Thursday 30 March 2023

Wimbo Mpya : NTEMI OMABALA - OBHUKWINGWA

 

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI MACHI 30,2023





















Share:

Wednesday 29 March 2023

MERIDIANBET INARUDISHA DAU LAKO MPAKA X100 UKICHANA MKEKA


Sub-Heading: Pata mizunguko 50 ya bure kucheza sloti na michezo ya kasino ya mtandaoni ukijisajili na Meridianbet. Jisajili kupitia link hii.

Waswahili waliwahi kusema ukiona moshi ujue kuna shughuli na shughuli ni wat una watu wenyewe ni wewe, usemi huu una maana kubwa sana Meridianbet nyumba ya Odds kubwa, wamekuja na OFA Kabambe kwaajili yako unayechana mkeka/tiketi kila kukicha.

Habari njema zikufikie popote ulipo mdau wa kubashiri na Meridianbet kwakuwa unapata odds kubwa, machaguo Zaidi ya 1000+ na Ofa za kumwanga, kuna hii nyingine ya kijanja Zaidi unaambiwaje usijali endapo mkeka wako utachanika kwa timu moja, kwao Meridianbet mkeka bado umeshinda kwa sababu wanakurudishia mara 100 ya dau lako uliloweka.

Nifanyeje Nirudishiwe Hela Zangu?

Kitu unachopaswa kufanya ni kuhakikisha umebashiri tiketi yenye odds kubwa kuanzia 25+ hadi 950+ utarejeshewa mara 100 ya dau lako endapo ikatokea timu moja imechana mkeka wako.


Mchanganuo Uko hivi!



Zingatia:



Ø Tiketi haitakiwi kuwa na bashiri ya mechi moja tu

Ø Unatakiwa uwe na angalau bashiri moja kutoka bashiri za kabla ya mechi.

Ø Haitakiwa kuweka machaguo mengi (Mult-bet) kutoka mechi moja

Ø Hii ni maalumu kwa tiketi zilizopoteza mechi moja na dau la bonasi halihusiki kwenye promosheni hii.

Ø Kupata jumla ya ushindi zidisha jumlaya odds zilizoshinda pekee (Odds za bonasi hazihesabiwi) kisha zidisha kwa namba zilizoainishwa kwenye jedwali hapo kulingana na idadi ya mechi kwenye tiketi yako.

Ø Hesabu za Odds kubwa zilizoshinda hazihusishi ongezeko la odds za bonasi.
Share:

WAZIRI MABULA AWATAKA WAKURUGENZI KULINDA NA KUSIMAMIA UVAMIZI WA MAENEO YA WAZI


WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk.Angeline Mabula,akizungumza wakati akifungua Mkutano wa nane wa mwaka wa Bodi ya Usajili wa Wataalam wa Mipango Miji ulioanza leo Machi 29 hadi 30,2023 jijini Dodoma.


WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk.Angeline Mabula,akisisitiza jambo wa washiriki wa Mkutano wa nane wa mwaka wa Bodi ya Usajili wa Wataalam wa Mipango Miji ulioanza leo Machi 29 hadi 30,2023 jijini Dodoma.


KATIBU Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhandisi Anthony Sanga ,akizungumza wakati wa Mkutano wa nane wa mwaka wa Bodi ya Usajili wa Wataalam wa Mipango Miji ulioanza leo Machi 29 hadi 30,2023 jijini Dodoma.


MKUU wa Mkoa wa Dodoma Bi.Rosemary Senyamule,akitoa salama za Mkoa wake ka washiriki wa Mkutano wa nane wa mwaka wa Bodi ya Usajili wa Wataalam wa Mipango Miji ulioanza leo Machi 29 hadi 30,2023 jijini Dodoma.


Rais wa Chama Cha Wataalam wa Mipangomiji Tanzania, Dk.Juma Matindana,akizungumza wakati wa Mkutano wa nane wa mwaka wa Bodi ya Usajili wa Wataalam wa Mipango Miji ulioanza leo Machi 29 hadi 30,2023 jijini Dodoma.


MWENYEKITI wa Bodi ya Usajili wa Wataalam wa Mipango Miji Prof.John Lupala,akielezea lengo la Mkutano wa nane wa mwaka wa Bodi ya Usajili wa Wataalam wa Mipango Miji ulioanza leo Machi 29 hadi 30,2023 jijini Dodoma.


MSAJILI wa Bodi ya Usajili wa Watalaam wa Mipangomiji, Lucas Mwaisaka,akitoa taarifa ya Mkutano wa nane wa mwaka wa Bodi ya Usajili wa Wataalam wa Mipango Miji ulioanza leo Machi 29 hadi 30,2023 jijini Dodoma.


SEHEMU ya Washiriki wakisikiliza hotuba ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk.Angeline Mabula (hayupo pichani) wakati akifungua Mkutano wa nane wa mwaka wa Bodi ya Usajili wa Wataalam wa Mipango Miji ulioanza leo Machi 29 hadi 30,2023 jijini Dodoma.


MAKAMU Mwenyekiti wa Bodi Bi.Immakulata Senje,akitoa neno la shukrani kwa niaba ya washiriki mara baada ya Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk.Angeline Mabula,(hayupo pichani) kufungua Mkutano wa nane wa mwaka wa Bodi ya Usajili wa Wataalam wa Mipango Miji ulioanza leo Machi 29 hadi 30,2023 jijini Dodoma.


WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk.Angeline Mabula,akitoa tuzo kwa mshiriki mmoja aliyefanya vizuri mara baada ya kufungua Mkutano wa nane wa mwaka wa Bodi ya Usajili wa Wataalam wa Mipango Miji ulioanza leo Machi 29 hadi 30,2023 jijini Dodoma.

Na.Alex Sonna-DODOMA

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Dk.Angeline Mabula ,amewaagiza Wakurugenzi wa Mamlaka za Serikali za mitaa kupima, kulinda na kusimamia maeneo yote ya umma na maeneo ya wazi ili kuondokana na mwenendo mbaya unaoendelea kukithiri wa kuvamia maeneo hayo.

Agizo hilo amelitoa leo Machi 29,2023 jijini Dodoma wakati akifungua Mkutano wa nane wa mwaka wa Bodi ya Usajili wa Wataalam wa Mipango Miji.

Dk.Mabula amesema Wakurugenzi hao wanapaswa kulinda maeneo hayo ili kuondokana na mwenendo mbaya unaoendelea kukithiri wa kuvamia maeneo hayo.

“Umejitokeza utaratibu mbaya na usiovumilika, wa kuvamia maeneo ya wazi, maeneo ya umma pamoja na maeneo hatarishi na kuyabadilisha kuwa ya matumizi mengine, hasa makazi, maeneo hatari kimazingira pamoja na maeneo ya wazi, yakiwemo maeneo maalum kwa matumizi ya baadaye yanapaswa kupimwa, kumilikishwa na kulindwa dhidi ya wavamizi,”amesema Dk.Mabula

Amesema kuwa ili tuwe na mijini nadhifu na iliyopangwa vyema katika nchi yetu hakuna budi kuanza kusimamia upangaji wa miji midogo na vitovu vya vijiji.

"Takwimu za Sensa ya Watu na Makazi 2022 inaonyesha kuwa miji inakuwa kwa asilimia 4.8 na taarifa tulizonazo tuna jumla ya miji midogo inayochipukia 4310 nchini ambayo isiposimamiwa ipasavyo itakuwa miji holela ya baadae," Amesema

Na kuongeza"Kwa kutambua umuhimu wa miji hiyo na uwepo wa kasi ndogo ya upangaji wa vijiji nchini, Wizara imeandaa mwongozo wa upangaji na ujenzi wa nyumba bora vijijini ili kuwezesha jamii yetu kuanza kupanga maeneo yao kuanzia vijijini," amesema waziri Mabula

Aidha ametoa maelekezo kwa Bodi ya Usajili wataalam wa Mipangomiji na wanataaluma wote kuweka mkazo Zaidi katika namna ya kuzuia miji yetu midogo na vijiji kuwa makazi holela yabaadae kwa kusimamia na kuelimisha jamii matumizi ya mwongozo wa upangaji na ujenzi wa nyumba bora vijijini.

Hata hivyo amesema Pia Serikali itaendelea na jukumu lake la kuimarisha mahusiano ya kitaasisi ili kuimarisha maendeleo ya miji pamoja na kupata fedha kwa ajili ya kupanga na kusimamia miji.

''Naelekeza kuwa gharama za kuweza kumudu kupanga, kupima na kumilikisha maeneo yote nchini ni kubwa,Ninaelekeza Mamlaka za Upangaji nchini kutenga fedha kutokana na mapato ya ndani ya kila mwaka, kwa ajili ya kazi ya kupanga,kupima, kumilikisha,kuendeleza na kusimamia miji katika maeneo yao.''amesisitiza Waziri Mabula

Kwa upande wake Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mhandisi Anthony Sanga,amesema kuwa sasa ni wakati wa kujikita kwenye TEHAMA ili kurahisisha wananchi kupata huduma kwa haraka na kuondokana na migogoro ya ardhi.

Awali, Msajili wa Bodi ya Usajili wa Watalaam wa Mipangomiji, Lucas Mwaisaka, amesema kuwa watalaam wa mipangomiji 508 wamesajiliwa huku kati yao 36 wamefutiwa usajili kwa kukiuka maadili ya taaluma hiyo.
Share:

PROF. MBARAWA- LIPENI KODI KWA WAKATI

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa akisisitiza jambo kwa Wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam, wakati alipozindua nyumba za makazi za watumishi wa umma zilizopo Magomeni Kota na Canadian Village
Msasani Peninsula -Masaki jijini Dar es Salaam.

Naibu Katibu Mkuu Ujenzi, Bw. Ludovick Nduhiye akizungumza na Wananchi wa Mkoa wa Dar es Salaam (hawapo pichani), wakati wa uzinduzi wa nyumba
za makazi za watumishi wa umma zilizopo Magomeni Kota na Canadian Village Msasani Peninsula -Masaki jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya Watumishi wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), wakimsikiliza Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa (hayupo pichani) wakati alipozindua nyumba za makazi za watumishi wa umma zilizopo
Magomeni Kota na Canadian Village Msasani Peninsula -Masaki jijini Dar es Salaam.

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa akifurahia jambo na Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Arch. Daud Kondoro mara ya kuzindua nyumba za makazi za watumishi wa umma zilizopo
Magomeni Kota na Canadian Village Msasani Peninsula -Masaki jijini Dar es Salaam.


Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa akimsikiliza Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), Arch. Daud Kondoro kuhusu ujenzi wa nyumba za makazi za watumishi wa umma zilizopo
Magomeni Kota na Kanadiani Village Msasani Peninsula -Masaki jijini Dar es Salaam, kabla ya Waziri huyo kuzindua nyumba hizo.


Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali na Taasisi za Ujenzi akikata utepe kuashiria uzinduzi wa wa nyumba za makazi za watumishi wa umma zilizopo Magomeni Kota na
Canadian Village Msasani Peninsula -Masaki jijini Dar es Salaam, kabla ya Waziri huyo kuzindua nyumba hizo.


Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa akitoa malekezo kwa Viongozi wa Wizara na Taasisi kabla ya kuzindua ujenzi wa nyumba za makazi za watumishi wa umma zilizopo Magomeni Kota na Canadian Village Msasani
Peninsula -Masaki jijini Dar es Salaam, kabla ya Waziri huyo kuzindua nyumba hizo.


Muonekano wa jengo la nyumba za Watumishi wa Umma ambalo limejengwa katika eneo la Magomeni Kota jijini Dar es Saalaam.

…………………………………..


Serikali itaendelea kuuwezesha Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kujenga nyumba za kisasa kwa ajili ya watumishi wa Umma na za kibishara ili kukabiliana na ongezeko la mahitaji ya nyumba yanayoongezeka siku kwa siku
nchini.

Akifungua Majengo kwa ajili ya makazi kwa watumishi wa Umma katika eneo la Magomeni Kota na Canadian Village Msasani Peninsula Masaki jijini Dar es Salaam Waziri wa Ujenzi na Uchkuzi Profesa Makame Mbarawa amesema nia ya Serikali ni kuhakikisha watumishi wake wanaishi katika makazi yaliyo bora na hivyo kuleta tija na ufanisi katika kazi za Umma.

“Lengo kuu la Serikali ni kuhakikisha watumishi wanapata makazi salama na ya kisasa yanayoendana na sayansi na teknolojia., hivyo TBA hakikisheni wapangaji wote watakaopata nafasi ya kuishi kwenye nyumba hizi wanalipa kodi kwa wakati’ amesema Waziri Prof. Mbarawa.

Prof. Mbarawa amesema Serikali inatambua umuhimu wa makazi bora kwa wananchi wake ambapo mahitaji ya nyumba bora yanakadiriwa kuwa zaidi ya nyumba milioni tatu kwa nchi nzima hivyo Serikali itaendeelea kujenga nyumba za ghorofa zitakazoweza kuhudumia watumishi wengi katika eneo dogo.

Waziri Prof Mbarawa amewtaka TBA kuhakikisha watakaopanga kwenye nyumba hizo wanazitunza kwa kuzingatia kanuni za usafi na matumizi bora ya nyumba ili zidumu kwa muda mrefu.

“Watakaoshindwa kulipa kodi kwa wakati watoeni muweke wengine tunataka nyumba hizi ziweze kukusanya fedha na fedha hizo hizo zitumike kujenga nyumba nyingine nyingi zaidi’ amesisitiza Waziri Prof. Mbarawa.

Naibu Katibu Mkuu wa Ujenzi, Bw. Ludovick Nduhiye amesema Wizara itaiwezsha TBA kwa kuipa fedha ili kutimiza malengo ya Serikali .

Kwa upande Wake Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miudombinu, Mhe Selemani Kakoso ameipongeza Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kwa namna inavyofanya kazi kwa ubora na ubunifu na kuitaka Wizara kuiwezesha TBA kukusanya madeni wanayodai watumishi mbalimbali ili kujiimarisha kiuchumi na kujenga miradi mingine.

“Mfumo mpya mliuoanzisha sasa wa kukusanya kodi ambao utamuwezesha mwenye nyumba kulipa kodi kwa wakati utasaidia kupata makusanyo kwa wakati na hivyo kutimiza malengo hivyo uendelezeni’ amesisitiza Mhe.
Kakoso. 

Mtendaji Mkuu wa TBA, Arch. Daud Kondoro amesema ujenzi wa nyumba za kisasa katika maeneo ya Magomeni kota na Canadian village jijijini Dar es Salaam ni mwendelezo wa Wakala huo kujenga nyumba za watumishi katika maeneo mbalimbali nchini ambapo miradi kama hiyo inaendelea katika eneo la Nzuguni-Dodoma, Mtwara, Shinyanga, Kilimanjaro na Kagera lengo likiwa kukabiliana na upungufu wa nyumba bora kwa watumishi wa umma.

Zaidi ya Shilingi bilioni kumi zimetumika katika ujenzi wa miradi miwili ya Magomeni Kota na Canadian Village na nyumba hizo zina uwezo wa kuhudumia familia 28 kwa wakati mmoja.
Share:

GGML, STAMICO WASAINI MKATABA WA SH BILIONI 55.2 KUCHORONGA MIAMBA


Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML), Elder Damon (kushoto) akisaini mkataba kati ya kampuni hiyo na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) wenye thamani ya Sh bilioni 55.2 kwa lengo la kuendeleza shughuli za uchorongaji miamba kwenye migodi ya kampuni hiyo. Kulia na Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO, Dk. Venance Mwasse.


Na Mwandishi wetu

KAMPUNI ya Geita Gold Mining Limited (GGML) na Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), imesaini mkataba wa miaka miwili wenye thamani ya Sh bilioni 55.2 kwa lengo la kulipatia shirika hilo kandarasi ya kuchoronga miamba ndani ya mgodi wa GGML.


Akizungumza katika hafla fupi ya kutia saini makubaliano hayo jana mjini Geita, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa GGML, Elder Damon alisema kuwa tangu kuanzishwa kwa kanuni za ushirikishaji wazawa kwenye shughuli za uchimbaji madini mwaka 2018, idadi ya wafanyabiashara watanzania waliofanikiwa kushinda kandarasi mbalimbali ndani ya mgodi huo, imeongezeka.


"Nia yetu imekuwa kusaidia jamii kwa kuwapa ujuzi ili kuwawezesha kushindana kikamilifu. STAMICO imekuwa ikitoa huduma za uchorongaji miamba ndani ya GGML, kusaidia programu za uchimbaji wa wazi tangu Septemba 2020.


“STAMICO imetoa huduma za uchorongaji miamba kwa viwango vya juu kwa kuzingatia usalama na ufanisi katika sekta ya uchimbaji madini kulingana na malengo ya sekta hii. Makubaliano haya na STAMICO yanaonyesha uungaji mkono unaoendelea katika ukuzaji wa ujuzi na utaalamu kuhusu uchorongaji miamba na utafiti wa madini nchini,” alisema Damon.


Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa STAMICO, Dk. Venance Mwasse aliipongeza GGML kwa imani waliyoionesha kwao tangu walipoanza kufanya kazi mwaka 2020.


“Tunapenda kuwahakikishia GGML na Serikali kuwa kazi yetu itatekelezwa kwa ubora na viwango vya juu,” alisema Dkt. Mwasse.

Mgeni rasmi aliyehudhuria hafla ya utiaji saini, Waziri wa Madini, Dk. Doto Biteko alisema kuwa hali ya STAMICO imebadilika na kuwa bora zaidi tangu mkataba wao wa awali na Geita Gold Mining Limited ulipoanza.


“Tangu 2020 STAMICO iliposaini mkataba wake wa kwanza na GGML, mambo yameboreshwa ndani ya Shirika. STAMICO imefanya vizuri sana kwa kuzingatia ubora na ufanisi wa kazi jambo ambalo wengi wetu tunajivunia.

“STAMICO imeiwakilisha vizuri nchi yetu ndiyo maana wawekezaji wengi kama GGML bado wana imani ya kufanya nao kazi,” alisema Dkt. Biteko.

Aidha, Dkt. Biteko alizitaka kampuni nyingine za ndani kunufaika na zabuni za nje kila zinapotangazwa kwa sababu kanuni za sheria hiyo ya madini ya mwaka 2017 zinatoa nafasi kwa watanzania kuchangamkia fursa zinazojitokeza kwenye sekta ya madini.

Share:

TBS YAADHIMISHA SIKU YA VIWANGO BARANI AFRIKA



WAFANYABIASHARA wadogo na wa kati wanakabiliwa na changamoto kadhaa,zikiwemo mitaji midogo, teknolojia duni, elimu ndogo ya masuala ya ujasiriamali, elimu ndogo kuhusiana masuala ya ubora na usalama na pia kukosekana kwa masoko ya uhakika ambapo kwa kiasi kikubwa huwadumaza. 

Ameyasema hayo jana Machi 28,2023 Mkuu wa Wilaya ya Mbeya Mhe.Beno Malisa kwa niaba ya mkuu wa Mkoa wa Mbeya katika Maadhimisho ya Siku ya Viwango Afrika, yaliyofanyika katika ukumbi wa Beaco, Jijini Mbeya. 

Amesema kuwa ni ukweli usiopingika kwamba wajasiriamali wadogo na wa kati wanapokuwa katika mazingira ya changamoto mbalimbali hawawezi kuchangia ipasavyo katika maendeleo, kutokomeza umaskini na kukuza viwanda na uchumi wa Taifa kwa ujumla. 

"Ni wazi kuwa wakiendelezwa na kuondolewa changamoto zinazowakabili watachangia kwa kiasi kikubwa katika mipango ya Taifa ya kuondoa umaskini, kujenga ustawi wa jamii na kukuza uchumi". Amesema 

Pamoja na hayo amesema wajasiriamali wadogo na wa kati hawawezi kufikia malengo yao iwapo watapuuza masuala ya ubora na usalama katika uzalishaji wao. 

Amesema kwa mujibu wa takwimu za Chama cha Wafanyabiashara, Wenye Viwanda na Wakulima Tanzania (TCCIA), asilimia 95 ya biashara zinazofanyika nchini ni biashara za wajasiriamali wadogo na wa kati, ambazo huchangia takriban asilimia 35 ya Pato la Taifa (GDP) na kuzalisha hadi asilimia 40 ya ajira. 

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Uandaaji Viwango (TBS), Bw.David Ndibalema amesema mbali na mafunzo na elimu ambayo hutolewa mara kwa mara kwa wajasiriamali wadogo, wa kati na umma kwa ujumla, Serikali hutenga fedha kila mwaka kwa ajili ya kuhudumia wajasiriamali wadogo na wa kati pale wanapoomba kuthibitisha ubora wa bidhaa zao. 

"Anachotakiwa kuwa nacho mjasiriamali huyu mdogo ni leseni ya biashara na barua ya utambulisho kutoka Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo (SIDO) ambapo TBS hupokea barua hiyo na kuendelea na taratibu zingine za uthibitishaji ubora". Amesema 

Amesema tangu kuanza kwa utaratibu huo, tumefanikiwa kuthibitisha ubora wa bidhaa za wajasiriamali 1,515 nchini kote na wengine wengi wako katika hatua mbalimbali za michakato ya kupata leseni ya kutumia alama ya ubora.
Share:

Tuesday 28 March 2023

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO MACHI 29,2023















Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger