Saturday 26 February 2022

Picha : RAIS SAMIA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA MTAWALA WA DUBAI



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Makamu wa Rais ambaye pia ni Waziri Mkuu wa Umoja wa Falme za Kiarabu UAE na Mtawala wa Dubai Sheikh Mohammed bin Rashid Al Maktoum mara baada ya kuhutubia katika Maonesho ya Dubai Expo 2020 yanayoendelea katika Mji wa Dubai leo tarehe 26 Februari, 2022. PICHA IKULU

Share:

KARIBU BEHAC KWA HUDUMA YA CHAKULA, BAA, PHARMACY NA MIAMALA YA FEDHA


Karibu Behac Company Limited kwa huduma za Chakula halisi cha Kitanzania/Kiafrika, Bar, Order, Miamala ya Fedha, Pharmacy .Pia tunakodisha viti, meza na sahani. 

Tunapatikana Bwalo la Polisi Mjini Shinyanga . Wasiliana nasi kwa simu namba 0782767034 / 0753474488  Email : info@behac.co.tz  Website : www.behac.co.tz


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI FEBRUARI 26,2022

Share:

Friday 25 February 2022

SERIKALI YATAKA MEWATA KUHAMASISHA JAMII KUKABILIANA NA MABADILIKO YA MAGONJWA



Waziri Dkt. Dorothy Gwajima akiongea na chama cha madaktari wanawake Tanzania(MEWATA) katika Mkutano wa 19 wa Chama hicho uliofanyika Jijini Dodoma.
Waziri Dkt. Dorothy Gwajima akiongea na chama cha madaktari wanawake Tanzania (MEWATA) katika Mkutano wa 19 wa Chama hicho uliofanyika Jijini Dodoma.

Na Dotto Kwilasa, Malunde1 blog-DODOMA.

WIZARA ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wanawake na Makundi maalum kwa kushirikiana na Chama Cha Madaktari Wanawake nchini (MEWATA) imejipanga kuhamasisha na kuelimisha jamii kuhusu kukabiliana na mabadiliko ya hali ya afya yanayojitokeza na kuziwezesha jamii kuibua mbinu rahisi na sahihi za kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazojitokeza .


Hayo yameelezwa leo Jiji Dodoma na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia ,Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Dorothy Gwajima kwenye Mkutano mkuu wa 19 wa MEWATA na kueleza kuwa kupitia wataalamu wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii watahamasisha na kuelimisha jamii yakiwemo makundi maalum ili kuwandaa wananchi kupokea na kukubaliana na mabadiliko ya afya.

Ameeleza kuwa ushirikiano huo utawezesha kuwapatia wanajamii huduma za kisaikolojia pale wanapokumbana na changamoto mbalimbali za kiafya au taharuki za mlipuko ya magonjwa kama ilivyotokea wakati wa mlipuko wa ugonjwa wa UVIKO 19.

Amesema mkutano huo umekuja katika muda muafaka, kwa kuwa mpaka sasa bado Dunia inaendelea kutekeleza jitihada mbalimbali za kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa virusi vya korona ambavyo vimesababisha vifo vya maelfu ya watu ulimwenguni.

"MEWATA yenye wataalamu wanawake ikishirikiana na wizara ya maendeleo ya jamii, jinsia, wanawake na makundi maalamu itaweza kufikisha ujumbe wake kwenye jamii kwa ufanisi zaidi na siyo tu kwa UVIKO 19 bali hata kwa mambo mengine yanayohusu changamoto za afya ili jamii ielewe kwa lugha nyepesi ,"amesema

Pamoja na hayo ameweka wazi kuwa licha ya juhudi zilozopo bado kuna wananchi wengi ambao bado hawajapata elimu ya kutosha ya chanjo ya UVIKO-19 hivyo kuwataka madaktari hao kushirikiana na kuwafikia kwa kuwapa elimu ya afya juu ya magonjwa mbalimbali na kuondokana na mila potofu za jamii zinazopelekea kuathiri afya hasa kwa watoto na wanawake.

"Wito wangu kwenu, tuendeleze jitihada za kulinda afya za akina mama kwani wao ndio chimbuko la familia na nguzo muhimu ya maendeleo ya Taifa kutokana na mchango wao katika uzalishaji, malezi, makuzi na kuimarisha uchumi wa kaya,nawakaribisha pia kufanyakazi nasi kwani maendeleo na ustawi wa jamii unategemea jamii yenye kufanya maamuzi yenye tija juu ya kuboresha afya,"amesisitiza

Mbali na hayo Dkt. Gwajima amesema ili kufikia malengo nguvu ya pamoja inahitajika kwa kuwa jukumu kubwa la sekta ya maendeleo ya jamii ni kuijengea uwezo jamii uelewa wa mambo ili kupokea, kubadilika na kuwajibika kwa kuchukua hatua stahiki kuhusu masuala ya afya.
Share:

Dkt. YONAZI : SERIKALI ITAENDELEA KUWALINDA WANANCHI WAKE DHIDI YA UHALIFU MTANDAONI

Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt.Jim Yonazi akifunga mafunzo ya siku tano yanayohusu usalama mtandaoni kwa wapelelezi na askari wa chumba cha mashtaka Jijini Dodoma.

Na Dotto Kwilasa-Malunde 1 Blog-DODOMA.

KATIBU Mkuu,Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Jim Yonazi amesema  Serikali itaendelea kuwalinda wananchi wake kutokana na uhalifu wa mitandao ili kuhakikisha nchi inakuwa salama.

Dkt. Yonazi ameeleza hayo leo Jijini Dodoma wakati akifunga mafunzo ya siku tano yanayohusu usalama mtandaoni kwa wapelelezi na askari wa chumba cha mashtaka na kueleza kuwa jambo la usalama mtandao ni  muhimu  kutiliwa mkazo hasa katika zama hizi za kidigitali kwa kuwa uwepo wa usalama  katika matumizi ya mitandao ni sawa sawa na kuhakikishia dunia inakuwa salama.

Mbali na hayo amebainisha kuwa zaidi ya watu milioni 18 duniani ni watumiaji wa huduma ya mtandao (internet) idadi ambayo ni kubwa hivyo ni muhimu sana kuweka namna sahihi ya kulinda usalama wa watumiaji hao.

“Dunia imebadilika sana tofauti na ilivyokuwa zamani,hivi sasa masuala ya usalama na ulinzi yanategemea TEHAMA,wachafuzi nao wanapata fursa kuharibu kutumia Teknolojia hiyo kuvuruga amani,nawaomba mkaendelee kuboresha mbinu mlizojifunza hapa  kuhakikisha usalama katika matumizi ya mitandao unaboreshwa,hakikisheni mnaepusha  madhara ya matumizi mabovu ya mitandao,” amesema Dkt. Yonazi.

Amesema, kupitia mafunzo hayo ya siku tano,walinzi hao wa usalama mtandaoni wanapaswa kushirikiana katika hatua changamoto zote uhalifu mtandao na kwamba Kwa kufanya hivyo watadhihirisha namna ambavyo Tanzania imejipanga katika kuhakikisha matumizi ya mitandao yanakuwa salama.

"Tunaamini kuwa tunayo nchi inayojilinda ,tunao wananchi wanaotegemea sana ulinzi wa mtandao Ili waishi Kwa amani na kuendelea kufanya shughuli nyingine za uzalishaji bila woga,ni jukumu lenu kulinda usalama wa taifa hili kwa kuzuia uhalifu wowote wa mtandao,"amesema

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DCI) Camilius Wambura amesema Idara hiyo itahakikisha inaboresha mifumo ya kuhakiki uhalali wa taarifa zinazopitia kwenye mitandao ambayo imebuniwa na wataalam wa Teknolojia ya Habari nchini Ili kuzuia matumizi mabaya ya mitandao.

"Makosa ya mtandao yanakuwa mengi na kusababisha uvunjifu wa amani na kuharibu furaha Kwa watu wengine,kupitia mafunzo hayo yataleta matokeo chanya kutokana na mbinu mlizopata ili kukabiliana na uhalifu wa kimtandao kwani maarifa yatawasaidia katika kubadilishana taarifa,"amesema.

Kadhalika Wambura ametumia nafasi hiyo kuwataka wapelelezi hao pamoja na askari kuhakikisha wanazingatia misingi ya kazi na wito wa maadili ya kazi yao ikiwa ni pamoja na  kufanya  kazi kwa kushirikiana ili kuweza kufikia malengo.

"Nendeni mkahakikishe  mnafanya kazi kwa uadilifu na nidhamu katika utendaji kazi wenu kwani tabia za wachache zimekuwa zikiharibu taswira ya Jeshi jambo ambalo si jema,"amesisitiza.
Share:

Pich : EWURA YATOA MAFUNZO YA HUDUMA ZA NISHATI NA MAJI KWA WENYEVITI WA MITAA MANISPAA YA SHINYANGA..MMARI ATAKA WATUMIAJI WAKIZINGULIWA WADAI FIDIA

Katibu Mtendaji wa EWURA CCC Mhandisi Goodluck Mmari akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga yaliyoandaliwa na EWURA CCC kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Maji na Nishati zinazodhibitiwa na EWURA (EWURA Consumer Consultative Council - EWURA CCC) Mkoa wa Shinyanga limetoa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga ili kujenga na kukuza uelewa na ufahamu kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji sambamba na kuwezesha upatikanaji na utoaji wa taarifa juu ya miongozo, sera, kanuni na sheria zinazosimamia huduma za maji na nishati kwa mtumiaji na wananchi kwa ujumla.

Mafunzo hayo yaliyokutanisha wenyeviti wa mitaa na vitongoji kutoka kata 10 za Manispaa ya Shinyanga yamefanyika leo Ijumaa Februari 25,2022 katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga na kuhudhuriwa na Katibu Mtendaji wa Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Maji na Nishati zinazodhibitiwa na EWURA (EWURA CCC), Mhandisi Goodluck Mmari.

Akizungumza katika semina hiyo, Katibu Mtendaji wa EWURA CCC Mhandisi Goodluck Mmari amesema mafunzo hayo yamekuwa na tija kubwa kwa wenyeviti wa mitaa na vitongoji kwani mada zilizotolewa na mjadala uliofanyika unagusa huduma za nishati na maji na unagusa maisha ya watu.

“Kwa kiasi kikubwa lengo la Programu hii ya mafunzo limefanikiwa,lengo la semina hii ilikuwa ni kutoa elimu na tumejifunza mambo mengi ikiwemo kujua EWURA CCC ni kitu gani,mambo na utaratibu wa kuwasilisha malalamiko kwa sababu unapokuwa na malalamiko kama hujui utaratibu wa kuwasilisha utabaki na kero yako. Kama hujui sheria,hujui haki zako huwezi jua namna ya kuzidai”,amesema Mhandisi Mmari.

“Huduma zinazozalishwa hazitoshelezi,maji hayatoshelezi hivyo kila tunachokipata tunatakiwa kukitumia vizuri hata kama una hela ya kulipia bili lakini kwanini umwage maji, kwanini utumie maji hovyo, unapotumia maji ujue kuwa kuna watu hawana hiyo huduma. Tutumie vizuri huduma ili huduma ziweze kuwafikia watu wengi zaidi ambao hawafaidiki na hizi huduma”,ameongeza Mhandisi Mmari.

Amewataka wenyeviti wa serikali za mitaa waliopata mafunzo hayo wakayaweke kwenye vitendo waliyojifunza kwa kuwapatia elimu wananchi kwenye maeneo yao.

“Kundi hili la wenyeviti wa serikali za mitaa ni kundi muhimu, mna watu wengi nyuma yenu, wapo karibu na watu na wana ushawishi, naamini mtafikisha elimu hii kwa wananchi",amesema.

"Na msiogope kwenda kudai fidia ili watoa huduma wetu hawa wasilale usingizi kwa sababu tusipokuwa tunawadai huduma hata haki zetu zinapokiukwa watalala usingizi. Tusipoamka na kuwasukuma huduma zetu zitazorota pia na serikali inataka kila taasisi iwajibike.Tudai fidia zile na wakiona tunadai fidia kila tunapokuwa tumekwazwa,wataamka na kuwajibika. Haki ni staki haihitaji kubembeleza ili upewe”,ameongeza Mhandisi Mmari.

Mwenyekiti wa EWURA CCC Mkoa wa Shinyanga, Kudely Sokoine ameitaja miongoni mwa mifano ya malalamiko ya watumiaji wa huduma za maji na nishati ambayo imekuwa ikilalamikiwa na wateja ni pamoja na ongezeko la bili za umeme na maji, kuunguliwa vyombo vya umeme na makazi,migogoro ya usomaji mita, Makampuni kushindwa kutengeneza miundombinu inayopitisha huduma na uharibifu unaotokea majumbani kutokana na maji machafu na hitilafu za umeme.

Malalamiko mengine ni ucheleweshaji wa kuunganishwa kwenye huduma husika kwa watumia huduma wapya wanaotaka kuunganishwa na huduma za umeme na maji, Watoa huduma kushindwa kutoa mwitikio wa kuridhisha kwa maswali au malalamiko kutoka kwa watumiaji/wateja na maswali kuhusu namna bili zisizo na mita zinavyoandaliwa na ukadiriaji viwango vyake.

Mweka Hazina wa EWURA CCC Mkoa wa Shinyanga, Joseph Ndatala amesema mtumiaji wa huduma za maji na nishati ana wajibu wa kulipa Ankara kwa wakati, kutunza miundombinu ya huduma ili iweze kuwa endelevu huku akisisitiza kuwa Huduma bora ni haki ya mtumiaji wa huduma za nishati na maji.

Katibu wa EWURA CCC Mkoa wa Shinyanga, Zezema Nyangaki Shilungushela amesema kazi ya EWURA CCM ni kutetea watumiaji wa maji na nishati ili kuelewa haki zao huku akizitaja huduma zinazodhibitiwa na EWURA ni Maji,bidhaa zitokanazo na petrol (petroli,mafuta ya taa na mafuta mazito), umeme na gesi asilia.

Amewashauri watumiaji wa nishati ya umeme kuwa wanapokuwa nyumbani watumie umeme muda unaotakiwa, kuwasha taa eneo walipo na kuepuka kumwaga mwaga maji ili kupunguza gharama

Mjumbe wa EWURA CCC Mkoa wa Shinyanga, Jonathan Manyama amesema Mtumiaji wa huduma za maji na nishati ana haki ya kuhudumiwa kwa wakati na kwa mujibu wa miongozo,kanuni, sheria na bei ya halali zilizopitishwa na kutangazwa na mamlaka husika na kwamba ana haki ya kupata taarifa kuhusu huduma zinazotolewa mfano kusitishwa kwa huduma kutokana na matengenezo.

Afisa Huduma kwa Wateja Msaidizi wa SHUWASA, Masaka Kambesha amesema hivi sasa Mamlaka imeanza kutoa Bili za maji kila ifikapo tarehe 20 ya kila mwezi na wateja kutakiwa kulipia bili zao ndani ya siku 30 na kwamba wamekuwa wakituma bili kupitia namba za simu za wateja wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 25,000 mpaka sasa hivyo kuwaomba wale ambao hawajaunganishwa na huduma hiyo wafike katika ofisi za SHUWASA ili waanze kupata bili za maji kwa nji ya simu.

Nao wenyeviti hao wa serikali za mitaa wameishukuru EWURA CCC kuandaa semina hiyo ambayo imewajengea uelewa na kuahidi kwenda kutoa elimu hiyo kwa wananchi ili kujua haki na wajibu wao wanapotumia huduma za nishati na maji.
Katibu Mtendaji wa EWURA CCC Mhandisi Goodluck Mmari akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga yaliyoandaliwa na EWURA CCC kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Katibu Mtendaji wa EWURA CCC Mhandisi Goodluck Mmari akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga yaliyoandaliwa na EWURA CCC kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji.
Katibu Mtendaji wa EWURA CCC Mhandisi Goodluck Mmari akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga yaliyoandaliwa na EWURA CCC kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji.
Katibu Mtendaji wa EWURA CCC Mhandisi Goodluck Mmari akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga yaliyoandaliwa na EWURA CCC kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji.
Mwenyekiti wa EWURA CCC Mkoa wa Shinyanga, Kudely Sokoine akizungumza wakati wa semina ya Wenyeviti wa serikali za mitaa iliyoandaliwa na Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Maji na Nishati zinazodhibitiwa na EWURA (EWURA CCC) Mkoa wa Shinyanga.
Katibu wa EWURA CCC Mkoa wa Shinyanga, Zezema Nyangaki Shilungushela akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga yaliyoandaliwa na EWURA CCC kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji.
Katibu wa EWURA CCC Mkoa wa Shinyanga, Zezema Nyangaki Shilungushela akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga yaliyoandaliwa na EWURA CCC kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji.
Mweka Hazina wa EWURA CCC Mkoa wa Shinyanga, Joseph Ndatala akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga yaliyoandaliwa na EWURA CCC kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji.
Mjumbe wa EWURA CCC Mkoa wa Shinyanga, Jonathan Manyama akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga yaliyoandaliwa na EWURA CCC kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji.
Mtoa Huduma kwa Wateja EWURA CCC Mkoa wa Shinyanga Leonce Bizimana akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga yaliyoandaliwa na EWURA CCC kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji.
Afisa Huduma kwa Wateja Msaidizi wa SHUWASA, Masaka Kambesha akitoa ufafanuzi kuhusu maswali ya washiriki wa semina hiyo.
Mwakilishi kutoka TANESCO Shaban Chein akitoa ufafanuzi kwa maswali yaliyoulizwa na washiriki wa semina hiyo.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Miti Mirefu Manispaa ya Shinyanga, Nassor Warioba akiuliza swali wakati wa semina hiyo.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Kitangili Manispaa ya Shinyanga Habiba Jumanne akiuliza swali wakati wa semina hiyo.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Dome Manispaa ya Shinyanga Solomoni Nalinga Najulwa 'Cheupe' akiuliza swali wakati wa semina hiyo.
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Busalala Nhelegani kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga Sophia Henerico Shitobelo akiuliza swali wakati wa semina hiyo.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Bugwandege Manispaa ya Shinyanga , Amani Abdalah akiuliza swali wakati wa semina hiyo.
Katibu Mtendaji wa EWURA CCC Mhandisi Goodluck Mmari akifuatilia mjadala ukumbini
Wenyeviti wa serikali za mitaa wakiwa ukumbini
Mafunzo yanaendelea
Mafunzo yanaendelea
Wenyeviti wa serikali za mitaa wakiwa ukumbini
Mafunzo yanaendelea
Wenyeviti wa serikali za mitaa wakiwa ukumbini
Wenyeviti wa serikali za mitaa wakiwa ukumbini.

Picha zote na Kadama Malunde- Malunde 1 blog


Share:

TANZANIA YATOA TAARIFA KUHUSU WATANZANIA WANAOISHI UKRAINE

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger