Monday 3 October 2022

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE OKTOBA 4,2022

MAGAZETI












Share:

BENKI YA CRDB YAWASHUKURU WATEJA MAFANIKIO YA HUDUMA BORA KWA JAMII


Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Godwin Gondwe (wa pili kulia) akimkabidhi zawadi mmoja wa wateja wa Benki ya CRDB, Dkt. Redempta Mbatia (kushoto) katika hafla ya ufunguzi rasmi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja yenye kauli mbiu "Sherehekea Huduma" iliyofanyika leo kwenye Tawi la Benki ya CRDB, Oysterbay, jijini Dar es salaam. Wengine pichani ni Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya CRDB, Fredrick Nshekanabo (wapili kushoto) pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Yolanda Uriyo. Benki ya CRDB imeianza wiki hiyo kwa kuwashukuru wateja wake kwa maoni na ushauri ambao umeiwezesha benki hiyo kutoa huduma bora na zenye viwango vya kimataifa kwa jamii.
Wakati makampuni na taasisi dunia nzima zikiadhimisha ‘Wiki ya Huduma kwa Wateja’ mwaka 2022, Benki ya CRDB imeianza wiki hiyo kwa kuwashukuru wateja wake kwa maoni na ushauri ambao umeiwezesha benki hiyo kutoa huduma bora na zenye viwango vya kimataifa kwa jamii.


Salamu hizo za shukrani zimetolewa na Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya CRDB, Fredrick Nshekanabo wakati wa hafla iliyofanyika katika tawi la Benki hiyo lililopo Oysterbay, Jijini Dar es Salaam. Nshekanabo alisema wateja wamekuwa msingi mkubwa kwa Benki ya CRDB kufikia mafanikio ambayo imekuwa ikiyapata kufikia kuwa ‘Benki Bora zaidi Tanzania’.
“Tukiongozwa na kaulimbiu yetu ya ‘Benki inayomsikiliza mteja’ tumekuwa tukipokea maoni na ushauri wa wateja ambao kwa kiasi kikubwa umechangia ubora wa huduma na bidhaa zinazotolewa na benki yetu. Hii inaonyesha ni kwanamna gani mteja amepewa kipaumbele kikubwa katika mkakati wa biashara yetu,” aliongezea Nshekanabo.


Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja Benki ya CRDB, Yolanda Uriyo amesema pamoja na kuwashukuru wateja, katika Wiki ya Huduma kwa Wateja mwaka huu wamedhamiria kuwasherekea wale wote walio mstari wa mbele kuiwezesha benki hiyo kutoa huduma bora”.
“Wakati dunia nzima ikiadhimisha wiki hii kwa kaulimbiu ya ‘Celebrate Service’ inayomaanisha kusherehekea huduma, kwetu sisi hii ni zaidi ya kaulimbiu kwani mafanikio tuliyonayo yanatulazimisha kuwasherehekea wanaotufanya tuwe bora zaidi; wateja na wafanyakazi wetu,” alifafanua Uriyo.


Uriyo alisema Benki ya CRDB itaitumia wiki hii kuwashkuru na kuwasherehekea wateja ambao wamekuwa chachu ya huduma bora zinazotolewa na benki hiyo. Aidha, watakuwa wakiwasherekea wafanyakazi ambao wamekuwa wakitoa huduma bora kwa weledi na ubunifu mkubwa.


Benki ya CRDB inatajwa kuwa benki inayoongoza kwa huduma bora kwa wateja. Mwaka huu benki hiyo imetunukiwa tuzo ya ‘Benki Bora Tanzania’ na jarida maarufu duniani la nchini Uingereza la Euromoney. Mwaka jana mwishoni benki hiyo ilitunukiwa ‘Tuzo ya Ubora’ na Taasisi ya Utafiti wa Ubora barani Ulaya (European Society for Quality Research).
Katika miaka ya hivi karibuni Benki ya CRDB imeweka kipaumbele na kufanya uwekezaji mkubwa katika huduma kwa wateja. Benki hiyo imewekeza katika mifumo ya kisasa na ya kidijitali ya utoaji huduma, ikiwamo mifumo ya mawasiliano, ambayo imesaidia kuongeza ufanisi katika matawi yake zaidi ya 260 yaliyosambaa kote nchini.


Uwekezaji huu pia umeongeza ufanisi katika njia mbadala za utoaji huduma; CRDB Wakala zaidi ya 22,000, ATMs zaidi ya 550, na huduma za SimBanking, SimAccount, na Internet banking. “Benki pia imewekeza katika mafunzo kwa wafanyakazi ili kuwawezesha kupata weledi pindi wanapowahudumia wateja. Hii imeenda sambamba na uboreshaji wa taratibu zetu za utoaji huduma (processes) ili ziendane na mahitaji ya wateja,” alisema Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya CRDB, Fredrick Nshekanabo.
Baadhi wa Wateja wa Benki ya CRDB wakishiriki shidano fupi la kupamba Keki ikiwa ni sehemu ya kusherehekea ufunguzi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja yenye kauli mbiu "Sherehekea Huduma" iliyofanyika leo kwenye Tawi la Benki ya CRDB, Oysterbay, jijini Dar es salaam.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Godwin Gondwe (wa pili kulia) akimkabidhi zawadi ya Shampeni Mkuu wa Kitengo cha Masoko wa Benki ya CRDB, Joseline Kamuhanda baada ya kushiriki shidano fupi la kupamba Keki ikiwa ni sehemu ya kusherehekea ufunguzi wa Wiki ya Huduma kwa Wateja yenye kauli mbiu "Sherehekea Huduma" iliyofanyika leo kwenye Tawi la Benki ya CRDB, Oysterbay, jijini Dar es salaam. Wengine pichani ni Afisa Mkuu wa Fedha wa Benki ya CRDB, Fredrick Nshekanabo (wapili kushoto) pamoja na Mkuu wa Kitengo cha Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Yolanda Uriyo.
Sehemu ya wateja wa wafanyakazi wa Benki ya CRDB wakiwa kwenye hafla hiyo.


Share:

MUME WANGU KAZAA NJE YA NDOA, NIFANYE NINI?

Share:

MZEE AMUUA BINTI YAKE KWA KUMKATA KATA KWA SHOKA NA VISU KISA KACHELEWA KULETA MAJI





Mzee wa makamo kutoka wadi ya Mwingi magharibi, Kitui nchini Kenya kwa sasa anazuiliwa katika kituo cha polisi cha Migwani baada ya kumuua mwanawe.


Inasemekana mshukiwa aliyejulikana kwa jina la Mwendwa, alitumia shoka kumuua mtoto wa miaka 14, Mumo Mwendwa ambaye mpaka kifo chake alikuwa ni mwanafunzi wa shule ya msingi ya Kyomo katika darasa la nane.



Esther Mwendwa, mkewe anayefanya kazi Kibwezi, alisema hakuwa nyumbani wakati kisa hicho kilipotokea na alifahamishwa na jamaa kuhusu kufariki kwa mwanawe.


“Baba yake alikuwa amemtuma kuchota maji mtoni, badala yake Mumo alienda kucheza na marafiki,” alisema.

Mtoto huyo alikimbia alipomwona babaake ambaye kulingana na mkewe alisema alikuwa ni mtu mwenye vurugu kufuatia tabia yake ya kutumia dawa za kulevya.

“Alimkatakata hadi kumuua kwa kutumia shoka na visu,” alisema.

Esther pia aliongeza kuwa mwezi uliopita, alimpiga kichwani na kumjeruhi vibaya.

Alisema mwili wake umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya Migwani.

“Mwanangu alikufa kifo cha maumivu sana na ninaiomba serikali kuingilia kati na kuhakikisha haki inatendeka,” aliongeza

Florence Muli, binamu wa marehemu alisema kuwa kisa hicho kilitokea mwendo wa saa tano za usiku wa Jumapili.

Alisema alikuwa amefunga nyumba kutoka ndani na alipiga kelele kuomba msaada kutoka kwa majirani.

Benard Mwangangi kaka yake mkubwa alisema usiku huo huo, alisikia kelele nyingi kutoka kwa kaka yake na kudhani ni tabia yake dhahiri ya kumpiga mwanawe.

Alisema amekuwa na uadui sana na watu wengi hata waliogopa kutembelea nyumba yake.

“Baada ya kumsikia akipiga kelele, mara moja nilimsikia mwanawe, Mumo akipiga kelele kuomba msaada,” alisema

Muda mfupi baadaye, alisikia baba yao akigombana naye na akamwambia baba yake anataka kumuua mwanawe.

Mwangangi alipoenda kwenye nyumba hiyo, alimkuta mtoto wa miaka 14 akiwa amelala amefariki huku mshukiwa akiwa amefungwa kamba na wananchi waliokuwa wakisubiri maafisa wa polisi.

Pia aliongeza kuwa mkewe amekuwa akiishi kwa hofu kufuatia visa kadhaa vya unyanyasaji wa nyumbani.

Akithibitisha kisa hicho, chifu wa eneo hilo Grace Mwikali Muli alisema mwanaume huyo kwa sasa anazuiliwa katika kituo cha Polisi cha Migwani akisubiri uchunguzi zaidi.
Share:

WATU WATATU WAUAWA KOLANDOTO SHINYANGA, ALIYEANZA KUUA ACHOMWA MOTO

 


Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga Janeth Magomi akizungumza na waandishi wa habari kuhusu tukio la mauaji Kolandoto Shinyanga.

Na Halima Khoya, SHINYANGA

Watu wawili ambao ni Nicholaus Leonard na Badmalta Melikiad, wameuawa kwa kupigwa na kitu chenye ncha kali sehemu mbalimbali za mwili wao na wengine watatu kujeruhiwa, na mtu ambaye hajafahamika akidaiwa kurukwa na akili ambaye naye ameuawa kwa kupigwa kisha kuchomwa moto na wananchi wenye hasira kali.



Tukio hilo limetokea jana Oktoba 2 ,2022 katika Kata ya Kolandoto Manispaa ya Shinyanga majira ya saa moja jioni.

Akisimulia tukio hilo leo mmoja wa majeruhi Daniel Emmanuel, amesema mtu huyo alivamia katika nyumba ya bwana Nicholaus Leonard, na kuwakuta mke wa Nicholaus ambaye ni Lucia Luhende akisukana na Rafiki yake Badmalta ndipo akaanza kuwashambulia.

Anasema wakati akiwashambulia akajitokeza kuwasaidia ndipo na yeye akapigwa kichwani na kitu kizito kichwani akapasuka na kuanza kuomba msaada, huku mmoja wa wanawake hao Badmalta akipigwa vibaya na kusabisha kifo chake papo hapo.

“Nilienda kuwasaidia baada ya kusikia kelele katika nyumba hiyo ya bwana Nicholaus, ambapo mtu huyo alikuwa amefunga mlango na mimi nilivyofika nikafungua mlango lakini bahati mbaya jamaa alikuwa amejibanza katika kona nilivyoingia tu akanipiga kichwani nikaanguka chini,”Amesema Daniel.

“Wakati vurugu hizo zikiendelea na mimi kuelemewa kushindwa kutoa msaada kutokana na kuvuja damu nyingi, mume wa Lucia Luhende bwana Nicholaus Leonard aliingia ndani kutoa msaada, lakini na yeye akapigwa kichwani akaanguka chini na kupoteza maisha papo hapo,”anaongeza.

Kwa upande wake Mke wa Marehemu Lucia Luhende, amesema yeye alifanikiwa kutoka nje wakati mtu huyo akiendelea kumshambulia Rafiki yake, ndipo mume wake akaingia ndani ili kumuokoa lakini hakufanikiwa kutokana na kupigwa vibaya kichwani kisha akapoteza maisha.

Naye Diwani wa Kolandoto Mussa Andrew, amesema baada ya kupokea taarifa alifika eneo la tukio na kumkuta jamaa akiwa bado ndani ya nyumba hiyo, akapiga simu kuomba msaada Polisi, lakini wananchi wenye hasira kali walifanikiwa kumtoa nje na kisha kuanza kumkimbiza.

Anasema wananchi hao walifanikiwa kumkamata na kisha kuanza kumpiga kwa mawe na baadae kumchoma moto.

Mganga Mkuu wa Hospitali ya Kolandoto Dk. Joseph Wallace, amethibitisha kupokea miili ya marehemu watatu akiwamo na kijana huyo ambaye aliuawa na wananchi, pamoja na majeruhi watatu huku mmoja akipewa rufaa ya kwenda Bugando jijini Mwanza kwa matibabu zaidi.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga Janeth Magomi, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo la mauaji, na kutoa wito kwa wananchi wakimuona mtu analeta taharuki watoe taarifa ili kuzuia maafa yasitokee.
Share:

MASHIRIKA YANAYO LEA USHOGA YAONYWA


Mwenyekiti wa Bodi ya Mashirika yasiyokuwa ya kiserikali nchini Mwantumu Mahiza.

Na Dotto Kwilasa,DODOMA


MWENYEKITI wa Bodi ya Mashirika yasiyokuwa ya kiserikali nchini Mwantumu Mahiza, ameyataka mashirika yasiyo ya kiserikali ambayo yatajihusisha na kutetea ndoa za jinsia moja  kuacha mara moja kwani ni kinyume na mila na desturi za kitanzania.


Mahiza, amezungumza hayo  jijini Dodoma, wakati akifungua mkutano mkuu wa mwaka wa wakurugenzi wa mashirikika yasiyokuwa ya kiserikali na kueleza kuwa yapo mashirika  nchini yanaishi kwa kivuli Cha kutetea ushoga kwa madai ya kulinda haki za binadamu.


Amesema, katika kipindi chake akiwa mwenyekiti wa Bodi hiyo hatopenda kuona jambo hilo linatokea kwa kuwa ni kinyume na mila na desturi za Watanzania na ni aibu .


“Kama kuna shirika lolote ambalo katika utekelezaji wa majukumu yake limepanga kufanya vitu kama hivyo naomba lifute mpango huo mara moja hatuwezi kuviruhusu vitu kama hivi katika taifa ambalo serikali ipo na dini zipo”amesema Mwantumu na kuongeza;

Si jambo la busara kwa taifa kuruhusu vitendo vya ndoa za jinsia moja kwa mwanamke kuolewa na mwanamke mwezake au mwaume kuoa mwanaume mwenzake , tusipofanya juhudi tutashindwa kutofautisha kati ya mwanaume na mwanamke,"anasisitiza 


Pamoja na hayo ametilia mkazo suala hilo kuwa Serikali  haiwezi kuruhu haki za binadamu zinazopingana na mila na kueleza kuwa takwimu zinaonyesha kuwa idadi ya wanawake ni kubwa ukilinganisha na wanaume hivyo ndoa za jinsia moja ni jambo ambalo halipaswi kupewa nafasi.


“Hata ukienda leo hospitali kati ya watoto kumi wanaozaliwa kwa siku wanawake ni saba wanaume ni watatu hivyo kama tusipokuwa makini hii nchi itakuwa ya wanawake tupu wanaume watakwisha kwasababu wanaoana wao kwa wao”amesisitiza


Kwa upande wake Mkurugenzi wa Mtandao wa watetezi wa haki za binadamu (THRDC), Onesmo Olengurumwa amesema lengo la mkutano huo ni pamoja kupata fursa ya kukumbushana mambo mbalimbali.


Mkurugenzi huyo pia ametumia nafasi hiyo kuiomba serikali kufanyia marekebisho ya sera inayosimamia mashirika yasiyo ya kiserikali ikiwa ni pamoja na kuyaondolea kodi katika vitu mbalimbali ambavyo wamekuwa wakiingiza kutoka nje ya nchi.



Share:

TCU YAONGEZA MUDA WA UDAHILI WA SHAHADA YA KWANZA KATIKA TAASISI ZA ELIMU YA JUU NCHINI

Share:

NIC YAZINDUA MKATABA WA HUDUMA KWA MTEJA

Msajili wa Hazina Bw.Mgonya Benedicto akiwa pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Dkt. Elirehema Doriye akizindua Mkataba wa Huduma kwa Mteja wakati wa Maadhimisho ya Kimataifa ya Wiki ya Huduma kwa wateja iliyofanyika leo Oktoba 3,2022 Jijini Dar es Salaam. Msajili wa Hazina Bw.Mgonya Benedicto akiwa pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Dkt. Elirehema Doriye akizindua Mkataba wa Huduma kwa Mteja wakati wa Maadhimisho ya Kimataifa ya Wiki ya Huduma kwa wateja iliyofanyika leo Oktoba 3,2022 Jijini Dar es Salaam. Msajili wa Hazina Bw.Mgonya Benedicto akizungumza katika uzinduzi wa Mkataba wa Huduma kwa Mteja wakati wa Maadhimisho ya Kimataifa ya Wiki ya Huduma kwa wateja iliyofanyika leo Oktoba 3,2022 Jijini Dar es Salaam. Msajili wa Hazina Bw.Mgonya Benedicto akizungumza katika uzinduzi wa Mkataba wa Huduma kwa Mteja wakati wa Maadhimisho ya Kimataifa ya Wiki ya Huduma kwa wateja iliyofanyika leo Oktoba 3,2022 Jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Bima la Taifa (NIC) Dkt. Elirehema Doriye akizungumza katika uzinduzi wa Mkataba wa Huduma kwa Mteja wakati wa Maadhimisho ya Kimataifa ya Wiki ya Huduma kwa wateja iliyofanyika leo Oktoba 3,2022 Jijini Dar es Salaam. Baadhi ya wadau wa NIC wakifuatilia uzinduzi wa Mkataba wa Huduma kwa Mteja wakati wa Maadhimisho ya Kimataifa ya Wiki ya Huduma kwa wateja iliyofanyika leo Oktoba 3,2022 Jijini Dar es Salaam. (PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

************************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

SHIRIKA la Bima la Taifa (NIC) imezindua Mkataba wa Huduma kwa Mteja wakati wa Maadhimisho ya Kimataifa ya Wiki ya Huduma kwa wateja iliyofanyika leo Oktoba 3,2022 Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza wakati akifungua huduma hiyo, Msajili wa Hazina Bw.Mgonya Benedicto amewataka watumishi wa NIC kufuata ahadi iliyowekwa kwenye mkataba huo na asiwepo mtumishi yeyote wa kutenda kinyume na mkataba huo kwani atachukuliwa hatua kwa mujibu wa Sheria na Miongozo ya Utumishi wa Umma.

Amesema madhumuni ya mkataba huu ni kuboresha uhusiano baina ya Shirika na wateja wake lakini pia ukikusudia kuongeza uelewa kuhusu aina na ubora wa huduma zinazotolewa, haki na wajibu wa mteja na jinsi anavyoweza kuwasiliana.

"Mkataba wa Huduma kwa Mteja ni makubaliano kati yenu watoa huduma na mteja wenu ikiwa ni ahadi ya kutoa huduma bora kwa mteja, mkataba huu unaelekeza na kuainisha viwango vya huduma ambavyo wateja wenu wanatarajia kupata ili kufikia malengo yao". Amesema

Aidha amesema Ofisi ya Msajili wa Hazina na Serikali kwa ujumla ipo tayari kuwapa ushirikiano mnaostahili ikiwa tu mtaweka bidii katika kazi na kuboresha huduma zaidi ya zilivyo sasa.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa NIC Dkt. Elirehema Doriye, amesema Shirika limekuwa likifanya mabadilikko kwenye kuwahudumia wateja ambapo wamekuwa wakiboresha huduma ili kuendana na ushindani ulioko sokoni jambo lililowavutia wateja kununua bidhaa zao za Bima na kuwafanya kuwa na ukuaji wa faida ya zaidi ya asilimia 100 katika miaka minne mfululizo.

"Mojawapo ya misingi inayotuongoza NIC yetu ni kutambua kuwa siku zote "Mteja Kwanza" yaani "Customer first" hii inamaanisha kwamba mteja kwetu ni kipaumbele namba moja katika utoaji huduma". Amesema Dkt.Doriye.

Aidha Dkt.Doriye amesema katika kuadhimisha wiki hii na kutambua umuhimu wa wateja, Shirika limezindua Mkataba wa Huduma kwa Mteja "ikiwa ni ahadi yetu kwa wateja kuwa tutawapatia huduma inayostahili kulingana na ahadi tuliyowapa". Amesema

Share:

JAMAA AJICHIMBIA KABURI , AWALIPA WATAKAOMLILIA NA ATAYEPIGIA SALUTI MAITI YAKE

Mwanaume ambaye amejichimbia kaburi akiwa hai amefunguka kuwa alichukuwa hatua hiyo ili kuwapa watu funzo.


Afrimax iliangazia kwa kina ya mipango madhubiti ya mwanaume huyo ambayo tayari ameweka kwa ajili ya mazishi yake siku za usoni.

Kando na kujichimbia kaburi, tayari amepata watu ambao watamlilia na kumchezea ngoma pamoja na mtu ambaye atapigia saluti maiti yake. Katika mipango yake pia amekamilisha kutayarisha nguo atakazozikwa nazo.

Kulingana na mwanamume huyo, kisa cha kusikitisha cha mwanamume ambaye wanawe wanaishi ng'ambo kilimtia moyo kuwapa watu funzo.

Alijifunza kutoka kwa mtu huyo kwamba watu wanapenda wafu kuliko walio hai. Mzee huyo aliishi katika umaskini wa sina sinani licha ya kuwa na watoto ughaibuni. Alipofariki, wale watoto waliokataa kumtunza akiwa hai, walirudi na kujenga mahali pazuri.

Alipokuwa hai, aliishi katika nyumba iliyobomoka akikabiliwa na njaa huku akivaa nguo chafu. Mtu huyo ambaye jina lake halikutambulika alipanga mazishi akisema anatarajia kuwafunza watu kuwapenda na kuwajali wazazi wao wakati bado wangali hai.

Kama ilivyoripotiwa hapo awali, mwanamume mmoja kutoka Murang'a alianza mipango ya jinsi mazishi yake yatafanywa baada ya kukata roho katika tarehe isiyojulikana. Samuel Karanja, ambaye pia anajiita Kumenya, kumaanisha "Kujua" alijenga eneo lake la kuzikwa ili kuondolea familia yake gharama ya kuchimba kaburi lake atakapokufa.

Akiongea na mwanahabari Victor Kinuthia, mzee huyo alisema pia amejiandika ratiba yake ya mazishi ambayo anatarajia kusomwa wakati wa hafla hiyo kwa sababu hakuna anayemfahamu zaidi yake.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU OKTOBA 3,2022


Magazetini leo Jumatatu October 3 2022













Share:

Sunday 2 October 2022

DAKTARI MTANZANIA AFARIKI KWA EBOLA UGANDA


Daktari raia wa Tanzania, Dkt. Mohamed Ali Hafidh anayefanya kazi nchini Uganda aliyeambukizwa Ebola amefariki dunia, mhudumu wa kwanza wa afya aliyefariki kwa ugonjwa huo katika mlipuko wa hivi karibuni nchini humo, waziri wa afya wa Uganda amesema Jumamosi.

“Nasikitika kutangaza kwamba tumempoteza daktari wetu wa kwanza, Dk. Mohammed Ali, raia wa Tanzania, Mwanaume mwenye umri wa miaka 37” Waziri wa Afya Jane Ruth Aceng, aliandika kwenye ukurasa wake wa Twitter.


Alisema Ali alifanyiwa vipimo vya Ebola Septemba 26 na kufariki wakati akipokea matibabu katika hospitali moja ya Fort Portal, mji ulioko umbali wa kilomita 300 magharibi mwa mji mkuu Kampala.


Mamlaka katika taifa hilo la Afrika Mashariki ilitangaza kuzuka kwa homa kali ya virusi vya Ebola Septemba 20 na kusababisha hofu ya mgogoro mkubwa wa kiafya katika nchi hiyo yenye watu milioni 45.


Hakuna chanjo ya Ebola yenye vimelea aina ya Sudan ambapo maambukizi yake yamezuka hivi karibuni nchini Uganda.


Wizara ya afya ilisema Ijumaa, kabla ya kifo cha Dr. Ali, kwamba ugonjwa huo hadi sasa umewaambukiza watu 35 na kuua watu saba.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger