Friday 22 January 2021

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO IJUMAA JANUARI 22,2021




























Share:

Thursday 21 January 2021

Tanzia : ALIYEKUWA RC KIGOMA BRIGEDIA JENERALI MSTAAFU EMMANUEL MAGANGA AFARIKI DUNIA


 Brigedia Jenerali mstaafu, Emmanuel Maganga enzi za uhai wake.
***
Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma, Brigedia Jenerali mstaafu, Emmanuel Maganga amefariki dunia leo Alhamis usiku Januari 21,2021.

Taarifa za awali inaelezwa kuwa Brigedia Jenerali mstaafu, Emmanuel Maganga amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Jeshi mkoani Tabora.

Taaifa zaidi tutawaletea hivi punde

Share:

ALIYESHUKA KUJISAIDIA AFARIKI KWA KUKANYAGWA NA TRENI AKIDANDIA


Picha ya mfano wa treni
Na Mwandishi wetu  - Moshi
Mtu mmoja aliyejulikana kwa jina moja la Noa amefariki dunia baada ya kukanyagwa na treni ya abiria akiidandia wakati ikiwa imeanza kuondoka katika stesheni ya Moshi mkoani Kilimanjaro. 

Noa anayedaiwa kuwa fundi ujenzi na aliyekuwa akitoka Dar es Salaam kwenda Arusha amekanyagwa na treni wakati akijaribu kudandia treni hiyo iliyokuwa ikitoka Dar es Salaam kwenda Arusha leo Alhamis Januari 21,2021.

Kaimu kamanda wa polisi Mkoa wa Kilimanjaro Ronald Makona amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa treni hiyo ilipofika tesheni ya Moshi, Noa alishuka na kwenda kujisaidia na hivyo treni hiyo kumuacha na alipojaribu kuikimbiza ili apande kwenye behewa lake kwa bahati mbaya aliteleza na ikamkanyaga na kumkata vipande
Share:

MAABARA YA TMDA KANDA YA ZIWA KUWA BOBEZI KWENYE CHUNGUZI ZA VIPUKUSI


Meneja wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Kanda ya Ziwa Sophia Mziray akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake wakati walipozuru katika maabara hiyo jijini Mwanza kuona shughuli za uchunguzi wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi zinavyoendeshwa. 
Meneja wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Kanda ya Ziwa Sophia Mziray akiwa na Kaimu Mkuu wa Maabara ya TMDA Kanda ya Ziwa Bw.Bugusu Nyamweru pamoja na baadhi ya waandishi wa habari katika maabara hiyo. 
Meneja wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Kanda ya Ziwa Sophia Mziray akiwa ofisini kwake pamoja na Meneja Mawasiliano na Elimu kwa Umma,wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA),Gaudensia Simwanza kushoto pamoja na baadhi ya waandishi wa habari ofisini kwake jijini Mwanza. 
Meneja Mawasiliano na Elimu kwa Umma,wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA),Gaudensia Simwanza akifafanua jambo kwa mwandishi wa habari Eveyline Kitomari wakati waandishi wa habari walipozuru Maabara hiyo jijini Mwanza kutoka kulia ni Kaimu Mkuu wa Maabara ya TMDA Kanda ya Ziwa Bw.Bugusu Nyamweru. 
Meneja Mawasiliano na Elimu kwa Umma,wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA),Gaudensia Simwanza kushoto akikabidhi Camera kwa Meneja wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Kanda ya Ziwa Sophia Mziray ambayo ni Kitendea kazi kwa ajili ya matukio mbalimbali ya mamlaka hiyo Kanda ya Ziwa.

................................................

Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) imeanza maandalizi ya kuifanya maabara ya Kanda ya Ziwa kuwa maabara bora na maalumu kwa uchunguzi wa dawa za kuua viini vya bakteria (vipukusi), mpango unatarajiwa kukamilishwa ndani ya miaka mitatu.

Hayo yamebainishwa na Meneja wa TMDA Kanda ya Ziwa Sophia Mziray kwa waandishi wa Habari waliozuru katika maabara hiyo jijini Mwanza kuona shughuli za uchunguzi wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi zinavyoendeshwa.

"Maabara hii ipo kwenye taratibu za kufanywa kuwa maabara kubwa ya kisasa, bora na bobezi ya kupima vipukusi katika Afrika; na nchi za kusini mwa Afrika (SADC)," alisema Mziray.

Amesema kuwa Mamlaka ipo kwenye hatua mbalimbali za kuwaandaa wachunguzi waweze kuwa wabobezi lakini vile vile kuandaa mahitaji ya kuifanya maabara hii iwe bora kwa Afrika katika kuchunguza vipukusi.

Mziray amesema kwasasa maabara ya kanda ya ziwa ndiyo pekee kwa nchi wanachama wa jumuia ya Afrika Mashariki (EAC) yenye uwezo wa kupima vipukusi na kutoa majibu yasiyo na shaka.

""Kwa kuwa ni maabara pekee katika kanda ya ziwa tunaendelea kuchunguza dawa kutoka kanda nyingine, kutoa elimu kwa umma, na kuhakikisha Watanzania wanapata bidhaa bora, salama na zenye ufanisi," alisema Mziray.

Ameongeza: "Tunaendelea kuwaelimisha wananchi kuwa wao pia ni sehemu ya wadhibiti wa dawa na vifaa tiba, hivyo wanapotumia na kubaini madhara watoe taarifa kwa haraka kwenye ofisi zetu nasi tuzifanyie kazi."

Amebainisha kuwa maabara ina mifumo ambayo imethibitishwa. Mamlaka inaandaa nyaraka, upembuzi yakinifu ujiridhisha kama rasilimali zinatosheleza ili kutimiza nia ya kuwa na maabara bora zaidi.

"Ili kuhakikisha ubora wa dawa vifaa tiba na vitendanishi unaendelea kuwepo, tuna tumia mfumo wa ufuatiliaji na udhibiti wa dawa sokoni (PMS) uchunguzi hulenga kubaini madhara ya Dawa kuanzia kwenye vifungashio," alisisitiza.

Mziray ameeleza kuwa Kanda ya Ziwa yenye mikoa Sita bado inakabiliwa na changamoto ya udhibiti wa bidhaa kwenye mipak ya Mutukula, Sirari, Kyerwa, na pia bandari ya Mwanza South na Uwanja wa ndege wa Mwanza kwakuwa dawa hizo huvushwa kwa njia zisizohalali.

"Kanda hii ni kubwa inajumuisha mikoa ya Mwanza, Shinyanga Kagera, Simiyu na Mara, watumishi wa TMDA pekee yake hawatoshi kufanikisha udhibiti hivyo Mamlaka inashirikiana na wakurugenzi wa halmashauri ambao huteua wakaguzi toka maeneo yao kisha tunawafundisha na kuwapa vitambulisho," ameeleza.

Meneja mawasiliano na elimu kwa umma wa TMDA Gaudensia Simwanza amesema ili maabara itoe majibu yasiyo na shaka lazima iwe imekidhi vigezo elekezi vya Shirika la Afya Duniani (WHO): hivyo maabara hii imekidhi na kuwa yenye kutoa majibu sahihi yanayokubalika ya uchunguzi wa sampuli za vipukusi.

"Maabara hii imepokea vipimo vya sampuli zilizochunguzwa Ujerumani na Afrika Kusini ambako baada ya kupima majibu yalionesha kutofautiana lakini baada ya sampuli hizo kupimwa toka Maabara ya TMDA yakawa suluhisho," alieleza.

Share:

WAGANGA WA TIBA ASILI WATUMIE SUA NA WATAFITI WAKE KATIKA KUBORESHA BIDHAA ZILIZOPO NA KUANZISHA MPYA


Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) Utawala na Fedha Amandus Muhairwa akifungua kongamano kwa niaba ya Makamu Mkuu wa Chuo hicho Prof. Raphael Chibunda wakati akifungua Kongamano la siku moja la Watalaamu wa Tiba asili na kutoka maeneo mbalimbali nchini lililofanyika Chuoni kabla ya maonesho na uzinduzi wa jukwaa la ubunifu wa bidhaa za mimea dawa kwa maendeleo ya taifa lililoandaliwa na Mradi wa GRILI. 
Mratibu wa Utafiti na machapisho katika kurugenzi ya shahada za uzamili,utafiti,uhaulishaji wa teknolojia na ushauri wa kitaalamu ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA Prof. Japhet Kashaigiri akitoa salamu za kurugenzi yake kwenye kongamano hilo la wadau wa tiba asili nchini. 
Mtafiti Mkuu wa mradi wa GRILI Dkt. Faith Mabiki Akileza malengo ya mradi huo wa GRILI na malengo ya Kongamano hilo la wadau wa tiba asili nchini. 
Mkuu wa Ndaki ya Solomoni Mahlangu ya Sayansi na Elimu Dkt. Geofrey akitoa salamu za Ndaki yake na kuwakaribisha wageni hao Chuoni hapo. 
Wadau wa kongamano hilo ambao ni waganga wa tiba asili kutoka mikoa mbalimbali ya Tanzania wakifuatilia hotuba ya ufunguzi. 
Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) Utawala na Fedha Amandus Muhairwa (Katikati) akisikiliza maelezo toka kwa viongozi wa mradi, Prof. Samweli Kabote amabye ni Muwakilishi wa Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Utawala na fedha (Wa kwanza Kushoto) Akifuatilia hotuba ya ufunguzi, wa kwanza Kushoto ni Dkt. Geofrey Kalugila Rasi wa ndaki ya Solomon Mahlangu ya sayansi na Elimu. 
Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) Utawala na Fedha Amandus Muhairwa akiangalia maonesho ya bidhaa mbalimbali za tiba asili zilizoletwa kwenye kongamano hilo kabla ya maonesho rasmi siku ya ijumaa. 
Washiriki wa Kongamano hilo wakifuatilia ufunguzi wa Kongamono hilo na mada mbalimbali kutoka kwa wadasu wa tiba asili,Watafiti na watunga sera. 

***************************** 

Na: Calvin Gwabara – Morogoro. 
Waganga wa tiba asili nchini wametakiwa kuangalia kwa undani namna ya kutumia matokeo ya tafiti zinazofanywa na watafiti wa Chou Kikuu Cha Sokoine cha Kilimo (SUA) na Taasisi zingine ili kuboresha bidhaa zilizopo na kuanzisha bidhaa mpya ili kuendana na mahitaji ya jamii kwa wakati sahihi. 

Wito huo ulitolewa na Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA) Utawala na Fedha Prof. Amandus Muhairwa kwa niaba ya Makamu Mkuu wa Chuo hicho Prof. Raphael Chibunda wakati akifungua Kongamano la siku moja la Watalaamu wa Tiba asili na kutoka maeneo mbalimbali nchini lililofanyika Chuoni kabla ya maonesho na uzinduzi wa jukwaa la ubunifu wa bidhaa za mimea dawa kwa maendeleo ya taifa lililoandaliwa na Mradi wa GRILI. 

Prof. Mhairwa alisema kuwa njia hiyo ni muhimu sana hasa katika wakati huu ambao dunia inahangaika kutafuta chanjo na tiba ya ugonjwa wa COVID 19 ambapo dawa za mimea zimeonekana kufanya vizuri Zaidi kuliko za hospitalini, 

” Wanasayansi na waganga wa tiba ya asili sio kama vyama viwili vya upinzani, sisi tunafanya kazi kwa kutegemeana, sisi tunavitu tunavumbua kisayansi lakini pia kuna vitu vingine tunavifanyia utafiti vile ambavyo mmevianzisha nyinyi ili kuweza kupata udani Zaidi wa dawa mnazogundua kwahiyo hatupingi kazi zenu wala msituone kama vile maadui sisi tufanye kazi kwa pamoja kwa faida ya jamii na taifa letu” Alisisitiza Prof. Mhairwa. 

Alisema bidaa za mimea dawa zinakabiliwa na changamoto zinazohusiana na uzalishaji,uvunaji,utengenezaji,uuzaji na upatikanaji endelevu wa malighafi hivyo ili kupunguza changamoto hizo na kuzindoa kabisa kunahitajika utafiti Zaidi wa kisayansi,ubunifu Zaidi katika masoko,uzingatiaji wa hali ya juu wa vigezo vya ubora vinavyotakiwa na kufuata taratibu za biashara zenye tija. 

Lakini pia aliwataka Wataalamu hao wa Tiba asili kuangalia masuala ya kisera yanayoleta changamoto katika kuhaulisha teknolojia hizi ili ziweze kutumika kibiashara na kuanzisha viwanda vya uzalishaji wa mimea dawa na hasa katika kipindi hiki ambapo sera ya serikali ni kusukuma uanzishwaji wa viwanda kwenye sekta hii. 

Naibu Makamu huyo wa Mkuu wa Chuo Utawala na Fedha aliwahakikishia kuwa SUA na hasa kurugenzi ya uzamili,Utafiti,Uhaulishaji wa teknolojia na ushauri wa kitaalamu kwa kushirikiana na serikali wataendelea kuwa nao bega kwa bega kwa kusaidia jitihada za wadau wote kwenye sekta hii katika kuboresha tafiti za oaina hii kwa kadri mazingira yatakavyoruhusu. 

Akitoa salamu kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kufungua kongamano hilo Mratibu wa Utafiti na machapisho katika kurugenzi ya shahada za uzamili,utafiti,uhaulishaji wa teknolojia na ushauri wa kitaalamu ya Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA Prof. Japhet Kashaigiri alisema kuwa kurugenzi hiyo na vitengo vingne vya SUA vimekuwa na utaratibu wa kuandaa makongamano ya aina hiyo ili kujaribu kuboresha biashara za mazao ya Kilimo,Ufugaji na Misitu kwa kushirikiana na wadau mbalimbali katika sekta hizo. 

“Katika makongamano haya SUA imekuwa ikishirikisha wasimamizi na wakaguziwa ubora wa biashara hizi pamoja na watunga sera kwa ujumla na utaratibu huu umeongeza mchango mkubwa wa chou chetu katika kutatua changamoto mbalimbali na kuboresha biashara za mazao nah ii ni muhimu hasa katika awamu hii ya serikali ya tano ambayo mwelekeo wake ni kuwa uchumi wa viwanda. 

Prof. Kashaigili alisema Vyuo Vikuu kote duniani ni vitovu vya maendeleo ya kitaaluma na Tafiti mbalimbali na kwa muktadha huo kurugenzi ya uzamili kupitia kitengo chake cha uhaulishaji wa teknolojia pamoja na mradi wa GRILI zimeona ni vyema kutumia uzoefu wake wa ndani na kwa kushirikiana na wadau wengine kuandaa kongamano hili hapa SUA ili kuwaleta wadau wote pamoja na kujadili namna ya kukuza uelewa na kutatua changamoto hizo. 

Akileza malengo ya mradi huo wa GRILI na malengo ya Kongamano hilo Mtafiti mkuu wa mradi huo Dkt. Faith Mabiki amesema Utekelezaji wa mradi huu ulianza mwaka 2018 ukiwa na lengo la kuchangia katika kuongeza ubora wa bidhaa za miti dawa ili kuboresha Maisha ya watengenezaji,afya za watumiaji na kuchangia katika pato la taifa. 

Dkt. Mabiki alisema ili kufikia malengo hayo ya muda mrefu mradi huo unajenga uwezo wa kitafiti wa kitafiti kwa wanafunzi wa shahada za uzamivu 5 na shahada za uzamili 2 katika maeno muhimu ya kemikali,usugu wa dawa na masoko na unategemea kutoa matokeo ya kitafiti yatakayo tumika na wadau muhimu wa kuboresha biadhaa hizi. 

“Kongamano hili la kitaalamu la wadau likiwa ni moja ya shughuli za uzinduzi wa Jukwaa la ubunifu wa bidhaa za mimea dawa kwa maendeleo ya taifa litajikita Zaidi kwenye kujadili Uboredhaji wa uzalishaji,uchakataji,ufungsdhsji na uuzaji wa bidhaa zinazotokana na mimea dawa hapa Tanzania na namna ya kutatua changamoto hizo” Alisema Dkt. Mabiki. 

Kwa upande wake Mkuu wa Ndaki ya Solomoni Mahlangu ya Sayansi na Elimu Dkt. Geofrey alisema kwa upande wa utafiti ndaki hiyo ni ya pekee inayotoa shahada ya uzamili ambazo zinajikita moja kwa moja katika utafiti wa mazao ya mimea dawa ambayo mojawapo inahusika katika tukio hili na ina miradi Zaidi ya tisa ambayo kwa namna moja au nyingine zinagusa bidhaa hizi za mimea dawa. 

“Kwa sababu hiyo tunategemea kuchangia juhudi za SUA na Taifa katika kuongeza ubora wa bidhaa hizi ili zipate Masoko” Alisisitiza Dkt. Kalugila. 

Pia Dkt. Geofrey Kalugila aliwashukuru wadau hao kutoka maeneo yote nchini kufiki akushiriki kwenye kongamano hilo,maonesho na uzinduzi wa Jukwaa la ubunifu na kuwataka watumia siku chache watakazokuwa SUA kujifunza na kujionea mambo mbalimbali ya kistoria kwenye kampasi hiyo ambayo ilikuwa kambi ya wapigania uhuru wa Afrika kusini. 

Kongamano hilo litafuatiwa na Maonesho makubwa ya Tiba asili na bidhaa zake litakalofanyika kwenye viwanja vya soko kuu la mkoa wa Morogoro tarehe 22/01/2021 na baada siku ya jumamosi kutakuwa na uzinduzi wa Jukwaa la ubunifu wa bidhaa za tiba asili litakalofanyika kwenye kampasi ya Solomon Mahlangu Mazumbu tarehe 23/01/2021 zilizoandaliwa na Mradi wa GRILi.
Share:

Post write off Recoveries Officer at Absa

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Post write off Recoveries Officer    Bring your possibility to life! Define your career with us With over 100 years of rich history and strongly positioned as a local bank with regional and international expertise, a career with our family offers the opportunity to be part of this exciting growth journey, to reset our future […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Regional Senior Technical Officer at FHI 360

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Regional Senior Technical Officer     FHI 360 is a nonprofit human development organization dedicated to improving lives in lasting ways by advancing integrated, locally driven solutions. Our staff include experts in Health, Education, Nutrition, Environment, Economic Development, Civil Society, Gender, Youth, Research and Technology; creating a unique mix of capabilities to address today’s interrelated development […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Senior Trainer/Mentor at BBC Media Action

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Title: Senior Trainer/Mentor Reports to: Partnership Development Manager (PDM) Location: Tanzania Contract: 12 months (with possible extension) Special requirements: Legal right to live and work in Tanzania. Fluent in spoken and written English and Swahili Closing date: 31 January 2021 BBC Media Action: We are the BBC’s international charity, and we believe in the power […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Mentor/Producer-Presenter at BBC Media Action

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Job Title: Mentor/Producer-Presenter Reports to: Senior Trainer Mentor Locatin: Tanzania. The post holder will be required to spend at least 80% of their time in the field, working with radio producers at partner stations throughout Tanzania. Special requirements: Legal right to live and work in Tanzania. Fluent in spoken and written English and Swahili Contract: February […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Senior Exploration Geologist at Barrick Gold Corporation

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Senior Exploration Geologist     Barrick Gold Corporation seeks to employ a Geologist to work with the Exploration Department across our operations in Tanzania. This role reports to the Exploration Manager. The role holder will be accountable to execute the exploration programs, provide leadership, strategy and systems that delivers optimal evaluation and development of potential resources […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Research Scientists at Ifakara Health Institute

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Positions: Research Scientists (3 Posts) Reports to:   Principal Investigator Work station: Dar es Salaam Apply by:   January 29th 2021 Project: Developing and Strengthening Data Science Capacity Institute overview  Ifakara Health Institute (IHI) is a leading research organization in Africa with a strong track record in developing, testing and validating innovations for health. Driven by a core strategic mandate for research, […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Research Officers at Ifakara Health Institute

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Positions: Research Officers (3 Posts) Reports to:  Principal Investigator Work station:  Dar es Salaam Apply by:  January 29th 2021 Project:   Developing and Strengthening Data Science Capacity Institute overview  Ifakara Health Institute (IHI) is a leading research organization in Africa with a strong track record in developing, testing and validating innovations for health. Driven by a core strategic mandate for research, […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Grants Coordinator at Norwegian Refugee Council

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Grants Coordinator   Kibondo Job Description The purpose of the Grants Coordinator position is to provide essential grant management support to HoP and AM in delivering quality programmes in line with the NRC COs strategy and PoA for Tanzania. Adherence to NRC policies, guidance and procedures   Develop and maintain overview of all grants, donor […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Data Entry Officer at Norwegian Refugee Council

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Data Entry Officer    Job Description The WASH Data entry Officer  will be based in GOAL’s office in NRC supporting the WASH Team in managing all the program data. This position will support the WASH team in data collection and analysis, designing and managing a WASH database and the provision of analyzed data for donor […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

Various Posts UTUMISHI at MUHAS

This this content has been copied from Udahiliportal , please kindly visit udahiliportal.com to access full content

Overview:   The Public Service Recruitment Secretariat (PSRS) is a government organ with a status of independent Department established specifically to facilitate the recruitment process of employees to the Public Service. Public Service Recruitment Secretariat was established by the Public Service Act No. 8 0f 2002 as amended by Act No. 18 of 2007, section […]

This this content has been copied from udahiliportal.com , please kindly visit Udahiliportalto access full original content content or click here for more details

 

 

Share:

MWANAUME MWINGINE AFARIKI DUNIA AKIWA GESTI NA MPENZI WAKE MWANZA


Picha ya kitanda

Na Mgongo Kaitira - Mwananchi
Mtu mmoja ambaye jina lake halijatambulika amefariki dunia katika nyumba ya kulala wageni akiwa na mwanamke anayehisiwa kuwa ni mpenzi wake.

Tukio hilo limetokea Januari 18, 2021 katika nyumba ya kulala wageni ya Fimbo Lodge iliyopo mtaa wa Kilimahewa Wilaya ya Ilemela jijini Mwanza.

Mmiliki wa nyumba hiyo, Christopher Lyang’ombe akizungumza na Mwananchi Digital leo Alhamisi Januari 21, 2021 amekiri kutokea kwa tukio hilo akisisitiza watafutwe polisi kwa kuwa ndio wanaoendelea na uchunguzi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Jumanne Muliro amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba wanamshikilia kwa mahojiano mwanamke mmoja (jina linahifadhiwa) anayedaiwa kuwa mtu wa karibu wa marehemu na ndiyo alikuwa naye katika nyumba hiyo.

“Mtu anayetuhumiwa inadaiwa ni mtu wake wa siku nyingi tunamhoji tu ila upo ushahidi wa awali unaoonyesha alikuwa na matatizo ya presha,” amesema Muliro.

Tukio hilo limetokea ikiwa zimepita siku tano tangu kutokea kwa tukio kama hilo ambapo mkazi wa Goba jijini Dar es Salaam, David Makerege (80) alifariki dunia katika hoteli ya Mbezi Garden alipokuwa na Neema Kibaya (33).

CHANZO - MWANANCHI

Share:

SERIKALI YAWATAKA WACHIMBAJI WALIOVAMIA MGODI WA AL-HILAL KISHAPU WAONDOKE MARA MOJA


Wachimbaji wadogo wakimsikiliza Naibu Waziri, Prof. Shukrani Manya wakati akitoa maagizo ya serikali juu ya sakata la kuvamia eneo la mwekezaji

Na Suzy Luhende, Shinyanga 
WACHIMBAJI wadogo wa madini ya Almasi waliovamia na kuanza kuchimba katika kijiji cha Mwanh'olo kata ya Mwadui Lohumbo wilayani Kishapu mkoani Shinyanga wamepewa siku mbili wawe wameshaondoka eneo hilo kwa hiari ili kumpisha mwekezaji mkubwa mwenye leseni aendelee kufanya shughuli zake katika eneo hilo.

Agizo hilo limetolewa leo Januari 21,2021 na Naibu Waziri wa Madini, Prof. Shukrani Manya, akiwa kwenye ziara yake ya siku moja mkoani Shinyanga, ambapo alizungumza na wanunuzi wa madini viongozi wa ChamaCcha wachimbaji (SHIREMA) pamoja na wachimbaji wadogo wanaochimba katika kijiji cha Mwanh"olo kata ya Mwadui Lohumbo wilayani Kishapu mkoani Shinyanga. 

Manya amesema serikali ya awamu ya tano inawapenda wananchi wake na inataka waweze kupata maendeleo wao wenyewe na Taifa kwa ujumla, hivyo inawaomba wachimbaji hao waweze kuondoka katika eneo hilo kwa sababu ni eneo la mwekezaji Al-Hilal ambaye tayari ana leseni yake na kwamba wao watatafutiwa eneo jingine ili waweze kuendelea kuchimba.

"Nawaombeni sana muwe wasikivu na muweze kuelewa vizuri huu ujumbe wa serikali niliouleta kwenu, kwa sababu serikali inawapenda, hivyo inawapa siku mbili mkusanye mchanga wenu mliouandaa halafu mujiunge vikundi muwe na leseni yenu, serikali itawatafutia eneo zuri ambalo mtaendelea kuchimba bila bughuza yeyote, kinachotakiwa muwe waaminifu mnapopata mali muuzie katika soko letu na serikali iweze kuingiza kipato," amesema Manya.

"Msikubali kudanganywa na mtu awanunulie madini yenu tukikuta unauza kwa mtu tunakutaifisha hiyo mali yako na usafiri ulionao, hivyo tunatakiwa kuuzia kwenye mfumo ulioandaliwa na serikali, na serikali haihitaji faida kubwa inahitaji faida kidogo tu na na mtajulishwa sehemu mtakayopelekwa baada ya kutii kuondoka hapa," ameongeza.

Naibu Waziri Manya amesema eneo hilo siyo shamba la mtu kama wanavyojua bali ni mali ya serikali ambayo imeshakatiwa leseni na mwekezaji Hamad Hilal, hivyo wanatakiwa watoke kwa hiari kwani watatafutiwa eneo jingine la kuchimba ili mwenye leseni yake aendelee kufanya shughuli zake za uchimbaji.

Baadhi ya wachimbaji wadogo wanaochimba katika eneo hilo Zainab Said na Leonard Daudi wamesema wamekubali kuondoka pale ila wapewe muda wa wiki moja ili waweze kuosha mchanga wao na waweze kujiandaa kuondoka na mchanga wao kwa sababu muda waliopewa ni mdogo sana na waambiwe watapelekwa sehemu gani ili wakaendelee na kazi zao za uchimbaji. 

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack akitoa taarifa kwa naibu waziri Manya amesema anashukuru kwa kufika naibu waziri huyo, hivyo anaamini atasaidia kuondoa mgogoro wa wachimbaji wadogo na mwekezaji Al-Hilal, maana tayari nae alikuwa na mpango wa kuwapa siku chache wawe wameshaondoka eneo hilo

"Mimi na kamati yangu ya usalama wa madini tulishaenda katika kijiji hicho na tumejitahidi na tayari wachimbaji hao tulikuwa tumeshawatoa na sasa wameanza kurudi tena, lakini tunasikia wanaowafadhili ni hawa viongozi wao na baadhi ya wanunuzi tuliwataka wawaondoe watu wao katika eneo hilo," amesema Telack

Naye Afisa Madini wa mkoa wa Shinyanga Joseph Kumburu amesema tayari ofisi ya madini April 20, 2020 ilishawatoa wachimbaji 400 ambao walivamia eneo hilo lakini wakaja kurudi tena na sasa lina wachimbaji zaidi ya 1000 ivyo ofisi ya madini ilikuwa inajiandaa jinsi ya kuwaondoa na kuwakamata wachimbaji wanaovamia katika eneo la muwekezaji Al-Hilal, na kuwakamata wale wanaojimilikisha maeneo hayo.
Naibu Waziri wa Madini, Prof. Shukrani Manya akizungumza na wanunuzi wa madini na viongozi wa Chama cha Wachimbaji wadogo wa madini mkoa wa Shinyanga (SHIREMA) katika ukumbi wa ofisi ya Mkuu wa mkoa huo, mapema wakati wa ziara yake mkoani Shinyanga
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Zainab Telack (katikati) akizungumza katika kikao hicho. Kulia ni Naibu Waziri wa Madini, Prof. Shukrani Manya
Naibu Waziri wa Madini, Prof. Shukrani Manya akizungumza na wachimbaji wadogo wa madini ya Almasi katika Kijiji cha Mwanh'olo wilayani Kishapu ambao wanaodaiwa kuvamia eneo la mwekezaji, Mgodi wa Al-Hilal
Maeneo ya uchimbaji wa madini ya Almasi katika Kijiji cha Mwanh'olo wilayani Kishapu yanayodaiwa kuwa ya Mwekezaji Kampuni ya Al-Hilal ambayo yamevamiwa na wachimbaji wadogo
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger