Friday 9 December 2022

DUCE YAADHIMISHA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA 

Wanafunzi wakiwa kwenye maandamano katika Kilele cha Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia yaliyofanyika katika Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) leo Desemba 8,2022

************************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

JAMII yatakiwa kushirikiana na wadau mbalimbali katika kuhakikisha inapinga masuala zima ya ukatili wa kijinsia kwani imekuwa ikikithiri kwa kiasi kikubwa kwenye jamii inayotuzunguka.

Akizungumza leo Desemba 8,2022 Jijini Dar es Salaam katika Kilele cha Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia Naibu Rasi (Utawala, Fedha na Mipango) Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) Dkt.Method Samwel wakati akimwakilisha Rasi wa Chuo hicho amesema katika maadhimisho hayo wamewashirikisha wanafunzi kikamilifu kutoa mafunzo miongoni mwao wenyewe juu ya ukatilli wa kijinsia na utoaji taarifa za ukatili.

Amesema wanaofanyiwa ukatili wamekuwa wagumu kutoa ushirikiano na kushindwa kuchukuliwa hatua kwa wale ambao wamefanya ukatili wakihofia kudharauriwa na jamii inayomzunguka.

Amesema mwaka 1993 Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa lilipitisha Azimio la kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake kupitia azimio namba 48/104, kuweka njia kuelekea kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na wasichana duniani kote.

"Mwaka huu, Duce kwa kushirikiana na UNESCO kupitia Mradi wake wa 03 Plus (Our Right, Our Lives, Our Future) tumeshirikiana katika kampeni hizi kikamilifu kwa kufanya shughuli mbalimbali zikiwa ni pamoja na kutoa mafunzo kwa wafanyakazi kuhusu ukatili wa kijinsia". Amesema

Pamoja na hayo amewapongeza UNESCO kupitia mradi wa 03 Plus kwa kuwashika mkono kwani nguvu yao imekuwa chachu katika utekelezaji wa kazi kama DUCE katika kupinga ukatili wa kijinsia.

Kwa upande wake Afisa Msaidizi kutoka UNESCO (Idara ya Elimu ya Afya kwa Ustawi) Bi. Catherine Amri amesema ni wajibu wao kushirikiana na Serikali kuondoa changamoto ambazo zinakuwa vikwazo kwa wanafunzi kufikia elimu ya juu.

Amesema wamekuwa wakishirikiana na Wizara ya Maendeleo ya Jamii kuhamasisha vijana kuhakikisha wanatoa taarifa za ukatili na kutumia madawati ya jinsia yaliyoanzishwa katika vyuo vya elimu ya juu na kati.

Naibu Rasi (Utawala, Fedha na Mipango) Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) Dkt.Method Samwel akizungumza katika Kilele cha Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia yaliyofanyika katika Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) Desemba 8,2022 Jijini Dar es Salaam

Afisa Msaidizi kutoka UNESCO (Idara ya Elimu ya Afya kwa Ustawi) Bi. Catherine Amri akizungumza katika Kilele cha Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia yaliyofanyika katika Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) Desemba 8,2022 Jijini Dar es Salaam Naibu Rasi (Utawala, Fedha na Mipango) Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) Dkt.Method Samwel (katikati) akipata picha ya pamoja na wadau mbalimbali katika Kilele cha Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia yaliyofanyika katika Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) Desemba 8,2022 Jijini Dar es Salaam Naibu Rasi (Utawala, Fedha na Mipango) Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) Dkt.Method Samwel (katikati) akipata picha ya pamoja na wadau mbalimbali katika Kilele cha Maadhimisho ya Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia yaliyofanyika katika Chuo Kishiriki cha Elimu Dar es Salaam (DUCE) Desemba 8,2022 Jijini Dar es Salaam

Share:

TBS YAKABIDHI LESENI 246 KWA WAZALISHAJI WA BIDHAA NCHINI

Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt.Athuman Ngenya akikabidhi leseni na vyeti kwa wazalishaji wa bidhaa nchini katika wa hafla ya utoaji leseni na vyeti vya ubora kwa wazalishaji ambao bidhaa zao zimethibitishwa kukidhi matakwa ya Viwango kwa kipindi cha kuanzia mwezi Aprili hadi Septemba 2022. Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt.Athuman Ngenya akikabidhi leseni na vyeti kwa wazalishaji wa bidhaa nchini katika wa hafla ya utoaji leseni na vyeti vya ubora kwa wazalishaji ambao bidhaa zao zimethibitishwa kukidhi matakwa ya Viwango kwa kipindi cha kuanzia mwezi Aprili hadi Septemba 2022. Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt.Athuman Ngenya akizungumza katika wa hafla ya utoaji leseni na vyeti vya ubora kwa wazalishaji ambao bidhaa zao zimethibitishwa kukidhi matakwa ya Viwango kwa kipindi cha kuanzia mwezi Aprili hadi Septemba 2022.Mkurugenzi wa Udhibiti Ubora TBS, Bw.Lazaro Msasalaga akizungumza katika wa hafla ya utoaji leseni na vyeti vya ubora kwa wazalishaji ambao bidhaa zao zimethibitishwa kukidhi matakwa ya Viwango kwa kipindi cha kuanzia mwezi Aprili hadi Septemba 2022. Baadhi ya wazalishaji wa bidhaa wakiwa katika wa hafla ya utoaji leseni na vyeti vya ubora kwa wazalishaji ambao bidhaa zao zimethibitishwa kukidhi matakwa ya Viwango kwa kipindi cha kuanzia mwezi Aprili hadi Septemba 2022.

************************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS), limekabidhi leseni 246 kwa wazalishaji wa bidhaa nchini na vyeti vya ubora wa mifumo (system certification) vilivyotolewa ni vitatu, huku leseni zilizoongezewa bidhaa (Licence extension) ni 35.

Ameyasema hayo leo Desemba 8,2022 Mkurugenzi Mkuu wa TBS, Dkt.Athuman Ngenya wakati wa hafla ya utoaji leseni na vyeti vya ubora kwa wazalishaji ambao bidhaa zao zimethibitishwa kukidhi matakwa ya Viwango kwa kipindi cha kuanzia mwezi Aprili hadi Septemba 2022.

Aidha amesema leseni na vyeti 128 ambayo ni sawa na asilimia 52 vilitolewa kwa wajasiriamali wadogo. Vyeti na leseni hizo ni za bidhaa za vyakula, vipodozi, vifaa vya ujenzi, vilainishi, vitakasa mikono, vifaa vya umeme, vifaa vya makenika, magodoro, vibebeo pamoja na vifungashio.

"Leseni na vyeti vilivyotolewa leo vitazisaidia bidhaa zilizothibitishwa kuongeza imani kwa umma juu ya ubora wa bidhaa iliyothibitishwa, zitakubalika sokoni, zitapata faida ya kiushindani (competitive advantage) na kuingia na kuuzwa katika soko la la Afrika Mashariki pasipo kufanyiwa vipimo". Amesema Dkt.Ngenya.

Hata hivyo amesema kwa kipindi cha kuanzia mwezi Aprili mpaka Septemba 2022 wamekwisha sajili majengo 5,228 ya biashara na ya kuhifadhia bidhaa za vyakula na vipodozi na katika kipindi hicho wameweza kusajili bidhaa 906 za vyakula na vipodozi

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA DESEMBA 9,2022





































Share:

Thursday 8 December 2022

JICA, TANZANIA WAJIVUNIA MAFANIKIO LUKUKI MIAKA 60 YA USHIRIKIANO


Mwakilishi Mwandamizi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA,) Watanabe Hideki (wa tatu kushoto,) akipata maelezo ya mtambo unaopooza na kusambaza umeme katika Hospitali ya Taifa Mhimbili kutoka kwa Mhandisi wa Idara ya Usafirishaji umeme Gwamaka Thobias (Kulia,) walipotembelea mradi huo.
Mwakilishi Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan Nchini (JICA,) Naofumi Yamamura akizungumza na waandishi wa habari wakati akifungua semina hiyo na kueleza kuwa miaka 60 ya ushirikiano baina ya Tanzania na JICA wataendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya kijamii na uchumi pamoja na kubadilishana ujuzi, Leo jijini Dar es Salaam.
Mwakilishi Mwandamizi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA,) Wanatabe Hideki akizungumza na waandishi wa habari wakati wa semina hiyo na kueleza kuwa bidhaa za Tanzania zinazokubalika katika soko la Japan ni pamoja na kahawa ya Tanzania, korosho na bidhaa za kilimo.Mshauri wa JICA Raymond Msofe akiendesha semina hiyoo.


*Kahawa ya ‘Kilimanjaro coffee’ korosho na bidhaa za kilimo kutoka Tanzania zatajwa kukubalika soko la Japan

*Watanzania 22,064 wanufaika kupitia JICA

MIAKA 60 ya ushirikiano baina ya Serikali na Tanzania na Japan kupitia Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA,) imekuwa ya mafanikio makubwa hasa kwa JICA kuendelea kukua na kujitanua zaidi katika kusaidia katika kutoa misaada na kutekeleza miradi mbalimbali ya kijamii na uchumi nchini kwa kushirikiana na Serikali kwa kufuata vipaumbele vya watanzania.

Hayo yameelezwa leo na Mwakilishi Mkuu wa wa JICA nchini Naofumi Yamamura wakati wa semina maalum kwa waandishi wa habari pamoja na ziara ya kutembelea baadhi ya miradi iliyofadhiliwa na JICA uki wemo mradi wa kituo cha kupooza umeme kilichopo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili pamoja na mradi wa daraja la juu ‘Mfugale Flyover’ lililopo Tazara jijini Dar es Salaam.

Amesema mahusiano baina ya Tanzania na Japan na Tanzania yalianza 1962 mara baada ya Uhuru wa Tanganyika na wataendelea kushiriki na kufadhili miradi mengi Tanzania Bara na Visiwani Zanzibar kwa manufaa ya nchi hizo mbili ambapo watanzania 22,064 wamenufaika na programu za mafunzo zilizodhaminiwa na Serikali ya Japan huku Wajapan 1,679 wameshiriki program hizo za mafunzo na kunufaika na mambo mengi kutoka Tanzania ikiwemo utamaduni na lugha ya Kiswahili.

Aidha ameeleza ushirikiano huu uliudumu kwa miaka 60 na kutekeleza miradi mbalimbali Tanzania ikiwemo mradi wa ujenzi wa daraja la Salender 1980 utaendelea kudumu kwa manufaa ya watanzania.

Kwa upande wake Mwakilishi Mwandamizi wa (JICA,) Watanabe Hideki ameeleza kuwa kwa miaka 60 Serikali ya Japan kupitia JICA wameendelea kukuwa na kutekeleza miradi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi kwa kushirikiana na Serikali ya Tanzania kupitia vipaumbele vya watanzania, huku Japan ikinufaika na mengi kutoka Tanzania ikiwemo kahawa ya Kilimanjaro Coffee, korosho na bidhaa za kilimo ambazo zinakubalika sana katika soko la Japan.


Amesema, kuanzia awamu ya kwanza ya uongozi wa Hayati. Julius K. Nyerere hadi katika awamu hii ya sita JICA inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imekuwa ikifadhili miradi mbalimbali ya kijamii na maendeleo ikiwemo miradi ya ujenzi wa soko la samaki ‘Malindi Fish Market’ Zanzibar, ujenzi wa daraja la juu Gerezani, Dar es Salaam, ujenzi wa barabara mpya ya Bagamoyo ‘New Bagamoyo road’ Dar es Salaam sambamba na mradi mpya wa kuhimiza ujasiriamali na uvumbuzi kupitia Japan Project ‘NINJA na mradi wa kuhimiza usawa wa kijinsia ‘Ladies First’ mradi utakaoshirikisha sekta binafsi pamoja na mafunzo kupitia elimu na kubadilishana teknolojia.

Katika mradi wa kituo cha kupooza na kusambaza umeme kilichopo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili Mhandisi mwandamizi wa Idara ya Usafirishaji Umeme wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO,) Kanda ya Mashariki Gwamaka Thobias amesema, kituo hicho kilichozinduliwa mwaka 2017 kwa ufadhili wa JICA kimekuwa msaada mkubwa katika uendeshaji wa hospitali hiyo kutokana na uhakika wa nishati ya umeme kwa muda wote.

‘’Taasisi nne zinanufaika na umeme kutoka katika kituo hiki ikiwemo Taasisi ya Moyo (JKCI,) Taasisi ya Mifupa (MOI,) Muhimbili pamoja na Chuo….nishati ni ya uhakika inafika moja kwa moja na kupoozwa katika kituo hiki na upatikanaji wa nishati ni wa uhakika na muda wote.’’ Amesema.

Mhandisi Gwamaka amesema JICA imesaidia kwa kiasi kikubwa katika eneo hilo nyeti ambayo nishati haikuwa ya uhakika kutokana na umbali na miundombinu kupita katika eneo la Jangwani ambalo limekuwa likikumbwa na mafuriko.

Katika mradi wa barabara ya juu ya Mfugale ‘Mfugale Flyover’ ambayo ni Flyover ya kwanza kujengwa Tanzania mhandisi kutoka TANROAD Elisony Mweladzi amesema mradi huo uliojengwa kwa ufadhili wa JICA na kukamilika 2018 umeongeza ufanisi wa hali ya juu katika usafiri hasa wa abiria wanaotoka mjini na kuelekea uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere na maeneo ya Gongolamboto.

‘’Mradi huu umeongeza ufanisi mkubwa katika sekta ya usafiri, watu wanawahi Air port, na makazini ….kabla ya daraja hili magari yapatayo 21,557 yalikuwa yanapita kwa siku lakini baada ya mradi huu kwa takwimu za Novemba mwaka huu magari 39,300 yanapita katika daraja hili ikiwa ni ongezeko la asilimia 45.4.’’ Amesema.

Mhandisi Mweladzi ameishukuru JICA kwa ufadhili wa mradi huo na kueleza kuwa TANROAD inaona fahari kuwa na daraja hilo la juu la kwanza na la mfano Tanzania na kueleza kuwa kuna uhitaji wa madaraja nane zaidi katika maeneo mbalimbali ikiwemo eneo la Fire jijini Dar es Salaam.

JICA ni shirika la maendeleo la kimataifa la Japan linalosimamia miradi yote inayofadhiliwa na Serikali ya Japan Tanzania, ikiwa na ofisi zaidi ya 90 ulimwenguni kote JICA Tanzania inafadhili katika ushirikiano wa kiufundi, mikopo ya masharti nafuu pamoja na misaada mbalimbali.
Afisa kutoka JICA akiwasilisha mada katika semina hiyo.
Mwakilishi Mwandamizi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA,) Watanabe Hideki (wa tatu kushoto,) akipata maelezo ya mtambo unaopooza na kusambaza umeme katika Hospitali ya Taifa Mhimbili kutoka kwa Mhandisi wa Idara ya Usafirishaji umeme Gwamaka Thobias (Kulia,) walipotembelea mradi huo.
Share:

MBEBA MKAA ASABABISHA KIFO CHA WANANDOA


Uchunguzi wa awali kuhusu ajali iliyoondoa uhai wa wanandoa Tumaini John na Geofrey John mkoani Kagera unaonesha kuwa chanzo cha ajali hiyo ni dereva mmoja wa pikipiki aliyekuwa amepakia magunia ya mkaa kuisukuma pikipiki waliyokuwa wamepanda watu hao.

Aidha majirani wa wanandoa hao wameeleza kuwa wakati wanapata ajali hiyo mume alikuwa akimpeleka mke wake kazini kwa kutumia pikipiki baada ya gari lao kupata pancha.

"Waliofariki ni mume na mke, wameacha watoto watatu mkubwa wa kiume yupo kidato cha tatu na wa mwisho bado ni mdogo zaidi ananyonya", amesema Joachim Kahumbi ambaye ni jirani wa wanandoa hao.  

Chanzo - EATV
Share:

GGML YAONGOZA TUZO YA UWAJIBIKAJI BORA KWA JAMII

KAMPUNI ya Geita Gold Mining Ltd (GGML) imenyakua tuzo ya juu ya uwajibikaji wa Kampuni kwa Jamii katika Tuzo za Mwajiri Bora wa Mwaka zilizoandaliwa na Chama cha Waajiri Tanzania (ATE) wiki iliyopita.


Aidha, GGML ilipokea tuzo ya juu kwa miradi yake ya uwajibikaji kwa jamii na mshindi wa pili katika kipengele cha muajiri bora wa sekta binafsi.


Kampuni ya AngloGold Ashanti - Geita Gold Mining Limited inajivunia kwamba mafanikio haya yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na michango ya wafanyakazi wake, wakandarasi, uongozi, na kuendelea kuungwa mkono na kuongozwa vyema na serikali.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger