Thursday 4 August 2022

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI AGOSTI 4,2022


















Share:

Wednesday 3 August 2022

WAKULIMA WA SOYA WASHAURIWA KUTUMIA MBOLEA YA ASILI


****************

Na Mwandishi Wetu-Arusha



Wakulima wa zao la Soya (soyalishe) nchini wameshauriwa kutumia mbolea asilia ili kuongeza uzalishaji wa zao hilo.

Rai hiyo imetolewa na Mwanafunzi wa Shahada ya Uzamivu (PhD) ya Kilimo Endelevu ya Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela Bi. Monica Nakei katika maonesho ya 28 ya Nanenane Kanda ya Kaskazini yanayoendelea viwanja vya Themi Arusha Agosti 2, 2022.

Bi. Monica amesema kwa sasa anafanya utafiti mbolea asilia itokanayo na vimelea vya bakteria jamii ya rhizobia ambayo inasaidia kuongeza virutubisho vya nitrogeni na fosforasi kwa mimea ya Soya.

" nimefanya utafiti wa mbolea hii kupitia zao la Soya na matokeo ni mazuri ,utafiti utakapokamilika mbolea hii itakuwa tayari kwa matumizi" amesema Bi .Monica

Aidha, ameeleza kuwa, mbolea hiyo ina faida nyingi ikiwemo kuimarisha afya ya udongo na kuweka usawa katika mfumo wa ikilojia ya udongo pamoja na kutunza mazingira kama maji, hewa na udongo.

Bi. Monica ameeleza kuwa, faida nyingine ni pamoja na mazao yatokanayo na mbolea hiyo kutokuwa na kemikali zenye kuleta madhara kwa walaji na gharama yake ni nafuu kwa wakulima.

Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela imekuwa mstari wa mbele katika kutoa elimu iliyolenga kusaidia jamii na kukuza viwanda kupitia tafiti na bunifu zinazofanywa na wanafunzi wa Taasisi hiyo, ambao wanashiriki katika maonesho ya 28 ya nanenane Kanda ya Kaskazini kwa nia ya kutoa elimu na kuonesha bunifu mbalimbali zinazozalishwa na taasisi hiyo.

Mbali na bunifu ya mbolea asilia , Taasisi hiyo imetoa elimu ya migomba iliyoboreshwa, kiatilifu biologia cha kudhibiti wadudu katika zao la Kabeji, upimaji wa udongo , chakula cha samaki chenye lishe, buheri wa Afya,Nutrano,NUSA,Omega -3DHA,Ngwara,Kweme na vyakula visivyo vya kemikali.

Share:

WATUMISHI WA WILAYA YA TEMEKE WAMPONGEZA RAIS SAMIA KWENYE NYONGEZA YA MSHAHARA

Mtumishi wa Wilaya ya Temeke Bi.Makungu Shomari akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 3,2022 wakati wakitoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya. Mtumishi wa Wilaya ya Temeke Bi.Makungu Shomari akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 3,2022 wakati wakitoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya. Mtumishi wa Wilaya ya Temeke Bi.Makungu Shomari akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 3,2022 wakati wakitoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya. Baadhi ya watumishi wa Wilaya ya Temeke Jijini Dar es Salaam wakiwa katika mkutano na waandishi wa habari leo Agosti 3,2022 wakati wakitoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya. Baadhi ya watumishi wa Wilaya ya Temeke Jijini Dar es Salaam wakiwa katika mkutano na waandishi wa habari leo Agosti 3,2022 wakati wakitoa pongezi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

*********************

Na Mwandishi wetu.

WATUMISHI wa kada mbalimbali katika Wilaya ya Temeke Jijini Dar es Salaam wamempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa juhudi ambazo anazifanya hasa kuwajali watumishi na kuzingatia maslahi yao.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 3,2022 Jijini Dar es Salaam,Mtumishi wa Wilaya ya Temeke Bi.Makungu Shomari amesema kuwa Rais Samia ndani ya kipindi chake cha muda mfupi ameweza kuleta nafuu na faraja kwa watumishi wa Umma.

"Kuhusu suala la nyongeza ya asilimia 23 sisi watumishi tumelielewa sana mana lengo kuu Rais Samia amezingatia kuboresha Hali za kiuchumi za watumishi wa kiwango cha chini ambao ni wengi zaidi katika kada mbalimbali za utumishi wa umma, hapa amezingatia wenye viwango vidogo vya mishahara". Amesema Bi.Makungu

Aidha amesema kuwa Rais Samia amejipambanua kuwa anawajali watumishi sana na kwa kuzingatia maslahi yao na alianza kwa kuwaondolea kadhia ya watumishi wenye deni la mkopo wa elimu ya juu,

"Rais Samia alipoingia madarakani alifuta penati hii na imeleta ahueeni kubwa na Sasa Deni linalipika, baada ya mabadiliko hayo aliyekuwa analipa milioni 8 Sasa analipa milioni 4 pekee."Amesema

Pamoja na hayo amesema kuwa suala la posho na nauli amesema Rais Samia ameongeza kiwango kwa asilimia 100 na hii imeleta ahueni kwa watumishi wanapopewa kazi maalumu.
Share:

AMUUA MKEWE KWA KUMPIGA NA KUMNG'ATA KIDEVU UKWENI KWENYE MSIBA


Sehemu ya mauaji yalipofanyika
**

Mariam Masanja 22, mkazi wa Kijiji cha Nyabugela, Kata ya Mganza wilayani Chato mkoani Geita, ameuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani na kung'atwa kidevu na mme wake Edward Franscis 20, ambao walikutana kwenye familia ya mwanamke kuhani msiba baada ya ugomvi wao wa muda mrefu.

Wawili hao walikutana kwenye msiba wa kaka wa marehemu ambapo marehemu alikuwa mkoani Mwanza kwa dada yake baada ya kugombana na mme wake ndipo aliporudi kwao baada ya kusikia kaka yake amefariki.

Wazazi wa marehemu wameeleza walivyopata taarifa za mtoto wao kuuawa na mme wake huku baba mzazi wa marehemu anasema wawili hao walikuwa na ugomvi wa mara kwa mara wa wivu wa kimapenzi.

Mwenyekiti wa Kijiji cha Nyabugela Metusela Mgema, amesema wawili hao walifika mara kadhaa kwenye ofisi yake kwa ajili ya migogoro ndani ya familia yao ambayo ilikuwa inasuruhishwa mara kwa mara lakini mpaka kufikia kifo cha mwanamke wawili hao walikuwa wameachana.

Share:

NILIPATA NG’OMBE WANGU WAWILI BAADA YA KUIBIWA

Share:

KARSAN ANG'ATUKA RASMI, MKURUGENZI MPYA WA UTPC KENNETH SIMBAYA AKABIDHIWA MIKOBA


Mkurugenzi mpya wa muungano wa Klabu za Waandishi wa habari Tanzania (UTPC) Bw. Kenneth Simbaya (kulia), kushoto ni Rais wa Utpc Bw. Deogratius Nsokolo na katikati ni Bw. Abubakar Karsan Mkurugenzi ambaye amemaliza muda wake
Rais wa Muungano wa Klabu za Waandishi wa Habari Tanzania(UTPC)  Deogratius Nsokolo amemkabidhi rasmi ofisi Bw. Kenneth Simbaya ambaye ni Mkurugenzi mpya wa UTPC. 

Bw. Simbaya anachukua nafasi ya Bw. Abubakar Karsan ambaye amemaliza muda wake.

Makabidhiano hayo yamefanyika tarehe 1/8/2022 katika ofisi za UTPC zilizopo Isamilo Jijini Mwanza ambapo Rais Nsokolo amesema UTPC ina matarajio makubwa kutoka kwa Bw. Simbaya na kwamba uzoefu wake kwenye kazi utasaidia kuendeleza kazi nzuri iliyoachwa na mtangulizi wake na kuipeleka taasisi mbali zaidi.

Pamoja na mambo mengine Rais Nsokolo ametoa nasaha zake kwa mkurugenzi mpya, huku akigusia zaidi kuendeleza ushirikiano kati ya UTPC na wadau mbalimbali lakini pia kutumia fursa ya uwepo wa mkurugenzi aliyemaliza muda wake katika kubadilishana maarifa ya kiuongozi.

Pia amemtaka Bw. Simbaya kushirikiana na wafanyakazi wa UTPC, Bodi ya Wakurugenzi pamoja na viongozi wa Klabu za waandishi wa habari katika utendaji wa kazi kwani anaamini ushirikishwaji huleta tija zaidi kwa maendeleo ya taasisi na kwamba taasisi haiwezi kuendeshwa na mawazo ya mtu mmoja.

Aidha amesisitiza kuhusu uadilifu na ubunifu katika utendaji wake wa kazi na kuimarisha ushirikiano na wafadhili ikiwemo kutafuta fursa mpya za kupata fedha. 

Hata hivyo alimdokeza kuhusu uwepo wa changamoto ndogondogo zilizopo katika klabu za waandishi wa habari licha ya jitihada zilizofanyika kutatua changamoto hizo.

"Uhai wa UTPC unategemea uwepo wa klabu za waandishi wa habari hivyo ni lazima tuhakikishe tunashirikiana kuzisimamia na kuzijengea uwezo klabu zetu'' ,amesema Rais Nsokolo.

Naye Mkurugenzi anayemaliza muda wake ndugu Abubakar Karsan ameeleza changamoto iliyokuwepo wakati anakabidhiwa nafasi ya ukurugenzi na kwamba hapakuwa na nyaraka zozote za makabidhiano hali iliyompa wakati mgumu katika kuifufua na kuiendeleza taasisi hiyo mpaka kuifikisha hapa ilipo leo.

"Nilikabidhiwa ukurugenzi hapa bila kuwa na nyaraka zozote, niliambiwa chukua kijiti nenda ukafufue taasisi" Karsan.

Hata hivyo Bw. Karsan ameahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa mkurugenzi mpya kwa kipindi cha muda wa miezi mitatu ili kubadilishana uzoefu wa kiutendaji na ndugu Kenneth Simbaya.

Kwa upande wake Bw. Kenneth Simbaya amesema nafasi ya ukurugenzi ni nafasi ambayo anaweza kupewa mtu yeyote hivyo ameahidi kuhakikisha anataguliza mbele maslahi ya waandishi wa habari na klabu zake na yale yote mazuri yatabaki kuwa mazuri kwa maslahi ya waandishi wa habari Tanzania.


Pia ameahidi kushirikiana na wafanyakazi pamoja na wadau wa UTPC katika kuhakikisha taasisi inasonga mbele "Maamuzi binafsi huyumbisha mwelekeo wa taasisi, hivyo niwahakikishe Bodi ya Wakurugenzi kwamba kila kitu kitaenda sawa kulingana taratibu zilizowekwa na kwa mujibu wa miongozo ya UTPC ", amesema Simbaya.

Aidha ameongeza kuwa kesho ya UTPC inategemea maamuzi mazuri yatakayofanywa leo, hivyo ili kuacha alama ni lazima kufanya kazi kwa ufanisi na weledi wa hali ya juu na kwa maslahi ya waandishi wa habari nchini.

Share:

Tuesday 2 August 2022

TANGA JIJI YAONGOZA UKUSANYAJI MAPATO, MANISPAA YA SHINYANGA YANG'ARA, MBULU MJI BALAA, KIBAHA DC YATISHA


NA GODFREY NNKO


KATIKA kipindi cha Julai hadi Juni 2022 Halmashauri ya Jiji la Tanga imeongoza kwa kukusanya mapato kwa asilimia 113 ya makisio yake ya mwaka ikifuatiwa na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam asilimia 108.

Huku Halmashauri ya Jiji la Arusha ikiwa asilimia 104, Halmashauri ya jiji la Dodoma asilimia 103, Halmashauri ya Jiji la Mwanza asilimia 100 na Halmashauri ya Jiji la Mbeya imekua ya mwisho kwa kukusanya asilimia 92.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Mhesshimiwa Innocent Bashungwa ameyasema hayo leo Agosti 2, 2022 jijini Dar es Salaam wakati akitoa taarifa kuhusu mapato na matumizi ya ndani ya halmashauri kwa mwaka wa fedha 2021/2022.

Wakati huo huo, kwa upande wa halmashauri za manispaa, Mheshimiwa Bashungwa amesema kuwa, Manispaa ya Shinyanga imeongoza kwa kukusanya mapato kwa asilimia 125 ya makisio yake ya mwaka ikifuatiwa na Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni na Ubungo asilimia 118 na Halmashauri ya Manispaa ya Moshi asilimia 117.

“Katika kundi hili Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara imekuwa ya mwisho kwa kukusanya asilimia 78 ya makisio ya mwaka ikifuatiwa na Halmashauri ya Manispaa ya Lindi asilimia 90 na Manispaa ya Morogoro asilimia 91,”amefafanua Mheshimiwa Waziri Bashungwa.

Akizungumzia kwa upande wa Halmashauri ya Mji wa Mbulu amesema kuwa, imeongoza kwa kukusanya asilimia 140 ya makisio ya mwaka ikifuatiwa na Halmashauri ya Mji wa Mafinga asilimia 129 na Halmashauri ya Mji wa Ifakara asilimia 125.

Aidha, Halmashauri ya Mji wa Nanyamba imekuwa ya mwisho kwa kukusanya asilimia 71 ya makisio ya mwaka ikifuatiwa na Halmashauri za Mji wa Korogwe asilimia 84 na Halmashauri ya Mji wa Geita asilimia 88.

Halmashauri ya Mji wa Mbulu imeongeza ufanisi kwani kwa kipindi cha miaka mitatu mfululizo imekuwa ikishika nafasi ya mwisho kwenye Halmashauri za Miji kwa kukusanya chini ya Shilingi Bilioni moja kwa mwaka.

Kwa upande wa halmashauri za wilaya, amesema kuwa, Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha imeongoza kwa kukusanya asilimia 247 ya makisio ya mwaka ikifuatiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Mlele asilimia 185 na Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro asilimia 158.

Aidha, Halmashauri ya Wilaya ya Bumbuli imekuwa ya mwisho kwa kukusanya asilimia 58 ya makisio ya mwaka ikifuatiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe asilimia 67 ya makisio ya mwaka na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda asilimia 70.

Chanzo - Dira Makini blog

Share:

RAIS WA MAREKANI JOE BIDEN ATOA KAULI NZITO JUU YA KIFO CHA KIONGOZI WA KUNDI LA KIGAIDI LA AL QAEDA


Ayman al- Zawahiri akiwa na aliyekuwa Kiongozi wa kundi la Al-Qaeda Osama Bin Laden
Ayman al-Zawahiri aliyekuwa kiongozi wa kundi la lkigaidi la Al- Qaeda

***
RAIS wa Marekani Joe Biden amelihutubia Taifa hilo na kutoa kauli nzito juu ya kifo cha kiongozi wa kundi la kigaidi la Al Qaeda Ayman al-Zawahiri, aliyeuawa na ndege ya Marekani isiyokuwa na Rubani.

Rais Biden amesema kuwa kifo cha al- Zawahiri ni malipo ya unyama alioufanya kwa wananchi wa Taifa hilo kufuatia kuhusika katika utekelezaji wa shambuliola kigaidi la Septemba 11 mwaka 2001 ambalo liliua zaidi ya raia 3000 nchini humo.

Rais wa Marekani Joe Biden

“Kiongozi wa ugaidi hayupo tena.” Alinukuliwa akisema Rais Biden ambaye aliendelea kwa kusisitiza kuwa kifo cha gaidi huyo kinarudisha tena faraja kwa familia za wahanga wa shambulio la Septemba 11.

Rais huyo wa Marekani amesisitiza kuwa Afghanistan haitakuwa tena makazi ya ugaidi baada ya shambulio hilo kutekelezwa ikiwa ni mwaka mmoja tangu vikosi vya Marekani vindoke nchini humo.

Aidha kiongozi huyo wa kundi la kigaidi ambaye ana asili ya Misri aliuawa majira ya asubuhi wakati akiwa katika nyumba yake kwenye mji wa Kabul ambapo kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Rais Biden ni kwamba hakuna mtu mwingine yeyote yule kutoka katika familia ya al- Zawahiri aliyeathirika au kujeruhiwa katika shambulio hilo.


Al-Zawahiri aliuawa vipi?

Maafisa wa Marekani wamesema Zawahiri alikuwa amesimama kwenye veranda ya nyumba yake ya mafichoni. Ghafla, ndege isiyokuwa na rubani- inayofahamika kama drone- ikadondosha makombora mawili.


Taarifa inasema kuwa kombora lilimpiga Zawahiri ambaye alikuwa amesimama nyumbani kwake.


Ndugu wengine wa familia ya Ayman Al-Zawahiri walikuwepo pamoja naye katika eneo hilo, lakini hakuna mtu mwingine aliyeuawa wala kujeruhiwa katika shambulio hilo, na kiongozi wa Al-Qaeda akafa mara moja pale peke yake, maafisa walisema.
Share:

BIMA YA KILIMO YA NBC YAWAVUTIA WADAU WA KILIMO MAONESHO YA NANENANE MBEYA


Mkurugenzi wa Wateja wadogo wa Benki ya NBC, Elibariki Masuke (Kulia) akibadilishana mawazo na Mkurugenzi wa Benki Kuu Tanzania tawi la Mbeya Bw Ibrahimu Malogoi alipotembelea banda la maonesho ya kilimo la benki ya NBC inayoshiriki Maonesho ya Kilimo Nanenane yanayofanyika katika Uwanja wa John Mwakangale mkoani Mbeya.


Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo wadogo, Lariba na wakulima kutoka Benki ya NBC, Bw Raymond Urassa (kulia) akibadilishana mawazo na wadau wa kilimo waliotembelea banda la maonesho ya kilimo la benki hiyo inayoshiriki Maonesho ya Kilimo Nanenane yanayofanyika katika Uwanja wa John Mwakangale mkoani Mbeya.


Meneja wa Benki ya NBC Tawi la Mbeya Bi Asia Mselemu (kulia) akibadilishana mawazo na wadau wa kilimo waliotembelea banda la maonesho ya kilimo la benki hiyo inayoshiriki Maonesho ya Kilimo Nanenane yanayofanyika katika Uwanja wa John Mwakangale mkoani Mbeya.


Maofisa wa benki ya NBC wakitoa ufafanuzi kuhusu huduma zinazotolewa na benki hiyo kwa wadau mbalimbali waliotembelea banda la maonesho ya kilimo la benki hiyo inayoshiriki Maonesho ya Kilimo Nanenane yanayofanyika katika Uwanja wa John Mwakangale mkoani Mbeya.


Timu ya maofisa wa benki ya NBC wakiongozwa na Mkurugenzi wa Wateja wadogo wa Benki ya NBC, Elibariki Masuke (wa tano kulia), Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo wadogo, Lariba na wakulima kutoka Benki ya NBC, Bw Raymond Urassa (wa tano kushoto) na Meneja wa Benki ya NBC Tawi la Mbeya Bi Asia Mselemu (wan ne kulia) wakiwa kwenye picha ya pamoja kwenye banda la maonesho ya kilimo la benki hiyo inayoshiriki Maonesho ya Kilimo Nanenane yanayofanyika katika Uwanja wa John Mwakangale mkoani Mbeya.

.....................................

Na Mwandishi Wetu-Mbeya

Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imeendelea kung’ara kwenye Maonesho ya Kilimo Nanenane yanayofanyika katika Uwanja wa John Mwakangale mkoani Mbeya, huku huduma ya Bima ya Kilimo inayotolewa na benki hiyo kwa wakulima ikiwa ni moja ya vivutio vikubwa miongoni mwa washiriki wanaotembelea maonesho hayo.

Akizungumza kwenye maonesho hayo yaliyozinduliwa jana na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango, Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo wadogo, Lariba na wakulima kutoka Benki ya NBC, Bw Raymond Urassa alisema ushiriki wa benki hiyo kwenye maonesho hayo ni muendelezo wa jitihada zake za kuendelea kujiweka karibu zaidi na wadau wa sekta hiyo muhimu.

“Kupitia Maonesho haya tunapata fursa ya kutangaza huduma zetu zinazohusiana na sekta nzima ya kilimo pamoja na kupokea mrejesho wa huduma hizo kutoka kwa wakulima.’’

Alisema ushiriki wa benki hiyo kwenye sekta ya kilimo unahusisha mkakati mkubwa wa benki hiyo unaolenga kuinua sekta ya kilimo nchini unaofahamika kama ‘NBC Shambani’ unaohusisha mnyororo wote wa sekta ya kilimo kuanzia kwa mkulima, mchakataji wa mazao ya kilimo hadi msambazaji.

“Zaidi pia tunalenga kuhakikisha tunashirikiana vema na serikali katika kutimiza adhma ya msingi kabisa ya kuhakikisha tunaongeza kwa kasi ukuaji wa sekta ya kilimo nchini ikiwa ni sambamba na kuboresha maisha ya wakulima wenyewe,’’ alibainisha.

Akizungumzia baadhi ya huduma zinazotolewa na benki hiyo mahususi kwa wakulima Bw Urassa aliitaja huduma ya Bima kwa wakulima inayotolewa na benki hiyo kwa kushirikiana na kampuni ya Bima ya Jubilee Insurance inayolenga kuwalinda wakulima, wavuvi na wafugaji nchini dhidi ya hasara pindi wanapopata majanga mbalimbali yanayoweza kuathiri uzalishaji wao.

“Benki ya NBC tuinatambua vema sekta ya kilimo na zaidi tunatambua mchango wa wa wakulima katika uchangiaji wa uchumi wa nchi na kwa msingi huu tumeona ni vema kuja na Bima ya mazao kwa wakulima. Katika kuthibitisha ufanisi wa huduma hii, ni hivi karibuni tu kwa kushirikiana na wenzetu kampuni ya Bima ya Jubilee Insurance tuliwafidia wakulima wa tumbaku mkoani Tabora ambao mazao yao yaliathiriwa na hali ya hewa,’’ alibainisha.

Zaidi, aliongeza kuwa benki hiyo pia inawawezesha wakulima kwa kuwapatia pembejeo za kilimo kwenye baadhi ya mazao hususani yale ya kimkakati ikiwemo pamba, kahawa na tumbaku lengo likiwa ni kuongeza tija kwenye sekta hiyo muhimu.

“Kupitia mpango wetu wa NBC Shambani tumekuwa tukishirikiana na wadau mbalimbali katika kutoa mikopo mbalimbali kwa wakulima ikiwemo ya zana mbalimbali za kilimo ikiwemo matrekta na mashine nyingine nyingi,’’ alitaja huku akiwaomba wadau mbalimbali wa kilimo waliohudhuria maonesho hayo kutembelea banda la benki hiyo ili kupata ufafanuzi na huduma mbalimbali zinazohusiana na sekta hiyo.
Share:

RAIS WA ZAMBIA MHE.HAKAINDE HICHILEMA AWASILI NCHINI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Hakainde Hichilema mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Terminal one Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya ziara ya siku moja nchini

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa amesimama pamoja na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Hakainde Hichilema wakati Nyimbo za Taifa (Tanzania na Zambia) zikipigwa mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Terminal one Jijini Dar es Salaam


Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Hakainde Hichilema akikagua Gwaride la Heshima lililoandaliwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Terminal one Jijini Dar es Salaam


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Hakainde Hichilema wakati wakisalimiana na viongozi mbalimbali waliofika kwenye mapokezi katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Terminal one Jijini Dar es Salaam.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Hakainde Hichilema wakati wakiangalia vikundi mbalimbali vya ngoma za asili na matarumbeta vilivyokuwa vikitoa burudani wakati wa mapokezi katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Terminal one Jijini Dar es Salaam


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Hakainde Hichilema mara baada ya kuwasili katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) Terminal one Jijini Dar es Salaam.

PICHA NA IKULU
Share:

HALMASHAURI 100 ZAKUSANYA MAPATO YA NDANI KWA 100%

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Mhe Innocent Bashungwa akizungumza na waandishi wa habari wakati akitoa taarifa kuhusu Mapato na Matumizi ya Ndani ya Halmashauri kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 leo Agosti 2,2022 Jijini Dar es Salaam
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Mhe Innocent Bashungwa (katikati) akizungumza na waandishi wa habari wakati akitoa taarifa kuhusu Mapato na Matumizi ya Ndani ya Halmashauri kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 leo Agosti 2,2022 Jijini Dar es Salaam Katibu Mkuu mpya Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Prof. Riziki Shemdoe akizungumza na wakuu wa Mikoa pamoja na Makatiibu Tawala wa Mkoa wakati wakitoa taarifa kuhusu Mapato na Matumizi ya Ndani ya Halmashauri kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 leo Agosti 2, 2022 Jijini Dar es Salaam Wakuu wa Mikoa wakifuatilia mkutano wa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Mhe Innocent Bashungwa wakati akitoa taarifa kuhusu Mapato na Matumizi ya Ndani ya Halmashauri kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 leo Agosti 2, 2022 Jijini Dar es Salaam Wakuu wa Mikoa wakifuatilia mkutano wa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Mhe Innocent Bashungwa wakati akitoa taarifa kuhusu Mapato na Matumizi ya Ndani ya Halmashauri kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 leo Agosti 2, 2022 Jijini Dar es Salaam

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

****************************

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Mhe Innocent Bashungwa amesema katika mwaka wa fedha 2021/2022 Halmashauri 100 zimekusanya mapato ya ndani kwa asilimia 100 au zaidi ya lengo la mwaka.

 Ameyasema hayo leo Agosti 2 , 2022 Jijini Dar-es-Salaam wakati akitoa taarifa kuhusu Mapato na Matumizi ya Ndani ya Halmashauri kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022.

Bashungwa amesema, Halmashauri 78 zimekusanya kati ya asilimia 80 hadi asilimia 99, na Halmashauri 7 zimekusanya kati ya asilimia 58 hadi 79. Halmashauri zilizofikia malengo ya mwaka zimeongezeka kutoka Halmashauri 57 katika mwaka wa fedha 2020/21, hadi kufikia Halmashauri 100 katika mwaka wa fedha 2021/22.


Amefafanua kuwa ulinganisho wa ufanisi wa ukusanyaji wa mapato ya ndani, kwa kigezo cha asilimia ya makusanyo, unaonesha kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Kibaha imeongoza katika Halmashauri zote kwa kukusanya asilimia 247 ya makisio yake ya mwaka, ikifuatiwa na Halmashauri za Wilaya ya Mlele asilimia 185, na Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro asilimia 158.


Vilevile, Waziri Bashungwa amesema , Halmashauri ya Wilaya ya Bumbuli imekuwa ya mwisho kwa kukusanya asilimia 58 ya makisio yake ya mwaka, ikifuatiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe asilimia 67, na Halmashauri ya Wilaya ya Bunda asilimia 70 ya makisio yake ya mwaka.

Ameendelea kusema kuwa katika kuzipima Halmashauri zote kwa Kigezo cha wingi wa mapato (pato ghafi), jumla ya Halmashauri 35 zimekusanya zaidi ya Shilingi Bilioni 5. Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imekusanya mapato mengi zaidi kuliko Halmashauri zote, kwa kukusanya Shilingi Bilioni 75.3 ikifuatiwa na Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni Shilingi Bilioni 47.3, na Halmashauri ya jiji la Dodoma Shilingi Bilioni 45.1.


Bashungwa amesema, Halmashauri 4 zimekusanya chini ya Shilingi Bilioni 1 ambapo Halmashauri ya Wilaya ya Bumbuli imekua ya mwisho kwa kukusanya Shilingi Milioni 599.7, ikifuatiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma Shilingi Milioni 692.1, Halmashauri ya Wilaya ya Madaba Shilingi Milioni 792.3, na Halmashauri ya Wilaya ya Buhigwe Shilingi Milioni 880.2.

Aidha, Halmashauri 4 zilizokusanya chini ya shilingi bilioni 1 zimeonekana kuongeza ufanisi katika ukusanyaji wa mapato. na haakuna Halmashauri iliyokusanya chini ya asilimia 50 kwa miaka yote miwili mfululizo
Share:

PAKUA APP YA MALUNDE 1 BLOG...Imeboreshwa zaidi

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger