Saturday 26 February 2022

KARIBU BEHAC KWA HUDUMA YA CHAKULA, BAA, PHARMACY NA MIAMALA YA FEDHA


Karibu Behac Company Limited kwa huduma za Chakula halisi cha Kitanzania/Kiafrika, Bar, Order, Miamala ya Fedha, Pharmacy .Pia tunakodisha viti, meza na sahani. 

Tunapatikana Bwalo la Polisi Mjini Shinyanga . Wasiliana nasi kwa simu namba 0782767034 / 0753474488  Email : info@behac.co.tz  Website : www.behac.co.tz


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI FEBRUARI 26,2022

Share:

Friday 25 February 2022

SERIKALI YATAKA MEWATA KUHAMASISHA JAMII KUKABILIANA NA MABADILIKO YA MAGONJWA



Waziri Dkt. Dorothy Gwajima akiongea na chama cha madaktari wanawake Tanzania(MEWATA) katika Mkutano wa 19 wa Chama hicho uliofanyika Jijini Dodoma.
Waziri Dkt. Dorothy Gwajima akiongea na chama cha madaktari wanawake Tanzania (MEWATA) katika Mkutano wa 19 wa Chama hicho uliofanyika Jijini Dodoma.

Na Dotto Kwilasa, Malunde1 blog-DODOMA.

WIZARA ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wanawake na Makundi maalum kwa kushirikiana na Chama Cha Madaktari Wanawake nchini (MEWATA) imejipanga kuhamasisha na kuelimisha jamii kuhusu kukabiliana na mabadiliko ya hali ya afya yanayojitokeza na kuziwezesha jamii kuibua mbinu rahisi na sahihi za kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazojitokeza .


Hayo yameelezwa leo Jiji Dodoma na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia ,Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Dorothy Gwajima kwenye Mkutano mkuu wa 19 wa MEWATA na kueleza kuwa kupitia wataalamu wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii watahamasisha na kuelimisha jamii yakiwemo makundi maalum ili kuwandaa wananchi kupokea na kukubaliana na mabadiliko ya afya.

Ameeleza kuwa ushirikiano huo utawezesha kuwapatia wanajamii huduma za kisaikolojia pale wanapokumbana na changamoto mbalimbali za kiafya au taharuki za mlipuko ya magonjwa kama ilivyotokea wakati wa mlipuko wa ugonjwa wa UVIKO 19.

Amesema mkutano huo umekuja katika muda muafaka, kwa kuwa mpaka sasa bado Dunia inaendelea kutekeleza jitihada mbalimbali za kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa virusi vya korona ambavyo vimesababisha vifo vya maelfu ya watu ulimwenguni.

"MEWATA yenye wataalamu wanawake ikishirikiana na wizara ya maendeleo ya jamii, jinsia, wanawake na makundi maalamu itaweza kufikisha ujumbe wake kwenye jamii kwa ufanisi zaidi na siyo tu kwa UVIKO 19 bali hata kwa mambo mengine yanayohusu changamoto za afya ili jamii ielewe kwa lugha nyepesi ,"amesema

Pamoja na hayo ameweka wazi kuwa licha ya juhudi zilozopo bado kuna wananchi wengi ambao bado hawajapata elimu ya kutosha ya chanjo ya UVIKO-19 hivyo kuwataka madaktari hao kushirikiana na kuwafikia kwa kuwapa elimu ya afya juu ya magonjwa mbalimbali na kuondokana na mila potofu za jamii zinazopelekea kuathiri afya hasa kwa watoto na wanawake.

"Wito wangu kwenu, tuendeleze jitihada za kulinda afya za akina mama kwani wao ndio chimbuko la familia na nguzo muhimu ya maendeleo ya Taifa kutokana na mchango wao katika uzalishaji, malezi, makuzi na kuimarisha uchumi wa kaya,nawakaribisha pia kufanyakazi nasi kwani maendeleo na ustawi wa jamii unategemea jamii yenye kufanya maamuzi yenye tija juu ya kuboresha afya,"amesisitiza

Mbali na hayo Dkt. Gwajima amesema ili kufikia malengo nguvu ya pamoja inahitajika kwa kuwa jukumu kubwa la sekta ya maendeleo ya jamii ni kuijengea uwezo jamii uelewa wa mambo ili kupokea, kubadilika na kuwajibika kwa kuchukua hatua stahiki kuhusu masuala ya afya.
Share:

Dkt. YONAZI : SERIKALI ITAENDELEA KUWALINDA WANANCHI WAKE DHIDI YA UHALIFU MTANDAONI

Katibu Mkuu, Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt.Jim Yonazi akifunga mafunzo ya siku tano yanayohusu usalama mtandaoni kwa wapelelezi na askari wa chumba cha mashtaka Jijini Dodoma.

Na Dotto Kwilasa-Malunde 1 Blog-DODOMA.

KATIBU Mkuu,Wizara ya Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Dkt. Jim Yonazi amesema  Serikali itaendelea kuwalinda wananchi wake kutokana na uhalifu wa mitandao ili kuhakikisha nchi inakuwa salama.

Dkt. Yonazi ameeleza hayo leo Jijini Dodoma wakati akifunga mafunzo ya siku tano yanayohusu usalama mtandaoni kwa wapelelezi na askari wa chumba cha mashtaka na kueleza kuwa jambo la usalama mtandao ni  muhimu  kutiliwa mkazo hasa katika zama hizi za kidigitali kwa kuwa uwepo wa usalama  katika matumizi ya mitandao ni sawa sawa na kuhakikishia dunia inakuwa salama.

Mbali na hayo amebainisha kuwa zaidi ya watu milioni 18 duniani ni watumiaji wa huduma ya mtandao (internet) idadi ambayo ni kubwa hivyo ni muhimu sana kuweka namna sahihi ya kulinda usalama wa watumiaji hao.

“Dunia imebadilika sana tofauti na ilivyokuwa zamani,hivi sasa masuala ya usalama na ulinzi yanategemea TEHAMA,wachafuzi nao wanapata fursa kuharibu kutumia Teknolojia hiyo kuvuruga amani,nawaomba mkaendelee kuboresha mbinu mlizojifunza hapa  kuhakikisha usalama katika matumizi ya mitandao unaboreshwa,hakikisheni mnaepusha  madhara ya matumizi mabovu ya mitandao,” amesema Dkt. Yonazi.

Amesema, kupitia mafunzo hayo ya siku tano,walinzi hao wa usalama mtandaoni wanapaswa kushirikiana katika hatua changamoto zote uhalifu mtandao na kwamba Kwa kufanya hivyo watadhihirisha namna ambavyo Tanzania imejipanga katika kuhakikisha matumizi ya mitandao yanakuwa salama.

"Tunaamini kuwa tunayo nchi inayojilinda ,tunao wananchi wanaotegemea sana ulinzi wa mtandao Ili waishi Kwa amani na kuendelea kufanya shughuli nyingine za uzalishaji bila woga,ni jukumu lenu kulinda usalama wa taifa hili kwa kuzuia uhalifu wowote wa mtandao,"amesema

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DCI) Camilius Wambura amesema Idara hiyo itahakikisha inaboresha mifumo ya kuhakiki uhalali wa taarifa zinazopitia kwenye mitandao ambayo imebuniwa na wataalam wa Teknolojia ya Habari nchini Ili kuzuia matumizi mabaya ya mitandao.

"Makosa ya mtandao yanakuwa mengi na kusababisha uvunjifu wa amani na kuharibu furaha Kwa watu wengine,kupitia mafunzo hayo yataleta matokeo chanya kutokana na mbinu mlizopata ili kukabiliana na uhalifu wa kimtandao kwani maarifa yatawasaidia katika kubadilishana taarifa,"amesema.

Kadhalika Wambura ametumia nafasi hiyo kuwataka wapelelezi hao pamoja na askari kuhakikisha wanazingatia misingi ya kazi na wito wa maadili ya kazi yao ikiwa ni pamoja na  kufanya  kazi kwa kushirikiana ili kuweza kufikia malengo.

"Nendeni mkahakikishe  mnafanya kazi kwa uadilifu na nidhamu katika utendaji kazi wenu kwani tabia za wachache zimekuwa zikiharibu taswira ya Jeshi jambo ambalo si jema,"amesisitiza.
Share:

Pich : EWURA YATOA MAFUNZO YA HUDUMA ZA NISHATI NA MAJI KWA WENYEVITI WA MITAA MANISPAA YA SHINYANGA..MMARI ATAKA WATUMIAJI WAKIZINGULIWA WADAI FIDIA

Katibu Mtendaji wa EWURA CCC Mhandisi Goodluck Mmari akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga yaliyoandaliwa na EWURA CCC kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Maji na Nishati zinazodhibitiwa na EWURA (EWURA Consumer Consultative Council - EWURA CCC) Mkoa wa Shinyanga limetoa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga ili kujenga na kukuza uelewa na ufahamu kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji sambamba na kuwezesha upatikanaji na utoaji wa taarifa juu ya miongozo, sera, kanuni na sheria zinazosimamia huduma za maji na nishati kwa mtumiaji na wananchi kwa ujumla.

Mafunzo hayo yaliyokutanisha wenyeviti wa mitaa na vitongoji kutoka kata 10 za Manispaa ya Shinyanga yamefanyika leo Ijumaa Februari 25,2022 katika ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga na kuhudhuriwa na Katibu Mtendaji wa Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Maji na Nishati zinazodhibitiwa na EWURA (EWURA CCC), Mhandisi Goodluck Mmari.

Akizungumza katika semina hiyo, Katibu Mtendaji wa EWURA CCC Mhandisi Goodluck Mmari amesema mafunzo hayo yamekuwa na tija kubwa kwa wenyeviti wa mitaa na vitongoji kwani mada zilizotolewa na mjadala uliofanyika unagusa huduma za nishati na maji na unagusa maisha ya watu.

“Kwa kiasi kikubwa lengo la Programu hii ya mafunzo limefanikiwa,lengo la semina hii ilikuwa ni kutoa elimu na tumejifunza mambo mengi ikiwemo kujua EWURA CCC ni kitu gani,mambo na utaratibu wa kuwasilisha malalamiko kwa sababu unapokuwa na malalamiko kama hujui utaratibu wa kuwasilisha utabaki na kero yako. Kama hujui sheria,hujui haki zako huwezi jua namna ya kuzidai”,amesema Mhandisi Mmari.

“Huduma zinazozalishwa hazitoshelezi,maji hayatoshelezi hivyo kila tunachokipata tunatakiwa kukitumia vizuri hata kama una hela ya kulipia bili lakini kwanini umwage maji, kwanini utumie maji hovyo, unapotumia maji ujue kuwa kuna watu hawana hiyo huduma. Tutumie vizuri huduma ili huduma ziweze kuwafikia watu wengi zaidi ambao hawafaidiki na hizi huduma”,ameongeza Mhandisi Mmari.

Amewataka wenyeviti wa serikali za mitaa waliopata mafunzo hayo wakayaweke kwenye vitendo waliyojifunza kwa kuwapatia elimu wananchi kwenye maeneo yao.

“Kundi hili la wenyeviti wa serikali za mitaa ni kundi muhimu, mna watu wengi nyuma yenu, wapo karibu na watu na wana ushawishi, naamini mtafikisha elimu hii kwa wananchi",amesema.

"Na msiogope kwenda kudai fidia ili watoa huduma wetu hawa wasilale usingizi kwa sababu tusipokuwa tunawadai huduma hata haki zetu zinapokiukwa watalala usingizi. Tusipoamka na kuwasukuma huduma zetu zitazorota pia na serikali inataka kila taasisi iwajibike.Tudai fidia zile na wakiona tunadai fidia kila tunapokuwa tumekwazwa,wataamka na kuwajibika. Haki ni staki haihitaji kubembeleza ili upewe”,ameongeza Mhandisi Mmari.

Mwenyekiti wa EWURA CCC Mkoa wa Shinyanga, Kudely Sokoine ameitaja miongoni mwa mifano ya malalamiko ya watumiaji wa huduma za maji na nishati ambayo imekuwa ikilalamikiwa na wateja ni pamoja na ongezeko la bili za umeme na maji, kuunguliwa vyombo vya umeme na makazi,migogoro ya usomaji mita, Makampuni kushindwa kutengeneza miundombinu inayopitisha huduma na uharibifu unaotokea majumbani kutokana na maji machafu na hitilafu za umeme.

Malalamiko mengine ni ucheleweshaji wa kuunganishwa kwenye huduma husika kwa watumia huduma wapya wanaotaka kuunganishwa na huduma za umeme na maji, Watoa huduma kushindwa kutoa mwitikio wa kuridhisha kwa maswali au malalamiko kutoka kwa watumiaji/wateja na maswali kuhusu namna bili zisizo na mita zinavyoandaliwa na ukadiriaji viwango vyake.

Mweka Hazina wa EWURA CCC Mkoa wa Shinyanga, Joseph Ndatala amesema mtumiaji wa huduma za maji na nishati ana wajibu wa kulipa Ankara kwa wakati, kutunza miundombinu ya huduma ili iweze kuwa endelevu huku akisisitiza kuwa Huduma bora ni haki ya mtumiaji wa huduma za nishati na maji.

Katibu wa EWURA CCC Mkoa wa Shinyanga, Zezema Nyangaki Shilungushela amesema kazi ya EWURA CCM ni kutetea watumiaji wa maji na nishati ili kuelewa haki zao huku akizitaja huduma zinazodhibitiwa na EWURA ni Maji,bidhaa zitokanazo na petrol (petroli,mafuta ya taa na mafuta mazito), umeme na gesi asilia.

Amewashauri watumiaji wa nishati ya umeme kuwa wanapokuwa nyumbani watumie umeme muda unaotakiwa, kuwasha taa eneo walipo na kuepuka kumwaga mwaga maji ili kupunguza gharama

Mjumbe wa EWURA CCC Mkoa wa Shinyanga, Jonathan Manyama amesema Mtumiaji wa huduma za maji na nishati ana haki ya kuhudumiwa kwa wakati na kwa mujibu wa miongozo,kanuni, sheria na bei ya halali zilizopitishwa na kutangazwa na mamlaka husika na kwamba ana haki ya kupata taarifa kuhusu huduma zinazotolewa mfano kusitishwa kwa huduma kutokana na matengenezo.

Afisa Huduma kwa Wateja Msaidizi wa SHUWASA, Masaka Kambesha amesema hivi sasa Mamlaka imeanza kutoa Bili za maji kila ifikapo tarehe 20 ya kila mwezi na wateja kutakiwa kulipia bili zao ndani ya siku 30 na kwamba wamekuwa wakituma bili kupitia namba za simu za wateja wanaokadiriwa kuwa zaidi ya 25,000 mpaka sasa hivyo kuwaomba wale ambao hawajaunganishwa na huduma hiyo wafike katika ofisi za SHUWASA ili waanze kupata bili za maji kwa nji ya simu.

Nao wenyeviti hao wa serikali za mitaa wameishukuru EWURA CCC kuandaa semina hiyo ambayo imewajengea uelewa na kuahidi kwenda kutoa elimu hiyo kwa wananchi ili kujua haki na wajibu wao wanapotumia huduma za nishati na maji.
Katibu Mtendaji wa EWURA CCC Mhandisi Goodluck Mmari akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga yaliyoandaliwa na EWURA CCC kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Katibu Mtendaji wa EWURA CCC Mhandisi Goodluck Mmari akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga yaliyoandaliwa na EWURA CCC kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji.
Katibu Mtendaji wa EWURA CCC Mhandisi Goodluck Mmari akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga yaliyoandaliwa na EWURA CCC kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji.
Katibu Mtendaji wa EWURA CCC Mhandisi Goodluck Mmari akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga yaliyoandaliwa na EWURA CCC kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji.
Mwenyekiti wa EWURA CCC Mkoa wa Shinyanga, Kudely Sokoine akizungumza wakati wa semina ya Wenyeviti wa serikali za mitaa iliyoandaliwa na Baraza la Ushauri la Watumiaji wa Huduma za Maji na Nishati zinazodhibitiwa na EWURA (EWURA CCC) Mkoa wa Shinyanga.
Katibu wa EWURA CCC Mkoa wa Shinyanga, Zezema Nyangaki Shilungushela akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga yaliyoandaliwa na EWURA CCC kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji.
Katibu wa EWURA CCC Mkoa wa Shinyanga, Zezema Nyangaki Shilungushela akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga yaliyoandaliwa na EWURA CCC kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji.
Mweka Hazina wa EWURA CCC Mkoa wa Shinyanga, Joseph Ndatala akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga yaliyoandaliwa na EWURA CCC kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji.
Mjumbe wa EWURA CCC Mkoa wa Shinyanga, Jonathan Manyama akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga yaliyoandaliwa na EWURA CCC kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji.
Mtoa Huduma kwa Wateja EWURA CCC Mkoa wa Shinyanga Leonce Bizimana akizungumza wakati wa mafunzo kwa Wenyeviti wa serikali za mitaa Manispaa ya Shinyanga yaliyoandaliwa na EWURA CCC kuhusu haki na wajibu wa mtumiaji wa huduma za nishati na maji.
Afisa Huduma kwa Wateja Msaidizi wa SHUWASA, Masaka Kambesha akitoa ufafanuzi kuhusu maswali ya washiriki wa semina hiyo.
Mwakilishi kutoka TANESCO Shaban Chein akitoa ufafanuzi kwa maswali yaliyoulizwa na washiriki wa semina hiyo.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Miti Mirefu Manispaa ya Shinyanga, Nassor Warioba akiuliza swali wakati wa semina hiyo.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Kitangili Manispaa ya Shinyanga Habiba Jumanne akiuliza swali wakati wa semina hiyo.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Dome Manispaa ya Shinyanga Solomoni Nalinga Najulwa 'Cheupe' akiuliza swali wakati wa semina hiyo.
Mwenyekiti wa Kitongoji cha Busalala Nhelegani kata ya Kizumbi Manispaa ya Shinyanga Sophia Henerico Shitobelo akiuliza swali wakati wa semina hiyo.
Mwenyekiti wa Mtaa wa Bugwandege Manispaa ya Shinyanga , Amani Abdalah akiuliza swali wakati wa semina hiyo.
Katibu Mtendaji wa EWURA CCC Mhandisi Goodluck Mmari akifuatilia mjadala ukumbini
Wenyeviti wa serikali za mitaa wakiwa ukumbini
Mafunzo yanaendelea
Mafunzo yanaendelea
Wenyeviti wa serikali za mitaa wakiwa ukumbini
Mafunzo yanaendelea
Wenyeviti wa serikali za mitaa wakiwa ukumbini
Wenyeviti wa serikali za mitaa wakiwa ukumbini.

Picha zote na Kadama Malunde- Malunde 1 blog


Share:

TANZANIA YATOA TAARIFA KUHUSU WATANZANIA WANAOISHI UKRAINE

Share:

SABABU ZA URUSI KUIVAMIA UKRAINE...PUTIN ANATAKA NINI??

 

Ukrainian President Volodymyr Zelensky visiting positions on the frontline with pro-Russian militants in the Donetsk region, Ukraine, 06 December 2021

CHANZO CHA PICHA,

EPAKupitia angani , nchi kavu, na baharini, Urusi imeanzisha shambulio baya dhidi ya Ukraine, nchi yenye demokrasia barani Ulaya ya watu milioni 44.

Kwa miezi kadhaa Rais Vladimir Putin alikuwa amekanusha kuwa angevamia jirani yake, lakini kisha akavunja makubaliano ya amani, na kutuma vikosi kuvuka mipaka ya kaskazini, mashariki na kusini mwa Ukraine.

Huku idadi ya waliofariki ikipanda, sasa anashutumiwa kwa kuvunja amani barani Ulaya na kitakachofuata kinaweza kuhatarisha muundo mzima wa usalama wa bara hilo.

Wanajeshi wa Urusi wameshambulia wapi na kwa nini?

Viwanja vya ndege na makao makuu ya jeshi vilipigwa kwanza, karibu na miji kote Ukraine pamoja na uwanja mkuu wa ndege wa kimataifa wa Boryspil huko Kyiv.


Kisha vifaru na wanajeshi wakaingia Ukrainia kaskazini-mashariki, karibu na Kharkiv, jiji la watu milioni 1.4; mashariki karibu na Luhansk, kutoka Belarusi jirani kaskazini na Crimea kusini. Wanajeshi wa kijeshi walikamata kambi muhimu ya anga nje kidogo ya Kyiv na wanajeshi wa Urusi walitua katika miji mikubwa ya bandari ya Odesa na Mariupol pia ya Ukraine.

Muda mfupi kabla ya uvamizi huo kuanza, Rais Putin alienda kwenye TV akitangaza kwamba Urusi haiwezi kujisikia "salama, kuendeleza na kuwepo" kwa sababu ya kile alichokiita tishio la mara kwa mara kutoka kwa Ukraine ya kisasa.

TH
1px transparent line

Hoja zake nyingi zilikuwa za uwongo au zisizo na mantiki. Alidai lengo lake lilikuwa kuwalinda watu wanaodhulumiwa na mauaji ya halaiki na kulenga "kuondoa kijeshi na kuondoa Unazi" wa Ukraine. Hakujakuwa na mauaji ya halaiki nchini Ukraine - ni demokrasia iliyochangamka inayoongozwa na rais ambaye ni Myahudi. "Ningewezaje kuwa Nazi?" alisema Volodymr Zelensky, ambaye alifananisha mashambulizi ya Urusi na uvamizi wa Ujerumani ya Nazi katika Vita vya Pili vya Dunia.

    Rais Putin mara kwa mara amekuwa akiishutumu Ukraine kwa kuchukuliwa na watu wenye itikadi kali, tangu rais wake anayeiunga mkono Urusi, Viktor Yanukovych, kuondolewa madarakani mwaka 2014 baada ya miezi kadhaa ya maandamano dhidi ya utawala wake. Kisha Urusi ililipiza kisasi kwa kuliteka eneo la kusini la Crimea na kuanzisha uasi mashariki mwa nchi hiyo, ikiunga mkono watu wanaotaka kujitenga ambao wamepigana na vikosi vya Ukraine katika vita vilivyogharimu maisha ya watu 14,000.

    Mwishoni mwa 2021 alianza kupeleka idadi kubwa ya wanajeshi wa Urusi karibu na mipaka ya Ukraine. Kisha wiki hii alitupilia mbali mkataba wa amani wa 2015 kwa upande wa mashariki na maeneo yaliyotambuliwa chini ya udhibiti wa waasi kuwa huru.

    Urusi kwa muda mrefu imekuwa ikipinga hatua ya Ukraine kuelekea Umoja wa Ulaya na muungano wa kijeshi wa kujihami wa nchi za Magharibi Nato. Akitangaza uvamizi wa Urusi, aliishutumu Nato kwa kutishia "mustakabali wetu wa kihistoria kama taifa".

    Map showing the Donetsk and Luhansk regions in eastern Ukraine and the Russian-backed separatist-held areas within those regions.
    1px transparent line

    Je Urusi itaenda umbali gani?

    Urusi imekataa kusema kama inataka kupindua serikali iliyochaguliwa kidemokrasia ya Ukraine, ingawa inaamini kwamba Ukraine inapaswa "kuachiliwa, kusafishwa kutoka kwa Wanazi". Bw Putin alizungumzia kuwafikisha mahakamani "wale waliofanya uhalifu mwingi wa umwagaji damu dhidi ya raia".

    Ilikuwa ni dokezo nyembamba na kwa kuvamia kutoka Belarus na kukamata uwanja wa ndege wa Antonov karibu na viunga vya Kyiv, kuna shaka kidogo kwamba mji mkuu uko vizuri ndani ya vituko vyake.

    Katika siku za kabla ya uvamizi huo, wakati hadi askari 200,000 walikuwa karibu na mipaka ya Ukraine, alikuwa ameelekeza fikira zake mashariki.

    Kwa kutambua maeneo yanayoungwa mkono na Urusi yaliyojitenga ya Luhansk na Donetsk kama huru, alikuwa tayari ameamua kuwa hayakuwa tena sehemu ya Ukrainia. Kisha akafichua kwamba aliunga mkono madai yao kwa eneo la mbali zaidi la Kiukreni. Jamuhuri za watu wanaojiita huru zinachukua zaidi ya theluthi moja ya maeneo yote ya Luhansk ya Ukraine na Donetsk lakini waasi wanatamani mengine pia.

    line

    Je, uvamizi huu ni hatari kwa Ulaya?

    Hizi ni nyakati za kutisha kwa watu wa Ukraine na za kutisha kwa bara zima, kushuhudia serikali kuu ikivamia jirani ya Uropa kwa mara ya kwanza tangu Vita vya Pili vya Dunia.

    Makumi ya watu wamekufa tayari katika kile Ujerumani imekiita "Vita vya Putin", raia na wanajeshi. Na kwa viongozi wa Ulaya uvamizi huu umeleta baadhi ya saa za giza zaidi tangu miaka ya 1940. Ilikuwa, alisema Emmanuel Macron wa Ufaransa, hatua ya mabadiliko katika historia ya Uropa. Akikumbuka siku za Vita Baridi vya Umoja wa Kisovieti, Volodymyr Zelensky alizungumzia jitihada za Ukraine za kuepuka pazia jipya la chuma lililoifunga Urusi kutoka kwa ulimwengu wa kistaarabu.

    Ukrainian President Volodymyr Zelensky visiting positions on the frontline with pro-Russian militants in the Donetsk region, Ukraine, 06 December 2021

    CHANZO CHA PICHA,

    EPA

    Kwa familia za vikosi vyote viwili kutakuwa na siku za wasiwasi mbele. Wananchi wa Ukraine tayari wamekabiliwa na vita vikali vya miaka minane na washirika wa Urusi. Jeshi limewaita askari wa akiba wote wenye umri wa miaka 18 hadi 60. Afisa mkuu wa jeshi la Marekani Mark Milley alisema ukubwa wa vikosi vya Urusi utamaanisha hali "ya kutisha" na migogoro katika maeneo yenye miji minene.

    Uvamizi huo una madhara makubwa kwa nchi nyingine nyingi zinazopakana na Urusi na Ukraine. Latvia, Poland na Moldova wanasema kuwa wanajiandaa kwa wimbi kubwa la wakimbizi. Hali ya hatari imetangazwa nchini Lithuania na Moldova, ambako maelfu ya wanawake na watoto tayari wameingia.

    Hii sio vita ambayo idadi ya watu wa Urusi ilitayarishwa kwa ajili yake, kwani uvamizi huo ulipigwa chapa na baraza la juu la bunge lisilo na uwakilishi.

    Nchi za Magharibi zinaweza kufanya nini?

    Nato imeweka ndege za kivita katika hali ya tahadhari lakini muungano wa Magharibi umeweka wazi hakuna mipango ya kutuma wanajeshi wa kivita nchini Ukraine yenyewe. Badala yake wametoa washauri, silaha na hospitali za kutumiwa vitani . Wakati huo huo, wanajeshi 5,000 wa Nato wametumwa katika mataifa ya Baltic na Poland. Wengine 4,000 wangeweza kutumwa Romania, Bulgaria, Hungaria na Slovakia.

    Badala yake, nchi za Magharibi zinalenga uchumi wa Russia, viwanda na watu binafsi.

    • Umoja wa Ulaya umeahidi kuwekea vikwazo Urusi katika masoko ya mitaji na kukata tasnia yake kutokana na teknolojia ya kisasa zaidi. Tayari imewawekea vikwazo wabunge 351 waliounga mkono Urusi kutambua maeneo yanayodhibitiwa na waasi.

    • Ujerumani imesitisha uidhinishaji wa bomba la gesi la Nord Stream 2 la Russia, uwekezaji mkubwa wa Urusi na makampuni ya Ulaya.

    •Marekani imesema itaitenga serikali ya Urusi kutoka kwa mashirika ya fedha ya nchi za Magharibi na kuwalenga "watu" wa ngazi za juu.

    • Uingereza inasema benki zote kuu za Urusi zitafungiwa mali zao, huku watu binafsi na mashirika 100 yakilengwa; na shirika la ndege la taifa la Urusi Aeroflot pia litapigwa marufuku kutua nchini Uingereza

    Ukraine imewataka washirika wake kuacha kununua mafuta na gesi ya Urusi. Mataifa hayo matatu ya Baltic yametoa wito kwa jumuiya nzima ya kimataifa kutenganisha mfumo wa benki wa Russia na mfumo wa malipo wa kimataifa wa Swift. Hilo linaweza kuathiri vibaya uchumi wa Marekani na Ulaya.

    Jiji la Urusi la St Petersburg halitaweza tena kuandaa fainali ya Ligi ya Mabingwa mwaka huu kwa sababu za kiusalama. Shirikisho la soka barani Ulaya Uefa pia linapanga hatua zaidi.

    Nato and US extra troops in Eastern Europe

    Putin anataka nini?

    Rais Putin kwa sehemu alilaumu uamuzi wake wa kushambulia upanuzi wa Nato kuelekea mashariki. Hapo awali alilalamika kuwa Urusi "haikuwa na mahali pengine pa kurudi - wanadhani tutakaa tu bila kufanya kitu?"

    Ukraine inatafuta ratiba ya wazi ya kujiunga na Nato na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi Sergei Ryabkov alieleza: "Kwetu sisi ni lazima kabisa kuhakikisha Ukraine kamwe, kamwe inakuwa mwanachama wa Nato."

    Mwaka jana Rais Putin aliandika kipande kirefu kinachowaelezea Warusi na Waukraine kama "taifa moja", na ameelezea kuporomoka kwa Umoja wa Kisovieti mnamo Desemba 1991 kama "mgawanyiko wa Urusi ya kihistoria". Amedai Ukrainia ya kisasa iliundwa kikamilifu na Urusi ya kikomunisti na sasa ni nchi ya vibaraka, inayodhibitiwa na Magharibi.

    Rais Putin pia ametoa hoja kwamba ikiwa Ukraine itajiunga na Nato, muungano huo unaweza kujaribu kuteka tena Crimea.

    1px transparent line

    Lakini Urusi haijazingatia tu Ukraine. Inataka Nato kurejea katika mipaka yake ya kabla ya 1997.

    Bw Putin anataka Nato kuondoa vikosi vyake na miundombinu ya kijeshi kutoka kwa mataifa wanachama waliojiunga na muungano huo kuanzia 1997 na sio kupeleka "silaha za kushambulia karibu na mipaka ya Urusi". Hiyo ina maana Ulaya ya Kati, Ulaya Mashariki na Baltiki.

    Katika macho ya Rais Putin, nchi za Magharibi ziliahidi mwaka 1990 kwamba Nato ingepanua "sio inchi moja kuelekea mashariki" lakini walifanya hivyo hata hivyo.

    Hiyo ilikuwa kabla ya kuanguka kwa Muungano wa Sovieti, hata hivyo, hivyo ahadi iliyotolewa kwa Rais wa Soviet Mikhail Gorbachev ilirejelea tu Ujerumani Mashariki katika muktadha wa Ujerumani iliyounganishwa tena.

    Bw Gorbachev alisema baadaye "mada ya upanuzi wa Nato haikujadiliwa kamwe" wakati huo.

    Nato amesema nini?

    Nato ni muungano wa kiulinzi na sera yake ni kuwa na mlango wa wazi kwa wanachama wapya, na nchi zake 30 wanachama zinashikilia kuwa hazitabadilika.

    Hakuna matarajio ya Ukraine kujiunga kwa muda mrefu, kama kansela wa Ujerumani ameweka wazi.

    Lakini wazo kwamba nchi yoyote ya sasa ya Nato ingetoa uanachama wake ni jambo lisilo la mwanzo.

    Graphic showing Nato's expansion since 1997
    1px transparent line

    Je, kuna njia ya kidiplomasia?

    Sio kwa sasa, lakini mpango wowote wa mwisho utalazimika kufunika vita vya mashariki na udhibiti wa silaha.

    Russian President Vladimir Putin holds talks with U.S. President Joe Biden via a video link in Sochi, Russia December 7, 2021

    CHANZO CHA PICHA,

    REUTERS

    Marekani ilikuwa imejitolea kuanzisha mazungumzo juu ya kuzuia makombora ya masafa mafupi na ya kati na pia juu ya mkataba mpya wa makombora ya mabara. Urusi ilitaka silaha zote za nyuklia za Marekani zizuiwe kutoka nje ya maeneo yao ya kitaifa.

    Urusi ilikuwa na chanya kuelekea "utaratibu wa uwazi" uliopendekezwa wa ukaguzi wa pande zote kwenye besi za makombora - mbili nchini Urusi, na mbili nchini Romania na Poland.


    CHANZO - BBC SWAHILI


    Share:
    Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

    Popular Posts

    Unordered List

    Pages

    Blog Archive


    Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger