Saturday 2 July 2022

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JULAI 2,2022

Magazetini leo Jumamosi July 2 2022




















Share:

Friday 1 July 2022

COSTECH KUENDELEA KUWEKA MAZINGIRA WEZESHI KWA WABUNIFU NCHINI.

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania -COSTECH Dkt Amos Nungu akizungumza na waandishi wa habari wakati alipotembelea na kuzungumza kwenye Banda la Tume hiyo katika Maonyesho ya 46 ya kimataifa ya Biashara Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania -COSTECH Dkt Amos Nungu akitembelea na kujionea kazi za wabunifu mbalimbali katika Banda la Tume hiyo katika Maonyesho ya 46 ya kimataifa ya Biashara Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es salaam. Watumishi wa Tume ya Sayansi na Teknolojia Tanzania – COSTECH kwenye Banda la Tume hiyo katika Maonyesho ya 46 ya kimataifa ya Biashara Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es salaam.Baadhi ya wananchi wakiwemo wanafunzi waliojitokeza kujionea na kujifunza kwenye Banda la Tume hiyo katika Maonyesho ya 46 ya kimataifa ya Biashara Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es salaam.

Picha ya pamoja

..............................

NA MUSSA KHALID

Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia -COSTECH imesema itaendelea kuweka mazingira wezeshi kwa wabunifu mbalimbali nchini ili kusaidia bunifu zao ziweze kwenda sokoni.

Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, Dkt Amos Nungu wakati alipotembelea na kuzungumza kwenye Banda la Tume hiyo katika Maonyesho ya 46 ya kimataifa ya Biashara Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es salaam.

"Wabunifu Rai yangu kwanza waendee kubuni suluhisho kwenye changamoto ambazo zipo lakini pia wafikirie jambo la kibiashara ili wasikose fursa mbalimbali zinazojitokeza"amesema Dkt Nungu

Dkt Nungu amefafanua kuwa Serikali itaendelea kuunga mkono juhudi za vijana wabunifu nchini ili kusaidia kurahisisha matumizi ya teknolojia za ndani na kuachana na utamaduni wa kuagiza bidhaa kutoka Nje.

Aidha, ameongeza kuwa kwa Mwaka huu 2022 wameweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha bunifu mbalimbali kutoka sekta isiyo rasmi wanapata nafasi ya kuzitangaza bunifu hizo kupitia maonesho ya sabasaba zinawanufaisha wabunifu pamoja na kutoa suluhisho kwa wanachi katika maisha yao.

Kwa upande wake Elia Kinshaga kutoka kampuni inayohusika na Ubunifu DTBi iliyopo chini ya Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) amewahimiza vijana kujikita katika ubunifu wa teknolojia ili kuweza kurahisisha kazi na mawasilino.

Hata hivyo vijana wametakiwa kuonesha bunifu zenye tija kwenye mfumo ili kuweza kupata nafasi kwa wakati pindi fursa zinapojitokeza ili kuweza kutatua matatizo yanayoikabli jamii.

Share:

ATUPWA JELA KWA KUMPIGA JIWE LA JICHO NA KUMSABISHIA UPOFU MWANAFUNZI


Yusufu Chacha. 

Mahakama ya Wilaya ya Serengeti mkoani Mara imemhukumu, Yusufu Chacha(22) mkazi wa kijiji cha Nyansurura kwenda jela miaka mitatu na kulipa faini ya Sh milioni 1 baada ya kukutwa na hatia ya kumpiga na jiwe na kumsababishia upofu mwanafunzi wa kidato cha nne, Esther Chacha(18).


Hukumu hiyo imetolewa jana Juni 30, mwaka huu na Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo, Judith Semkiwa, baada ya kujiridhisha na hoja za ushahidi zilizowasilishwa mahakamani hapo pasi na shaka.


“Mahakama baada ya kuzingatia maelezo ya pande zote mbili bila kuacha shaka yoyote inakuhukumu kutumikia kifungo cha miaka mitatu jela pamoja na kulipa faini Sh milioni 1 kwa kosa la kumpiga jiwe na kumsababishia upofu wa jicho la kushoto, Esther Chache(18) mwanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya Sekondari ya Nyansurura,” amesema Hakimu Semkiwa.


Upande wa Mashtaka ukiongozwa na Mwendesha Mashtaka, Faru Maengela ulikuwa na mashahidi sita akiwemo mlalamikaji huku upande wa mlalamikiwa ukiwa na mashahidi watatu ambapo kati yao mmoja alikataa kutoa ushahidi wake kwa kile alichoeleza kuwa mazingira ya kosa hayafahamu vizuri.


Aidha, upande wa mshtakiwa mmoja wa mashahidi ulitoa ushahidi ambao ulitofautiana na kwa maelezo kuwa hata jina la mshtakiwa halijui huku shahidi wa pili alidai kuwa siku ya tukio yeye alikuwa nyumbani kwake na familia na kwamba alishanga kuitwa mahakamani kutoa ushahidi.


Kwa mujibu wa hati ya mashtaka, katika kesi hiyo ya jinai namba 48 ya mwaka 2021, Yusufu Chacha(22) Novemba 1, 2020 akiwa katika sherehe ya mahafali ya kidato cha nne katika kijiji cha Nyansurura alimpiga na jiwe, Esther Chacha katika jicho lake la kushoto na kuanguka chini alipokuwa akicheza muziki.


Chanzo - Mtanzania
Share:

TAARIFA WALIOITWA KAZINI AJIRA ZA KADA YA AFYA




WIZARA ya Afya imetoa orodha ya watumishi walioitwa kazini kufuatia waombaji wa ajira za kada za afya zilizotangazwa kwenye tovuti ya wizara ajira.moh.go.tz tarehe 16 Aprili, 2022 hadi tarehe 03 Mei, 2022.

Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa Juni 30, 2022 na Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya,Prof. Abel N. Makubi ambapo amefafanua kuwa, hatua hiyo imefikiwa baada ya zoezi la uchambuzi wa maombi ya kazi yaliyopokelewa kukamilika.

BOFYA <<HAPA>> KUTAZAMA 

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JULAI MOSI, 2022


















Share:

Thursday 30 June 2022

OJADACT YAADHIMISHA SIKU YA KUPIGA VITA DAWA ZA KULEVYA NA USAFIRISHAJI HARAMU WA BINADAMU



Mwandishi wetu - Mwanza.

Chama Cha Waandishi wa Habari wa Kupiga Vita Matumizi ya Dawa za Kulevya na Uhalifu Tanzania (OJADACT )kwa kushirikiana na ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza imeadhimisha siku ya kupiga vita dawa za kulevya na usafirishaji haramu wa binadamu kwa kuwahimiza waandishi wa habari kutumia kalamu zao kuielimisha jamii athari za dawa za kulevya.

Mgeni rasmi ambaye pia ni Mganga Mkuu wa Mwanza Dkt. Thomas Rutachunzibwa amesisitiza waandishi wa habari kuwa daraja la kuelimisha jamii juu ya athari za dawa.


Dkt. Rutachunzibwa pia ameishukuru OJADACT kwa kuandaa maadhikisho hayo kwa kuwaleta waandishi pamoja na kuwapitisha kwenye kujifunza athari za dawa za kulevya na kusema kitendo cha OJADCT kuwepo Mwanza kunasaidia kwenye mapambano ya dawa za kulevya.


Mwenyekiti wa OJADACT Bwana Edwin Soko amesema kuwa kauli mbiu ya mwaka huu ni tukubaliane na dawa za kulevya kwa ustawi wa jamii itumike kwenye kuielimisha jamii juu ya athari za dawa za kulevya nchini.

Pia mtoa mada Dkt. Eunice Masangu amesema kuwa, kwa sasa hospitali ya Mkoa ya Sekeouture inatoa huduma ya methadone kwa watumiaji wa dawa za kulevya za iroine kwa Mikoa ya Kanda ya Ziwa.

OJADACT inajikita kwenye mapambano ya dawa za kulevya nchini hivyo kila mwaka inaadhimisha siku hiyo.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger