Sunday 25 October 2020

Benard Membe Azungumzia Kuhusu Barua Inayosambaa Mitandaoni


Mgombea wa Urais kupitia chama cha ACT Wazalendo, Bernard Membe, ametoa sababu ya kuandika barua iliyokuwa ikisambaa mitandaoni ikieleza kuhusu kujitoa kwenye kinyanganyiro cha Urais wa Tanzania bara.


Membe kupitia ukurasa wake wa Twitter leo, amethibitisha kuwa barua hiyo iliyosambaa mitandaoni kuwa ni ya kweli na yeye ndiye aliyeandika barua hiyo.

“Barua inayosambaa ya tarehe 24/9 ya kujiondoa kwenye mbio za Urais ni ya kweli, niliandika baada ya kutofautiana na msimamo wa Viongozi wangu wa kutaka nimuunge mkono Tundu Lissu. Hata hivyo barua hiyo ilikataliwa kwa sababu maneno " msimamo wa viongozi wangu" yanawatia hatiani.” amesema Bernard Membe

Aidha katika barua hiyo inayosambaa iliyoelekezwa kwa mwenyekiti wa chama hicho Maalim Seif, na Katibu Mkuu wa cha hicho , Membe aliahidi kujikita katika kuwasaidia madiwani na wabunge wote wa chama hicho.
 





Share:

Majaliwa: Sh. Bilioni 5.26 Zanunua Dawa Lindi


MJUMBE wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Kassim Majaliwa amesema katika kipindi cha miaka mitano, Serikali imetumia sh. bilioni 5.26 kwa ajili ya ununuzi wa dawa kwenye Manispaa ya Lindi.

“Serikali imetoa shilingi bilioni 5.26 ambapo kati ya hizo, shilingi bilioni 4 zilikuwa za Hospitali ya Rufaa ya Sokoine na shilingi bilioni 1.26 zilitolewa kwa Halmashauri ya Manispaa ya Lindi kwa ajili ya ununuzi wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi. Fedha za ununuzi wa dawa kwa mwezi, ni wastani wa shilingi milioni 21,” alisema.

Ametoa kauli hiyo jana (Jumamosi, Oktoba 24, 2020) wakati akizungumza na wakazi wa mji wa Lindi na vitongoji vyake waliofurika kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika jana kwenye uwanja wa Ilulu mjini Lindi.

Akielezea kuhusu uboreshaji wa sekta ya afya, Mheshimiwa Majaliwa alisema katika Manispaa ya Lindi, kuna magari matano ya kubeba wagonjwa kwa ajili ya vituo vya afya Mjini, Mnazimmoja, Kitomanga, Milola na Rutamba.

Mheshimiwa Majaliwa ambaye yuko mkoani Lindi kumuombea kura mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dkt. John Pombe Magufuli, alitumia fursa hiyo kuwanadi mgombea ubunge wa jimbo la Lindi, Bi. Hamida Abdallah na wagombea udiwani wa kata 20 za jimbo hilo.

Kuhusu sekta ya maji, alisema sh. bilioni 50 zimetolewa kwa ajili ya miradi mikubwa ya maji ikiwemo ujenzi wa skimu ya pampu Mtutu, skimu ya pampu Cheleweni, Narunyu, Tandangongoro na Muungano na kwamba zimesaidia kuongeza upatikanaji wa maji kwenye mji wa Lindi.

“Fedha hizo zimetumika pia kwa ajili ya mradi wa maji safi na usafi wa mazingira Lindi Mjini (Mradi wa Maji Ng'apa) na kwenye mradi wa maji Ng'apa kijijini na usambazaji mtandao wa mabomba,” alisema.

Alisema sh. bilioni 1.26 zilitolewa kwa ajili ya miradi mingine ya maji ikiwemo ya kuchimba visima virefu katika maeneo ya Jangwani, Nanyanje, Kitumbikwela, Nachingwea, Kitunda, Likotwa, Mtange, Tulieni, Mitumbati, Mayani na Ngongo-Nanenane.

Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Majaliwa alisema mkoa wa Lindi utanufaika zaidi kwa sababu Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kimeamua kuanzisha kitivo cha kilimo mkoani humo. “Taratibu zimeshakamilika na tumewapa ekari 150 katika eneo la Ngongo ili waweze kujenga kitivo cha kilimo,” alisema.

Leo Mheshimiwa Majaliwa anaendelea na kampeni kwenye jimbo la Liwale.

(mwisho)


Share:

SERIKALI YAKABIDHI BAISKELI 103 KWA WAHUDUMU WA AFYA IKUNGI

 

 Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Edward Mpogolo akikabidhi usafiri wa Baiskeli na Vipaza sauti kwa Wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii wilayani hapo juzi kama nyenzo muhimu zitakazowasaidia. kurahisisha utekelezaji wa majukumu yao.

Hafla ya makabidhiano ikiendelea.
Afisa Lishe na Mratibu wa Huduma za Jamii wilayani hapo, Agnes John akisoma taarifa fupi ya Mradi wa Boresha Lishe kwenye Halmashauri ya Ikungi.
Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii wakiwa na baiskeli na vipaza sauti muda mfupi baada ya kukabidhiwa.
Mwonekano wa Baiskeli hizo.

Mkuu wa Wilaya Mpogolo akiendesha hafla hiyo.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Ikungi (DAS), Winfrida Funto (katikati) akifuatilia kwa makini makabidhiano hayo, kulia ni Afisa Tarafa, Josephine Kadaso na DC Mpogolo.

Hafla ikiendelea.

Afisa Mradi wa Boresha Lishe kutoka shirika la SEMA, Hudson Kazonte akizungumzia tija ya mradi huo na namna usafiri huo wa baiskeli utakavyopunguza changamoto ya utoaji huduma.


Na Godwin Myovela, Ikungi

SERIKALI kwa kushirikina na Umoja wa Nchi za Ulaya na Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) imetoa jumla ya baiskeli 103 kwa wahudumu wote wa afya ngazi ya jamii sambamba na ‘vipaza sauti’ vyenye idadi kama hiyo wilayani hapa, lengo ni kuwapunguzia changamoto ya usafiri wakati wakitekeleza majukumu yao.

Katika kuboresha afya ya uzazi na lishe, kupitia mradi wa ‘Boresha Lishe’ serikali kupitia halmashauri ya Ikungi kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, wakiwemo mashirika yasiyo ya kiserikali ya ‘SEMA’ na ‘RECODA’ imeazimia kupunguza udumavu wa siku 1000 za mtoto-yaani tangu kutungwa kwa mimba hadi anapofikisha miaka 2.

Akizungumza katika hafla ya kukabidhi baiskeli hizo ofisini kwake jana, Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Edward Mpogolo aliwataka waliokabidhiwa baiskeli hizo kuhakikisha wanazitunza na zinatumika kwa malengo kusudiwa.

“Niwasihi muwe waangalifu na mzitunze baiskeli hizi, serikali itaendelea kuweka mazingira rafiki kwenye sekta ya afya hususani kwenye eneo hili la afya ya uzazi na lishe, azma ikiwa ni kuhakikisha tunaondoa kabisa kiwango cha utapiamlo wa udumavu kutoka asilimia 7 mpaka 0,” alisema Mpogolo.

Aidha, aliyashukuru mashirika na nchi wahisani wanaoendelea kushirikiana na serikali katika kutekeleza mradi wa Boresha Lishe kwa vijiji 43 kuzunguka Ikungi huku akisisitiza ni mradi wenye tija kwa makundi yote ya jamii wilayani hapo, na hasa akinamama wajawazito, wanaonyonyesha na watoto chini ya miaka miwili.

Naye Afisa Lishe na Mratibu wa Huduma za Jamii wilayani hapo, Agnes John, alisema Halmashauri ya Ikungi ina jumla ya Kata 28 na Vijiji 101 vyote vina wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii, na wote wamepatiwa mafunzo ya msingi ya awali ya afya ya uzazi na lishe.

Halmashauri ya Ikungi ina jumla ya wakazi 329,520, ambapo watoto chini ya miaka mitano ni 58,707, na wanawake wenye umri wa kuzaa (miaka 15-49) wanafikia 22,884.

“Mafanikio tuliyoyapata mpaka sasa ni kujikwamua mapema kwenye rangi nyekundu, kwa miaka miwili mfululizo mpaka sasa viashiria vyote vinavyohusiana na huduma za wahudumu wa afya ngazi ya jamii vina alama ya kijani kuashiria tunafanya vizuri,” alisema John.

Aidha, mratibu huyo alisema hata kiwango cha utapiamlo wa udumavu kimepungua kutoka asilimia 7 mpaka asilimia 5, wakati kimkoa ni asilimia 29.8. Alisema ukondefu umepungua kutoka asilimia 1 hadi kufikia 0.4, wakati kimkoa ni asilimia 4.7.

 

Share:

MGOMBEA URAIS DK. MAGUFULI ANAENDELEA NA KAMPENI ZA UCHAGUZI LEO MANYARA

Tukiwa na siku 2 kuelekea Jambo letu, kazi ya Kuendelea na kukutana na Wananchi wa Kila sehemu kueleza Sera na Ilani bora ya CCM inaendelea na Leo Oktoba 25, 2020 Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli ataunguruma Mkoani Manyara. Watanzania tuna Jambo Letu haswa.

#KuraKwaMagufuli2020
#T2020JPM

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi October 25
















Share:

Saturday 24 October 2020

LIVE: Rais Magufuli Akizindua Safari Za Treni Dsm - Tanga -Arusha.


 LIVE: Rais  Magufuli Akizindua Safari Za Treni Dsm - Tanga -Arusha.




Share:

Nchi Za Afrika Zahimizwa Kushikamana Ili Kuondokana Na Utegemezi


Nchi za Afrika zimehimizwa kushikamana katika masuala ya maendeleo, biashara na uwekezaji ili kuondokana na utegemezi jambo litakaloliwezesha Bara hilo kufanya mambo yake kwa uhuru bila kuingiliwa na mataifa mengine ya nje kwa kisingizio cha demokrasia na haki za binadamu.
Kauli hiyo imetolewa Jijini Dar es Salaam na Kiongozi wa Mabalozi wa nchi za Afrika hapa Tanzania Dkt. Ahamada El Badaoui Mohamed wakati Mabalozi hao walipokutana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi ikiwa ni utaratibu wa kukutana na Mabalozi mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao Tanzania kwa lengo la kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizo na Tanzania.

Kiongozi huyo wa Mabalozi hapa nchini ambaye pia ni Balozi wa Visiwa vya Comoro amesema njia pekee ya Afrika kutoingiliwa katika mambo yake ya ndani ni kuhakikisha kuwa bara hilo linaweka mikakati madhubuti itakayowezesha bara hilo kujitegemea.

"Njia pekee ya Afrika kutoingiliwa katika mambo yake ya ndani ni kuhakikisha kuwa sisi kama waafrika tunaweka mikakati madhubuti itakayowezesha bara letu kujitegemea kwa umoja, mshikamano wetu wenyewe," Amesema Dkt. Mohamed

Nae Balozi wa Kenya hapa Nchini Mhe. Dan Kazungu amesema kikao hicho cha mabalozi wa Afrika na Prof. Kabudi hususani katika kipindi hiki cha kuelekea katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 28, umewawezesha mabalozi hao kufahamu namna Tanzania ilivyojiandaa kutekeleza demokrasia na kuwataka waafrika kujivunia nchi zao na kuwa wazalendo.

"MKutano wa leo umetuwezesha sisi mabalozi wa Afrika tunaowakilisha nchi zetu hapa Tanzania kufahamu namna Tanzania ilivyojiandaa kutekeleza demokrasia na kuwataka waafrika kujivunia nchi zao na kuwa wazalendo," Amesema Balozi Kazungu.   

Kwa upande wake Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Prof. Palamagamba John Kabudi ameitumia fursa hiyo kuwaeleza Mabalozi hao namna Tanzania inavyoheshimu na kukuza diplomasia na mahusiano baina ya nchi za Afrika,kulinda demokrasia na haki za binadamu lakini pia kutumia fedha zake katika kuleta maendeleo ya watu na vitu jambo lililoiwezesha Tanzania kuingia katika nchi za uchumi wa kati kabla ya muda uliotarajiwa.  

"Waheshimiwa Mabaalozi napenda kuwahakikishia kuwa Tanzania inaheshimu na imedhamiria kukuza diplomasia na mahusiano baina ya nchi za Afrika, kulinda demokrasia na haki za binadamu pamoja na kuhakikisha kuwa inatumia fedha zake za ndani katika kuleta maendeleo ya watu na vitu jambo lililoiwezesha Tanzania kuingia katika nchi za uchumi wa kati kabla ya muda uliotarajiwa," Amesema Prof. Kabudi.  

Mkutano huo uliohudhuriwa Mabalozi 15 na wawakilishi wa Balozi 8 walitumia fursa hiyo kumuombea Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Baba wa Taifa hayati Julius Kambarage Nyerere kama Baba wa demokrasia Barani Afrika pamoja na kuuombea uchaguzi mkuu wa Oktoba 28.

Mabalozi waliohudhuria katika mkutano huo ni Balozi wa Visiwa vya Comoro, Mhe. Ahamada El Badaoui Mohamed, Balozi wa Msumbiji, Mhe. Patricio Clemente, Balozi wa Namibia, Mhe. Theresia Samaria, Balozi wa Somalia, Mhe. Mohammed Abdi, Balozi wa Morocco, Mhe. Abdelilah Benryane, Balozi wa Zambia, Mhe. Benson Chali.

Wengine ni Balozi wa Burundi, Mhe. Gervais Abayeho, Balozi wa Kenya, Mhe. Dan Kazungu, Balozi wa Ethiopia, Mhe. Yonas Yosef Sanbe, Balozi wa Misri, Mhe. Mohamed Gaber Mohamed Abdulwafa, Balozi wa Angola, Mhe. Sandro De Oliveira, Balozi wa Malawi, Mhe. Chembe Mnthali, Balozi wa Saharawi, Mhe. Mahayub Buyema, Balozi wa Rwanda, Mhe. Meja Jenerali, Charles Karamba pamoja na Balozi wa Algeria, Mhe. Ahmed Djelal.

Wawakilishi waliowakilisha Balozi nane ni Bw. Jaafar Nasir Abdalla kutoka Ubalozi wa Sudan, Mr. Sizwe Ernest Mayoli kutoka Ubalozi wa Afrika Kusini, Balozi William Wani Ruben kutoka Ubalozi wa Sudani Kusini, Bibi. Bintu Bwala Ekikor kutoka Ubalozi wa Nigeria, Bw. Kamal Krista kutoka ubalozi wa Libya, Bw. Adjanga Bissa Benjamin kutoka ubalozi wa DRC, Bibi. Musekura Esezakutoka ubalozi wa Uganda pamoja na Bw. Chrispen Chibuwe kutoka Ubalozi wa Zimbabwe.


Share:

TUMA second round selected applicants 2020/2021

The Tumaini University Makumira TUMA second round selected applicants 2020/2021 are the names of students who have passed the Second-round admission selection stage and successfully approved by TCU to join undergraduate studies at Tumaini University Makumira (TUMA) for the 2020/2021 academic year second round application window. The Tumaini University Makumira TUMA second round applications and […]

The post TUMA second round selected applicants 2020/2021 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

UAUT second round selected applicants 2020/2021

The United African University of Tanzania UAUT second round selected applicants 2020/2021 are the names of students who have passed the Second-round admission selection stage and successfully approved by TCU to join undergraduate studies at United African University of Tanzania (UAUT) for the 2020/2021 academic year second round application window. The United African University of […]

The post UAUT second round selected applicants 2020/2021 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

MUM second round selected applicants 2020/2021

Muslim University of Morogoro MUM second round selected applicants 2020/2021 are the names of students who have passed the Second-round admission selection stage and successfully approved by TCU to join undergraduate studies at Muslim University of Morogoro (MUM) for the 2020/2021 academic year second round application window. The Muslim University of Morogoro MUM second round […]

The post MUM second round selected applicants 2020/2021 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

STEMMUCO second round selected applicants 2020/2021

The Stella Maris Mtwara University College STEMMUCO second round selected applicants 2020/2021 are the names of students who have passed the Second-round admission selection stage and successfully approved by TCU to join undergraduate studies at Stella Maris Mtwara University College (STEMMUCO) for the 2020/2021 academic year second round application window. The Stella Maris Mtwara University […]

The post STEMMUCO second round selected applicants 2020/2021 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Procurement Officer at International Rescue Committee

Requisition ID: req10845 Job Title: Procurement Officer Sector: Supply Chain Employment Category: Fixed Term Employment Type: Full-Time Open to Expatriates: No Location: Kasulu, Tanzania Job Description   The International Rescue Committee, one of the world’s largest humanitarian agencies, provides relief, rehabilitation, and post-conflict reconstruction support to victims of natural disaster, oppression, and violent conflict in 42 countries. The IRC is committed to […]

The post Procurement Officer at International Rescue Committee appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

AMUCTA second round selected applicants 2020/2021

The Archbishop Mihayo University College of Tabora AMUCTA second round selected applicants 2020/2021 are the names of students who have passed the Second-round admission selection stage and successfully approved by TCU to join undergraduate studies at Archbishop Mihayo University College of Tabora (AMUCTA) for the 2020/2021 academic year second round application window. The Archbishop Mihayo […]

The post AMUCTA second round selected applicants 2020/2021 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

KIUT second round selected applicants 2020/2021

The Kampala International University in Tanzania KIUT second round selected applicants 2020/2021 are the names of students who have passed the Second-round admission selection stage and successfully approved by TCU to join undergraduate studies at Kampala International University in Tanzania (KIUT) for the 2020/2021 academic year second round application window. The Kampala International University in […]

The post KIUT second round selected applicants 2020/2021 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

IRDP second round selected applicants 2020/2021

Institute of Rural Development Planning IRDP second round selected applicants 2020/2021 are the names of students who have passed the Second-round admission selection stage and successfully approved by TCU to join undergraduate studies at Institute of Rural Development Planning (IRDP) for the 2020/2021 academic year second round application window. The Institute of Rural Development Planning […]

The post IRDP second round selected applicants 2020/2021 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

TEKU second round selected applicants 2020/2021

Teofilo Kisanji University TEKU second round selected applicants 2020/2021 are the names of students who have passed the Second-round admission selection stage and successfully approved by TCU to join undergraduate studies at Teofilo Kisanji University (TEKU) for the 2020/2021 academic year second round application window. The Teofilo Kisanji University TEKU second round applications and TEKU […]

The post TEKU second round selected applicants 2020/2021 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

MNMA second round selected applicants 2020/2021

The Mwalimu Nyerere Memorial Academy MNMA second round selected applicants 2020/2021 are the names of students who have passed the Second-round admission selection stage and successfully approved by TCU to join undergraduate studies at The Mwalimu Nyerere Memorial Academy (MNMA) for the 2020/2021 academic year second round application window. The The Mwalimu Nyerere Memorial Academy […]

The post MNMA second round selected applicants 2020/2021 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger