Monday 2 October 2023

BENKI YA CRDB SHINYANGA YAADHIMISHA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA...YAAHIDI KUBORESHA ZAIDI HUDUMA

 

Na Marco Maduhu,SHINYANGA

BENKI ya CRDB Tawi la Shinyanga imeadhimisha wiki ya huduma kwa wateja, huku akiahidi kuendelea kutoa huduma bora zaidi.

Maadhimisho yao yamefanyika leo Oktoba 2,2023 katika benki hiyo ambayo yatakwenda hadi Oktoba 6 na yamehudhuriwa na wateja wake pamoja na kushiriki kifungua kinywa(Break Fast) na utoaji wa zawadi kwa baadhi ya wateja na Wafanyakazi wa Benki ya CRDB.
Akizungumza wakati wa maadhimisho hayo, Meneja Tawi la Benki ya CRDB Shinyanga Luther Mneney, amewashukuru wateja kwa kuendelea kuiamini benki hiyo, huku akiahidi wataendelea na utoaji wa huduma bora zaidi.

"Hii ni wiki ya huduma kwa wateja, na sisi Benki ya CRDB tumeanza kuadhimisha leo na wateja wetu, na tunaahidi kuendelea kutoa huduma bora zaidi," amesema Mneney.
Naye Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi Jumanne Wagana, amesema Benki hiyo inawathamini sana wateja wake, na mafanikio makubwa ambayo imekuwa ikiyapata ni kutokana na wao.

Aidha, amesema pale wateja wao wanapoona kuna changamoto mahali, wasisite kuwasiliana na benki hiyo ili kufanya marekebisho na kuendelea kutoa huduma bora kwao.
Kwa upande wake Mgeni Rasmi katika wiki hiyo ya huduma kwa wateja Benki ya CRDB Jackton Koyi, ambaye ni mteja maarufu wa benki hiyo zaidi ya miaka 30, amewapongeza watumishi wa CRDB kwa kufanya kazi kwa weledi,bidii, ubunifu na kutoa huduma stahiki kwa wateja wake.

Ameiomba Benki hiyo ya CRDB waendelee na utoaji wa huduma nzuri na bora kwa wateja wao,sababu ni benki ambayo inafanya kazi vizuri ndani na nje ya nchi.
Mgeni Rasmi Jackton Koyi akizungumza kwenye maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja Benki ya CRDB.
Meneja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga Mjini Luther Mneney akizungumza kwenye Maadhimisho hayo ya wiki ya huduma kwa wateja Benki ya CRDB.
Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi Jumanne Wagana akizungumza kwenye Maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja.
Meneja Biashara CRDB Kanda ya Magharibi Anselm Mwenda akizungumza kwenye maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga Mjini.
Meneja Biashara Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga Mjini Mwanahamisi Iddy akizungumza kwenye Maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja.
Meneja wa CRDB Tawi la Shinyanga Luther Mneney akiwa na Mwenyekiti wa Mawakala wa huduma za kifedha mkoani Shinyanga Juliana Shilatu wakikata Keki kwenye maadhimisho hayo ya wiki ya huduma kwa wateja.
Mwenyekiti wa Mawakala wa huduma za kifedha Juliana Shilatu (kulia) akimlisha Keki Meneja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga Luther Mneney.
Meneja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga Luther Mneney (kushoto)akimlisha Keki Mwenyekiti wa Mawakala wa huduma za kifedha mkoani Shinyanga Juliana Shilatu.
Muonekano wa Keki.
Wateja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga wakiwa kwenye maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja.
Wateja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga wakiwa kwenye maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja.
Wateja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga wakiwa kwenye maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja.
Meza kuu.
Watumishi wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga.
Watumishi wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga.
Wateja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga wakiwa kwenye maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja.
Wateja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga wakiwa kwenye maadhimisho ya wiki ya huduma kwa wateja.
Wateja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga wakishirikia kifungua kinywa (Break Fast).
Wateja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga wakipata kifungua kinywa (Break Fast).
Wateja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga wakipata kifungua kinywa (Break Fast).
Wateja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga wakipata kifungua kinywa (Break Fast).
Wateja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga wakipata kifungua kinywa (Break Fast).
Wateja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga wakipata kifungua kinywa (Break Fast). 
Wateja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga wakipata kifungua kinywa (Break Fast).
Wateja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga wakipata kifungua kinywa (Break Fast).
Wateja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga wakipata kifungua kinywa (Break Fast).
Wateja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga wakipata kifungua kinywa (Break Fast).
Wateja wa Benki ya CRDB Tawi la Shinyanga wakipata kifungua kinywa (Break Fast).
Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi Jumanne Wagana (kushoto) akimkabidhi Zawadi Mteja wa Benki hiyo Jackton Koyi.
Zawadi zikiendelea kutolewa kwa wateja wa Benki ya CRDB.
Zawadi zikiendelea kutolewa kwa watumishi wa Benki ya CRDB
Zawadi zikiendelea kutolewa kwa Wafanyakazi wa Benki ya CRDB.
Zawadi zikiendelea kutolewa kwa wateja wa Benki ya CRDB.
Picha za pamoja zikipigwa.
Picha za pamoja zikipigwa.
Picha za pamoja zikipigwa.
Picha za pamoja zikipigwa.
Share:

Sunday 1 October 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU OKTOBA 2,2023













































































Share:

RAIS SAMIA AMTEUA MOBHARE MATINYI KUWA MSEMAJI MKUU WA SERIKALI

Share:

RC MANYARA LAUNCHES THE CHEMCHEM CUP 2023, 33 TEAMS WILL TAKE PART



Staff writter.Babati
Maipacarusha20@gmail.com


The 16th Chemchem Cup 2023, which aims to combat giraffe poaching, was launched in the Burunge Widlife Management Area .


Speaking at the launch, Babati District Commissioner Lazaro Twange on behalf of the Regional Commissioner, said that the chemchem CUP , in spite of raising sports talents, promotes preservation.


Twange has said that the 10 villages that make up Burunge WMA, ought to collaborate with the chem chem foundation that has managed tourism and conservation exercises in the area.


"We expect you to be good conservation ambassadors, provide information on those involved in poaching, and also continue to benefit from conservation," he said.


The Founder Chemchem association,Fabia Bausch  said that the chemchem CUP since its beginning, has been known to be of great benefit to include the community in preservation through conservation.


He said this year, for the first time, there will be 10 young ladies and soccer teams.


He said that the institution has set aside more than Sh 99 milion to make this year's championship a success.


Earlier, the chairman of the championship, Elasto Belela said that the preparations for the championship have been completed, and all participating teams have already been given sets of jerseys and balls for preparation.

He said that the first winner will be given a prize of sh 2.5 milion  the second 1.5 milioni the third 1 million.

Belela said for Queens soccer winner 1.5 milioni,second winner 1milioni and Third team winner 500,000

He added under18 winner will be given a prize of
1milioni,Second winner 600,000 and third under 18 winner 400,000.
The end.

Share:

UJUMBE MZITO WA MHE. STEPHEN MASELE AKISHEREHEKEA SIKU YAKE YA KUZALIWA

 STEPHEN JULIUS MASELE: UJUMBE WANGU KWENU WAPIGANAJI LEO KATIKA SIKU YANGU YA KUZALIWA LEO TAREHE 01 OKTOBA 2023. 


Habari za leo ndugu zangu wapendwa? 

Ndugu zangu kwa mapenzi ya Mwenyezi Mungu sasa nimekuwa mtu mzima, busara na maarifa vimeongezeka,, na akili imekomaa zaidi na uzoefu na uvumilivu umeongezeka na  nimekomaa zaidi, nimekuwa kiumri na kiuongozi. Namtukuza Mwenyezi Mungu kwa zawadi hii muhimu ya afya na uhai. Tuzidi kumuomba yeye Mwenyezi Mungu kwani ndie muweza wa yote. 


Kiukweli ndugu zangu, Sina maneno mazuri zaidi ya kuelezea jinsi ninavyowapenda kwa dhati ya moyo wangu, nawapenda sana ndugu zangu, kwa namna tunavyoishi kwa kushirikiana kama familia moja, napenda umoja wetu uliojengwa kwa misingi ya upendo na kuta za ukweli na kuezekwa kwa paa ujasiri. 


Nafurahia maisha pamoja nanyi ndugu zangu. Leo katika siku yangu ya kuzaliwa Nataka nitamke kwamba ninyi ni sehemu ya familia yangu. Tumepitia magumu pamoja, ni wakati wetu sasa wa kujenga furaha ijayo kupitia umoja na mshikamano wetu, tuendelee kusaidiana kwenye shida na raha bila kubaguana.

 Natambua kwenye familia kubwa hapakosi tofauti za hapa na pale, tuendelee kuvumiliana kwani hakuna aliye mkamilifu kwani Mola wetu ametuumba tukiwa dhaifu. Tusisahau malengo yetu na malengo ya chama chetu ni kushinda dola 2024/2025 kwa kushindo kwa nafasi za mitaa, udiwani, ubunge na Urais. 


Najua njia haitakuwa nyepesi, mawimbi na dhoruba zitakuwepo cha muhimu ni kushikamana pamoja na hakika tutashinda. Kwa pamoja tutashinda, kwa umoja wetu tutashinda, kwa nguvu zetu tutashinda. 


Chama chetu kinapaswa kuendelea kusimamia HAKI na UKWELI , kutengenezeana  ajali za kisiasa kunadhoofisha chama, tabia hii haikuwepo huko nyuma, najua sote mnajua tabia hii wapi ilikotoka, hatuwezi kukubali iendelee kwani itakivunja na kukisambaratisha chama. Hatuwezi kukubali uonevu, dhuruma na ubaguzi viendelee. 


Tutapigana mpaka tone la mwisho la damu kuhakikisha chama kinashinda chaguzi zijazo. Tunataka wana CCM shinyanga mjini warejee kwenye furaha kama zamani, natambua mioyo yenu inaumia sana lakini hamna la kufanya, nawaomba vumilieni. 


Hakika ukweli unaenda unajulikana, taifa litatambua na dunia itajua nini kimekuwa kikiendelea shinyanga mjini. Pongezi kwa chama kwa kufanya mabadiliko hivi karibuni, dhambi na uovu ulifunikwa na uongo unatoweka kwa uwezo wa Allah na Mungu wa mbinguni anasikiliza na kupokea maombi yenu, nawaambieni tutashinda vita, tutavuka pamoja. 


Namalizia kwa kusema msije hata siku moja mkakisaliti chama, kipiganieni chama kwa nguvu zenu zote, kilindeni chama kwa nguvu zenu zote, bila chama wote hatuna heshima tulizonazo.


Msaidieni kusema mambo mazuri anayoyafanya Rais wetu mpendwa mama Samia Suluhu Hassan, ana roho nzuri sana na upendo wa dhati kwa taifa lake, ni zawadi ya kipekee toka kwa Mungu, Muombeeni kwa Mungu ampe afya njema na maisha marefu na atuongoze vizuri zaidi. 


Nawaombea Mwenyezi Mungu awatunze ninyi na familia zenu. Nawapenda sana. 


Asanteni sana kwa salamu za kunitakia kheri ya siku yangu ya kuzaliwa. 


Wenu mtiifu, 

SM.



Share:

RAIS SAMIA AONGOZA KIKAO MAALUM CHA KAMATI KUU YA HALMASHAURI KUU YA CCM YA TAIFA JIJINI DAR LEO


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger