Saturday 19 September 2020
AHMED SALUM AWAOMBA WANANCHI WAMPE MIAKA MITANO MINGINE SOLWA...ATOA AHADI KWA WACHIMBA MADINI MWAKITOLYO
Serikali Kutokomeza Wadudu Waenezao Magonjwa Ya Mifugo
Na. Edward Kondela
Serikali imelenga kukabiliana na magonjwa ya mifugo nchini kupitia taasisi zilizo chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi, kwa kutumia njia ya chanjo pamoja na kutokomeza wadudu wakiwemo mbung’o ambao wanaathiri afya ya wanyama.
Akizungumza katika ziara ya kikazi ya siku moja aliyofanya Mkoani Tanga mwishoni mwa wiki hii, baada ya kutembelea Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA), Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amewataka watanzania kutambua kazi kubwa zinafonywa na taasisi za serikali katika kufanya tafiti na kutafuta tiba ya magonjwa ya mifugo nchini.
“Wito wangu kwa wafugaji ambao bado wanasumbuliwa na mbung’o, tayari kituo chetu cha TVLA Mkoani Tanga wameshapata njia nzuri na rahisi kabisa, lengo kubwa kabisa ni kuhakikisha tunatokomeza magonjwa ya mifugo kadri inavyowezekana, niombe watanzania watambue kazi kubwa zinazofanywa na taasisi zetu, ili tuondoke katika ufugaji wa mazoea bali sasa tufanye ufugaji wa kisayansi.” Amesema Prof. Gabriel
Afisa Utafiti wa Mifugo kutoka TVLA Mkoani Tanga Bw. Peter Lucas, amemfahamisha Prof. Gabriel kuhusu njia rahisi ambazo wafugaji wanaweza kutumia katika kutokomeza mbung’o kuwa ni pamoja na mtego wa kukamata mbung’o na njia ya kuweka dawa maalum ya kuua mbung’o kwenye vitambaa vyenye rangi ya bluu na nyeusi ambazo zimekuwa zikiwavutia wadudu hao.
Akiwa katika chuo cha Wakala ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA) Kampasi ya Buhuri Mkoani Tanga, Katibu Mkuu Prof. Gabriel amewataka wakufunzi wa chuo hicho wawe na upeo mkubwa ili waweze kutoa wahitimu waliopata elimu bora.
“Kikubwa wafundisheni wanafunzi kujiajiri na anayefundisha somo hilo lazima awe amejiajiri, lazima tuwajengee wanafunzi wetu kazi siyo mpaka kuajiriwa, kujiajiri pia ndiyo msingi hasa wa kuendeleza maendeleo na nchi zilizoendelea walioleta maendeleo ni wajasiriamali.” Amefafanua Prof. Gabriel.
Katika ziara hiyo ya siku moja Mkoani Tanga, Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel alijionea shughuli zinazofanywa na Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) mkoani humo, ambapo ameitaka taasisi hiyo kutoa taarifa ya tafiti mbalimbali za mifugo ikiwemo ya ng’ombe bora wa maziwa na kuongeza idadi ya mifugo iliyopo katika eneo hilo.
Aidha, akizungumza na watumishi wa taasisi hizo Prof. Gabriel amewataka watumishi hao kuwa wazalendo na kujituma kwa kutoa michango yenye tija katika taasisi wanazofanyia kazi.
Wakizungumza katika nyakati tofauti Kaimu Meneja wa Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA), Dkt. Oliva Manangwa amemuarifu katibu mkuu huyo kuwa TVLA imefanikiwa kufanya tafiti mbalimbali ikiwemo ya kutokomeza kabisa vimelea vya ndorobo visiwani Zanzibar kwa kuwahasi mbung’o dume.
Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) Mkoa wa Tanga Dkt. Zabron Nziku amemweleza Katibu Mkuu Prof. Gabriel kuwa wameanzisha maabara ya kisasa kwa ajili ya kutengeneza virutubisho vya mifugo vinavyotokana na zao la muhogo ambavyo havina gharama kubwa kwa wafugaji.
Naye Meneja wa Wakala ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA) Kampasi ya Buhuri Mkoani Tanga Bw. Venance Tarimo amesema chuo hicho kimekuwa kikitoa mafunzo ya muda mfupi na muda mrefu ili kupata wataalam bora wa mifugo nchini.
Akihitimisha ziara ya kikazi ya siku moja Mkoani Tanga katika taasisi zilizo chini ya Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Katibu Mkuu wa wizara hiyo anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel amekutana na Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Bi. Judica Omari na kuzungumzia changamoto mbalimbali zinazowakumba wafugaji katika mkoa huo na namna ya kuzitatua.
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi anayeshughulikia Mifugo Prof. Elisante Ole Gabriel alikuwa katika ziara ya kikazi ya siku moja Mkoani Tanga mwishoni mwa wiki hii ili kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na Wakala ya Maabara ya Veterinari Tanzania (TVLA), Wakala ya Vyuo vya Mafunzo ya Mifugo Tanzania (LITA) na Taasisi ya Utafiti wa Mifugo Tanzania (TALIRI) ambazo zote zipo chini ya wizara hiyo.
Mwisho.
Orodha Kamili Ya Viti Maalum Ubunge Na Udiwani Kutolewa Baada Ya Ushiriki Wa Kampeni
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Bashiru Ally Kakurwa, ametoa msimamo wa Chama katika kuteua wabunge wa viti maalum, ambapo ameeleza kuwa, kwa upande wa Udiwani aliyeshinda kura za maoni ndio atateuliwa, isipokuwa kama itadhihirika ushiriki wake wa kampeni haukuwa wa kuridhisha.
Ameyasema hayo tarehe 18 Septemba, 2020 katika kikao cha viongozi wa CCM wa ngazi ya mashina, Matawi, Kata na Wilaya ya Bukoba Mjini.
*"Kwa wagombea wa viti Maalum, Udiwani na Ubunge, orodha kamili itatolewa baada ya tathmini ya ushiriki wao katika kutafuta kura",*
Amesisitiza kuwa, *"wakati wa kura za maoni za udiwani wa viti maalum, halmashauri kuu za mikoa ndio zilikuwa zinafanya uteuzi wa mwisho wapo baadhi ya viongozi wamechezea matokeo ya kura za maoni na kuwaonea walioshinda kura za maoni kwa visingizio visivyokuwa na kichwa wala miguu,"*
Katibu Mkuu, ametumia wasaa huo katika kikao hiko cha ndani, kutoa msimamo wa Chama kuhusu madiwani hao wa viti maalum,
*"Aliyeshinda kura za maoni za udiwani ndiye anayeteuliwa, aliyeongoza kura za maoni Udiwani viti maalum, ndiye anayeteuliwa mpaka itakapothibitika kuwa ushiriki wake katika kuomba kura haukuridhisha.., kuna mkoa mmoja hawakuchukua wakwanza mpaka watano, eti kwa sababu hawakuchangia asilimia 10, zile pesa ni za hiyari sio lazima."*
*"Kanuni zetu zinasema, kura za maoni, sio kigezo pekee cha uteuzi lakini kuongoza kura ni kigezo muhimu sana mpaka upate sababu zenye ushahidi na zenye kusimamia uhai wa chama ndipo usimteue."* Dkt. Bashiru amefafanua.
Aidha, Katibu Mkuu pamoja na mambo mengine, amekemea vikali, tabia za baadhi ya wanaCCM wanaopanga kikisaliti chama katika kipindi hiki cha uchaguzi kwa maslahi yao binafsi,
*"Sasa nawahakikishia msaliti na mnafiki akibainika hatutamgusa wakati wa vita na msiwaguse hawa wakati wa vita, Wakati wa vita sio wakati wa kugombana, lakini tusizushiane tukawachonga wasaliti tukawachonga wanafiki kumbe watu wanaonewa."*
Katibu Mkuu amesisitiza kuwa, *"Tutajiridhisha kwa ushahidi na tunaendelea kushughulika nao, tukimaliza uchaguzi, wanafiki watasafishwa wote kwenye chama chetu, hata kama una urefu kama mnara wa baberi tutakuangusha."*
Awali kabla ya kikao hiko, Katibu Mkuu kwa niaba ya Mwenyekiti wa CCM na Mgombea Urais na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Joseph Pombe Magufuli, amehudhuria hafla ya kuaga miili ya marehemu Kumi wanafunzi wa shule ya Msingi Byamungu vilivyotokea Septemba 14, 2020 kwa ajali ya moto Wilayani Kyerwa.
Vikao hivyo, ni mfululizo wa ujenzi na uimarishaji wa mshikamano, nidhamu, na moyo wa kujitolewa hasa katika kipindi hiki cha Uchaguzi Mkuu, ili kijihakikishia ushindi Mkubwa kwa CCM.
Imetolewa na;
Said Said Nguya
Afisa Habari
Ofisi ya Katibu Mkuu
CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM)
PICHA: Rais Wa Tanzania Dr Magufuli Ampokea Mgeni Wake Rais Wa Burundi Evariste Ndayishimiye Mkoani Kigoma
Watanzania Chagueni Viongozi Wanaohubiri Amani – Majaliwa
MJUMBE wa Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Kassim Majaliwa amewataka Watanzania wawachague viongozi wanaohubiri amani ikiwa ni moja ya tunu ya Taifa hili.
Ametoa wito huo jana jioni (Ijumaa, Septemba 18, 2020) alipokuwa akizungumza na wakazi wa kata Bunda Stoo, wilaya ya Bunda, mkoani Mara kwenye mkutano uliofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Miembeni.
Alikuwa akimuombea kura mgombea urais kwa tiketi ya CCM, Dkt. John Pombe Magufuli, mgombea ubunge wa jimbo la Bunda Mjini, Bw. Robert Chacha Maboto, mgombea udiwani wa kata ya Bunda Stoo, Bw. Joseph Nyamangoko na wagombea udiwani wengine 13 wa kata za wilaya ya Bunda waliokuwepo kwenye mkutano huo.
Mheshimiwa Majaliwa alisema ni muhimu kwa wananchi kuchagua chama ambacho kitalinda amani ya nchi hii. “Amani ya nchi hii inaanza kuonekana kwa viongozi wenyewe wanapokuja kuomba ridhaa kwenu, sina mashaka mmeshaanza kuona na kujifunza ni kiongozi yupi ataleta amani katika nchi hii.”
Alisema kuwa Chama cha Mapinduzi kinaomba ridhaa ya Watanzania kwa awamu ya tano ya kipindi cha pili ili kuifanya Tanzania kuwa na amani na iendelee kuwa kimbilio kwa nchi zilizokosa amani.
Mheshimiwa Majaliwa aliongeza kuwa ni muhimu kupata kiongozi atakayeleta amani, maendeleo, mpenda mabadiliko, mpenda Watanzania na wanyonge wote; “na kwa sasa ni Rais Dkt. John Magufuli anayeweza kutekeleza hayo,” alisisitiza.
Mheshimiwa Majaliwa alisema kuwa Rais Dkt. Magufuli kwa kutambua umuhimu wa sekta ya mifugo na kilimo aliamua kuviacha vijiji 920 kati ya 970 viendelee na shughuli za malisho na kilimo kwenye maeneo ya hifadhi na eneo la kinga la mita 500.
Akifafanua kuhusu mafanikio yaliyopatikana kwenye sekta ya elimu ikiwa ni utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2015-2020, Mheshimiwa Majaliwa alisema sh. bilioni 4.9 zilitolewa kwa shule za msingi 100 za wilaya hiyo kwa ajili ya ukarabati, masuala ya utawala, michezo, mitihani na posho kwa maofisa elimu kata na walimu wakuu.
“Kwenye shule zenu za sekondari hapa Bunda, shilingi bilioni 1.8 zilitolewa kwa shule 17 kwa ajili ya fidia ya ada, chakula kwa shule za bweni na posho ya madaraka kwa wakuu wa shule.”
Akielezea mfumo wa uboreshaji wa miundombinu ya shule wa Lipa Kutokana na Matokeo (EP4R) uliotekelezwa tangu 2015 hadi 2020, Mheshimiwa Majaliwa alisema sh. milioni 364.2 zilitolewa kwa ajili ya ukamilishaji wa miundombinu ya madarasa, vyoo na nyumba.
Alizitaja shule zilizonufaika na maboresho hayo kuwa ni shule za msingi Ikizu, Busore, Bigegu, Haruzale, Tingirima, Karukekere A, Rakana, Bunyunyi, Kasuguti, Nyabuzame, Kiloleri, ibwagalilo na Nyamitwebili.
“Shule za sekondari zilipatiwa shilingi milioni 667 kwa ajili ya ukarabati na ujenzi wa miundombinu ya shule ikiwemo maabara, madarasa, mabweni na vyoo kwa shule za Makongoro, Mwibara, Bulamba, Chisorya, Nyamag’uta, Hunyari, Nyeruma, Esperanto na Mwigundu,” alisema.
Kwenye sekta ya barabara, Mheshimiwa Majaliwa alisema wilaya ya Bunda imepatiwa sh. bilioni 46.5 ambazo zinatumika kujenga km. 56.4 za barabara ya Nyamuswa – Bunda – Bulamba kwa kiwango cha lami ikiwa ni awamu ya kwanza.
Alisema kiasi kingine cha sh. bilioni 2.9 kimetumika kutengeneza barabara kwenye sehemu korofi, madaraja na makaravati na matengenezo ya kawaida
Majaliwa Amjulia Hali Mama Maria Nyerere
FULL POWER, ZATI 50 NI KIBOKO YA TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA UUME MDOGO
UMMY MWALIMU KUCHOCHEA UJENZI WA VIWANDA VIPYA JIJINI TANGA
MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu akizungumza na wananchi wa Kata ya Mnyanjani Jijini Tanga wakati wa mkutano wake wa kampeni |
MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu kushoto akimndai Mgombea Udiwani wa Kata ya Mnyanjani Yakubu Nuru wakati wa mkutano wa kampeni wa Ummy
MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu katikati akiwa na viongozi wa CCM wilaya ya Tanga kulia ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga Meja Mstaafu Mkoba na Katibu wa CCM wilaya ya Tanga Salim Kidima kushoto ni Mgombea Udiwani wa Kata ya Mnyanjani Yakub Nuru
MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu katikati akiwa kwenye meza akifuatia matukio mbalimbali kwenye mkutano wake wa kampeni kulia ni Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Tanga Meja Mstaafu Mkomba na kushoto ni Mgombea Udiwani wa Kata ya Mnyanjani Yakub Nuru BONDIA Hasani Mwakinyo akimuombea kura Mgombea Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu kwenye mkutano huo
MSANII wa mziki wa Bongofleva Kassim Mganga akiimba wakati wa kampeni hizo
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu akishiriki kucheza kabla ya kunadi sera zake
MSANII mchina mweusi akiimba wakati wa mkutano huo
BONDIA Hassani Mwakinyo kushoto akiwa akimsikiliza Mgombea Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu
Wananchi wakifuatilia mkutano wa Mgombea Ubunge wa Jimbo la Tanga Ummy Mwalimu
Wananchi wakifuatilia mkutano wa Mgombea Ubunge wa Jimbo la Tanga Ummy Mwalimu Wananchi wakifuatilia mkutano wa Mgombea Ubunge wa Jimbo la Tanga Ummy Mwalimu
Sehemu ya wananchi waliojitokeza kwenye mkutano huo
MGOMBEA Ubunge wa Jimbo la Tanga (CCM) Ummy Mwalimu amesema endapo akichaguliwa atachochea ujenzi wa viwanda vipya katika Jiji la Tanga ili kuongeza fursa za ajira kwa vijana na wakina mama ili kukuza uchumi.
Ummy ambaye pia ni Waziri wa Afya Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto aliyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Mnyanjani Jijini Tanga wakati wa mkutano wake wa kampeni.
Alisema kwamba hilo litafanikiwa kutokana na kuwa na mtandao wa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi hivyo ataweka msukumo wao kuja Jijini Tanga kujenga viwanda ili wakina mama waweze kupata ajira na vijana.
Mgombea huyo alisema wakishakuwepo itachangia fursa za ajira huku wajasiriamali wapata biashara,mama lishe ,bodaboda watapata biashara hatua ambayo itawasaidia kuinuka kiuchumi wao na jamii zao
“Lakini jambo la pili ni nitainua uchumi wa Tanga na kusukuma uboreshaji wa Bandari ya Tanga huku akimshukuru Rais Dkt John Magufuli kupawatia Bilioni 372 ili kuboresha Bandari ya Tanga”Alisema
“Hivyo niwaombe wana Mnyanjani mnichague ili nikasukume maboresho ya awamu ya pili ya Bandari ya Tanga tuweze kuona meli kubwa zikitia nanga kwenye Bandari ya Tanga”Alisema
Alisema meli zikitia nanga kwenye Bandari hiyo itasaidia kufungua fursa za ajira kwa wananchi na hivyo kuinua uchumi wa wakazi wa Jiji la Tanga .
“Lakini Bandari ya Tanga ikiboreshwa nitapigania mizigo yote inayoingia nchini na kwenda mikoa ya Kanda ya Kaskazini ishushwe kwenye Bandari ya Tanga badala ya Dar es Salaam”Alisema
Hata hivyo alisema ameamua kugombea ubunge ili aweze kuwatumikia wana Tanga sambamba na kuchochea mradi mkubwa wa ujenzi wa bombo la Mafuta kutoka hoima nchini Uganda hadi Bandari ya Tanga.