Monday 1 March 2021

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMATATU MACHI 1,2021



Magazetini leo Jumatatu March 1 2021





























Share:

Sunday 28 February 2021

Market Sales Manager at TalentintheCloud International

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Market Sales Manager   TalentintheCloud International Zanzibar West, Tanzania The continent’s most successful and fastest growing payments company is looking to add a talented and experienced Market Sales Manager to their team. Since identifying a gap in the African online payments landscape, they have rapidly led the online payments industry into centre stage – turning […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Medical Specialist II (Dermatologist) at Muhimbili National Hospital

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

  POST: MEDICAL SPECIALIST II (DERMATOLOGIST) – 1 POST POST CATEGORY(S) HEALTHCARE AND PHARMACEUTICAL EMPLOYER Muhimbili National Hospital APPLICATION TIMELINE: 2021-02-26 2021-03-11  DUTIES AND RESPONSIBILITIES   To provide routine specialized medical services for in-patients and out patients; To supervise ward rounds and advice on appropriate medication; To participate in the training of student doctors in their areas […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Tanzia : MFANYABIASHARA MAARUFU JIJINI ARUSHA AFARIKI DUNIA


Andrew Mollel enzi za uhai wake

Na Mussa Juma - Arusha
 Mfanyabiashara maarufu mkoani Arusha, Andrew Mollel ambaye alikuwa mwanzilishi na Mkurugenzi wa kampuni mbalimbali mkoani Arusha amefariki dunia na kuibua simanzi kwa wakazi wengi wa jiji hilo.

Akizungumza na Mwananchi leo, Februari 28, Mbunge wa jimbo la Monduli , Fredrick Lowassa amesema kifo cha Mollel ni pigo kubwa katika jiji la Arusha kutokana na mchango wake.

Lowassa amesema taratibu za mazishi wa Mollel zinaendelea kufanywa na wanafamilia lakini, kubwa ambalo Arusha watamkumbuka ni kuandaa michoro ya mradi mkubwa wa nyumba za PPF zilizopo eneo la Kijenge jijini hapa ambalo lilikuwa ni eneo lake.

Mollel alikuwa pia ni mkurugenzi wa kampuni ya Happy Sausages ,Kijenge Animal Products Limited, Georges Center Ltd na AGM Holding na pia mjumbe wa bodi mbalimbali hapa nchini.

Via Mwananchi
Share:

JOGOO ASHIKILIWA POLISI KWA KUUA MMILIKI WAKE


Mtu mmoja ameuawa na Jogoo wake aliyekuwa amefungwa kisu mguuni kwa ajili ya mchezo uliopigwa marufuku wa kupambanisha jogoo Kusini mwa India.

Mmiliki wa jogoo alichomwa kisu usawa wa kati ya tumbo na nyonga wakati kuku huyo akijaribu kutoroka. Mwanaume huyo alipoteza maisha akiwa njiani kuelekea hospitali kwasababu ya kupoteza damu nyingi.

Polisi hivi sasa wanawatafuta watu wengine 15 waliohusika kwenye tukio hilo, ambalo lilifanyika kwenye kijiji cha Lothunur jimbo la Telangana wiki hii.

Kuku huyo alishikiliwa katika kituo cha polisi kabla ya kupelekwa shambani.

Polisi wamesema mnyama huyo alikuwa akitayarishwa kwa ajili ya kushiriki mpambano alipojaribu kutoroka.

 Mmiliki alijaribu kumkamata lakini alichomwa na kisu hicho chenye urefu wa sentimita 7 kilichokuwa kimefungwa kwenye mguu wa kuku huyo wakati wa purukushani hizo.

Wale waliohusika katika tukio hilo wanakabiliwa na mashtaka ya mauaji ya kutokusudia, kujihusisha na mchezo haramu wa kamari na kuhodhi mchezo wa kupiganisha kuku, shirika la habari la Ufaransa limeripoti.

Afisa polisi katika eneo hilo B Jeevan amesema kuku huyo atapelekwa mahakamani kwa ajili ya ushahidi, kwa mujibu wa gazeti la The New Indian Express.

Mchezo wa kuwapambanisha jogoo ulipigwa marufuku India mwaka 1960, lakini mchezo huo bado ni maarufu vijijini kama Telangana wengi hasa katika matamasha ya jamii ya Hindu wa Sankranti.

Si mara ya kwanza kwa mmiliki wa kuku kuuawa na jogoo wake.

Mwaka jana mwanaume mmoja huko Andhra Pradesh aliaga dunia baada ya kukatwa shingoni na kiwembe kilichokuwa kimefungwa kwenye mguu wa jogoo.

Kwa mujibu wa Shirika la habari la CNN, mmiliki alikuwa akimchukua jogoo wake tayari kwa mpambano wa jogoo wakati tukio hilo lilipotokea.

CHANZO- BBC SWAHILI

Share:

AWESO ATOA SIKU SABA MKANDARASI KULIPWA DENI LAKE


Waziri wa Maji, Jumaa Aweso akipanda kwenye tanki la Mradi wa maji Lusilile, Manyoni kujiridhisha na viwango vya ujenzi wake.
Waziri wa Maji, Jumaa Aweso akikabidhi Mkataba kwa Jumuiya ya Watumiaji maji kwa mmoja wa wakazi wa kijiji cha Kashangu Itigi wilayani Manyoni. Wanaoshuhudia makabidhiano hayo ni Mbunge wa Manyoni Magharibi, Yahya Massare ( mwenye miwani) na Mkuu wa wilaya hiyo, Rahabu Mwagisa( kulia).


Na Abby Nkungu,  Manyoni

WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso amemwagiza Meneja wa Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) mkoa wa Singida kumlipa ndani ya siku saba Mkandarasi wa Kampuni ya CMG Construction takriban Sh milioni 700 anazodai kutokana na kujenga tanki la kuhifadhia na kusambaza maji Lusilile wilayani Manyoni lenye ujazo wa lita milioni mbili.

Waziri Aweso alilazimika kutoa agizo hilo baada ya Mbunge wa Manyoni Mashariki, Dk Pius Chaya kudai kuwa wananchi wake zaidi ya 50,000 katika vijiji 11 vilivyopo eneo hilo hawajaanza kunufaika na huduma ya maji ya mradi huo kutokana na Mkandarasi huyo kutolipwa deni lake.

"Lengo la mradi huu lilikuwa kupeleka maji kwenye Kituo cha Afya Kintinku na vijiji vilivyopo eneo hili lakini usambazaji wa maji unasuasua sana japo tanki lipo tayari." alisema Mbunge huyo na kuongeza;

Kituo hiki cha afya kinahudumia wananchi wa tarafa mbili; hivyo ni matamanio yangu huduma hii ya maji ifikishwe hapo mapema ili huduma nyingine za kiafya pia ziweze kufanyika ipasavyo".

Kutokana na hoja hiyo, Waziri Aweso alimuuliza Meneja RUWASA mkoa, Mhandisi Lucas Saidi iwapo ni kweli Mkandarasi huyo anaidai Serikali naye akathibitisha kuwa anadai takriban Sh milioni 700.

"Ndio maana mradi huu unasuasua. Hakikisha ndani ya siku saba Mkandarasi huyu awe amelipwa. Katoe Sh milioni 700 kwenye akaunti yenu umpe ili amalizie kazi wananchi waanze kupata huduma ya maji" aliagiza Waziri Aweso.

Akiwa kijiji cha Kashangu, Itigi Jimbo la Manyoni Magharibi, kwenye ziara yake ya kikazi ya siku moja mkoani Singida kukagua miradi mbalimbali ya maji, Waziri Aweso alielezwa kuwa jumla ya Sh milioni 150 ziliweza kuokolewa katika ujenzi wa mradi huo wa maji.

Meneja wa RUWASA wilaya ya Manyoni, Gabriel Ngongi alimweleza Waziri kuwa mradi huo ingawa ulitengewa jumla ya Sh milioni 350, lakini kwa kutumia wataalam wa ndani na mbinu nyingine mbadala, wameweza kutumia Sh milioni 200 tu; hivyo kuokoa Sh milioni 150.

Waziri Aweso aliipongeza hatua hiyo huku akiahidi kuwa Serikali haitakuwa kikwazo bali itatoa ushirikiano  wake wote kwa watumishi wanaojituma kama RUWASA Manyoni.

Aidha, alitoa mwito kwa wananchi wa eneo hilo na popote ilipo miradi ya aina hiyo Nchini kuitunza na kuilinda kwa nguvu zao zote kwa kuwa Serikali inatumia gharama kubwa katika kutekeleza miradi hiyo.  


Share:

Picha : ASKOFU MACHIMU AZINDUA WIMBO MAALUMU WA TANZANIA YA AMANI WA KWAYA YA DYNAMIC EAGT...AONGOZA MAOMBI DHIDI YA CORONA

Askofu wa Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akionesha DVD ya Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani kutoka Dynamic Choir EAGT Ushirika Shinyanga. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Tazama Video : Dynamic Choir EAGT Ushirika Shinyanga - Tanzania ya Amani

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Askofu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu amezindua Wimbo Maalumu wa Tanzania ya Amani kutoka Kwaya ya Dynamic ya kanisa la EAGT Ushirika Shinyanga.

Uzinduzi wa wimbo wa Tanzania ya Amani umefanyika leo Jumapili Februari 28,2021 katika kanisa hilo lililopo Ushirika Mjini Shinyanga ambapo pia Askofu Raphael Machimu ameongoza Maombi Maalumu kuombea Amani ya Tanzania pamoja na Kumuomba Mungu aliepushe Taifa na Ugonjwa wa Corona.

Akizindua na kuweka Wakfu CD/DVD ya Wimbo huo, Askofu Machimu amesema wimbo wa Tanzania ya Amani kutoka Dynamic Choir EAGT Ushirika Shinyanga umegusa viongozi wan chi kwa kazi wanayofanya katika kulinda amani ya nchi hivyo kuwaomba Wakisto na watu mbalimbali kununua CD ya wimbo huo ambao pia umewekwa katika Mtandao wa Youtube katika Chaneli ya Dynamic Choir EAGT Ushirika Shinyanga.

“Tunazindua CD hivyo tunapozindua CD hii ni muhimu tuombe kwa ajili ya Rais wetu Mpendwa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa sababu amekuwa kiongozi wa mfano katika kuimarisha amani ya nchi yetu”,amesema Askofu Machimu.

Askofu Machimu ameeleza kuwa Rais Magufuli ameonesha mfano mkubwa katika kusimamia imani na hasa katika kukabiliana na Ugonjwa hatari wa Corona na amekuwa mhamasishaji mkubwa kwa Watanzania kumtegemea Mungu ili aondoe na kutokomeza ugonjwa wa Corona.

Katika kumuombea Rais Magufuli na viongozi wengine wa kitaifa, Askofu Machimu pia amemuombea Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Zainab Telack, Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba na Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko kwa jinsi ambavyo amesimamia vyema mkoa wa Shinyanga ambao hapo awali ulikuwa unasifika kwa matukio mabaya ikiwemo mauaji ya vikongwe, watu wenye ualbino n.k

Aidha amesema wimbo wa Tanzania ya Amani ni wimbo mzuri akisema "Hii CD ya wimbo huu ukiwa nayo nyumbani utafurahi,waimbaji wamefanya kazi nzuri. Hii ni kazi takatifu kwa ajili ya kumpa heshima Mungu".

Mwenyekiti wa Kwaya ya Dynamic Daniel Chunga amesema lengo la wimbo huo maalumu wa picha walioupa jina la Tanzania ya Amani ni Kumshukuru Mungu kwa ajili ya kuilinda nchi ya Tanzania na kuliepusha taifa na majanga mbalimbali ikiwemo ugonjwa wa Corona.

“Kupitia wimbo huu tumezalisha nakala 150 zitakazouzwa leo na tutaweka wimbo huu katika Chaneli ya kwaya yetu Youtube”,amesema.

Kwa upande wake, Mgeni wakati wa uzinduzi huo, Mhandisi Edward Mollel amewapongeza wanakwaya kwa kutunga na kuimba wimbo wenye ujumbe mzuri huku akiwasisitiza waimbaji kuendelea kuwa wamoja, kushikamana na kushirikiana.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Waimbaji wa Kwaya ya Dynamic ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga wakiimba wakati wa uzinduzi wa Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo leo Jumapili Februari 28,2021 . Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog 
Waimbaji wa Kwaya ya Dynamic ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga wakiimba wakati wa uzinduzi wa Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo.
Waimbaji wa Kwaya ya Dynamic ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga wakiimba wakati wa uzinduzi wa Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo.
Askofu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akiweka Wakfu CD ya  Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo leo Jumapili Februari 28,2021 
Askofu wa Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akikata utepe kuzindua rasmi wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo leo Jumapili Februari 28,2021. Wa kwanza kushoto ni Mweka Hazina wa Kwaya ya Dynamic Veronica Shinyanga akifuatiwa na Mgeni rasmi Mhandisi Edward Mollel. Kulia ni Mwenyekiti wa kwaya ya Dynamic, Daniel Chunga.
Askofu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akifurahia baada kuzindua Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo leo Jumapili Februari 28,2021 
Askofu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akizungumza baada kuzindua Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo leo Jumapili Februari 28,2021 
Mweka hazina akifungua boksi maalumu lililobeba CD/DVD za wimbo wa Tanzania ya Amani baada ya Askofu wa Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu kuzindua Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo leo Jumapili Februari 28,2021 
Mweka Hazina wa Kwaya ya Dynamic Veronica na Mwenyekiti wa kwaya ya Dynamic, Daniel Chunga wakitoa CD/DVD kwenye boksi.
Askofu wa Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akiangalia CD/DVD ya Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani kutoka Dynamic Choir EAGT Ushirika Shinyanga.
Askofu wa Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akiangalia CD/DVD ya Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani kutoka Dynamic Choir EAGT Ushirika Shinyanga.
Askofu wa Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akionesha CD/DVD ya Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani kutoka Dynamic Choir EAGT Ushirika Shinyanga.
Askofu wa Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akionesha CD/DVD ya Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani kutoka Dynamic Choir EAGT Ushirika Shinyanga.


Muonekano wa DVD ya wimbo wa Tanzania ya Amani
Mgeni rasmi Mhandisi Edward Mollel akizungumza wakati wa uzinduzi wa Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani  
Mgeni rasmi Mhandisi Edward Mollel akionesha CD ya wimbo wa Tanzania ya Amani.
Waimbaji wa Kwaya ya Dynamic ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga wakiimba wakati wa uzinduzi wa Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo.
Awali MC Johnson Daniel akizungumza wakati Waimbaji wa Kwaya ya Dynamic ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga wakiimba kwenye uzinduzi wa Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo.
MC Johnson Daniel akizungumza wakati Waimbaji wa Kwaya ya Dynamic ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga wakiimba kwenye uzinduzi wa Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo.
Mwenyekiti wa Kwaya ya Dynamic Daniel Chunga akisoma risala kuhus Wimbo wa Tanzania ya Amani ambapo alisema lengo la wimbo huo maalumu wa picha ni Kumshukuru Mungu kwa ajili ya kuilinda nchi ya Tanzania na kuliepusha taifa na majanga mbalimbali ikiwemo ugonjwa wa Corona.
Askofu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akiongoza Maombi Maalumu kuombea Amani ya Tanzania pamoja na Kumuomba Mungu aliepushe Taifa na Ugonjwa wa Corona.
Askofu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akiongoza Maombi Maalumu kuombea Amani ya Tanzania pamoja na Kumuomba Mungu aliepushe Taifa na Ugonjwa wa Corona.
Askofu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akiongoza Maombi Maalumu kuombea Amani ya Tanzania pamoja na Kumuomba Mungu aliepushe Taifa na Ugonjwa wa Corona.
Maombi Maalumu kuombea Amani ya Tanzania pamoja na Kumuomba Mungu aliepushe Taifa na Ugonjwa wa Corona yakiendelea.
 Maombi Maalumu kuombea Amani ya Tanzania pamoja na Kumuomba Mungu aliepushe Taifa na Ugonjwa wa Corona yakiendelea.
Maombi Maalumu kuombea Amani ya Tanzania pamoja na Kumuomba Mungu aliepushe Taifa na Ugonjwa wa Corona yakiendelea.
Maombi Maalumu kuombea Amani ya Tanzania pamoja na Kumuomba Mungu aliepushe Taifa na Ugonjwa wa Corona yakiendelea.

Waumini wakiwa ndani ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga
Waumini wakiwa ndani ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga
Wageni waalikwa wakiwa ndani ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga
Wanakwaya wa Dynamic Choir EAGT Ushirika Shinyanga wakiwa ndani ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga
Waumini wakiwa ndani ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga.

Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger