Thursday 30 September 2021

Chui auawa baada ya kujeruhi wanne Wilaya Ya Hai, Kilimanjaro


Watu wanne wamejeruhiwa na chui wilayani Hai mkoani Kilimanjaro, baada ya chui huyo kuvamia zahanati ya Huruma iliyopo wilayani humo.

Kamanda wa polisi wa mkoa wa Kilimanjaro, Simon Maigwa amesema chui huyo anayedaiwa kutoka Hifadhi ya Taifa ya Mlima Kilimanjaro, alionekana majira ya asubuhi katika eneo la Bomang’ombe.

Amewataja waliojeruhiwa kuwa ni  Emmanuel Usara,  Jesca Nnko, Urusula Cosmas na Maliki Sakia wote wakazi wa Bomang’ombe wilayani Hai.

Hata hivyo askari kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) walifanikiwa kumdhibiti na baadaye kumuua chui huyo kabla hajaleta madhara zaidi.


Share:

FCS YAZINDUA MPANGO MKAKATI MPYA KUSAIDIA WANANCHI... DKT. TENGA ATAKA ASASI ZA KIRAIA KUSHIKAMANA

Rais wa Taasisi ya Foundation For Civil Society (FCS) Dkt. Stigimana Tenga amezitaka Asasi za kiraia nchini kushikamana kwa pamoja na kuhakikisha wanazisemea kazi wanazofanya katika Taasisi zao ili ziweze kufahamika kwa wananchi na jamii kwa ujumla.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa Mpango Mkakati mpya wa Foundation For Civil Society (FCS) Dkt. Tenga amesema Asasi za Kiraia zinapaswa kujengwa kutokana na kwamba ni muhimili mkubwa wa maendeleo nchini na wananchi wanapaswa kuzifahamu.

Pia amezitaka Asasi hizo kuhakikisha zinaangalia mifumo mbalimbali inayowaongoza ambayo ndiyo miundombinu ya uwajibikaji katika kazi zao hususani katika kutatua matatizo ya wananchi.

“Tuisemee sekta hii na yale yote ambayo sekta hii inayafanya kwenye jamii, yasemeeni mnayoyafanya ili yajulikane msione aibu yeyote,”alisema Dkt. Tenga.

Aliongeza kuwa Asasi zinapaswa kutatua matatizo ya wananchi na kusaidia kuyaondoa hilo ndiyo lengo kubwa la FCS katika Dira yake.

“Tujenge uwajibikaji katika misingi ya ubinadamu na utu bila kujali kuna nini, bali kuwashirikisha wenzetu matatizo ambayo sekta ya Asasi za kiraia nchini inapitia ambayo yanahitaji kutatuliwa kwani ni matatizo yanayojikita katika mifumo,” aliongeza Dkt. Tenga.

Aidha alisema hawapaswi kutatua matatizo kwa mbinu zile zile za zamani ambazo sio mbinu za kujenga mifumo bali ni mbinu za kutoa huduma.

“Tusipoangalia hivyo tutazidi kuona hizo mbinu zinaongezeka na kuwa kubwa sana na kuhakikisha wanaangalia mifumo ambayo ndio miundombiniu ya uwajibikaji katika asasi,” alisema.

Kwa Upande wake,Mkurugenzi Mtendaji wa FCS Francis Kiwanga alisema wamezindua mpango mkakati mpya wa FCS ambao unalenga kushuka chini hususani vijijini katika kuwasaidia wananchi.

Alisema kupitia mpango huo, Taasisi yao itaendelea kufanya kazi na Asasi mbalimbali za kiraia ambao ndiyo wadau wao muhimu katika kuwafikia wananchi.

Alisema falsafa ya Taasisi yao inaamini kuwa umaskini,hali ya kutokuwa na haki katika jamii,hali ya ukandamizaji watu wengine ni tatizo kubwa na ni adui wakubwa wa maendeleo.

Alisema katika rasilimali zao takribani asilimia 90 zinakwenda vijijini kuhudumia wananchi.

“Rasilimali zetu tunayogawa kila mwaka asilimia 90 inakwenda vijijini ,tunaamini waliopo Dar es Salaam ,Taasisi nyingi zinaweza kufanya kazi na watu wengine kokote duniani kuliko waliopo vijijini” alisema Kiwanga.

Pia aliongeza kwa kusema kuwa katika mpango kazi wao wanazingatia usawa wa kijinsia,kufanya kazi na wadau wao kuwapa heshima inayostahili na kuwaheshimu kwani wao ndio wabia wao wakubwa na kwamba sauti yao ina ukubwa wa kuweza kuwafikia wananchi.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Asasi za kiraia, Dkt. Richard Samabiga aliipongeza FCS kwa hatua hiyo ya kuzindua mpango mkakati huo ambao unaonyesha dira ya kusaidia wananchi katika maeneo mbalimbali.

Alisema mpango huo unaleta matumaini makubwa kwa Asasi za kiraia katika kufanya kazi zao za kusaidia wananchi.

Mpango mkakati huo umejikatika katika kutekeleza miradi ya utawala bora, usawa wa kijinsia na watu wenye ulemavu, kukuza uchumi na kujenga amani na utatuzi wa migogoro.
Rais wa FCS Dkt. Stigimana Tenga akizungumzia mpango huo mara baada ya kuzinduliwa rasmi mwishoni mwa wiki Jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa FCS Francis Kiwanga (wa tatu kulia) akiwa na Rais wa Taasisi hiyo Dkt. Stigimana Tenga (katikati) na mwenyekiti wa Bodi ya FCS Dkt. Richard Samabiga (wa kwanza kulia) wakiangalia mpango mkakati utakaotekelezwa kwa kipindi cha miaka mitano mara baada ya kufanyika uzinduzi rasmi wa mpango huo uliofanyika mwishoni mwa wiki kwenye Ofisi za FCS Jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mtendaji wa FCS Francis Kiwanga akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi huo akielezea namna ambavyo FCS itavyotekeleza majukumu yake katika kuusimamia mpango huo.
Baadhi ya watumishi wa FCS na wageni mbalimbali waalikwa wakiwa kwenye hafla ya uzinduzi huo.



Share:

350 Jobs Opportunities at Tanzania Immigration Department (Ajira uhamiaji)

350 Jobs at Tanzania Immigration Department (Ajira uhamiaji) September, 2021. The Immigration Services Department is established under Section 4(1) of the Immigration Act of 1995 Chapter 54 as amended by Act No.8 of 2015.  It gives the Department the authority to control and facilitate immigration issues in the United Republic of Tanzania. The Department is […]

This post 350 Jobs Opportunities at Tanzania Immigration Department (Ajira uhamiaji) has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Global Compliance Manager at Pathfinder

Pathfinder Overview   Pathfinder International is driven by the conviction that all people, regardless of where they live, have the right to decide whether and when to have children, to exist free from fear and stigma, and to lead the lives they choose. Since 1957, we have partnered with local governments, communities, and health systems […]

This post Global Compliance Manager at Pathfinder has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

JUA BANDIA KUFANYA KAZI MWAKA 2035


Picha ya mradi wa International Thermonuclear Experimental Reactor (ITER)
 ****
China ni miongoni mwa mataifa yaliyopiga hatua kwenye upande wa Teknolojia na hivi karibuni wameweka rekodi mpya baada ya kufanikiwa kutengeneza ‘Plasma’ ya nyuzi joto Milioni 120 kwa sekunde 101 na joto la Milioni 160 Celsius kwa sekunde 20.

Kituo hicho cha utafiti ni sehemu ya mradi mkubwa wa dunia “International Thermonuclear Experimental Reactor” (ITER), ambapo nchi nyingi zinashiriki kufanya majaribio ya kutengeneza nishati salama inayotokana na ‘nuclear fusion’ na itaanza kufanya kazi mwaka 2035 kwenye nchi kama 35.
Share:

General Trade Executive at TotalEnergies

Description Du Poste   HSEQ   Respect of the Golden rules and all the HSE rules and standards of TOTAL by all the staff, contractors, customers…   PLANNING   Implements the affiliate marketing strategy Participates in the development of affiliate marketing plans on General Trade on the basis of GT in the box master plan, […]

This post General Trade Executive at TotalEnergies has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

6 Job Opportunity at Sikonge District Council and MDH

Share:

IT Officer Cum Software Developer at MDH

POSITION: IT Officer Cum Software Developer (1 Post)   LOCATION:        Dar es Salaam REPORTS TO:    IT Manager Job Summary:  IT Officer Cum Software Developer will be responsible to study existing systems and procedures and develop software applications to automate various MDH programmatic and operations activities. She/He will design and develop software applications […]

This post IT Officer Cum Software Developer at MDH has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Serikali Kuendelea Kuboresha Mazingira Ya Watu Wenye Ulemavu


NA MWANDISHI WETU, DODOMA
SERIKALI imesema inaendelea na utaratibu wa kujenga na kukarabati vyuo vya watu wenye ulemavu kwa lengo la kuwasaidia wenye ulemavu kupata ujuzi ili kujikomboa kiuchumi.

Akizungumza Jijini Dodoma baada ya kupokea msaada wa vifaa visaidizi kwa ajili ya wenye ulemavu vyenye thamani ya shilingi milioni 13.9 ambavyo ni viti mwendo 55 na fimbo nyeupe 50 za wasioona kutoka kwa Taasisi ya kutoa huduma ndogo za kifedha (ASA Microfinance Company Limited), Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga alisema dhamira ya Serikali ni kuhakikisha kila mtanzania anapata haki yake bila vikwazo.

Aliongeza kuwa ipo mikakati madhubuti ya kuhakikisha masuala ya wenye ulemavu yanapewa kipaumbele ikiwemo uboreshwaji wa vyuo ikiwemo Chuo cha Mwanza ambacho ujenzi wake unatarajiwa kukamilika kuanzia mwezi Januari mwakani kuwawezesha vijana kupata mafunzo ambayo yatawasaidia kufanya shughuli zao za uzalishaji na kushiriki katika maendeleo ya Taifa kwa ujumla.

“Kwasasa Wizara inaratibu kwa kasi ujenzi wa vyuo vya watu wenye ulemavu na ufufuaji wa vile ambavyo vipo.Tunaendelea kufanya hivyo katika Chuo cha Yombo Dar es salam, tumezindua Chuo kingine Tabora ambacho kilikuwa kimefungwa kwa miaka 10 na kumalizia ujenzi wa chuo cha kisasa Mkoa wa Tanga,” alisema Naibu Waziri Ummy.

Pia Naibu Waziri huyo alibainisha kuwa Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan imeweka mkazo kuwasaidia watu wenye ulemavu kwa kuendelea kutoa fedha ya elimu bila malipo ambapo watu wenye ulemavu nao hunufaika na mfumo huo huku akieleza kuwa Serikali inatambua changamoto zinazowakabili watu wenye ulemavu.

“Serikali kupitia bohari kuu ya dawa inaendelea kuagiza mafuta ili kuwakinga dhidi ya saratani ya Ngozi kwa watu wenye ualbino sambamba na kuzitaka Halmashauri kuendelea kutenga fedha za mapato ya ndani kupitia asilimia 10 inayotolewa na kila Halmashauri kwa wanawake, vijana na wenye ulemavu kwa sababu hii inawasaidia kupambana na umasikini,”alieleza.

Hata hivyo aliishukuru kampuni hiyo kwa moyo wake wa kujitoa na kuiunga mkono serikali katika juhudi za kuwaletea ustawi wananchi wake na kuwahimiza wadau wengine wa maendeleo kujitokeza kuwasaidia watu wenye ulemavu hatua itakayofanya kujiona wana thamani na kutambulika ndani ya jamii.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa ASA Microfinance Limited , Muhammad Shah Newaj alieleza kwamba wametoa msaada huo wenye thamani ya Sh. milion 13.9 kama sehemu ya kutambua mchango wa watu wenye ulemavu katika maendeleo kuanzia ngazi ya familia hadi Taifa akisema wana uwezo wa kufanya kazi kama watu wengine endapo watapewa fursa na kuhudumiwa katika mahitaji yao wataendelea kushirikiana na Serikali kuhakikisha wanaisaidia jamii kuepukana na umaskini.

Naye Afisa Sheria kutoka ASA Microfinance Limited, Zephania Paul alifafanua kwamba vifaa hivyo ni sehemu ya kutoa huduma kwa jamii na awamu hiii ni yapili kufanyika akisema awamu ya kwanza ilifanyika jijini Dar es salaam huku akibainisha kuwa taasisi hiyo ipo katika Mikoa nane ya Tanzania Bara na Zanzibar na hadi sasa wamewafikia wanawake 1,600 na kutoa ajira .

Akitoa shukrani zake mama wa mtoto mwenye ulemavu Martha Mshama aliishukuru serikali kwa kushirikiana na wadau kuendelea kuwajali watu wenye ulemavu akieleza kuwa kiti alichopewa kitamsaidia kufanya kazi zake kwani awali alikuwa akitumia muda mwingi kuwa karibu na mtoto akihofia kuanguka na kupata madhara.

” Tunaishukuru serikali kwa kutupatia viti mwendo ambapo ni msaada mkubwa kwangu maana nilikuwa nikihofia usalama wa mtoto wangu kuna wakati anaweza kuanguka natakiwa kuwa naye karibu sana lakini sasa walau nitaweza kufanya kazi zangu nawashukuru sana Mungu awabariki,”alishukuru Martha.

Naye Selina Nigangwa (mwenye ulemavu wa miguu) mkazi wa Swaswa aliishukuru serikali kwa kuwapatia msaada huo na kushauri wakati mwingine kutoa viti vya kuendesha kwa kutumia mikono.

“Tunashauri serikali wakati mwingine watoe viti vya kuendesha kwa mikono ili tuweze kuendesha wenyewe bila kumtegemea mtu,” alieleza Selina.


Share:

HUYU NDIYO MTU MCHAFU KULIKO WOTE DUNIANI..HUYU ' MWAMBA' HAJAOGA ZAIDI YA MIAKA 60, ANAVUTA KINYESI KAMA SIGARA



Je, wewe huwa unapenda kuoga au hupendi kuoga. Kama hupendi kuoga basi nadhani leo utafarijika baada ya kufahamu kuwa yupo mtu asiyependa kuoga kuliko wewe.

Unasema hupendi kuoga lakini huwezi kupitisha wiki bila kuoga, acha kutudanganya wewe unapenda kuoga. Kama hupendi kuoga kweli unaonaje miezi au miaka kadhaa ikapita bila ya mwili wako kugusa maji? Usijali hutakufa.

Yupo mtu ambaye hajaoga kwa miongo kadhaa lakini bado anaishi, yaani tunaweza kusema kwamba yeye ni mchafu kuliko uchafu wenyewe, lakini hilo kwake halimsumbui na huyu si mwingine bali ni mzee ajulikanaye kama Amou Haji.

Haji anaogopa maji, kwa hivyo anachukia kuoga, anaamini ataugua ikiwa ataoga na hii imemzuia kuoga kwa zaidi ya miongo sita.

 Amou Haji, raia wa Irani mwenye umri wa miaka 83 ametajwa kama mtu mchafu zaidi ulimwenguni kwani hajaoga katika kipindi cha miaka 65.

Maisha katika jangwa la Irani, na nyama ya nungu nungu iliyooza ikiwa kama chakula chake akipendacho, ndio amezoea. Maisha yake ni uchafu kuanzia anachokula anapoishi na hata mwili wake binafsi.

Ili kuwa na afya hunywa lita tano za maji kutoka kwenye kopo la mafuta lenye kutu kila siku. Pia anapenda kuvuta sigara lakini mtindo wake wa kuvuta sigara unajumuisha kuvuta kinyesi kikavu cha ng’ombe badala ya tumbaku lo! Hutatamani kuwa karibu naye.

Wenyeji wanaamini kuwa moyo uliovunjika ndio sababu Amou Haji alichagua mtindo huu wa maisha. Lakini, bado hajakata tamaa ya kupata upendo.

Haji hana nyumba, anazurura karibu na kijiji kilichotengwa cha Dejgah katika mkoa wa Kusini mwa Irani wa Fars na anaishi kwenye mashimo yaliyotengenezwa jangwani nje ya kijiji. Ingawa wanakijiji walimjengea kibanda lakini alichagua kutoishi hapo.

Amekuwa na rangi inayotaka kufanana na ardhi inayomzunguka na anajichanganya kabisa na mazingira yake. Wenyeji wanasema mara nyingi huwa wanamfanisha na mwamba wakati anapokuwa ametulia kimya. Haji hajali raha za ulimwengu na anaridhika kuishi maisha ya uchafu na ya kuhamahama.
Share:

MZEE NATABAY AFARIKI AKIWA NA UMRI WA MIAKA 127...FAMILIA YAOMBA AINGIE KWENYE KITABU CHA GUINNESS WORLD RECORDS


Mzee mmoja aitwaye Natabay Tinsiew huko nchini Eritrea amefariki akiwa na umri wa miaka 127, familia yake imesema.

Aidha familia hiyo imesema ina matumaini kwamba Natabay Tinsiew atapata nafasi ya kuandikwa kwenye kitabu cha Guinness World Records kama mtu aliyewahi kuishi miaka mingi zaidi.

"Uvumilivu, ukarimu na maisha ya furaha" ndio siri ya mzee huyo kuishi kwa muda mrefu, mjukuu wake Zere Natabay aliiambia BBC Tigrinya.

Bwana Natabay alifariki siku ya Jumatatu akiwa na amani katika kijiji chake, Azefa - ambacho kina idadi ya watu takribani 300 na kipo kwenye korongo lililozungukwa na milima.

Mjukuu wake amesema rekodi za kanisa - pamoja na cheti chake cha kuzaliwa - kinaonesha kuwa alizaliwa mnamo mwaka 1894 - na ndio mwaka ambao alibatizwa - na hivyo kumfanya awe amefariki akiwa na miaka 127.

Lakini familia ya Bw. Natabay inaamini kuwa mzee huyo alizaliwa mnamo mwaka 1884, lakini alibatizwa miaka 10 baadaye, wakati mapadre walipokuja karibu na kijijini kwao.Kulikuwa na mapadre wachache wakati huo, na watu walikuwa wakiwasubiri watembelee kijiji chao.

Padre Mentay, wa kanisa katoliki ambaye alihudumu katika kijiji hicho kwa miaka saba, alithibitisha kwamba rekodi zilionesha kwamba Bwana Natabay alizaliwa mnamo 1894. Alisema alikuwepo wakati wanakijiji wakisherehekea alipotimiza miaka 120 mnamo 2014.

Bwana Zere aliiambia BBC kuwa tayari alikuwa amewasiliana na Guinness World Record ili kuthibitisha hati rasmi za kuzaliwa kwa babu yake, na alikuwa akingojea kusikia kutoka kwao.

Katika kitabu cha Guinness World Records kimemrekodi mwanamke wa Ufaransa Jeanne Calment, aliyekufariki mnamo 1997 akiwa na miaka 122, kama mtu aliyeishi miaka mingi zaidi.

Bwana Natabay alioa mnamo mwaka 1934, mke wake alifariki mwaka 2019 akiwa na umri wa miaka 99.

Wakati wa maisha yake, Bwana Natabay alikuwa mfugaji, mwenye ng'ombe wengi, mbuzi na nyuki.

Vilevile alifanikiwa kuishi na kuona vizazi vitano vya familia yake vikikua.

Bwana Zere alisema babu yake atakumbukwa kama "mtu wa kushangaza", ambaye alikuwa mwema, anayejali na mchapa kazi.
Share:

GGML YATOA MILIONI 800 KUKARABATI HOSPITALI YA RUFAA GEITA



Baadhi ya madaktari ambao ni wanachama wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), wakishirikiana na wadau mbalimbali kutoa huduma za afya bure kwa wakazi wa mji wa Geita. Mpango huo maalumu wa siku tatu umefadhiliwa na GGML chini ya uratibu wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita na chama hicho.
 ***
Na Mwandishi Wetu 
Kampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita na Chama cha Madaktari Tanzania (MAT) imetoa kiasi cha Shilingi milioni 800 kukarabati Hospitali ya Rufaa Geita.

Pia imesaidia uchunguzi wa bure wa matibabu kwa watu wa Geita kwa siku tatu kuanzia tarehe 27 Septemba 2021 hadi 29 Septemba 2021.

Akizungumzia program hiyo ya matibabu bure, Rais wa Chama cha Madaktari (MAT), Dk. Shadrack Mwaibambe alisema chama chake kina utamaduni wa kutoa huduma za afya bure kwa jamii kabla ya mkutano wao wa kila mwaka.

"Kwa kawaida MAT huwa na mizunguko tofauti katika mikoa yote inayotoa huduma za matibabu bure kwa jamii. Hii ni mara yangu ya kwanza kuja katika mji wa Geita na kupata vifaa vya kisasa vya matibabu ambavyo vilitolewa kama msaada kutoka GGML kwenda kwa Hospitali ya Rufaa ya Geita. Msaada huu umetusaidia sana katika uchunguzi wa awali wa wagonjwa wetu.

"Wakazi wa Geita wanapaswa kujivunia uwekezaji huu wa GGML katika hospitali hii kwani vifaa vingi vinavyopatikana hapa pia vinapatikana katika hospitali kuu kama Bugando na Muhimbili. Mchango wa GGML kwa vifaa hivi vya kisasa unapaswa kupongezwa, "alisema.

Aidha, Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa katika Hospitali ya Rufaa ya Geita Dk. Michael Mashallah alikiri msaada wa GGML na wadau wengine waliohusika katika mradi huo utainufaisha vilivyo jamii ya wana Geita.

"Huu ni msaada ambao umma wa aina yoyote ungependa kupata kwa sababu upatikanaji wa huduma za afya ni muhimu sana kwa sababu inaweza kuokoa maisha.

“Nawashukuru wadau wote kwa msaada wao, haswa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Geita, GGML, MAT, AMREF, CORDET, NELICO, Fhi360, MNH, BMC, ORCI, JKI, TANCDA, Maria Stope, MDH na SHDEPHA, "alisema Dk. Mashallah.

Kwa upande wake Makamu wa Rais wa GGML, Simon Shayo alisema kama raia na mshirika wa maendeleo, GGML imejitolea kushirikiana na serikali kuhakikisha huduma za afya zinazopatikana katika mkoa wa Geita.

Alisema kuwa GGML imetoa Shilingi milioni 800 kwa Hospitali ya Rufaa ya Geita kwa lengo la kuhudumia zaidi ya wakazi milioni 1.7 wanaoishi katika mji huo.

"GGML imekarabati majengo mbalimbali ya Hospitali ya Mkoa ya Geita, ambayo yalijengwa mwaka 1957. Pia imewapa vifaa vya matibabu vinavyoiwezesha hospitali kutoa huduma za uchunguzi wa moyo na meno.

“Msaada huu utahakikisha wan- Geita wanaanza kupata huduma za matibabu ya kibingwa kama zile zilizokuwa zinatolewa kule kwenye Hospitali ya Rufaa Moi jijini Dar es Salaam.

“Msaada huo umejumuisha ununuzi wa mashine ya ECG, jenereta ya dharura ya vifaa vya meno na ujenzi wa majengo ya kisasa ya dharura na kwa watoto wanaozaliwa kabla ya muda yaani njiti," alisema.

Alisema mkoa wa Geita unakua haraka na ndoto ya GGML ni kujenga vituo vya afya vya kisasa ndani jamii inayowazunguka.

“GGML imetekeleza miradi kadhaa ya afya, hasaa ujenzi wa zahanati huko Nyamalembo, Nyakahongola, Kasota na Kakubiro ambazo kila moja iligharimu zaidi ya Sh milioni 260.

“Mwaka wa 2019, GGML pia ilitoa vifaa vya matibabu kwa vituo vya afya vyenye thamani ya Sh milioni 142 kusaidia zahanati za Katoro na Bukoli huko Geita. Katika mwaka huo huo, GGML pia ilitoa darubini mbili za kisasa zenye thamani ya takriban Sh milioni 13 kwa Mkuu wa Mkoa wa Geita.

“Mwaka jana, GGML ilitoa vifaa na vifaa vya matibabu, pamoja na vifaa vya upasuaji wa mifupa, mashine ya ECG na kifaa cha kuangazia, kwa idara ya mifupa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Sekou Toure.
Baadhi ya madaktari ambao ni wanachama wa Chama cha Madaktari Tanzania (MAT), wakishirikiana na wadau mbalimbali kutoa huduma za afya bure kwa wakazi wa mji wa Geita. Mpango huo maalumu wa siku tatu umefadhiliwa na GGML chini ya uratibu wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Geita na chama hicho.
Share:

HUAWEI YAWAPIGA MSASA WATALAAM 19 WA TEHAMA KUENDANA NA MABADILIKO YA TEHAMA


Mwakilishi kutoka Huawei Tanzania, Yohana Mathias (kulia) akimkabidhi cheti Rweyemamu Barongo ambaye ni mmoja wa washiriki mafunzo ya uchakataji wa data kubwa yaliyotolewa jijini Dar es salaam na Kampuni ya Huawei Tanzania kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya Tehama kwa muda wa siku saba. Kushoto ni Msimamizi wa shughuli za uendeshaji wa Tehama kutoka katika Tume hiyo, Mhandisi Jasson Ndanguzi.
Mwakilishi kutoka Huawei Tanzania, Yohana Mathias (kulia) akimkabidhi cheti Catherine Teodor ambaye ni mmoja wa washiriki mafunzo ya uchakataji wa data kubwa yaliyotolewa jijini Dar es Salaam na Huawei Tanzania kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya Tehama kwa muda wa siku saba. Kushoto ni Msimamizi wa shughuli za uendeshaji wa Tehama kutoka katika Tume hiyo, Mhandisi Jasson Ndanguzi.
Baadhi ya washiriki wa mafunzo ya uchakataji wa data kubwa yaliyoratibiwa na Kampuni ya Huawei Tanzania kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya Tehama jijini Dar es Salaa. Jumla ya watalaam 19 wa Tehama wamepatiwa mafunzo hayo ya siku saba.
Msimamizi wa shughuli za uendeshaji wa Tehama kutoka katika Tume hiyo, Mhandisi Jasson Ndanguzi akizungumza na washiriki wa mafunzo ya uchakataji wa data kubwa yaliayofanyika jijini Dar es Salaam kwa muda wa siku saba.
Mwakilishi kutoka Huawei Tanzania, Yohana Mathias akizungumza na washiriki wa mafunzo ya uchakataji wa data kubwa yaliayofanyika jijini Dar es Salaam kwa muda wa siku saba.
Washiriki mafunzo ya uchakataji wa data kubwa yaliyotolewa na Kampuni ya Huawei kwa kushirikiana na Tume ya Taifa ya Tehama kwa muda wa siku saba jijini Dar es salaam wakiwa katika picha ya pamoja.
**


Na Mwandishi wetu
Kampuni ya Huawei Tanzania kwa kushirikiana na Tume ya Tehama imetoa mafunzo kwa wataalamu 19 wa Tehama kutoka katika sekta ya umma na binafsi kwa lengo la kuwaongezea ujuzi watalaam wazalendo.

Akifunga mafunzo hayo jijini Dar es Salaam hivi karibuni, Mwakilishi wa uongozi kutoka Kampuni ya Huawei Tanzania, Yohana Mathias amesema mafunzo hayo ni chachu katika kuendelea kuibua ubunifu mpya kwenye sekta ya Tehama.

Amesema mafunzo hayo yaliyofanyika kwa siku saba ni kielelezo tosha namna Huawei inashirikiana na Serikali katika kunoa Watanzania wengi waweze kumudu kufanya kazi kubwa zinazohusu uchakataji wa data badala ya kwenda kuchukua watalaam kutoka nje ya nchi.

“Huawei kila mara tumekuwa tukishirikiana na Serikali kutoa mafunzo ya aina hii kwa sababu tunaamini Tehama ni sekta ambayo inakua kwa kasi hivyo ni vema kuwaandaa Watanzania kuendana na mapinduzi ya nne ya viwanda duniani,” amesema.

Aidha, Msimamizi wa shughuli za uendeshaji wa Tehama kutoka Tume ya Taifa ya Tehama, Mhandisi Jasson Ndanguzi pamoja na kuishukuru kampuni ya Huawei kwa jitihada hizo, amesema mafunzo hayo ni moja ya mikakati ya Tume hiyo katika kutengeneza mpango wa Taifa wa miaka mitatu wa maendeleo.

Amesema mpango huo pia unalenga kuwasajili watalaam wa Tehama, pamoja na kuwaendeleza kwa kuwajengea uwezo ili kuenenda na maendeleo ya Tehama duniani.

“Ndani ya mapinduzi ya nne ya viwanda kunatumika teknolojia ya hali ya juu ndio maana Tume tumeona kuna haja ya kuwajengea uwezo mpya kwa sababu inawezekana teknolojia wanazotumia zinapitwa na wakati…na hii ndio sababu tunawashukuru sana wenzetu wa Huawei kwa jitihada zao katika kufanikisha mpango huu,’’

“Kwa hiyo mbali na mafunzo tunawasajili ili tuweze kujua tuna wanataalam wangapi kama nchi na watalaam hao kila mwaka na kila siku wanajiendeleza kivipi ili kama nchi tujue tuna ujuzi kiasi gani na tunaweza kunufaika vipi na fursa zilizopo kwenye Tehama,” amesema.

Ameongeza kuwa Serikali imekuwa ikiboresha miundombinu ya Tehama lakini sasa inaanza kuweka mkazo kwenye uboreshaji wa rasilimali watu ili Tanzania iwe na watalaam wa kutosha.

“Kwa hiyo mafunzo haya yanahusu big data analysis yaani uchakataji wa data kubwa ambazo zinaweza kusaidia kutoa taarifa sahihi na kuwezesha kufanya maamuzi sahihi ya kiutawala na kimaendeleo,” amesema.

Amesema tangu wazindua mpango wa mafunzo hayo Aprili mwaka huu, jumla ya washiriki 157 wamefaidika na kuongezewa ujuzi katika maeneo ya uchakataji wa data kubwa, usimamizi wa miradi ya Tehama, Cyber security na mafunzo mengine.

Aidha, Mmoja wa wakufunzi wa mafunzo hayo kutoka Huawei, Oscar Mashauri amesema Mwalimu amesema mafunzo hayo ni muarobaini kwa watalaam hao ambao walikuwa wanashindwa kuchakata data kubwa kwenye ofisi zao kwa kuwa hawakuwa na mbinu wala utalaam wa kuzichakata.

“Wameridhika na mafunzo kutoka Huawei kwa sababu wamegundua wanaweza kufanyia kazi wakiwa kwenye maofisi yao,” amesema.

Aidha, mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo Rweyemamu Barongo ambaye ni mtaalam wa Tehama kutoka Benki Kuu ya Tanzania (BOT), amesema mafunzo hayo yanakwenda kuwapeleka kwenye ulimwengu mpya.

“Tuna imani yatatusaidia kwenye maeneo yetu ya kazi na kuonggeza ubunifu mpya kwa manufaa yetu na manufaa ya nchi kwa ujumla…na zaidi niishukuru sana kampuni ya Huawei kwa kufanikisha hili,” amesema.

Share:

KIJANA AUAWA KWA VISU KISHA KUNING'INIZWA JUU YA MTI WA MPARACHICHI



Kijana Melkezedik Robert mwenye umri wa miaka 35, mkazi wa kijiji cha Nyerezi, Arumeru mkoani Arusha, amekutwa amekufa huku mwili wake ukiwa umening’inizwa juu ya mti ya mparachichi.

Mwenyekiti wa ulinzi wa wa Kitongoji cha Achi, aliyejitambulisha kwa jina moja la Agesmun, amesema walikuta mwili wa kijana huyo ukiwa umekatwakatwa visu katika maeneo mbalimbali mgongoni.

Alisema mara baada ya polisi kufika, waliwashikilia baba na mdogo wa marehemu ambaye inasadikika alikuwa na ugomvi na marehemu kaka yake.
Share:

Retention Officer (RO) at MDH

POSITIION: Retention Officer (RO) (8 Posts)   LOCATION:        Geita, Kagera, Tabora and Dar es Salaam REPORTS TO:    District Project Manager/ Regional Retention Manager Job Summary: The Retention Manager (RO) is responsible for the day to day implementation of MDH’s retention and continuity of care programs and services. She/he work with Council Health […]

This post Retention Officer (RO) at MDH has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Community ART Officer (CAO) at MDH

POSITION: Community ART Officer (CAO) (8 Posts)   LOCATION:        Kagera, Geita & Dar es Salaam REPORTS TO:    District Community Services Manager (DCSM) Job Summary:  The Community ART Officer (CAO) is responsible for the day-to-day field implementation of MDH’s community ART program and services. She/He will work with the Council Health Management Teams […]

This post Community ART Officer (CAO) at MDH has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

TAMISEMI: Call for Work at Benjamin Mkapa Foundation (BMF) Released Today 29th September, 2021 | Download All Names Here

Overview   The Benjamin William Mkapa Foundation (BMF) is a non- profit Trust, established in 2006 with the vision towards healthy lives and well-being for all, in Tanzania and the rest of Africa. Its strategic focused results areas include to combat HIV and AIDS, TB, Malaria and Reproductive, Maternal New Born, Child and Adolescent Health […]

This post TAMISEMI: Call for Work at Benjamin Mkapa Foundation (BMF) Released Today 29th September, 2021 | Download All Names Here has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger