Saturday 31 July 2021

MWANZA FRIENDS WAKUTANA SHINYANGA MJINI KUZINDUA KATIBA ,KUSAKA FURSA ZA UWEKEZAJI


Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association, Patrick Joseph akionesha Katiba na Nyaraka mbalimbali za Kikundi cha Mwanza Friends Association.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Wanachama wa Kikundi cha Wafanyabiashara na Watumishi wa Umma  Marafiki kutoka Mwanza maarufu ‘Mwanza Friends Association’ wanaofanya shughuli zao kwenye mikoa mbalimbali nchini Tanzania wamekutana Mjini Shinyanga kwa ajili ya kikao na kuzindua rasmi Katiba yao pamoja na kutafuta fursa za uwekezaji katika Mkoa wa Shinyanga.

Wanachama hao wa Mwanza Friends Association wamefanya kikao chao kilichoambatana na ziara ‘Tour’ mkoani Shinyanga leo Jumamosi Julai 31 katika Hoteli ya Liga Mjini Shinyanga.

Akizungumza katika kikao hicho, Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association, Patrick Joseph amesema walianzisha kikundi hicho mwaka 2014 kwa lengo ya kusaidiana katika shida na raha.

“Kikundi cha Marafiki kutoka Mwanza 'Mwanza Friends Association' chenye Makao yake Makuu Jijini Mwanza kinaundwa na Wafanyabiashara na Watumishi wa Umma wanaotoka Mkoa wa Mwanza lakini sasa wanaishi kwenye mikoa mingine nchini”,amesema Joseph.

“Sisi tunajihusisha na masuala ya kusaidiana kijamii katika shida na raha. Hivi sasa tuna wanachama 35 na tuna miradi ukiwemo mradi wa VIP Bar iliyopo Maduka Tisa Ilemela Jijini Mwanza”,ameeleza.

Amesema wanachama wa Mwanza Friends Association kutoka mikoa mbalimbali nchini wameamua kufanya kikao chao Mjini Shinyanga na kuzindua rasmi Katiba yao ikiwa ni sehemu ya ziara yao ya kutafuta fursa za uwekezaji zilizopo mkoani Shinyanga.

Joseph ametumia fursa hiyo kuwakaribisha wanaotaka kujiunga na Mwanza Friends Association na kuwaomba wawasiliane na Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association kwa simu namba 0755 863 330 (Patrick Joseph) au Katibu Omary Haji (0653261226).

ANGALIA PICHA HAPA
Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association, Patrick Joseph akionesha Katiba ya Kikundi cha Mwanza Friends Association wakati wa kikao cha Wanachama wa kikundi hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Liga Hotel Mjini Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association, Patrick Joseph akizungumza wakati akifungua kikao cha Wanachama wa kikundi hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Liga Hotel Mjini Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021. Kulia ni Mweka Hazina, Respicius Rwegoshora, kushoto ni Katibu, Omary Haji.
Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association, Patrick Joseph akizungumza wakati akifungua kikao cha Wanachama wa kikundi hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Liga Hotel Mjini Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021.
Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association, Patrick Joseph akizungumza wakati akifungua kikao cha Wanachama wa kikundi hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Liga Hotel Mjini Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021.
Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association, Patrick Joseph akiwakaribisha wanaotaka kujiunga na Mwanza Friends Association na kuwaomba wawasiliane na Mwenyekiti wa Mwanza Friends Association kwa simu namba 0755 863 330 (Patrick Joseph) au Katibu Omary Haji (0653261226).
Katibu wa Mwanza Friends Association Omary Haji akizungumza kwenye kikao cha Wanachama wa kikundi hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Liga Hotel Mjini Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021.
Mweka Hazina wa Mwanza Friends Association, Respicius Rwegoshora akizungumza kwenye kikao cha Wanachama wa kikundi hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Liga Hotel Mjini Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakiwa kwenye kikao

Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Mweka Hazina wa Mwanza Friends Association, Respicius Rwegoshora akipata chakula
Katibu wa Mwanza Friends Association Omary Haji akipata chakula
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakila chakula cha pamoja Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakipiga picha ya kumbukumbu Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakipiga picha ya kumbukumbu Liga Hotel Mjini Shinyanga.
Wanachama wa kikundi cha Mwanza Friends Association wakipiga picha ya kumbukumbu Liga Hotel Mjini Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021.


Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:

MBUNGE NEEMA LUGANGIRA ATOA NENO FEDHA ZINAZOKUJA NCHINI KWA AJILI YA NGOs

 

MBUNGE wa Viti Maalumu CCM (NGOs Tanzania Bara) Neema Lugangira akizungumza  wakati wa  Uzinduzi wa Wiki ya Azaki imefanyika Jijini Dar es Salaam Julai 29 Julai 2021

MBUNGE wa Viti Maalumu CCM (NGOs Tanzania Bara) Neema Lugangira amesema wakati umefika kuhakikisha fedha za ufadhili ambazo zinatoka nje ya nchi zinazokuja nchini ziweze kufanyiwa kazi na kutelezwa na NGOs na CSOs kutoka ndani ya nchi.

Aliyasema hayo Siku ya Uzinduzi wa Wiki ya Azaki imefanyika Jijini Dar es Salaam Julai 29 Julai 2021 ambapo alisema takwimu zinaonyesha kwamba zile fedha ambazo zinazoingia kwa ajili ya Sekta ya Azaki ni asilimia 1 pekee yake ndio zinaekwenda kwa CSOs, NGOs ambazo zimeanzishwa na Watanzania.

Mbunge Lugangira alisema kwa sababu takwimu zinaonyesha asilimia 99 ya fedha zinazotoka nje zinapita kupitia mashirika ambazo sio ya kiserikali lakini ni ya Kimataifa 
 
Alisema  ili miradi iwe endelevu lazima NGOs/CSOs za ndani ziweze kushiriki katika utekelezaji wa miradi hiyo na ndio maana mara nyingi wanaona kuna miradi fulani ukishaasha ufadhili na mfadhili akishaondoka mradi unakuwa hauendelei.

Alisema pia mara nyingi Sekta ya Azaki wanahesabiwa kama sehemu ya Sekta Binafsi lakini Sekta Binafsi ni tofauti zaidi kwa sababu wale ni wafanyabiashara zaidi na wanapokwenda kuongea mwakilisha Sekta Binafasi hawezi kuwakilisha Sekta ya Azaki.

“Nimejaribu kutoa changamoto kama wadau mnatambulika kama sekta inayosimama inachangia kwenye maendeleo ili kufanya hivyo lazima waonyeshe mchango wao dhahiri ni upi ili waweze kutambulika”Alisema

Hivyo alisema ni matarajio yake itapoandaliwa wiki ya Azaki mwezi Octoba mwaka huu basi watapata majawabu kwenye eneo hilo na watafanya mikakati madhubiti ya kutoka asilimia 1 na iongezeke



Share:

TVMC YATOA ELIMU UKATILI WA KIJINSIA, LISHE MAONESHO YA BIASHARA NA TEKNOLOJIA YA MADINI SHINYANGA


Mratibu wa Miradi wa Shirika lisilo Kiserikali la The Voice of Marginalized Community (TVMC) la Mjini Shinyanga, Mary Mahanya (kulia) akizungumza katika banda la TVMC kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga leo Jumamosi Julai 31,2021.

Shirika la TVMC limeshiriki Maonesho hayo  kwa kuelimisha wananchi kuhusu kupinga ukatili wa kijinsia kwa wanawake na watoto, kutoa elimu ya masuala ya Lishe zikiwemo njia sahihi za kunyonyesha mtoto na kutoa msaada wa Kisheria  ili kusaidia kutatua migogoro mbalimbali kama vile ya ardhi na ndoa.

Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga yanayoongozwa na kauli mbiu “Uwekezaji wa Madini na Viwanda Shinyanga kwa Uchumi Endelevu” yameanza tarehe 23 Julai, yanatarajiwa kuhitimishwa tarehe 1 Agosti, 2021.

Mratibu wa Miradi wa Shirika lisilo Kiserikali la The Voice of Marginalized Community (TVMC) la Mjini Shinyanga, Mary Mahanya (kulia) akielezea huduma zinazotolewa na TVMC kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
 Afisa Utawala wa Shirika lisilo Kiserikali la The Voice of Marginalized Community (TVMC) la Mjini Shinyanga, Chiku Hamis akionesha kipeperushi kinachoelezea masuala ya Lishe kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.
 Afisa Utawala wa Shirika lisilo Kiserikali la The Voice of Marginalized Community (TVMC) la Mjini Shinyanga, Chiku Hamis akionesha kipeperushi kinachoelezea masuala ya Lishe kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga.

Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Share:

BROTHERHOOD SURVEY SERVICES YATUMIA MAONESHO SHINYANGA KUTANGAZA MCHONGO WA VIWANJA IBADAKULI

Afisa Masoko wa Kampuni ya Brotherhood Survey Services Company Limited, Victoria Mahindi akionesha ramani mahali ulipo mradi wao wa uuzaji wa Viwanja ‘Diamond City Project’ katika kata ya Ibadakuli Manispaa ya Shinyanga.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kampuni ya Brotherhood Survey Services Company Limited ya Mjini Shinyanga imeshiriki Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga kwa kuonesha huduma wanazotoa pamoja na kuwatangazia wananchi kuhusu mradi wao wa uuzaji wa Viwanja ‘Diamond City Project’ unaopatikana katika kata ya Ibadakuli Manispaa ya Shinyanga.

Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga yanayoongozwa na kauli mbiu “Uwekezaji wa Madini na Viwanda Shinyanga kwa Uchumi Endelevu” yameanza tarehe 23 Julai, yanatarajiwa kuhitimishwa tarehe 1 Agosti, 2021 katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.

Akizungumza leo Jumamosi Julai 31,2021 Afisa Masoko wa Kampuni ya Brotherhood Survey Services Company Limited, Victoria Mahindi amesema Kampuni yao inajihusisha na Uendelezaji wa ardhi, ushauri kuhusu masuala ya ardhi, usimamizi wa mali yakiwemo majengo, magari na viwanja, ukusanyaji wa ushuru na mikopo, udalali, uchoraji wa ramani za majengo, uuzaji wa vifaa vya ujenzi pamoja na kufanya tafiti mbalimbali.

Amesema Kampuni ya Brotherhood Survey Services Company Ltd imeshiriki kwenye Maonesho hayo kwa ajili ya kuonesha huduma wanazozitoa.

“Kwenye maonesho haya pia tumekuja kuwatangazia wananchi kuhusu mradi wetu wa uuzaji Viwanja unaojulikana kwa jina la Diamond City Project unaopatikana katika kata ya Ibadakuli Manispaa ya Shinyanga",amesema.

“Mradi huu wa viwanja upo Kilomita 8 kutoka Mjini Shinyanga na mita 500 kutoka barabara kuu ya Shinyanga - Mwanza. Katika mradi huu tunauza viwanja kwa bei nafuu kuanzia shilingi 540,000/= na unaweza kulipa kidogo kidogo hadi miezi sita. Viwanja vimepimwa na pia Kampuni yetu itafuatilia upatikanaji wa Hati Miliki ya Kiwanja chako kama utahitaji”,ameongeza Victoria.

Eneo la mradi huo wa uuzaji viwanja lipo jirani na mahali patakapojengwa Stendi Kuu ya Mabasi Mkoa wa Shinyanga, Ibadakuli eneo ambalo ni zuri kwa uwekezaji wa biashara na viwanda vidogo vidogo lakini rafiki kwa makazi na tayari kuna huduma ya umeme ,maji na zahanati ya Ibadakuli.

Ofisi za Kampuni ya Brotherhood Survey Services Company Limited zipo Mjini Shinyanga jengo la NSSF Mafao ghorofa ya Pili Wasiliana nao zaidi kwa simu namba 0746633364 ,0768992606, 0754 763263,0757462260 au Email
 info@brotherhoodsurveyservices.com
Afisa Masoko wa Kampuni ya Brotherhood Survey Services Company Limited, Victoria Mahindi akionesha ramani mahali ulipo mradi wao wa uuzaji wa Viwanja ‘Diamond City Project’ katika kata ya Ibadakuli Manispaa ya Shinyanga leo Julai 31,2021 kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga yanayofanyika katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Afisa Masoko wa Kampuni ya Brotherhood Survey Services Company Limited, Victoria Mahindi akionesha ramani  ya nyumba kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga yanayofanyika katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.
Afisa Masoko wa Kampuni ya Brotherhood Survey Services Company Limited, Victoria Mahindi akielezea kuhusu huduma zinazotolewa na Kampuni yao kwenye Maonesho ya Pili ya Biashara na Teknolojia ya Madini Mkoa wa Shinyanga yanayofanyika katika uwanja wa Zainab Telack kijiji cha Butulwa kata ya Old Shinyanga Manispaa ya Shinyanga.
Afisa Masoko wa Kampuni ya Brotherhood Survey Services Company Limited, Victoria Mahindi akiwakaribisha wananchi kuchangamkia fursa ya viwanja wanavyouza kupitia mradi wao wa uuzaji wa Viwanja ‘Diamond City Project’ unaopatikana katika kata ya Ibadakuli Manispaa ya Shinyanga.

Ofisi za Kampuni ya Brotherhood Survey Services Company Limited zipo Mjini Shinyanga jengo la NSSF Mafao ghorofa ya Pili Wasiliana nao zaidi kwa simu namba 0746633364 ,07689926060754 763263,0757462260 au Email
 info@brotherhoodsurveyservices.com


Share:

Maelekezo 10 ya Waziri Ummy kwa Mamlaka za Serikali za Mitaa

Nteghenjwa Hosseah, OR-TAMISEMI
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mhe. Ummy Mwalimu ametoa maelekezo 10 kwa Halmashauri za Majiji, Manispaa, Miji na Wilaya ya kuimarisha ukusanyaji mapato na upelekaji wa fedha za maendeleo kwenye  miradi inayogusa wananchi.

Akizungumza leo na waandishi wa habari jijini Dodoma kuhusu matumizi na mapato ya ndani ya Halmashuari hizo kwa mwaka 2020/21, Mhe.Waziri Ummy amezitaka Halmashauri ziendelee kubuni vyanzo vipya vya mapato ya ndani ambavyo haviitakuwa kero kwa wananchi ili kuongeza uwezo wa utoaji huduma kwa wananchi hususani huduma bora za Afya, Elimu na Miudombinu ya Barabara.

Pia, amesema Halmashauri ziimarishe usimamizi wa ukusanyaji wa mapato ya ndani ikiwa ni pamoja na matumizi ya mifumo ya kielektroniki ya ukusanyaji wa mapato ili kuondoa mianya ya uvujaji wa mapato na kusisitiza kila chanzo kikusanywe kwa kutumia POS machine ili kudhibiti upotevu huo.

BONYEZA HAPA KUJUA VITUO VITAKAVYOTOA CHANJO YA CORONA TANZANIA

“Halmashauri zihakikishe kuwa fedha za makusanyo ya ndani zinazokusanywa zinapelekwa benki ndani ya masaa 24 baada ya kuzikusanya. Ni marufuku na ni kosa la kisheria kwa Halmashauri kutumia fedha zilizokusanywa kabla ya kuzipeleka benki (fedha mbichi) kwa sababu yoyote ile,”amesema.

Amesisitiza Halmashauri zihakikishe zinapeleka na kutumia angalau asilimia 40 ya mapato yaliyokusanywa (kwa Halmashauri zinazokusanya chini ya Shilingi bilioni 5 kwa mwaka) na asilimia 60 (kwa Halmashauri zinazokusanya zaidi ya Shilingi bilioni 5 kwa mwaka) kwenye miradi ya maendeleo ili kutatua kero za wananchi hususan kuboresha huduma za Afya, Elimu na miundombinu ya barabara. Fedha hizi zitumike kwenye miradi yenye tija na inayogusa moja kwa moja wananchi na sio kugharamia semina, vikao, safari na mambo mengine yasiyogusa wanananchi moja kwa moja.

 Aidha, amesema kwa Halmashauri zenye makusanyo kuanzia bilioni 5 na zaidi kwa mwaka, zihakikishe zinatumia angalau asilimia 10 ya sehemu ya fedha zao za maendeleo kwenye uboreshaji wa Miundombinu ya barabara kupitia TARURA.

“Ninazitaka Halmashauri kuhakikisha fedha za mapato ya ndani zinatumika kutekeleza na kukamilisha miradi kwa asilimia 100 ili wananchi waweze kuona faida za mapato ya ndani na hatimaye kuongeza mwamko wa ulipaji wa kodi na ushuru,”amesema.

Mhe. Waziri Ummy amesema Halmashauri zihakikishe zinapeleka asilimia 10 ya fedha za mikopo ya Vikundi vya Wanawake, Vijana na Watu wenye Ulemavu kwenye shughuli zenye tija kama ilivyoelekezwa na Mh.Rais Samia Suluhu Hassan na katika hilo Halmashauri zihakikishe angalau asilimia 60 ya fedha za mikopo zinatolewa kwenye Vikundi hivyo.

“Halmashauri zihakikishe zinakamilisha miradi ambayo haijakamilika (viporo) kabla ya kuanzisha miradi mipya, Halmashauri zitumie sehemu ya fedha za matumizi ya kawaida kutoka kwenye mapato ya ndani ili kulipa madeni na hatimaye kuondoa malimbikizo ya madeni yasiyokuwa na msingi,”amesema.

Amehimiza Mabaraza ya Madiwani yahakikishe yanasimamia ipasavyo matumizi ya fedha za Halmashauri ili kupata thamani halisi ya fedha zinazotumika na kwamba yana wajibu wa kuhakisha fedha zinatumika kwenye miradi ya maendeleo yenye tija na manufaa ya moja kwa moja kwa wananchi.

 Kuhusu maelekezo kwa Mikoa, Mhe.Waziri huyo amesema Sekretarieti za Mikoa zifanye ufuatiliaji wa ukusanyaji wa mapato ya ndani na matumizi ya mapato hayo kwa Halmashauri zilizo ndani ya Mikoa yenu mara kwa mara ili kujiridhisha na ukusanyaji wa mapato ya ndani ya Halmashauri pamoja na matumizi yake na kuwasilisha taarifa za utekelezaji Ofisi ya Rais – TAMISEMI kila robo mwaka kabla ya tarehe 20 baad ya robo husika kuisha.

“Sekretarieti za Mikoa zifanye ufuatiliaji wa fedha za miradi inayotekelezwa kwa mapato ya ndani iliyopo kwenye Halmashauri zao ili kujiridhisha na ubora wa Miradi inayotekelezwa. Aidha Sekretariat zifanye ufuatiliaji wa kina wa miradi inayotekelezwa kwa fedha kutoka Serikali Kuu na wadau wengine,”amesema.



Share:

AFARIKI AKILALA NA JIKO LA MKAA KIBANDANI KUWAHI WATEJA




Na Amiri Kilagalila,Njombe
Editha Mangita (40) mkazi wa mtaa wa Matema kata ya Maguvani mjini Makambako amefariki dunia baada ya kujifungia na jiko la mkaa katika kibanda chake cha biashara.

Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi mkoa wa Njombe Hamisi Issa amesema tukio hilo limetokea Julai 28,2021 ambapo marehemu Editha aliamua kubaki na kulala katika kibanda chake cha biashara ili kuwahi wateja wake wa asubuhi.

Aidha Kamanda Issa amewataka wananchi wa mkoa wa Njombe kuacha kulala na majiko ya mkaa ndani huku akitoa wito kwa wataalamu wa afya kuendelea kutoa elimu kuhusu madhara hayo Ili jamii.

Hivi karibuni mjini Njombe kulitokea kifo cha watu wawili wapenzi baada ya kulala na jiko la mkaa ili kupunguza baridi katika chumba chao.

Kamanda Issa ametaja tukio lingine la mwanamke mmoja Imelda Mgeni ametelekeza mtoto mwenye umri wa miezi mitatu kwa mume wake naye kwenda kusikojulikana.

Share:

TAZAMA HAPA ORODHA YA VITUO VYA KUTOLEA CHANJO YA CORONA KATIKA MIKOA YOTE TANZANIA

Katibu Mkuu Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia na Watoto, Prof.Abel Makubi akionesha chanjo aina ya Jonson Jonson kwa Wana habari.
**
Baada ya taasisi tano zilizo chini ya wizara ya afya kufanya uchunguzi na kujiridhisha kuwa chanjo za Johnson & Johnson ni salama kutumika kwa Watanzania, zimeanza kusafirishwa  katika mikoa 26 kwa ajili ya makundi matatu yaliyopewa kipaumbele wakiwemo watoa huduma za afya, wazee na wenye magonjwa sugu.


Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JULAI 31,2021











Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger