marehemu majira ya saa 3:00 usiku wa Aprili 3, 2026, ambapo alikula chakula pamoja na marehemu na wajukuu wake.

 Baadaye marehemu alimsindikiza mtuhumiwa huyo kwa lengo la kumpeleka kwa mtalaamu wa tambiko linalodaiwa kuzuia kupata watoto pacha.

Inaelezwa kuwa muda mfupi baada ya kutoka, mtu huyo alirejea nyumbani na kurejesha tochi, akiwataarifu wajukuu wa marehemu kuwa bibi yao angerudi asubuhi kutoka kwa mganga anayeelezwa kuwa ni ndugu yake.

Mwili wa marehemu uligunduliwa asubuhi na mjukuu wake aliyekuwa akielekea shambani, baada ya kuona damu nyingi na nguo za marehemu njiani. Baada ya kutoa taarifa kwa ndugu, walifanikiwa kuufuatilia mwili huo uliokuwa umetupwa shambani ukiwa na jeraha kubwa la kukatwa shingoni.

Kamanda Magomi amesema uchunguzi unaendelea ili kubaini wahusika wote na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.


Share:

KAHAMA KUCHEKA KWA NGUVU JUMAMOSI HII !! LIVE COMEDY SHOW UKUMBI WA MALEX 🔥



Meneja wa Vipindi na Ubunifu kutoka Jambo Media, Renatus Kiluvia maarufu kama Bizzo Fresh, akizungumza na kuelezea maandalizi na umuhimu wa Live Comedy Show itakayofanyika Kahama.
Mchekeshaji Joo Master akizungumza kwa kujiamini kuhusu maandalizi ya wasanii, akieleza namna walivyojipanga kikamilifu kuhakikisha wakazi wa Kahama mkoani Shinyanga wanapata burudani ya vichekesho yenye viwango vya juu.
Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Kampuni ya Lake Talent, kwa kushirikiana na Gakala Health Center, wanakuletea tamasha kubwa la vichekesho litakalotikisa mji wa Kahama, Jumamosi, Aprili 4, 2026, katika Mkesha wa Pasaka, kuanzia saa 1:00 usiku katika Ukumbi wa Malex.

Tamasha hili linatarajiwa kuwakutanisha mastaa mbalimbali wa vichekesho na burudani kutoka ndani na nje ya nchi, kwa usiku mmoja wa kicheko kisicho na kikomo.

Akizungumzia maandalizi ya tukio hilo, Meneja wa Vipindi na Ubunifu kutoka Jambo Media, Renatus Kiluvia maarufu Bizzo Fresh, amesema kila kitu kimekamilika kuhakikisha show hiyo inakuwa ya kipekee na ya kukumbukwa.

“Kahama show kubwa ni moja tu , pale Ukumbi wa Malex! Tumejipanga kuleta burudani ya kiwango cha juu kabisa,” amesema Bizzo Fresh.
Ameongeza kuwa lengo kuu ni kuwakutanisha wakazi wa Kahama na maeneo ya jirani kupitia burudani safi ya vichekesho vyenye ubunifu na mvuto wa hali ya juu.

"Tamasha hili linalenga kutoa burudani kwa wananchi pamoja na kukuza vipaji vya vijana katika tasnia ya vichekesho. Stand-up comedy imekuwa chanzo cha ajira kwa vijana wengi, na sasa imebadilika kutoka uchekeshaji wa kawaida hadi kuwa biashara inayowaingizia kipato. Sisi kama Jambo Media tumeamua kuwaunga mkono vijana hawa,” amesema Kiluvia.

Akizungumza kwa niaba ya wenzake, mchekeshaji Joo Master (Jo Master) amewataka wakazi wa Kahama kujitokeza kwa wingi kushuhudia tamasha hilo, akiahidi burudani ya hali ya juu.

“Tupo Kahama, show ipo, na tumejipanga kikamilifu kuhakikisha kila mtu anacheka bila kikomo,” amesema.
Amesema tamasha hilo litakuwa la kipekee na wasanii wote wako tayari kuwapa mashabiki burudani ya kiwango cha juu, itakayowafanya kuvunja mbavu kwa kicheko.

Jo Master amewahamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi kushuhudia burudani hii ya kipekee, akisisitiza kuwa huu ni usiku maalum wa kuondoa msongo wa mawazo na kufurahia maisha kupitia vichekesho vyenye ubunifu na vicheko visivyo na kikomo.

Tamasha hilo litapambwa na mastaa maarufu wakiwemo:
👉 Wanani
👉 Dogo Pepe
👉 MC Ndembo
👉 Shaf Brand
👉 Godfrey Steven
👉 Man Kush (254 Kenya)
👉 Joo Master

Pia, tamasha litashirikisha wachekeshaji chipuzi wakali, wakiwemo MC Ndabitha na Daines, wakiahidi kuwachangamsha mashabiki kwa vichekesho vya kipekee.

🎟️ VIINGILIO:
Platinum: Sh 15,000/- (Mlangoni Sh 20,000/-)
💫 Gold: Sh 50,000/-
🛋️ Sofa Single: Sh 150,000/-
❤️ Sofa Couple: Sh 250,000/-

📍 SEHEMU ZA KUPATIA TIKETI:
🛒 Vunja Bei
📻 Magic 101
🏬 Best Choice Store
👗 Sodox Fashion
💄 JJ Cosmetic
🎬 Kichomi Studio
📲 Pia kupitia Nilipe App

USIKOSE! Kahama inaenda kucheka kwa nguvu – nawe uwe sehemu ya burudani hii kubwa! 😂🔥

📞 MAWASILIANO:

📲 0754 418 189
📲 0787 581 013
Meneja wa Vipindi na Ubunifu kutoka Jambo Media, Renatus Kiluvia maarufu Bizzo Fresh




Share:

Friday, 3 April 2026

BAGAMOYO YAVUTA WAWEKEZAJI, MAOMBI 48 YAPOKELEWA



Mkurugenzi wa Mamlaka ya Uwekezaji na Maeneo Maalum ya Kiuchumi Tanzania (TISEZA), Gilead Teri, akizungumza leo Aprili 2, 2026 jijini Dar es Salaam

***

DAR ES SALAAM:

Kongani ya Bagamoyo imeendelea kuwa kitovu cha uwekezaji nchini baada ya kupokea maombi 48 kati ya maombi 86 yaliyowasilishwa TISEZA hadi kufikia Aprili Mosi mwaka huu.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mkuu wa TISEZA, Gilead Teri, amesema mwitikio huo unaonyesha imani kubwa ya wawekezaji katika eneo hilo.

Amesema mbali na Bagamoyo, kongani ya Kwale imepokea miradi 20, huku Nala na Buzwagi zikibaki na miradi miwili kila moja.

Kwa mujibu wa Teri, mafanikio hayo yanachangiwa na uwepo wa miundombinu bora pamoja na sera rafiki za uwekezaji zinazotekelezwa na Serikali.




Amebainisha kuwa mradi wa Bagamoyo Eco Maritime City umeendelea kuvutia wawekezaji wengi zaidi wanaotaka kuwekeza katika sekta mbalimbali za uzalishaji.




Katika hatua nyingine, TISEZA imesaini mikataba na kampuni tisa zitakazowekeza zaidi ya Shilingi bilioni 177 katika miradi ya viwanda na huduma.





Amesema uwekezaji huo unatarajiwa kuongeza ajira pamoja na kuchochea ukuaji wa uchumi wa viwanda nchini.

Aidha, Teri ametoa wito kwa wawekezaji wa ndani kutumia fursa zilizopo kwa kusajili miradi yao kupitia TISEZA ili kunufaika na vivutio vya Serikali.




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger