Friday 2 July 2021

Picha : SHEMAHONGE AFUNGUA SHINA LA WAKEREKETWA, OFISI YA CCM TAWI LA NEGEZI - MWAWAZA.... ASEMA VIJANA CCM HAWANA MPANGO NA KATIBA MPYA


Kushoto ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Shinyanga Baraka Shemahonge akifungua Shina la Wakereketwa wa CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Shinyanga Baraka Shemahonge amefungua Rasmi Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga huku akiweka wazi kuwa Vijana wa CCM mkoa wa Shinyanga hawana mchakato wala mawazo ya Katiba Mpya zaidi ya kujenga chama na nchi.

Akizungumza leo Ijumaa Julai 2,2021 wakati wa ufunguzi wa shina la wakereketwa na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza iliyopo katika Manispaa ya Shinyanga, Shemahonge amesema Chama cha Mapinduzi (CCM) hakina ajenda ya katiba mpya sasa.

“Sisi Chama cha Mapinduzi hatuna ajenda ya Katiba Mpya kwa sasa,huo ndiyo msimamo na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan amesema hivi sasa anajenga nchi, anajenga uchumi. Sasa vile vyama ambavyo havina malengo wala ajenda ndiyo vinalazimisha katiba mpya.

“Hivi sasa hatuna mchakato wala mawazo na Katiba Mpya, wazo letu ni kujenga chama na nchi.Sisi vijana wa CCM mkoa wa Shinyanga tunaungana na Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan kwamba mchakato wa Katiba kwa sasa haupo, sasa hivi tunajenga chama, tunajenga nchi iweze kuwa na uchumi tukiangalia uchumi wa nchi yetu umeyumba kutokana na ugonjwa wa Corona ambao umeikumba dunia nzima”,amesema Shemahonge.

Baraka amewataka vijana wa CCM kumuunga mkono Rais Samia Suluhu akisema katika kipindi cha siku 100 amefanya mambo makubwa akionesha kwa vitendo kuwa wanawake wanaweza kuongoza nchi.

“CCM tembeeni kifua mbele kuwa wanawake wanaweza. Rais wetu Mpendwa Mhe. Samia Suluhu amefanya mambo makubwa kwa kipindi kifupi. Tuendelee kumuunga mkono kwa kufanya kazi kwa bidii, kuwa waadilifu, waaminifu, kumlinda na kulinda amani ya nchi huku tukieleza na kuyasemea mambo mema anayofanya katika kujenga nchi yetu”,amesema Shemahonge.

Mwenyekiti huyo wa UVCCM mkoa wa Shinyanga ametumia fursa hiyo kumpongeza kada wa CCM, Edwin Masha Charles kwa kutoa jengo la nyumba yake litumike kama ofisi za Chama Cha Mapinduzi tawi la Negezi kata ya Mwawaza kwa ajili ya shughuli za chama hicho.

“Nimefarijika kuona kijana mwenzetu Edwin Masha Charles kwa kutoa mali yake itumike kwa shughuli za chama. Tunamshukuru kwa kujitolea kukijenga chama. Hii ni kazi ya chama kwani chama kinajengwa na vijana.Najua kuna mambo mengi yataibuka kwamba kwanini amefanya hivi labda anataka uongozi. Nikusihi ndugu ya Edwin usikatishwe tama na maneno ya watu, umefanya kazi ya kizalendo kujenga chama”,amesem Shemahonge.

Naye Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Shinyanga Mjini, Dotto Joshua mbali na kumpongeza kada wa CCM Edwin Charles kutoa jengo lake litumike kama ofisi ya CCM pia amewaomba vijana kuendelea kujenga chama na kukipambania huku akiwasihi vijana kuendeleza umoja na mshikamano walionao.

Kwa upande wake, Katibu wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini, Agnes Bashemu amesema ofisi hiyo ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza itatumiwa na chama na Jumuiya zote za CCM wakati CCM inaendelea na mchakato wa kujenga ofisi zake katika eneo hilo.

Bashemu ametumia fursa hiyo kuwakumbusha viongozi wa serikali za mitaa pamoja na Madiwani kufanya mikutano ya hadhara na kuwaeleza wananchi kuhusu miradi na kazi wanazofanya katika kuwaletea maendeleo wananchi huku akiwataka vijana kujitokeza kushiriki shughuli za maendeleo ikiwemo ujenzi wa vyoo na vyumba vya madarasa shuleni.

Kwa upande wake, Edwin Masha Charles amekishukuru Chama Cha Mapinduzi kwa kukubali ombi lake la kutoa chumba cha nyumba yake kitumike kama ofisi ya CCM huku akibainisha nia yake ilikuwa ni jengo hilo litumike kwa shughuli za UVCCM kwani tamanio lake ni kuona kila tawi la CCM lina ofisi kwa ajili ya vijana.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Kushoto ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Shinyanga Baraka Shemahonge akifungua Shina la Wakereketwa wa CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga leo Ijumaa Julai 2,2021. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kushoto ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Shinyanga Baraka Shemahonge akifurahia baada ya kufungua Shina la Wakereketwa wa CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga leo Ijumaa Julai 2,2021.
Shina la Wakereketwa wa CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga
 Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Shinyanga Baraka Shemahonge akipandisha Bendera ya CCM baada ya kufungua Shina la Wakereketwa wa CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga leo Ijumaa Julai 2,2021.
 Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Shinyanga Baraka Shemahonge akipandisha Bendera ya CCM baada ya kufungua Shina la Wakereketwa wa CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga leo Ijumaa Julai 2,2021.
 Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Shinyanga Baraka Shemahonge akipandisha Bendera ya CCM baada ya kufungua Shina la Wakereketwa wa CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga leo Ijumaa Julai 2,2021.
 Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Shinyanga Baraka Shemahonge akikata utepe wakati akifungua ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga leo Ijumaa Julai 2,2021.
 Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Shinyanga Baraka Shemahonge akipiga makofi baada ya kukata utepe akifungua ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
 Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Shinyanga Baraka Shemahongenaa viongozi mbalimbali wa CCM wakiwa ndani ya ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Shinyanga Baraka Shemahongenaa viongozi mbalimbali wa CCM wakiwa nje ya ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Shinyanga Baraka Shemahonge, viongozi mbalimbali wa CCM na wananchi wakipiga picha ya kumbukumbu kwenye shin la wakereketwa wa CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Shinyanga Baraka Shemahonge, viongozi mbalimbali wa CCM na wananchi wakipiga picha ya kumbukumbu kwenye shin la wakereketwa wa CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga 
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Shinyanga Baraka Shemahonge akizungumza wakati wa ufunguzi wa Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Shinyanga Baraka Shemahonge akizungumza wakati wa ufunguzi wa Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Shinyanga Baraka Shemahonge akizungumza wakati wa ufunguzi wa Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Mkoa wa Shinyanga Baraka Shemahonge akizungumza wakati wa ufunguzi wa Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Katibu wa UVCCM, Muhsin Zikatim akizungumza wakati wa ufunguzi wa Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Mwenyekiti wa UVCCM wilaya ya Shinyanga Mjini, Dotto Joshua akizungumza wakati wa ufunguzi wa Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga
Katibu wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini, Agnes Bashemu akizungumza wakati wa ufunguzi wa Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga
Kada wa CCM Edwin Masha Charles aliyetoa jengo la nyumba yake litumike kama ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza akizungumza wakati wa ufunguzi wa Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Kada wa CCM Edwin Masha Charles aliyetoa jengo la nyumba yake litumike kama ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza akizungumza wakati wa ufunguzi wa Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
 Katibu wa UVCCM wilaya ya Shinyanga Mjini, Raphael Nyandi akizungumza wakati wa ufunguzi wa Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Katibu wa CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza, Suzana Dotto akisoma risala wakati wa ufunguzi wa Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
 Katibu wa Hamasa na Chipukizi CCM mkoa wa Shinyanga , Hashim Issa akizungumza wakati wa ufunguzi wa Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
 Diwani wa kata ya Mwawaza, Juma Nkwabi akizungumza wakati wa ufunguzi wa Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye ufunguzi wa Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Wananchi na wanaCCM wakiwa kwenye ufunguzi wa Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Mwenyekiti wa CCM Kata ya Mwawaza, Dotto Mamboleo akizungumza kwenye ufunguzi wa Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Viongozi mbalimbali wa CCM wakiwa kwenye ufunguzi wa Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Viongozi mbalimbali wakifurahia jambo kwenye ufunguzi wa Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Shinyanga, Baraka Shemahonge (katikati) akiandamana na vijana wa CCM kuelekea kwenye ufunguzi wa Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Shinyanga, Baraka Shemahonge (katikati) akicheza muziki na vijana wa CCM kuelekea kwenye ufunguzi wa Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.
Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Shinyanga, Baraka Shemahonge (katikati) akicheza muziki na vijana wa CCM kuelekea kwenye ufunguzi wa Shina la Wakereketwa wa CCM na ofisi ya CCM tawi la Negezi kata ya Mwawaza katika Manispaa ya Shinyanga.

Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


Share:

SERIKALI KUANZISHA SHULE ZA MICHEZO UMISSETA 2021

 


Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa akihutubia leo Julai 2,2021 kwenye ufungaji wa UMISSETA mjini mtwara.

Waziri bashungwa akiwa na Katibu Mkuu wake Dkt. Hassan Abbasi, viongozi na wachezaji wa timu za mpira wa miguu kwenye fainali baina ya timu ya Pemba na Mtwara ambapo Pemba wameibuka washindi baada ya kuiadhibu mtwara mabao 2-0.



Katibu Mkuu wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi akitoa maneno ya kumkaribisha Bashungwa leo Julai 2,2021 ili atoe hotuba ya ufungaji wa UMISSETA 2021



Msanii Sholo Mwamba akitumbuiza leo Julai 2,2021 kwenye sherehe ya ufungaji wa UMISSETA 2021 katika uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.



Msanii Nandy akitumbuiza leo Julai 2,2021 kwenye sherehe ya ufungaji wa UMISSETA 2021 katika uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara.



Msanii Mr Bluu akitumbuiza leo Julai 2,2021 kwenye sherehe ya ufungaji wa UMISSETA 2021 katika uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara



Na John Mapepele, Mtwara

Serikali imesema ipo kwenye hatua za mwisho za kuanzisha shule maalum za michezo, za msingi na sekondari, katika mikoa yote nchini lengo likiwa ni kuwa na shule na vituo maalum vya kuendelezea vipaji vya michezo (sports academies).

Akizungumza kwenye Sherehe za kufunga mashindano ya Michezo na Taaluma kwa Shule za Sekondari(UMISSETA) mjini Mtwara leo Julai 2,2021 Waziri wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa amese Shule hizi zitakuwa zinalea na kuendeleza vipaji vya michezo mbalimbali, na Serikali itakuwa inasimamia kwa ukaribu, kuhakiksiha kuwa vituo vya michezo vya shule za msingi na sekondari, vinapatiwa mahitaji muhimu yatakayo saidia katika kuendeleza vipaji hivyo.

Amesema Serikali kupitia Chuo cha Maendeleo ya Michezo – Malya, inaanzisha kituo maalum cha michezo cha kuendeleza vipaji (Centre of Sports Excellency), vitakavyokuwa vinapatikana kutokana na mashindano haya, na maeneo mengine mbalimbali nchini.

« Chuo cha maendeleo ya michezo Malya kimeanzisha mafunzo ya astashahada, ili kupanua wigo wa wanufaika wake, pia kimefungua kituo cha mafunzo Dar es salaam na Ruvuma, ili kusogeza huduma kwa wananchi wengi zaidi. Ni matumaini yetu kuwa, kupitia Chuo hiki, tutaweza kupunguza pengo la watalaam, na walimu wa Michezo ambalo tunalo hivi sasa » amesisitiza Mhe. Bashungwa

Katika mashindano ya mwaka huu ya UMISSETA mkoa wa Dar es Salaam umeibuka mshindi wa kwanza wa jumla katika michezo yote.

Pia amememshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Hassan Suluhu, kwa maelekezo yake ya kuondoa kodi ya VAT, katika kununua na kuingiza nyasi bandia nchini, ili tuweze kujenga na kukarabati miundombinu yetu ya michezo.

« Wizara yangu imejipanga kuanza kuhamasisha taasisi na wadau mbalimbali, kuchangamikia fursa iliotolewa kwa kuboresha miundombinu ya viwanja vyao. Nimatumaini yetu kuwa, kwa hatua hii tunakwenda kuimarisha, na kuboresha mioundombinu ya michezo nchini » amefafanua Mhe. Bashungwa.

Ameongeza kuwa, Mhe. Rais kupitia bunge la bajeti lililoisha mwezi Juni, 2021, ameruhusu asilimia 5 kutoka kwenye michezo ya kubashiri (sport betting), kuingia kwenye mfuko wa maendeleo ya michezo, unaosimamiwa na Baraza la Michezo Tanzania (BMT), ili fedha hizo ziweze kutumika kwa ajili ya maendeleo ya Michezo.

Amesema kutunishwa kwa mfuko huo kutatoa fursa ya kuendeleza michezo mbalimbali nchini, kwa ngazi zote, ikiwemo mashindano ya UMITASHUMTA na UMISETA.

Amemhakikishia Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, Majaliwa utekelezaji wa maagizo mbalimbali, ya kuhakikisha Wizara yake inaweka mikakati mbalimbali ya kuendeleza michezo nchini ambayo aliyatoa wakati wa ufunguzi wa UMITASHUMTA hivi karibuni ambapo amesema baadhi ya maelekezo tayari yameshafanyiwa kazi.

Baadhi ya maelekezo hayo ni pamoja na, kufanya tahimini ya Vyuo vya Elimu, vilivyokuwa vinafundisha michezo na sasa havifundishi; na uanzishwaji wa shule maalum za michezo mikoani.

. « Kupitia ushirikiano na umoja wa Wizara zetu maagizo haya na mengine tutayashughulikia kwa kasi na weledi, ili kuhakikisha sekta ya michezo inakuwa nchini »

Aidha amesema Serikali kwa, kupitia Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo itazindua mpango mkakati wa Taifa wa Maendeleo ya Michezo mwezi Julai, 2021. Mpango mkakati huo umetoa muelekeo wa jinsi ya kuendesha michezo, kwa kuzingatia maelekezo mbalimbali yaliotolewa kwenye Ilani ya Uchaguzi ya mwaka 2020-2025, ambapo pamoja na mambo mengine, mpango huo unaweka mkakati wa jinsi ya kuingia kwenye michezo ya kulipwa, ili kuwapatia vijana ajira kwa kutumia vipaji vyao, na kujipatia vipato wao binafsi lakini pia kuongeza pato la Taifa kupitia sekta ya michezo. Kama Waziri mwenye dhamana, nitahakikisha kwamba tunafikia malengo hayo na kazi inaendelea.

Pia ametumia muda huo kuwashukuru wasanii wa kizazi kipya waliokuwa wakitoa burudani katika kipindi chote cha UMITASHUMTA na UMISSETA ambao wameleta hamasa kubwa na burudani kwa wanamichezo na wadau mbalimbali walioshiriki mashindano ya mwaka huu.

Miongoni mwa wasani wa kizazi kipya waliotoa burudani kwenye ufungaji wa UMISSETA leo Julai 2,2021 na kuteka mji wa mtwara na viunga vyake ni pamoja na Maarifa, Kala Jermiah, G-Nako, Mr Blue, Shishi, Nandy na Sholo Mwamba.

“Asanteni sana kwa ushirikiano wenu mkubwa, pamoja na burudani mlioionesha, na mtakayo endelea kuifanya hapa leo, ili kutoa burudani ya kuhitimisha michezo hii. Kwa hakika wana Mtwara wamefurahi na kuburudika sana. Michezo sasa ni ajira, hivyo kwa kuendeleza michezo hii, ni kuaandaa eneo muhimu litakalowapatia vijana wetu ajira kupitia vipaji walivyonavyo” amesisitiza Bashungwa

Naye Katibu Mkuu wa Habari, Utamaduni Sanaa na Michezo, Dkt. Hassan Abbasi amesema Wizara ya habari itaendelea kusimamia sera na kuweka mikakati madhubuti ili kuinua maendeleo ya wasanii nchini.
Share:

WAZIRI AWESO –WAKANDARASI WANAOSUASUA KWENYE UTEKELEZAJI WA MIRADI TUTAENDELEA KUWACHUKULIA HATUA

WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso akizungumza wakati wa kikao hicho kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mngandilwa
WAZIRI wa Maji Jumaa Aweso akizungumza wakati wa kikao hicho kushoto ni Mkuu wa wilaya ya Tanga Hashim Mgandilwa

MKUU wa wilaya ya  Tanga Hashim Mgandilwa akizungumza wakati wa kikao hicho
Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Tanga Mhandisi Upendo Lugongo akizungumza jambo ewakati wa kikao hicho
Baadhi ya washiriki wakifiatikia kikao kazi cha watumishi wa sekta ya maji mkoani Tanga
Baadhi ya washiriki wakifiatikia kikao kazi cha watumishi wa sekta ya maji mkoani Tanga

 

NA OSCAR ASSENGA, TANGA

Waziri wa Maji Jumaa Aweso amesema kuwa hatashindwa kuendelea kuwachukulia hatua za kinidhamu ikiwemo kuwapokonya kazi wakandarasi wanaosuasua ikiwemo wanaokwamaisha utekelezaji wa miradi ya maji nchini

Kauli hiyo alilitoa wakati wa ufunguzi wa kikao kazi cha watumishi wa sekta ya maji mkoani Tanga ambapo alisema kuwa katika kutekeleza tayari ameshawafuta kazi jumla ya wakandarasi 118 pamoja na makampuni 69 yaliyokuwa yanaendesha miradi ya maji katika maeneo mbalimbali nchini.

Alisema kuwa lengo la Serikali ni kuhakikisha inampatia mwananchi huduma ya maji safi na salama karibu na maeneo yake bila ya kulazimika kutembea umbali mrefu lakini uwepo wa huduma ya uhakika.

"Uhandisi wa maji ni pamoja na kufuatilia miradi uliyopewa n a kujiridhisha kama huduma ipo, pale unapo sema Mradi umekamilika basi inamana unatoa maji kwa asilimia 100% na sio ujanja ujanja"Alisema Waziri Aweso.

Aliwataka wataalamu wabadili fikra zao juu ya utekelezaji wa miradi ya maji akitolea mfano miradi ya maji vijijini una sehemu tatu ya kwanza ni chanzo eneo la pili tanki la maji la tatu ni kituo cha usambazaji au kama kuna eneo lenye maji ya mserereko lazima kuwea na eneo la kitibu maji.

“Sasa unajenga chanzo, unajenga tenki la maji, unatandaza vituo vya maji halafu unaangiza pump miezi sita watu wanaona vituo vya maji lakini maji hayatoki unatengeneza malalamiko, manung’uniko na masononeko yalisiyo na ulazima “Alisema Waziri Aweso.

Alisema kumbe wakati unapojenga kwanini usiangize na pampu hata kabla maji hayajaingia kwenye tenki watu wayatumie lakini wanaweza kuyatumia wakati wa ujenzi wa tenki.

“Kwa hiyo hizo ndio fikra ambazo lazima zibadilike kwenye wizara ya maji umejenga intake ya maji agiza pampu ya maji ili twende sambamba watu waweze kuyatumia maji kuhakikisha dhamira ya Rais wetu Samia Suluhu inatimilika”Alisema







Share:

TAKUKURU Dodoma Yaokoa Mamilioni Ya Fedha


Na.Faustine Gimu Galafoni ,Dodoma.
Taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa nchini (TAKUKURU) imefanikiwa kuokoa na kudhibiti Jumla ya Tsh . Milioni mia mbili kumi na tano ,laki sita na sitini elfu (215,660,000)/= ambazo zingepotea kwa kuchepushwa ,kufujwa  ama kulipwa kwa watu wasiostahili.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Julai 2,2021 jijini Dodoma,Mkuu wa TAKUKURU mkoa wa Dodoma Sosthenes Kibwengo  ametaja mmoja wa uchepushaji ni gari la Ofisi ya katibu tawala  mkoa wa Dodoma ambalo baada ya kupata ajali  lilipelekwa kwenye gereji moja mkoani Dodoma  na kubainika vifaa 101 vyenye thamani ya Tsh. Milioni themanini na Saba ,laki Saba na themanini na tano elfu(87,785,000/=) vilichepushwa kutoka kwenye gari hilo.

"Tulishirikiana na wakala wa ufundi na Umeme (TEMESA) mkoa wa Dodoma ikabainika katika gari hilo kuna vifaa 101 vilichepushwa  tuliingilia kati vifaa hivyo vikarejeshwa"amesema .

Bw. Kibwengo amesema kitendo cha uchepushaji ni kosa chini ya Sheria ya kuzuia na kupamba na rushwa sura ya 329 marejeo ya mwaka 2019 ambapo amewataka wamiliki wa gereji  binafsi mkoani Dodoma  kuacha mara Moja tabia ya wizi wa vipuri vya magari ya umma .

Aidha, Kibwengo amesema miradi 20 ya Maendeleo yenye thamani ya shilingi  bilioni Moja ,milioni mia Saba sabini na tano  laki Saba  ,sitini na tatu elfu na mia Saba arobaini na sita (1,775,763,746/=) imekaguliwa katika sekta za elimu,Afya na ujenzi  na kubaini uchepuzi wa vifaa vya ujenzi  vyenye thamani ya Tsh. Milioni arobaini na Moja  laki nane na hamsini elfu( 41,850,000/=) huku miradi 19 ikibainika kutekelezwa kwa kiwango stahiki.

Katika hatua nyingine Bw.Kibwengo amesema TAKUKURU mkoa wa Dodoma imepokea taarifa 124 za malalamiko zikiwa ni taarika 52 pungufu ya zile zilizopokelewa kwa robo ya mwaka Jana ambapo taarifa zinazohusu rushwa ni 70  na 54 hazihusiani na rushwa .
Sekta zinazoongoza kwa kulalamikiwa kwa vitendo vya rushwa ni serikali za mitaa kwa asilimia 39,ardhi asilimia 19,sekta binafsi asilimia 7,elimu,Afya,na polisi kila Moja asilimia 6.

"Tumepokea taarifa 124 za malalamiko ambapo pia majalada 20 ya uchunguzi yalikamilika na mashauri mapya mawili yalifunguliwa Mahakamani na mashauri mawili yalitolewa maamuzi  ambapo jamhuri ilishinda Moja na kushindwa Moja.

Sanjari na hayo Mkuu huyo wa TAKUKURU amesema elimu imetolewa kwa makundi mbalimbali ya Kijamii wakiwemo Vijana  na kufanya semina 28 ,mikutano 7 ya hadhara ,vipindi 11 vya redio,maonesho mawili na ufunguzi wa klabu 41 za wapinga rushwa na kusikiliza kero za rushwa Kupitia mpango wa TAKUKURU inayotembea.

Pia katika robo ya Julai,hadi Septemba ,2021 Kibwengo amesema wataweka msisitizo katika uelimishaji wakati wa mbio maalum za mwenge na kwa makundi hasa ya Vijana huku akitoa msisitizo ushiriki wa kila mwananchi katika mapambano dhidi ya rushwa.





Share:

Kesi Ya Lengai Ole Sabaya Yaahirishwa Hadi July 16


Kesi ya unyang’anyi kwa kutumia silaha inayomkabili aliyekuwa mkuu wa wilaya ya Hai Lengai ole Sabaya pamoja na wenzake wawili,imeahirishwa mara baada ya shahid wa upande wa jamhuri kupata dharura.

Wakili wa serikali kwenye kesi hiyo Trasila Gervas ameiambia mahakama mbele ya hakimu wa mahakama ya hakimu mkazi Salome Mshasha kuwa shahidi waliyempanga ameshindwa kufika mahakamani hapo nakuahidi mashahidi kuwepo mahakamani july 16,2021


Share:

MKURUNGEZI YONO AFAGILIA UONGOZI WA RAIS SAMIA NDANI YA SIKU 100... 'AMETUTOA GIZANI'

MKURUGENZI Mtendaji wa Kampuni ya Udalali ya Yono Auction Mart na Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake wa Chama chama Mapinduzi Mkoa wa Njombe (UWT) Scolastica Kevela amempongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa utendaji wake wa siku 100 madarakani ulionyesha mabadiriko makubwa kwa Tanzania.

Akizungumza Dar es Salaam Mama Kevela alisema kwa kipindi hicho cha siku 100, Rais Samia amefanya mambo makubwa ikiwemo kukutana na makundi mbalimbali ya wazee, wanawake, vijana na kurejesha mahusiano mengi ya kidiplomasia kiasi cha mataifa mengi kupongeza uongozi wake.

"Ameonyesha kweli nini maana halisi ya uongozi kwa kujali maslahi mapana ya wananchi wake na Taifa hili kwa ujumla huku akifungua fursa nyingi za uwekezaji kwa watu wote wenye nia ya kutaka kuja na kufanya uwekezaji wao nchini", alisema Mama Kevela

Alisema katika kipindi hicho Rais Samia amewatoa gizani watu wengi waliokuwa na changamoto za kimahakama ambapo kwa muda mrefu mashauri yao yalikuwa na changamoto mbalimbali.

Mbali na hilo Mwenyekiti huyo wa UWT alisema ndani ya uongozi huo wa siku 100 madarakani za Rais Samia Suluhu Hassan ameonyesha kuwa na imani yake kubwa kwa vijana kupitia uteuzi alioufanya hivi karibuni kwa wakuu wa Wilaya mbalimbali.

"Uteuzi wake umegusa makundi ya vijana kutoka maeneo mbalimbali jambo lilionyesha kuwa anawaamini katika utendaji wao wa kazi, hili limewafanya watu wengi kuzidi kumuunga mkono", aliongeza Kevela

Aidha alisema hatua ya Rais Samia Suluhu Hassan kuunda tume maalumu ya kufuatilia mwenendo wa ugonjwa wa Covid 19, imeonyesha wazi nia ya kuifanya Tanzania kuungana na mataifa mengine katika mapambano dhidi ya ugonjwa huo baada ya kipindi kirefu kuwa kama kisiwa kilichokuwa kimejitenga katika mapambano hayo.

Alisema kwa kipindi hicho cha siku 100 za uongozi wake, watanzania wengi wamejenga imani naye na kujawa na matumaini kuwa ataliwezesha taifa kupiga hatua kubwa kimaendeleo huku akiwataka watanzania kumuombea afya njema.
Share:

Waziri Mkuu Atoa Rai Kwa Watanzania Na Warundi


 WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amewataka wananchi wa Tanzania na Burundi wafanye kazi kwa kuzingatia weledi na uaminifu mkubwa huku wakijiepusha na vitendo vya rushwa.

“Mataifa yetu yako kwenye ujenzi wa uchumi ni lazima kwa kila mmoja wetu afanye kazi kwa bidii. Waliopo maofisini, mashambani na viwandani wote kwa pamoja tuchapeni kazi.”

Waziri Mkuu ameyasema hayo jana (Alhamisi, Julai Mosi, 2021) alipotembelea kiwanda cha kutengeneza mbolea cha FOMI kilichoko jijini Bujumbura nchini Burundi.

Waziri Mkuu jana alimuwakilisha Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 59 ya uhuru wa Burundi, baada ya hafla hiyo alitembelea kiwanda hicho.

“Kilichinivutia kuja hapa ni mabadiliko yanayofanywa na Rais wenu Mheshimiwa Evariste Ndayishimiye na leo nchi inaonekana kwenda mbio kwenye maendeleo hasa ukuaji wa uchumi.”

“…Wana-Burundi si rahisi nyinyi kuyaona mabadiliko mnayoyafikia sisi tuliopo nje ya nchi ya Burundi ndiyo tunawaona mnavyobadilika kimaendeleo, endeleeni kuchapa kazi,” awalisisitiza.

Waziri Mkuu alisema mahitaji ya mbolea Tanzania ni zaidi ya tani 700,000 na nchi inatumia fedha nyingi kuagiza kutoka nje hivyo amemkaribisha mwekezaji huyo kuja kuwekeza nchini.

Alitumia fursa hiyo kuwakaribisha Wana-Burundi waje wawekeze na kufanya biashara nchini kwa sababu kuna ardhi kubwa na nzuri, umeme wa uhakika na mazingira mazuri ya uwekezaji.

Waziri Mkuu ambaye aliambatana na Waziri wa Kilimo wa Burundi Deo Guide Rurema kiwandani hapo alisema Tanzania na Burundi si majirani ni ndugu wa baba na mama mmoja.

Alisema undugu huo uliasisiwa na viongozi wa kwanza wa mataifa hayo Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na Mwanamfalme, Louis Rwagasore. “Jukumu letu ni kuienzi tunu hii.”

(Mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU


Share:

TIGO MDHAMINI NI RASMI WA MAWASILIANO KATIKA MAONESHO YA 45 YA BIASHARA YA KIMATAIFA (SABA SABA) KWA MIAKA SITA SASA


KAMPUNI ya simu za mkononi ya Tigo, imedhamini rasmi Maonyesho ya 45 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (Sabasaba). 

Tigo imeweka rekodi ya kudhamini maonyesho hayo kwa mwaka wa sita ambapo wateja wa Tigo wataendelea kupata ofa maalum katika msimu huu wa maonyesho ya Saba Saba. Katika maonyesho hayo ya 45 ya biashara ya Kimataifa, mwaka huu yataendeshwa chini ya kauli mbiu ya 'Utengenezaji wa ajira na biashara endelevu'.

 Akizungumza Dar es Salaam jana, Meneja Mawasiliano wa Kampuni ya Tigo, Woinde Shisael, alisema kuwa Tigo imekuwa Mdhamini wa mawasiliano wa maonyesho hayo na kuweka rekodi ya mwaka wa sita mfululizo. 

Alisema mpango huo ni moja ya malengo ya Tigo ikiwemo kusaidia serikali ukiwa moja ya dhamira kukuza biashara na ukuaji wa viwanda vya ndani kwa ustawi wa uchumi wa nchi. 

Alisema Tigo pia imeshirikiana na watengenezaji wa vifaa vitano kutoa matangazo ya kipekee ya mtandao na simu mahiri kwa maelfu ya wateja wake ambao watahudhuria maonyesho ya biashara katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam. 

"Tunapoingia msimu mwingine wa kusisimua wa Sabasaba, tumeandaa matoleo ya kuvutia ya mtandao na simu mahiri kwa wateja wetu. Tumeshirikiana na Xiaomi, Infinix, Samsung, TECNO Mobile na Itel kwa ajili ya kuendelea kutoa huduma nzuri katika maonyesho haya.

 "Tunatarajia wafanyabiashara watatumia huduma zetu za Lipa Kwa Simu. Kwa kuongezea, wateja wa Tigo Pesa watapata habari juu ya App ya Tigo Pesa, huduma ya Kujitunza fedha na ofa zingine za kufurahisha" alisema Woinde.
Kwa upande wa TANTRADE, Kaimu Mkurugenzi wa Biashara, Twilumba Mlelwa, aliipongeza Tigo kwa udhamini huo. Twilumba alisema kuwa TANTRADE ina bahati kuwa na mshirika wa kuaminika katika sekta ya mawasiliano, na kwamba wanatarajia kuendelea kupata huduma nzuri katika kipindi chote cha maonyesho.

 "Kumekuwa na ongezeko kubwa la masoko, mapato na uwekezaji kwa sababu ya kuongezeka kwa matumizi ya mawasiliano ya simu katika," alisema.
Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JULAI 2,2021

















Share:

Thursday 1 July 2021

Wizara Ya Mawasiliano Yazindua Tovuti Na Mpango Mkakati Wa Utendaji Kazi Na Upimaji Wa Miaka Mitano


Na Mwandishi wetu, Dodoma
Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari imezindua Tovuti ya Wizara hiyo inayopatikana katika kikoa cha www.mawasiliano.go.tz  pamoja  Mpango Mkakati wa Wizara hiyo wa miaka mitano kuanzia mwaka wa fedha 2021/22 hadi 2025/26 ambao ni mwongozo wa utendaji kazi na upimaji wa malengo iliyojiwekea ya kuibadilisha jamii ya Tanzania kuwa yenye msingi wa maarifa ambayo yamewezeshwa kidijitali

Hafla ya uzinduzi huo imefanyika leo tarehe 1/07/2021 mjini Dodoma na kuhudhuriwa na
viongozi mbalimbali wa Serikali wakiwemo Manaibu Waziri, Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Miundombinu Mhe. Moshi Kakoso, wakuu wa taasisi zilizo chini ya Wizara na mjumbe  kutoka Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Uchukuzi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar

Akifungua hafla hiyo Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile amesema kuwa Mpango Mkakati huo umejikita katika nyaraka mbalimbali za kisera na zile za malengo ya maendeleo ya kitaifa na kimataifa pamoja na Ilani ya uchaguzi ya CCM ya mwaka 2021-2025 katika vipengele vinavyogusa masuala ya mawasiliano na teknolojia ya habari.

Alisema kuwa Wizara hiyo ina jukumu la kuhakikisha wananchi wanatumia fursa zinazoenda sambamba na maendeleo ya kidijitali kwa kuweka mazingira wezeshi ya mwananchi kupata huduma za kijamii na kiuchumi kwa njia ya mtandao mahali popote alipo

Aidha, amesema kuwa Wizara hiyo inakwenda kuandaa mpango wa uwekezaji katika uchumi wa kidijitali ambao utaelezea malengo na mikakati ya nchi katika kuipeleka nchi ya Tanzania katika  uchumi wa dijitali.

Katika hatua nyingine Mhe. Dkt. Ndugulile ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa kuiona Wizara hiyo ni nyenzo kuu ya uchumi na maendeleo ya nchi na kuiongezea bajeti ya maendeleo kutoka bilioni 15 hadi bilioni 246 zilizopitishwa kwa mwaka wa fedha 2021/22

Naye Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Mhandisi Kundo Mathew amesema kuwa Mpango Mkakati huo  unaenda kujibu mahitaji ya watanzania ambapo Wizara na taasisi zilizo chini yake zimejipanga vema kuhakikisha inatimiza malengo waliyojiwekea ya kuwa na jamii iliyowezeshwa kidijitali

Awali akitoa wasilisho la Mpango Mkakati huo, Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Zainab Chaula amezungumzia malengo ya mpango mkakati huo kuwa ni pamoja na kuboresha upatikanaji wa huduma za mawasiliano,Teknolojia ya Habari,  na Huduma za Posta, kuimarisha uwezo wa taasisi zake katika utoaji wa huduma, kuimarisha fursa za kidijitali na kuboresha usimamizi wa teknolojia ya habari, mawasiliano ya simu na huduma za posta nchini.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari




Share:

Wananchi Watakiwa Kupata Ramani Zinazotolewa Na Wizara Ya Ardhi

Na Munir Shemweta
Wakati Maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara yakiendelea katika viwanja vya Mwl. Nyerere Dar es Salaam wananchi wametakiwa kutembelea Banda la Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa ajili ya kujipatia Ramani za Tanzania na ile ya jiji la Dar es Salaam.

Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kupitia idara yake ya Upimaji na Ramani ndiyo yenye jukumu la kutoa Ramani ya Tanzania, mikoa pamoja na zile za wilaya kwa kuwa ndiyo yenye mamlaka ya kupima mipaka yote ikiwemo ya nchi kavu na majini.

Akizungumza katika maonesho ya Sabasaba tarehe 1 Julai 2021 mkoani Dar es Salaam Afisa Upimaji wa Wizara ya Ardhi Vicky Sonda alisema, wananchi wanaotembelea Banda la Wizara mbali na huduma nyingine wataweza kujipatia Ramani za Tanzania pamoja na zile za jiji la Dar es Salaam.

Alisema, Ramani za jiji la Dar es Salaam zinazopatikana kwenye Banda la Wizara katika Maonesho ya Sabasaba zitawasaidia wananchi hasa wageni kujua maeneo mbalimbali ya jiji kwa haraka bila kulazimika kuuliza.

"Ramani za jiji la Dar es Salaam zinazopatikana hapa zitaweza kumsaidia mwananchi kutambua eneo analoenda kwa uharaka bila kuuliza" alisema Vicky

Kwa mujibu wa Vicky, wananchi watakaotembelea Banda la Wizara pia watajua uhalali wa umiliki wa tanzania maeneo ya mipaka ya bahari kupitia ramani alizozieleza kuwa zinaonesha maeneo ya mipaka baina ya Tanzania na nchi nyingine.

Aidha, Afisa huyo Upimaji kutoka Wizara ya Ardhi Ofisi ya Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa wa Dar es Salaam alisema kuwa, fursa nyingine wanayoweza kunufaika wananchi wanaotembelea banda la wizara ya Ardhi ni kufahamu uwepo wa kisiwa ndani ya kisiwa cha Mafia  kinachoitwa Bwejuu.

"Wananchi watakaotembelea Banda letu watapata fursa ya kufahamu uwepo kisiwa ndani ya kisiwa cha Mafia kinachoitwa Bwejuu na kisiwa hicho ni maarufu sana kwa shughuli za utalii" alisema Vicky.

Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi inaendelea kutoa huduma mbalimbali katika maonesho ya 45 ya Kimataifa ya Biashara ikiwemo kutoa hati za papo hapo kwa wananchi waliorasimishiwa makazi yao kwenye mikoa ya Dar es Salaam na Pwani.


Share:

SUPER – NHESHA: Dawa Bora Ya Kutibu Tatizo La Kisukari


SUPER – NHESHA
Ni dawa ya kutibu tatizo la sukari au jina la kitaalamu (Diabetes Mellitus) ni kundi la magonjwa yanayohusiana na ufanyaji kazi wa mwili ambapo Mtu anakuwa na kiwango kikubwa cha sukari aina ya Glucose katika mwili kutokana na mwili wake kukosa uwezo wa kutengeneza Insulin ya kutosha au seli za mwili wake kutumia insulin iliyopo au pengine mwili kuwa na matatizo yote kwa pamoja na kupelekea mgonjwa wa sukari kupata haja ndogo mara kwa mara (Polyuria) uhisi kiu kila wakati (Polydipsia) Na (Polyphagia).


AINA YA KISUKARI
Kuna aina chache tofauti za ugonjwa wa kisukari (1) ni ugonjwa wa Auto hii aina mgonjwa wa Auto hushambulia mfumo wa kinga na kuharibu seli katika kongosho ambako insulin huzalishwa asilimia 10% ya watu wenye ungonjwa wa kisukari wanayo aina hii (Auto).


AINA YA PILI
Hii hutokea wakati mwili wako unakuwa sugu kwa insulin na sukari hujenga katika damu yako hii husababishwa na kuwa na sukari nyingi kwenye damu yako kuliko kawaida.


CHANZO CHA UGONJWA SUKARI
Viko vyanzo vingi mbalimbali vya sukari
1.     Shinikizo la damu (B.P)
2.     Viwango vya juu vya triglyceride (mafuta)
3.     Lishe yenye mafuta mengi na wanga
4.     Utumiaji mkubwa wa pombe kupita kiasi
5.     Ulaji wa vyakula vyenye sukari nyingi
6.     Mtindo wa maisha usiofaa kiafya
7.     Uzito na unene uliozidi
8.     Kutofanya mazoezi
9.     Umri
10.     Kurith


UNAJUAJE KUWA UNADALILI ZA KISUKARI
1.     Kusikia njaa mara kwa mara
2.     Kusikia kiu mara kwa mara
3.     Kupungua uzito
4.     Maono machafu
5.     Uchovu mara kwa mara
6.     Ukipata kidonda hakiponi
7.     Kushuka kwa kinga mwili


DALILI ZA KISUKARI KWA MWANAUME
Mbali na dalili za jumla za ugonjwa wa sukari wanaume wenye tatizo hilo wanakuwa na upungufu wa nguvu za kiume na kushindwa kufanya tendo la ndoa uume hushindwa kusimama misuri hulegea na kusinyaa, maumivu ya mgongo, kiuno, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kupata choo  kama cha mbuzi


DALILI ZA WANAWAKE
Wanawake wenye ugonjwa wa sukari wanaweza pia kuwa na dalili kama vile maambukizi kwa njia ya mkojo (U.T.I) maambukizi  ya gonzi kukakamaa


TIBA YA MAGONJWA YA SUKARI
Ugonjwa wa sukari unatibika bila kujali ni mda gani umepata hilo tatizo wengi wamekata tama na kuwa wabishi amini tatizo hili linatibika vizuri sana wengi wemepona.


Tumia dawa ya SUPER-NHESHAambayo ni dawa ya miti shamba yaani (asilia) ambayo humfanya mtu kupona na kuimalika kabisa.


Tutakuelekeza pia mfumo wa mtindo wa maisha utakao takiwa kutumia ili kutoluhusu tatizo hilo kurudi tena.


BABU MADUHU ANAPATIKANA MAGOMENI MOROCCO/KANISANI NJIA PANDA YA KWENDA SINZA  SIMU: 0652 102 152/0788 330 105/ 0755 684 297 NYOTE MNAKARIBISHWA PIA TUNATUMA MIKOANI WHATAPPS NO 0652 102 152 



Share:

Rais Samia Apokea Taarifa ya Ukaguzi wa BOT na Sensa



Share:

Dkt. Mwigulu Ateta Na Chama Cha Watoa Huduma Wa Simu Tanzania


Na Benny Mwaipaja, Dodoma
WAZIRI wa Fedha na Mipango Mheshimiwa Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), amekutana na kufanya mazungumzo na Chama cha Watoa Huduma wa Simu Tanzania (TAMNOA), na kuwaeleza kuwa kodi ya miamala ya simu na bando za mitandao inayotakiwa kuanza kutozwa na mitandao ya simu ni ya kizalendo inayolenga kila Mtanzania kuchangia mapato ya Serikali kwa ajili ya maendeleo ya nchi.

Dkt. Nchemba alisema kuwa Serikali imepanga kutekeleza miradi mingi ya maendeleo ya wananchi na inayohitaji fedha nyingi na kwamba jukumu la kukamilisha miradi hiyo ni la Watanzania wote wenye uchungu wa maendeleo.

“Fedha zitakazo patikana kwenye tozo hizo hazitatumika kulipa mishahara wala kugharamia matumizi mengine yoyote ya Serikali bali zitapelekwa moja kwa moja kutatua changamoto za afya, elimu, maji, miundombinu ya barabara, elimu na mingine mingi ikiwemo miradi ya kimkakati kama ujenzi wa reli ya kisasa na Bwawa la kuzalisha umeme la Julius Nyerere” alisema Dkt. Nchemba.

Dkt. Nchemba alisema kuwa jambo la kutia moyo ni kwamba Watanzania wengi wameunga mkono kutozwa kodi hiyo kwa kutambua umuhimu wa maendeleo yao ambayo kukamilika kwake kunahitaji mchango wao mkubwa.

“Kampuni za simu msichukulie makato haya kama kodi nyingine mnazowatoza wateja wenu bali Serikali iliamua kuweka makato haya kwenye miamala ya kuweka muda wa maongezi na kufanya miamala kwa njia ya simu ili kuwafanya Watanzania na watumiaji wengine wa simu kuchangia maendeleo ya nchi”alisisitiza Dkt. Nchemba.

Dkt. Nchemba alitoa muda wa siku 14 kuanzia tarehe 1 hadi 15 Julai, 2021, kwa watoa huduma wote wa Mitandao ya Simu kurekebisha mifumo yao na kuanza kutoza rasmi makato hayo ili Serikali ianze kukusanya fedha hizo ambazo amesema zitatumika kwa malengo yaliyokusudiwa ya kuwakwamua wananchi kutoka katika adha mbalimbali.

Kwa upande wao Chama cha Watoa huduma za mitandao ya simu, waliiomba Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango iwape muda wa kurekebisha mifumo yao itakayotumika kukusanya tozo hizo kwa kuwa zoezi hilo linahitaji muda wa kiufundi.

Akizungumza kwa niaba ya Chama hicho, Mkurugenzi wa Uhusiano wa Kampuni ya Simu ya Vodacom Bi. Roselynn Mworia, alisema kuwa chama chao kimeupokea mpango huo kwa mikono miwili na kuwataka wateja wao kuiunga mkono Serikali kwa kuendelea kutumia huduma za kupiga simu na kufanya miamala ya simu.

“Lengo la Serikali la kuamua kukusanya fedha za maendeleo kwa njia hiyo ni zuri kwani litaharakisha utekelezaji wa miradi ya huduma za kijamii, kwa kweli ni kodi ya kizalendo” alisema Bi. Mworia.

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, hivi karibuni, lilipitisha tozo ya kuanzia shilingi 10 hadi shilingi 10,000 kutozwa katika kila muamala wa kutuma au kupokea pesa na kiwango cha shilingi 10 hadi 200 kwa siku kila mteja anapoongeza salio la muda wa maongezi kwenye simu ambapo kwa pamoja, Serikali inatarajia kukusanya wastani wa shilingi trilioni1.7 kwa mwaka.
Mwisho



Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger