Tuesday 29 June 2021

Rais Samia akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi wa Idara ya Afrika-IMF Abebe Aemro Selassie Ikulu Jijini Dodoma



Share:

Mpango Wa Tatu Wa Maendeleo Wa Taifa Wazinduliwa


 Na. Saidina Msangi, WFM,
Serikali imezindua rasmi Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22 hadi 2025/26 unaotarajiwa kugharimu shilingi trilioni 114.8 ambapo Serikali itachangia Sh. trilioni 74.2 na sekta binafsi itachangia Sh. trilioni 40.6.

Mpango huo unaotarajiwa kutekelezwa kwa ushirikiano kati ya sekta ya umma na sekta binafsi umezinduliwa jijini Dodoma na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa katika ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete.

Akizungumza katika uzinduzi huo Waziri kuu Mhe. Kassim Majaliwa (Mb), alisema kuwa Mpango huo umezingatia Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025, sera na mikakati mbalimbali ya kisekta, matokeo ya tafiti zilizofanywa na vyuo na taasisi mbalimbali hapa nchini pamoja na dira ya Afrika Mashariki ya 2050.

“Mpango huu una dhima ya kujenga Uchumi Shindani na Viwanda kwa Maendeleo ya Watu na umejikita katika kuchochea uchumi shindani na shirikishi na kuimarisha ukuaji wa uzalishaji wa ndani na utoaji huduma, kukuza uwekezaji na biashara, kuchochea maendeleo ya watu na kuendeleza rasilimali watu”, alisema Mhe. Majaliwa.

Mhe. Majaliwa alisema kuwa katika mpango huu wa tatu Serikali itaendelea kutekeleza miradi ya kielelezo kama ilivyokuwa katika mpango wa pili hususani ujenzi wa Reli ya Kati kwa Kiwango cha Standard Gauge (SGR), Ujenzi wa Mradi wa Kufua Umeme wa Maji Julius Nyerere (JNHPP) – 2,115 MW, Ujenzi wa Bomba la Mafuta - East African Crude Oil Pipeline (EACOP) na Ununuzi wa Meli na Ujenzi wa Bandari ya Uvuvi (Mbegani).

“Mpango huo una ushirikishwaji wa kitaifa na kimataifa na kuwa wote kwa pamoja tuna jukumu la kuhakikisha utekelezaji wake unafanikiwa kikamilifu”, alisisitiza Mhe. Majaliwa.

Mhe. Majaliwa ameielekeza Wizara ya Fedha na Mipango kuhakikisha inatoa elimu ya kutosha ili kuwezesha kila mmoja kushiriki kikamilifu katika utekelezaji wake.

Aidha Mhe. Majaliwa ameagiza wizara zote, taasisi za umma, idara zinazojitegemea wakala wa Serikali, sekta binafsi na wadau wote wa maendeleo kuhakikisha kuwa ofisi zao zina nakala ya mpango huo ili kuwezesha utekelezaji wa viwango.

Amesisitiza kuwa Serikali imedhamiria kuhakikisha kuwa malengo ya mpango huo yatafikiwa na kuwa Serikali haitafumbia macho ukwepaji kodi, uzembe kazini, ufujaji wa fedha na rushwa.

Akizungumza wakati wa kumkaribisha mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Massauni (Mb) alisema kuwa mpango huo ni nyenzo muhimu katika kuharakisha maendeleo ya nchi.

Alisema maandalizi ya mpango huo yameshirikisha kikamilifu makundi mbalimbali ya wadau wakiwemo sekta binafsi, asasi za kiraia, mashirika yasiyo ya kiserikali, washirika wa maendeleo na jamii kwa ujumla umezingatia mahitaji halisi ya makundi yote.

“utekelezaji wa Mpango huu utahitimisha utekelezaji wa Mpango Elekezi wa Muda Mrefu (2011/12 – 2025/26) ili kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 ambayo ni: maisha bora kwa wananchi; amani, utulivu na umoja; utawala bora; jamii iliyoelimika na inayopenda kujifunza; na uchumi imara na shindani”, alisema Mhandisi Massauni.

Alifafanua kuwa  Serikali imeanza maandalizi ya Dira mpya itakayotekelezwa baada ya kuhitimishwa kwa Dira ya sasa mwaka 2025. Dira hiyo itaendeleza maono na mafanikio yaliyopatikana katika utekelezaji wa Dira 2025 ikijumuisha kuchochea ukuaji wa uchumi na kuboresha maisha ya watu.

Awali akizungumza katika ufunguzi huo Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Emmanuel Tutuba alisema kuwa mpango huo umejikita katika maeneo makuu Matano ya kipaumbele ikiwemo kuchochea uchumi shindani na shirikishi.

Pia mpango huo umejikita katika kuimarisha uwezo wa uzalishaji wa viwanda na utoaji wa huduma ambapo itajikita katika kujumuisha miradi ya viwanda  inayolenga kuongeza thamani kwa kuzalisha bidhaa zitakazotumia rasilimali za ndani.

“Serikali inalenga kujumuisha programu za kuimarisha masoko ya ndani na kutumia fursa za masoko ya kikanda na kimataifa kwa bidhaa zinazozalishwa nchini kukuza uwekezaji na biashara”alisema Bw. Tutuba.

Aliongeza kuwa mpango huo pia unalenga kuchochea maendeleo ya watu ambapo Serikali inakusudia kutekeleza miradi itakayoboresha maisha ya watu ikijumuisha eneo la elimu na mafunzo eneo la afya na ustawi wa jamii, upatikanaji wa huduma za maji na uhifadhi mazingira.

Alisema katika kuendeleza rasilimali watu Serikali inajumuisha programu na mikakati mbalimbali ambayo inalenga kuendeleza maarifa na ujuzi wa rasilimali watu nchini katika ngazi zote za elimu ili kuwawezesha vijana waweze kujiajiri.

Aidha katika kuhakikisha vipaumbele vilivyoelezwa vinatekelezwa kwa ufanisi na fedha zinazopatikana kwa ajili ya utekelezaji wa miradi hiyo kwa wakati mpango huo umeainisha mfumo wa ufuatiliaji na tathmini ili kuwezesha uwepo wa uwajibikaji.

Naye Mwakilishi Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa Nchini (UNDP) Bi. Christina Musisi, alipongeza Serikali kwa kukamilisha mpango huo kwa wakati na kueleza kuwa wananchi, Serikali, wadau wa maendeleo sekta binafsi na mashirika yasiyo ya kiserikali watatumia mpango huo kama nyenzo muhimu ya utekelezaji katika kufikia malengo ya dira ya maendeleo 2025 na ajenda 2030.

Alisema kuwa mashirika ya Umoja wa Mataifa yatashirikiana na Serikali katika kutekeleza mpango huo wa maendeleo kwa miaka mitano ijayo.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Sekta Binafsi Bw. Zaki Mbena alisema kuwa mpango huo umetoa nafasi na fursa kwa sekta binafsi kutekeleza majukumu yake na kupata wigo mpana wa kufanya kazi na kupata maelekezo ili kufanikisha mpango huo kwa ufanisi.

Aliongeza kuwa Sekta binafsi nchini itatoa mchango wake kwa Serikali unaokadiriwa kuwa shilingi trilioni 40.6 na hata kuzidi kwa kuwa sekta hiyo imeshirikishwa ipasavyo wakati wa maandalizi ya mpango huo ambao ameuelezea kuwa ni muhimu na unaungwa mkono.

Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/22-2025/26 ni wa mwisho katika utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2025 na unatarajiwa kuanza utekelezaji wake kuanzia mwaka wa fedha 2021/22.

Mpango huo ni mwendelezo wa jitihada za Serikali za kusimamia rasilimali za ndani ya nchi ikijumuisha rasilimali za madini, maliasili, gesi asilia, fedha na rasilimali watu kwa lengo la kuboresha hali ya Maisha ya Watanzania wote.

MWISHO.


Share:

Waziri Mkuu Azindua Mpango Wa Tatu Wa Maendeleo


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amezindua Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/2022–2025/2026 utakaogharimu shilingi trilioni 114.8, ambapo sekta binafsi inatarajiwa kuchangia shilingi trilioni 40.6 na sekta ya umma shilingi trilioni 74.2.


“...fedha hizo zinajumuisha mikopo na misaada ya wabia wetu wa maendeleo. Kwa niaba ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, napenda kuwahakikishia kwamba fedha hizi zitapatikana na malengo tuliyojiwekea yatatekelezwa.”

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumanne, Juni 29, 2021) wakati akizindua Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2021/2022–2025/2026 katika Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete, jijini Dodoma.

Waziri Mkuu amesema mpango huo una dhima ya kujenga uchumi shindani na viwanda kwa maendeleo ya watu na umejikita katika kuchochea uchumi shindani na shirikishi; kuimarisha uwezo wa uzalishaji viwandani na utoaji huduma; kukuza uwekezaji na biashara; kuchochea maendeleo ya watu; na kuendeleza rasilimali watu.

Amesema Serikali itahakikisha malengo ya Mpango huo yanafikiwa. “Kamwe hatutafumbia macho tabia ya ukwepaji kodi, kazini, ufujaji wa fedha na rushwa na tutaendelea kuenzi bunifu na kupokea mawazo mbadala yenye lengo la kuboresha utekelezaji wa Mpango huu.”

“Katika Mpango huu wa Tatu tutaendelea kutekeleza miradi ya kielelezo kama ilivyokuwa katika Mpango wa Pili hususan ujenzi wa reli kwa kiwango cha Kimataifa (SGR), ujenzi wa mradi wa kufua umeme wa maji wa Julius Nyerere wenye uwezo wa kuzalisha megawati 2,115; ujenzi wa bomba la kusafirisha mafuta (EACOP) na ununuzi wa meli na ujenzi wa bandari ya uvuvi (Mbegani).”

Kadhalika, Waziri Mkuu ameongeza kuwa mpango huo ni mkakati mahsusi wa utekelezaji wa Ilani ya CCM ya Mwaka 2020. “Niwaahidi Watanzania kwamba mambo yote tuliyoahidi wakati wa kampeni za uchaguzi wa mwaka 2020, yanaenda kutekelezwa kupitia Mpango huu.”


Waziri Mkuu amesema mpango huo umezingatia Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2025; Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya 2020; Mpango Elekezi wa Muda Mrefu 2011/2012–2025/2026 na Matokeo ya Tathmini Huru ya utekelezaji wa Mpango wa Pili wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano 2016/2017–2020/2021.

Pia, Waziri Mkuu amesema mpango huo umezingia sera na mikakati mbalimbali ya kisekta; matokeo ya tafiti zilizofanywa na vyuo na taasisi mbalimbali nchini; Dira ya Afrika Mashariki 2050; Dira ya Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika 2050; Ajenda 2063 ya Maendeleo ya Afrika; Malengo ya Maendeleo Endelevu 2030; na Makubaliano ya Paris chini ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi.

“Wizara ya Fedha na Mipango endeleeni na utaratibu wa kutoa elimu ya kutosha ili kumwezesha kila mmoja kushiriki kikamilifu katika utekelezaji. Aidha, ninaagiza Wizara, Taasisi za Umma, Idara Zinazojitegemea Wakala za Serikali, Sekta Binafsi na Wadau wote wa maendeleo kuhakikisha ofisi zao zina nakala ya Mpango huu na kuanza kuutekeleza.”

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango, Emmanuel Tutuba amesema mpango huo ni mwendelezo wa jitihada za Serikali za kuimarisha upangaji mipango na kusimamia rasilimali za ndani ya nchi ikijumuisha rasilimali za madini, maliasili, gesi asilia, ardhi, fedha na rasilimali watu kwa lengo la  kuboresha hali ya maisha ya Watanzania wote.

Amesema ili kuhakikisha mpango huo unatekelezwa kwa ufanisi na unafikia malengo yaliyopangwa, Wizara imeandaa mwongozo wa kitaifa wa ufuatiliaji na tathmini wa miradi na programu za maendeleo na mfumo wa kitaifa wa kusimamia miradi ya maendeleo.

Naye, Mwakilishi Mkaazi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) Nchini Tanzania, Christine Musisi amesema wananchi, Serikali, wadau wa maendeleo, sekta binafsi watautumia mpango huo kama nyenzo muhimu ya utekelezaji wa kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo ya 2025 na Malengo ya Maendeleo Endelevu 2030. Pia ameihakikishia Serikali kwamba mashirika yote ya Umoja wa Mataifa yataunga mkono utekelezaji wa mpango huo ili kufikia malengo yaliyokusudiwa.

(Mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU



Share:

IGP Sirro afanya mabadiliko kwa baadhi ya Makamanda wa Polisi wa Mikoa



Share:

Tanzia :MHANDISI MFUGALE AFARIKI DUNIA



Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), Mhandisi Patrick Mfugale, amefariki dunia leo Juni 29, 2021 katika Hospitali ya Benjamin Mkapa jijini Dodoma.

Taarifa zinaeleza kuwa Mhandisi Mfugale aliondoka jana jijini Dar es Salaam na kuelekea Dodoma akiwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi kwa safari ya kikazi ambapo majira ya saa tano asubuhi ya leo, alianza kujisikia vibaya na kukimbizwa hospitali ambapo muda mfupi baadaye, alifariki dunia.

Enzi za uhai wake, Mfugale atakumbukwa kwa kufanya utafiti na kutengeneza mfumo wa madaraja nchini ambapo miongoni mwa madaraja aliyosimamia ujenzi wake ni Daraja la Kikwete lililopo kwenye Mto Malagarasi, Daraja la Mkapa lililopo Rufiji, Daraja la Umoja linalounganisha Tanzania na Msumbiji lililopo Ruvuma na Daraja la Nyerere lililopo Kigamboni jijini Dar es Salaam.

Pia Mfugale atakumbukwa kwa kubuni na kusimamia ujenzi wa barabara za kitaifa zenye urefu wa takribani kilometa 36,258 na ndiye aliyekuwa mwenyekiti wa kikosi cha ujenzi wa reli ya kisasa SGR inayoendelea kujengwa.

Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina!
Share:

Wallace Karia Apitishwa na Kuwa Mgombea Pekee wa Urais TFF


Kamati ya Uchaguzi ya Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) leo Juni 29, 2029 imempitisha Wallace Karia kuwa mgombea pekee wa nafasi ya Rais wa shirikisho hilo, baada ya kukidhi vigezo vyote.

Wallace Karia ambae ndio Rais wa sasa wa TFF jina lake pekee ndio lililopitishwa na kamati ya uchaguzi, baada ya wagombea wengine wa nafasi hiyo ya Urais Hawa Mniga pamoja na Evance Mgeusa kukosa vigezo vinavyokidhi kwa wao kuendelea na hatua inayofata kwenye uchaguzi.

Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF Benjamini Kalume amesema kwa sasa kitakachofanyika ni Wallace Karia akiwa kama mgombea pekee ni kwenda kuthibitishwa na Mkutano mkuu na si kumpigia Kura.

Mkutano Mkuu wa TFF utafanyika Agosti 7, 2021 Mkoani Tanga ambapo moja ya Ajenda ya mkutano huo ni Uchaguzi wa kuchagua viongozi wa shirikisho hilo ikiwemo nafasi ya Urais na nafasi sita (6) za wajumbe wa kamati ya Utendaji.
 



Share:

Jacob Zuma. Ahukumiwa Miezi 15 Jela


Mahakama nchini Afrika Kusini imemhukumu kifungo cha miezi 15 aliyekuwa rais wa taifa hilo, Jacob Zuma.

Hii ni baada ya Korti ya Katiba kumpata na hatia ya kukaidi agizo la kufika mahakamani baada yakukosa kufika kwenye kikao cha uchunguzi wa kesi ya ufisadi wakati alipokuwa rais.

Mahakama ilikuwa na jukumu la kuamua kama Bw.Zuma anapaswa kuadhibiwa kwa kukataa wito wa mahakama na amri ya mahakama ya kumtaka afike mahakamani kutoa ushahidi kuhusu shutuma za rushwa wakati wa utawala wake.

Mwenyekiti wa kamati maalum ya uchunguzi wa mahakama ,Raymond Zondo ambayo imekuwa ikichunguza madai hayo aliiomba mahakama itamke kuwa rais huyo wa zamani alidharau mahakama na imhukumu kifungo cha miaka miwili.

Tangu alipojiuzulu mnamo mwaka 2018,  Zuma amekuwa akifika mahakamani akikabiliwa na shutuma za ufisadi ambazo amekuwa akizikanusha.


Share:

Mwenyekiti Wa CCM Na Rais Wa Jamhuri Ya Muuungano Wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan Aongoza Kikao Cha Halmashauri Kuu Ya Taifa Ya CCM

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akifungua Kikao cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi NEC, kilichokutana leo Juni 29,2021 katika Ukumbi wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM Jijini Dodoma.(Picha na Ikulu)



Share:

Regional Planning, Monitoring, Evaluation and Reporting Specialist at WaterAid

Job Title: Regional Planning, Monitoring, Evaluation and Reporting Specialist Location- Any country with WaterAid presence in East Africa (Uganda, Tanzania, Rwanda and Ethiopia) Salary: Grade F Contract type: 3 Years Fixed Contract (Renewable) Reports to: Regional Programme Manager in East Africa Region Relationships: Programme Support Units at Country Programme level, Monitoring & Evaluation Officers, PMER Project team in the […]

This post Regional Planning, Monitoring, Evaluation and Reporting Specialist at WaterAid has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

WANAUME WAWILI WABADILISHANA WAKE ZAO KUMALIZA SKENDO YA UZINZI VICHAKANI

Wanaume wawili kutoka Uganda wameamua kubadilishana wake zao ili kumaliza sakata ya uzinzi kwa amani.

Hii ni baada ya mmoja wao Ali Mudde, mkazi wa kijiji cha Musoma katika kisiwa cha Jagozi kufahamishwa kuwa Bryan Masaba alikuwa anafanya mapenzi na mke wake katika kichaka kilichoko karibu.

Kwa mujibu wa Daily Monitor, Mudde akiwa na hasira za mkizi aliripoti suala hilo kwa mwenyekiti wa kijiji Peter Balikowa ambaye aliitisha kikao cha kutatua mzozo huo.

Ni wakati wa kikao hicho cha korti ya kijiji ndipo Balikowa aliwaagiza wanaume hao wawili kubadilishana wake zao iwapo wako sawa na bila kupoteza wakati wawili hao walikubali uamuzi huo.

"Sina pingamizi na uamuzi uliotolewa na mahakama hii na niko tayari kabisaa kumpa (Masaba) mke wangu," Mudde alisema.

Baada ya Mudde kukubali, mwenyekiti huyo alimuuliza mke wa Masaba iwapo yuko tayari kuwa na mke mwenza lakini alikataa katakata na badala yake kupendekeza kuwa mke wa Mudde.

Balikowa alikubali pendekezo hilo na kisha wanaume hao wawili walibadilishana wake zao bila tatizo.

Hakuna mwanandoa kati yao aliyekuwa na mtoto.

Katika tukio sawia na hilo lililoshudiwa nchini Kenya, wanawake wawili kutoka kaunti ya Busia waliwaacha wengi na bumbuwazi baada ya kubadilishana waume zao kwa lengo la kutafuta furaha.

Lilian Weta mwenye umri wa 28, mama wa watoto watatu na Millicent Auma mwenye umri wa miaka 29, mama wa watoto wawili walizua gumzo kwa kufanya jambo la lisilokuwa la kawaida. Wanawake hao wanadai walifanya uamuzi huo baada ya kusukumwa na sakata ya uzinzi usioisha katika familia zao.
Share:

AKUTWA AMEFARIKI KWA KUPIGWA NJE YA DUKA LA VINYWAJI VIKALI



Mwili wa mwanaume anayedaiwa kuwa ni mfugaji mkazi wa kijiji cha Arirai wilayani Ngorongoro mkoa wa Arusha, Sabore Shumbi (44) umekutwa pembeni ya duka la kuuza vinywaji vikali katika kijiji cha Haydom wilaya ya Mbulu Mkoa wa Manyara ukiwa na majeraha kichwani kwa kupigwa na kitu chenye ncha kali.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Merrisone Mwakyoma amesema chanzo cha kifo hicho hakijajulikana akisema mwili huo umekutwa na majeraha matatu kichwani na kwamba watu waliokuwa wakipita eneo hilo ndio walioutambua mwili huo na kutoa taarifa polisi.

"Jina la mmiliki wa kibanda hicho linahifadhiwa wakati huu tunaoendelea na uchunguzi kwa sababu tangu kifo chake hakuna muuzaji wala mmiliki wa duka aliyeonekana wala kufungua duka",amesema Kamanda Mwakyoma



Share:

LEGAL OFFICER II – 4 POST at BRELA

POST LEGAL OFFICER II – 4 POST POST CATEGORY(S) LEGAL EMPLOYER Business Registrations and Licensing Agency (BRELA) APPLICATION TIMELINE: 2021-06-28 2021-07-11 JOB SUMMARY N/A DUTIES AND RESPONSIBILITIES i. To process, scrutinize and approve applications; ii. To reconcile files/documents and update into the ORS; iii. To respond to the online and offline official searches. iv. To […]

This post LEGAL OFFICER II – 4 POST at BRELA has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Masseuse (Spa Therapist) at One Nature Hotels

Position: Masseuse (Spa Therapist) Company Name & Location One Nature Hotels – Arusha Office, Tanzania   Qualification • 5-6 years’ experience  working as a Masseuse in a luxury hotel • Good communication skills ·  Must have the ability to multi Task ·  Ability to handle pressure. ·  Maintain high standards of personal hygiene & grooming How to […]

This post Masseuse (Spa Therapist) at One Nature Hotels has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Forensic Analyst at Vodacom

At Vodacom, we’re working hard to build a better future. A more connected, inclusive and sustainable world. As a dynamic global community, it’s our human spirit, together with technology, that empowers us to achieve this. We challenge and innovate in order to connect people, businesses, and communities across the world. Delighting our customers and earning […]

This post Forensic Analyst at Vodacom has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

Head; HR Shared Services at CRDB Bank

Job Summary Reporting directly to the Director of Human Resources, this is a key position responsible for ensuring HR service excellence at CRDB Bank PLC with a broad scope across all generalist HR queries and administration, reward and benefits, payroll and people analytics. The role requires a focus on continuing to improve service excellence, standardize […]

This post Head; HR Shared Services at CRDB Bank has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:

TAASISI YA WAJIBU YAZINDUA RIPOTI ZA UWAJIBIKAJI MWAKA 2019/2020, WADAU WAPONGEZA

WADAU mbalimbali kutoka taasisi za Serikali, viongozi, wabunge ,Asasi za Kiraia na wanafunzi vyuo vikuu wameshuhudia uzinduzi wa Ripoti tano za Uwajibikaji ambazo zimetokana na Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali( CAG).

Ripoti hizo zimeandaliwa na Taasisi ya WAJIBU ambayo imeziandaa ripoti hizo za uwajibikaji baada ya kuichambua kwa kina ripoti ya CAG ambayo iliwasilishwa kwa Rais Samia Suluhu Hassan Machi 28 mwaka huu na baadae ripoti hiyo ya CAG ikakabidhiwa kwa Bunge Aprili 4 mwaka huu.

Akizungumza jana Juni 28,2021 jijini Dodoma, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya WAJIBU,Bwa. Ludovic Utouh ambaye amewahi kuwa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG), amesema ripoti hizo ni za tano tangu waanze kuandaa na kuzitayarisha kutokana na ripoti za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.

"Kama tunavyojua ripoti za mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali ambazo zimewasilishwa kwa Rais Machi 28 na kuwasilishwa bungeni Aprili 4, ni ripoti zinazotayarishwa kitaalamu, ni ripoti kubwa na ripoti ambazo kusema kweli kwa Watanzania wangi huwa hawana shauku ya kuisoma kwa sababu ya ukubwa wake.

"Sasa sisi WAJIBU tunachukua ripoti zile na kuchambua kwa undani na tunachukua yale tunayoamini yanauzito na umuhimu mkubwa kwa watanzania, kwa hiyo utakuta ripoti ya WAJIBU iliyozinduliwa leo ya Serikali kuu na mashirika ya umma inatokana na ripoti mbili kubwa za CAG za Serikali Kuu na mashirika ya umma na tumeweza kuja na kitabu cha kurasa 31.

"Na utakuta katika ripoti ile kubwa tumechambua mambo 10 ambayo tumeona yana umuhimu zaidi kwa maendeleo ya nchi yetu na ukienda kwenye ripoti ya serikali ya mtaa na miradi ya maendeleo ambayo nayo imetokana na ripoti mbili za CAG ambayo ina mambo 21 ina mambo nane ambayo tumeona yana umuhimu kwa umma.

"Ukija kwenye ripoti ya tatu ambayo ni ripoti ya Ufanisi ile kwa kuwa imetokana na ripoti ya CAG mwaka jana aliwasilisha bungeni ripoti 15 za ufanisi, sisi katika kupitia ripoti zile tumeona zina mambo muhimu zaidi kwa maendeleo ya nchi na tumeweza kuja na ripoti yenye page 31 ambayo inajikita kwenye maeneo hayo, "amesema Utouh.

Amesema ombi lake baada ya kuzinduliwa kwa ripoti hizo za uwajibikaji, ni vema wananchi wakazisoma kwani watazisambaza katika maeneo mbalimbali na zitakuwepo kwenye Website ya WAJIBU ,pia zitapatikana kwenye taasisi.

"Tutazigawa kupitia taasisi mbalimbali ili watanzania wapate ripoti hizi na wazisome, wakati tunasherehekea siku 100 za uongozi wa Rais Samia kweli sisi kama wananchi wa Tanzania tuwe na ari ya kuungana naye na kumsaidia kwa nia yake njema aliyonayo ya kuleta maendeleo ya nchi katika kudai uwajibikaji pale.

"Ambapo tunaona taasisi ya serikali au chombo cha Serikali hakitimizi wajibu wake , ndio lengo la WAJIBU tunasema kwamba rasimali za Serikali za taifa zikisimamiwa vizuri zinakuwa za kila Mtanzania.

Kwa upande wake Mwakilishi Ofisi ya Msajili wa NGO's Charles Mpaka amewapongeza WAJIBU kwa kuja na ubunifu waliokuja nao wa kupitia ripoti ya CAG na kuziandikia taarifa fupi ."Tumeona ripoti ya CAG ni kubwa na WAJIBU wameona umuhimu wa kuichambua na kuja na taarifa fupi.Ripoti ya CAG ilikuwa na zaidi ya kurasa 250 lakini wao wamekuja na taarifa yenye 21 mpaka 31.

"Maana yake tunaongea asilimia nane mpaka 11 wamekwenda kuipunguza, hivyo itakwenda kusaidia wananchi kupata tafsiri ya haraka na uelewa mwepesi wa ripoti ya CAG,"amesema

Wakati huo huo Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) Mhe.​Naghenjwa Kaboyoka amesema wamekuwa wakifanya kazi na WAJIBU kwa karibu sana na kwamba WAJIBU wamekuwa kama Bunge nje ya Bunge, wamekuwa wakiwakilisha wananchi , maana hizo ripoti zao wanazichambua kiasi kwamba wananchi wanaweza kuzisoma na kuzielewa.

"Kwa hiyo imekuwa mkono wetu wa kulia wa kusaidia kamati zetu mbili za PAC na LAAC , unakuta wenzetu wanakwenda mbali zaidi kueleza yale ambayo hatupati muda wa kuyazungumzia bungeni lakini wenzetu WAJIBU wanayachambua na kuyaeleza kwa wadau, na hivyo wadau wanapata nafasi ya kujua kilichopo.

"Kwa mfano tukiangalia bajeti ya mwaka huu siku zote tunasema kilimo ndio uti wa mgongo lakini akangalia bajeti iliyopita nafikiri ilitolewa tu asilimia mbili na hii ndio sekta ya uzalishaji, sasa kama sekta ya uzalishaji hazitatengewa hela nyingi zikazalisha tunategemea maendeleo gani, yatakuwa maendeleo ya vitu sio watu.

"Serikali za mitaa tuna tatizo moja, tatizo linawezekana hawa wanzetu tangu wamemaliza shule hajawahi kupelekwa kozi , hajui tena taratibu za kimataifa za kutoa ripoti zimekuaje , matokeo yake inawezekana kweli hajaiba lakini akawa hajui jinsi ya kuandaa ripoti, kwa hiyo anapata ripoti chafu.

"Lakini kusema kweli ni vizuri hawa wenzetu ambao wapo katika taaluma ya kusimamia masuala ya fedha mara kwa mara wapelekwe kwenye kozi, mara kwa mara waelezwe taratibu mpya na kufundishwa ,maana unakuta wanasema hawa wamezoea kuandika vocha tu,"amesema.

Ameongeza inawekana ni wasomi wazuri lakini viwango vya kimataifa vya kuandaa ripoti ambavyo vimewekwa havijui , hivyo halmashauri inapata hati chafu, mwingine anapata hati safi na anayepata hati safi haina maana mambo yao ni mazuri kuliko aliyepata hati chafu."Lakini ina maana gani , hesabu zao hawajazifunga kwa utaratibu unaokubalika kimataifa".

Aidha amesema anashukuru kusikia kuna halmashauri ambazo zimeanza kuchukua hatua za kuwapeleka watu wao wa kuandaa ripoti kupata kozi za kuwaongezea ujuzi huku akieleza CAG anaweza kusaidia hao watu wakaelekezwa namna ya kufunga hesabu.
Mwakilishi Ofisi ya Msajili wa NGO's Charles Mpaka (kushoto) akikata utepe kwa pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya WAJIBU,Bwa. Ludovic Utouh (kulia) kuashiria uzinduzi wa ripoti za Uwajibikaji mwaka 2019-2020 jijini Dodoma,huku tukio hilo likishuhudiwa na Wadau wengine mbalimbali zikiwemo taasisi za Serikali, viongozi, Wabunge,Asasi za Kiraia na wanafunzi vyuo vikuu.
Mwakilishi Ofisi ya Msajili wa NGO's Charles Mpaka (kushoto) kwa pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya WAJIBU,Bwa. Ludovic Utouh (kulia) wakiangalia vitabu vya ripoti hizo namna ya kuwagawia Wadau mbalimbali walioshiriki kwenye uzinduzi wa ripoti za Uwajibikaji mwaka 2019-2020 jijini Dodoma.

WADAU mbalimbali kutoka taasisi za Serikali, Wabunge ,Asasi za Kiraia na wanafunzi vyuo vikuu ambao wameshuhudia uzinduzi wa Ripoti hizo,wakipitia kwamakini Ripoti hiyo mara baada ya kuzinduliwa rasmi jijini Dodoma.
Picha ya pamoja mara baada ya uzinduzi wa ripoti hiyo
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya WAJIBU,Bwa. Ludovic Utouh akizungumza jambo mbele ya Wadau mara baada ya ripoti hiyo kuzinduliwa
Share:

Capacity Development Specialist at UONGOZI Institute

About us UONGOZI Institute was established in 2010 by the Government of Tanzania to inspire and equip Tanzanian and African leaders to deliver inclusive and sustainable solutions. This is done through the provision of high-quality executive education programmes, facilitation of policy dialogues, action-oriented research and technical assistance for public institutions. The Institute is currently seeking […]

This post Capacity Development Specialist at UONGOZI Institute has been posted by Udahiliportaldaily

Get more post by visiting Udahiliportal.com

know more details about Udahiliportal.com by visiting Udahiliportal.com - Find Jobs & Ajira mpya leo, ajira portal Tanzania, ajira yako, brighter Monday, mabumbe, mwananchi ajira, secretariet ya ajira, tamisemi ajira za afya, wizara ya afya, ajira Tanzania - selection za vyuo , selection, second selection vyuo, second selection, tamisemi selection, selection form one 2020/2021

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger