Tuesday 29 November 2022

BARAZA HURU LA USULUHISHI WA MALALAMIKO YA WANANCHI VIJIJI VINAVYOZUNGUKA MGODI WA MWADUI LAZINDULIWA


Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude akikata utepe wakati akizindua Taratibu za Baraza la Huru la Usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui kuhusu madhira mbalimbali waliyopata wananchi kwenye mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy kulia ni Simon Mutinda kutoka Kampuni ya Pricewaterhouse Coopers (PWC).

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui (Williamson Diamonds Limited) kwa njia ya maridhiano kuhusu madhira ,mbalimbali waliyopata wananchi kwenye mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu limezinduliwa rasmi mkoani Shinyanga

Uzinduzi wa Baraza la Malalamiko ya Wananchi pamoja na Utaratibu wake katika Mgodi wa Mwadui umezinduliwa leo Jumanne Novemba 29,2022 na Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Mkude amesema matarajio kupitia baraza hilo ni kuona kutenda haki kwa wananchi waliopata madhara kupitia mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu.


“Tunahitaji haki itendeke lakini pia kwa kuzingatia mambo yote tuliyoelezekana ngazi mbalimbali, tuoneshe uhalisia wa haki hizo zinazotolewa na kuwe na tija kwa walengwa wenyewe”,amesema Mkude.


Amesema mara baada ya uzinduzi huo Baraza hilo litaanza kusikiliza malalamiko yaliyowasilishwa na wananchi wa vijiji vinavyozunguka mgodi wa Mwadui.


“Utaratibu wa kuunda Baraza Huru la Usuluhishi wa malalamiko ya wananchi ulivyoandaliwa vizuri ukisimamiwa na kufadhiliwa na Petra Diamonds Ltd. Utaratibu wote uliotumika mpaka kufikia leo umekuwa wa wazi na tumekuwa tukieleweshwa ngazi moja hadi nyingine kwa kushirikisha taasisi mbalimbali kuhusu baraza hili la malalamiko na namna likatavyokwenda kufanya kazi”, ameongeza Mkude.

“Lakini nitumie nafasi hii kupongeza imeonekana kwamba Baraza hili likianza kazi kwa ujumla malalamiko yaliyosajiliwa na wananchi yapo 5575 na wameongeza muda wa kuyasikiliza badala ya miaka mitatu imeenda zaidi, hili ni jambo jema, jambo la kiutu ambalo litasaidia kuangalia kwa undani zaidi haki za watu ambazo wamewasilisha malalamiko yao”,ameeleza.


Mkuu huyo wa wilaya amesema serikali itaendelea kushirikiana Baraza hilo wakati wote na pale ambapo panatokea tatizo au viashiria vya shida au tatizo basi jopo zima lisisite kuwasiliana na uongozi ngazi ya mkoa na wilaya ili kutatua mapema matatizo yanayoweza kujitokeza kabla ya kuleta athari kubwa.

Kwa upande wake, Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy amesema wana imani Baraza la Huru la Usuluhishi wa malalamiko ya wananchi litafanya kazi kwa weledi mkubwa ili haki iweze kupatikana.

“Petra Diamonds Ltd tukiwa ni wamiliki wa Mgodi wa Mwadui tunatambua changamoto zilizokuwepo, tulifanya mabadiliko mbalimbali ikiwa ni sehemu ya kukidhi matakwa ya sheria za nchi na kimataifa”,amesema Duffy.

Mwenyekiti wa Jopo Huru la Usuluhishi wa Malalamiko ya Wananchi wanaozunguka mgodi wa Mwadui, Dkt. Rugemeleza Nshala amesema tangu mwaka 2009 hadi 2021 jumla ya malalamiko 5575 yamesajiliwa na usikilizwaji wa hatua ya awali unaanza mara moja kwa kuzingatia utaratibu uliowekwa.

“Kila mwananchi aliyesajili malalamiko yake na atayesajili malalamiko yake atafikiwa na Baraza hili kuhusu la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi”,amesema Dkt. Nshala.


Naye Mbunge wa Jimbo la Kishapu Mhe. Boniphace Butondo kuzinduliwa kwa Baraza Huru la Usuluhusihi wa malalamiko ya wananchi yanayotokana nan a shughuli za uzalishaji wa madini katika mgodi wa Mwadui unafungua Ukurasa mpya wa ushirikiano baina ya wananchi na mgodi.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Mhe. William Jijimya ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Rais Samia Suluhu kuruhusu kuundwa kwa Baraza hilo huku akilitaka Jopo Huru la Usuluhishi wa Malalamiko ya Wananchi kwenda kufanya kazi kwa weledi na kutenda haki.
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude akizungumza wakati akizindua Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui kuhusu madhira mbalimbali waliyopata wananchi kwenye mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu
kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Sophia Mjema leo Jumanne Novemba 29,2022 Mjini Shinyanga. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude akizungumza wakati akizindua Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui kuhusu madhira mbalimbali waliyopata wananchi kwenye mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui kuhusu madhira mbalimbali waliyopata wananchi kwenye mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu mkoani Shinyanga.
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui kuhusu madhira mbalimbali waliyopata wananchi kwenye mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu mkoani Shinyanga.
Mwenyekiti wa Jopo Huru la Usuluhishi wa Malalamiko ya wananchi wanaozunguka mgodi wa Mwadui, Dkt. Rugemeleza Nshala akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui.

Mwenyekiti wa Jopo Huru la Usuluhishi wa Malalamiko ya wananchi wanaozunguka mgodi wa Mwadui,Dkt. Rugemeleza Nshala akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui.
Simon Mutinda kutoka Kampuni ya Pricewaterhouse Coopers (PWC) akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui ambapo amesema jopo la usuluhishi litaenda kufanya kazi kwa weledi ili jamii ipate suluhisho la malalamiko yao kwa ajili ya kuleta maendeleo katika taifa.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Mhe. William Jijimya akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui
Mbunge wa Jimbo la Kishapu Mhe. Boniphace Butondo akizungumza wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui

Mkuu wa wilaya ya Kishapu Joseph Mkude (kulia) akikata utepe kuzindua Baraza huru la kushughulikia malalamiko ya wananchi ambao wanazunguka Mgodi wa Almasi Mwadui, (kushoto) ni Mtendaji Mkuu wa Kampuni ya Petra Diamond Limited Richard Duffy
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude  akikata utepe wakati akizindua Taratibu za Baraza la Huru la Usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji 12 vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui kuhusu madhira mbalimbali waliyopata wananchi kwenye mgodi wa Mwadui uliopo wilayani Kishapu.
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude akionesha Vitendea kazi vya Baraza Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi katika mgodi wa Mwadui
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude akimkabidhi Vitendea kazi vya baraza huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi katika mgodi wa Mwadui Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy (kushoto).
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy (kushoto) akimkabidhi Katibu Tawala wilaya ya Kishapu, Shadrack Kengese Vitendea kazi vya baraza huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi katika mgodi wa Mwadui
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy akimkabidhi Mbunge wa Jimbo la Kishapu, Boniphace Butondo, Vitendea kazi vya baraza huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi katika mgodi wa Mwadui
Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy akimkabidhi Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Mhe. William Jijimya  Vitendea kazi vya baraza huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi katika mgodi wa Mwadui
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited, inayomiliki Mgodi wa Almasi wa Mwadui, Richard Duffy (kushoto) wakikabidhi vitendea kazi kwa Mwenyekiti wa Jopo Huru la Usuluhishi wa Malalamiko ya wananchi wanaozunguka mgodi wa Mwadui, Dkt. Rugemeleza Nshala na Simon Mutinda kutoka Kampuni ya Pricewaterhouse Coopers (PWC).

Zoezi la makabidhiano ya Vitendea kazi vya baraza huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi katika mgodi wa Mwadui likiendelea
Zoezi la makabidhiano ya Vitendea kazi vya baraza huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi katika mgodi wa Mwadui likiendelea
Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui uliopo Kishapu

Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui uliopo Kishapu
Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui uliopo Kishapu
Wadau wakiwa kwenye uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui uliopo Kishapu
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited wakipiga picha na wadau mbalimbali wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui uliopo Kishapu
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Mhe. Joseph Modest Mkude na Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Petra Diamonds Limited wakipiga picha na wadau mbalimbali wakati wa uzinduzi wa Baraza la Huru la usuluhishi wa malalamiko ya wananchi wa vijiji vinavyozunguka Mgodi wa Almasi wa Mwadui uliopo Kishapu.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


Share:

UGANDA YAJA TANZANIA KUJIFUNZA USIMAMIZI WA HUDUMA ZA MAWASILIANO

Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Mhandisi Kundo Mathew (wa kwanza kushoto) akizungumza jambo na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Dkt. Jabiri Bakari (wa pili kulia) walipomkaribisha Waziri wa Nchi anaeshughulikia TEHAMA na Ulinzi-Uganda Mhe. Kabbyanga Godfrey (katikati) kwenye Ofisi za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA). Wa kwanza kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma-TCRA Bi. Lucy Mbogoro. Picha na TCRA)

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania Dkt Jabiri Bakari (kushoto) akiwa sambamba na Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Kundo Mathew (wa pili katikati) wakimkaribisha Waziri wa Nchi anaeshughulikia TEHAMA na Ulinzi-Uganda Mhe. Kabbyanga Godfrey aliefika TCRA kwa ziara ya mafunzo akiambatana na Maafisa Waandamizi wa Tume ya Mawasiliano Uganda(UCC) (hawamo pichani). Wa kwanza kulia anaeshuhudia ni Msaidizi wa Waziri wa Uganda. PICHA NA TCRA Naibu Waziri wa Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Mhandisi Kundo Mathew (kulia) akiperuzi jambo kwenye kijitabu wakati alipomkaribisha Mgeni wake Waziri wa Nchi anaeshughulikia TEHAMA na Ulinzi-Uganda Mhe. Kabbyanga Godfrey (anaesaini kitabu cha wageni kushoto) Waziri huyo wa Uganda alioongozana ujumbe wa maafisa wa Tume ya Mawasiliano Uganda (UCC) waliokuja Tanzania kwa ziara ya mafunzo ya usimamizi wa sekta ya Mawasiliano kupitia Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), ikiwa ni mkakati wa kuboresha Sheria ya Mawasiliano ya nchini kwao. Picha na TCRA)

Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kundo Mathew (kushoto), akimweleza jambo Waziri wa Nchi anaeshughulikia TEHAMA na Ulinzi-Uganda Mhe. Kabbyanga Godfrey aliefika Tanzania kwa ziara ya mafunzo. Katika tukio hili anakaribishwa kujifunza kutoka TCRA namna Sheria za Mawasiliano zinavyowezesha usimamizi wa Sekta ya mawasiliano nchini. PICHA NA TCRA

**************************

Na Mwandishi Wetu

Tanzania imeihakikishia Uganda kuwa itaendelea kuipa ushirikiano katika kujenga uwezo wa usimamizi wa sekta ya Mawasiliano na TEHAMA, sambamba na kudumisha ushirikiano wa kitaalam katika usimamizi wa sekta hizo.

Akizungumza wakati alipoukaribisha ujumbe wa Tume ya Mawasiliano Uganda (UCC) ukiongozwa na Waziri wa Nchi anaeshughulikia Ulinzi na TEHAMA Mheshimiwa Kabbyanga Godfrey uliofika katika Ofisi za Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kwa ziara ya Mafunzo na kubadilishana ujuzi, Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhandisi Kundo Andrew Mathew alibainisha kuwa, Tanzania imefanikiwa kusimamia vilivyo sekta ya Mawasiliano kwa kuweka Sera Madhubuti za usimamizi wa huduma za Mawasiliano, huku akiwahakikishia wageni fursa tele ya kujifunza katika sekta ya Mawasiliano.

“Tanzania imepitisha sera zinazounga mkono ukuaji wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano - TEHAMA na mfumo wa kisheria na udhibiti unaounga mkono ukuzaji wa uchumi wa kidijiti,” alisisitiza Kundo na kuongeza kuwa “Ninakuhakikishia ujumbe wako kwamba utapata fursa ya kujifunza na kubadilishana uzoefu ambao utakuwa muhimu katika marekebisho ya Sheria yenu ya Mawasiliano ya 2013,” alibainisha.

Kwa upande wake Waziri Kabbyanga akishukuru baada ya ukaribisho alimweleza Naibu Waziri Kundo, Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Dkt. Jabiri Bakari na Menejimenti ya TCRA lengo la ziara yao Tanzania kuwa ni kujifunza zaidi namna Tanzania inavyosimamia huduma za Mawasiliano ambao ziara yao mahususi katika ofisi za TCRA ililenga kujifunza namna Sheria, Kanuni na miongozo mbalimbali inavyowezesha usimamizi wa sekta ya Mawasiliano.

Akizungumza muda mfupi baada ya kuwasili kwenye ofisi za TCRA jijini Dar es salaam Waziri wa Nchi anaeshughulikia Ulinzi na TEHAMA Mheshimiwa Kabbyanga Godfrey alimweleza mgeni wake Naibu Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari wa Tanzania, Mheshimiwa Kundo Mathew kwamba Uganda imeona vema kuja kujifunza Tanzania kwa kuzingatia ujirani na namna ambavyo Tanzania imefanikiwa katika kusimamia na kudhibiti sekta ya Mawasiliano.

“Tumeambiwa kwamba Tanzania mnazo Sheria Madhubuti za usimamizi wa sekta ya mawasiliano Tumekuja hapa kwa sababu mazingira yetu ni sawa na ya Tanzania hivyo tumeona hapa kwenu tutajifunza na kupata maarifa yenye uhalisia zaidi, tofauti na tungeamua kwenda kujifunza sehemu nyingine,” alisisitiza Kabbyanga.

Alieleza kwamba pia Uganda inanuia kuboresha huduma za Mawasiliano ya simu kwa raia wake hivyo imeamua kuja Tanzania kujifunza katika eneo linalohusu Mawasiliano ya simu.

Ziara ya Tume ya Mawasiliano Uganda kuzuru Tanzania, na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania ni mwendelezo wa Mamlaka mbalimbali za Usimamizi wa Mawasiliano za Afrika kufika Tanzania kujifunza na kubadilishana ujuzi wa usimamizi wa huduma za Mawasiliano. Miongoni mwa nchi nyingine zilizozuru TCRA mwaka huu ni pamoja na Malawi, Zimbabwe, Burundi, Rwanda, Uganda, na Msumbiji.
Share:

Monday 28 November 2022

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE NOVEMBA 29,2022










Share:

WADAU WA NISHATI NCHINI WAKUTANA KUJADILI MPANGO WA MATUMIZI BORA YA NISHATI KWENYE MAJENGO



Shirika la Umoja la Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP) kwa kushirikiana na Wizara ya Nishati imeandaa warsha ya siku mbili ya wadau wa nishati kutoka Wizara ya Nishati, Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, EWURA, TANESCO, Baraza la Taifa la Ujenzi, na TAMISEMI yamefanyika Bagamoyo kuanzia 25-26 Novemba 2022 kujadili namna bora ya matumizi bora ya nishati nchini. 


Mradi huu wa Mpango wa Matumizi Bora ya Nishati Tanzania unafadhiliwa na Umoja wa Ulaya (EU) na kutekelezwa na Wizara ya Nishati kwa kushirikiana na Shirika la Umoja aa Mataifa la Mpango wa Maendeleo (UNDP).  
     
 
‘Mratibu wa mradi wa Mpango wa Matumizi Bora ya Nishati Tanzania, Bwana Aaron Cunningham alisema “warsha hii imekusudia kujadili majukumu ya washikadau katika kutekeleza na kuendeleza matumizi bora ya nishati katika majengo, kwa kushirikiana na Baraza la Ujenzi la Taifa tumekusudia kushirikiana na wizara ya ujenzi kuandaa mfumo wa matumizi bora ya nishati katika majengo makubwa. 


Aliongeza kwa kusema ‘mpango huu wa uundaji na uendelezaji wa majengo yenye kuzingatia matumizi bora ya nishati yatasaidia kupunguza matumizi yasiyosahihi ya nishati na kuokoa fedha pamoja na kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya Tabianchi.” – Aaron Cunningham, UNDP. 

Ripoti ya nishati Tanzania ya mwaka 2018 inaonyesha nishati kwa kiasi kikubwa inatumika kwenye majengo ya biashara, makazi ya watu na viwandani. Mpango kazi wa taifa wa nishati umetambua sekta ya majengo kama sekta muhimu kwenye kupunguza matumizi yasiyo sahihi ya nishati.  


Nae mkurugenzi wa huduma za kiufundi kutoka baraza la Taifa la Ujenzi, Mhandisi Moses Lawrence alisema ‘Wizara ya ujenzi na uchukuzi ipo kwenye mchakato wa kuandaa sheria ya ujenzi wa majengo (building act and building codes) ambapo itazingatia nishati bora na endelevu na hivyo kuwataka wadau kutoa michango ya mawazo ili kufanikisha mchakato huu.

 Mradi wa Mpango wa Matumizi Bora ya Nishati Tanzania unaotekelezwa na UNDP kwa kushirikiana na Wizara ya Nishati utangalia na kuzingatia namna bora ya kushirikiana na Baraza la Taifa la Ujenzi kufanikisha malengo haya.


Mhandisi Moses aliongeza kwa kusema uzingatiaji wa matumizi bora ya nishati kwenye majengo katika hatua za mwanzo za ujenzi ni wa gharama nafuu zaidi kuliko uboreshaji baada ya ujenzi. Kwa hiyo, maamuzi yaliyofanywa hatua za mwanzo za ujenzi wa jengo yataamua matumizi ya baada ya jengo kukamilika. – Eng. Moses Lawrence.


Ujenzi wa kuzingatia matumizi bora ya nishati utasaidia kubadilisha sekta ya ujenzi kuwa mazingira rafiki, gharama nafuu, na matumizi bora ya nishati. Kama matokeo ya muda mrefu, kanuni za ujenzi wenye kuzingatia matumizi bora ya nishati zitachangia lengo la 7 la Maendeleo Endelevu (SDGs) ambalo linahusu nishati safi na himilivu (Affordable and Clean Energy) kwa wote, na lengo la 13 linalohusu hatua za kuchukuwa kupambana na mabadiliko ya tabianchi (Climate Action) ambalo linalingana na vipaumbele vya maendeleo vya kitaifa.


Mpango wa matumizi bora ya nishati katika sekta ya ujenzi utasaidia juhudi za serikali za kutoa nishati ya kutosha na ya uhakika, hususani umeme, ili kukidhi ongezeko la mahitaji. Pia itaongeza ufahamu wa watumiaji kuhusu manufaa ya majengo yenye kufuata kanuni za ujenzi na matumizi bora ya nishati.
Share:

STAKEHOLDERS MEET TO DISCUSS ENERGY EFFICIENCY AND BUILDING CODES IN TANZANIA


Bagamoyo, 26 November 2022. The United Nations Development Programme (UNDP) in collaboration with the Ministry of Energy has organized a two-day workshop for Tanzania energy stakeholders from the Ministry of Lands, Housing and Human Settlement, EWURA, TANESCO, National Construction Council (NCC) and the President's Office - Regional Administration and Local Government (PO-RALG), held in Bagamoyo from 25-26 November 2022 to discuss the stakeholder’s roles to effectively implement Project Action 3 "Development and implementation of a framework for energy performance certification in large buildings in the country. 


The Tanzania Energy Efficiency Action Plan project is funded by the European Union (EU) and implemented by the Ministry of Energy in collaboration with UNDP.


The Energy Efficiency Project Coordinator, Mr Aaron Cunningham, argues that the workshop intends to discuss stakeholders’ roles in effectively implementing Project Action 3 "Development and implementation of a framework for energy performance certification in large buildings. 


He added, "This plan for the development and promotion of energy-efficient building codes and building energy performance certification will help reduce greenhouse gas emissions and pollution produced by the combustion fuel fossils, also the potential to save money."


The 2018 Energy Report in Tanzania estimates that 67% of energy consumption is in residential, commercial, and public buildings. As a result, the national action plan on energy efficiency has identified the building sector as an important sector for energy consumption reduction.


Eng. Moses Lawrence, the director of technical services for the Tanzania National Construction Council, said that the Ministry of Works and Transportation is in the process of developing the Building Act, which has considered the importance of energy efficiency in buildings. Through the NCC, the government will work with UNDP and other stakeholders to ensure the energy efficiency segment is part of the new Building Act and aligned with the National Energy Policy of 2015 and Goal 7 (Affordable and Clean Energy) of the Sustainable Development Goals (SDGs). 


He added, "improvement of buildings’ efficiency at the planning stage is more cost-effective compared to improvements after their initial construction. Therefore, decisions made during a building’s project phase will hence determine consumption over a building’s lifetime". 


Energy efficiency building codes can help transform the sector to be more environmentally friendly, cost-effective, and energy efficient. As a long-term impact, the energy efficiency building codes will contribute to SDG 7 on energy and promote progress towards Goal 13 on climate action, which aligns with the national development priorities. Energy efficiency in the building sector will support the effort of the government to provide sufficient and reliable energy, particularly electricity, to meet increased demand. It will also raise awareness among users of the benefits of more energy-sustainable buildings.
Written by Jolson Masaki, Communications Analyst - UNDP

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOVEMBA 28,2022

Magazetini leo Jumatatu November 28, 2022










Share:

Sunday 27 November 2022

RAIS WA BURUNDI AIPONGEZA BENKI YA CRDB

 

Rais wa Jamhuri ya Burundi, Evariste Ndayishimiye akiwa kwenye mazungumzo na ujumbe wa Benki ya CRDB, ulioongozwa na Mwenyekiti wake, Dkt. Ally Laay na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela wakati walipomtembelea kwenye makazi rasmi yaliyopo eneo la Kiriri, Bujumbura, Novemba 25, 2022. Mkutano huo ilikuwa ni sehemu ya muendelezo wa maadhimisho ya miaka 10 ya kampuni tanzu ya Benki ya CRDB Burundi, ambayo kilele chake kilifanyika mwishoni mwa wiki. Picha zote na Othman Michuzi.
 
=========   ========    ========
 
Bujumbura, Burundi. Ikitarajia kufungua tawi la tano mapema mwakani itakapofikisha miaka 11 ya kutoa huduma za fedha nchini Burundi, Rais wa Jamhuri ya Burundi, Evariste Ndayishimiye ameipongeza Benki ya CRDB kwa huduma bora ilizozitoa kwa muongo mmoja sasa.

Benki hiyo iliyoingia nchini Burundi mwaka 2012 ina matawi manne kwa sasa yanayotoa huduma pamoja na mawakala zaidi ya 600 wanaohakikisha wananchi na wafanyabiashara wanahudumiwa kwa wakati na mapato ya Serikali kukusanywa kwa utaratibu rahisi nchini humo.
Rais Ndayishimiye ametoa pongeza hizo alipozungumza na menejimenti ya Benki ya CRDB iliyoongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wake, Abdulmajid Nsekela aliyeambatana na wajumbe wa bodi ya wakurugenzi kusherehekea miaka 10 ya kutoa huduma nchini humo.

“Burundi tumeipokea Benki ya CRDB kwa mikono miwili na tunajivunia uwepo wake. Tanzania na Burundi ni ndugu wa karibu, hata mipaka iliyopo ni matokeo ya ukoloni lakini haiwezi kuwa kikwazo cha mahusiano mazuri yenye historia kubwa ya ushirikiano. Tunashukuru kuwa Tanzania ilishiriki kwa kiasi kikubwa kupatikana kwa amani Burundi na sasa mnakuja tufanye maendeleo kwa pamoja kwa manufaa ya nchi zetu,” alisema Rais Ndayishimiye.

Katika kipindi hicho cha kutoa huduma nchini Burundi, Benki ya CRDB imefanya vyema sokoni hadi kushika nafasi ya tatu kwa kupata faida kubwa kati ya benki 13 zilizopo. Mpaka Septemba mwaka huu, benki hiyo ilikuwa imetoa mikopo kiasi cha faranga 300 bilioni (Sh338 bilioni).

Mwaka 2019 Serikali ya Burundi iliyahamisha makao makuu yake kutoka Bujumbura kwenda jiji la Gitega hivyo Benki ya CRDB inatarajia kufungua tawi jipya huko ili kuihudumia pamoja na wafanyakazi wake, wafanyabiashara na wananchi wa kawaida. Tawi hilo litafunguliwa mapema mwakani.
 
“Tunawashuru sana kwa jitihada zenu ya kutoa elimu ya fedha kwa Warundi ili wajifunze namna nzuri ya usimamizi wa fedha na kuwekeza. Tungependa kushirikiana nanyi zaidi katika programu za vijana na wanawake ambao ni kipaumbele chetu kikubwa kwa sasa,” alisema Rais Ndayishimiye.

Kwa upande wake, Ofisa Mtendaji Mkuu wa CRDB, Nsekela alisema Serikali ya Burundi inawapa ushirikiano mkubwa unaowasaidia kupata mafanikio ndani ya miaka 10. Serikali imeipa benki9 hiyo eneo la kujenga ofisi katika Jiji la Gitega.

“Benki ya CRDB itaendelea kuunga mkono jitihada za kukuza uchumi wa Burundi kwa manufaa ya Warundi, Tanzania na Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa ujumla. Tunatarajia kuingia DRC (Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo) hivi karibuni na tutafungua matawi katika mikoa iliyo karibu na mpaka wa Burundi na DRC ili kuchochea biashara kati ya nchi hizo mbili,” alisema Nsekela.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa CRDB, Dk Ally Laay alisema haikuwa rahisi kuridhia uamuzi wa kufungua biashara nchini Burundi kwa kuwa ilikuwa ni mara ya kwanza kutoa huduma nje ya nchi.

“Maswali yalikuwa mengi juu ya kuichagua Burundi lakini leo hii sote tunajivunia na kuona nchi zote mbili zinanufaika. Hapa Burundi tunalipa kodi na kutoa ajira huku faida inayopatikana ikiwanufaisha wanahisa wetu hadi Tanzania,” alisema Dk Laay.
 Rais wa Jamhuri ya Burundi, Evariste Ndayishimiye (katikati) akimpongeza Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki ya CRDB, Tully Esther Mwambapa (kulia) wakati walipomtembelea kwenye makazi rasmi yaliyopo eneo la Kiriri, Bujumbura, Novemba 25, 2022. Kushoto ni Mjumbe wa Bodi ya Benki ya CRDB Burundi, Kahumbya Bashige
Rais wa Jamhuri ya Burundi, Évariste Ndayishimiye akiagana na Afisa Mtendaji Mkuu wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela, baada ya kumaliza mazungumzo yao walipomtembelea kwenye makazi yake rasmi yaliyopo eneo la Kiriri, Bujumbura, Novemba 25, 2022. Wengine pichani ni Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya CRDB, Dkt. Ally Laay (watatu kulia), Mwenyekiti wa Bodi ya Benki ya CRDB Burundi, Hosea Kashimba (kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Burundi, Fredrick Siwale (wapili kushoto), Afisa Mkuu wa Uwendeshaji wa Benki ya CRDB, Bruce Mwille (kulia), Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Benki ya CRDB, Tully Esther Mwambapa, Mjumbe wa Bodi ya Benki ya CRDB Burundi, Kahumbya Bashige pamoja na Naibu Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Burundi, Menard Bucumi. Mkutano huo ilikuwa ni sehemu ya muendelezo wa maadhimisho ya miaka 10 ya kampuni tanzu ya Benki ya CRDB Burundi, ambayo kilele chake kilifanyika mwishoni mwa wiki.

Share:

SIMBA SC YAIFANYIA UMAFIA POLISI TANZANIA, YAICHAPA 3-1



****************

NA EMMANUEL MBATILO

KLABU ya Simba imefanikiwa kuonoka na alama tatu mbele ya timu ya Polisi Tanzania baada ya kuichapa mabao 3-1 kwenye mchezo huo ambao ulichezwa kwenye dimba la Ushirika mjini Moshi.

Kwenye mechi hiyo tumeshuhudia mshambuliaji wao Moses Phiri akiweka kambani mabao mawili na kumfanya awe na mabao nane kwenye ligi kuu NBC na kuwa nafasi ya pili kwenye ufungaji mabao huku akiongza Fiston Kalala Mayele ambaye anamabao kumi.

Simba Sc ilianza kupata bao la kwanza kupitia kwa mshambuliaji wao John Bocco ambaye kwasasa amekuwa kwenye kiwango kizuri katika mechi tatu za hivi karibunu alivyoanza kupata nafasi kwenye kikosi.

Bao pekee la Polisi Tanzania limefungwa na Zuberi Khamisi dakika za lala salama
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger