Tuesday 28 November 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE NOVEMBA 28,2023





Share:

Monday 27 November 2023

TCRA CCC YAKUTANA NA WATOA HUDUMA ZA MAWASILIANO KUBORESHA HUDUMA KWA MTUMIAJI WA MAWASILIANO


Katika kutekeleza majukumu yake ya Kisheria Baraza la washauri la watumiaji huduma za mawasiliano (TCRA CCC), 
chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Hawa Ng'humbi
 imefanya mkutano na Umoja wa Watoa Huduma za Mawasiliano (TAMNOA) kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali yanayomhusu mtumiaji wa huduma za mawasiliano ili kuboresha huduma kwa mtumiaji. 

Mkutano huo uliofanyika leo Jumatatu Novemba 27, 2023 pamoja na mambo mengine umeangazia changamoto za watumiaji na namna ambavyo TCRA CCC, Watoa Huduma na wadau wengine wanaweza kuzishughulikia ili kuondoa kero kwa watumiaji.

#HudumaBoraZaMawasilianoNiHakiYako
#TanzaniaYaKidijitali
Share:

ANDAENI WAINJILISTI WA KUDUMU WATAKAO FANYA KAZI YA KUENEZA INJILI - MCH. MWAZYUNGA



Na. Gideon Gregory, Dodoma.

Kiongozi wa Uinjilisti Kanisa la Moravian Nkuhungu Jijini Dodoma Mch. Boaz Mwazyunga ametoa wito kwa kanisa hilo jimbo la Kaskazini kuwa na mpango wa kuandaa wainjilisti wa kudumu ambao pamoja na kazi yao watafanya kazi ya kueneza injili ikiwa ni pamoja na kufungua na kupanda makanisa mapya vijijini.


Mch. Mwazyunga ametoa wito huo leo Novemba 26,2023 wakati akiongoza waumini wa kanisa la Moravian Tanzania jimbo la Kaskazini ushirika wa Nkuhungu kuadhimisha miaka 16 ya kutoa huduma ya kiroho kwa waumini hao nakuongeza kuwa hapaswi kuogopa gharama na kuangalia nani yupo katika maeneo wanayokwenda pamoja na mazingira yaliyopo.


“Wito wangu ni kuona kuwa kanisa linatii agizo la Bwana Yesu Kristo alilosema, basi nendeni mkawafanye mtaifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la baba, na mwana na roho mtakatifu na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi na tazama mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari (Mathayo 28:19-20),”amesema.


Aidha ameongeza kuwa Kanisa hilo limekuwa nyuma kwasababu ya kutokufanya uinjilisti na watu kuwa na dhana ya kuwa kazi ya kufanya uinjilisti ni ya watu au kikundi fulani, kumbe ni kazi hiyo ni ya watu wote.


“Umefika wakati sasa wa kwenda maeneo ya pembezoni na vijiji kununua viwanja na mashamba ili tunapofanya uinjilisti wale tutakaowapa wawe na mahali pa kuanzia kuabudia,”ameongeza.


Awali akitoa mafundisho Mwenyekiti wa Kanisa la Moravian Tanzania jimbo la Kaskazini Mch. Isaac Siame ametoa rai kwa waumini kumruhusu Mungu awatumie katika utumishi wao na kuongeza kuwa wasikubali shetani akawatumia katika mipango yake hovu kwa wanadamu.



Amesema mpango wa Mungu kwa mwanadamu ni kipaumbele tosha katika kukabiliana na changamoto mbalimbali ambazo mwanadamu peke yake hawezi kuzitatua pasipo kumshirikisha Mungu na kutenda yale ambayo yanapendeza mbele Bwana.


Akisoma risala mbele ya mgeni rasmi Wakili wa Ushirika 2023 Lilian Nzowa amesema tangu ushirika huo uanzishwe umefanikiwa kuongeza wakristo 170 kutoka 58 hapo awali wakati unaanzishwa ongezeko linalojumuisha watu wazima pamoja na watoto.


Sambamba na hayo maeongeza kuwa kwa mwaka 2024 wanatarajia kuanza ujenzi wa jengo la kuabudia linalotarajia kugharimu kiasi cha shilingi bilioni 2 ambalo litakuwa na uwezo wa kuchukua jumla ya watu 800 kwa ibada moja.


Kanisa la Moravian Tanzania jimbo la Kaskazini wilaya ya Kati ushirika wa Nkuhungu lilianza ibada rasmi Novemba 25,2007 kutoka ushirika wa Dodoma na Mch. Esau Kalinga ndiye aliyeongoza ibada hiyo na kutangaza rasmi kwamba Nkuhungu ni ushirika siyo mtaa.
Share:

Tanzia : MSANII MAARUFU WA NYIMBO ZA ASILI BHUHULU LUSAFISHA AFARIKI DUNIA

Msanii Maarufu wa Nyimbo za Asili za Kabila la Wasukuma Bhuhulu Lusafisha / Buhulu Lusafija mkazi wa Ngaya Wilaya ya Kahama amefariki dunia.

Taarifa zinaeleza kuwa Msanii Bhuhulu Lusafisha amefariki dunia Jana Jumapili Novemba 26,2023 wilayani Kahama baada ya kuugua muda mrefu na mazishi yatafanyika leo kijiji cha Mwakuzuka kata ya Ngaya wilayani Kahama mkoani Shinyanga.
Bhuhulu Lusafisha enzi za uhai wake.

HIZI HAPA BAADHI YA NYIMBO ZA MSANII BHUHULU LUSAFISHA

   
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOVEMBA 27,2023






Share:

Sunday 26 November 2023

MAKATIBU WAKUU WAFANYA ZIARA HANDENI WANAPOHAMIA WAKAZI WA NGORONGORO


Makatibu Wakuu wakikagua maendeleo ya ujenzi nyumba na miundo mbinu ya kuhamisha wananchi wanaotoka eneo la Hifadhi ya Ngorongoro kwenda Kijiji cha Msomera Wilaya ya Handeni  wakati wa ziara yao mkoani Tanga.

Na Mwandishi wetu - Tanga

Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge na Uratibu, Dkt. Jim Yonazi Dkt. Yonazi amesema Serikali imejipanga katika kuhakikisha kuwa wizara zote za kisekta zinashiriki kikamilifu katika kuhakikisha kuwa miradi iliyopo katika Kijiji cha Msomera inakamilika kwa wakati ili kuwezesha wananchi wanaoendelea kujiandikisha kuhamia katika eneo hilo ili kuendelea shughuli zao. 

Dkt. Yonazi aliyasema hayo wakati  wa ziara ya kikazi  ya Makatibu Wakuu wa Wizara za kisekta waliyoifanya katika  Kijiji cha Msomera, Wilaya, Handeni mkoani Tanga kujionea hatua mbalimbali za ujenzi wa miundombinu  kabla ya kuanza kwa awamu ya pili ya kuhamisha wananchi wanaoishi katika hifadhi ya Ngorongoro waliojiandikisha kuhama kwa hiari.

Amesema Makatibu Wakuu  hao wamekagua ujenzi wa miundo mbinu mbalimbali ikiwemo maji, umeme, madaraja, barabara, shule, Nyumba za makazi na uboreshaji wa huduma za mawasiliano.

“Niwaombe wanaohamia eneo hili waiamini Serikali kwamba inawatengenezea mazingira yaliyo bora sana hapa Msomera, nyumba  zinazojengwa  na huduma zote zina ubora ili wananchi wetu wanufaike  na Serikali yao waachane na upotoshaji kwa sababu imewekeza fedha nyingi kuhakikisha wanaishi katika mazingira salama,”Amesema Dkt. Yonazi.

Naye  Kamanda wa Kikosi  Kazi cha Ujenzi wa nyumba 5000  kutoka Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ) Brigedia Jenerali Hassan Mabena amesema kila taasisi ya kisekta na Wizara  zinawajibika ipasavyo kuhakikisha ujenzi huo unakamilika kwa wakati  akisema kuwa  licha ya changamoto za mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali lakini kazi inaendelea vizuri .

“Mpaka sasa ujenzi wa Msomera  ambao tumeugawanya katika vitalu kuanzia A mpaka D tuko katika hatua mbalimbali za ujenzi nyumba 1000 katika eneo la Msomera B kitalu F viwanja 768  taratibu zake zimekamilika eneo liko tayari kwa ajili ya uchimbaji na kuanza msingi na kuendelea na hatua za ujenzi,”Ameeleza Brigedia Jenerali Mabena.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mhe. Albert Msando  amewashukuru Makatibu Wakuu hao kwa kutembelea mradi huo hatua inayoongeza kasi yake kusonga mbele akiahidi kusimamia kwa karibu mradi huo ambao umefanyika kama hatua ya kuboresha maisha ya watanzania kila mwananchi kuishi katika hali ya ustawi pamoja na uwepo wa miundo mbinu muhimu pamoja na huduma za kijamii.

“Hii inaonyesha nia ya dhati ya Serikali  ya kukamilisha mradi huu muhimu kwa wakati siyo tu kuhamisha watu lakini unaenda kuboresha maisha ya watanzania tunaendelea kuwaahidi kwamba tutasimamia kwa karibu tunajua unatekelezwa wakati wa mvua ambapo kwetu ni fursa ya kuona namna ya kuyavuna maji  kwa ajili ya matumizi,”Amebainisha  


Aidha Mwenyekiti wa Kijiji cha Msomera Bw. Martin Oleikayo Paraketi amempongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kufanya mradi huo akisema umekuja kwa wakati muafaka kwani umesaidia  wakazi waliokuwa wakiishi katika maeneo hayo kupata huduma muhimu zikiwemo mawasiliano, ujenzi wa shule za sekondari, kituo cha afya na barabara.

“Hii kwetu ni neema kubwa sana Serikali inafanya kazi kubwa na niwaambie waliopo Ngorongoro wasikubali kupotoshwa na watu wachache wasio na nia njema  kijiji cha Msomera ni kijiji mojawapo  kati ya Vijiji 91 ndani ya Wilaya ya Handeni mradi huu umeleta faida kubwa kupitia wenzetu waliohamia kutoka Ngorongoro,”Amepongeza Mwenyekiti huyo.



Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger