Thursday 24 September 2020

NITAPIGANIA AWAMU YA PILI YA MABORESHO YA BANDARI YA TANGA ILI KUFUNGUA FURSA ZA AJIRA-UMMY MWALIMU

MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu akizungumza na wananchi wa Kata ya Duga Jijini Tanga wakati wa mkutano wake wa kampeni
MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu akizungumza na wananchi wa Kata ya Duga Jijini Tanga wakati wa mkutano wake wa kampeni
MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu kushoto akimnadi mgombea udiwani wa Kata ya Duga (CCM)
MWENYEKITI wa UWT Mkoa wa Tanga Dkt Aisha Kigoda akimuombea kura kwa wananchi wa Kata ya Duga mgombea Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu
Mkuu wa Mkoa Mstaafu Mwatumu Mahiza akimuombea Kura mgombea Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM)Ummy Mwalimu
KATIBU Mwenezi wa CCM wilaya ya Tanga Lupakisyo kapange akimuombea kura Mgombea Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu wakati wa mkutano huo
MGOMBEA Ubunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Tanga (CCM) Mhandisi Mwanaisha Ulenge
Umati Mkubwa wa wananchi wakimsikiliza mgombea Ubunge wa Jimbo la Tanga Ummy Mwalimu(CCM)
Umati Mkubwa wa wananchi wakimsikiliza mgombea Ubunge wa Jimbo la Tanga Ummy Mwalimu(CCM)
Msanii wa mziki wa Bongofleva Kassim Mganga akitumbuiza wakati wa mkutano huo
Msanii wa mziki wa Bongofleva Kassim Mganga akitumbuiza wakati wa mkutano huo


MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu amesema iwapo atachaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo atapigania maboresho ya awamu ya pili ya Bandari ya Tanga ili kuongeza fursa za ajira na kuongeaza vipato vya wakazi wa Jiji hilo.

 

Ummy ambaye pia ni Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto aliyasema hayo wakati akiwahutubia wananchi wa Kata ya Duga Jijini Tanga katika mkutano wake wa kampeni alisema huo ni mkakati wake wa kutaka kuona meli kubwa zinatia nanga kwenye bandari hiyo.

 

“Ndugu zangu wana Duga naombeni kura zenu niweze kulibadilisha Jiji la Tanga kwa kuhakikisha tunasukuma maboresho ya awamu ya pili ya Bandari ya Tanga kuweza kuongeza fursa za ajira kwa vijana”Alisema

 

Alisema pia licha ya uwepo wa fursa za ajira kwa vijana lakini pia vipato vya wakazi wa mji wa Tanga vitaongezeka kutokana na mzunguko mkubwa wa biashara .

 

“Katika hili tunamshukuru Rais Dkt John Magufuli kwa kutuwezesha milioni 372 kwa ajili ya maboresha ya awamu ya kwanza ya Bandari hiyo lengo langu ni kutaka bandari ya Tanga meli kubwa zote ziweze kutia nanga kwenye bandari”Alisema

 

Alisema meli hizo kubwa zikitia nanga kwenye Bandari hiyo itawawesha vijana waweze kupata ajira wanaume na wanawake na mji utachangamka na hivyo kuchochea kipato cha mtu mmoja mmoja na jamii kwa ujumla.

 

“Nitumeni Bungeni ninaaminika ninaweza kupiga hodi kwa kiongozi yoyote, waziri yoyote ili bandari ya Tanga iweze kuboreshwa na kuweza kufungua fursa za ajira kwa vijana wanawake na wanaume “Alisema

 

Hata hivyo alisema kwamba amedhamiria kupigania mizigo yote inayokwenda mikoa ya kanda ya kaskazini ishushwe kwenye bandari ya Tanga badala ya Dare s Salama ili mji huo uweze kuchangamsha .

 

“Hili nitalipigania usiku na mchana ili kuweza kurejesha heshima ya Jiji la Tanga nataka kuona mji huu unapata mafanikio makubwa na kuwa kama Singapori.

Share:

KONGWA YAANZA MKAKATI WA KILA KAYA KULIMA EKARI MOJA YA KOROSHO


Mkuu wa Wilaya ya Kongwa Suleiman Serera akizungumza na Maafisa Ugani na Wakulima wakati akifungua mafunzo ya kilimo bora cha korosho yanayotolewa na Kituo cha Utafiti wa Kilimo TARI Naliendele Mtwara, wilayani humo mkoani Dodoma. Kushoto ni Afisa Kilimo Umwagiliaji na Ushirika wa Wilaya ya Kongwa, Jackson Shija na Mratibu wa Kitaifa wa Zao la Korosho kutoka  TARI Naliendele, Dkt.Geradina Mzena.

Mratibu wa Kitaifa wa Zao la Korosho kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo TARI Naliendele, Dkt.Geradina Mzena, akitoa mada kwenye mafunzo ya kilimo bora cha korosho yaliyotolewa kwenye ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kongwa kwa Maafisa Ugani na Wakulima mkoani Dodoma. 

Mtafiti Mwandamizi na Mdhibiti wa Visumbufu vya wadudu na magonjwa kwenye zao la korosho, kutoka Tari- Naliendele  Dkt.Wilson Nene, akitoa mada kwenye mafunzo hayo.

Mtafiti  kutoka Tari- Naliendele Programu ya Zao la Korosho, Kasiga Ngiha, akitoa mada kuhusu 'Agronomia' ya korosho.

Meneja wa Bodi ya Korosho Kanda ya Kati na Magharibi, Ray Mtangi, akizungumzia masoko ya zao hilo.

Washiriki wakiwa katika mafunzo hayo.
Mafunzo yakiendelea.
Washiriki wakiwa katika mafunzo hayo.
Afisa Kilimo Umwagiliaji na Ushirika wa Wilaya ya Kongwa, Jackson Shija, akizungumza kwenye mafunzo hayo.
Washiriki wakiwa katika mafunzo hayo.
Afisa Kilimo wa Kata ya Mkoka, Marcelin Chingilile, akizungumza kwenye mafunzo hayo.
Mkulima wa Korosho wa Kata ya Mkoka, Rajab Singo, akizungumza kwenye mafunzo hayo.
Afisa Kilimo wa Kata ya Mlali, Markusi Wongo, akizungumza kwenye mafunzo hayo.
Mkulima wa Korosho, Sospeter Chiwuyo, akizungumza kwenye mafunzo hayo.
Afisa Kilimo wa Kata ya Songambele, Asha Malekela, akizungumza kwenye mafunzo hayo.
Afisa Kilimo wa Kata ya Zoissa, Emmanuel Mongi, akizungumza kwenye mafunzo hayo.


Godwin Myovela na Doto Mwaibale, Kongwa 

WILAYA ya Kongwa ipo mbioni kuanza kutekeleza mpango wa kuhakikisha kila kaya 
inalima ekari moja ya zao la miche ya mikorosho bora azma ikiwa ni kuongeza kipato sambamba na kusaidia kurejesha hali ya uoto wa asili na kupunguza athari za mabadiliko ya tabia nchi.

Hayo yalibainishwa jana na Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Suleiman Serera, wakati akifungua mafunzo ya Kilimo Bora cha Korosho yanayoendelea kutolewa na Kituo cha Utafiti wa Kilimo Tari Naliendele kwa wakulima na Maafisa Ugani wa Halmashauri wilayani hapa.

“Mkakati wa Wilaya ya Kongwa ni kuhakikisha angalau kila kaya inakuwa na ekari moja ya zao la korosho bora sababu ni zao la kudumu la kibiashara lenye manufaa kiuchumi, lakini tunataka kuikijanisha Kongwa yetu kupitia mbegu bora za mikorosho kutoka Tari Naliendele ,” alisema Serera.

Alisema ili kukamilisha mpango huo ambao hata hivyo tayari umeanza kutekelezwa kwa awamu itahitajika miche zaidi ya milioni 2 ili kuzifikia kaya zote 74,000 zilizopo ndani ya wilaya hiyo.

Serera alisema kilimo cha zao la Korosho katika Wilaya ya Kongwa kilianza rasmi msimu wa kilimo wa 2007l2008 na mpaka sasa kuna jumla ya mikorosho mikubwa 75,591 na midogo 231,295, hivyo kuwa na jumla ya mikorosho 306,886 sawa na ekari 10229.5.

“Naamini baada ya mafunzo haya maafisa ugani mtaendelea kutoa mafunzo ya kilimo bora cha korosho kwa wakulima kwenye maeneo yenu ili kuongeza tija na uzalishaji kwa ustawi wa wilaya yetu,” alisema Serera.

Kwa upande wake, Mratibu wa zao la Korosho Kitaifa kutoka Tari Naliendele, Dkt.Geradina Mzena alisema mafunzo hayo ya nadharia na vitendo yana lengo la kuongeza ujuzi kwa wakulima na maafisa ugani ili kuinua tija kwenye zao la korosho.

“Kwenye mafunzo haya pamoja na mambo mengine tutajikita katika kuangalia namna 
bora ya kuanzisha shamba jipya, ‘agronomia ya Korosho’ na namna bora ya kudhibiti wadudu na magonjwa ya zao hilo,” alisema Mzena. 
 
Share:

VIWANDA VYA KATI NA VIDOGO YAHIMIZWA KUJITOKEZA KUSHIRIKI KWA WINGI SHINDANO LA 15 LA TUZO ZA RAIS ZA MZALISHAJI BORA (PMAYA)

 

Afisa wa masoko kutoka ALAF Ltd. Bi. Theresia Mmasy akielezea jinsi Tuzo za Raisi za Mzalishaji Bora wa Viwanda(PMAYA) zilivyo za haki na huru.

Waandishi mbalimbali walioshiriki katika kuunga mkono uzinduzi wa shindano la 15 la Tuzo za Raisi za Mzalishaji bora wa mwaka(PMAYA)Afisa wa masoko kutoka ALAF Ltd. Bi. Theresia Mmasy akielezea jinsi Tuzo za Raisi za Mzalishaji Bora wa Viwanda(PMAYA) zilivyo za haki na huru. Waandishi mbalimbali walioshiriki katika kuunga mkono uzinduzi wa shindano la 15 la Tuzo za Raisi za Mzalishaji bora wa mwaka(PMAYA)

Mkurugenzi mtendaji wa Shirikisho la Viwanda Tanzania (CTI) Bwana. Leodegar Tenga akisisitiza ushiriki wa viwanda vidogo na vya kati kushiriki katika mashindano ya Tuzo za Raisi za Mzalishaji Bora (PMAYA)

*************************************

Dar Es Salaam, Septemba 23 2020.

Kwa miaka 15 mfululizo, shindano la tuzo la Rais za mzalishaji bora wa mwaka wa viwandani linalofanyika kila mwaka maarufu kama “PMAYA” limepangwa kufanyika mwezi Novemba mwaka huu.

Dhumuni la shindano la PMAYA ni kutambua makampuni yanayojihusisha na uzalishaji wa bidhaa na huduma nchini Tanzania katika sekta mbalimbali kwenye vipengele vya viwanda vikubwa, vya kati na vidogo.

Akitangaza rasmi shindano la PMAYA kwa mwaka huu wa 2020, mkurugenzi wa Shirikisho la viwanda Tanzania (CTI) Bw. Leodegar Tenga alikaribisha viwanda kushiriki na kuungana na mlezi wa Shirikisho la viwanda Tanzania, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. John Pombe Joseph Magufuli katika jitihada zake za kuifanya Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati wa viwanda ifikapo mwaka 2025.

“Kwa kipindi chote tumepata ushirikiano wa kutosha kutoka kwa wadau mbalimbali, na kwa mwaka huu tumekwisha pokea idadi kubwa ya washiriki kutoka viwanda mbalimbali kote nchini. Tunahamasisha makampuni mengi ya uzalishaji kushiriki na hususani tunahamasisha ushiriki wa viwanda vya kati na vidogo” alisema Bw. Tenga.

“Mbuyu ulianza kama mchicha , hivyo ni muda mwafaka kwa viwanda vya kati na vidogo kutumia jukwaa hili kama nafasi kwao kuongoza kwenye nyanja tofauti, kutambulika, kuchangia ukuaji wa biashara zao na kutambulika” aliongeza Bw. Tenga.

Shindano la PMAYA linaloandaliwa kwa heshima ya Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania akiwa kama mlezi wa Shirikisho la viwanda Tanzania, linadhamiria kutambua mchango wa sekta ya viwanda , kutangaza umuhimu wa sekta ya viwanda nchini, kuongeza tija kwenye viwango vya ufanyaji biashara pamoja na kukuza utawala bora wa makampuni nchini.

Meneja masoko wa kampuni ya ALAF Ltd iliyokuwa mshindi wa kiwango kikubwa kwenye kipengele cha chuma na bidhaa za chuma kwenye shindano la mwaka jana Bi. Theresia Mmasy alisema, “ALAF imekua ikishiriki kwenye PMAYA na tumekua washindi wa vipengele mbalimbali kwa kipindi cha miaka 10 mfululizo kwenye kipengele cha chuma na bidhaa za chuma.

Kwetu ALAF tumeona umuhimu wa PMAYA na ni kwa sababu taratibu zote za ushiriki na mchakato wa kutafuta washindi unafanyika kwa haki na huru jambo linalotoa nafasi sawa kwa kila mshiriki kushinda. Sambamba na hilo, PMAYA ndio tuzo pekee za viwanda ambapo makampuni ya uzalishaji yanapata kutambulika.

Nayasihi makampuni mengine kuchangamkia fursa hii na kushiriki waweze kushinda.

Mashindano ya PMAYA yamekuwa moja ya njia fasaha kwa makampuni kuongeza ubora wa bidhaa na huduma zao kwa jamii. Tathmini ya shindano inafanywa na jopo huru la wakaguzi, na mwishoni hutoa taarifa na majibu ya tathmini iliyofanywa.

Washiriki hupewa taarifa ya tathmini ili waweze kufahamu mapungufu na umahiri wao kiutendaji kwa maendeleo yao kama kampuni

Akizungumza kwa niaba ya kampuni ya PLASCO Ltd waliokua washindi kiwango kikubwa kwenye kipengele cha plastiki na mipira, meneja wa masoko na mauzo Bi. Edith James alisema,”Tuzo za PMAYA zimetoa fursa nzuri na ya kipekee kwa viwanda vya ndani. Zimesaidia pia katika kukuza ufahamu juu ya umuhimu wa kuhakikisha ubora kwenye sekta zote kwa mtazamo wa kuhamasisha mchango wa viwanda vya ndani kwenye miradi mikubwa ya miundombinu. Kampuni ya PLASCO imekua ikishiriki kwenye mashindano haya ya PMAYA na tumekuwa washindi katika vipengele mbalimbali jambo linalotupa nafasi kuongoza na pia kukuza biashara yetu. Nahamisisha Viwanda vyote Tanzania haswa ya kati na vidogo kushiriki na kuitumia kwa ufasaha nafasi hii kujitangaza kibiashara”

Uzinduzi wa shindano hili linafungua milango kwa wadau mbalimbali kwenye sekta ya viwanda kujisajili ili kushiriki kwenye shindano hili. Kujisajili tafadhali tembelea toviti ya shirikisho www.cti.co.tz. Mwisho wa kuwasilisha maombi ya kushiriki ni tarehe 12 Oktoba 2020.

Tuzo za Rais za mzalishaji bora wa viwandani PMAYA mwaka huu zinaandaliwa na Shirikisho la viwanda Tanzania (CTI) kwa kushirikiana na GIZ – Kuunda mitazamo: kwa maendeleo ya Afrika Mashariki

Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti Ya Leo Septemba 24





















Share:

Wednesday 23 September 2020

NDUGAI AFUNGUA SHINA LA WAKEREKETWA CCM LA WAFANYA BIASHARA IPEMBE SINGIDA

Mjumbe wa kamati kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) taifa Ndugu Job Ndugai Akihutubia wanachama na wapenzi wa Chama cha Mapinduzi wa shina na 3 la Ipembe mkoani Singida.
 Eneo la Shina la wakereketwa wa Chama Cha Mapinduzi CCM  Mbacho Guest ambalo lipo kata ya Ipembe Manispaa ya Singida.
 Mjumbe wa kamati kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) taifa Ndugu Job Ndugai akiwakabidhi kadi za CCM wanachama wapya waliohamia Chama Cha Mapinduzi CCM kutoka vyama vingine vya upinzani.
Mjumbe wa kamati kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) taifa Ndugu Job Ndugai akiwakabidhi kadi za CCM wanachama wapya waliohamia Chama Cha Mapinduzi CCM kutoka vyama vingine vya upinzani.

Na Ismail Luhamba, Singida.


MJUMBE wa kamati kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa Ndugu Job Ndugai amesema Bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania linatarajia kuboresha sheria kwa wafanyabiashara nchini ili wafanye biashara zao kwa tija.


Mjumbe huyo ambaye pia ni Spika wa bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aliyasema hayo jana wakati akizindua shina la wakereketwa wa CCM ambao ni wafanyabiashara kata ya Ipembe Wilaya ya Singida mjini. 

Ndugai alitumia nafasi hiyo kuwaomba wanachama wote na wasio wanachama siku ya kupiga kura kujitokeza kwa wingi kwenda kupiga kura na kukipigia chama cha CCM kwani kina mambo makubwa ya kimaendeleo kwa wananchi wake.

Awali akisoma taarifa fupi ya shina hilo kabla ya kuzinduliwa, atibu msaidizi wa shina hilo Florian Malya alisema wafanyabiashara hao wanaiomba serikali kuwawekea mazingira mazuri ya kufanikisha biashara zao ili waweze kujipatia kipato na kuweza kulipa kodi mbalimbali kwa mujibu wa sheria.

"Sisi wafanyabiashara tunakiunga mkono chama cha Mapinduzi na tutahakikisha kinashinda kwa kishindo kwa ngazi zote kuanzia diwani,mbunge na Rais",alisema Malya.

Shina hilo ambalo lipo eneo la Mbacho Guest kata ya Ipembe lina wanachama 50 likiwa linaongozwa na mwenyekiti wake Philipo Masawe, katibu ni Mark Kimboka na katibu msaidizi akiwa ni Florian Malya.

Share:

Monitoring and Evaluation (M&E) Officer at EGPAF

VACANCY ANNOUNCEMENT “Sometimes in life there is that moment when it’s possible to make a change for the better. This is one of those moments.” -Elizabeth Glaser The Elizabeth Glaser Pediatric AIDS Foundation is a global leader in the fight against pediatric HIV and AIDS, working in 19 countries and supporting close to 6,000 sites […]

The post Monitoring and Evaluation (M&E) Officer at EGPAF appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Jobs in Tanzania – latest Jobs Today  in Tanzania September 2020

56Browse all latest Jobs Today  in Tanzania JOB ADVERTISEMENTS FROM GOVERNMENT, TANZANIA NGOs AND INTERNATIONAL NGOs Find Latest Tanzanian Job Vacancies – Tanzania Jobs Today – Current 2020 Jobs in Tanzania July 2020 – Daily Jobs in Tanzania: A listing of latest jobs in Tanzania from top employers. Over 50 new job vacancies in Tanzania posted […]

The post Jobs in Tanzania – latest Jobs Today  in Tanzania September 2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Nafasi za kazi serikalini (Utumishi wa Umma/ ajiraportal.go.tz) September 2020

The Public Service Recruitment Secretariat (PSRS)-Nafasi za Kazi serikalini (Utumishi wa Umma/ ajiraportal.go.tz) What is The Public Service Recruitment Secretariat (PSRS)? The Public Service Recruitment Secretariat (PSRS) is a government organ with a status of independent Department established specifically to facilitate the recruitment process of employees to the Public Service. Public Service Recruitment Secretariat was […]

The post Nafasi za kazi serikalini (Utumishi wa Umma/ ajiraportal.go.tz) September 2020 appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Energy Specialist at RTI International

Background: RTI International is an independent, nonprofit research institute dedicated to improving the human condition by turning knowledge into practice. The organization provides research, development, and technical services to government and commercial clients in more than 75 countries. Power Africa East Africa Energy Program is a four-year project working to increase on-grid electricity access, accelerate […]

The post Energy Specialist at RTI International appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

MHPSS/Psycho Social Officer at International Rescue Committee

Requisition ID: req10442 Job Title: MHPSS/Psycho Social Officer Sector: Health Employment Category: Fixed Term Employment Type: Full-Time Open to Expatriates: No Location: Kibondo, Tanzania Job Description The International Rescue Committee (IRC) Tanzania is present in the Kigoma Region, Northwestern Tanzania, providing services in one remaining refugee camp in Kasulu District and at a transit Centre in Kigoma town.  Approximately 65,000 Congolese receive protection […]

The post MHPSS/Psycho Social Officer at International Rescue Committee appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Business Analyst Graduate Trainee at Total

Job Description Business Analyst– Graduate Trainee. Specifically, the holder of this position is responsible for the following: Prepare and submit timely and comprehensive weekly network sales, margins and purchase analysis reports Collect and prepare weekly and monthly station sales reports per station, per region and per TM for all products and services with explanations in […]

The post Business Analyst Graduate Trainee at Total appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Territory Manager at Total

Job Description Under the authority of the Network Operation Manager, he is responsible for a profit center that he pilots with the support of functional and operational units (customer service, maintenance, SFS, accounting, etc.). He is the main person responsible for the service stations he handles. He spells out, coordinates, develops and supervises the policies […]

The post Territory Manager at Total appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

Majaliwa: Tarehe 28 Oktoba Siyo Siku Ya Mzaha

MJUMBE wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Kassim Majaliwa amemaliza ziara yake mkoa wa Mara na kuwaeleza wananchi kwamba tarehe 28 Oktoba, 2020 siyo siku ya mzaha.

"Tarehe 28 Oktoba, 2020 siyo siyo ya mzaha na wala siyo siku ya majaribio. Ni siku ya kuchagua Kiongozi atakayetufaa, na huyo si mwingine bali Dkt. John Pombe Magufuli, " amesema.

Ametoa kauli hiyo jana mchana (Jumanne, Septemba 22, 2020) wakati akizungumza na wakazi wa Kibara, wilayani Bunda, mkoani Mara kwenye mkutano wa kuwanadi wagombea wa CCM uliofanyika katika uwanja wa michezo wa Kibara.

Amesema kiongozi wa nchi anayefaa kuchaguliwa ni yule anayeweza kusimamia rasilmali za Taifa. "Ni yule anayeweza kusimamia tunu za Taifa... siyo mnapata kiongozi halafu akipewa nchi anabadilisha hadi wimbo wa Taifa."

"Tunahitaji kiongozi anayeweza kupambana na rushwa, awe mtu wa kutetea watu wake wapate haki bila kuombwa rushwa. Huyo si mwingine bali ni Dkt. John Pombe Magufuli," amesema. 

Mheshimiwa Majaliwa ambaye alikuwa mkoani Mara kumuombea kura mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dkt. John Pombe Magufuli alitumia fursa hiyo kuwaombea kura mgombea ubunge wa jimbo la kuwaombea kura Charles Kajege na diwani wa Kibara, Bw. Nyanguli Mtesigwa na madiwani wengine wa jimbo hilo. Jioni hii anaingia mkoa wa Mwanza.

Akielezea umuhimu wa chama kuwa na Ilani ya Uchaguzi, Mheshimiwa Majaliwa amesema Chama cha Mapinduzi kimeandaa ilani yake yenye kurasa 303 ikisimamia yale yaliyokuwemo kwenye ilani iliyopita ambayo ilikuwa na kurasa 236 na mengine mengi mapya. 

"Watekelezaji wa hayo yote yaliyoainishwa kwenye Ilani ni hawa watatu ambao nawaombea kura leo. Namwombea kura Dkt. Magufuli ili akamilishe aliyoyaanza na atekeleze yaliyomo kwenye Ilani ya sasa. Ni lazima tumpatie mbunge na diwani wa CCM ili waweze kuzungumza lugha moja."

Kuhusu uboreshaji kwenye sekta ya afya, Mheshimiwa Majaliwa alisema zilitumika sh. bilioni 1.8 za kujenga hospitali ya wilaya hiyo na bado kuna sh. milioni 152 zilitolewa ili kuisaidia Halmashauri kujenga zahanati.

Kuhusu sekta ya maji, Mheshimiwa Majaliwa amesema sh. bilioni 6.2 zimetumika kukarabati na ujenzi wa miradi mbalimbali kwenye Halmashauri ya wilayani Bunda, ikiwemo uchimbaji wa visima virefu na vifupi, utengenezaji wa matenki ya kuvuna maji na uchimbaji wa mabwawa. 
“Vijiji vilivyonufaika na miradi hii ni Nyatwali, Nyamuswa, Mgeta –Nyang’aranga, kinyabwiga, Bulamba na Kibara. Pia jumla ya shilingi milioni 90.1 zimetumika kwa ajili ya ukarabati na usafishaji wa pampu za mkono 67 na visima vitatu,” amesema.

Mapema asubuhi, akiwa kata ya Kisorya, Mheshimiwa Majaliwa aliwaeleza wananchi hao kwamba Serikali ya CCM ina mpango wa kuboresha kituo chao cha afya kwa kuongeza wodi tatu za wanawake, wanaume na watoto.

Pia alisema zimetengwa sh. milioni 550 za kuimarisha kituo hicho kwa kuongeza majengo ya jiko, chumba cha kufulia na chumba cha kuhifadhia maiti.

Kuhusu barabara, amesema kiasi cha sh. bilioni 2.9 kimetumika kutengeneza barabara za kuunganisha vijiji kwa vijiji, kukarabati sehemu korofi zilizoharibiwa na mafuriko, madaraja, makalvati na matengenezo ya kawaida.

Kuhusu umeme, amesema vijiji 77 kati ya 78 vina umeme isipokuwa kijiji kimoja tu cha Nafubu kilichopo kisiwani, ambacho amesema watapelekewa huduma ya umeme wa jua kwa vile siyo rahisi kupitisha nyaya za umeme majini.

(mwisho) 


Share:

Plumber at U.S. Embassy Dar es Salaam

Overview Hiring Path: • Open to the public Who May Apply/Clarification From the Agency: All Interested Applicants / All Sources Security Clearance Required: Public Trust – Background Investigation Appointment Type Permanent Appointment Type Details: Indefinite subject to successful completion of probationary period Marketing Statement: We encourage you to read and understand the Eight (8) Qualities of […]

The post Plumber at U.S. Embassy Dar es Salaam appeared first on Udahiliportal.com.

Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger