Wednesday 30 June 2021

Picha : TGNP YAENDESHA KONGAMANO LA TAFAKURI YA SIKU 100 ZA RAIS SAMIA ...'AMETUONESHA MWANGA, TUMPE USHIRIKIANO'

Share:

Waziri Mkuu Awataka Viongozi Waendelee Kusimamia Amani


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amefungua mafunzo ya Wakuu wa Mikoa na Makatibu Tawala wa mikoa na kuwataka viongozi hao waendelee kusimamia amani na utulivu kwenye mikoa yao ili watu waendelee kufanya shughuli zao bila wasiwasi wowote.

“Amani na utulivu ndiyo itatuwezesha kama nchi, tuendelee kuwavutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kuwekeza mitaji yao hapa nchini. Tunakumbushwa sisi viongozi wa Tanzania tuwe wazalendo na tuhakikishe tunaziendeleza rasilimali za nchi hii kwa faida ya Watanzania wote.”

Waziri Mkuu ametoa agizo hilo leo (Jumatano, Juni 30, 2021) wakati akifungua mafunzo ya siku nne yaliyoandaliwa na Taasisi ya Uongozi kwa lengo la kuwaimarisha viongozi ili matokeo ya uongozi wao yawapatie majawabu endelevu wananchi dhidi ya changamoto mbalimbali zinazowakabili kwenye maeneo yao.  Mafunzo hayo yanafanyika jijini Dodoma.

Amesema baada ya mafunzo hayo Serikali inatarajia viongozi hao watasimamia kikamilifu nidhamu katika utumishi wa umma na kuwa kioo katika kuzingatia maadili na miiko bila kubagua jinsia, kabila, dini, rangi ya ngozi, mtu atokako ndani ya nchi ilimradi hajavunja sheria.

Waziri Mkuu ameongeza kuwa mafunzo yatawawezesha viongozi hao kusimamia kikamilifu miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika ofisi zao za mikoa na za Mamlaka za Serikali za Mitaa katika maeneo yao ya utawala na kuongeza udhibiti katika ukusanyaji na matumizi ya mapato ya ndani ya halmashauri.

“Mtazingatia kikamilifu mipaka yenu ya madaraka na hatua mtakazozichukua zitazingatia sheria, kanuni na taratibu zilizopo. Mtasimamia kikamilifu mapambano dhidi ya dawa za kulevya pamoja na kudumisha uhusiano baina yenu na watumishi walio chini yenu, kwa kuzingatia kuwa kila mtumishi anao mchango katika kuboresha utendaji kwenye kituo chake cha kazi.”

Waziri Mkuu amesisitiza viongozi hao kwamba lazima wawe makini muda wote na watumishi wazembe, wezi na wabadhirifu kwenye halmashauri zao lazima wote wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za Serikali. Ameagiza ubadhirifu ushughulikiwe mapema kwa weledi na utaalam bila kulazimika kusimamisha utekelezaji wa miradi kwa muda mrefu.

 “Lazima watu wachache ambao wamezoea kupanga njama za kijinai kuiba au kutumia vibaya fedha za umma washughulikiwe kisheria kama upo ushahidi wa wazi kabla hata CAG hajakagua au viongozi wa juu wachukue hatua wakati ninyi mpo. Lazima mianya yote ya ubadhirifu izibwe na tusioneane haya.”

Pia, Waziri Mkuu ametoa wito kwa viongozi hao kuwa wa wakafanyeni kazi kwa uadilifu kulingana na viapo vyao na kila mmoja katika eneo lake awe msimamizi mzuri na kutanguliza mbele maslahi mapana ya Taifa, ikiwa ni pamoja na kuhakikisha miradi inakamilika kwa wakati.

Akizungumzia kuhusu miradi ya maendeleo kutokamilika kwa wakati na kwa ukamilifu, Waziri Mkuu amesema kuna changamoto ya baadhi ya miradi katika kutokukamilika kwa wakati na kwa kiwango kilichokusudiwa. “Pamoja na sababu nyingine tumebaini pia kuna baadhi ya viongozi huingilia michakato ya zabuni, manunuzi na ya ujenzi ikiwa ni katika hatua mbalimbali na wengine wanakwenda mbali zaidi kudai wapewe asilimia 10 ya fedha.”

“Nieleze bayana kuwa hili sasa tunalifuatilia kwa karibu na hatutakuwa na uvumilivu pale tutakapowabaini.  Nisistize kuwa Serikali ina macho mengi tutakapopata taarifa za baadhi yenu kujihusisha na vitendo vya ubadhirifu wa fedha za Serikali kupitia fedha zinazoletwa za Miradi ya Maendeleo au zile zinazokusanywa na Halmashauri hatua kali zitachukuliwa dhidi yenu.”

Mafunzo hayo yamehudhuriwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Ummy Mwalimu, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mohamed Mchengerwa, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, David Silinde, Naibu Waziri, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Festo Dugange.

Wengine ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Prof. Riziki Shemdoe, Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Dkt. Laurean Ndumbaro, Naibu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais - TAMISEMI; (Elimu), Gerald G. Mweli, Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais – TAMISEMI (Afya), Dkt. Grace E. Magembe  na Afisa Mtendaji Mkuu, Taasisi ya Uongozi, Kadari Singo.

(Mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU


Share:

Serikali Kuendelea Kuunga Mkono Kazi Za Sanaa


Serikali kupitia Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) wameahidi kuendelea kuunga mkono kazi mbalimbali za sanaa hapa nchini.

Hayo yamesememwa leo jijini Dar es Salaam na Afisa Sanaa Mwandamizi toka Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) Abel Ndaga wakati akizungumza na waandishi wa habari juu ya utoaji wa tuzo kwa wanafunzi wa vyuo wenye vipaji kupitia sanaa mbalimbali.

“Serikali kupitia Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo wenye zamana na Sekta ya Sanaa kupitia BASATA tutaendelea kutoa ushirikiano na wasanii mbalimbali ili kuweza kufanikisha malengo ya kukuza sekta ya sanaa nchini.

Afisa Sanaa Mwandamizi Ndaga ameongeza kuwa kuelekea siku ya utoaji tuzo kwa wanafunzi wa vyuo wenye vipaji kupitia sanaa mbalimbali wanataraji kuwa tuzo hizo zitakuwa zitatoa hamasa kwa vijana wengi hapa nchini.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya utoaji tuzo kwa wanafunzi wa vyuo wenye vipaji kupitia sanaa mbalimbali  Joseph Ndalu ameahidi kuwa tuzo hizo zitaweka historia kwa kushirikisha wasanii wa tansia mbalimbali.

“Katika tuzo hizi tunatarajia kuwa na wasanii wa tasnia mbalimbali kama wasanii wafilamu, bongo fleva na sanaa mbalimbali hivyo ni imani yangu tuzo hizi zitakuwa za kipekee sana”alisema Bw. Ndalu.

Tuzo kwa wanafunzi wa vyuo wenye vipaji kupitia sanaa mbalimbali zitafanyika siku ya jumamosi Juai tatu katika Kituo cha Mikutano Cha Kimataifa cha Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam kuanzia saa moja jioni.


Share:

Basi La Abiria Laacha Njia Na Kugonga Nyumba

Basi kampuni la Ulamaa T 330 DGB lililokuwa likisafiri kwenda Arusha kutokea Mwanza limepata ajali alfajiri ya leo kwa kuacha njia na kugonga nyumba eneo la Mkolani darajani jijini Mwanza.

Imeelezwa kwamba ndani ya nyumba hiyo kulikuwa na Watu 6 ambapo hakuna taarifa za kifo bali Majeruhi tu ambao wamepelekwa Hospitali ya Butimba.

Chanzo cha ajali kinaelezwa kuwa ni baada ya Dereva wa Basi kulikwepa gari dogo kulikosababisha gari kuacha njia baada ya kushindwa kulimudu



Share:

National Individual Consultant at UNICEF

Job no: 541473 Contract type: Consultancy Level: Consultancy Location: Tanzania,Uni.Re Categories: Education, Innovation UNICEF works in some of the world’s toughest places, to reach the world’s most disadvantaged children. To save their lives. To defend their rights. To help them fulfill their potential. Across 190 countries and territories, we work for every child, everywhere, every day, to build a better […]

This post National Individual Consultant at UNICEF has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Bashe Aagiza Ras Tabora Kuwaondoa Watumishi Wa Manispaa Ya Tabora Waliochukua Mashamba Katika Mashamba Katika Skimu Inala


 NA TIGANYA VINCENT
NAIBU Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amemwagiza Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Msalika Makungu kuwaondoa watumishi wote wa Manispaa ya Tabora ambao wamejimilikisha mashamba katika mradi wa Umwagiliaji wa Inala.

Alisema wamechukua maeneo hayo na kusababisha wananchi wanaozunguka mradi huo kukosa mashamba kwa ajili ya kulima kilimo cha mpunga.

Bashe alitoa kauli hiyo jana  wakati wa kufungua maadhimisho ya sherehe za siku ya Ushirika Duniani (SUD) ambapo Kitaifa inafanyika Mkoani Tabora na kilele kitakuwa tarehe 3 Julai mwaka huu.

Alisema licha ya Serikali kutumia fedha nyingi kujenga Bwawa hilo bado mradi huo haufanyikazi vizuri kama ulivyokusudiwa kwa sababu ya watumishi wa Manispaa ya Tabora kujimilikisha mashamba ambayo hawayalimi.

Katika hatua nyingine Naibu Waziri huyo alimwagiza Mrajis wa Vyama Vya ushirika Nchini Dkt. Benson Ndiege kufanya miaka mitatu mfululizo  maadhimisho ya sherehe za siku ya Ushirika Duniani (SUD) katika Mkoa mmoja badala ya kila mwaka kuanga katika eneo jipya.

Alisema hali hiyo itasaidia kuleta matokeo chanya kutokana na Washirika kujifunza katika eneo mmoja kwa kipindi cha miaka mitatu.

Wakati huo Naibu Waziri amewataka vijana kujiunga na ushirika ili kuondoa dhana potofu kuwa Ushirika na wazee na watu waliochoka.

Alisema ushirika ndio silaha pekee itakayowasaidia wakulima kupanga katika masoko na kupata bei nzuri itakayowasaidia kuondoa katika umaskini.

Bashe alisema Serikali itaendelea kuunga mkono Ushirika ili hatimaye uweze kuwa msaada mkubwa kwa wakulima kuchangia katika pato la Taifa kutoka la sasa la asilimia 26 na kuongezeka Zaidi.

Alisema kilimo ndio Sekta inayotoa ajira kwa wananchi wengi ni vema ikachangia kwa kiasi kikubwa katika pato la Taifa.

Kauli mbiu ya maadhimisho ya siku ya ushirika Duniani mwaka huu ni Ushirika  pamoja tujijenge uya kwa ubora na tija.


Share:

Makamu Wa Rais Dkt.Mpango Awasili Nchini Ufaransa Kuhudhuria Jukwaa La Kizazi Chenye Usawa


 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango  Juni 29, 2021 amewasili  Paris nchini Ufaransa  ambako atahudhuria Jukwaa la Kizazi Chenye Usawa ( Generation Equality Forum) linalofanyika Paris Ufaransa kuanzia Juni 30 – Julai 2, 202.  Makamu wa Rais anamuwakilisha  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan katika Jukwaa hilo.

Aidha, Makamu wa Rais alipata maelezo jinsi Ubalozi wa Tnazania unavyotekeleza Sera ya Diplomasia ya Uchumi katika eneo lake uwakilishi ambalo ni Ufaransa,  Hispania; Ureno; Algeria na Morocco.   Maelezo hayo yalitolewa na Mhe. Samwel Shelukindo, Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa. Pia Balozi Shelukindo anaiwakilisha Tanzania katika Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO)

Makamu wa Rais Dkt. Philip Isdor Mpango amempongeza Balozi Shelukindo kwa uwakilishi mzuri katika nchi hizo na kumuhakikishia serikali itaendelea kutatua changamoto zinazojitokeza katika ubalozi huo. Amemtaka kuendelea kutafuta mahusiano na sekta binafsi zilizopo nchini Ufaransa kwa manufaa ya nchi zote mbili. Hapo kesho juni 30,2021 Makamu wa Rais  anatarajia Kuhudhuria ufunguzi wa Jukwaa la kizazi cha usawa lenye lengo la kuchagiza haki za usawa wa kijinsia kama zilivyokubaliwa katika mkutano wa Beijing wa mwaka 1995.


Share:

Project Coordinator – Covid19 Case Management at Save the Children

Child Safeguarding: Level 3 – The responsibilities of the post may require the post holder to have a regular contact with or access to Pregnant Women, Mothers and Children ROLE PURPOSE: The Project Coordinator will be responsible for delivery of the Save the Strengthening COVID-19 Case Management in Regional Referral Hospitals. He/ She will be […]

This post Project Coordinator – Covid19 Case Management at Save the Children has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Sub Regional Director for Eastern and Southern Africa at Plan International

Location: Nairobi, Tanzania Company: Plan International The Organisation Plan International is an independent development and humanitarian organisation that advances children’s rights and equality for girls. We believe in the power and potential of every child. But this is often suppressed by poverty, violence, exclusion and discrimination. And it’s girls who are most affected. Working together with children, […]

This post Sub Regional Director for Eastern and Southern Africa at Plan International has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Office Secretary at TANROADS

Tanzania National Roads Agency (TANROADS) is an Executive Agency under the Ministry of Works and Transport, established under section 3 (1) of the Executive Agencies Act (Cap 245) and came into operation in July, 2000. The Agency is responsible for the Maintenance and development of the trunk and Regional road network in Tanzania. The Regional […]

This post Office Secretary at TANROADS has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Work Inspector/Road Work at TANROADS

Tanzania National Roads Agency (TANROADS) is an Executive Agency under the Ministry of Works and Transport, established under section 3 (1) of the Executive Agencies Act (Cap 245) and came into operation in July, 2000. The Agency is responsible for the Maintenance and development of the trunk and Regional road network in Tanzania. The Regional […]

This post Work Inspector/Road Work at TANROADS has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

UHURU WA VYOMBO VYA HABARI NA MATARAJIO YA UONGOZI WA AWAMU YA SITA YA SERIKALI YA TANZANIA


Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Uhuru wa vyombo vya habari ni miongoni mwa haki za msingi za kila raia wa Tanzania. Haki hii huwawezesha raia kupata na kutoa taarifa, kujieleza ili kutoa maoni yao katika masuala mbalimbali yenye maslahi yao. 

Pia, uhuru wa vyombo vya habari huchochea kukua kwa misingi ya haki za binadamu, demokrasia, na utawala bora.

 Kuwepo kwa misingi hii husaidia wananchi kushiriki katika uendeshaji wa nchi, kuchagua viongozi wanaowataka, kuhoji uendeshaji wa serikali pamoja na kufahamu masuala yanayoathiri maisha yao.

Katika miaka ya hivi karibuni, kumekuwepo na changamoto zinazoathiri au kuminya uhuru vya vyombo vya habari. Taasisi na asasi za kiraia zikiwemo Baraza la Habari Tanzania (MCT), Taasisi ya Vyombo vya Habari Kusini mwa Afrika (MISA TAN), LHRC, na zinginezo zimeripoti matukio kadhaa kuashiria kuwepo kwa mazingira magumu kwa vyombo vya habari na wanahabari kutekeleza uhuru huu.

 Matukio hayo ni pamoja na kufutwa au kufungia vyombo vya habari, kutoza faini na karipio dhidi ya vyombo vya habari, ukamataji na uwekaji kizuizini kwa waandishi wa habari na vikwazo vya kisheria na kikanuni zinazodhibiti vyombo vya habari na wanahabari kutekeleza wajibu wao kwa uhuru.

Hata hivyo, kuapishwa kwa Mhe. Samia Suluhu Hassan kuwa Rais wa Awamu ya Sita ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kunaleta matumaini ya kuwepo kwa mazingira wezeshi yanayohimiza uhuru wa vyombo vya habari nchini.

 Matumaini haya yanajikita katika nia thabiti ya Mhe. Rais Samia ya kuhakikisha vyombo vya habari vinatimiza wajibu wake wa kuhabarisha umma kwa uhuru.

Akizungumza wakati wa kikao chake na wahariri wa vyombo vya habari kilichoafanyika tarehe 28 June 2021, Mhe. Rais Samia alinukuliwa akihimiza vyombo vya habari vilivyofungiwa kufunguliwa huku akivitaka kuzingatia sheria na miongozo ya serikali. 

Aidha, Mhe. Rais Samia mbali ya kuelekeza kulindwa na kuheshimiwa kwa uhuru wa vyombo vya habari, alitoa hakikisho la serikali yake kuzingatia kuwepo kwa sheria zisizokwaza upatikanaji na usambazaji wa habari nchini.

Ni matumaini ya wanahabari nchini kwamba Mhe. Rais Samia ameonesha dhamira ya wazi ya kuweka mazingira mazuri yanayochagiza uhuru wa vyombo vya habari. 

Hata hivyo, ni wajibu wa kila chombo cha Habari na waandishi wa Habari kuutumia vizuri uhuru huu kwa kutimiza Wajibu kwa kuzingatia weledi na maadili katika kutafuat, kuchakata na kusambaza taarifa na habari mbalimbali zenye maslahi kwa umma.

 Daima watambue kwamba hakuna uhuru bila wajibu.
Share:

Material Engineer at TANROADS

Tanzania National Roads Agency (TANROADS) is an Executive Agency under the Ministry of Works and Transport, established under section 3 (1) of the Executive Agencies Act (Cap 245) and came into operation in July, 2000. The Agency is responsible for the Maintenance and development of the trunk and Regional road network in Tanzania. The Regional […]

This post Material Engineer at TANROADS has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Senior Core Banking Systems Administrator at NMB Bank

Job Purpose Perform extensive business analysis and documentation of the requirements of complex product management projects coordinating with cross-functional resources to achieve project objectives. Main Responsibilities Support product life cycle team during product set up in the Core Banking system Partner internal with business stakeholders to understand technical trade-offs and, positioning, requirements architecture to drive […]

This post Senior Core Banking Systems Administrator at NMB Bank has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JUNI 30,2021



















Share:

Tuesday 29 June 2021

Video : BAHATI BUGALAMA - UKOO

Share:

TUME YA UTUMISHI WA UMMA YAENDELEA NA MKUTANO WA NNE KWA MWAKA WA FEDHA 2020/2021 JIJINI DAR ES SALAAM

Makamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma wakiwa katika Mkutano leo 29 Juni 2021: Mheshimiwa Khadija A.M. Mbarak (kushoto) na Mheshimiwa Immaculata P. Ngwale (kulia) wakishiriki katika Mkutano wa Nne kwa mwaka wa fedha 2020/2021 unaofanyika Jijini Dar es Salaam. (Picha na PSC)
Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bw. Nyakimura Muhoji (kushoto) akiwa na Makamishna wa Tume ya Utumishi wa Umma, Mhe. Balozi (Mstaafu) Daniel Ole Njoolay (katikati) na Mhe. Balozi (Mstaafu) John Haule wakishiriki katika Mkutano wa Tume leo 29 Juni 2021 unaofanyika Jijini Dar es Salaam.
Maafisa wa Tume ya Utumishi wa Umma: Bw. Peleleja Masesa, Katibu Msaidizi, Idara ya Rufaa na Malalamiko (kushoto), Bw. Evarist Mashiba, Afisa Sheria Mkuu (katikati) na Bw. Charles Mulamula, Mkurugenzi wa Kitengo cha Huduma za Sheria (kulia) wakishiriki Mkutano wa Tume unaoendelea kufanyika Jijini Dar es Salaam. (Picha na PSC)
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger