Saturday 29 October 2022

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI OKTOBA 29,2022












Share:

Friday 28 October 2022

MAENEO YALIYOMEGWA KWENYE HIFADHI YAPANGIWE MPANGO WA MATUMIZI YA ARDHI

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akizungumza katika mkutano wa hadhara na wananchi wa kijiji cha Mpanga wilayani Wanging’ombe wakati Kamati ya Mawaziri Nane wa Wizara za Kisekta ilipotembelea kijiji hicho mkoani Njombe Oktoba 27, 2022'

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula (kushoto), Naibu Waziri Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega (wa pili kushoto) na Naibu Waziri Maliasili na Utalii Mery Masanja wakicheza na bibi aliyekuwa akifurahia maamuzi ya serikali kukibakisha kijiji cha Mpanga kilichokuwa kwenye hifadhi ya Mpanga Kipengele wakati Kamati ya Mawaziri Nane wa Wizara za Kisekta ilipotembelea kijiji hicho mkoani Njombe Oktoba 27, 2022'


Naibu Waziri wa Kilimo Anthony Mavunde (katikati) na Mkuu wa Mkoa wa Njombe Anthony Mtaka (kulia) wakimsiliza Bi Neema (kushoto) ambaye ni mkulima wa mahindi na mkazi wa kijiji cha Mpanga wilaya ya Wanging’ombe wakati Kamati ya Mawaziri Nane wa Wizara za Kisekta ilipotembelea kijiji hicho mkoani Njombe Oktoba 27, 2022'

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akisisitiza jambo mbele ya Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula na Mkuu wa mkoa wa Njombe Anthony Mtaka wakati Kamati ya Mawaziri Nane wa Wizara za Kisekta ilipowasili ofisi ya Mkuu wa mkoa Njombe Oktoba 27, 2022 (PICHA ZOTE NA WIZARA YA ARDHI)

************************

Na Munir Shemweta, WANMM NJOMBE

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ametaka maeneo ya yanayomegwa kwa ajili ya kupatiwa wananchi waliovamia hifadhi yapangiwe mpango wa matumizi ya ardhi na kutolewa hati kwa wamiliki wake.

Dkt mabula alitoa kauli hiyo oktoba 27, 2022 katika kijiji cha Mpanga kilichopo wilaya ya Wanging'ombe wakati timu ya mawaziri nane wa wizara za kisekta inayoshughulikia migogoro ya matumizi ya ardhi katika vijiji 975 ilipotembelea mkoa wa Njombe ikiwa ni mfululizo wa ziara zake kawenye mikoa ya Tanzania Bara.

Kijiji cha Mpanga ni moja ya vijiji 11 vilivyopo wilaya ya Wanging'ombe na Makete mkoani Njombe ambavyo vimemegewa eneo kutoka hifadhi ya Pori la Akiba la Mpanga Kipengele.

Dkt Mabula alisema, serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imeridhia baadhi ya vijiji kwenye mkoa wa Njombe kubaki maeneo ya hifadhi za Mapori ya Akiba ingawa wananchi wake waliingia bila ridhaa ya serikali.

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, ili kuondokana na migogoro ya ardhi vijiji vilivyomegewa maeneo vitapimwa na kumilikishwa ili wamiliki kujua mipaka sambamba na kuweza kutumia hati kukopa fedha benki na fedha kutumika kuboresha shamba au mifugo.

"Kinachofanyika hapa siyo tu kutoa maeneo, eneo linatolewa lakini liwekewe mpango mzuri na endelevu ili kuona jinsi gani mnaweza kutumia ardhi mliyopewa kwa faida na kwa sababu tunaongezeka basi mpango uwe mzuri na endelevu" alisema Dkt Mabula.

Amebainisha kuwa, ni lazima maeneo yanayopangwa yaanishwe matumizi yake kama vile maeneo ya akiba, hifadhi, makazi na uwekezaji na kutaka wakati wa utekelezaji wataalamu wazingatie mpango wa matumizi katika maeneo hayo.

Timu ya Mawaziri Nane wa Wizara za Kisekta ambayo inashughulikia migogoro ya matumizi ya ardhi kwenye vijiji 975 imemaliza ziara yake katika mkoa wa Njombe ukiwa ni mkoa wa 22 kati ya 26 ya Tanzania Bara na inaendelea na ziara yake katika mkoa wa Ruvuma.

Share:

MADEREVA WA MALORI WAIGOMEA TICTS BANDARINI

 

Mohammed Abdallah, mmoja wa madereva walioshiriki kwenye mgomo wakiilalamikia huduma mbovu za TICTS

***

* Tanzania yanusurika kupata aibu kubwa mbele ya Rais wa Congo

* Ni kutokana na huduma mbovu za upakuaji wa makontena

Na Mwandishi Wetu - Dar es salaam


MADEREVA malori wameigomea kampuni ya kimataifa ya kuhudumia makontena Tanzania katika bandari ya Dar es Salaam (TICTS) kutokana ucheleweshaji mkubwa wa huduma ya kupakua makontena unaofanywa na kampuni hiyo.


Mgomo huo wa madereva wa malori ulianza usiku wa Ijumaa Oktoba 21, siku ambayo Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo (DRC), Felix Tshisekedi, aliwasili nchini kwa ziara.


"TICTS ni wazembe sana. Utendaji kazi wao ni mbovu, kuanzia asubuhi hadi sasa hivi saa sita ya usiku tumekwama hapa bandarini kutokana na ucheleweshaji wa huduma ya upakiaji wa makontena," alisema Mohammed Abdallah, dereva wa lori la makontena, usiku wa mgomo ulipoanza.


Madereva hao, ambao wamekuwa wakigoma mara kwa mara kutokana na huduma mbovu za TICTS, wamesema miundombinu ya eneo la Kitopeni bandarini lililo chini ya TICTS ni mibovu, ikiwemo uhaba wa vyoo.


"Licha ya kucheleweshewa huduma za makontena kwa visingizio vya kreni kuharibika mara kwa mara na msongamano wa malori, kuna matundu ya vyoo mawili tu ambayo yanahudumia mamia ya madereva," alisema Abdallah.


Siku ambayo madereva malori wameanza mgomo wao mpya, Rais Tshisekedi, ambaye nchi yake ya DRC ndiyo mteja mkubwa kuliko wote wa bandari ya Dar es Salaam, aliwasili Zanzibar kwa mapumziko binafsi kabla ya kuanza ziara rasmi ya kikazi nchini Tanzania Oktoba 23.


Moja ya shughuli ambayo Rais wa Congo alipangiwa kufanya wakati wa ziara yake nchini ni kutembelea bandari ya Dar es Salaam.


"Tunashukuru kuwa Rais Tshisekedi alipata udhuru akalazimika kukatisha ziara yake nchini, hivyo hakwenda tena bandarini Dar es Salaam. Maana kama angeenda bandarini angekutana na mgomo wa madereva malori kutokana na huduma mbovu ya TICTS na hii ingekuwa ni fedheha kubwa kwa taifa," alisema Juma Hafidh, mdau wa bandari ya Dar es Salaam.


Hivi karibuni, wafanyakazi wa TICTS walilaumiwa kwa kudondosha makontena kwenye bahari na kufanya meli zishindwe kupita kwenda kupakua mafuta eneo la Kurasini KOJ kwa siku kadhaa na kuisababishia taifa hasara.


Kumekuwa na mlolongo wa tuhuma za uzembe na ukosefu wa ufanisi wa TICTS ambayo imekuwa ikisimamia eneo la makontena la bandari ya Dar es Salaam kwa zaidi ya miaka 20 bila tija.


Serikali ya Tanzania kwa sasa iko kwenye majadiliano na TICTS kuhusu kuongeza au kutoongeza mkataba wake, huku kampuni hiyo ikilaumiwa na wadau wa biashara na usafirishaji kwa kukosa ufanisi.


Wadau wa sekta za biashara na usafirishaji wameitaka serikali kutoipa kampuni ya TICTS mkataba mpya wa kuendesha eneo la kontena la bandari ya Dar es Salaam kwa kushindwa kufikia lengo la kuongeza wingi wa mzigo kwa asilimia 37 kwa mwaka na kuwa na ufanisi mdogo.

Share:

MWANAFUNZI DARASA LA TANO SHINYANGA AJINYONGA BAADA YA KUMALIZA KUNYWA CHAI


Picha siyo ya tukio halisi

Na Halima Khoya, SHINYANGA

WANAFUNZI wa darasa la tano shule ya msingi Ndala ‘A’ Manispaa ya Shinyanga Brayton Daniel (11) amekutwa amejinyonga kwa kamba nyuma ya mlango nyumbani kwao.

Tukio hilo limetokea Oktoba 26 mwaka huu majira ya saa 4 asubuhi, nyumbani kwao Mtaa wa Mwabundu Kata ya Ndala Manispaa ya Shinyanga.

Akielezea tukio hilo jana mama mkubwa wa marehemu Joyce Kalulu, amesema mtoto huyo hakuwa hana tatizo lolote, lakini siku hiyo walipomaliza kunywa chai, yeye aliondoka kwenye mihangaiko yake ya maisha na aliporudi nyumbani majira ya saa 8 mchana akakuta mlango umefungwa kwa ndani, walipovunja wakamkuta kijana wao amejinyonga.

“Asubuhi nimeamka na kufanya kazi zote nikawa nimewaacha kijana wangu na bibi yake, nimerudi saa 8 kutoka kazini nikamkuta mama anahangaika kumuita Brayton afungue mlango, ndipo tulipoamua kwenda kumuita Mwenyekiti ambaye alifanikiwa kutoboa nyavu za dirisha na kumuona Brayton akiwa amening’inia mlangoni,”amesema Kalulu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mtaa wa Mwabundu Pili Masanja amesema taarifa za tukio hilo alizipata majira ya saa 9 mchana, na alipofika kwenye familia hiyo ikabidi watoboe nyavu ya dirisha alipochungulia akamuona mtoto huyo akiwa amejinyonga nyuma ya mlango.

“Majira ya saa 9 nilikuja kuitwa na Joyce Kalulu ili nikawasaidie kufungua mlango ambapo nilizunguka nyuma yumba ili kutoboa dirisha lakini tulichokiona baada ya kutoboa dirisha ni Brayton akiwa amejinyonga na kamba nyeusi kwenye mlango, ndipo nikapiga simu Polisi,”amesema Masanja.

Kwa upande wake Kamanda wa Jeshi la polisi Mkoa Shinyanga Janeth Magomi, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo huku akibainisha kuwa Jeshi hilo bado linaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo cha tukio hilo.

Share:

UNAWEZA KUWA MTU MWENYE BAHATI MAISHANI KULIKO KAWAIDA, FANYA HIVI!

Share:

MABUSHI ACHAGULIWA KUWA ASKOFU MKUU WA MAKANISA YA IEAGT TANZANIA

Askofu wa Kanisa la IEAGT Mjini Shinyanga David Mabushi, (kulia) ambaye kwa sasa pia ni Askofu Mkuu wa Makanisa ya IEAGT Tanzania, akizungumza mara baada ya kuibuka mshindi kwenye uchaguzi.

Na Mwandishi Wetu, SHINYANGA

Umoja wa Kanisa la International evangelical Assemblies of God Tanzania (IEAG) kwa mara ya kwanza limefanya uchaguzi wa viongozi wa baraza la umoja huo, na kumchagua Askofu David Mabushi kuwa Askofu Mkuu wa Makanisa ya IEAGT Tanzania.

Uchaguzi huo umefanyika Oktoba 27,2022 katika Kanisa la IEAGT lililopo mkoani Shinyanga ambapo watumishi wa Mungu wa Umoja wa Makanisa ya IEAGT kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini, wamepiga kura kuchagua viongozi wa nafasi ya Askofu Mkuu, Makamu Askofu Mkuu, Katibu Mkuu, Muwekahazina wa umoja wa baraza hilo.

Akizungumza mara baada ya zoezi la upigaji kura kwenye uchaguzi huo Mwenyekiti Mtendaji bodi ya wadhamini Kanisa la IEAGT ambaye pia ni msimamizi wa uchaguzi huo Lucas Lugwila, amesema uchaguzi huo umefanywa na wajumbe wapatao 71, wa dhehebu la IEAGT kutoka sehemu mbalimbali hapa nchini.

Mara baada ya zoezi la upigaji kura kumalizika msimamizi wa uchaguzi Lucas Lugwila amemtangaza Askofu David Mabushi kuwa ndiye Askofu Mkuu wa Umoja wa Kanisa la INTERNATIONAL EVANGELICAL ASSEMBLIES OF GOD TANZANIA (IEAGT), kwa kupata kura 68 kati ya kura 71 zilizopigwa.

“Nafasi ya Askofu Mkuu, David Mabushi ameibuka mshindi kwa kupata 68, nafasi ya Makamu Askofu Mkuu mshindi ni Simon Laizer amepata kura 58, nafasi ya Katibu Mkuu mshindi ni Flagson Ndibwa kwa kura 46 na nafasi ya Mwekahazina mshindi ni Timoth Mwantake ambaye amepata kura 58”, amesema Lugwila.

Mara baada ya uchaguzi huo kumalizika Askofu Mkuu David Mabushi akizungumza mbele ya baraza hilo, ameahidi kuendelea kushirikiana na viongozi hao na kuitumikia vyema nafasi hiyo aliyochagulia kwa kusimamia miongozo, Katiba na Misingi iliyowekwa na umoja huo.

Aidha Makamu Mwenyekiti kutoka CPCT taifa, Bartholomeo Sheggah amewapongeza viongozi hao waliochaguliwa, na kuwataka kutumikia vizuri nafasi hizo ili kuendelea kujenga umoja wa kanisa hilo katika msingi mzuri.

Nao baadhi ya Wajumbe wa baraza hilo akiwemo Mchungaji Joseph Jackson amesema wanaimani na viongozi waliowachagua watakwenda kutumika vyema kwenye nafasi zao.

“Jambo la kwanza tunamshukuru mungu ametusimamia tumemaliza salama, ulikua ni uchaguzi mzuri na wa haki, tunawaamini viongozi wetu tuliowachagua na tunaimani watakwenda kufanyakazi kama itakavyompendeza mungu, tutashirikiana nao vizuri”, amesema Mchungaji Jackson.





Mwenyekiti mtendaji bodi ya wadhamini Kanisa la IEAGT mkoani Shinyanga ambaye pia ni msimamizi wa uchaguzi huo Lucas Lugwila akitangaza matokeo ya uchaguzi huo.
Askofu wa Kanisa la IEAGT Mjini Shinyanga David Mabushi, (kulia) ambaye kwa sasa pia ni Askofu Mkuu wa Makanisa ya IEAGT Tanzania, akiwa na Makamu wake Askofu Simon Laizer mara baada ya kupata ushindi kwenye uchaguzi huo.
Viongozi walioshinda kwenye uchaguzi wakiombewa.
Picha ya pamoja ikipigwa mara baada ya uchaguzi kumalizika na washindi kupatikana.
Picha ya pamoja ikipigwa mara baada ya uchaguzi kumalizika na washindi kupatikana.
Share:

Thursday 27 October 2022

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA OKTOBA 28,2022



















Share:

BENKI YA CRDB KUANZISHA PROGRAMU YA UWEZESHAJI KWA WAJASIRIAMALI VIJANA NA WANAWAKE



Benki ya CRDB imetangaza kuanzisha programu ya uwezeshaji kwa vijana na wanawake wajasiriamali ikiwa na lengo la kukuza ujumuishi wa kiuchumi nchini.

Taarifa hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela wakati wa hafla ya ufunguzi wa Kongamano la sita la TEHAMA (TAIC) linalofanyika visiwani Zanzibar kwa muda wa siku tatu kuanzia leo 26 hadi 28 Oktoba 2022.


Kongamano hilo limezinduliwa na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali, na taasisi kutoka ndani na nje ya nchi.


Nsekela alibainisha kuwa kwa kushirikiana na Tume ya TEHAMA, katika kongamano hilo Benki ya CRDB inakwenda kuzindua programu wezeshi kwa wajasiriamali vijana na wanawake wenye biashara na mawazo bunifu katika sekta mbalimbali ikiwamo sekta TEHAMA iliyopewa jina la “IMBEJU”.


Benki ya CRDB ni mdhamini mkuu wa Kongamano la TAIC 2022 ambalo limepewa kauli mbiu ya“Mabadiliko ya Kidijitali kwenye Uchumi wa Buluu kwa Maendeleo ya Jamii na Kiuchumi”.
Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi akimkabidhi cheti cha udhamini mkuu wa Mkutano wa Mwaka wa Sekta ya TEHEMA, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela katika hafla ya ufunguzi wa mkutano huu unaofanyika katika hoteli ya Golden Tulip, Zanzibar kuanzia leo Oktoba 26 hadi 28, 2022. Kulia ni Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano, na Uchukuzi Zanzibar, Dkt. Khalid Salum.
Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi akizungumza wakati akitoa hotuba yake katika hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Mwaka wa Sekta ya TEHEMA nchini, ulioanza leo kwenye hoteli ya Golden Tulip, Zanzibar. Mkutano huo utafanyika kwa siku tatu kuanzia leo Oktoba 26 hadi 28, 2022.
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Mwaka wa Sekta ya TEHEMA nchini, ulioanza leo kwenye hoteli ya Golden Tulip, Zanzibar. Mkutano huo utafanyika kwa siku tatu kuanzia leo Oktoba 26 hadi 28, 2022.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Mwaka wa Sekta ya TEHEMA nchini, ulioanza leo kwenye hoteli ya Golden Tulip, Zanzibar. Mkutano huo utafanyika kwa siku tatu kuanzia leo Oktoba 26 hadi 28, 2022.
Sehemu ya washiriki wa Mkutano wa Mwaka wa Sekta ya TEHEMA nchini, ulioanza leo kwenye hoteli ya Golden Tulip, Zanzibar. Mkutano huo utafanyika kwa siku tatu kuanzia leo Oktoba 26 hadi 28, 2022.
Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi akipata maelezo kuhusu huduma za kidijitali zinazotolewa na Benki ya CRDB kutoka kwa Meneja wa Tawi la Benki hiyo Michenzani Zanzibar, Ahmad Aboubakar (kushoto) wakati alipotembelea banda la Benki ya CRDB katika uzinduzi wa Mkutano wa Mwaka wa Wadau wa Sekta ya TEHEMA unaofanyika katika hoteli ya Golden Tulip, Zanzibar kuanzia leo Oktoba 26 hadi 28, 2022. Wengine pichani ni Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye (wapili kulia), Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi Zanzibar, Dkt. Khalid Salum (watatu kulia), na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger