Sunday 1 November 2020

POLISI SHINYANGA WAONYA WATAKAOTHUBUTU KUANDAMANA KUPINGA MATOKEO YA UCHAGUZI


Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga Debora Magiligimba 

Na Marco Maduhu- Shinyanga.
Jeshi  la Polisi mkoani Shinyanga, limewaonya viongozi wa vyama vya siasa pamoja na wafuasi wao, wasijaribu kufanya maandamano ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 28 mwaka huu ,bali waende mahakamani kupinga matokeo hayo.

Kamanda wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga Debora Magiligimba ametoa onyo hilo leo Jumapili Novemba 1,2020 wakati akizungumza na waaandishi wa habari.

Amesema kuwa kuna matamko yametolewa na viongozi wa kisiasa kutaka kufanya maandamano yasiyo na kikomo nchi nzima na kuanzia kesho ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu.

Kamanda Magiligimba amesema maandamano hayo ni batili, ambapo viongozi hao walipaswa kufuata sheria kwa kupinga matokeo hayo mahakamani, na siyo kufanya maandamano ambayo yana viashiria vya uvunjifu wa amani.

"Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga halitasita kamwe kuchukua hatua kali za kisheria, kwa kikundi chochote kile cha kisiasa chenye nia ya kuvuruga amani ya nchi," amesema Magiligimba.

"Kama wagombea hawajaridhika na matokeo ya uchaguzi mkuu wafuate sheria ,kanuni, na taratibu za nchi na kupeleka malalamiko yao Mahakamani na siyo kufanya maandamano ya bila kikomo yenye viashiria ya uvunjifu wa amani," ameongeza.

Pia amewataka wananchi wa mkoa wa Shinyanga kutojiingiza kwenye maandamano hayo, bali waendelee na shughuli zao za kila siku za kujiingizia kipato ,na wasiwe na hofu ikiwa ulinzi utaimarishwa kila kona.

Katika hatua nyingine amewaomba viongozi wa dini, kuendelea kusisitiza umuhimu wa amani kwa waumini wao,ili kuendelea kuilinda amani ya nchi iliyopo hivi sasa.

Share:

NEC YAMKABIDHI MAGUFULI CHETI CHA USHINDI KITI CHA URAIS TANZANIA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akionesha Cheti cha Ushindi wa Kiti cha Urais alichokabidhiwa na Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage mara baada ya kutangazwa mshindi kwa Kiti cha Urais katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipokea Cheti cha Ushindi wa Kiti cha Urais kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage mara baada ya kutangazwa mshindi kwa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020, hafla hiyo ya kukabidhiwa Cheti imefanyika katika Makao Makuu ya Tume ya Uchaguzi NEC Njedengwa jijini Dodoma leo tarehe 01 Novemba 2020.
Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akipokea Cheti cha Ushindi wa Kiti cha Makamu wa Rais kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli kutangazwa mshindi kwa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Kiongozi wa Jopo la Waangalizi wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020 Rais Mstaafu wa Burundi Silvestre Ntibantunganya mara baada ya kukabidhiwa Cheti cha Ushindi wa Kiti cha Urais kutoka kwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jaji Mstaafu Semistocles Kaijage leo tarehe 01 Novemba 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa amesimama na Waliogombea Urais kupitia vyama Mbalimbali vya Upinzani nchini wakati Wimbo wa Taifa ukipigwa katika hafla fupi ya kukabidhi Cheti cha Ushindi kwa Kiti cha Urais zilizofanyika katika Makao Makuu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC Njedengwa jijini Dodoma leo tarehe 01 Novemba 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimpongeza Makamu wa Rais Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan mara baada ya kukabidhiwa Cheti cha Ushindi kwa Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wageni mbalimbali waliofika katika hafla fupi ya kukabidhiwa Cheti cha Kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020.
Share:

Dkt. Magufuli na Dkt. Mwinyi kuapishwa wiki ijayo


 Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa, Itikadi na Uenezi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Humphrey Polepole amesema shughuli ya kuapishwa kwa Rais Mteule wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Dkt. Hussein Mwinyi na Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano, Dkt. John Magufuli zitafanyika wiki ijayo.

Akizungumza na waandishi wa habari katika ofisi ndogo za chama hicho jijini Dar es Salaam Polepole amesema Dkt. Mwinyi ambaye alishinda katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 28, 2020 ataapishwa Novemba 2, 2020 katika Uwanja vya Amani Zanzibar kuwa Rais wa awamu ya nane wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar baada ya rais Dkt. Ali Mohamed Shein kumaliza muda wake.

Siku mbili zimepita tangu Tume ya ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kumtangaza Dkt. Mwinyi kuwa mshindi wa kiti cha urais kwa kujipatia kura 380,02 sawa na asilimia 76.27 ya kura zote halali.

Kwa upande wa Rais Mteule wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli, Polepole amebainisha kuwa shughuli ya kuapishwa kwake kuongoza dola kwa muhula itafanyika Novemba 5, 2020 katika Uwanja wa Jamhuri Dodoma.

Dkt. Magufuli alitangazwa kuwa mshindi baada ya kupata kura 12,516,252 sawa na asilimia 84.4 ya kura zote halali.

Katibu mkuu huyo amewashukuru Watanzania wote kwa kuendelea kukiamini Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kukipatia ushindi wa kishindo, hivyo kuwataka kujitokeza kwa wingi katika matukio hayo muhimu la kuapishwa kwa viongozi wateule
.

Share:

Polisi yatoa onyo wanaotaka kuandamana


Kamishna wa Operesheni na Mafunzo, CP Liberatus Sabas, amesema kuwa jeshi la polisi halitamvumilia mtu yeyote awe kiongozi wa chama au mfuasi, atakayefanya maandamano batili na kama kuna yeyote ambaye hakuridhika na matokeo afuate taratibu za kisheria kudai haki zao kama zipo.

CP Sabas ametoa kauli hiyo hii  Oktoba 31,2020, na kuwasihi akina mama kuongea na watoto wao kwamba, wasithubutu kushiriki katika maandamano hayo na wasije wakarubuniwa na watu ambao hawana nia nzuri na Taifa.

"Nasisitiza kwamba jeshi la polisi halitakuwa na simile kwa yeyote atakayejihusisha na chokochoko hizi ambazo tunaziona zinaanza kuanzishwa na watu hawa ambao hawalitakii mema Taifa hili, nawaomba akina mama mkanye mwanao kwa sababu mwisho wa siku mtoto atakapopata matatizo atakulilia mama, sasa kabla matatizo hayajamfika nakuomba mkanye mwanao", amesema CP Sabas.


Share:

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Aboubakar Kunenge atoa onyo kwa waliopanga kufanya vurugu Dar


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Aboubakar Kunenge ametoa onyo kwa watu au vikundi vya watu vilivyopanga kufanya vurugu mkoani kwake na kueleza kuwa sheria itachukua mkondo wake kwa yeyote atakayejaribu kuvuruga amani.

Kunenge ametoa onyo hilo wakati wa Uzinduzi wa Baraza la Wafanyakazi wa Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC).

Mkuu huyo wa mkoa ameongeza kuwa jiji lipo kwenye hali ya amani na utulivu huku usalama ukiwa umeimarishwa
.

Share:

RC SHIGELLA APIGA MARUFUKU MAANDAMANO NA MIKUSANYIKO

MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella akizungumza
madereva wa pikipiki maarufu bodaboda waliokusanyika kwa ajili ya kumpongeza Rais Dkt John Magufuli kwa kuchaguliwa tena kuongoza Tanzania kwa kipindi kingine cha miaka mitano kushoto Katibu wa kikundi cha Tanga One cha wilaya ya Tanga  Omari Ahmed
MKUU wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella akizungumza
madereva wa pikipiki maarufu bodaboda waliokusanyika kwa ajili ya kumpongeza Rais Dkt John Magufuli kwa kuchaguliwa tena kuongoza Tanzania kwa kipindi kingine cha miaka mitano kushoto Katibu wa kikundi cha Tanga One cha wilaya ya Tanga  Omari Ahmed
Mkuu wa Mkoa wa Tanga Martine Shigella kulia akiteta jamboi na viongozi waendesha pilkipiki bodaboda Jijini Tanga cha Tanga One wakati akipokea maandamano yao waliokusanyika uwanja wa Lamore kwa ajili ya kumpongeza Rais Dkt John Magufuli kwa kupata ushindi katika uchaguzi mkuu uliofanyika Octoba 28 mwaka huu
KATIBU Mwenezi wa CCM wilaya ya Tanga Lupakisyo Kapange akizungumza


MKUU wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigella amepiga marufuku aina yoyote ya maandamano na mikusanyiko huku akiwataka wananchi kuendelea kujikita kwenye shughuli za kimaendeleo kwa maslahi mapana ya Taifa kutokana na kwamba uchaguzi umekwisha na walioshindwa wakubali matokeo.

RC Shigella aliyasema hayo wakati madereva wa pikipiki maarufu bodaboda waliokusanyika kwa ajili ya kumpongeza Rais Dkt John Magufuli kwa kuchaguliwa tena kuongoza Tanzania kwa kipindi kingine cha miaka mitano.

Alisema kwamba amepokea maandamano hayo ili atumie nafasi hiyo kuwatangazia wananchi kwamba serikali hairuhusu mikusanyiko yoyote katika kipindi hiki ambacho uchaguzi umemalizika.

Hatua ya Mkuu huyo wa Mkoa kupiga marufuku maandamano au mikusanyiko yoyote imekuja kutokana na uwepo wa tetesi kwamba wafuasi wa baadhi ya vyama vya upinzani wanaandaa maandamano ya kupinga matokeo ya uchaguzi huo.

Awali akisoma risala ya umoja wa waendesha bodaboda kikundi cha Tanga One cha wilaya ya Tanga iliyosomwa na Katibu wao Omari Ahmed alisema wanampongeza Rais Dkt John Magufuli kwa ushindi walioupata na kwamba wana matumaini kwamba sasa wana uhakika wa kufanya kazi zao kwa utulivu.

Alisema wanampongeza kwa dhati Rais Magufuli kwa kuibuka na ushindi wa kishindo kwani walikuwa wanamuombea kila wakati katika mchakato huo wa kuwania nafasi hiyo.

“Lakini tunapongeza vyombo vya ulinzi na usalama kwa kuhakikisha amani ya Taigfa inakuwa shwari wakati wote huu wa uchaguzi na umekwisha sasa tunaangalia maendeleo zaidi na kauli mbiu ya Rais Dkt Magufuli hapa kazi tu”Alisema

Hata hivyo alisema wao bodaboda kwa niaba ya wenzao wanaombi kwa Rais wanaomba aendelee kuwakumbuka watu wa Tanga huku wakiomba wakati akiapishwa waalikwe watu 10 wa bodaboda waende kushuhudia tukio hilo.

Share:

Electronics Technician at Fastlink Safaris

Electronics Technician Fastlink Safaris Engineering & Technology Dar es Salaam|Full Time IT & Telecoms Job Summary We are looking for electronic technicians for our mobile repair shops to set up, maintain, and repair electronic systems and devices. Minimum Qualification: Diploma Experience Level: Entry level Experience Length: 1 year Job Description This role requires hands-on experience […]

The post Electronics Technician at Fastlink Safaris appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Site Roll Out Manager at TIGO Tanzania

Site Roll Out Manager Job Country: Tanzania JOB PURPOSE To deliver a steady throughput of on air sites to the Head of Operations within a specified budget and according to specifications following MIC policies and processes that are given to the network roll out team. WE LEAD AND CONTRIBUTE. by connecting, by owning, by delivering, by […]

The post Site Roll Out Manager at TIGO Tanzania appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Finance Manager at Natural Extracts Industries

Finance Manager Natural Extracts Industries Ltd Accounting, Auditing & Finance Arusha & Moshi|Full Time Manufacturing & Warehousing Job Summary NEI is looking for a Finance Manager to oversee overall finance operations and liaising with senior stakeholders such as Board Directors Minimum Qualification: Bachelor Experience Level: Senior level Experience Length: 6 years Job Description Overall responsibility […]

The post Finance Manager at Natural Extracts Industries appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Customer Service Agents at WinPrincess

CUSTOMER SERVICE AGENTS POSTS(4) JOB Description Handling and replying to customer inquiries through live chats, phone calls, social media interaction with customers Maintaining customer relations. Providing feedback to Supervisor/ Head on customer’s needs/feedbacks.  Preparing and generating reports/relating customer’s queries.  Researching into customer’s queries/concerns into the systems. Assist players with specifics about promotions, loyalty programs, and […]

The post Customer Service Agents at WinPrincess appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Portfolio and Analytics Manager at Standard Chartered Bank

Portfolio and Analytics Manager Standard Chartered Bank Dar es Salaam, Dar es Salaam, Tanzania About Standard Chartered We are a leading international bank focused on helping people and companies prosper across Asia, Africa and the Middle East. To us, good performance is about much more than turning a profit. It’s about showing how you embody […]

The post Portfolio and Analytics Manager at Standard Chartered Bank appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Manager Alliance and Partnerships at Standard Chartered Bank

Manager Alliance and Partnerships Standard Chartered Bank Dar es Salaam, Dar es Salaam, Tanzania About Standard Chartered We are a leading international bank focused on helping people and companies prosper across Asia, Africa and the Middle East. To us, good performance is about much more than turning a profit. It’s about showing how you embody […]

The post Manager Alliance and Partnerships at Standard Chartered Bank appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Senior Sales Manager at Standard Chartered Bank

Senior Sales Manager Standard Chartered Bank Dar es Salaam, Dar es Salaam, Tanzania About Standard Chartered We are a leading international bank focused on helping people and companies prosper across Asia, Africa and the Middle East. To us, good performance is about much more than turning a profit. It’s about showing how you embody our […]

The post Senior Sales Manager at Standard Chartered Bank appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

MARUCO second round selected applicants 2020/2021

The Marian University College MARUCO second round selected applicants 2020/2021 are the names of students who have passed the Second-round admission selection stage and successfully approved by TCU to join undergraduate studies at Marian University College (MARUCO) for the 2020/2021 academic year second round application window. The Marian University College MARUCO second round applications and […]

The post MARUCO second round selected applicants 2020/2021 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

LIVE: Rais Mteule Wa Tanzania, Dkt. Magufuli Akikabidhiwa Cheti Cha Ushindi Wa Uchaguzi Mkuu


Rais Mteule Wa Tanzania, Dkt. Magufuli Akikabidhiwa Cheti Cha Ushindi Wa Uchaguzi Mkuu


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili Novsmber 01



Share:

Saturday 31 October 2020

Tanzia : MUIGIZAJI MAARUFU WA FILAMU YA JAMES BOND AFARIKI DUNIA

James Bond
Sir Sean Connery, muigizaji wa sinema ya James Bond amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 90, familia yake imethibitisha.

Muigizaji huyo wa Uskochi alifahamika sana kwa kuwa mhusika wa katika sinema ya James Bond, na alikuwa wa kwanza kuleta sinema hiyo katika ukumbi wa sinema.

Wasanii tofauti wameigiza nafasi ya James Bond katika filamu kadhaa, lakini mcheza sinema gwiji, Sean Connery, ndiye aliyecheza nafasi hiyo kwa mara ya kwanza.

Jason Connery, mtoto wa kiume wa nyota huyo aliyependwa na Waingereza wengi, amesema baba yake amefariki kwa amani akiwa usingizini mjini Nassau katika visiwa vya Bahamas, ambako ana nyumba yake, baada ya hali yake kutokuwa nzuri kwa muda mrefu.

"Wote tunafanyia kazi kuelewa tukio hili kubwa kwa kuwa ndio kwanza limetokea," aliongeza, akielezea kifo cha baba yake kuwa ni "pigo kwa watu wote duniani ambao walifurahia zawadi aliyokuwa nayo kama muigizaji.

Hafla ya heshima za mwisho kwa Connery itakayofanyika baadaye, kwa mujibu wa ofisa habari wake.

Kazi yake ya uigizaji wa miongo mitano ilimwezesha kushinda tuzo ya Oscar mwaka 1988 kutokana na jukumu lake katika 'The Untouchable'.

Filamu zingine alizoigiza Sir Sean ni pamoja na The Hunt for Red October, Highlander, Indiana Jones na the Last Crusade and The Rock.

Jason Connery alisema baba yake "alikuwa na sehemu kubwa ya familia yake Bahamas ambayo ilikuwa naye" alipofariki usiku mjini Nassau.

Alisema: "Sote tunajaribu kukubaliana na msiba huu mkubwa kwani limetokea sasa, ingawa baba yangu amekuwa mgonjwa kwa muda.

"Ni siku ya huzuni kwa watu wate waliomfahamu baba yetu mpendwa na watu wote waliovutiiwa na uigizaji wake kote duniani.

Sir Sean, anayetokea Fountainbridge, Edinburgh aliigiza filamu ya first James Bond mwaka 1962 na kuendelea mbele na kuigiza filamu zingine tano rasmi - na zingine ambayo sio rasmi kama vile Never Say Never Again mwaka 1983.

Aliamminiwa na watu wengi kuwa muigizaji mahiri ambaye aliigiza 007 kwa muda mrefu, akiitwa majina hayo.

Alikabidhiwa tuzo ya knigh na Malikia Queen katika Holyrood Palace mwaka 2000. Mwezi Augosti, alisherehekea mwaka wa 90 wa siku yake ya kuzaliwa.
Aliunga mkono kwa muda mrefu uhuru wa Uskochi, akisema hayo katika mahojiano kuelekea kura ya maoni ya mwaka 2014 na kugusia kwamba huenda akarejea nyumbani kutoka Bahamas na kuishi Scotland inadapo itapiga kura kujitenga na Uingereza.

Waziri wa Kwanza wa Scotland Nicola Sturgeon amesema: "Nimevunjika moyo kupokea taarifa za kifo cha Sir Sean Connery. taifa letu linaomboleza kwa kumpoteza mpendwa wetu.

Mcheza filamu huyo, ambaye pia alipewa na malkia wa Uingereza heshima ya kuwa Sir mwaka 2000, alitwaa tuzo kadhaa wakati wa kipindi cha uigizaji wake kilichodumu kwa miongo, zikiwemo tuzo za Oscar, Golden Globes na Bafta.

Lakini ilikuwa ni sinema maarufu ya 007, aliyoigiza akitumia Kiingereza chenye lafudhi ya Scotland akiigiza kama mpelelezi aliyekuwa na leseni ya kuua, iliyompatia umaarufu mkubwa duniani kote.

Alikuwa ni muigizaji wa kwanza kutoa maneno yasiyosahaulika ya "Bond, James Bond" na aliigiza filamu sita zilizotokana na mtunzi wa vitabu vya hadithi, Ian Fleming.

"Alikuwa na siku zote ataendelea kukumbukwa kama James Bond halisi," walisema watayarishaji filamu maarufu, Michael G. Wilson na Barbara Broccoli.

Mara kadhaa , mcheza sinema huyo kutoka Scotland alipigiwa kura na mashabiki ya kuwa muigizaji bora wa nafasi ya Bond, akiwashinda waigizaji wengine kama Daniel Craig wa sasa na Roger Moore.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger