Wednesday 31 August 2022

KEMIKALI SUMU KATIKA TUMBAKU HUSABABISHA MAGONJWA YASIYOAMBUKIZA : ADAM FIMBO

 

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Adam Fimbo akionesha orodha ya Kemikali sumu zinazopatikana katika Bidhaa za Tumbaku alipokuwa akiongea na waandishi wa habari katika maonesho ya Kimataifa ya wadau wa bidhaa za afya ya Afrika Mashariki katika ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam.

Naibu Waziri wa Afrya Naibu Waziri wa Afya Dr.Godwin Mollel (wa pili kulia) akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Adam Fimbo (wa kwanza kulia aliyevaa suti) alipokuwa akizungumzia juu ya Kemikali sumu zinazopatikana katika Bidhaa za Tumbaku wakati waziri huyo alipotembelea katika banda la Mamlaka hiyo kwenye maonesho ya Kimataifa ya wadau wa bidhaa za afya ya Afrika Mashariki Jijini Dar es Salaam.

Meneja Mawasiliano na Elimu kwa Umma,wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA),Gaudensia Simwanza (kulia) akifurahia jambo na Baadhi ya wadau wa Sekta ya Dawa waliotembelea kwenye Banda la Mamlaka hiyo kweye maonesho ya Kimataifa ya wadau wa bidhaa za afya ya Afrika Mashariki Jijini Dar es Salaam.

 Na: Hughes Dugilo, DAR ES SALAAM

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Bw. Adam Fimbo amesema kuwa Mamlaka hiyo imefanya uwekezaji katika mitambo ya kisasa inayoweza kubaini  kemikali sumu zilizopo kwenye bidhaa za tumbaku kwa lengo la kulinda afya za wananchi wanaotumia Bidhaa hizo.

Ameyasema hayo kwenye mahojiano maalumu yaliyofanyika kwenye Banda la Taasisi hiyo katika  maonesho ya Kimataifa ya wadau wa bidhaa za afya ya Afrika Mashariki yaliyoanza leo agosti 30,2022Jijini Dar es Salaam ambapo amesema kuwa bidhaa za tumbaku zenye kemikali hizo zinaweza kusababisha magonjwa yasiyombukiza na kwamba  TMDA imeweka orodha ya Kemikali zinazopatikana kwenye bidhaa za hizo ikiwemo sigara kwa lengo la kutoa elimu kwa wananchi mbalimbali wanaotembelea maonesho hayo.

"kwa upande wetu sisi tunashiriki kwenye maonesho haya kwa lengo la kutoa elimu kwa wananchi wanaotembelea na hapa tumeleta orodha ya kemikali ambazo zipo kwenye bidhaa za tumbaku, Tunachokifanya sisi ni kupima bidhaa za tumbaku zikiwemo sigara ili kuhakikisha hizi kemikali haziwepo kwenye bidhaa hizo "

"Hii ni horodha ya Kemikali sumu ambazo zipo kwenye Bidhaa za Tumbaku, horodha hii ya Kemikali ndizo zinazosababisha madhara  kwa binadamu ukisikia magonjwa kama kansa ya koo, shinikizo la damu na magonjwa mengi yasiyoambukiza ambayo yanatokana na utumiaji wa tumbaku" Ameeleza Fimbo.

Ameongeza kuwa Mamlaka hiyo imefanya uwekezaji mkubwa  kwenye mitambo kwaajili ya kupima na kubaini uwepo wa kemikali hizo  kwenye bidhaa za tumbaku ili kuhakikisha kemikali hizo haziwepo kwenye bidhaa hizo.

"Tunataka hizi kemikali zisiwepo kwenye sigala kwa hiyo kazi yetu kubwa ni kuhakikisha kila sigara hazina hizi kemikali zilizopo hapa" ameongeza. 

Share:

Tuesday 30 August 2022

GGML WATOA MAGODORO 50 KWA KITUO CHA WAZEE BUKUMBI

Afisa Mwandamizi wa Mahusiano ya Jamii kutoka GGML, Shunashu Musa (kulia) akimkabidhi magodoro 50 msimamizi wa Kituo cha Wazee Bukumbi, Jonas Tarimo. Anayetazama ni Afisa Mahusiano wa Jamii wa GGML, Fredrick Musa (wa kwanza kulia).
Sehemu ya wazee wa Kituo cha Wazee cha Bukumbi wakisubiri msaada wa GGML.

Na Mwandishi wetu - Mwanza

KATIKA kuunga mkono juhudi za Serikali kuwajali na kuboresha maisha ya wazee nchini, Kampuni ya Uchimbaji Madini ya Dhahabu Geita (GGML) imetoa msaada wa magodoro 50 kwa Kituo cha Wazee Bukumbi kilichopo mkoani Mwanza.


Akizungumza katika hafla ya kukabidhi msaada huo jana mkoani Mwanza, Ofisa Mwandamizi wa Mahusiano ya Jamii kutoka GGML, Shunashu Musa alieleza kuwa msaada huo unalenga kuboresha makazi bora na hali ya maisha ya wazee wanaoishi katika kituo hicho.


Aliongeza kuwa baadhi ya wafanyakazi wa GGML na wenzao wamekuwa wakisaidia kituo hicho kwa nyakati tofauti na kuchangia baadhi ya vifaa vya matumizi. Kipindi hiki menejimenti ya kampuni hiyo imeamua kusaidia kituo hicho kwa kuchangia uboreshaji wa vyumba vya kulala vya wazee hao.


“Tulipokea ombi la kufikiria kusaidia kituo hiki kwa njia mbalimbali. Tunafahamu kituo hicho kilianzishwa miaka mingi iliyopita hivyo baadhi ya miundombinu na vifaa vinahitaji maboresho ndiyo maana uongozi uliamua kuchangia magodoro 50.

"Kama sehemu ya AngloGold Ashanti, moja ya maadili ya biashara ya GGML ni kwamba jumuiya na jamii tunakofanyia kazi lazima ziwe na maisha bora. Tunatumaini magodoro haya yataboresha maisha ya wazee zaidi ya 50 wanaoishi hapa,” alisema.



Aidha, Msimamizi wa Kituo cha Wazee cha Bukumbi, Jonas Tarimo alishukuru GGML kwa msaada huo na kuongeza kuwa utasaidia kutoa huduma za malazi bora na salama kwa wazee wa kituo hicho.



“Hiki ndicho kituo pekee cha kuishi wazee kilichopo karibu na mikoa ya Geita na Mwanza. Tumebahatika kuungwa mkono na Mgodi wa Dhahabu wa Geita ndio maana tunaona wakazi wengi wanafurahia msaada huu,” alisema.


GGML imekuwa kinara wa uwekezaji katika jamii tangu ilipoanzishwa mwaka 2000, huku vipaumbele vikubwa vikiwa ni miradi ya afya, elimu, maji, barabara, miradi ya maendeleo na miradi mingine ya kijamii inayolenga kuboresha ustawi wa jamii inayowapokea.


Mapema mwaka huu, Kampuni ilitangazwa kuwa mshindi wa jumla wa makampuni yaliyofanya vyema katika sekta ya madini nchini Tanzania kwa mwaka wa 2020/2021 baada ya kushinda tuzo za uwajibikaji wa kampuni kwa jamii, mazingira, usalama, mlipakodi bora na maudhui ya ndani.

Share:

BENKI YA CRDB YAFUNGUA RASMI TAWI LAKE WILAYANI LUSHOTO , TANGA

Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Omary Mgumba (katikati) kwa pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori (wapili kushoto), Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya CRDB, Boma Raballa (kushoto) wakikata utepe kuashiria ufunguzi rasmi wa tawi la Benki ya CRDB lililopo wilayani Lushoto mkoani Tanga, jana Agosti 29, 2022. wengine pichani ni Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga, Suleiman Mzee (wa pili kulia), Mkuu wa wilaya ya Lushoto, Kalist Lazaro (kulia), pamoja na Meneja wa Benki ya CRDB Tawi la Lushoto, John Mtani.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Omary Mgumba (kulia) kwa pamoja na Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Prof. Neema Mori wakifungua kitambaa kwenye jiwe la msingi kuashiria ufunguzi rasmi wa tawi la Benki ya CRDB lililopo wilayani Lushoto mkoani Tanga, jana Agosti 29, 2022.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Omary Mgumba akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi rasmi tawi jipya la Benki ya CRDB lililopo wilayani Lushoto mkoani Tanga, jana Agosti 29, 2022.
Afisa Mkuu wa Biashara wa Benki ya CRDB, Boma Raballa akizungumza wakati wa hafla ya ufunguzi rasmi tawi jipya la Benki ya CRDB lililopo wilayani Lushoto mkoani Tanga, jana Agosti 29, 2022.
Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Mhe. Omary Mgumba ameongoza sherehe za ufunguzi rasmi wa tawi jipya la Benki ya CRDB lililopo wilayani Lushoto na kuwataka wananchi wa Wilaya hiyo kuchangamkia fursa mbalimbali za kiuchumi zitolewazo na Benki hiyo.

Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mhe. Mgumba alisema "Wakazi wa Lushoto na vitogoji vyote vinavyozunguka wilaya hii, niwape rai ya kuitumia benki hii kama chachu ya maendeleo wilayani hapa, haswa katika kutumia huduma za kibenki lakini pia kujipatia mikopo mbalimbali iltolewayo na benki hii ya CRDB".

Aidha, Mgumba aliendelea kusema "Serikali kwa kushirikiana na wadau imedhamiria kuwawezesha wananchi kiuchumi ndio maana inasogeza huduma zikiwamo za kifedha jirani yenu. Kila mmoja aangalie fursa zilizopo kukuza uchumi wake," alisisitiza.

Kwa upande wa Afisa Mkuu wa Biashara Benki ya CRDB, Boma Raballa alisema, wakazi wa Lushoto na vitongoji vyake sasa wanayo fursa ya kulitumia tawi hilo ambalo kwa sasa limeondoa changamoto ya kufuata huduma za kibenki wilayani Korogwe, kwa kusogeza huduma kwa wananchi na leo tumefika Lushoto,

Naye Makamu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya CRDB, Profesa Neema Mori alisema, wataendelea kushirikiana na Serikali kufanikisha shughuli mbalimbali za kiuchumi nchini hasa katika kuhakikisha wananchi wanapata fursa zitolewazo na benki ya CRDB ikiwemo mikopo nafuu ya kilimo ambayo kwasasa riba yake ni asilimia 9 tu. Hivyo aliwataka wanalushoto kuchangamkia fursa hiyo na kuhakikisha wanainua uchumi wa mtu mmoja mmoja lakini pia katika vikundi na kufanikisha miradi ya maendeleo.
Share:

HAYA NDIYO MADHARA YA KULA CHIPS


KIUKWELI katika vyakula vitamu duniani na vinavyopendwa haswaa na watu duniani usiposema chipsi utakuwa mtu waajabu sana. Chipsi haziliki bongo tu ata ughaibuni chips zinalika sana na zinapendwa haswaa, chipsi zinaenda na vitu vingi kama chipsi yai, chipsi kuku na kadhalika.

Hizi ndio athari za ulaji wa chipsi.

Husababisha magonjwa ya moyo

Kwa kuzingatia ukweli kwamba zimekaangwa sana katika mafuta ya hidrojeni, chipsi huja na kiasi kikubwa cha mafuta, ambayo huongeza cholesterol yako mbaya na kupunguza cholesterol yako nzuri. Athari kubwa ya hii ni kwamba utaongeza hatari ya ugonjwa wa moyo.

 Hupunguza kinga ya mwili

Kulingana na utafiti uliochapishwa katika jarida la Current Opinion in Clinical Nutrition & Metabolic Care, kula chakula chenye mafuta mengi na vyakula vya kukaanga vingi unaweza kuwa unaharibu utumbo wako kwa kuongeza bakteria wasio na afya na kupunguza bakteria wa afya ya mwili wako. Kwa kuzingatia jukumu la utumbo katika kusaidia kufahamisha mfumo wa kinga ya mwili wako, unaweza kuwa unaweka mwili wako hatarini kupata magonjwa.

Huongeza uzito wa mwili

Vyakula vya kukaangwa katika mafuta, huwa mabomu ya kalori, na kusababisha kupata uzito. Utafiti uliochapishwa katika jarida la The American Journal of Clinical Nutrition uligundua kuwa kula vyakula vya kukaanga kunahusishwa moja kwa moja na unene kupita kiasi.


Imeandikwa na Peter Nnally kwa msaada wa mitandao.
Share:

JAMAA WA MIAKA 46 AMBAKA MTOTO WA MIAKA 8 KISHA KUMPA SH. 500


Mtoto aliyebakwa

Mwanaume mmoja anayefahamika kwa jina la Sunday (46), mkazi wa mtaa wa Mkudi, Kata ya Nyamanoro Manispaa ya Ilemela jijini Mwanza, anadaiwa kumbaka mtoto wa 8 (Pichani) na kumsababishia maumivu makali ikiwemo kumharibu kisaikolojia.

Mtoto huyo akizungumzia tukio hilo amesema mwanaume huyo alimuita wakati akiwa anacheza na kumvutia ndani.

"Nilikuwa nacheza ndipo Sunday akaniita akanivuta ndani akaniambia naomba nikubake nikakataa, nilivyokataa nikataka kupiga kelele akaniziba mdomo akanitishia kisu, akanivua nguo akanibaka kisha akanipa shilingi mia tano akamaliza akafunga mlango akaondoka baada ya mama kujua nimebakwa akamuita bibi ndipo tukaenda polisi", ameeleza mtoto huyo

Wakizungumza kwa uchungu wazazi wa mtoto huyo wameviomba vyombo vya dola kuwasaidia kutokana na mtoto wao kuharibiwa na kuambulia kupata maumivu makali huku akitakiwa kutumia dawa mwezi mzima ili kumuepusha na maambukizi ya virusi vya Ukimwi lakini wanashangaa mtuhumiwa akiwa nje kwa dhamana licha ya kumfungulia kesi ya ubakaji na ushahidi kuwepo.

Share:

Monday 29 August 2022

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE AGOSTI 30,2022



Magazetini leo Jumanne August 30 2022





















































Share:

JAMAA AKIMBIA KILOMITA 90 KUONESHA MAHABA APATE MREMBO AOE


Joseph Kagiso Ndlovu akiwa na mke wake
Joseph Kagiso Ndlovu akifanikiwa kukutana na mke wake.
**

Mzee mmoja mwenye umri wa miaka 57, aliyetambulika kwa jina la Joseph Kagiso Ndlovu, alikimbia mbio za kilomita 90 (maili 56) ili kumposa mwanamke anayeitwa Prudence.


Alisema wamechumbiana tangu mwanzoni mwa mwaka huu na wanapanga kufunga ndoa mwakani.


Mwanaume wa Afrika Kusini ambaye alifanya hatua ya ziada kuthibitisha mapenzi yake kwa mwanamke wake amewafanya watumiaji wa mtandao kuwa na wasiwasi na amekuwa akivuma kwenye mitandao ya kijamii.


Alipigwa picha akiwa ameshika bango la kumtaka mwanamke huyo amuoe, alipokuwa akikaribia kumaliza mbio za Comrades Marathon siku ya Jumapili.

“Prudence utanioa? Nimekimbia kilomita 90 kwa ajili yako,” ilisomeka kwenye bango.

Vyombo vya habari vya ndani na watumiaji wa mitandao wamekuwa na siku ya uwanjani wakizungumza juu ya urefu ambao mwanamume alilazimika kwenda kumtongoza mpenzi wake.


Imeandikwa na Peter Nnally kwa msaada wa mitandao
Share:

MLINZI WA KANISA ATUPWA JELA KWA KUMUIBIA SISTA

MLINZI wa Hospitali ya Kanisa Katoliki la Kijiji cha Mwanzugi wilayani Igunga, Peter Marco apata kifungo cha miaka 30 gerezani kwa kosa la kumuibia kwa kutumia silaha Sista Aline Nicette vitu kadhaa, ikiwamo simu ya mkononi, vyote vikiwa na thamani ya Tsh.720,000/-


Mahakimu Augustine Mwarija, Lugano Mwandambo na Lilian Mashaka walitupilia rufaa ambayo Marco, mrufani, aliwasilisha kupinga hukumu iliyotolewa na Mahakama Kuu.

“Tumeridhika kwamba ushahidi ulithibitisha kesi dhidi ya Marco bila shaka yoyote, kiwango cha uthibitisho kinachotumika katika kesi za jinai. Hatuoni umuhimu wa kukata rufaa na tumeitupilia mbali,” walisema katika hukumu yao waliyoitoa Tabora hivi karibuni.


Wakati wa kusikilizwa kwa rufaa hiyo, Marco alilalamika kuwa ushahidi wa utambulisho wa vielelezo kupitia mashahidi wawili wa upande wa mashtaka ambao ni Mlinzi na Sista Aline uliotegemewa na Mahakama Kuu kuthibitisha hukumu yake ya unyang’anyi wa kutumia silaha unatia shaka na kesi inayomkabili haikuthibitishwa.

Shahidi wa tukio hilo ambaye alikuwa mlinzi mwenza wa mtuhumiwa(Marco) alisema majambazi nane walivamia kanisani hapo, huku wanne wakiwa na mapanga. Alifanikiwa kumtambua Marco ambaye alimuona akiwa ameshika panga na bunduki.

Shahidi huyo aliiambia mahakama ya mwanzo kuwa aliweza kumtambua Marco kupitia taa ya umeme inayomulika mahali hapo na majambazi hao walikuwa karibu naye kiasi kwamba hata baada ya kuumia kufuatia kupigwa risasi na kupoteza fahamu, aliweza kumkumbuka Marco kuwa mmoja wao.

Imeandikwa na: John Mbwambo kwa msaada wa mitandao.
Share:

TPDC MARATHON KUCHANGIA GHARAMA ZA UPASUAJI WA WATOTO 511 JKCI

Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la maendeleo ya petroli Tanzania (TPDC), DKT. James mataragio akizungumza katika uzinduzi wa TPDC Marathon leo Agosti 29,2022 katika Ofisi za TPDC Jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Prof. Mohamed Janabi akizungumza katika uzinduzi wa TPDC Marathon leo Agosti 29,2022 katika Ofisi za TPDC Jijini Dar es Salaam. Mratibu wa mbio hizo Bw.Fred Kwezi akizungumza katika uzinduzi wa TPDC Marathon leo Agosti 29,2022 katika Ofisi za TPDC Jijini Dar es Salaam.

********************************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) wamezindua mbio za hisani (TPDC Marathon) zenye lengo la kuchangia gharama za upasuaji kwa watoto wenye matatizo ya moyo ambapo imebainishwa kuwa kuna watoto 511 wanasubiri upasuaji katika taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI)

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Agosti 29, 2022 Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la maendeleo ya petroli Tanzania (TPDC), DKT. James mataragio amesema Malengo yao ni kusaidia na kuunga mkono juhudi za kuokoa maisha ya watanzania na kwa kuanzia mbio hizo ambapo watarajiwa kusaidia upasuaji wa watoto 50 wenye matatizo ya moyo.

"Tumelenga kusaidi Taasisi ya Jakaya kikwete (JKCI) na tumeamua kuunga mkono katika kuokoa maisha ya watanzania wenzetu ambapo baada ya kukamilika mbio hizi tunategemea kusaidia watoto 50 kwa kuanzia"

Aidha Dkt.Mataragio alisema kuwa Mbio hizo ni endelevu kwa kila mwaka hivyo amewaasa wananchi kushiriki kwa wingi kama sehemu ya mazoezi ili kulinda afya zao lakini pia kwa upande mwingne kusaidia watoto wenye matatizo ya moyo.

"Mbio hizi ni za kila mwaka na tutakua tunaendelea kuchangia kwa kadri ambavyo tutakua tunafanikiwa hivyo wananchi wote washiriki katika mbio hizi ili kuweza kuwasaidia wananchi wenzetu kuokoa maisha yao".Amesema Dkt.Mataragio.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete Prof. Mohamed Janabi alisema kila mwaka asilimia moja ya watoto milioni mbili wanaozaliwa nchini Tanzania sawa na watoto elfu ishirini huzaliwa na matatizo ya moyo na kati yao asilimia ishirini na tano sawa na watoto elfu tano wanafanyiwa upasuaji wa moyo katika taasisi ya jakaya kikwete.

"Fedha zitakazopatikana zitatumika kikamilifu kwa malengo yaliyokusudiwa lakini pia kwa siku hiyo kutakuwa na upimaji wa magonjwa wa moyo bure, utoaji wa chanjo UVIKO-19 na uchangiaji wa damu kwa hiyari". Amesema

Nae Mratibu wa mbio hizo Bw.Fred Kwezi aliwahakikishia washiriki wa mbio hizo kuwa kutakuwepo na huduma zote za kimichezo, kiusalama na kiafya na kuwa Usajili unafanyika kwa kupitia TPDC pamoja na waratibu wa mbio hizo ambao ni Goba Rose Runners.

Mbio hizo zenye kauli mbiu isemayo “kimbia kwa afya yako” zinatarajiwa kufanyika septemba 11 mwaka huu katika viwanja vya farasi oysterbay jijini dar es salaam huku mgeni rasmi akitarajiwa kuwa raisi mstaafu wa serikali ya awamu ya nne Mhe. Jakaya mrisho kikwete.
Share:

PSPTB YAPIGA MARUFUKU WATAALAMU WANAOFANYA KAZI ZA MANUNUZI NA UGAVI ZA SERIKALI AMBAO HAWAJASAJILIWA

Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Manunuzi na Ugavi (PSPTB) Bw.Godfrey Mbanyi akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi za PSPTB leo Agosti 29,2022 Jijini Dar es Salaam. Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Manunuzi na Ugavi (PSPTB) Bw.Godfrey Mbanyi akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi za PSPTB leo Agosti 29,2022 Jijini Dar es Salaam.

*******************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Bodi ya Umma Manunuzi na Ugavi (PSPTB) iwapiga marufuku Wataalamu wanaofanya kazi za Manunuzi na Ugavi za serikali ikiwa hawajasajiliwa na yeyote atakayebainika yuko kinyume sheria itachukuliwa dhidi yake.

Agizo hilo limetolewa leo Dar es salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Manunuzi na Ugavi (PSPTB) Bw.Godfrey Mbanyi ambapo amesema Wizara ya Fedha na Mipango inaendelea kukamilisha wa Mfumo mpya hivyo kabla ya kuanza kufanya kazi bodi watakwenda kufanya ukaguzi katika taasisi, Ofisi zote za serikali na ikibainika kuwa kuna mtu ameajiriwa kufanya kazi hiyo na hana sifa stahiki mwajiri aliyemuajiri atawanibika kisheria .

Sanjari na hayo amesema hapo awali kulikuwa na madhaifu mengi ambayo yalikuwa yakitokea kupitia mfumo wa zamani sababu wataalamu ambao waliokuwa hawana sifa stahiki kufanya shughuli hizo na kusababisha madhaifu ambayo Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali akija kukagua anakuta hasara hivyo jambo hilo halitavumiliwa linakwenda kutafutiwa mwarobaini.

"Mtaalamu yeyote hata Kama ni Afisa Manunuzi mwandamizi ana cheo kama hana usajiliwa na bodi hii Psptb hatoweza kutoka kwenda hatua moja nyingine kufanya kazi hatoweza kama hajaainisha taarifa zake za usajili katika mfumo huu mpya hivyo tunapofanya ukaguzi tukimbaini Mwajiri aliyemuajiri atawajibika kisheria "alisema Mbanyi

Hata hivyo mfumo huo upo kwenye majaribio na wote watakaokuwa katika usajili wa Mfumo mpya itasaidia kutoa huduma kwa urahisi bila kuchelewesha kazi za serikali hivyo nawasisitiza Waalamu wote wa Manunuzi na Ugavi kujisajili mapema .

Hata hivyo amesema ikitokea taasisi,Ofisi yeyote ya serikali Maafisa wake hawajasajiliwa na Mfumo huo mpya sheria Kali zitachikuliwa kwani hapo awali kabla ya mfumo huo mpya kulikuwa na changamoto ambapo hata ambao siyo wataalamu wasio na sifa ikiwemo taaluma usajili walikuwa wakitumia mfumo na kusababisha taarifa za Mkaguzi Mkuu wa hesabu za serikali akikagua kukuta mapungufu .

Aidha Serikali mpaka sasa inaingia gharama ya kujenga mfumo huo mpya wa Manunuzi na Ugavi na inakwenda kukamilika hivyo utasaidia kurahisisha huduma na kuwatambua wataalamu wote wanaofanya kazi hiyo ambao wana sifa stahiki.
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger