Saturday 30 January 2021

AGIZO LA WAZIRI NDAKI LATEKELEZWA... WATATU MBARONI

Na. Edward Kondela

Jeshi la polisi Mkoa wa Arusha kwa kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi pamoja na vyombo vingine vya ulinzi na usalama tarehe 27.01.2021 limewakamata watuhumiwa watatu kwa tuhuma za wizi na utoroshaji wa mifugo maeneo ya mipakani.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa mwishoni mwa wiki na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Polisi Salum Hamduni amesema jeshi hilo limewakamata watuhumiwa hao katika tarafa ya Loliondo, Wilaya ya Ngorongoro mkoani humo kufuatia agizo alilolitoa Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki Jumatano iliyopita la kukamatwa kwa watuhumiwa 67 wa utoroshaji wa mifugo na mazao yake.

Kamanda Hamduni amesema kukamatwa kwa watuhumiwa hao watatu kunatokana na baada ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi kutangaza operesheni ya kudhibiti wizi na utororshaji wa mifugo maeneo ya mipakani ambapo zilipatikana taarifa za uwepo wa watu wanaojihusisha na wizi na utoroshaji wa mifugo katika Wilaya ya Ngorongoro.

Ameongeza kuwa upelelezi bado unaendelea kuhusiana na tukio hilo, mara utakapokamilika jalada litapelekwa Ofisi ya Taifa ya Mashtaka kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria.

Ametoa wito kwa wananchi kuepuka usumbufu kwa kuhakikisha wanafuata sheria za biashara ya usafirishaji wa mifugo kwani wasipofanya hivyo watakamatwa na kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Jumatano ya wiki iliyopita Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki akiwa katika ofisi za wizara hiyo zilizopo katika mji wa serikali Mtumba jijini Dodoma wakati akiwasilishiwa ripoti ya uchunguzi, kuhusu utoroshaji wa mifugo mipakani aliliagiza Jeshi la Polisi nchini Kikosi cha Kuzuia Wizi wa Mifugo kuwakamata mara moja watuhumiwa 67 wa utoroshaji wa mifugo na mazao yake kwenda nchi za jirani.

Katika ripoti ya uchunguzi, kuhusu utoroshaji wa mifugo mipakani, iliyowasilishwa na Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Polisi Julius Mjengi kwa Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki imeeleza kuwa kabla ya tarehe 7 Novemba, 2020, mifugo iliyokuwa inatoka kwenye minada ya awali ya Handeni na Kilindi kuelekea nchini Kenya kupitia mpaka wa Horohoro haikuwa inafuata taratibu za forodha kama shehena nyingine.

Aliongeza kuwa takwimu za daftari la mifugo katika mpaka wa Horohoro zinaonyesha idadi ya mifugo iliyopitishwa kuelekea nchini Kenya kwa kipindi cha miaka 17 kutoka mwaka 2003 hadi Novemba, 2020 ilikuwa ni ng’ombe 24,980 na Mbuzi na Kondoo 9,368 (sawa na wastani wa Ng’ombe 122 na Mbuzi/Kondoo 46 kwa mwezi).

Taarifa hiyo ilibainisha pia baada ya uchunguzi, ilionekana kuwa kati ya tarehe 7 Novemba, 2020 hadi tarehe 9 Desemba, 2020 (kipindi cha mwezi mmoja tu) jumla ya Ng’ombe 1,096 na Mbuzi na Kondoo 1,044 walipitishwa katika kituo cha Forodha kuelekea nchini Kenya, ambapo huo ni wastani wa idadi ya mifugo iliyopita mpakani ndani ya mwezi mmoja ukilinganisha na siku za nyuma.

Taarifa imebaini pia viashiria vya udanganyifu wa kurekodi idadi sahihi ya mifugo inayokaguliwa kwenda Kenya hususan katika mpaka wa Hororohoro – Tanga.

Mwisho.

Imetolewa: Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

Wizara ya Mifugo na Uvuvi

30.01.2021

Share:

WAZIRI JAFO ATANGAZA SIKU 7 ZA WATANZANIA KUPIGA NYUNGU KUCHUKUA TAHADHARI YA CORONA



Waziri wa Tamisemi, Seleman Jafo ametangaza kuanzia Februari mosi hadi 7, 2021 zitakuwa siku saba za kupiga nyungu kwa Watanzania ili kuchukua tahadhari ya ugonjwa wa corona.

Akizungumza mkoani Tabora leo Jumamosi Januari 30, 2021 katika ziara ya Rais John Magufuli, waziri huyo amesema wananchi wanatakiwa kuendelea na majukumu ya kujenga Taifa bila hofu sambamba na kuchukua tahadhari kwa kupiga nyungu akimaanisha kujifukiza.

"Hakuna Mtanzania atajifungia ndani kwa ajili ya hofu ya ugonjwa huu wote tutapiga nyungu kuanzia Februari moja mpaka saba baada ya hapo shughuli nyingine ziendelee kama kawaida,” amesema Waziri Jafo.

Amesema hakuna hofu ya kuacha kufanya shughuli za maendeleo na nyungu ni shughuli inayotakiwa kufanyika mara kwa mara.



Share:

Naibu Waziri Ummy- Watu Wenye Ulemavu Changamkieni Asilimia 2 Ya Mikopo Inayotolewa Na Serikali


Na: Mwandishi Wetu
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Watu wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga amewataka Watu wenye Ulemavu kuchangamkia fursa ya mikopo ya asilimia 2 inayotolewa na Halmashauri zilizopo nchini kupitia asilimia 10 ya mapato ya ndani ya halmashauri (4% Wanawake, 4% Vijana na Watu wenye Ulemavu 2%) ili waweze kuanzisha miradi mbalimbali itakayowainua kiuchumi.

Ameeleza hayo wakati wa ziara ya kikazi Mkoani Mara alipokutana na kufanya mazungumzo na Viongozi wa Mkoa huo pamoja na Viongozi wa vyama vya Watu Wenye Ulemavu katika Mkoa huo, Mheshimiwa Ummy alieleza kuwa watu wenye ulemavu wanatakiwa kuchangamkia fursa ya mikopo ambayo wanatengewa na serikali kwa kuwa mikopo hiyo haina riba ili ziwasaidie kuboresha Maisha yao kupitia miradi mbalimbali watakayoianzisha.

“Mkiwa kama viongozi wa Vyama vya Watu wenye Ulemavu hakikisheni mnahamasisha wenzenu kuanzisha vikundi ili muweze kuchangamkia fursa ya mikopo hii inayotolewa na serikali ili muweze kuanzisha shughuli zitakazo waletea maendeleo,” alieleza Ummy

“Nimefurahishwa kuona Mkoa wa Mara umekuwa mstari wa mbele katika kuwawezesha watu wenye ulemavu kupata mikopo hiyo, zaidi ya milioni 115,226,660 zimeweza kutolewa kwenye vikundi mbalimbali vya watu wenye ulemavu vilivyopo kwenye mkoa huu, ninawapongeza sana uongozi wa mkoa kwa jitihada hizo,” alisema Naibu Waziri Ummy

Alieleza kuwa, Serikali ina dhamira ya dhati na nia njema kwa Watu wenye Ulemavu hivyo ilitoa fursa ya mikopo hiyo ya asilimia 2 ili wenye ulemavu na wao waweze kupata fursa ya kufanya shughuli mbalimbali zitakazo wawezesha na wao kuchangia katika pato la taifa.

“Mnafahamu kuwa serikali yetu imeingia kwenye uchumi wa kati na dhamira ya serikali ni kukuza uchumi wake kupitia viwanda, hivyo ni vyema watu wenye ulemavu wakatumia fursa hiyo ya mikopo ya asilimia 2 inayotolewa na halmashauri ili na nyie muanzishe viwanda vidogo vidogo, uwezo huo mnao,”

“Mmemsikia Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli anataka nchi hii iwe na mabilionea wengi, kati ya hao mabilionea natamani kuona na watu wenye ulemavu mkiwemo uwezo huo natambua mnao kwa kuwa mnaweza kufanya mambo makubwa na yakawashangaza watu wengi kwamba watu wenye ulemavu wanaweza kama wengine wasio na ulemavu,” alisema Mheshimiwa Ummy

“Maafisa Ustawi wa Jamii hakikisheni mnawasaidia watu wenye ulemavu wanapokuja katika ofisi zenu na mawazo au maandiko ya kuanzisha biashara au miradi mbalimbali ya uzalishajimali ili waweze kupata mikopo ya asilimia 2 waliyotengewa,” alisema

Alifafanua kuwa, Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli imekuwa ikiwajali watu wenye ulemavu sambamba kuboresha huduma za msingi za kundi hilo, huku akielezea pia juu ya namna uzingatiwaji huo kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi katika Ibara ya 94, 95 na 96 ambazo zinaelezea na kufafanua mwelekeo wa namna masuala ya Watu wenye Ulemavu yatakavyokuwa yakishughulikiwa, kuendelea kutambua na kuwapatia kipaumbele katika masuala mbalimbali ya kimaendeleo.

Sambamba na hayo, Naibu Waziri Ummy alihimiza juu ya Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya kujumuisha masuala ya wenye ulemavu kwenye Mabaraza ya mashauriano ya Mkoa (Regional Consultative Councils) na Mabaraza ya Mashauriano ya Wilaya (District Consultative Councils) ili waweze kutambua mahitaji yao ikiwemo kuwapatia huduma bora, haki zao za msingi kwa lengo la kuimarisha ustawi wao, kuimarishwa kwa huduma za afya na zenye staha kwa watu wenye ulemavu wa kila aina, kuimarisha ulinzi, kuendelea kuwawezesha watu wenye ulemavu kiuchumi, kuwapatia elimu kwa kuimarisha elimu jumuishi, kujengwa kwa miundombinu fikivu na kuendelea kutoa elimu kwa jamii kuhusiana na masuala mbalimbali ya wenye ulemavu.

Aidha, Mheshimiwa Ummy amewataka pia Viongozi wa Vyama vya Watu wenye Ulemavu kuimarisha ushirikiano baina yao na viongozi wa mkoa kwa kuwa na upendo na amani ili waweze kujadiliana na kushauriana masuala mbalimbali yanayohusu Watu wenye Ulemavu.

Sambamba na hayo, Naibu Waziri Ummy alitoa wito kwa jamii kuacha kuwanyanyapaa na kuwaficha watu wenye ulemavu badala yake wawaibue na kuwaunganisha na fursa mbalimbali katika jamii.

Naye, Katibu Tawala wa Mkoa wa Mara Mhe. Karolina Mthapula alisema kuwa Mkoa wa Mara utaendelea kutoa hamasa kwa watu wenye ulemavu kujitokeza na kuchangamkia fursa mbalimbali zinazotolewa kwa ajili ya watu wenye ulemavu.  

Pia, alieleza uongozi wa Mkoa utaendelea kushirikiana na Viongozi wa Vyama vya Watu wenye Ulemavu katika mkoa huo pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama, mamlaka za serikali za mitaa kuhakikisha watu wasio waadilifu katika jamii na wenye nia ovu katika kuwatumia watu wenye ulemavu wanachukuliwa hatua za kisheria.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Shirikisho la Watu wenye Ulemavu Mkoa wa Mara, Ndg. Iddy Mtani alitumia fursa hiyo kuishukuru Serikali namna inavyowajali Watu wenye Ulemavu na alieleza kuwa vikao ambavyo amekuwa akifanya Naibu Waziri anayeshughulikia masuala ya watu wenye ulemavu vitaleta tija na kuongeza uelewa wa masuala ya watu wenye ulemavu hususan kwa jamii na viongozi katika kutambua namna watakavvyokuwa wakishirikiana kwa pamoja katika kuendesha gurudumu la maendeleo.

Katika Ziara hiyo Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Watu wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga alitembelea Shule ya Mingi Msingi ya Mwisenge iliyopo mkoani Mara kwa lengo kujionea mazingira na miundombinu fikivu iliyojengwa katika shule hiyo kwa ajili ya kuwawezesha watu wenye ulemavu kupata elimu bora. Aidha Shule hiyo ya Msingi ya Mwisenge ina historia kubwa katika kataifa ambapo Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerer alisoma katika shule hiyo.


Share:

Serikali Kuwachukulia Hatua Watumishi Wanaofanya Kazi Vituo Binafsi Katika Muda Wa Kazi


 Na WAMJW- Kilimanjaro
SERIKALI kupitia Wizara ya Afya Afya imeanza kufuatilia Watumishi walioajiriwa na Serikali wanaofanya kazi katika vituo vya kutolea huduma za Afya binafsi katika muda wanaotakiwa kuwa katika vituo vyao vya Serikali.

Hayo yamesemwa jana na Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Abel Makubi ambae pia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Hospitali za Watu Binafsi nchini wakati akiongea na Waandishi wa habari baada kikao na wajumbe wa Bodi hiyo ikiwani sehemu ya maboresho ya huduma za Afya nchini, Mkoani Kilimanjaro.

"Tumeanza kufuatilia Watumishi wa Umma wanaofanya kazi katika Hospitali binafsi muda wa kazi, mtumishi yeyote atakayethibitika kufanya hivyo atachukuliwa hatua kali pamoja na mmiliki wa kituo atakachokuwa akifanya kazi ndani ya muda wa kazi" amesema Prof. Makubi.

Aliendelea kusema kuwa, wamiliki wa Hospitali Binafsi wahakikishe kuwa wanazingatia na wanafuata Sheria, kanuni, miongozo na taratibu, za usajili wa vituo hivi ikiwemo watumishi wanaowasimamia.

Aidha, Prof. Makubi ameagiza Waganga Wakuu wa Mikoa, Wilaya, Wafawidhi wa Vituo na Waratibu kufanya ufuatiliaji wa karibu ili kuhakikisha kuwa vituo hivi vinafuata sheria za Utumishi wa Umma na za Hospitali Binafsi

Amesema, Waganga Wakuu wa Mikoa, Wilaya na Wafawidhi wa Vituo waweke na kusimamia mifumo ya kuhakikisha watumishi wa Umma wanakuwepo katika vituo vyao ndani ya saa za kazi.

Mbali na hayo amewaagiza Wamiliki wa vituo binafsi wahakikishe watumishi wa Umma hawafanyi kazi kwenye vituo vyao katika muda wa serikali, huku akisisitiza kuwa, yoyote atakayebainika kuvunja sheria atachukuliwa hatua kwa mujibu wa Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo.

Hata hivyo, amewakumbusha wamiliki wote wa vituo binafsi nchini kufanya kazi kwa kushirikiana na Bodi za usimamizi wa kutoa huduma za afya ili kuboresha huduma za bila kuvunja Sheria, kanuni, miongozo na taratibu zilizopo.



Share:

Kampuni Nane Za Tanzania Kuingiza Samaki Nchini Saudi Arabia



Share:

Rais wa Zanzibar Dr Mwinyi Aendelea kuwasisitiza viongozi aliowateua kwenda kuwasikiliza wananchi changamoto walizonazo.


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk. Hussein Ali Mwinyi ameendelea kuwasisitiza viongozi aliowateua kwenda kuwasikiliza wananchi changamoto walizonazo.


Alhaj Dk. Hussein Mwinyi ameyasema hayo jana wakati akitoa salamu zake kwa wananchi wa kijiji cha Nungwi mara baada ya kuungana nao katika sala ya Ijumaa huko katika Masjid Rahman iliyopo Nungwi, Wilaya ya Kaskazini A, Mkoa wa Kaskazini Unguja. 


Katika salamu zake hizo, Alhaj Dk. Mwinyi alisema kuwa kuna kila sababu kwa viongozi wake wakiwemo Wakuu wa Wilaya na Mikoa kwenda kuwasikiliza wananchi changamoto zao ili ziweze kupatiwa ufumbuzi. 


Alisema kuwa amegombea nafasi ya Urais kwa ajili ya kuwatumikia wananchi kwa kuwasikiliza matatizo yao, kero zao zikiwemo huduma za jamii kama vile afya, elimu, maji na nyenginezo ambapo hivi sasa amekuwa akifanya mikutano kadhaa na wadau wa sekta hizo kwa azma ya kutatua changamoto zilizopo.


Alisema kuwa changamoto hizo zinashughulikiwa na kusisitiza kwamba tayari alishawaambia wateule wake  wakati akiwaapisha kwamba washuke chini wakawashughulikie wananchi changamoto zao za ardhi, kuondoa dhulma na changamoto nyenginezo.


Aliwapa maagizo Mkuu wa Mkoa wa Kaskazini Unguja na Mkuu wa Wilaya Kaskazini A, wakutane na uongozi kwa ajili ya kusikiliza changamoto za wananchi wa kijiji cha Nungwi na kuwataka wakatatue na yale yaliyo chini ya uwezo wao wamjuulishe ili ayafanyie utatuzi.


Alisema kuwa ana dhima ya kuhakikisha ana tenda haki kwa wananchi wote bila ya kujali uwezo wao kifedha, itikadi zao za kisiasa kwani yeye ni Rais wa Zanzibar na ana wajibu wa kuwatumikia wananchi wote bila ya kujali matabaka, rangi, dini wala kabila.



Share:

Serikali kushirikiana na wadau kuikuza Bongo Fleva nchini


 Na Eleuteri Mangi-WHUSM, Dar es Salaam
Mashindano ya Bongo Star Search yamehitimishwa usiku wa kuamkia Januari 30, 2021 jijini Dar es Salaam ambapo Msanii wa muziki wa Kizazi kipya Yusuph Nizar ameibuka kidedea na kujinyakulia kitita cha Sh. Milioni 20 na kukabidhiwa mfano wa hundi yenye thamani ya fedha hizo.

Akizungumza mara baada ya kutaja majina ya mshindi wa kwanza hadi wa watatu katika mashindano hayo, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Innocent Bashungwa alisema Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wa Sanaa katika kuendeleza vipaji vya vijana hatua inayosaidia kuwaongezea kipato na kuboersha maisha yao.

“Dhamira na malengo ya Serikali ni kusaidia Bongo Fleva iwe fani kubwa ndani na nje ya nchi na kuwazidi mataifa mengine, ili tuweze kufanikiwa tunahitaji wasanii wetu kushirikiana kuanzia wasanii wakubwa waliopata mafanikio ambao wamekuwa walimu na makocha wazuri kwa kuwapa ushauri wasaniii wadogo waweze kufanikiwa” alisema Waziri Bashungwa.

Aidha, Waziri Bashungwa ameahidi kusaidiana na kushirikiana na wadau wote wa Sanaa hatua inayosaidia wasanii walioibuliwa katika Bongo Star Search ili wasanii wote waweze kufanikiwa zaidi na kuvuka kwa pamoja katika maisha yao.   

Waziri Bashungwa amesema kuwa Serikali itaendelea kushirikiana na wadau wote wa Sanaa na kuliagiza Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA), Chuo cha Sanaa na Utamaduni (TaSUBa) kushirikiana na mwendeshaji wa mashindano hayo Madam Ritha Polsen hatua itakayosaidia vijana hao kufanikiwa kimaisha kwa kunufaika na kazi zao za Sanaa huku akiahidi kushirikiana nao ili kuhakikisha wanafanikiwa.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Benchmark Production ambao ni waandaaji wa mashindano ya Bongo Star Search (BSS) Madam Madam Ritha Poulsen amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa kuthamini na kuipa kipaumbele sekta ya Sanaa nchini katika Serikali anayoiongoza.

Hatua hiyo imesaidia vijana na wadau wengine wa Sanaa kuendelea kufanya kazi zao za Sanaa wakiwemo waandaaji wa miswada, watenegenezaji wa kazi za Sanaa, wasanii wenyewe pamoja na taasisi zinazosimamia maslahi ya wasanii.

Mashindano BSS yalianza kwa kushirikisha vijana zaidi ya 200 kutoka mikoa yote nchini na kupekelea washindi watatu kupatikana ambapo Mshindi wa pili ni Zanael Kinyala kutoka Dar es salaam na mshindi wa tatu akiwa ni Petro Jairos kutoka Dodoma huku mwanamuziki kipenzi cha watazamaji na wasikilizaji wa mashindano hayo kupitia kisimbusi cha Star Times akiwa ni Alfredy Ally ambaye amezawadiwa runinga yenye ukubwa wa inchi 55 kutoka kampuni ya Star Times kwa matumizi yake
binafsi.

Share:

Majaliwa: Viongozi Wa Sekta Ya Umma Na Binafsi Waendelezwe


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema viongozi wote wa Sekta za umma na binafsi wanatakiwa waendelezwe kitaaluma kwa ajili ya kukuza weledi, ubunifu na maadili ili waweze kusimamia ipasavyo maendeleo na kuongeza tija na mapato ya Taifa.

Amesema katika kipindi hiki ambacho nchi imeingia katika uchumi wa kati, Serikali ingependa kuona nguvukazi katika ngazi mbalimbali inaimarishwa na kuhakikisha viongozi wanatumia ujuzi na weledi katika maeneo ya usimamizi wa rasilimali watu, rasilimali fedha na miradi.

Waziri Mkuu ameyasema hayo jana (Ijumaa, Januari 29, 2021) katika Mahafali ya Wahitimu wa Programu ya Uanagenzi kwa Maafisa Watendaji Wakuu (Ceo Apprenticeship Program) yaliyofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Hyatt Regency, The Kilimanjaro, Dar-Es-Salaam.

“Dhana ya uanagenzi ni suluhisho la kuhakikisha wataalamu wetu wanajengewa ujuzi unaohitajika mara kwa mara ili kuwaongezea umahiri katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku. Nchi inahitaji viongozi wanaoongoza kwa vitendo na kuwa mfano bora kwa Taifa.”

Waziri Mkuu amesema pamoja na mambo mengine, dhana ya uanagenzi inalenga kukuza mtandao wa viongozi kupitia mafunzo kwa vitendo na ushauri ili kuwawezesha viongozi au maafisa watendaji wakuu kufanya maamuzi yenye maslahi mapana kwa Taifa.

Amesema ana imani kwamba wahitimu hao watakuwa watendaji wenye uwezo wa kusimamia mabadiliko, wasikivu, waadilifu na wenye mori ya kuleta maendeleo katika sekta mbalimbali wanazozifanyia kazi.

Waziri Mkuu amesema manufaa na faida za ujenzi wa uwezo wa wataalam wa ndani hususan viongozi na maafisa watendaji wakuu ni pamoja uwepo wa rasilimali na nguvu kazi ya Taifa yenye ubora wa ujuzi, weledi na umahiri wa hali ya juu unaowawezesha kutoa mchango stahiki katika maendeleo ya Kitaifa, Kikanda na Kimataifa.

Amesema manufaa mengine ni nchi kuwa na viongozi na watendaji wakuu wabunifu, wenye maadili na uzalendo ambao wapo tayari kujenga uchumi imara, endelevu na unaokua pamoja na kukuza uwezo wa kitaalam na ujuzi wa matumizi ya teknolojia mpya ya kidijitali.

Akizungumzia kuhusu sekta binafsi, Waziri Mkuu amesema Serikali inathamini sekta binafsi kwa kuwa ina nafasi kubwa katika kuchangia maendeleo ya nchi. “Hivyo kwa viongozi hawa kupata mafunzo haya itasaidia kusimamia nguvukazi yenye ujuzi na maarifa itakayozidi kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya nchi yetu.”

“Ni ukweli usiopingika kuwa, sekta binafsi na asasi za kiraia zikiwemo taasisi za dini zimekuwa zikitoa mchango muhimu katika kuongeza fursa za upatikanaji wa elimu, maarifa na ujuzi nchini. Hivyo, napenda kutambua na kupongeza mchango wa sekta binafsi katika kuwajengea uwezo Watanzania kielimu, maarifa na uwezo wa kuongoza katika nafasi za juu.”

Kadhalika, Waziri Mkuu ametoa wito kwa Bodi ya Wakurugenzi wa CEO Roundtable of Tanzania na Taasisi ya Uongozi washirikiane ili kubaini maeneo yenye uhitaji na kutoa mafunzo yenye tija. Amesema anatambua Taasisi ya Uongozi inaendesha programu za mafunzo ya uongozi kwa kushirikiana na Chuo Kikuu cha Alto cha Nchini Finland.

Waziri Mkuu amesema ushirikiano huo utaleta tija na utaondoa marudio na kuimarisha ubunifu katika kutoa mafunzo na kuleta manufaa kwa washiriki wa mafunzo hayo. Pia amewataka waandae mipango ya mafunzo yenye lengo la kutambua na kujenga uwezo wa Watanzania katika sekta za kipaumbele, hususan sekta ya madini, mafuta na gesi, ujenzi na TEHAMA.

Pia, Waziri Mkuu amewataka washirikiane katika kuwajengea uwezo wa wataalam wabobezi katika masuala ya uendeshaji wa miradi mikubwa ya kimkakati kama mradi wa ujenzi wa bwawa la kufua umeme wa Julius Nyerere na mradi wa reli ya kisasa (SGR) na usimamizi na ujenzi wa bomba la kusafirisha mafuta ghafi la Afrika Mashariki litakaloanzia Hoima, nchini Uganda hadi Chongoleani, Mkoani Tanga.

Awali, Mwenyekiti wa Jukwaa la Maafisa Watendaji; Wakuu Tanzania (CEO Roundtable of Tanzania – CEOrt); Sanjay Rughani alisema mafunzo hayo ya Uanagenzi kwa Maafisa Watendaji Wakuu yanalenga kuwaandaa Watanzania kushika nafasi za juu za kiuongozi na kiutendaji   katika taasisi mbalimbali.

Mkurugenzi huyo alisema mpango huo wa mafunzo kwa Maafisa Watendaji Wakuu umedhamiria kuwajengea Wataalam wa Kitanzania uwezo mkubwa ili waweze kushindana katika kuhudumu kwenye nafasi za Utendaji Mkuu katika Taasisi, Programu na miradi mikubwa ya Kitaifa na kimataifa.


Share:

MIGODI YA BUZWAGI NA BULYANHULU YALIPA USHURU BIL 2.3 KWA AJILI YA MAENDELEO MANISPAA YA KAHAMA NA HALMASHAURI YA MSALALA

Share:

Waziri mkuu wa DRC ajiuzulu


Sylvestre Ilunga Ilunkamba amejiuzulu rasmi kama waziri mkuu wa Jamuhuri ya kidemokrasi ya Congo, na kuwasilisha barua yake kwa Rais Félix Tshisekedi.

Bw Ilunga, ambaye ni mshirika mkuu wa mtangulizi wa Rais Tshisekedi, Joseph Kabila, ameongoza baraza la mawaziri la serikali ya Muungano kwa miezi 15.

Hata hivyo wabunge walipitisha kura ya kutokuwa na Imani na serikali yake Jumatano wiki hii na akapewa saa 24 awe amejiuzulu.

Kujiuzulu kwake kunatoa fursa kwa Rais Tshisekedi ya kuwateua washirika wake kama mawaziri.

Hadi sasa, utendaji wa Bw Tshisekedi umekuwa ukidhibitiwa na, muungano alionao na Bw Kabila ambao uliafikiwa wakati alipoingia madarakani miaka miwili iliyopita.

Ushindi wake katika uchaguzi mwezi Disemba 2018 ulisifiwa kama wa kihistoria-ambapo kulikuwa na makabidhiano ya kwanza ya utawala kwa njia ya amani ambayo hayakuwahi kushuhudiwa katika historia ya miongo sita nchini humo.


Share:

Delivery Sales Driver at Frostan Limited Tanzania

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

job Title: Delivery Sales Driver Reports To: Logistics and Inventory Manager Department: Transport and logistics Location: Dar es Salaam Key Responsibilities Transport and Deliver Goods, sales driver is responsible for moving materials along his/her assigned route and bring these goods to customers. Follow Routes and Schedules, sales drivers must maintain his/her scheduled deliveries and respond […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Civil Works Coordinator at Anotech Energy

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Civil Works Coordinator   Tanzania Reference : ANO/0421/CWC/MBE/EFR   Scope of work We are currently looking for a Civil Works Coordinator. The main missions will be to:   Follow Early Civil Works (ECW) contracts and coordinate the activities from point of view planning and cost; Follow the Engineering work that remains to be completed and […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Education M&E Officer at International Rescue Committee (IRC)

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Education M&E Officer Kibondo, Tanzania Requisition ID: req12094 Job Title: Education M&E Officer Sector: Education Employment Category: Fixed Term Employment Type: Full-Time Open to Expatriates: No Location: Kibondo, Tanzania Job Description The International Rescue Committee (IRC) responds to the world’s worst humanitarian crises and helps people to survive and rebuild their lives. Founded in 1933 at […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Sales Manager at ViewMedia

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Sales Manager   ViewMedia Dar es Salaam, Tanzania About The Company ViewMedia provides global distribution services to a variety of both Television and Radio channels. From start-up companies to larger organisations, we can provide a full TurnKey solution for whatever your requirements are. ViewMedia has a 24/7 fully managed teleport facility in Guildford, England with […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

WAZIRI MKUU WA DRC AJIUZULU

Sylvestre Ilunga Ilunkamba amejiuzulu rasmi kama waziri mkuu wa Jamuhuri ya kidemokrasi ya Congo, na kuwasilisha barua yake kwa Rais Félix Tshisekedi.

Bw Ilunga, ambaye ni mshirika mkuu wa mtangulizi wa Rais Tshisekedi, Joseph Kabila, ameongoza baraza la mawaziri la serikali ya Muungano kwa miezi 15.

Hata hivyo wabunge walipitisha kura ya kutokuwa na Imani na serikali yake Jumatano wiki hii na akapewa saa 24 awe amejiuzulu.

Kujiuzulu kwake kunatoa fursa kwa Rais Tshisekedi ya kuwateua washirika wake kama mawaziri.

Hadi sasa, utendaji wa Bw Tshisekedi umekuwa ukidhibitiwa na, muungano alionao na Bw Kabila ambao uliafikiwa wakati alipoingia madarakani miaka miwili iliyopita.

Ushindi wake katika uchaguzi mwezi Disemba 2018 ulisifiwa kama wa kihistoria-ambapo kulikuwa na makabidhiano ya kwanza ya utawala kwa njia ya amani ambayo hayakuwahi kushuhudiwa katika historia ya miongo sita nchini humo.

Bw Tshisekedi bado hajamchagua waziri mkuu mpya,ambaye ataunda serikali ijayo.

 CHANZO - BBC SWAHILI

Share:

WAZIRI BASHUNGWA KUPOKELEWA KWA WIMBO MAALUMU KONGAMANO LA WANAMUZIKI

 

Wasanii wa Kikundi cha Sanaa cha Dofa kilichopo Karatu mkoani Arusha wakifanya mazoezi ya  wimbo maalumu watakao muimbia Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa  wakati wa kumpokea katika  kongamano la wanamuziki.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Wanamuziki Tanzania (TAMUFO) Stella Joel.

Na Dotto Mwaibale

WASANII wa Kikundi cha Sanaa cha Dofa kilichopo Karatu mkoani Arusha wanatarajia kumpokea Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Innocent Bashungwa kwa wimbo maalumu katika kongamano la wanamuziki.

Bashungwa atakuwa mgeni rasmi katika kongamano hilo la Umoja wa Wanamuziki Tanzania (TAMUFO) litakalofanyika Februari 20, 2021 jijini Arusha.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Arusha jana Katibu Mkuu wa TAMUFO, Stella Joel alisema hivi sasa kikundi hicho kipo katika mazoezi ya wimbo huo maalumu kwa ajili ya kumpokea Waziri Bashungwa.

" Waziri Bashungwa anakuja kwenye kongamano letu wanamuziki hivyo tumeona ni lazima tumpokee kwa wimbo maalumu kwa ajili ya kumpa heshima." alisema Joel.

Joel alisema katika kongamano hilo  pamoja na mambo mengine Bashungwa atatoa  kadi za Bima ya Afya ya NHIF kwa Wanamuziki wa kada zote na kusikiliza changamoto zao mbalimbali.

Alisema kadi hizo zitawasaidia kupata vipimo na matibabu katika hospitali za Serikali na binafsi.

"Serikali imetukumbuka wanamuziki kwa kutupatia kadi za bima ya afya ya Taifa kwa gharama nafuu kupitia Tanzania Music Foundation (TAMUFO) jambo litakalo tusaidia wanamuziki kupata matibabu." alisema Joel. 

Joel aliwataja baadhi ya wanamuziki watakao kabidhiwa kadi hizo kuwa ni wa muziki wa Injili, bongo fleva, dansi, taarabu na ngoma za asili. 

Aidha Joel alisema kitendo cha Serikali kutoa kadi hizo za bima ya afya kwa wanamuzikini utekelezaji wa ahadi ya Rais Dkt. John Magufuli ya kuwasaidia wasanii hapa nchini.

Katibu mkuu huyo wa TAMUFO alitumia nafasi hiyo kuishukuru Serikali kwa hatua hiyo na kuelezea kuwa wamepata ari na nguvu mpya  ya kutekeleza shughuli zao kwa vitendo kwa ajili ya maendeleo ya sanaa hapa nchini.

Alisema maandalizi yote ya kongamano hilo yamekwisha kamilika ikiwa na taratibu  za kuwapata wanamuziki. 

Joel aliongeza kuwa katika kongamano hilo maafisa kutoka Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA) na Maafisa Utamaduni na wadau wengine watakuwepo.

Share:

Call Centre Operators 10 Job Opportunities at Job Junction Tanzania

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

CALL CENTRE OPERATORS (10)   EMPLOYER:Job Junction Tanzania LOCATION:Dar Es Salaam PURPOSE: Serves customers by determining requirements answering inquiries resolving problems fulfilling requests maintaining database. Call Center Operator Job Duties:   Determines requirements by working with customers. Answers inquiries by clarifying desired information researching, locating, and providing information Resolves problems by clarifying issues researching and exploring […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger