Sunday 3 July 2022

BENKI YA CRDB YAKABIDHI PIKIPIKI 8 KWA WARAJISI WA USHIRIKA



Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi Said Pamui (kulia) akimkabidhi Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe ufunguo wa Pikipiki ishara ya kukabidhi pikipiki nane (8) zenye thamani ya shilingi Milioni 24 .5 zitakazo kwenda kutumiwa na warajisi kama nyenzo ya usafiri.

Na Mwandishi wetu  - Malunde 1 blog
Benki ya CRDB imekabidhi pikipiki nane (8)zenye thamani ya shilingi Milioni 24 .5 zitakazo kwenda kutumiwa na warajisi  wa vyama vya ushirika kama nyenzo ya usafiri.

Akikabidhi pikipiki hizo Jumamosi Julai 2,2022 kwa Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe katika maadhimisho ya Siku ya Ushirika duniani kwa mwaka 2022 ambayo kitaifa yamefanyika Mkoani Tabora ,Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi Said Pamui amesema pikipiki hizo zitakwenda kuwasaidia warajisi kuvitembelea vyama vya ushirika kwa urahisi katika maeneo yao pengine hata kwa mshirika mmoja mmoja.


Pamui amesema benki ya CRDB imekuwa na historia kubwa ya ushirika hivyo itahakikisha inaendelea kushirikiana na serikali ya awamu ya sita katika kuleta mageuzi makubwa ya kilimo tija kwa wakulima nchini.


Awali meneja wa biashara CRDB Kanda ya Magharibi Jumanne Wagana akimweleza Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe wakati alipotembelea banda la benki hiyo amesema mpaka sasa benki ya CRDB imetoa kiasi cha shilingi bilioni  494 katika kuinyanyua sekta ya kilimo.

Hata hivyo amesema benki ya CRDB imepunguza kiwango cha riba kwa wakulima kupitia kilimo kutoka 20% mpaka kufikia 9%.


Waziri Bashe ameipongeza benki hiyo huku akibainisha kuwa ni mwanzo mzuri kwa taasisi za kifedha kuanza kuwapa thamani wakulima.

Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi Said Pamui (kulia) akizungumza wakati akimkabidhi Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe pikipiki nane (8) zenye thamani ya shilingi Milioni 24 .5 zitakazo kwenda kutumiwa na warajisi kama nyenzo ya usafiri.
Muonekano wa pikipiki nane (8) zenye thamani ya shilingi Milioni 24 .5 zilizotolewa na Benki ya CRDB kwa ajili ya warajisi kama nyenzo ya usafiri.
Muonekano wa pikipiki nane (8) zenye thamani ya shilingi Milioni 24 .5 zilizotolewa na Benki ya CRDB kwa ajili ya warajisi kama nyenzo ya usafiri.
Muonekano wa pikipiki nane (8) zenye thamani ya shilingi Milioni 24 .5 zilizotolewa na Benki ya CRDB kwa ajili ya warajisi kama nyenzo ya usafiri.

Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe akisaini kitabu katika Banda la Benki ya CRBD

Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe akizungumza katika Banda la Benki ya CRBD


Share:

Saturday 2 July 2022

YANGA YAENDELEA KUCHEKA, YANYAKUA KOMBE LA ASFC


NA EMMANUEL MBATILO

Kwa mara nyingine tena Yanga inabeba ubingwa msimu huu mara baada ya kufanikiwa kunyakua kombe la Azam Sports Federation Cup kwa kuwachapa Coastal Union kwa mikwaju ya penati 4-1.

Fainali hii imekuwa ni yakuvutia hasa licha ya Coastal Union kucheza kandanda safi kwa vipindi vyote kwani waliweza kupachika mabao mazuri ambayo hayakusaidia kabisa kuwatawaza mabingwa.

Abdul Sopu ndiye tuseme ni mchezaji ambaye amekuwa kivutio kwa yeyote ambaye ameangalia mpira huu mpaka mwisho kwani ameweza kupachika bao tatu peke yake kwenye mchezo huo.

Kwenye mchezo huo ambao ulipigwa kwenye dimba la Sheikh Amri Abeid Jijin Arusha, Coastal Union walianza kupata bao kupitia kwa mshambuliaji wao hatari Abdul Sopu dakika ya 11 ya mchezo na kwenda mapumziko wakiwa wanaongoza.

Kipindi cha pili Yanga Sc ilisawazisha bao kupitia kwa Feisal Salumu na baadae Heritie Makambo kupachika bao la pili dakika ya 81 kabla ya Abdul Sopu kusawazisha kwa upande wa Coastal Unions dakika za lala salama.

Baada ya dakika 90 kumalizika ziliongezwa dakika 30 kutafuta mshindi wa fainali hiyo ambapo Sopu tena aliweza kuwalaza Yanga sc kwa bao safi kabisa akimtoka beki wa Yanga Kibwana Shomari lakini baadae Nkane aliweza kusawazisha bao na kwenda matuta.

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JULAI 2,2022

Magazetini leo Jumamosi July 2 2022




















Share:

Friday 1 July 2022

COSTECH KUENDELEA KUWEKA MAZINGIRA WEZESHI KWA WABUNIFU NCHINI.

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania -COSTECH Dkt Amos Nungu akizungumza na waandishi wa habari wakati alipotembelea na kuzungumza kwenye Banda la Tume hiyo katika Maonyesho ya 46 ya kimataifa ya Biashara Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania -COSTECH Dkt Amos Nungu akitembelea na kujionea kazi za wabunifu mbalimbali katika Banda la Tume hiyo katika Maonyesho ya 46 ya kimataifa ya Biashara Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es salaam. Watumishi wa Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania – COSTECH kwenye Banda la Tume hiyo katika Maonyesho ya 46 ya kimataifa ya Biashara Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es salaam.Baadhi ya wananchi wakiwemo wanafunzi waliojitokeza kujionea na kujifunza kwenye Banda la Tume hiyo katika Maonyesho ya 46 ya kimataifa ya Biashara Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es salaam.

Picha ya pamoja

..............................

NA MUSSA KHALID

Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia -COSTECH imesema itaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wabunifu mbalimbali nchini ili kusaidia bunifu zao ziweze kwenda sokoni.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, Dkt Amos Nungu wakati alipotembelea na kuzungumza kwenye Banda la Tume hiyo katika Maonyesho ya 46 ya kimataifa ya Biashara Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es salaam.

"Wabunifu Rai yangu kwanza waendee kubuni suluhisho kwenye changamoto ambazo zipo lakini pia wafikirie jambo la kibiashara ili wasikose fursa mbalimbali zinazojitokeza"amesema Dkt Nungu

Dkt Nungu amefafanua kuwa Serikali itaendelea kuunga mkono juhudi za vijana wabunifu nchini ili kusaidia kurahisisha matumizi ya teknolojia za ndani na kuachana na utamaduni wa kuagiza bidhaa kutoka Nje.

Aidha, ameongeza kuwa kwa Mwaka huu 2022 wameweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha bunifu mbalimbali kutoka sekta isiyo rasmi wanapata nafasi ya kuzitangaza bunifu hizo kupitia maonesho ya sabasaba zinawanufaisha wabunifu pamoja na kutoa suluhisho kwa wanachi katika maisha yao.

Kwa upande wake Elia Kinshaga kutoka kampuni inayohusika na Ubunifu DTBi iliyopo chini ya Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) amewahimiza vijana kujikita katika ubunifu wa teknolojia ili kuweza kurahisisha kazi na mawasilino.

Hata hivyo vijana wametakiwa kuonesha bunifu zenye tija kwenye mfumo ili kuweza kupata nafasi kwa wakati pindi fursa zinapojitokeza ili kuweza kutatua matatizo yanayoikabli jamii.

Share:

ATUPWA JELA KWA KUMPIGA JIWE LA JICHO NA KUMSABISHIA UPOFU MWANAFUNZI


Yusufu Chacha. 

Mahakama ya Wilaya ya Serengeti mkoani Mara imemhukumu, Yusufu Chacha(22) mkazi wa kijiji cha Nyansurura kwenda jela miaka mitatu na kulipa faini ya Sh milioni 1 baada ya kukutwa na hatia ya kumpiga na jiwe na kumsababishia upofu mwanafunzi wa kidato cha nne, Esther Chacha(18).


Hukumu hiyo imetolewa jana Juni 30, mwaka huu na Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Judith Semkiwa, baada ya kujiridhisha na hoja za ushahidi zilizowasilishwa mahakamani hapo pasi na shaka.


“Mahakama baada ya kuzingatia maelezo ya pande zote mbili bila kuacha shaka yoyote inakuhukumu kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela pamoja na kulipa faini Sh milioni 1 kwa kosa la kumpiga jiwe na kumsababishia upofu wa jicho la kushoto, Esther Chache(18) mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya Sekondari ya Nyansurura,” amesema Hakimu Semkiwa.


Upande wa Mashtaka ukiongozwa na Mwendesha Mashtaka, Faru Maengela ulikuwa na mashahidi sita akiwemo mlalamikaji huku upande wa mlalamikiwa ukiwa na mashahidi watatu ambapo kati yao mmoja alikataa kutoa ushahidi wake kwa kile alichoeleza kuwa mazingira ya kosa hayafahamu vizuri.


Aidha, upande wa mshtakiwa mmoja wa mashahidi ulitoa ushahidi ambao ulitofautiana na kwa maelezo kuwa hata jina la mshtakiwa halijui huku shahidi wa pili alidai kuwa siku ya tukio yeye alikuwa nyumbani kwake na familia na kwamba alishanga kuitwa mahakamani kutoa ushahidi.


Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, katika kesi hiyo ya jinai namba 48 ya mwaka 2021, Yusufu Chacha(22) Novemba 1, 2020 akiwa katika sherehe ya mahafali ya kidato cha nne katika kijiji cha Nyansurura alimpiga na jiwe, Esther Chacha katika jicho lake la kushoto na kuanguka chini alipokuwa akicheza muziki.


Chanzo - Mtanzania
Share:

TAARIFA WALIOITWA KAZINI AJIRA ZA KADA YA AFYA




WIZARA ya Afya imetoa orodha ya watumishi walioitwa kazini kufuatia waombaji wa ajira za kada za afya zilizotangazwa kwenye tovuti ya wizara ajira.moh.go.tz tarehe 16 Aprili, 2022 hadi tarehe 03 Mei, 2022.

Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Juni 30, 2022 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya,Prof. Abel N. Makubi ambapo amefafanua kuwa, hatua hiyo imefikiwa baada ya zoezi la uchambuzi wa maombi ya kazi yaliyopokelewa kukamilika.

BOFYA <<HAPA>> KUTAZAMA 

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JULAI MOSI, 2022


















Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger