Friday 14 January 2022
WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAKUTANA KWA MAJADILIANO BAADA YA AJALI ILIYOGHARIMU MAISHA YA WAANDISHI WA HABARI
Video : BHUDAGALA MWANAMALONJA - WALE WALE
CHAMA ATAMBULISHWA RASMI SIMBA SC
MHADHIRI ANAYEFAULISHA WANAFUNZI WA KIKE KWA NGONO ATUPWA JELA
Thursday 13 January 2022
Ashikiliwa Na Jeshi La Polisi Kwa Tuhuma Za Kumuua Baba Yake Mzazi Kwa Kisu
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia MUSSA EDWARD NDONDE @ SANGA MAPESA [31] Askari wa JWTZ MT.109772 Kikosi cha Ruvu JKT mkoani Pwani na Mkazi wa Mlandizi kwa tuhuma za kumuua baba yake mzazi aitwaye EDWARD NDONDE [75] Mwalimu Mstafuu, Mkazi wa Lumbila Jijini Mbeya kwa kumkatakata visu sehemu mbalimbali za mwili wake.
Tukio hilo limetokea mnamo tarehe 12.01.2022 majira ya saa 09:00 asubuhi huko Mtaa wa Lumbila uliopo Kata ya Iwambi, Tarafa ya Iyunga, Jijini Mbeya ambapo mtuhumiwa aliuawa EDWARD NDONDE [75] ambaye ni baba yake mzazi kwa kumchoma kisu sehemu mbalimbali za mwili wake na kisha kumkata kiganja cha mkono.
Chanzo cha tukio ni tuhuma za ushirikina kwani inaelezwa kuwa mtuhumiwa anadai kuwa marehemu ambaye ni baba yake mzazi ni mchawi anamloga ili hasifanikiwe kwenye mambo yake. Awali mtuhumiwa alifika nyumbani kwa marehemu majira ya 09:00 asubuhi pasipo kutoa taarifa yoyote ya kuja Mbeya na kuingia moja kwa moja sebuleni na kuanza kumshambulia kwa kisu na stuli na kupelekea kifo chake.
Mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya kwa uchunguzi wa kitabibu. Mtuhumiwa anaendelea kupatiwa matibabu chini ya ulinzi Hospitali ya Rufaa Kanda ya Mbeya baada kushambuliwa na wananchi waliojichukulia sheria mkononi kutokana na tukio alilofanya.
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linalaani tukio hili baya kutokea na litahakikisha mtuhumiwa anafikishwa kwenye mamlaka husika ya sheria kwa hatua zaidi. Aidha Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linatoa rai kwa wananchi kuachana na Imani potofu za kishirikina hasa kuamini waganga wapiga ramli chonganishi kwani ni hatari kwa ustawi wa jamii na maendeleo ya Taifa.
Imetolewa na:
[CHRISTINA A. MUSYANI – ACP]
KAIMU KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.
Rais Samia amuapisha Balozi wa Tanzania Nchini Kuweit na Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Ndugu. Aisha S. Amour kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi) katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Chamwino, Mkoani Dodoma leo tarehe 13 Januari 2022.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimuapisha Ndugu. Said Shaibu Mussa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Kuwait katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Chamwino, Mkoani Dodoma leo tarehe 13 Januari 2022.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiwa katika picha ya pamoja na Ndugu. Aisha S. Amour Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi (Sekta ya Ujenzi) kushoto na Ndugu. Said Shaibu Mussa Balozi wa Tanzania nchini Kuwait kulia, mara baada ya kuwaapisha katika hafla fupi iliyofanyika Ikulu Chamwino, Mkoani Dodoma leo tarehe 13 Januari 2022.
KATIBU MKUU UJENZI BALOZI MHANDISI AISHA AMOUR AWASILI RASMI WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
Wednesday 12 January 2022
RAIS SAMIA AKUTANA NA JOB NDUGAI IKULU
KAMERA KUFUNGWA BUIGIRI KUKABILI AJALI BARABARA KUU DAR-DODOMA
WATATU WAFARIKI KWA KULIPUKIWA NA KINACHODAIWA KUWA NI BOMU
Tuesday 11 January 2022
RAIS SAMIA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA RAIS MWINYI
WAZIRI JAFO AFANYA ZIARA YA KIKAZI KATIKA MSITU WA PUGU KAZIMZUMBWI, AFURAHISHWA NA UTENDAJI KAZI WA TFS
MBUNGE DODOMA APONGEZA TEUZI ZA RAIS SAMIA
MPC YATAJA MAJINA YA WAANDISHI WA HABARI WALIOFARIKI KATIKA AJALI YA GARI, YUMO HUSNA MILANZI... MAJERUHI WAWILI AKIWEMO VANY CHARLES
Video : BHUDAGALA - TULEBHALYO....NGOMA YA HUZUNI SANA
Pakua / Download App ya Malunde 1 blog Tuwe tunakutumia taarifa zote moja kwa moja kwenye simu yako bure kabisa