Tuesday 28 June 2022

LG SMART HOME APPLIANCES DIGITIZING TANZANIA HOMES; SAVES USERS TIME AND ENERGY

• Top benefits of the smart home appliances include offering ease and convenience to use for TVs and refrigerators, improved performance through Artificial Intelligence (AI) technology for the washers and energy-saving for the air conditioners.

• latest core technology featuring intelligence applications hailed for helping households conserve energy and water, being environmentally friendly while being easily usable, thus promoting key sustainable development goals

DAR ES SALAAM, TANZANIA, XX JUNE 2022… 

Tanzanians can now lead an easier, more practical and convenient life with LGs recently introduced smart home appliances aimed at complementing a busy, hectic schedule and challenging daily chores.

Ranging from among others refrigerators, microwaves, televisions and washing machines, the smart home appliances seek to digitize Tanzanians’ homes turning them into an interconnected network set up that allows them to control their home appliances remotely and/or by voice demands.

Commenting on the recent innovations and smart home products, LG Electronics East Africa Managing director Sa young Kim said, “the move to digitize living rooms, the kitchen and any other room in Tanzania homes is inspired by our commitment to priorities convenience and comfort for our customers. For all of us to achieve this, there must be enough supply of smart home appliances which we have made available”.

According to a recent survey by LG ThinQ Smart Home Report, 17.3 % of surveyed users selected energy saving as the biggest smart home benefit. Other top benefits mentioned in the survey included ease and convenience to use for TVs and refrigerators and improved performance through Artificial Intelligence (AI) technology for the washers and energy-saving for the air conditioners.

Among the key smart home appliances introduced by LG in the country include the Smart OLED TVs powered by advanced artificial intelligence technologies that make homes smart and convenient. The TVs have inbuilt AI processors that analyze on-screen content to adjust it to the best possible audio, picture and video by the user’s viewing environment.

Besides, the TVs have intelligent voice recognition feature that enables users to control them with simple commands. They also provide a home dashboard that displays the status of other smart home appliances in the home and notifies users of any situation that users should be aware of, such as the fridge door being open and the remaining time for the washing cycle to end.

To help with laundry, LG has stored up Smart washing machines such as the Vivace Washing machine and other (Artificial Intelligence Direct Drive) AI DD™ / DD washing machines which identify users’ laundry’s fabric type and recommend the best laundry course for it. They also troubleshoot minor issues quickly before they escalate.

For users who want to keep foods and fruits fresh for longer periods, LG has confirmed a lineup of smart Refrigerators designed to be connected to the user’s smartphone to control the refrigerator’s temperature, control Express Freeze, and receive any diagnostics of the user refrigerator and food expiration date notifications.

 This includes the LG Net 426(L) | Slim French Door Fridge, with InstaView Door-In-Door™ which with a compatible smartphone connected to the LG SmartThinQ™ app, users can remotely adjust temperature settings so the fridge is ready to accommodate a large shopping spree.

Other outstanding features include the modern French door with innovative storage options such as a folding Shelf that can be self-folded for storing taller items and the Slim SpacePlus™ Ice System that is built into the fridge door so users can utilise the whole top shelf.

According to Sa Young Kim, this latest core technology featuring intelligence applications helps households conserve energy, and water and are environmentally friendly while being easily usable, thus promoting key sustainable development goals.
END
 
Share:

Monday 27 June 2022

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JUNI 28,2022

























Share:

SIRI YA KUTOZEEKA MAPEMA


Mtu mwenye umri mkubwa zaidi duniani, Kiko Tanaka, alifariki akiwa na na umri wa miaka

Hapo zamani, maisha marefu yalionekana ni kitu kisichowezekana. Lakini sasa mambo yamebadilika. Je uzee kucheleweshwa au hata kuzuiwa? Je wale wenye umri wa zaidi ya miaka 100 wanasiri ambayo inaweza kumsaidia kula mtu kuishi miaka mingi?.


Ijumaa,Januari 2, 1903, mtoto mchanga wa kike anayeitwa Kiko Tanaka alizaliwa katika kijiji kidogo kilichopo katika kisiwa cha kusini mwa Japan. Katika mwaka huo huo, mashindano yam bio za baiskeli ya Tour de France yalianzishwa Paris na kampuni ya magari ya Ford iliuza gari lake la kwanza. Kiko Tanaka alifariki dunia Aprili akiwa na umri wa miaka 119, na alitambuliwa rasmi kama mtu mwenye umri mkubwa zaidi duniani.


Aliishi miaka yake ya mwisho ya maisha yake katika nyumba ya wazee, akiamka saa kumi na mbili asubuhi kila siku kufanya hesabu, kucheza michezo ya ndani ya nyumba, kula chokoleti na kunywa kahawa na soda.


Kuwapata watu wanaoishi miaka zaidi ya mia moja kama Koshi Tanaka sasa sio jambo lisilo la kawaida.

Chanzo - BBC SWAHILI

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU JUNI 27,2022


















Share:

Sunday 26 June 2022

SIMBA SC YASHINDWA KUFURUKUTA MBELE YA TANZANIA PRISONS


****************************

NA EMMANUEL MBATILO

KLABU ya Simba imeshindwa kufurukuta mbele ya Tanzania Prisons mara baada ya kupokea kichapo cha bao 1-0 mchezo ambao ulipigwa kwenye dimba la Sokoine mkoani Mbeya.

Simba Sc imecheza mchezo huo bila staa wao Sakho ambaye amefanya vizuri kwenye mechi za hivi karibuni kutokana na kupata majeruhi ya bega hivi karibuni na kufanya kukosa mchezo huo ambao haukuwa na faida kwao.

Tanzania Prisons imeshinda mchezo huu na kujiweka eneo zuri kuepuka kushuka daraja hivyo kusubiri mchezo wake unaofuata wa mwisho ambayo itaamua kama wataendela kusali kwenye ligi ama kushuka daraja.

Bao pekee la mchezo huo lilifungwa na nahodha wa Tanzania Prisons Benjamin Asukile dakika ya 54 ya mchezo ambaye aliingia kipindi cha pili .
Share:

Saturday 25 June 2022

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI JUNI 26,2022






Share:

ANUNUA JENEZA JIPYA LA MILIONI 1.2 AKIJIANDAA NA MAZISHI YAKE...ALISHANUNUA MENGINE MAWILI



Mzee mmoja kutoka kaunti ya Busia nchini Kenya amewaacha wenyeji vinywa wazi baada ya kujinunulia jeneza la tatu.

Alloise Otieng' Ominang'ombe mwenye umri wa miaka 87 amenunua jeneza jipya la thamani ya KSh 58,000  sawa na shilingi 1,218,000 za Tanzania na ambalo anatazamia kutumia kama gari lake la mwisho duniani.

Mzee huyo anatoka katika kijiji cha Kajoro huko Okatekok, eneo bunge la Teso Kusini kaunti ya Busia.

 Alikuwa amenunua majeneza mengine mwaka 2009 na 2012; hata hivyo alisema yalikuwa yamepitwa na wakati ikilinganishwa na mtindo wa sasa wa kuunda majeneza.

Aliambia runinga ya Citizen kwamba majeneza ya awali yatapasuliwa kuwa vipande vya kuni wakati wa mazishi yake, huku lile alilonunua jipya likitumika katika kumzika.

 "Mawili hayo yatapasuliwa vipande vipande ili vitumike kupika wakati wa mazishi yangu," alisema.

“Nataka hili liwe funzo kwa jamii yangu kwa ujumla. Unaweza kukosa mahitaji ya msingi ukiwa hai. Lakini ukifa, watu watachinja ng'ombe, watakununulia nguo nzuri na viatu wakati utakuwa umeenda kabisa. Ndiyo maana niliamua kupanga jinsi safari yangu ya mwisho itakavyokuwa inayolingana na hadhi yangu katika jamii,” aliongeza.

Katika taarifa sawia na hiyo aliyeishiwa nguvu huko Suna, kaunti ya Migori, jamaa aliyeonekana kuchoshwa na maisha alinunua jeneza nyeupe na buluu, na kulipeleka nje ya nyumba yake kisha akaingia na kujilaza ndani. Mzee huyo aliwaacha wengi vi nywa wazi wakishangaa ni vipi aliamua kufanya kitendo hicho cha ajabu.

Kulingana na Awino, alikuwa amechoshwa na mizozo ya kila mara baina yake, mkewe na wanawe na ndiposa akaamua kufanya kisa hicho cha kustaajabisha.

Akiwa amelewa kabisa, baba huyo wa watoto watatu alishtumu familia yake kwa kumsukuma ukutani huku akisema kila mara alitaka kujitoa uhai. Majirani zake walishtuka, wakatoka nje ya boma hilo mara moja na kurudi baadaye kumsihi Awino asijiue.

Chanzo - Tuko News
Share:

WANANCHI WATAKIWA KUCHUKUA HATUA KUKABILI UKATILI WA KIJINSIA


Mratibu wa vituo vya taarifa na maarifa kutoka TGNP Flora Ndaba akizungumza katika mdahalo wa kupinga ukatili wa klijinsia uliofanyika kijiji cha Titye wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma. (Picha zote na Fadhili Abdallah)
Mratibu wa vituo vya taarifa na maarifa kutoka TGNP Flora Ndaba akizungumza katika mdahalo wa kupinga ukatili wa klijinsia uliofanyika kijiji cha Titye wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma.
Polisi kata katika kata ya Titye wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma Mkaguzi wa polisi Bwire akizungumza katika mdahalo wa kupinga vitendo vya ukatili na unyanyasaji kijinsia uliofanyika kijiji cha Titye wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma
Polisi kata katika kata ya Titye wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma Mkaguzi wa polisi Bwire akizungumza katika mdahalo wa kupinga vitendo vya ukatili na unyanyasaji kijinsia uliofanyika kijiji cha Titye wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma
Viongozi wa kijiji na kata ya TITYE wakifuatilia mdahalo wa kupinga ukatli wa kijinsia ulioandaliwa na Mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP).
Wananchi wa kijiji cha Titye Halmashauri ya wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma wakifuatilia mdahalo wa kupinga ukatili wa kijinsia ulioandaliwa na TGNP.


Na Fadhili Abdallah,Kigoma

WITO umetolewa kwa jamii ya watanzania kuchukua hatua sasa katika kukabiliana na tatizo la ukatili wa kijinsia na watoto kwa kuamua kwa dhati kupambana na vitendo vya ukatili vinavyotokea kwenye maeneo yao.

Mratibu wa vituo vya taarifa na maarifa kutoka Mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP),Flora Ndaba alisema hayo katika mdahalo wa wananchi wa kupambana na ukatili uliofanyika kwenye kijiji cha Titye wilaya ya Kasulu mkoani Kigoma.

Mratibu huyo alisema kuwa serikali na mashirika yanasaidia kukabili jambo hilo kwa kusimamia sera, sheria na taratibu za kisheria lakini katika kuhakikisha matukio yanakoma jamii inapaswa kuwa ndiyo mtekelezaji mkuu kutokana na matukio hayo kutokea kwenye maeneo yao.

Mafunzo, elimu na uhamasishaji umeshafanyika sana lakini bado wananchi wanionyoshea kidole serikali wakati wanao wajibu na jukumu kubwa katika kusimamia ukomeshaji wa vitendo hivyo.

“Ukiangalia vitendo vya ubakaji, ulawiti, mimba za utotoni kwa wananfunzi, vipigo kwa wanawake na unyanyasaji mwingine vyote vinatokea kwa watu wa familia wenye mahusiano ambao ndiyo wanapaswa kuwa walinzi wa watoto na familia zao",alisema Flora Ndaba kutoka TGNP.

Alisema kuwa serikali na mashirika wanatoa elimu na kuhamasisha kutokomeza ukatili kwa sababu inataka kuwaelimisha kujua wajibu wao kwamba suala la ulinzi, matunzo na malezi ya familia yanaanza kwa baba na mama ambao wanapaswa kusimamia jukumu lao jambo ambalo litasaidia kukabili vitendo vya ukatili kwa kiasi kikubwa.

Kwa upande wake Afisa Maendeleo ya jamii Halmashauri ya wilaya Kasulu, Maria alisema kuwa familia kwa kutumia serikali za vijiji ndiyo msingi wa kuzuia ukatili wa kijinsia kwa kuweka mipango ambayo wataitekeleza na kuondoa changamoto hizo,

Pamoja na hilo Maria alisema kuwa utoaji wa taarifa kwa wanajamii kwenda kwenye vyombo vya ulinzi na serikali ni muhimu ili hatua ziweze kuchukuliwa lakini wananchi wamekuwa waoga kutoa taarifa na wakati mwingine kushiriki kuwaficha wahalifu ili wasichukuliwe hatua wengi wakiwa ndugu wa karibu wanaohusika na matukio hayo.

Hata hivyo kwa upande wao wananchi wa kijiji cha Titye akiwemo Mussa Ndofu ambao wamesema kuwa licha ya kuripotiwa kwa vitendo vya ukatili na mimba kwa wanafunzi lakini inashangaza kuona watuhumiwa wakikamatwa na baadaye kuachiwa bila kufanywa lolote.

Naye Isaya Haminimana alisema kuwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari wanapewa ujauzito na walimu lakini hakuna hatua zinazochukuliwa kwa wanafunzi kuacha masomo na walimu wanaendelea kufundisha bila kufanya lolote.
Share:

CHONGOLO - CHAGUENI VIONGOZI WATAKAOKIPAMBANIA CHAMA NA SERIKALI

Katibu Mkuu wa CCM Daniel Chongolo akizungumza

Na Fadhili Abdallah,Kigoma

 

KATIBU Mkuu wa CCM Daniel Chongolo amewataka wanachama wa CCM kuchagua viongozi ambao wenye dhamira ya dhati ya kukipambania chama hicho ambao wapo tayari kukilinda chama na serikali yake kwa jasho na damu.

Chongolo alisema hayo mkoani Kigoma akiwa njiani kuelekea nchini Burundi ambapo atafanya ziara ya siku tatu nchini humo ambapo pamoja na mambo mengine atafungua uwanja wa michezo na kituo cha kukuza vipaji unojulikana kama Nkurunzinza Peace Park Complex uliopo mkoa Makamba nchini Burundi.


Katibu huyo Mkuu wa CCM alisema kuwa katika uchaguzi huu wa viongozi wa ndani ya CCM ni lazima wapiga kura wazingatie kuchagua viongozi wenye mapenzi ya kweli kwa chama ambao ndiyo msingi wa viongozi wa serikali kwa siku zijazo hivyo wakati huu ni muhimu kwa wapiga kura kutoa mwelekeo wa umakini wa chama hicho.


“Ni lazima kuzingatia uchaguzi wa viongozi ambao kwa dhamira zao wanaonekana kuwa na dhamira za kuwatumikia wananchi, mkikosea sasa mtakuwa mmekosea kwa miaka yote hivyo umakini katika uchaguzi wa kiongozi anayefaa ufanyike sasa na kwa umakini mkubwa,”alisema Chongolo.


Alisema kuwa wapo wagombea wenye hila ambao wanawania nafasi za uongozi ndani ya chama kwa dhamira zao binafsi na kwamba ni vizuri wapiga kura wakaliona jambo hilo na kuwaweka kando wagombea hao.


Katibu huyo Mkuu wa CCM anafanya ziara nchini Burundi kwa Mwaliko wa Chama cha CNDD – FDD ambapo safari yake itamfikisha hadi Bujumbura mji mkuu wa Burundi ambako atakutana na viongozi wa chama hicho na serikali ya Burundi.


Chongolo alisema kuwa anafanya ziara sasa nchini Burundi baada ya Katibu Mkuu mwenzake wa CNDD – FDD, Reverien Ndikuriyo kuwa ameshafanya ziara za kichama nchini Tanzania mara tatu.

Share:

WAZIRI NDAKI AGAWA INJINI ZA BOTI KWA AJILI YA WAVUVI


Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki,akizungumza kabla ya kukabidhi Injini tatu za Boti zenye uwezo wa nguvu ya farasi 15 kwa wabunge wa majimbo ya Pangani, Mtwara Mjini na Iringa Vijijini ili ziweze kwenda kuwasaidia wavuvi katika shughuli zao za uvuvi ikiwa ni pamoja na ulinzi wa rasilimali za uvuvi, ambapo pia alisisitiza watumiaji wa injini hizo wazitumie kwa matumizi yaliyokusudiwa na si vinginevyo. Hafla iliyofanyika Jijini Dodoma.


Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Sekta ya Uvuvi), Dkt. Nazael Madala akitoa maelezo kuhusu malengo ya sekta katika kuwawezesha wavuvi kabla ya kumkaribisha Waziri wa Mifugo na Uvuvi kuzungumza na kukabidhi injini tatu za boti zenye uwezo wa nguvu ya farasi 15. Hafla iliyofanyika Jijini Dodoma.


Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso,akiipongeza Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Sekta ya Uvuvi) kwa kuipatia Jimbo lake la Pangani Injini moja ya Boti yenye uwezo wa nguvu ya farasi 15 kwa kuwa itakwenda kuwasaidia wavuvi katika shughuli zao za uvuvi lakini pia katika kulinda rasilimali za uvuvi. Hafla iliyofanyika Jijini Dodoma.


Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani kutoka Sekta ya Uvuvi, Prof. Mohammed Sheikh akielezea uwezo wa Injini tatu za Boti ambazo zina uwezo wa nguvu ya farasi 15 wakati wa hafla ya kukabidhi injini hizo. Lakini pia alisema kuwa mpaka sasa Wizara imeshanunua jumla ya injini za boti 26,hafla iliyofanyika Jijini Dodoma.


Mbunge wa Mtwara Mjini, Mhe. Hassan Mtenga (Mb) akiishukuru Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Sekta ya Uvuvi) kwa kulipatia Jimbo lake la Mtwara Mjini Injini moja ya Boti yenye uwezo wa nguvu ya farasi 15 wakati wa hafla ya kukabidhi injini hizo, ambapo amesema hayo yote yamewezekana kutokana na kuwepo kwa uongozi sikivu na wenye mshikamano. Hafla iliyofanyika Jijini Dodoma.


Mbunge wa Kalenga, Mhe. Jackson Kiswaga (Mb) akiipongeza Wizara ya Mifugo na Uvuvi (Sekta ya Uvuvi) kwa kuipatia Jimbo lake la Pangani Injini moja ya Boti yenye uwezo wa nguvu ya farasi 15 wakati wa hafla ya kukabidhi kwa kuwa itakwenda kuwasaidia wavuvi katika shughuli zao za uvuvi lakini pia katika kulinda rasilimali za uvuvi. Hafla iliyofanyika Jijini Dodoma.


Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (kulia) akimkabidhi injini ya boti Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (kushoto) aliyeipokea kwa niaba ya wananchi wa Pangani wakati wa hafla ya kukabidhi injini hizo iliyofanyika kwenye ofisi ndogo za Wizara zilizopo kwenye jengo la Benki ya NBC Jijini Dodoma.


Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (kulia) akimkabidhi injini ya boti Mbunge wa Kalenga, Mhe. Jackson Kiswaga (kushoto) aliyeipokea kwa niaba ya wananchi wa Pangani wakati wa hafla ya kukabidhi injini hizo iliyofanyika kwenye ofisi ndogo za Wizara zilizopo kwenye jengo la Benki ya NBC Jijini Dodoma.


Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki (kulia) akimkabidhi injini ya boti Mbunge wa Mtwara Mjini, Mhe. Hassan Mtenga (kushoto) aliyeipokea kwa niaba ya wananchi wa Pangani wakati wa hafla ya kukabidhi injini hizo iliyofanyika kwenye ofisi ndogo za Wizara zilizopo kwenye jengo la Benki ya NBC Jijini Dodoma.


Picha ya pamoja ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mashimba Ndaki (wa nne kutoka kushoto), Waziri wa Maji, Jumaa Aweso (wa tatu kutoka kulia) Waheshimiwa Wabunge wa Majimbo ya Mtwara Mjini na Kalenga na Watendaji wa Sekta ya Uvuvi mara baada ya kukabishi injini tatu za boti zenye uwezo wa nguvu ya farasi 15. Hafla hii imefanyika kwenye ofisi ndogo za Wizara zilizopo kwenye jengo la Benki ya NBC Jijini Dodoma.

..........................................

Na Alex Sonna-DODOMA

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Mashimba Ndaki amekabidhi injini za boti kwa ajili ya wavuvi katika Halmashauri za Wilaya za Pangani, Mtwara Mjini na Iringa.

Akizungumza kabla ya kukabidhi injini hizo leo Waziri Ndaki alisema kuwa Wizara imeendelea na utaratibu wake wa kuwawezesha wavuvi kwa kuwapatia vifaa vinakavyowasaidia kuongeza uwezo wa kuvua mazao ya uvuvi kwa wingi ili kuongeza uzalishaji wa mazao ya uvuvi hapa nchini.

“Injini za Boti tunazozikabidhi leo zina uwezo wa nguvu ya farasi 15 na tunazitoa kwenye Halmashauri za Wilaya za Pangani, Mtwara Mjini na Iringa ambapo kila Halmashauri itapata injini moja kwa ajili ya kuwawezesha wavuvi kuongeza uwezo wao wa kuvua lakini pia kulinda rasilimali za uvuvi,” alisema

Waziri Ndaki amewasihi wavuvi kuhakikisha wanavitunza vifaa wanavyopatiwa na Wizara pamoja na Wadau wengine wa uvuvi na kuhakikisha wanavitumia kwa matumizi yaliyokusudiwa ikiwa ni pamoja na ulinzi wa rasilimali za uvuvi.

Aidha, Waziri Ndaki amesema kuwa Serikali kupitia Wizara imejipanga kununua injini nyingine 250 za boti katika mwaka wa fedha wa 2022/2023 na kama kutakuwa na uwezakano zinaweza kuongezeka injini 70 zaidi ambapo kutakuwa na jumla ya injini 320.

Lengo ni kuhakikisha uzalishaji wa mazao ya uvuvi unaongezeka na mchango wake katika kukuza kipato cha mvuvi na taifa kwa ujumla kinaongezeka. Kwa kufanya hivyo lengo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan litakuwa limetimia kwa kuhakikisha kipato cha wavuvi kinaongezeka na mchango wa uvuvi kwenye pato la taifa unaongezeka.

Vilevile Waziri Ndaki amesema kuwa injini hizo zitakazo nunuliwa zitatolewa kwenye vyama vya ushiriki vya wavuvi na hata kwa mvuvi mmoja mmoja mwenye uwezo kwa kuwa zitakuwa zikikopeshwa kwa riba ndogo sana ambayo haitawaumiza wavuvi.

Kwa upande wake Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Sekta ya Uvuvi, Dkt. Nazael Madala amesema kuwa Wizara imekuwa na utaratibu wa kuwawezesha wavuvi kwa kuwapatia vifaa mbalimbali vinavyowasaidia kuweza kuongeza uwezo wao wa kuvua mazao hayo kwa wingi zaidi.

Naye Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso akizungumza kwa niaba ya wananchi wa Pangani ameishukuru Wizara kwa kuwapatia injini hiyo na kwamba itakwenda kuwa msaada mkubwa kwa wavuvi katika shughuli zao za uvuvi ikiwa ni pamoja na ulinzi wa rasilimaliza uvuvi. Lakini pia ameishukuru wizara kwa kuamua kujenga soko la samaki Pangani na kwamba wanapangani wataendelea kutoa ushirikiano kwa Wizara.

Mbunge wa Mtwara Mjini, Mhe. Hassan Mtenga licha ya kuishukuru Wizara kwa kuwakabidhi injini ya boti, ameiomba Wizara kuendelea kuwawezesha wavuvi kwenye vifaa vingine vya uvuvi ikiwemo majokofu ya kuhifadhia mazao ya uvuvi.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger