Saturday 31 December 2022

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI DESEMBA 31,2022










Share:

Friday 30 December 2022

WAANDISHI WA HABARI SIMIYU WAMTUNUKU CHETI CHA HESHIMA MBUNGE NJALU


Klabu ya waandishi wa Habari Mkoa wa Simiyu (SMPC) kupitia mkutano wake Mkuu maalumu uliofanyika leo Desemba 30,2022 Mjini Bariadi, imemtunuku Cheti Cha heshima mbunge wa Jimbo la Itilima Mkoani humo Njalu Silanga (CCM) kutokana na mchango wake uliotukuka kwenye taasisi hiyo tangu kuanzishwa kwake mwaka 2012 mpaka sasa.


Kabla ya kumkabidhi Cheti hiyo cha heshima, Mwenyekiti wa Klabu hiyo Frank Kasamwa, amemtaja Mbunge huyo kama mdau mkubwa kwenye Klabu hiyo ndani ya Mkoa, kwani amekuwa msaada Mkubwa katika kuhakikisha Klabu na waandishi wa Habari wanafanya kazi katika mazingira mazuri.


Amesema kuwa Klabu pamoja na wanachama wake Kuna nyakati wamekuwa wakipitia kipindi kigumi, lakini mbunge huyo amekuwa pamoja nao wakati wote, huku akiwa mstari wa mbele katika kusaidia kutatua baadhi ya Changamoto ambazo zimekuwa zikiwakabili.


" Kama Klabu Mheshimiwa Mbunge, tunakushukuru sana, ndiyo maana Leo tumeona tukutunuku Cheti hiki Cha heshima kwa kutambua mchango wako Mkubwa kwetu, umekuwa kiongozi na mwasiasa wa kuingwa, umekuwa kiongozi mwenye msaada mkubwa kwa Klabu yetu, lakini pia kuwa msaada mkubwa kwa wanachama ambao wamekuwa wakipata matatizo mbalimbali" Amesema Kasamwa.


Kwa upande wake Mbunge huyo ambaye alikuwa mgeni rasmi kwenye mkutano huo, amewashukuru Viongozi, na wanachama wa SMPC kwa kutambua mchango wake, huku akihaidi kuendelea kuwa mtetezi wa waandishi wa Habari Mkoa wa Simiyu kila wakati.


Aidha Mbunge huyo amehaidi kuendelea kutatua Changamoto mbalimbali zilizopo kwenye Chama ikiwemo tatizo miradi ya kuendesha Klabu, huku akihaidi kuwa mlezi wa Klabu hiyo.
Share:

SERIKALI YATOA MWONGOZO KWA WANAFUNZI WANAOJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2023...HAKUNA UHAMISHO WA KUTWA KWENDA BWENI, PIA HAKUNA CHAGUO LA PILI




Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Prof. Riziki Shemdoe amesema hakutakua na uhamisho wa wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kwenye shule za kutwa kuhamia bweni.

Shemdoe ametoa agizo hilo Desemba 29, 2022 Dodoma katika kikao kazi cha kufanya tathmini ya usimamizi na uendeshaji wa elimu nchini kwa mwaka 2022 kwa Maafisa Elimu wa Mikoa.


Amesema, tangu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Mhe.Angellah Kairuki atoe taarifa ya kuwapangia shule wanafunzi wa kidato Cha kwanza mwaka 2023, Desemba 14, 2022 Ofisi ya Rais-TAMISEMI imekuwa ikipokea maombi kutoka kwa wazazi ama walezi ya kuomba watoto wao kuhamia kwenye shule za bweni kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za ugonjwa au matamanio ya wazazi au watoto.

Kutokana na hali hiyo, Profesa Shemdoe amesema hakutakuwa na uhamisho wa wanafunzi waliochaguliwa shule za kutwa kwenda kwenye shule za bweni kwani upangaji wa wanafunzi umefuata vigezo na taratibu zilizowekwa.

"OR-TAMISEMI inasisitiza kuwa hakuna uhamisho kutoka shule ya kutwa kwenda bweni kwasababu wale waliopangiwa bweni wamekidhi vigezo vya kuchaguliwa katika shule hizo."

" Na kwa wanafunzi wenye changamoto za kimazingira, mfano amehama makazi ya awali wawasilishe changamoto hizo kwa Makatibu Tawala wa Mkoa ili zitatuliwe, maana upangaji wa wanafunzi kwenye shule umezingatia ukaribu wa shule na makazi ya wanafunzi hivyo endapo wamehama awali kunaweza kutokea changamoto ya umbali.

Profesa Shemdoe amesema kupangiwa shule kwa wanafunzi kumezingatia viwango vya ufaulu, ushindani pamoja ukaribu wa shule na makazi.

Aidha, idadi ya wanafunzi waliopangiwa kwenye shule za bweni imezingatia viwango vya juu vya ufaulu na nafasi zilizokuwepo katika shule hizo ili kuepusha msongamano kwa wanafunzi darasani na mahali pakulala.

Endapo zitatokea nafasi za bweni zitakazohitajika kujazwa hapo baadae, maombi yatakayokuwa yamefikishwa Ofisi ya Rais-TAMISEMI makao makuu yatachambuliwa na kamati maalum ambayo itaangalia sifa za walioomba kuhamishiwa huko.

Aidha, Prof. Shemdoe ametoa wito kwa wazazi kuhakikisha wanafunzi wote waliochaguliwa wanaripoti shuleni kwa wakati na kwamba hakutakua na chaguo la pili la mwanafunzi.

" Kwa mwaka huu hakutakuwa na chaguo la pili la wanafunzi kwasababu fedha zilizotolewa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika sekta ya elimu zimetosha kuboresha miundombinu ya kuwachukua watoto wetu wote kwa intake(mkupuo) mmoja ."

" Tangu Rais aingie madarakani ameshatoa fedha zilizowezesha kujenga zaidi ya vyumba vya madarasa 20,000 ndani ya miaka miwili hatua ambayo imewaondolea adha watoto kwa kuanza masono kwa pamoja huku wazazi wakiwa hawajachangishwa kitu."
Share:

Thursday 29 December 2022

PELE AFARIKI DUNIA


Nyota wa zamani wa timu ya Taifa ya Brazili na klabu ya Santos FC, Edson Arantes do Nascimento maarufu kama Pele amefariki Dunia mara baada ya kusumbuliwa na saratani kwa muda mrefu mpaka kufikia kulazwa hospitali hivi karibuni.

Ripoti ya utabibu kabla ya Krismasi ilionyesha alihitaji uangalizi kwa ajili ya ugonjwa wa Moyo na Figo, na amekuwa akipambana na Saratani ya Utumbo tangu Septemba 2021

Pele ambaye alitajwa kama mchezaji bora wa karne ya 21, enzi za uchezaji wake alifanikiwa kushinda mataji matatu ya Kombe la Dunia akiwa na timu ya taifa ya Brazil.
Share:

BABA AKAMATWA TUHUMA ZA KUWAPACHIKA MIMBA MABINTI ZAKE WAWILI.... MKEWE ANAJUA KILA KITU

Polisi wa eneo Bunge la Kandara, Kaunti ya Murang'a nchini Kenya wanamshikilia mume pamoja na mkewe wenye watoto wanne wa kike baada ya mtoto wao kufichua kuwa baba yao amekuwa akiwabaka.


Mume huyo anasemekana kufanya vitendo hivyo vya kuogofya huku mkewe akifahamu kikamilifu matendo yake nyumbani kwao Gichengo-Muruka.

Kulingana na ripoti, mkewe alinaswa baada ya mmoja wa binti zake wanne kukiri kuwa alipachikwa mimba na babaake huku mama yake akijua.

Wakazi walisema kwamba msichana wa miaka 14 ambaye alikuwa amemaliza darasa lake la nane alikuwa amepachikwa mimba pamoja na dadaake.

Walisema baba huyo alijaribu mara kwa mara kulala na binti zake wote wanne katika matukio tofauti na wengine wawili waliokolewa tu na majirani baada ya kupiga mayowe.

Chanzo: Citizen Digital
Share:

KASI YA UKUAJI MAHUSIANO YA KIDIPLOMASIA NA UCHUMI KATI YA TANZANIA NA CHINA, DKT SAMIA ANASTAHILI PONGEZI


Tunapoelekea kufunga mwaka 2022, ubalozi unatoa shukrani za dhati kwa wadau mbalimbali kwa ushirikiano wao uliowezesha utekelezaji wa Majukumu ya Ubalozi. Katika Mwaka 2022 mambo mbalimbali yenye tija na manufaa kwa wananchi yamefanyika kufuatia mwongozo na maelekezo ya Mwanadiplomasia No 1 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan. Yafuatayo ni baadhi ya mambo yaliyofanyika:


MOSI
Tarehe 2-4 Novemba 2022 Ilifanyika Ziara ya Kihistoria ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dk Samia Suluhu Hassan-nchini China. Kupitia ziara hiyo Tanzania na China zilipandisha hadi ya mahusiano kuwa ya Kimkakati katika nyanja zote.


PILI
Kwa upande wa biashara, Mauzo ya bidhaa za Tanzania katika soko la China yaliongezeka kutoka Dola za Kimarekani Milioni 409 hadi kufikia Dola za Kimarekani Milioni 605.5. Inatarajiwa katika mwaka 2023 mauzo yataongezeka kwa asilimia 20 kutokana na Tanzania kufunguliwa soko jipya la bidhaa wakati wa ziara ya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan nchini China.


TATU
Wakulima na wafanyabiashara wa Tanzania wanaoshughulika na zao la Parachichi walifunguliwa soko jipya la China Mwezi Novemba 2022. Kuanzia msimo ujao wa 2023 mauzo ya parachichi katika soko la China yataanza.

NNE
Wavuvi wa Tanzania walifunguliwa soko Jipya la kuuza mabondo ya Samaki na samaki aina sangara nchini China Mwezi Novemba 2022. Inatarajiwa mwaka 2023 mauzo ya bidhaa za uvuvi yataongezeka.


TANO
Bidhaa za Tanzania zilizoongezewa thamani zilianza kuuzwa katika soko la China kupitia Mtandao Maarufu wa Biashara wa JD.COM wenye watumiaji milioni 600- Mei 2022.


SITA
Watanzania walianza kufanya shughuli za usafirishaji wa mizigo yao moja kwa moja kutoka Tanzania hadi China kwa kutumia Shirika la Ndege la Air Tanzania- Mei 2022. Inatarajiwa mwaka 2023 baada ya China kufunguka shughuli zitaongezeka.

SABA
Usafiri wa abiria wa ndege wa moja kwa moja kutoka Dar es Salaam hadi Guangzhou ulianza Mwezi Julai 2022. Kuanzia Mwezi Januari 2023 Wafanyabiashara,wanafunzi & watalii watanufaika na huduma hiyo baada ya hatua ya China kufungua mipaka na kuondoa masharti ya udhibiti wa UVIKO19


NANE
Kufuatia maelekezo ya Mhe Rais @SuluhuSamia Ubalozi Mdogo wa Tanzania katika jijini la Biashara la China- Guangzhou ulifunguliwa rasmi mwezi Mei 2022. Watanzania wameanza kupata huduma mbalimbali za kufanikisha shughuli zao za biashara na Ubalozi mdogo umeanza kufungua fursa mpya za masoko ya bidhaa.


TISA
Filamu ya Tanzania Royal Tour ilioneshwa katika Televisheni ya Hainan Mwezi Oktoba 2022 na kutizamwa na watu milioni 60. Aidha filamu hiyo iliyotafsiriwa kwa lugha ya kichina imeoneshwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii ya China ikiwemo Bilibili m.bilibili.com/video/BV1jB4y1…

KUMI
Wanafunzi wa kitanzania watanufaika kwa kupata shahada na stashahada kufuatia kusainiwa kwa Makubaliano Mwezi December 2022 kati ya Tasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), na Taasisi ya Chongqing Vocation Institute of Engineering (CQVIE) ya China ya kuendesha mafunzo ya pamoja


KUMI NA MOJA
Vijana wa kitanzania wataanza kunufaika na mafunzo ya ufundi kufuatia hatua ya ufunguzi rasmi wa Chuo cha Ufundi cha VETA mkoani Kagera kilichojengwa kwa msaada kutoka China na kuzinduliwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dk @SuluhuSamia Mwezi Oktoba 2022


KUMI NA MBILI
Watanzania 122 wamepata ufadhili (scholarships) wa masomo ya Elimu ya Juu katika Vyuo Vikuu nchini China katika fani mbalimbali. Mwaka 2023 watanzania wataendelea kupata fursa za masomo ikiwa ni sehemu ya matokeo ya ziara ya Mheshimiwa Rais @SuluhuSamia nchini China


KUMI NA TATU
Katika mwaka 2022 Wafanyabiashara wa Tanzania wamepatiwa elimu kwa umma kuhusu fursa za biashara zilizopo nchini China pamoja na ushauri juu ya hatua za kuchukua ili kuepuka kuangukia mikononi mwa wafanyabiashara wasio waaminifu.

KUMI NA NNE
Katika Mwaka 2022 Vipindi vya Elimu kwa Umma vilianzishwa ili kuwapa wananchi ufahamu juu ya fursa za upatikanaji wa teknolojia mbalimbali za bei nafuu kwa ajili ya uzalishaji/usindikaji wa malighafi zinazopatikana nchini




Share:

BAADA YA KUIKACHA YANGA , FEI TOTO KUMBE KAJIFICHA JKU...ANASWA AKIGONGA MECHI YA KIRAFIKI NA MLANDEGE



Kiungo wa Yanga Feisal Salum Abdallah (Fei toto) asubuhi ya leo Alhamis Disemba 29, 2022 ameichezea Timu yake ya zamani JKU kwenye mchezo wa Kirafiki dhidi ya Mlandege kwenye Uwanja wa Mao Zedong, Zanzibar ambapo JKU walifanikiwa kupata ushindi wa Mabao 4-2 .

Katika mchezo huo Fei alicheza dakika 45 za kipindi cha pili ambapo wakati anaingia Fei JKU walikuwa tayari wapo nyuma kwa Mabao 2-0, lakini baada ya kuingia wakafanikiwa kusawazisha Mabao hayo na kuongeza mengine mawili huku Fei akifunga moja kati ya Mabao hayo 4 na akiwa na msaada mkubwa wa kupatikana Mabao hayo.

Mwandishi wa Habari hii alifanya jitihada ya kuzungumza na Fei mara baada ya kumalizika mchezo huo lakini Fei aliomba kutozungumza chochote.


“Naomba nisiongee chochote, naomba sana, ikifika siku ya kuongea nitaongea “. Alisema Fei.

Si mara ya kwanza Fei kuonekana kucheza JKU kwani ndio Timu yake ya zamani aliyoondoka mwaka 2018 kabla ya kujiunga na Yanga.

Jumamosi ya Disemba 24, 2022 kupitia mitandao yake ya Kijamii Fei aliwaaga Wanayanga huku timu yake hiyo siku hiyo hiyo ikitoa taarifa yakuwa bado Fei ana mkataba na Yanga mpaka Mei 30, 2024.

Hivi karibuni ziliibuka taarifa ya kuwa Fei huenda akajiunga na Azam FC kutokana na dau nono aliloahidiwa ambapo yeye binafsi aliwahi kusema hachezi mpira kufurahisha Watu bali anacheza Soka kwa kuangalia wapi kuna maslahi.
Share:

JENERALI MSTAAFU GEORGE MWITA WAITARA AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA UWANJA WA GOFU 'SERENGETI NATIONAL PARK GOLF COURSE'

Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA) Jenerali (Mstaafu) George Mwita Waitara ameweka jiwe la msingi la ujenzi wa uwanja wa gofu ambao umebeba jina la SERENGETI NATIONAL PARK GOLF COURSE wa kipekee duniani katika eneo la Fort Ikoma Wilayani Serengeti Mkoa wa Mara.

Akizungumza katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi na uzinduzi wa kampuni ya uwekezaji ya TANAPA – Tanapa Investment Ltd, Waitara ambaye ni mtaalam na mbobevu katika mchezo huo alisema dhumuni kubwa la kuanzisha zao hili la utalii ni kuunga mkono juhudi za Serikali katika kuongeza idadi ya watalii kufikia milioni tano na mapato ya dola za kimarekani kufikia bilioni sita ifikapo mwaka 2025.

“Ni Dhahiri kwamba kutokana na umaarufu wa Hifadhi ya Taifa Serengeti tuna kila sababu ya kuamini kwamba zao hili jipya la utalii litakuwa kivutio kikubwa na chachu ya kuongeza mapato yatokanayo na utalii katika shirika letu na Taifa kwa ujumla”, alisema Waitara.

Akifafanua zaidi, Mwenyekiti wa Bodi hiyo alisema kwamba sehemu ya kwanza ya mradi huo imekamailika ambapo mashimo mawili na sehemu ya mazoezi (range) yamekamilika na kwamba mtandao wa mashimo mengine 16 pia umekamilika.

Aidha, Waitara ametoa wito kwa wawekezaji na wafanyabiashara ya utalii kutambua uwepo wa zao hili, kulitangaza na hatimaye kuleta wachezaji wa golf ambao pia watatalii katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu.

Akizungumza katika taarifa yake juu ya mradi huu, Kamishna wa Uhifadhi, William Mwakilma wa TANAPA amebainisha kuwa mradi huu unatekelezwa na kampuni ya Uwekezaji ya shirika TANAPA INVESTMENT LIMITED ambayo imeanzishwa kwa maelekezo ya Serikali ili kutekeleza shughuli mbalimbali za ujenzi ndani nan je ya Shirika.

“Kukamilika kwa mradi huu kunategemea kuwavutia wacheza golf zaidi ya 3,000 kwa mwaka kutoka ndani nan je na shirikila linatarajia kupata TZs bilioni 2 kwa mwaka.” Alisema Kamishna Mwakilema.

Akiwasilisha salamu za kihandisi, Mwenyekiti wa Bodi ya Usajili wa wahandisi (ERB), Mhandisi Wakili, Menye Manga aliahidi kufanya kazi kwa karibu na kampuni ya TANAPA Investment Ltd na kupongeza uanzishwaji wa kampuni hiyo ambayo ina wataalam wa kutosha na vifaa vya kutekeleza kazi mbalimbali za kihandisi.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha gofu nchini, Gilman Kasiga aliishukuru TANAPA na hasa Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini ya TANAPA kwa kuendeleza michezo nchini hususan mchezo huu wa gofu na kuahidi kuleta mashindano makubwa ya kimataifa katika kiwanja hicho kwani kinakidhi viwango vya kimataifa.

Ujenzi wa uwanja huu wa golf unatarajiwa kugharimu jumla ya shilling bilioni 7.5 mpaka kitakapokamilika.




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger