Wednesday 30 December 2020

Aina mpya ya kirusi cha corona yaripotiwa Marekani

 


Aina mpya ya kirusi cha corona kinachoaminka kusambaa kwa kasi, imeripotiwa kwa mara ya kwanza nchini Marekani na Amerika ya Kusini

Aina hiyo mpya ya kirusi cha corona kilichogunduliwa kwa mara ya kwanza nchini Uingereza, sasa kimeripotiwa kuingia Marekani katika mji wa Colorado. 

Kirusi hicho kimegundulika kwa kijana wa miaka 20 ambaye hana historia ya kusafri. 

Taarifa za vyombo vya habari za ndani zinasema kuna uwezekano wa kisa kingine cha kirusi hicho. 

Wataalamu wanaamini kwamba aina hiyo mpya inaweza kuenea kwa kasi na itakuwa chanzo cha ongezeko la maambukizi Uingereza. 

Aina hiyo mpya ya kirusi kinachujulikana kama B.1.1.7 tayari pia imeripotiwa Canada, Italia, India na Umoja wa Falme za Kiarabu. Chile nayo imeripoti aina hiyo mpya na kulifanya kuwa taifa la kwanza Amerika ya Kusini kubaini maambukizi yake.



Share:

Waziri Mkuu Amuwakilisha Rais Dkt. Magufuli Mazishi Ya Askofu Banzi


 *Awataka Watanzania wamuenzi kwa kuuishi utumishi wake
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametoa wito kwa Watanzania kumuenzi Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Tanga, Baba Askofu Anthony Mathias Banzi kwa kuuishi utumishi wake uliogubikwa na upole na unyenyekevu aliowaonesha wakati wa kipindi cha uchungaji wake.

Ametoa wito huo leo (Jumanne, Desemba 29, 2020) kwenye mazishi ya Askofu Banzi yaliyofanyika ndani ya Kanisa Kuu la Mtakatifu Anthony wa Padua, Jimbo Katoliki la Tanga. Waziri Mkuu ameshiriki mazishi hayo kwa niaba ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli. Ibada ya mazishi imeongozwa na Askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki la Mtwara, Askofu Titus Mdoe.

Waziri Mkuu amesema katika maisha na utume wake wa kufundisha, kuongoza na kuwatakatifuza watu wa Mungu, Askofu Banzi alitoa kipaumbele katika masuala mbalimbali ya kijamii zikiwemo za elimu, afya na maji. Askofu Banzi alifariki dunia Jumapili, Desemba 20, 2020 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu.

“Leo hii tunapomsindikiza Baba Askofu Anthony Banzi tunajivunia mchango wake mkubwa katika kupigania amani, maelewano na mtangamano wa jamii kwa lengo la kujenga umoja, upendo na mshikamano wa Kitanzania. Sisi upande wa Serikali tutamkumbuka sana.”

Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kutoa pole kwa familia, ndugu na jamaa, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania na waamini wote wa kikatoliki nchini. “Tumuombee kwa Mwenyezi Mungu azipokee kazi zake za kiuchungaji alizozifanya katika kipindi cha uhai wake na ampumzishe kwa amani.”

Naye, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Ummy Mwalimu amesema kuwa wanawake wa Mkoa wa Tanga wamempoteza baba mwema na mlezi ambaye alipenda kuwashauri na kuwaunganisha kama watoto wake kwa kutumia kaulimbiu yake ya hekima, umoja na amani

“Mimi ni mmoja wa wanufaika wa upendo, wema na hekima za baba Askofu, licha ya kuwa mimi sio Mkatoliki lakini baba Askofu Banzi amekuwa akinikaribisha nyumbani kwake na kunipa baraka zake na kuniombea kwa sababu yeye anaamini watu wote ni wamoja”

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigela amesema Baba askofu Banzi alikuwa ni kiongozi mnyenyekevu, muadilifu na mpenda maendeleo aliyependa kuuona mkoa wa Tanga unapiga hatua.

Akisoma wasifu wa marehemu Askofu Banzi, Padri Richard Kimbwi alisema alizaliwa Oktoba 28, 1946 katika Parokia ya Tawa, Jimbo Katoliki la Morogoro, ambapo baada ya masomo na majiundo yake ya Kikasisi, Julai 29, 1973 alipewa daraja takatifu la upadre, Jimbo Katoliki la Morogoro.

Alisema kuwa Mwaka 1976 aliteulia kuwa Msarifu wa Seminari kuu ya Ntungano, Jimbo Katoliki la Bukoba na mwaka 1976 hadi mwaka 1981 alipelekwa nchini Austria kwa masomo ya juu na kufanikiwa kutunukiwa Shahada ya Uzamivu katika Falsafa. Mwaka 1981 hadi mwaka 1982 aliteuliwa kuwa Paroko wa Parokia ya Mandera na mhudumu wa maisha kiroho kwenye Hospitali ya Turiani, Jimbo Katoliki la Morogoro.

Aidha, mwaka 1981 hadi mwaka 1985 aliteuliwa kuwa Mhasibu wa Jimbo Katoliki la Morogoro na kati ya Mwaka 1985 hadi mwaka 1987 alikuwa ni Padre wa kiroho, Sekondari ya Masista Bigwa, Morogoro. Kati ya Mwaka 1988 hadi mwaka 1991 alikuwa mwalimu na mlezi, Seminari kuu ya Ntungano, Jimbo Katoliki la Bukoba na baadaye akateuliwa kuwa Gambera.

Mwaka 1992 hadi mwaka 1994 aliteuliwa kuwa Gambera wa Seminari kuu ya Kibosho, Jimbo Katoliki la Moshi na ilipofika tarehe 10 Juni 1994, Mtakatifu Yohane Paulo II akamteuwa kuwa Askofu wa Jimbo Katoliki Tanga na kuwekwa wakfu tarehe 15 Septemba 1994 na Kardinali Polycarp Pengo, Askofu mstaafu wa Jimbo kuu la Dar es Salaam.

Alisema Askofu Banzi amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 74 ya kuzaliwa, miaka 47 ya Daraja Takatifu la Upadre na miaka 26 ya Uaskofu, Utume ambao aliufanya kwa uaminifu mkubwa katika kuwaongoza, kuwafundisha na kuwatakatifuza watu wa Mungu ndani na nje ya Jimbo Katoliki la Tanga.


Share:

Kortini Kwa Kusambaza Picha za Ngono


Mkazi wa Mbagala Kizuiani, Faraji Omary(26) amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kujibu mashtaka manne, likiwemo la kusambaza picha za ngono na kusambaza machapisho yenye ujumbe mchafu unaoharibu maadili ya jamii.

Mshtakiwa huyo amefikishwa mahakamani hapo, jana Desemba 29, 2002 na kusomewa mashtaka yake na wakili wa Serikali Adolf Ulaya, mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Rashid Chaungu.

Wakili Ulaya amedai kuwa mshtakiwa anakabiliwa na kesi ya jinai namba 173/2020 na kwamba ameunganishwa na mshtakiwa mwenzake aitwaye Aisha Kiula, ambaye alisomewa mashtaka kama hayo, Desemba 23, 2020.

Akimsomea mashtaka yake, wakili Ulaya amedai kuwa mshtakiwa anadaiwa kutenda makosa yake kati ya Desemba 4 na Desemba 14, 2020 katika eneo la Kariakoo Jiji hapa.

Hata hivyo, mshtakiwa amekana mashtaka yake na kesi yake imeahirishwa hadi Januari 11, 2021 itakapotajwa.

Mshtakiwa amerudishwa rumande baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.


Share:

Form one selection 2021 Pwani region

The TAMISEMI via Pwani regional office website is about to officially release the Form one selection 2021 list for Primary School Leaving Examination (PSLE) candidates seeking admission into Government secondary school for 2021/2022 academic year in Pwani.. The form one selection 2021 Pwani list contains names of all selected Standard Seven – Primary School Leavers, […]

The post Form one selection 2021 Pwani region appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Form one selection 2021 Singida region

The TAMISEMI via Singida regional office website is about to officially release the Form one selection 2021 list for Primary School Leaving Examination (PSLE) candidates seeking admission into Government secondary school for 2021/2022 academic year in Singida.. The form one selection 2021 Singida list contains names of all selected Standard Seven – Primary School Leavers, […]

The post Form one selection 2021 Singida region appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Form one selection 2021 Mtwara region

The TAMISEMI via Mtwara regional office website is about to officially release the Form one selection 2021 list for Primary School Leaving Examination (PSLE) candidates seeking admission into Government secondary school for 2021/2022 academic year in Mtwara.. The form one selection 2021 Mtwara list contains names of all selected Standard Seven – Primary School Leavers, […]

The post Form one selection 2021 Mtwara region appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Form one selection 2021 Njombe region

The TAMISEMI via Njombe regional office website is about to officially release the Form one selection 2021 list for Primary School Leaving Examination (PSLE) candidates seeking admission into Government secondary school for 2021/2022 academic year in Njombe.. The form one selection 2021 Njombe list contains names of all selected Standard Seven – Primary School Leavers, […]

The post Form one selection 2021 Njombe region appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Form one selection 2021 Morogoro region

The TAMISEMI via Morogoro regional office website is about to officially release the Form one selection 2021 list for Primary School Leaving Examination (PSLE) candidates seeking admission into Government secondary school for 2021/2022 academic year in Morogoro.. The form one selection 2021 Morogoro list contains names of all selected Standard Seven – Primary School Leavers, […]

The post Form one selection 2021 Morogoro region appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Form one selection 2021 Katavi region

The TAMISEMI via Katavi regional office website is about to officially release the Form one selection 2021 list for Primary School Leaving Examination (PSLE) candidates seeking admission into Government secondary school for 2021/2022 academic year in Katavi.. The form one selection 2021 Katavi list contains names of all selected Standard Seven – Primary School Leavers, […]

The post Form one selection 2021 Katavi region appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Form one selection 2021 Arusha region

The TAMISEMI via Arusha regional office website is about to officially release the Form one selection 2021 list for Primary School Leaving Examination (PSLE) candidates seeking admission into Government secondary school for 2021/2022 academic year in Arusha.. The form one selection 2021 Arusha list contains names of all selected Standard Seven – Primary School Leavers, […]

The post Form one selection 2021 Arusha region appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Form one selection 2021 Kigoma region

The TAMISEMI via Kigoma regional office website is about to officially release the Form one selection 2021 list for Primary School Leaving Examination (PSLE) candidates seeking admission into Government secondary school for 2021/2022 academic year in Kigoma.. The form one selection 2021 Kigoma list contains names of all selected Standard Seven – Primary School Leavers, […]

The post Form one selection 2021 Kigoma region appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Finance Manager at MDH

Management and Development for Health (MDH) is a non-profit, non-governmental organization whose primary aim is to contribute to address public health priorities of the people of Tanzania and the world at large. These priorities include: communicable diseases such as HIV/AIDS, Tuberculosis and Malaria; Reproductive, Maternal, New-born and Child health (RMNCH); Nutrition; Non-Communicable Diseases of public […]

The post Finance Manager at MDH appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Form one selection 2021 Kilimanjaro region

The TAMISEMI via Kilimanjaro regional office website is about to officially release the Form one selection 2021 list for Primary School Leaving Examination (PSLE) candidates seeking admission into Government secondary school for 2021/2022 academic year in Kilimanjaro.. The form one selection 2021 Kilimanjaro list contains names of all selected Standard Seven – Primary School Leavers, […]

The post Form one selection 2021 Kilimanjaro region appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano Disemba 30



Share:

Tuesday 29 December 2020

Viwanda Kuondoa Umasikini Wa Wafugaji Na Wavuvi


 Na. Edward Kondela
Serikali imesema itahakikisha sekta za mifugo na uvuvi zinawaondoa wananchi katika umasikini, kupata ajira na nchi iweze kuuza bidhaa bora za mazao ya mifugo na uvuvi ndani na nje ya nchi.

Akizungumza jana (28.12.2020) katika siku yake ya kwanza ya ziara ya kikazi ya siku mbili Mkoani mwanza, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki wakati akihitimisha ziara hiyo kwenye kiwanda cha kuchinja na kuchakata nyama cha Chobo kilichopo Kata ya Usagara Wilaya ya Misungwi amesema wizara imekuwa ikichukulia kwa uzito mkubwa suala la viwanda ambalo litaweza kubadilisha fikra za wafugaji na wavuvi.

“Wananchi wetu waondoe umasikini, wananchi wetu wapate ajira na sisi tuuze bidhaa za mazao haya ya mifugo na uvuvi yaliyo bora hapa ndani na kule kwa wenzetu nje, sasa mimi nikikuta hali ya mkwamo kwa kitu ambacho kinatusaidia kuelekea huko napata shida.” Amesema Mhe. Ndaki

Waziri Ndaki akifuatana na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Pauline Gekul katika ziara hiyo amefafanua kuwa haridhishwi na baadhi ya changamoto wanazokutana nazo wawekezaji ambao wamejikita katika kuyaongezea thamani mazao ya mifugo na uvuvi na kumuagiza Kaimu Msajili wa Bodi ya Nyama nchini Bw. Iman Sichalwe kumpatia taarifa ya hali ya viwanda vya nyama nchini ili apate tathmini halisi ya utendaji kazi wa viwanda hivyo, baada ya Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha Chobo, Bw. John Chobo kubainisha baadhi ya changamoto ambazo Waziri Ndaki amesema wizara itahakikisha inafuatilia changamoto zinazoihusu wizara hiyo ili kuzipatia majibu.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda hicho Bw. John Chobo amesema kwa sasa kiwanda chake kimesimamisha uzalishaji na kinatarajia kuanza kurejea katika shughuli zake Mwezi Januari Mwaka 2021 baada ya ugonjwa wa Covid 19 kuathiri shughuli za kiwanda hicho ambacho kimekuwa kikisambaza nyama katika nchi za falme za kiarabu.

Bw. Chobo amesema kutopatikana kwa taarifa sahihi za mifugo kumekuwa kukichangia kwa kiasi kikubwa soko la nyama kutoka Tanzania kwenda nje ya nchi kuwekwa katika daraja la chini kwa kuwa mifugo mingi ambayo inachakatwa viwandani haina taarifa sahihi juu ya ukuaji wake, magonjwa na chanjo mbalimbali ambazo mfugo huo umepatiwa.

Akiwa katika Kiwanda cha kuchakata samaki Nile Perch kilichopo eneo la viwanda katika Kata ya Nyakato Wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki akiambatana na Naibu Waziri Mhe. Pauline Gekul amewataka wawekezaji wa viwanda vya samaki vilivyopo Mkoani Mwanza kuhakikisha wanatumia usafiri wa ndege kutoka katika kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Mwanza kusafirisha minofu ya samaki ili kutangaza bidhaa zinazotengezwa hapa Tanzania.

“Tungependa kuona usafirishaji wa minofu ya samaki unafanyika hapa nchini kwetu, badala ya nchi jirani kwa kusafirisha kwa malori kwenda nchi za jirani, kuna uwekezekano kabisa wa kutoa minofu ya samaki kutoka kiwanja cha ndege cha Mwanza kwenda nje ya nchi badala ya kutumia nchi za jirani.” Amefafanua Mhe. Ndaki

Aidha, amewataka wawekezaji wa viwanda vya samaki kuangalia namna ya kuongeza bei ya kununulia samaki kwa wavuvi wanaopeleka samaki katika viwanda hivyo ili wavuvi hao waweze kubadilisha maisha yao na kunufaika kupitia Sekta ya Uvuvi.

Waziri Ndaki amebainisha hayo baada ya Meneja Mkuu wa Kiwanda cha kuchakata samaki cha Nile Perch Bw. Rupesh Mohan kumueleza Waziri Ndaki na Naibu Waziri Gekul kuwa viwanda vya samaki vimekuwa vikikosa malighafi ya kutosha kutokana na soko la ndani kukua na wakati mwingine kupata samaki kwa bei ya juu, hali iliyomlazimu Waziri Ndaki kubainisha kuwa kama bei ya soko la ndani imepanda ni dhahiri wavuvi watauza samaki katika soko hilo badala ya kupeleka viwandani ambapo wanauza kwa bei ndogo.

Hivyo amevitaka viwanda vya kuchakata samaki kuangalia upya bei ya samaki wanayonunua ili wavuvi nao waweze kunufaika na kuboresha maisha yao na viwanda pia viweze kupata malighafi za kutosha.

Pia, Waziri Ndaki ametembelea kiwanda cha kukausha mabondo ya samaki cha Hong Lin International Ltd kilichopo Wilaya ya Ilemela jijini Mwanza na kufurahishwa na kiwanda hicho kwa kutumia kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Mwanza kusafirisha bidhaa zake kwenda nchi za nje.

Naye Mkurugenzi wa kiwanda hicho Bi. Wang Shenghong ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji hali inayomuwezesha kufanya shughuli zake bila matatizo huku akiomba pia baadhi ya tozo zipunguzwe.

Katika siku ya kwanza ya ziara yake Mkoani Mwanza, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki akiwa na Naibu Waziri Mhe. Pauline Gekul wametembelea pia Maabara ya Taifa ya Uvuvi, Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi nchini (FETA) na Kituo cha Ulinzi wa Rasilimali za Uvuvi (FRP).


Share:

VIWANDA KUONDOA UMASIKINI WA WAFUGAJI NA WAVUVI

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (wa pili kutoka kushoto), akiwa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Pauline Gekul (wa pili kutoka kulia) pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Uvuvi Dkt. Rashid Tamatamah (wa kwanza kutoka kushoto), wakati Waziri Ndaki alipofanya ziara ya kikazi katika kiwanda cha kuchakata samaki cha Nile Perch kilichopo kata ya Nyakato, Wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki (wa kwanza kutoka kushoto), akiwa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Pauline Gekul (anayemfuata) pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Uvuvi Dkt. Rashid Tamatamah (wa kwanza kutoka kulia), wakati Waziri Ndaki alipofanya ziara ya kikazi katika kiwanda cha kukausha mabondo ya samaki cha Hong Lin International Ltd kilichopo Wilaya ya Ilemela, jijini Mwanza.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki na Naibu Waziri wa wizara hiyo Mhe. Pauline Gekul wakiangalia mabondo ya samaki baada ya kukaushwa tayari kwa ajili ya kusafirishwa kwenda nje ya nchi, wakati walipofanya ziara ya kikazi katika kiwanda cha kukausha mabondo ya samaki cha Hong Lin International Ltd kilichopo Wilaya ya Ilemela, jijini Mwanza. Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki akiwa na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Pauline Gekul wakati walipofanya ziara ya kikazi katika Maabara ya Taifa ya Uvuvi iliyopo Kata ya Nyegezi Wilaya ya Nyamagana Mkoani Mwanza na kushuhudia namna maabara hiyo inayofanya kazi kwa kufanyia uchunguzi sampuli za samaki kutoka viwandani. Wa kwanza kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Uvuvi Dkt. Rashid Tamatamah.

**********************************************

Na. Edward Kondela

Serikali imesema itahakikisha sekta za mifugo na uvuvi zinawaondoa wananchi katika umasikini, kupata ajira na nchi iweze kuuza bidhaa bora za mazao ya mifugo na uvuvi ndani na nje ya nchi.

Akizungumza jana (28.12.2020) katika siku yake ya kwanza ya ziara ya kikazi ya siku mbili Mkoani mwanza, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki wakati akihitimisha ziara hiyo kwenye kiwanda cha kuchinja na kuchakata nyama cha Chobo kilichopo Kata ya Usagara Wilaya ya Misungwi amesema wizara imekuwa ikichukulia kwa uzito mkubwa suala la viwanda ambalo litaweza kubadilisha fikra za wafugaji na wavuvi.

“Wananchi wetu waondoe umasikini, wananchi wetu wapate ajira na sisi tuuze bidhaa za mazao haya ya mifugo na uvuvi yaliyo bora hapa ndani na kule kwa wenzetu nje, sasa mimi nikikuta hali ya mkwamo kwa kitu ambacho kinatusaidia kuelekea huko napata shida.” Amesema Mhe. Ndaki

Waziri Ndaki akifuatana na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Pauline Gekul katika ziara hiyo amefafanua kuwa haridhishwi na baadhi ya changamoto wanazokutana nazo wawekezaji ambao wamejikita katika kuyaongezea thamani mazao ya mifugo na uvuvi na kumuagiza Kaimu Msajili wa Bodi ya Nyama nchini Bw. Iman Sichalwe kumpatia taarifa ya hali ya viwanda vya nyama nchini ili apate tathmini halisi ya utendaji kazi wa viwanda hivyo, baada ya Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda cha Chobo, Bw. John Chobo kubainisha baadhi ya changamoto ambazo Waziri Ndaki amesema wizara itahakikisha inafuatilia changamoto zinazoihusu wizara hiyo ili kuzipatia majibu.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa kiwanda hicho Bw. John Chobo amesema kwa sasa kiwanda chake kimesimamisha uzalishaji na kinatarajia kuanza kurejea katika shughuli zake Mwezi Januari Mwaka 2021 baada ya ugonjwa wa Covid 19 kuathiri shughuli za kiwanda hicho ambacho kimekuwa kikisambaza nyama katika nchi za falme za kiarabu.

Bw. Chobo amesema kutopatikana kwa taarifa sahihi za mifugo kumekuwa kukichangia kwa kiasi kikubwa soko la nyama kutoka Tanzania kwenda nje ya nchi kuwekwa katika daraja la chini kwa kuwa mifugo mingi ambayo inachakatwa viwandani haina taarifa sahihi juu ya ukuaji wake, magonjwa na chanjo mbalimbali ambazo mfugo huo umepatiwa.

Akiwa katika Kiwanda cha kuchakata samaki Nile Perch kilichopo eneo la viwanda katika Kata ya Nyakato Wilaya ya Nyamagana jijini Mwanza, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki akiambatana na Naibu Waziri Mhe. Pauline Gekul amewataka wawekezaji wa viwanda vya samaki vilivyopo Mkoani Mwanza kuhakikisha wanatumia usafiri wa ndege kutoka katika kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Mwanza kusafirisha minofu ya samaki ili kutangaza bidhaa zinazotengezwa hapa Tanzania.

“Tungependa kuona usafirishaji wa minofu ya samaki unafanyika hapa nchini kwetu, badala ya nchi jirani kwa kusafirisha kwa malori kwenda nchi za jirani, kuna uwekezekano kabisa wa kutoa minofu ya samaki kutoka kiwanja cha ndege cha Mwanza kwenda nje ya nchi badala ya kutumia nchi za jirani.” Amefafanua Mhe. Ndaki

Aidha, amewataka wawekezaji wa viwanda vya samaki kuangalia namna ya kuongeza bei ya kununulia samaki kwa wavuvi wanaopeleka samaki katika viwanda hivyo ili wavuvi hao waweze kubadilisha maisha yao na kunufaika kupitia Sekta ya Uvuvi.

Waziri Ndaki amebainisha hayo baada ya Meneja Mkuu wa Kiwanda cha kuchakata samaki cha Nile Perch Bw. Rupesh Mohan kumueleza Waziri Ndaki na Naibu Waziri Gekul kuwa viwanda vya samaki vimekuwa vikikosa malighafi ya kutosha kutokana na soko la ndani kukua na wakati mwingine kupata samaki kwa bei ya juu, hali iliyomlazimu Waziri Ndaki kubainisha kuwa kama bei ya soko la ndani imepanda ni dhahiri wavuvi watauza samaki katika soko hilo badala ya kupeleka viwandani ambapo wanauza kwa bei ndogo.

Hivyo amevitaka viwanda vya kuchakata samaki kuangalia upya bei ya samaki wanayonunua ili wavuvi nao waweze kunufaika na kuboresha maisha yao na viwanda pia viweze kupata malighafi za kutosha.

Pia, Waziri Ndaki ametembelea kiwanda cha kukausha mabondo ya samaki cha Hong Lin International Ltd kilichopo Wilaya ya Ilemela jijini Mwanza na kufurahishwa na kiwanda hicho kwa kutumia kiwanja cha ndege cha kimataifa cha Mwanza kusafirisha bidhaa zake kwenda nchi za nje.

Naye Mkurugenzi wa kiwanda hicho Bi. Wang Shenghong ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuweka mazingira mazuri ya uwekezaji hali inayomuwezesha kufanya shughuli zake bila matatizo huku akiomba pia baadhi ya tozo zipunguzwe.

Katika siku ya kwanza ya ziara yake Mkoani Mwanza, Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki akiwa na Naibu Waziri Mhe. Pauline Gekul wametembelea pia Maabara ya Taifa ya Uvuvi, Wakala ya Elimu na Mafunzo ya Uvuvi nchini (FETA) na Kituo cha Ulinzi wa Rasilimali za Uvuvi (FRP).

Share:

Various Posts at Good Neighbors International (GNI) Tanzania

Jobs in Tanzania 2021: New Jobs Opportunities at Good Neighbors Tanzania  2021 Overview Good Neighbors International (GNI) is an international humanitarian and development organization with Headquarter based in Seoul, the Republic of Korea. It is in General Consultative Status with the United Nations Economics and Social Council (UNECOSOC). The Mission/Vision of GNI works to transform […]

The post Various Posts at Good Neighbors International (GNI) Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger