Sunday 28 February 2021

Picha : ASKOFU MACHIMU AZINDUA WIMBO MAALUMU WA TANZANIA YA AMANI WA KWAYA YA DYNAMIC EAGT...AONGOZA MAOMBI DHIDI YA CORONA

Askofu wa Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akionesha DVD ya Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani kutoka Dynamic Choir EAGT Ushirika Shinyanga. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Tazama Video : Dynamic Choir EAGT Ushirika Shinyanga - Tanzania ya Amani

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Askofu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu amezindua Wimbo Maalumu wa Tanzania ya Amani kutoka Kwaya ya Dynamic ya kanisa la EAGT Ushirika Shinyanga.

Uzinduzi wa wimbo wa Tanzania ya Amani umefanyika leo Jumapili Februari 28,2021 katika kanisa hilo lililopo Ushirika Mjini Shinyanga ambapo pia Askofu Raphael Machimu ameongoza Maombi Maalumu kuombea Amani ya Tanzania pamoja na Kumuomba Mungu aliepushe Taifa na Ugonjwa wa Corona.

Akizindua na kuweka Wakfu CD/DVD ya Wimbo huo, Askofu Machimu amesema wimbo wa Tanzania ya Amani kutoka Dynamic Choir EAGT Ushirika Shinyanga umegusa viongozi wan chi kwa kazi wanayofanya katika kulinda amani ya nchi hivyo kuwaomba Wakisto na watu mbalimbali kununua CD ya wimbo huo ambao pia umewekwa katika Mtandao wa Youtube katika Chaneli ya Dynamic Choir EAGT Ushirika Shinyanga.

“Tunazindua CD hivyo tunapozindua CD hii ni muhimu tuombe kwa ajili ya Rais wetu Mpendwa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa sababu amekuwa kiongozi wa mfano katika kuimarisha amani ya nchi yetu”,amesema Askofu Machimu.

Askofu Machimu ameeleza kuwa Rais Magufuli ameonesha mfano mkubwa katika kusimamia imani na hasa katika kukabiliana na Ugonjwa hatari wa Corona na amekuwa mhamasishaji mkubwa kwa Watanzania kumtegemea Mungu ili aondoe na kutokomeza ugonjwa wa Corona.

Katika kumuombea Rais Magufuli na viongozi wengine wa kitaifa, Askofu Machimu pia amemuombea Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mhe. Zainab Telack, Kamanda wa Polisi mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba na Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Jasinta Mboneko kwa jinsi ambavyo amesimamia vyema mkoa wa Shinyanga ambao hapo awali ulikuwa unasifika kwa matukio mabaya ikiwemo mauaji ya vikongwe, watu wenye ualbino n.k

Aidha amesema wimbo wa Tanzania ya Amani ni wimbo mzuri akisema "Hii CD ya wimbo huu ukiwa nayo nyumbani utafurahi,waimbaji wamefanya kazi nzuri. Hii ni kazi takatifu kwa ajili ya kumpa heshima Mungu".

Mwenyekiti wa Kwaya ya Dynamic Daniel Chunga amesema lengo la wimbo huo maalumu wa picha walioupa jina la Tanzania ya Amani ni Kumshukuru Mungu kwa ajili ya kuilinda nchi ya Tanzania na kuliepusha taifa na majanga mbalimbali ikiwemo ugonjwa wa Corona.

“Kupitia wimbo huu tumezalisha nakala 150 zitakazouzwa leo na tutaweka wimbo huu katika Chaneli ya kwaya yetu Youtube”,amesema.

Kwa upande wake, Mgeni wakati wa uzinduzi huo, Mhandisi Edward Mollel amewapongeza wanakwaya kwa kutunga na kuimba wimbo wenye ujumbe mzuri huku akiwasisitiza waimbaji kuendelea kuwa wamoja, kushikamana na kushirikiana.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Waimbaji wa Kwaya ya Dynamic ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga wakiimba wakati wa uzinduzi wa Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo leo Jumapili Februari 28,2021 . Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog 
Waimbaji wa Kwaya ya Dynamic ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga wakiimba wakati wa uzinduzi wa Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo.
Waimbaji wa Kwaya ya Dynamic ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga wakiimba wakati wa uzinduzi wa Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo.
Askofu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akiweka Wakfu CD ya  Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo leo Jumapili Februari 28,2021 
Askofu wa Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akikata utepe kuzindua rasmi wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo leo Jumapili Februari 28,2021. Wa kwanza kushoto ni Mweka Hazina wa Kwaya ya Dynamic Veronica Shinyanga akifuatiwa na Mgeni rasmi Mhandisi Edward Mollel. Kulia ni Mwenyekiti wa kwaya ya Dynamic, Daniel Chunga.
Askofu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akifurahia baada kuzindua Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo leo Jumapili Februari 28,2021 
Askofu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akizungumza baada kuzindua Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo leo Jumapili Februari 28,2021 
Mweka hazina akifungua boksi maalumu lililobeba CD/DVD za wimbo wa Tanzania ya Amani baada ya Askofu wa Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu kuzindua Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo leo Jumapili Februari 28,2021 
Mweka Hazina wa Kwaya ya Dynamic Veronica na Mwenyekiti wa kwaya ya Dynamic, Daniel Chunga wakitoa CD/DVD kwenye boksi.
Askofu wa Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akiangalia CD/DVD ya Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani kutoka Dynamic Choir EAGT Ushirika Shinyanga.
Askofu wa Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akiangalia CD/DVD ya Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani kutoka Dynamic Choir EAGT Ushirika Shinyanga.
Askofu wa Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akionesha CD/DVD ya Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani kutoka Dynamic Choir EAGT Ushirika Shinyanga.
Askofu wa Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akionesha CD/DVD ya Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani kutoka Dynamic Choir EAGT Ushirika Shinyanga.


Muonekano wa DVD ya wimbo wa Tanzania ya Amani
Mgeni rasmi Mhandisi Edward Mollel akizungumza wakati wa uzinduzi wa Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani  
Mgeni rasmi Mhandisi Edward Mollel akionesha CD ya wimbo wa Tanzania ya Amani.
Waimbaji wa Kwaya ya Dynamic ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga wakiimba wakati wa uzinduzi wa Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo.
Awali MC Johnson Daniel akizungumza wakati Waimbaji wa Kwaya ya Dynamic ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga wakiimba kwenye uzinduzi wa Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo.
MC Johnson Daniel akizungumza wakati Waimbaji wa Kwaya ya Dynamic ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga wakiimba kwenye uzinduzi wa Wimbo Maalumu wa Picha uliopewa jina la Tanzania ya Amani katika kanisa hilo.
Mwenyekiti wa Kwaya ya Dynamic Daniel Chunga akisoma risala kuhus Wimbo wa Tanzania ya Amani ambapo alisema lengo la wimbo huo maalumu wa picha ni Kumshukuru Mungu kwa ajili ya kuilinda nchi ya Tanzania na kuliepusha taifa na majanga mbalimbali ikiwemo ugonjwa wa Corona.
Askofu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akiongoza Maombi Maalumu kuombea Amani ya Tanzania pamoja na Kumuomba Mungu aliepushe Taifa na Ugonjwa wa Corona.
Askofu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akiongoza Maombi Maalumu kuombea Amani ya Tanzania pamoja na Kumuomba Mungu aliepushe Taifa na Ugonjwa wa Corona.
Askofu wa Kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu akiongoza Maombi Maalumu kuombea Amani ya Tanzania pamoja na Kumuomba Mungu aliepushe Taifa na Ugonjwa wa Corona.
Maombi Maalumu kuombea Amani ya Tanzania pamoja na Kumuomba Mungu aliepushe Taifa na Ugonjwa wa Corona yakiendelea.
 Maombi Maalumu kuombea Amani ya Tanzania pamoja na Kumuomba Mungu aliepushe Taifa na Ugonjwa wa Corona yakiendelea.
Maombi Maalumu kuombea Amani ya Tanzania pamoja na Kumuomba Mungu aliepushe Taifa na Ugonjwa wa Corona yakiendelea.
Maombi Maalumu kuombea Amani ya Tanzania pamoja na Kumuomba Mungu aliepushe Taifa na Ugonjwa wa Corona yakiendelea.

Waumini wakiwa ndani ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga
Waumini wakiwa ndani ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga
Wageni waalikwa wakiwa ndani ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga
Wanakwaya wa Dynamic Choir EAGT Ushirika Shinyanga wakiwa ndani ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga
Waumini wakiwa ndani ya Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga.

Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Share:

MKURUGENZI WA SHIRIKA LA AGRI THAMANI FOUNDATION MH NEEMA LUGANGIRA AONGOZA ZOEZI LA KUGAWA TAULO ZA KIKE WANAFUNZI 1,800 MANISPAA YA BUKOBA

 

MKURUGENZI wa Agri Thamani ambaye Pia ni Mbunge wa Viti Maalumu kupitia NGOs Mh Neema Lugangira akigawa taulo za kike kwa wanafunzi wa shule za Sekondari
WANAFUNZI wa kike wa shule za Sekondari wakifurahia kupokea mfuko wao uliojaa taulo za kike za kutosha mwaka mzima kwa kila mmoja
FUSO lililokuwa limejaa Taulo za kike za wanafunzi wa kike 1800 wa Bukoba Manispaa likiingia kwenye uwanja wa Kaitaba Bukoba mjini likitokea Dar es Salaam
Mabox ya Taulo za kike ambazo zote zilikuwa zimeandikwa Jina la Shule ya Sekondari kwa Idadi Kamili ya Wanafunzi wa Kike
Hivi ndivyo kila mwanafunzi wa kike alivyoondoka uwanja wa Kaitaba na Furaha



Mkurugenzi wa Agri Thamani; Mhe Neema Lugangiea (Mb.) ambae pia ni Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) kupitia Kundi la Asasi za Kiraia (NGOs) Mh.Neema Lugangira ametoa msaada wa taulo za kike kwa wanafunzi 1800 kutoka kwenye shule 16 za Manispaa ya Bukoba .

 

Ambapo kila mwanafunzi mmoja ataweza kutumia taulo alizopewa kwa kipindi cha mwaka mmoja katika zoezi ambalo iliyofanyika kwenye uwanja wa Kaitaba mjini Bukoba.

Kwa Manispaa ya Bukoba jumla ya packet 25,200 za Taulo za Kike ziligawiwa kwa Wanafunzi wa Kike 1,800 kutoka Sekondari 16 za Kata zote 14 za Manispaa ya Bukoba.


Akizungumza wakati wa ugawaji wa taulo hizo katika zoezi ambalo liliratibiwa na Idara ya Elimu Sekondari Bukoba Manispaa na Afisa Elimu Taaluma Sekondari alishiriki zoezi zima.

 

Mhe Neema Lugangira amesema ameamua kufanya hivyo ili kuwasaidia wanafunzi hao kuweza kujihifadhi na kuweza kuendelea na masomo yao wakati wa  kipindi cha hedhi.

 

Alisema wanafunzi ambao watanufaika na msaada huo ni kuanzia kidato cha kwanza hadi cha nne ambao kwa sasa wataondoka na adha ambayo walikuwa wakikumbana nao wakati wakiwe kwenye kipundi cha hedhi.

 

“Naamini msaada huo utakuwa na manufaa makubwa kwao kutokana na kwamba watatumia muda mwingi kusoma hata wakiwa kwenye kipindi chao cha hedhi kutokana na kuwa na taulo ambazo zitawasaidia” Alisema Mbunge huyo.

 

Akizungumzia kuhusu msaada huo wa Taulo za Kike, Afisa Elimu Sekondari Manispaa ya Bukoba Mjini Emanuele Ebeneza alimshukuru Mbunge Neema kwa msaada wake wa taulo za wasichana ambao utakuwa chachu ya kupunguza utoro shuleni.

 

Alisema kupitia msaada huo wanafunzi wengi watajua namna ya kujihifadhi na kupunguza utoro shuleni kwa sababu ya kutokujisikia vizuri kwenye kipindi cha hedhi.

 

“Niseme tu kwamba licha ya kutoa msaada huo lakini pia Mbunge Neema anafundisha wanafunzi juu ya hedhi salama,  anawaandaa kisaikolojia kupita kwenye kipindi cha hedhi na hivyo kuwaondolea hofu na anawapa elimu ya lishe bora inayowasaidia waepukane na changamoto ya upungufu wa damu (anemia) ”Alisema Afisa Elimu Sekondari Bukoba Manispaa. 

 

Afisa Elimu Sekondari huyo alisema kwamba pia Mbunge Neema Lugangira anawafundisha usafi hatua ambayo inasaidia kupunguza utoro ambao ungetokana na wanafunzi kushindwa kuhudhuria masomo wakati wa mzunguko wa hedhi.

 

“Kama unavyojua mzunguko wa wasichana unatokea kila mwezi mara moja na wakati mwengine wakishindwa kuhudhuria masomo hivyo alilolifanya ni kitu cha muhimu sana sana kwa maana ya wanasichana “Alisema Ndg Ebeneza

 

Mmoja wa wanafunzi hao Alisema kwamba changamoto kubwa ni kubwa pale pedi zinapokuwa zimekwisha wanashindwa kuishi kwa amani kabisa wakati wakiwa wanaendelea na masomo

 

Naye mwanafunzi mwengine amesema wanashukuru kwa msaada huo kutokana na kwamba wakati mwengine wamekuwa wakikosa shule kutokana na kutokuwa na taulo za kujihifadhi wakati wakiwa kwenye kipindi cha hedhi.

 

Hata hivyo Avitha Faustini ambaye ni mwanafunzi wa kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari  Hamugumbe alimshukuru Mbunge Neema kwa msaada huo ambao amewapatia ambao umekuwa ni faraja kubwa kwao na kuwaondolea changamoto walizokuwa wakikumbana nazo.

 

Alisema wamepata ujasiri wa kuendele na masomo kwani kabla ya kupata Taulo  hizo walikuwa wakitokewa na hali hiyo wanakuwa wanyonge na wakati mwengine hulazimika kurudi nyumbani na  kukosa masomo. Aliongezea kwamba sasa hivi hawana haja ya kuwaomba wazazi pesa ya kununua pedi.

Mwanafunzi mwingine alikiri kwamba wengi hawajawahi kuziona taulo za kike na alielezea njia ambazo wengi wao wanatumia ambazo kwakweli hata sisi tunashindwa kuziandika maana sio salama kabisa. Mwanafunzi huyu alionyesha furaha ya aina yake kuona kwamba wamekumbukwa na kuthaminiwa hata kama wao ni watoto wa kimaskini.

Mradi huo wa Taulo za Kike umeshawanufaisha  Watoto wa Kike katika mikoa ya Dodoma, Tabora, Pwani, Tanga, Kigoma, Mtwara na Kagera na mikoa inayofuata kwa awamu hii ya kwanza ni Ruvuma na Lindi

Mbunge Neema Lugangira alimalizia kwa kusema kwamba Jumla ya Wanafunzi wa Kike 5,500 nchini watakuwa wamenufika ifikapo mwezi Mei 2021 ambapo Taulo za Kike zote zimetengenezwa na Kiwanda cha Tanzania ambacho kinauzoefu wa zaidi ya miaka 40 kwenye eneo hili. 

 


Share:

NAIBU WAZIRI WA MAJI AAHIDI NEEMA YA MAJI KIJIJI CHA KAZENGA

Naibu Waziri wa Maji, Mhandisi. Maryprisca Mahundi (Mb) amewataka wananchi wa kijiji cha Kazenga wilaya ya Chato mkoani Geita kutunza miundombinu ya maji ili iwe endelevu kwa vizazi vijavyo. 

Ameongea hayo wakati akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kazenga  waliosimamisha msafara wake ili waweze kuishukuru serikali kwa kuwajali kwa kuwakarabatia miundombinu ya mradi wao wa maji ambao uliacha kutoa maji tangu mwaka 1988.

“Tunafahamu mlikuwa na mradi wa siku nyingi ambao muda mrefu ulikuwa hautoi maji lakini sasa mradi umefufuliwa na umeanza kutoa maji, tunafahamu vituo vitatu vimeanza kutoa maji na baadhi ya maeneo bado hawajaanza kupata huduma hiyo, Nataka kuwahakikishia hivi vituo ambavyo havijapatiwa huduma ya maji baada ya mwezi mmoja vitapata maji”, amesema Mhandisi Mahundi.
Share:

MBUNGE KEMBAKI :HATA TUKIVAA BARAKOA KAMA MUNGU HAYUPO PAMOJA NA SISI NI BURE


Aliyenyoosha mkono ni Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato mtaa wa Majengo wilayani Tarime akifanya maombi maalumu kumwombea Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini Michael Kembaki (aliyevaa tai nyekundu). Picha na Dinna Maningo
Aliyenyoosha mkono ni Mchungaji wa kanisa la Waadventista Wasabato mtaa wa Majengo wilayani Tarime akifanya maombi maalumu kumwombea Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini Michael Kembaki (aliyevaa tai nyekundu).
Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini Michael Kembakiakizungumza na waumini wa kanisa la Waadventista Wasabato mtaa wa Majengo wilayani Tarime 
Mbunge wa Jimbo la Tarime Mjini Michael Kembaki akizungumza na waumini wa kanisa la Waadventista Wasabato mtaa wa Majengo wilayani Tarime 
Walioketi mbele katikati ni Mbunge wa jimbo la Tarime Mjini Michael Kembaki, wa kwanza kulia ni katibu Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Tarime Marema Sollo na wa kwanza kushoto ni Diwani wa Kata ya Kenyamanyori Farida Joel wakiwa kwenye ibada katika kanisa la Waadventista Wasabato Nkende ambapo walishiriki pia katika harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa
Wa Kwanza kulia ni Mbunge wa jimbo la Tarime mjini Michael Kembaki,anayemfuatia ni Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji Tarime Thobias Ghati na wa tatu kulia ni Diwani wa Kata ya Turwa Chacha Marwa wakiwa kwenye ibada Kanisa la Waadventista Wasabato Majengo.

***
Na Dinna Maningo, Tarime
Mbunge wa Jimbo la Tarime mjini Michael kembaki amesema kuwa Mungu ndiye tumaini la Watanzania hata watu wakivaa barakoa kama Mungu hayupo pamoja nao ni kazi bure na kwamba ni vyema kuzidi kuombeana na kuliombea Taifa ili mwenyezi Mungu aepushe janga la Corona.

Kembaki aliyasema hayo wakati akichangia sh. milioni mbili ya ujenzi wa nyumba ya Mchungaji wa Kanisa la Waadventista Wasabato mtaa wa Majengo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa ahadi yake huku akiwa ameambatana na Katibu Mwenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Marema Sollo, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji Tarime ambaye pia ni Diwani wa kata ya Nyamisangura Thobias Ghati na Diwani wa kata ya Turwa Chacha Marwa.

Mbunge huyo aliwaomba waumini hao kuzidi kuliombea taifa dhidi ya janga la Corona ambalo limesababisha hofu kwa wananchi huku akiwapongeza waumini hao kwa kutovaa barakoa na kuweka tumaini lao kwa Mungu.

"Nawashukuru sana kwa jinsi mnavyoliombea taifa Mungu ndiye tumaini letu bwana asipoulinda mji yeye aulindaye akesha bure, hata tukivaa barakoa kama Mungu hayupo pamoja na sisi ni bure, nimefurahi sijaona muumini hata mmoja aliyevaa barakoa.

"Kuna kanisa nilienda nikakuta asilimia 80 wamevaa barakoa na mimi nilikuwa sina barakoa ilinipa hofu sana, Mungu ndiye tumaini letu tuzidi kuliombea taifa letu ili lipite kwa ushindi katika janga hili ,mungu aliyetuepusha na janga hili wakati ule ndiye huyo huyo atatuokoa na janga hili",alisema Kembaki.

Mzee wa Kanisa la Majengo Simon Andrea alimshukuru mbunge kwa kutekeleza ahadi na kusema kuwa mtaa wa Majengo hauna nyumba ya mchungaji hivyo fedha hizo zitasaidia kuanza kujenga msingi kwa kuwa tayari wameshanunua uwanja.

"Mbunge katimiza ahadi yake mungu ambariki kuna watu wanatoa ahadi lakini hawatimizi, Mchungaji wetu anaishi nyumba ya kupanga kwa fedha hizi zitatusaidia kwenye hatua ya ujenzi nikuombe tutakapokuomba tena msaada tusikie na tusaidie", alisema Andrea.

Baada ya Mbunge huyo kuzungumza na waumini mchungaji wa mtaa wa Majengo Kumba Kihiri alifanya maombi maalumu kwa mbunge huyo ili mwenyezi mungu amuongoze katika kazi zake za kuwatumikia wananchi na familia yake pamoja na kumpatia afya njema.

Wakati huo huo, Mbunge Kembaki amechangia milioni 2.5 katika harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa la Nkende ambapo mgeni rasmi katika harambee hiyo alikuwa mbunge wa viti maalumu Ghati Chomete aliyechangia sh.milioni mbili na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mara Samwel Keboye (Namba tatu) akichangia mifuko 50 ya saruji.

Baadhi ya viongozi wengine waliochangia fedha na saruji ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya mji Tarime ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Nkende Daniel Komote alichangia sh.500.000,Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Thobias Ghati alichangia 100,000 na Marema Sollo akichangia mifuko mitano ya Saruji.

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mara Samwel Keboye aliwapongeza wabunge hao Madiwani na wana CCM kwa kujitolea kusaidia shughuli za kanisa, aliwaomba kuendelea kusaidia makanisa na misikiti mbalimbali pale kunapohitajika msaada Kwani kwakufanya hivyo Mungu atabariki na akawakumbusha waumini kuliombea Taifa lililokumbwa na Janga la Corona.
Share:

SHIRIKA LA GCI LATOA ELIMU YA UKATILI DHIDI YA WANAWAKE NA WATOTO KWA WANAUME WANYWA KAHAWA SHINYANGA MJINI


Meneja Mradi wa Sauti ya Mwanamke na Mtoto wa Shirika la GCI, Victoria Emmanuel (kulia) akizungumza wakati akitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume wanaokunywa Kahawa katika eneo la Nguzo Nane Mjini Shinyanga.

Na Kadama Malunde – Malunde 1 blog
Shirika la Green Community Initiatives (GCI) linalojihusisha na utetezi wa Haki za Wanawake na Watoto, Vijana, Wazee, Watu wenye ulemavu naWanaoishi na Maambukizi ya Virusi vya Ukimwi limetoa elimu ya Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto kwa Wanaume wanaokunywa Kahawa katika Kijiwe cha Nguzo Nane Mjini Shinyanga.

Shirika hilo lenye makao yake makuu Mjlimetoa elimu ya Ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume wanaokunywa Kahawa Jumamosi Februari 27,2021 kuelekea Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani Machi 8,2021 na utekelezaji wa Mpango Kazi wa Taifa wa kutokomeza Ukatili dhidi ya wanawake na watoto (MTAKUWWA).

Meneja Mradi wa Sauti ya Mwanamke na Mtoto wa Shirika la GCI, Victoria Emmanuel alisema wanatoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume kwani ni kundi linalolaumiwa kutenda ukatili kwa watoto na wanawake na kwamba pia watayafikia makundi ya wanawake na mikusanyiko ya kijamii ili wananchi wahamasike kushiriki kutokomeza vitendo vya ukatili.

“Kuelekea Siku ya Wanawake Duniani ambayo huadhimishwa kila ifikapo Mwezi Machi 8 lakini pia sisi GCI kama miongoni mwa watekelezaji wa Mpango Mkakati wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto, tunaendelea kutoa elimu ya masuala ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto “,alieleza Victoria.

Alieleza kuwa shirika la GCI limeanzisha kampeni ya Sauti ya Mwanamke na Mtoto likitumia kauli mbiu ya 'Tokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto' kwa lengo la kuelimisha jamii kuhusu madhara yatokanayo na vitendo vya ukatili kwa wanawake na watoto mkoani Shinyanga ambao ni miongoni mwa mikoa vinara wa matukio ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.

Aliyataja matukio ya ukatili kuwa ni pamoja na ndoa za utotoni,mimba za utotoni,utekelezaji wa familia,malezi duni ya watoto, watoto kuchomwa moto,kunyimwa chakula,kubakwa,kulawitiwa,kutelekezwa,kuitwa majina mabaya na ukatili wa kiuchumi,vipigo kwa wanawake na watoto kutoka kwa watu wao wa karibu mfano mume,mjomba,baba n.k.

Wakichangia mada ya ‘Nani alaumiwe kuwa chanzo cha ukatili dhidi ya wanawake na watoto’, wanaume hao waliokuwa katika Kijiwe cha Kahawa cha bwana Athumani Ibrahim kilichopo Mkabala na Zahanati ya Miti Mirefu Nguzo Nane Mjini Shinyanga, wanaume hao walisema migogoro ndani ya familia ni chanzo kikubwa cha vitendo vya ukatili.

Deogratius Moya alisema kutoelewana ndani ya familia ni chanzo kikubwa cha vitendo vya ukatili hali inasababisha wanaume wasiopenda maneno maneno huamua kuchelewa kurudi nyumbani, kutelekeza familia na kuendelea na maisha mengine hali inayosababisha watoto kukosa haki za msingi.

“Malezi ni changamoto kubwa, mfumo wa kuiga maisha kwa wanawake na watoto umetuletea balaa. Wanakuwa na tamaa ya kuiga maisha ya watu wengine na kupenda vitu vidogo vidogo. Vitu vya rahisi rahisi vinasumbua watoto wetu matokeo yake wanaambulia kupewa mimba na kukatishwa masomo yao”,alisema.

“Ndoa ni chanzo kikubwa cha ukatili. Wanaoana tu hawafanyi uchunguzi ndiyo maana tunaona leo harusi kubwa lakini baada ya siku chache ndoa chalii au mwanaume anabadilika,anaanza kupiga mke wake au unashangaa tu amepata mke mdogo anatekeleza mke wa kwanza,watoto na mke wanaanza kuteseka”,aliongeza.

Katika hatua nyingine aliwatupia lawama wanawake watumishi wa umma na wafanyabiashara kuwa chanzo cha matukio ya ukatili dhidi ya watoto kutokana na kuwa na muda wa kukaa na watoto badala yake wanawaachia wafanyakazi wa ndani kuhudumia watoto.

Elisha Philipo alisema baadhi ya wanawake wanawatumikisha watoto kwa kuwapa kazi ya kuuza vitafunwa,chai na kuokota chupa/makopo ya maji nyakati za masomo.

Naye Alex Elias na Adam Hussein walisema kitendo cha kukurupuka kuoa au kuolewa ni tatizo jingine kwani wanaoana kutokana na tama za kimwili, bila kuchunguzana tabia kwa kina matokeo yake wakioana migogoro inaanza,ndoa inavunjika watoto wanakosa uelekeo na kujikuta wakifanyiwa ukatili.

Kwa upande wake, Stephen Wilson alisema Utandawazi ni janga jingine ambapo sasa wanawake wengine hawataki kuwaheshimu waume zao wakidai haki sawa ambapo wanaume wasiopenda ugomvi huamua kutelekeza familia.

"Utandawazi unachangia sana wanawake kujiona wapo juu zaidi ya wanaume, wanadai haki sawa kwa kila kitu hawataki kuulizwa na waume zao. Hizi ganji zinasababisha ukatili, mwanaume akiacha pesa za mahitaji nyumbani hayanunuliwi, akimuuliza mke wake kulikoni hujawanunulia chakula watoto wakati wakati pesa nimekuachia mwanamke anapanda juu,ukimpiga makofi anakimbilia polisi anaonewa. Ndiyo maana wanaume wasiopenda ujinga/ugomvi wanaamua kuendelea na maisha mengine wanaacha familia au kuongeza mke",alieleza. 

Adam Hussein alisema mavazi yasiyofaa kwa wanawake ‘yakionesha maumbo yao’ yanachochea vitendo vya ukatili wa kijinsia kwa kuwaingiza wanaume katika tamaa ya kimapenzi ,hakuna ndoa tena na matokeo yake kuwapa ujauzito na kutelekeza mimba na watoto.

Kwa upande wake, Shaban Martin aliiomba serikali kukataza mavazi yasiyofaa kwani sasa baadhi ya wanawake wanavaa mavazi yanayoonesha viungo vyao na kuchochea vitendo vya kingono huku Adam Hussein akisisitiza watoto wafundishwe maadili.

Wanaume hao pia waliomba serikali mkoani Shinyanga kuchukua hatua dhidi ya wanawake wanaofanya biashara ya ngono katika baadhi ya maeneo kwani inamomonyoa maadili.

Mwakilishi wa Dawati la Jinsia na Watoto kutoka Jeshi la Polisi wilaya ya Shinyanga, Bryson John aliwataka wazazi kuacha tabia ya kuwalaza watoto chumba kimoja na wageni kwani baadhi yao siyo wema wamekuwa wakiwafanyia vitendo vya ukatili ikiwemo kuwalawiti na kuwabaka.

Aidha aliwasihi wanandoa kupendana na kuhakikisha wanaepuka migogoro huku akiwasisitiza wanaume wanaofanyiwa ukatili watoe taarifa kwenye dawati la jinsia na watoto.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Meneja Mradi wa Sauti ya Mwanamke na Mtoto wa Shirika la GCI, Victoria Emmanuel akizungumza wakati akitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume wanaokunywa Kahawa katika Kijiwe cha Athumani Ibrahimu kilichopo mkabala na Zanahati ya Miti Mirefu Nguzo Nane Mjini Shinyanga Jumamosi Februari 27,2021. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Meneja Mradi wa Sauti ya Mwanamke na Mtoto wa Shirika la GCI, Victoria Emmanuel akizungumza wakati akitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume wanaokunywa Kahawa katika Kijiwe cha Athumani Ibrahimu kilichopo mkabala na Zanahati ya Miti Mirefu Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Muonekano wa kijiwe cha Kahawa cha bwana Athumani Ibrahim kilichopo Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Wanaume wakiwa katika Kijiwe cha Kahawa cha Athumani Ibrahim Nguzo Nane Mjini Shinyanga wakipata elimu ya madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Wanaume wakiwa katika Kijiwe cha Kahawa cha Athumani Ibrahim Nguzo Nane Mjini Shinyanga wakipata elimu ya madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto.
Meneja Mradi wa Sauti ya Mwanamke na Mtoto wa Shirika la GCI, Victoria Emmanuel (kulia) akitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume wanaokunywa Kahawa katika Kijiwe cha Athumani Ibrahimu Nguzo Nane Mjini Shinyanga. Katikati ni Mhasibu wa shirika la GCI Mongo akiwa na mfanyakazi mwenzake, Elizabeth Samson
Mhasibu wa Shirika la GCI, Victoria Emmanuel akitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume wanaokunywa Kahawa katika Kijiwe cha Athumani Ibrahimu kilichopo mkabala na Zanahati ya Miti Mirefu Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Mfanyakazi wa Shirika la GCI, Elizabeth Samsonakitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume wanaokunywa Kahawa katika Kijiwe cha Athumani Ibrahimu kilichopo mkabala na Zanahati ya Miti Mirefu Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Mwakilishi wa Dawati la Jinsia na Watoto wilaya ya Shinyanga, Bryson John akitoa elimu kuhusu ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume wanaokunywa Kahawa katika Kijiwe cha Athumani Ibrahimu Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Mwakilishi wa Dawati la Jinsia na Watoto wilaya ya Shinyanga, Bryson John akitoa elimu kuhusu ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume wanaokunywa Kahawa katika Kijiwe cha Athumani Ibrahimu Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Deogratius Moya akichangia hoja kuhusu vyanzo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto na nini kifanyike kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika jamii wakati Shirika la GCI lilikitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume katika Kijiwe cha Kahawa Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Alex Elias akichangia hoja kuhusu vyanzo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto na nini kifanyike kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika jamii wakati Shirika la GCI lilikitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume katika Kijiwe cha Kahawa Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Wadau wakiendelea kupata huduma ya kahawa na kusikiliza maoni kuhusu masuala ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto
Stephen Wilson akichangia hoja kuhusu vyanzo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto na nini kifanyike kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika jamii wakati Shirika la GCI lilikitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume katika Kijiwe cha Kahawa Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Shaban Martin akichangia hoja kuhusu vyanzo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto na nini kifanyike kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika jamii wakati Shirika la GCI lilikitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume katika Kijiwe cha Kahawa Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Elisha Philipo akichangia hoja kuhusu vyanzo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto na nini kifanyike kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika jamii wakati Shirika la GCI lilikitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume katika Kijiwe cha Kahawa Nguzo Nane Mjini Shinyanga
John George akichangia hoja kuhusu vyanzo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto na nini kifanyike kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika jamii wakati Shirika la GCI lilikitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume katika Kijiwe cha Kahawa Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Wadau wakiwa katika kijiwe cha Kahawa
Adam Hussein akichangia hoja kuhusu vyanzo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto na nini kifanyike kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto katika jamii wakati Shirika la GCI lilikitoa elimu kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto kwa wanaume katika Kijiwe cha Kahawa Nguzo Nane Mjini Shinyanga
Wadau wa kahawa wakifuatilia majadiliano yaliyokuwa yanaendelea kuhusu masuala ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto
Wafanyakazi wa Shirika la GCI wakifuatilia mjadala kuhusu masuala ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto
Huduma ya kahawa ikiendelea
Wadau wakiwa katika kijiwe cha Kahawa Nguzo nane Mjini Shinyanga
Mwakilishi wa Dawati la Jinsia na Watoto wilaya ya Shinyanga, Bryson John na wafanyakazi wa Shirika la GCI katika Kijiwe cha Kahawa cha Athumani Ibrahimu kilichopo Nguzo Nane Mjini Shinyanga.

Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Share:

NAIBU WAZIRI MARY PRISCA ATOA ONYO KWA MENEJA WA RUWASA CHATO

Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Mhandisi Maryprisca Mahundi (Mb) ametoa onyo kwa Meneja wa Wakala wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) Chato Mhandisi Andrew Kilembe kwa kushindwa kutatua kwa wakati kero ya ubovu wa mita za maji zilizowekwa katika mradi wa maji wa Imalabupina Inchwankima na kusababisha wananchi wa eneo hilo kukosa maji kwa siku kadhaa. 

Ametoa onyo hilo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi wakati akikagua mradi huo unahohudumia wakazi wa vijiji hivyo. 

Amesema wananchi wanakosa huduma ya maji kwa sababu ya viongozi kufanya kazi kwa mazoea na kushindwa kutatua kero zinazojitokeza kwa wakati. 

“Natoa onyo na naomba fuatilieni hilo tatizo linalosababisha wananchi wasipate maji kwa wakati maeneo mengine yanatoa maji, na hakikisheni hizo mita zinazosumbua zinabadilishwa haraka ili kuondoa kero hiyo na wananchi hawa wapate maji”, amesema Mhandisi Mahundi na kusisitiza kezo zote ikiwemo matatizo ya umeme yasisubiri viongozi.
 
Aidha, amempongeza Meneja huyo wa RUWASA Chato kwa kuamua kutumia shilingi milioni 311 kukarabati miundombinu ya mradi wa maji Kasenga ambao ulichakaa na kuacha kutoa maji kwa muda mrefu. 

Katika ziara yake ya kukagua miradi ya maji mkoani Geita Naibu Waziri alikagua pia mradi wa maji wa Katoro Buseresere ambao utekelezaji wake unaendele vizuri na mradi huo ukikamilika utahudumia wananchi 20,000 wa kata ya Buseresere, Katoro, Ludete na Nyamigota.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger