Thursday 29 April 2021

Transport Officer at UNICEF /UN Volunteer

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Eligibility criteriaMinimum age: 25 years old. Nationals of the country of assignment are not eligible, except the assignments in Headquarters duty stations. Description of taskUnder the direct supervision of the Administrative Officer the UN Volunteer will undertake the following tasks: Support management of a team of drivers and a mechanic to offer quality transport services […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Chief Transformation Officer at ADD International

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

ADD International is a disability rights organisation with 35 years of experience. We fight for independence, equality and opportunity for disabled people living in poverty in Africa and Asia. We are looking for a Chief Transformation Officer to lead us for 9 months through a time of re-imagination and change. Someone with leadership experience and intrapreneurial drive to […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO ALHAMISI APRILI 29,2021



 






Share:

DKT. EGBERT MKOKO AWA MTANZANIA WA KWANZA KUPATA PHD KATIKA UANDISHI WA HABARI


Mwandishi wa Habari na Mhadhiri wa chuo Kikuu cha Dar es Salaam Egbert Mkoko, leo ametunukiwa shahada ya udaktari wa falsafa katika uandishi wa habari (PhD in Journalism and Media Studies) katika Chuo Kikuu cha Nelson Mandela mjini Port Elizabeth, Afrika Kusini.

Dr. Mkoko anakuwa ni mtanzania wa Kwanza kupata PHD katika Uandishi wa habari.
Share:

Wednesday 28 April 2021

Wabunge wataka wazee wa mabaraza kuongezewa posho


Wabunge  wameishauri Serikali kurejea upya viwango vya posho za wazee wa mabaraza ya Sh5,000 kwa kesi wakidai ni fedha kidogo.

Mwenyekiti wa kamati ya Bunge ya Bajeti, Sillo  Baran ameyasema hayo leo Jumatano Aprili 28, 2021 wakati akiwasilisha maoni ya kamati hiyo kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya mfuko wa mahakama kwa mwaka wa fedha 2021/2022.

Amesema kamati inaendelea kuishauri Serikali kuhusu kurejewa upya kwa viwango vya posho za wazee wa mabaraza ambao wanalipwa Sh5,000 tu kwa kesi kiasi ambacho ni kidogo  ikizingatiwa muda unaochukua kesi kuamuliwa.

“Hatua hii itasaidia kuziba mianya ya rushwa lakini pia itaongeza motisha, tija na ufanisi katika kazi za mabaraza husika,” amesema.



Share:

WEZI WAIBA KENGELE YA KANISA YENYE KILO 500

Watu wasiojulikana wameripotiwa kuiba kengele ya kanisa la Virgin Mary Orthodox lililoko eneo la Limuru kaunti ya Kiambu nchini Kenya ambapo tayari maafisa wa polisi wanaendelea na uchunguzi kuhusu tukio hilo. 

Kulingana na Katibu wa kanisa la Virgin Mary Ordhodox  James Warari alisema genge la wezi lilivamia kanisa hilo Alhamisi, Aprili 22,2021 na kuiba kengele hiyo ambayo inasemekana kuwa na uzito wa kilogramu 500. 

"Kisa hicho kilitokea Alhamisi Usiku, tuliamka asubuhi na tukagundua kwamba kengele hiyo haikuwepo. Mtu mmoja hawezi akabeba kengele hiyo kwa sababu ni nzito sana. Tunajua kulikuwa na watu kadhaa walishirikiana kubeba," Warari alisema. 

Warari alisema kengele hiyo ilikuwa imetengenezwa na shaba na ilikuwa ikitumiwa kuwakumbusha waumini saa za kuomba na pia kupanga ratiba ya kanisa hiyo.

Inasemekana kengele hiyo ilinunuliwa kutoka ng'ambo na Warari amemrai Mkenya yeyote ambaye atataka kuuziwa asiinunue bali awasiliane na wasimamizi wa kanisa hiyo.

 "Tungependa mtu yeyote ambaye ataiona kengele hiyo awasiliane nasi, nisingependa inunuliwe na mtu yeyote, naomba ipelekwe afisi yoyote ya chifu ilioko eneo la Limuru, kengele hiyo ulinunuliwa ng'ambo na hatuwezi ipata nyingine kama hiyo hapa Kenya," Wariru alisema.


Share:

TANLAP YATOA MAFUNZO YA SHERIA NA KANUNI ZA TAALUMA YA HABARI KWA WAANDISHI WA HABARI MWANZA


Mkurugenzi wa TANLAP, Christina Kamili akitoa neno la ufunguzi kwenye mafunzo hayo.
***
Mtandao wa Mashirika yanayotoa Huduma ya Msaada wa Kisheria Tanzania (TANLAP) umetoa mafunzo kwa waandishi wa Habari Mkoa Mwanza kuhusiana na Sheria na Kanuni zinazosimamia taaluma ya Habari ikiwemo Sheria ya Huduma za Habari, Sheria ya Haki ya kupata Taarifa pamoja na Sheria ya Makosa ya Mtandao.

Mkurugenzi wa TANLAP, Christina Kamili amesema mafunzo hayo yaliyofanyika Aprili 28, 2021 jijini Mwanza yanalenga kuwajengea uelewa waandishi wa habari kutambua Sheria hizo na changamoto zake hatua itakayowasaidia kutimiza majukumu yao kwa weledi.

Alisema kupitia mafunzo hayo, pia waandishi wa habari watatambua wajibu wao wa kuibua migogoro na changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi ikiwemo masuala ya mirathi ambao pia wanahitaji msaada wa kisheria.

“TANLAP kwa kushirikiana na wadau wengine tunasaidia wananchi kupata msaada wa kisheria bure hivyo kupitia mafunzo haya mtasaidia kuwaelimisha ili watambue taasisi zinazoweza kuwasaidia kupata haki zao mahakamani badala ya kujiwakilisha wenyewe kwa kukosa msaada” alieleza Kamili.

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari Mkoa Mwanza (MPC), Edwin Soko alisema mafunzo hayo yatawasaidia waandishi wa habari kutimiza wajibu wao kwa kuzingatia weledi bila kuingia kwenye mvutano na Sheria zilizopo.

Kwa upande wake Mwezeshaji wa mafunzo hayo, Wakili James Marenga alisema waandishi wa habari wanapaswa kuhakikisha hawaingii kwenye mgogoro na Sheria zinazoongoza taaluma yao na kuwahimiza kuzingatia sheria hizo ikiwemo Sheria ya Huduma za Habari inayowataka kuwa na taaluma ya habari angalau kuanzia Stashahada.

Mafunzo hayo yametolewa na TANLAP kwa kushirikiana na Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) ikiwa ni sehemu ya kuelekea kwenye Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari yatakayofanyika Mei 03, 2021 yakiwa na kauli mbiu isemayo “Habari kwa Manufaa ya Umma”.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mkurugenzi wa TANLAP, Christina Kamili akifungua mafunzo hayo ambapo amesisitiza waandishi wa habari kuwaelimisha wananchi kutambua taasisi zinazotoa huduma ya msaada wa kisheria ili ziwasaidia kuoata haki.
Mkurugenzi wa TANLAP, Christina Kamili amesema Sheria ya Huduma ya Msaada wa Kisheria inataka makundi mbalimbali ya wananchi ikiwemo wenye ulemavu, wanawake na watoto kupata msaada wa kisheria bure kutokana na changamoto mbalimbali zinazowakabili.
Baadhi ya waandishi wa habari (kushoto) awakimsikiliza Mkurugenzi wa TANLAP, Christina Kamili wakati akifungua mafunzo hayo.
Mafunzo hayo yamefanyika Monarch Hotel jijini Mwanza.
Meneja Programu TANLAP, Mchereli Machumbana akieleza umuhimu wa mafunzo hayo kwa Waandishi wa Habari.
Mwenyekiti wa MPC, Edwin Soko akizunguma wakati wa mafunzo hayo.
Wakili James Marenga akiwasilisha mada kwenye mafunzo hayo.
Washiriki wa mafunzo hayo wakifuatilia mada kutoka kwa Mwezeshaji, Wakili James Marenga.
Share:

LIS Database Systems Developer at THPS

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Tanzania Health Promotion Supports (THPS) is an indigenous NGO established under non- governmental organization act No 24 of 2002 in 2011. THPS works in partnership with the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children (MOHCDGEC), Regional Administration and Local Government (PORALG), Ministry of Home Affairs (MoHA) and Ministry of Health (MoH) in Zanzibar […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

MAFUNZO YA TBS KWA WADAU WA MCHELE YAMFURAHISHA DC NKUMBA

Share:

Project Accountant at THPS

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Tanzania Health Promotion Supports (THPS) is an indigenous NGO established under non- governmental organization act No 24 of 2002 in 2011. THPS works in partnership with the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children (MOHCDGEC), Regional Administration and Local Government (PORALG), Ministry of Home Affairs (MoHA) and Ministry of Health (MoH) in Zanzibar […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

LIS Data Analyst at THPS

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Tanzania Health Promotion Supports (THPS) is an indigenous NGO established under non- governmental organization act No 24 of 2002 in 2011. THPS works in partnership with the Ministry of Health, Community Development, Gender, Elderly and Children (MOHCDGEC), Regional Administration and Local Government (PORALG), Ministry of Home Affairs (MoHA) and Ministry of Health (MoH) in Zanzibar […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Rais Samia Suluhu Hassan Ahudhuria Kikao Cha Kamati Kuu Ya CCM Jijini Dodoma Leo


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan na wajumbe wengine wakiwa tayari kuanza kikao cha Kamati Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) kinachoongozwa na Makamu Mwenyekiti wa chama hicho (bara) Ndugu Philip Mangula akisaidiana na Makamu wa Mwenyekiti mwenza (Visiwani) Rais Mstaafu wa Zanzibar Ali Mohamed Shein katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre jijini Dodoma leo Jumatano Aprili 28, 2021.



PICHA NA IKULU




Share:

Officer, Procurement at Palladium

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

We are searching for an experienced Officer, Procurement at our Tanzania, United Republic of facility. Company Profile: Palladium is a global leader in the design, development and delivery of Positive Impact – the intentional creation of enduring social and economic value. We work with foundations, investors, governments, corporations, communities and civil society to formulate strategies […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Technical Director at Palladium

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Company Overview: Palladium develops and delivers innovative, locally relevant, evidence-based solutions to improve the health and well-being of people around the world. Since 1971, we have assisted governmental and non-governmental agencies, foundations, and the private sector by designing, implementing, and evaluating programs in HIV/AIDS, sexual and reproductive health, population and family planning, maternal and child […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Waziri Gwagima Apiga Marufuku Akina Mama Kuuziwa Kadi Za Kliniki


Na.WAMJW-Morogoro
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima   amepiga  marufuku utaratibu wa kuwauzia kadi za kliniki akina mama wajawazito pamoja na zile za watoto baada ya kuzaliwa wanapopelekwa kliniki za chanjo  kwani ni kinyume  na mwongozo wa serikali.

Dkt. Gwajima Aliyasema hayo jana mjini Morogoro alipokuwa akiongea na timu ya wataalamu wa afya halmashauri na mkoa huo kwenye kikao cha kujadili changamoto za afya ya uzazi, mama na mtoto.

"Nimekua nikipokea malalamiko mengi toka sehemu mbalimbali ya nchi kwamba mama mjamzito au mama akijifungua kadi ya kiliniki wanauziwa kutoka vituo vyetu vya kutolea huduma za afya, hii hapana". Alisema

Hata hivyo Waziri huyo alisema amebaini ni kweli kadi hizo zinauzwa Jambo ambalo siyo maelekezo ya serikali bali ni utaratibu binafsi wa  baadhi ya viongozi wa afya na watumishi wasio na mapenzi mema kwa serikali na wananchi.

Aidha, alisema kufanya hivyo ni kukosa  ubunifu na uwezo katika kukabiliana na changamoto za kawaida kabisa mahala pa kazi na hivyo kuwataka watumishi hao kutatua changamoto hiyo kwani gharama za kupata kadi hizo ziko ndani ya uwezo wa halmashauri kitu ambacho wanaweza kuondoa uhaba huo katika maeneo yao bila kusubiri .

Alizitaka pia  halmashauri zote nchini kuanzia leo kupata ufumbuzi wa ukosefu wa kadi hizo na asisikie tena malalamiko kutoka kwa akina mama wanaofika kliniki kwani Serikali haitaki kuwaona akina mama wajawazito na Watoto chini ya miaka mitano wanapata shida hizo.



Share:

Waajiri Zingatieni Masilahi Ya Watumishi Wa Umma


 Na. Veronica Mwafisi-Mtwara
Naibu Waziri, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Deogratius Ndejembi amewataka waajiri katika Taasisi za Umma kutoa kipaumbele kwenye masilahi ya watumishi, ikiwa ni pamoja kuwaasa Maafisa Utumishi kufanya ufuatiliaji ili kuwawezesha Watumishi wa Umma kupata stahili zao kwa wakati.   

Mheshimiwa Ndejembi ametoa wito huo kwa Waajiri na Maafisa Utumishi akiwa katika Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani, wakati wa ziara yake ya kikazi katika Manispaa hiyo.

Akitoa mfano wa uzembe wa Afisa Utumishi mmoja wa Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Mhe. Ndejembi amesema afisa huyo amesababisha watumishi wapatao 236 kutopata stahili ya kupandishwa madaraja kwa kisingizio cha kuchoka jambo ambalo halikubaliki katika Utumishi wa Umma.

Ameongeza kuwa, kitendo cha kutowapandisha madaraja watumishi hao kwa wakati kimewanyima haki yao ya msingi kwani katika Utumishi watalazimika kutengewa upya bajeti katika mwaka wa fedha mwingine ili waweze kupandishwa madaraja kwa mujibu wa sifa za miundo ya kada zao, ikiwa ni pamoja na kuzingatia uadilifu na utendaji kazi wao.

Sanjali na hilo, ameelezea kitendo cha waliokuwa Watumishi wa Umma katika Halimashuri ya Wilaya ya Kibaha ambao mpaka wanastaafu mwaka jana hawakupandishwa madaraja kwa wakati jambo ambalo limeathiri mafao yao.

Kutokana na changamoto ya watumishi hao kutopata stahili, Mhe. Ndejembi amesema Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan haitomvumilia mwajiri au Afisa Utumishi yeyote atakayesababisha Watumishi wa Umma kutopata masilahi au stahili zao kwa wakati.

“Tukibaini kuna Mwajiri au Afisa Utumishi yeyote anayezembea na kusababisha watumishi waliopo kwenye taasisi yake kukosa stahili zao kwa wakati, Serikali haitomvumilia kwani atakuwa anaharibu taswira nzuri ya ofisi yake ikiwa ni pamoja na taswira ya Mhe. Rais ambaye amehimiza Watumishi katika Taasisi zote za kupata stahili zao.

Kwa niaba ya Viongozi na Wakuu wa Idara waliopo katika Taasisi za Umma mkoani Mtwara, Mkuu wa Wilaya ya Masasi, Mhe. Seleman Mzee amemshukuru Mhe. Ndejembi kwa kuwahimiza kutekeleza majukumu yao kikamilifu hususani suala la uzingatiaji wa masilahi ya Watumishi wa Umma mkoani Mtwara.

Mhe. Mzee ameahidi kuyafanyia kazi maelekezo waliyowapewa na Mhe. Ndejembi mara watakaporudi kwenye vituo vyao vya kazi na kuongeza kuwa, watatoa kipaumbele kwenye suala la masilahi ya Watumishi wa Umma ili kuwajengea watumishi ari ya kutekeleza majukumu yao kikamilifu kwa lengo la kutoa huduma bora kwa umma.

Mhe. Ndejembi, amefanya ziara ya kikazi mkoani Mtwara kwa lengo la kuhimiza uwajibikaji kwa watumishi waliopo katika Taasisi za Umma mkoani humo.


Share:

Investments Impact Officer, Data Collection and Measurement at UN Volunteers /UNCDF

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Eligibility criteriaMinimum age: 35 years old, unless specified otherwise below. Applicants must be nationals of or legal residents in the country of assignment. Description of taskUnder the overall supervision of the Senior Investment Manager and day to day management of the LFI Global Manager based in Tanzania, the UNV member will support the practice investment […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger