Monday 29 March 2021
Waziri Mhagama aiogonza OSHA kukabidhi Tuzo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Mhe. Jenista Mhagama, kwa niaba ya serikali, kupitia Wakala wa Usalama na Afya Mahali pa Kazi (OSHA), ameikabidhi Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria Tuzo yenye lengo la kutambua mchango wa kamati hiyo katika kuboresha utendaji wa Wakala hiyo.
Waziri Mhagama ameikabidhi kamati hiyo tuzo leo tarehe 29 Machi, 2021 jijini Dodoma wakati kamati hiyo ilipokuwa ikipokea taarifa ya utekelezaji wa Wakala hiyo. Amebainisha kuwa ushauri wa kamati hiyo umeiwezesha wakala kuboresha Utendaji kwa kutengeneza mifumo ya kimtandao ya kurahisisha utendaji wa Wakala hiyo, Kupunguza tozo saba zilizokuwa kero kwa wadau wa OSHA pamoja kuongeza mapato ya Wakala hiyo.
“Mara nyingi tumezoea serikali kupewa tuzo kwa kufanya vizuri lakini tumekuwa tukisahau kuwa kuna baadhi ya walioisaidia serikali kufanya vizuri. Tumepima utekelezaji na utendaji wa OSHA katika kuzingatia ushauri wenu, tumeona kwa sasa hata gawio limeendelea kuongezeka linalotolewa na OSHA kwenye serikali, mifumo ya kimtandao imetengenezwa ya kurahisisha utendaji lakini pia tozo saba zimefutwa, hivyo hatunabudi kuwashukuru kwa mchango huo umeiboresha OSHA” Amesema Mhe. Mhagama.
Tozo saba ambazo OSHA tayari imezifuta kufuatia ushauri uliotolewa na Kamati hiyo ni; Tozo ya Usajili wa maeneo ya kazi, Tozo ya Fomu ya Usajili, Tozo ya ada ya leseni ya kukidhi matakwa ya sharia ya Usalama na Afya Mahali Pa kazi, Tozo ya Ushauri wa mambo Usala na Afya, Faini zinazohusiana na vifaa vya kuzimia moto, Tozo ya elimu kwa umma, Tozo ya Uchunguzi wa ajali ambayo imepunguzwa kutoka shilingi 500,000/= hadi shilingi 120,000/=.
Akiongeoa baada ya kupokea Tuzo hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, Mhe. Mohamed Mchengerwa amefafanua kuwa kamati hiyo imekuwa ikitoa ushauri kwa OSHA wa namna ya kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu pamoja na kuongeza kipato. Aidha, amebainisha kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu inayoirtaibu Wakala hiyo, imekuwa sikivu kwa kufuata ushauri wao wa kufuta tozo ambapo kwa kiasi kikubwa imekuwa ni faraja kwa watanzania na wawekezaji nchini.
Kikao hicho kimehudhuriwa na Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana na Ajira) Mhe. Patrobas Katambi, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu (Wenye Ulemavu) Mhe. Ummy Ngeriananga, Katibu Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Andrew Massawe, Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama na Afya Mahali Pa Kazi (OSHA), Bi. Khadija Mwenda, pamoja na baadhi ya Wakurugenzi wa OSHA.
OSHA ni Wakala wa serikali chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na wenye Ulemavu). Taasisi hii ina wajibu wa kuwalinda wafanyakazi dhidi ya vihatarishi vilivyopo katika sehemu za kazi ambavyo vinaweza kusabisha magonjwa na ajali. Wajibu huu unatekelzwa kupitia usimamizi wa Sheria Na. 5 ya Afya na Usalama Mahali pa Kazi ya mwaka 2003.
Mwaka 2001, ilianzishwa OSHA chini ya Sheria Na. 30 ya Wakala wa Serikali ya mwaka 1997 kama sehemu ya Mpango wa Maboresho katika utoaji wa Huduma za Serikali kwa wananchi. Makusudi ya kuanzishwa kwa OSHA ni kupata chombo cha serikali kwa ajili ya kusimamia Usalama na Afya mahali pa kazi.
OSHA ina jukumu la kuhakikisha kuwa wafanyakazi wanafanya kazi katika mazingira ambayo ni salama na yenye kulinda afya zao kwa kuzingatia taratibu zilizowekwa katika kuzuia ajali na magonjwa yatokanayo na kazi.
MWISHO.
KAMPUNI YA UDALALI YA YONO AUCTION MART YASEMA INA IMANI KUBWA NA RAIS SAMIA
MAMA WA MIAKA 50 NA WATOTO WATANO ARUDI SHULE KUSOMA SHULE YA MSINGI
Mwanae wa kiume kwa jina Chima Onwumere, ndiye alitangaza taarifa hiyo kupitia Facebook, huku akimsherehekea mama yake.
Chima alisimulia namna mama yake alimpigia simu mwaka 2020 kumfahamisha kuhusu hamu yake ya kutaka kurejea shuleni.
Huo ulikuwa wakati wa furaha kwake Chima huku mama yake akiamua kufuata ndoto yake aliyokuwa amewacha miaka mingi iliyopita.
Alifurahia kwamba hii itakuwa rekodi ya Justina huku mama huyo wa watano akisema ni mtu ambaye anapenda sana masomo.
"Mwaka jana nilipata simu kutoka kwa mama yangu akisema kuwa anataka kurejea shuleni kwa sababu alipoteza nafasi hiyo kutokana na ndoa ya mapema.
"Nilifurahia sana kama mpenzi wa masomo na umuhimu wake, nilimwamba nitaunga mkono uamuzi wake," aliandika mwanawe Justina.
Chanzo- Tuko News
BENKI YA CRDB YATOA ZAWADI KWA RPC MAGILIGIMBA, DC MBONEKO WANAWAKE MASHUJAA SHINYANGA
Head – Bancassurance at Exim Bank
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
Job Category : Management Job Code : 2021 Job Name : Head – Bancassurance Details :REPORTING TO:Head of RetailRESPONSIBLE FOR:Bancassurance Business Growth REGION: Dar es Salaam Overall Job Purpose Responsible for creating the overall business strategy and driving execution to achieve Targets, maximize revenue and profitability (both corporate and retail) from both internal and external customers Also, build a […]
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Assistant Manager – E-learning and HRIS at Exim Bank
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
Job Category : Management Job Code : 2021 Job Name : Assistant Manager – E-learning and HRIS Details :REPORTING TO:Manager – Training &Development PURPOSE OF THE POSITION To manage phases of e-learning and Human Resources Information System (HRIS)projects including designing, developing the online learning solutions. PRINCIPLE ACCOUNTABILITIES RESPONSIBILITIES Implement the bank’s eLearning strategy as agreed from time to […]
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Shamimu na mumewe kuhumiwa Jumatano
Mahakama Kuu kitengo cha Uhujumu Uchumi na Makosa ya Rushwa, maarufu kama Mahakama ya Mafisadi iliyopo Jijini Dar es Salaam, imepanga kutoa hukumu dhidi ya mfanyabiashara, Abdul Nsembo (45) maarufu kama Abdulkandida na mkewe, Shamim Mwasha (41) Jumatano Machi 31, Mwaka huu.
Hukumu hiyo itatolewa baada ya upande wa mashtaka na wa utetezi kumaliza kutoa ushahidi wao.
Upande wa mashtaka ulipeleka mashahidi sita na vielelezo 8 huku upande wa utetezi ukuwa na mashahidi watatu.
Shamimu ambaye ni mmiliki wa Blog ya 8020 na mumewe Nsembo, wanakabiliwa na mashtaka mawili ya kusafirisha dawa za kulevya aina ya heroini gramu 439.70, wanadaiwa kutenda tukio hilo Mei mosi 2019 huko Mbezi Beach jijini Dar es Salaam. Kesi hiyo inasikilizwa na Jaji Elinaza Luvanda.
Bibi wa Obama Afariki Dunia
Mama Sarah Obama ambaye ni bibi wa Rais wa zamani wa Marekani, Barack Obama, amefariki dunia, familia imethibitisha kutokea kwa kifo hicho.
Mama Sarah alikuwa akiugua kwa muda mrefu na amefariki wakati akipatiwa matibabu katika hospitali moja iliyopo katika Mji wa Kisumu nchini Kenya.
Marehemu alikuwa mke wa tatu wa Hussein Obama, amefariki akiwa na umri wa miaka 99 na anatarajiwa kuzikwa leo kwa mujibu wa taratibu na sheria ya dini ya kiislamu.
Obama ambaye ni mjukuu wa Mama Sarah aliwahi kuwa Rais wa 44 wa Marekani akiwa ni mwenye asili ya Afrika kutokea nchini Kenya.
MI & Analytics Manager at Exim Bank
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
Job Category : Management Job Code : 2021 Job Name : MI & Analytics Manager Details :REPORTING TO: Head Products & Revenue AssuranceRESPONSIBLE FOR: Retail MI and Analytic PURPOSE OF JOB The Manager MI & Analytic plays a crucial role in Business Performance and Planning, has the responsibility of providing daily accurate information on business direction, relevant management […]
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Assistant Manager: Retail Collections at Exim Bank
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
Job Category : Management Job Code : 2021 Job Name : Assistant Manager: Retail Collections Details :DEPARTMENT : Special Assets ManagementDIRECT REPORTING TO: Senior Manager: SAM & MIS DOTTED REPORTING LINE TO: Head of Special Assets Management HOURS OF WORK: 8am – 5pm; Monday to Friday. Additional hours as required by workload REGION: Dar es Salaam JOB PURPOSE: Assists in monitoring, impairment and […]
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Credit Admin Manager at Exim Bank
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
Job Category : Credit Job Code : 2021 Job Name : Credit Admin Manager Details :REPORTING TO: Head Products & Revenue AssuranceRESPONSIBLE FOR: Retail MI and Analytic PURPOSE OF JOB Administer the lending Portfolio by facilitating releasing of the credit facilities approved by the credit committee and to ensure the procedures are complied before disbursement. PRINCIPLE ACOUNTABILITIES RESPONSIBILITIES […]
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Manager – Credit Origination at Exim Bank
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
Job Category : Credit Job Code : 2021 Job Name : Manager – Credit Origination Details :REPORTING TO:Senior Manager – CreditRESPONSIBLE FOR:Credit Origination staff PURPOSE OF JOB Managing the origination and delivery processes of Credit Management. PRINCIPLE ACCOUNTABILITIES RESPONSIBILITIES: Assessing customers’ credit risks and credit worthiness and prepare overall assessment of existing and new business proposals. Planning, Budgeting […]
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Manager Card Issuing Credit and Debit cards – M2 at Exim Bank
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
Job Category : Management Job Code : Retail Job Name : Manager Card Issuing Credit and Debit cards – M2 Details : PURPOSE OF JOB To develop Manage the strategic development and operational functionality of the Bank’s debit and credit cards business in alignment with the Bank’s corporate objectives. Responsible for maintenance and growth of debit, prepaid and […]
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
ASSISTANT PROJECT MANAGER at Exim Bank
This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content
Job Category : Management Job Code : 2020 Job Name : ASSISTANT PROJECT MANAGER Self-driven and self-motivated individual Ability to work in a team and manage team dynamics Attentive to details Excellent communication skills Effective problem solving skills Conflict management Organizational skills Proficiency in Microsoft Office applications such as Word, Excel, Outlook, MS Project, PowerPoint etc. Master’s Degree […]
This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details
Serikali Kuendelea Kuzipatia Ufumbuzi Changamoto Za Muungano
Na Lulu Mussa
Serikali itaendelea kuzipatia ufumbuzi changamoto za Muungano kadiri zinavyojitokeza na kuhakikisha Hoja za Muungazo ambazo zimepatiwa ufumbuzi maazimio na makubaliano yake yanatekelezwa na pande zote mbili za Muungano.
Hayo yemesemwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Ummy Mwalimu wakati wa kuwasilisha Taarifa za Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2020/2021 na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa fedha 2021/2022 kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria.
Amesema kupitia vikao vya pamoja baina ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (SMT) na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) chini ya uenyekiti wa Mhe. Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania jumla ya hoja 25 zilisajiliwa na kati ya hizo hoja 15 zimepatiwa ufumbuzi, 10 ziko katika ngazi mbalimbali za maamuzi.
“Mhe. Mwenyekiti na Waheshimiwa Wabunge, changamoto za Muungano haziwezi kuisha azma ya Serikali zetu mbili ni kuhakikisha changamoto zinazojitokeza zinapatiwa ufumbuzi mapema kwa mustakabali endelevu wa Muungano wetu” Mhe. Ummy alisisitiza.
Waziri Ummy ameyataja mafanikio yaliyopatikana katika mwaka wa fedha wa 2020/2021 kuwa ni pamoja na Kuratibu Vikao vya Kamati ya Pamoja ya SMT na SMZ ya Kushughulikia Masuala ya Muungano ambapo kikao cha kusaini Hati Tano (5) za Makubaliano ya kuondoa kwenye orodha ya hoja za Muungano hoja zilizopatiwa ufumbuzi kilichofanyika tarehe tarehe 17 Oktoba, 2020 Jijini Dar es Salaam.
Aidha, katika kuratibu Masuala ya Kiuchumi na Kijamii jumla ya Taasisi kumi na mbili (12) zilitembelewa Tanzania Bara na Zanzibar kwa lengo la kufuatilia utekelezaji wa majukumu ya Taasisi za Muungano na Miradi ya Maendeleo inayotekelezwa pande mbili za Muungano; Kuratibu masuala yasiyo ya Muungano ili kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ambapo Vikao saba (7) vya Ushirikiano vilifanyika.
Amesema katika mwaka ujao wa fedha Ofisi yake itaweka mkazo katika kutatua changamoto za Muungano hususan masuala ya fedha, kuimarisha ushirikiano kwa taasisi zisizo za Muungano zenye sekta zinazoshabihiana na kutolea mfano sekta za Afya, Elimu na Mawasiliano.
Waziri Ummy amesema kuwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar zitaendelea kushirikiana katika kuibua miradi mbalimbali ya maendeleo ambayo hufadhiliwa na Washirika wa Maendeleo kwa manufaa ya wananchi wa pande mbili za Muungano. Miradi ambayo imewasaidia wananchi wa pande zote mbili za Muungano kushiriki na kuinua hali zao za kiuchumi pamoja na kuongeza ajira kupitia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Katiba na Sheria Mhe. Mohammed Mchengerwa ameishauri Serikali kuendelea kutoa elimu hususan kwa vijana waliozaliwa baada ya Muungano ikiwa ni pamoja na kuelezea fursa na faida za Muungano.