Monday 1 February 2021

Picha : EWURA YAENDESHA MAFUNZO KWA WAANDISHI WA HABARI KANDA YA ZIWA

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Godfrey Chibulunje (kulia) akizungumza kwenye mafunzo kuhusu EWURA kwa Waandishi wa Habari Kanda ya Ziwa.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) imeendesha mafunzo kwa Waandishi wa habari Kanda ya Ziwa kwa lengo la kuwafahamisha waandishi wa habari kuhusu kazi,wajibu na mafanikio ya EWURA katika udhibiti wa huduma za Nishati na Maji.

Mafunzo hayo ya siku moja yamefanyika leo Jumatatu Februari 1,2021 na kukutanisha waandishi wa habari kutoka Mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Mara, Geita na Simiyu katika ukumbi wa Gold Crest Jijini Mwanza ambapo wamepata fursa ya kufahamishwa kuhusu kuanzishwa kwa EWURA, sekta inazozitawala, muundo wake, mafanikio na changamoto zake.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Godfrey Chibulunje amesema EWURA itaendelea kutoa ushauri kwa serikali katika kuandaa sera,sheria na kanuni zitakazowezesha kukua kwa sekta za nishati na maji na kuendelea kusimamia watoaa huduma ili kuhakikisha huduma zinakuwa bora kwa manufaa ya taifa.

Aidha amesema EWURA imesaidia kuzuia mfumko wa bei, kuimarisha mamlaka za maji nchini na kukuza umeme binafsi na kwamba itaendelea kuzingatia misingi mikuu sita ya utawala bora katika maamuzi ya udhibiti ambayo ni weledi, uwajibikaji, utabirikaji, ushirikishaji, uwazi na kufuata sheria.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Godfrey Chibulunje akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Kanda ya Ziwa leo Jumatatu, Februari 1,2021. Kushoto ni Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano EWURA, Titus Kaguo. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Godfrey Chibulunje akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Kanda ya Ziwa leo Jumatatu, Februari 1,2021. Wa kwanza kushoto ni Meneja wa EWURA Kanda ya Ziwa, Geogre Mhia, katikati ni Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano EWURA, Titus Kaguo.
Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano EWURA, Titus Kaguo akizungumza wakati wa mafunzo kwa waandishi wa habari Kanda ya Ziwa. Wa kwanza kushoto ni Meneja wa EWURA Kanda ya Ziwa, Geogre Mhia. Wa kwanza kulia ni Mkurugenzi wa UTPC, Abubakar Karsan akifuatiwa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Godfrey Chibulunje.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Godfrey Chibulunje akiwasilisha mada kuhusu kuanzishwa kwa EWURA,sekta inazozitawala, muundo wake,mafanikio na changamoto zake.
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Godfrey Chibulunje akiwasilisha mada kuhusu kuanzishwa kwa EWURA,sekta inazozitawala, muundo wake,mafanikio na changamoto zake.
Meneja wa EWURA Kanda ya Ziwa, Geogre Mhia, katikati ni Meneja wa Mawasiliano na Uhusiano EWURA, Titus Kaguo akizungumza wakati wa mafunzo hayo.
Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa Habari  mkoa wa Mwanza, Edwin Soko akizungumza kwenye mafunzo hayo.
Waandishi wa habari Kanda ya Ziwa wakiwa ukumbini.
Waandishi wa habari kutoka Mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Mara, Geita na Simiyu wakiwa katika ukumbi wa Gold Crest Jijini Mwanza 
Waandishi wa habari kutoka Mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Mara, Geita na Simiyu wakiwa katika ukumbi wa Gold Crest Jijini Mwanza 
Waandishi wa habari kutoka Mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Mara, Geita na Simiyu wakiwa katika ukumbi wa Gold Crest Jijini Mwanza 
Waandishi wa habari kutoka Mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Mara, Geita na Simiyu wakiwa katika ukumbi wa Gold Crest Jijini Mwanza 
Waandishi wa habari kutoka Mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Mara, Geita na Simiyu wakiwa katika ukumbi wa Gold Crest Jijini Mwanza 

Waandishi wa habari kutoka Mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Mara, Geita na Simiyu wakiwa katika ukumbi wa Gold Crest Jijini Mwanza 
Waandishi wa habari kutoka Mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Mara, Geita na Simiyu wakiwa katika ukumbi wa Gold Crest Jijini Mwanza 
Waandishi wa habari kutoka Mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Mara, Geita na Simiyu wakiwa katika ukumbi wa Gold Crest Jijini Mwanza 
Waandishi wa habari kutoka Mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Mara, Geita na Simiyu wakiwa katika ukumbi wa Gold Crest Jijini Mwanza 
Waandishi wa habari kutoka Mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Mara, Geita na Simiyu wakiwa katika ukumbi wa Gold Crest Jijini Mwanza 
Waandishi wa habari kutoka Mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Mara, Geita na Simiyu wakiwa katika ukumbi wa Gold Crest Jijini Mwanza 
Waandishi wa habari kutoka Mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Mara, Geita na Simiyu wakiwa katika ukumbi wa Gold Crest Jijini Mwanza 
Waandishi wa habari kutoka Mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Mara, Geita na Simiyu wakiwa katika ukumbi wa Gold Crest Jijini Mwanza 
Waandishi wa habari kutoka Mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Mara, Geita na Simiyu wakiwa katika ukumbi wa Gold Crest Jijini Mwanza 
Waandishi wa habari kutoka Mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Mara, Geita na Simiyu wakiwa katika ukumbi wa Gold Crest Jijini Mwanza 

Waandishi wa habari kutoka Mikoa ya Shinyanga, Mwanza, Mara, Geita na Simiyu wakiwa katika ukumbi wa Gold Crest Jijini Mwanza 

Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Share:

Kaliua Waanza Kulinda Kisheria Eneo La Kihistoria La Makumbusho Ya Mtemi Milambo


NA TIGANYA VINCENT
HALMASHAURI ya Wilaya ya Kaliua imeanza mpango wa kuweka mawe ya utambuzi wa eneo la mipaka ya makumbusho ya Mtemi Milambo kwa ajili ya kulilinda kisheria ili lisiweze kuvamiwa na kupoteza histoaria yake.

Hatua hiyo inalengo la kuhakikisha kuwa eneo hilo lenye Historia kubwa hapa nchini linaendelea kuwa endelevu kwa ajili ya manufaa ya wakazi wa Kaliua na Taifa kwa ujumla.

Kauli hiyo imetolewa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa Halamashauri hiyo Jerry Mwaga wakati Baraza la Madiwani alipokuwa akijibu hoja ya Madiwani waliotaka maeneo yote ya vivuto vya Kihistoria na utalii kutunzwa kwa ajili ya kuongeza mapato ya ndani na Taifa  kwa ujumla

Alisema mbalimbali na eneo hilo wataendelea kuainisha maeneo yote ya kale na yenye vivutio kupitia vigezo vinavyotakiwa ili yaweze kutambuliwa na kulinda kisheria kwa lengo la kuwavutia watalii wa ndani na nje.

Diwani wa Kata ya Usimba Benjamin Masanja alishauri kuwa  maeneo ya kihistoria yaliyopo wilayani Kaliua yanatakiwa kuboreshwa na kuweka watu wanaoweza kuelezea kwa ufasaha historia ya eneo husika kwa ajili ya kuwavutia watu mbalimbali wanaofanya utafiti na wale watalii kuyatembelea.

Alisema  hatua hii itaiwezesha Halmashauri kupata mapato na baadhi ya wananchi kupata ajira ya kuongoza Watalii na watafiti watakaopenda kujifunza kuhusu utajiri wa historia ya mambo ya kale yaliyopo wilayani humo.

Naye Diwani wa Kata ya Kazaroho Haruna Kasele alishauri kuwa wakati umefika kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua ikaanza kuwekeza katika maeneo ya historia za kale ili kuvutia watalii wengi kutembelea maeneo husika.

Alisema hatua itawezesha Halmashauri hiyo kuongeza vyanzo vipya vya mapato ya ndani na kupata fedha kwa ajili ya kupeleka huduma za kuboresha maisha ya wananchi ikiwemo utoaji wa huduma za afya , elimu na zile za ugani.

Kasele alisema Halmashauri ikiwekeza fedha kuboresha  Makumbusho ya Mtemi Milambo, eneo la kunyongea watumwa ambalo lilikuwa maarufu kwa jina la  Iselamagazi na njia ya Wajerumani  ambayo inaanzia Ndorobo wilayani Urambo kupitia Kazaroho wilayani Kaliua wataongeza mapato ya ndani.

Mwisho


Share:

Watumishi HESLB Wapatiwa Mafunzo Ya Kuwajengea Uwezo


Na Mwandishi Wetu,HESLB,
MKURUGENZI Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), Abdul-Razaq Badru amesema taasisi hiyo itaendelea kuzingatia miongozo, sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma katika utoaji huduma wa zake kwa wateja.

Akizungumza wakati wa kufunga mafunzo elekezi ya kuwajengea uwezo watumishi wa HESLB jana (Jumapili Januari, 31 2021), Badru alisema HESLB ni miongoni mwa taasisi za umma zinazogusa maslahi ya makundi mbalimbali ya kijamii, hivyo inawajibika kuweka mikakati madhubuti ya kuhudumia wateja.

Badru alisema kwa kutambua umuhimu huo, Ofisi yake imeandaa miongozo mbalimbali kwa watumishi wake ili kuwajengea uwezo wa namna bora ya kuwahudumia wateja na kushughulikia malalamiko yanayojitokeza katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

“Mafunzo haya ni sehemu muhimu ya kutukumbusha wajibu wetu katika kuhuhudumia wateja, tukiwa kama taasisi ya serikali tumeendelea kuboresha utoaji wa huduma kwa wateja kwa kuzingatia miongozo ya utumishi wa umma ikiwemo kuandaa mkataba wa huduma kwa wateja na mwongozo wa kushughulikia malalamiko kwa wateja,” alisema Badru.

Aidha Badru alisema kupitia mada mbalimbali zilizowasilishwa katika mafunzo hayo, ni wakati muafaka kwa kila mtumishi wa HESLB kutafakari nafasi na wajibu alionao katika kutekeleza majukumu yake kwa mujibu wa miongozo ikiwemo umuhimu wa kuzingatia uadilifu sehemu za kazi.

“Tunamaliza mwezi Januari tukiwa katika mafunzo haya muhimu yanayotukumbusha utekelezaji wa majukumu yetu, tunapaswa kutimiza wajibu wetu kwa kuzingatia wajibu wa msingi wa kila mtumishi wa umma na kubwa zaidi ni uadilifu katika maeneo yetu ya kazi”, alisema Badru.

Awali, Mkurugenzi wa Fedha na Utawala wa HESLB, Neema Kuwite alisema kutokana na umuhimu wa mafunzo hayo, Ofisi yake inaandaa mpango wa mafunzo kwa watumishi kuhusu utekelezaji wa miongozo ya kuhudumia wateja mahali pa kazi kwa kupitia nyaraka mbalimbali ikiwemo mkataba wa huduma kwa mteja ulioanza kutekelezwa na HESLB.

“Kupitia mafunzo haya tumepokea ushauri, maoni na mapendekezo kutoka kwa watumishi kuhusu namna ya kuhudumia wateja wetu, tunaandaa mpango wa mafunzo kwa watumishi ili kuweza kuwajengea uwezo wa pamoja katika kuhudumia wateja wetu”, alisema Kuwite.

Mafunzo hayo ya siku mbili yalishirikikisha jumla ya watumishi 140 kutoka Ofisi ya Makao Makuu ya HESLB, Ofisi za Kanda ya Dodoma, Zanzibar, Mwanza, Mtwara, Arusha na Mbeya.

MWISHO


Share:

Accounts Finance Officer at CVPeople Tanzania

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

ACCOUNTS FINANCE OFFICER   Dar es Salaam , Tanzania Industry: Banking City: Dar es Salaam State/Province: Dar es Salaam Job Description   To ensure that the Finance departmental objectives are met, maximization of profit, maximization of LONG-TERM shareholder wealth and process internal and external payments. Preparing monthly management accounts and Monthly reporting pack for shareholders […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Crane Operator at Gas Entec Co. L.T.D

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

JOB OPPOETUNITY AT GAS ENTEC CO LTD   PROJECT TITLE: CONSTRUCTION OF 1200 PASSENGER FERRY SHIP DESIGNATION: Crane Operator (1 POST) PLACE OF WORK: MWANZA JOB SUMMARY: Responsible for Crane Operation and maintenance Inspecting equipment, structures, or materials to identify the cause of errors or other problems or defects. Servicing, repairing, adjusting, and testing machines. DUTIES & […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Logistics and Supply Chain – Talent Community at Kuehne+Nagel

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Logistics and Supply Chain – Talent Community   Kuehne+Nagel Dar es Salaam, Dar es Salaam, Tanzania Interested in working at Kuehne + Nagel? Then simply apply for this job and we will keep your profile in mind every time when we will have new vacancies. As the global market leader, Kuehne + Nagel has plenty […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger