Monday 6 July 2020

HAWA NDIYO MAKATIBU TAWALA WA WILAYA SITA WALIOTEULIWA MUDA HUU


Share:

WANAWAKE WATAKA KUUZA ALIZETI YAO KAMA BIDHAA BADALA YA MALIGHAFI


Viongozi na wajumbe wa kikundi cha Mkombozi na Tumaini wakionesha alizeti
Na Sumai Salum- Meatu

Vikundi vya wanawake vya Tumaini Group na Mkombozi Group vilivyopo kata ya Sakasaka wilayani Meatu mkoani Simiyu wamesema hawatauza tena alizeti kama malighafi bali watauza kama bidhaa kutokana na tathmini walizoziona kwenye zao hilo.


Hayo waliyabainisha wakati wanapoendelea na maandalizi maonesho ya Nane Nane yanayotarajia kufanyika kwa mwaka wa tatu sasa kama ilivyo agizo la serikali katika mkoa wa Simiyu ifikapo Agosti 8 mwaka huu.

Walidai kuwa kuuza malighafi kumewachelewesha kufikia malengo ya kundi hilo pamoja na maendeleo ya mtu mmoja mmoja kwani wamekuwa wakipata pesa kidogo ukilinganisha na mafuta ya zao hilo.

“Tumekusudia tuuze alizeti zetu baada ya kuchakata mafuta na kwa gunia moja linatoa lita 17 za mafuta na ukiuza unapata shilingi 60,000/= au 55,000/=/= na ukiuza alizeti bila kusindika unapata 30,000/= ambayo ni hasara kwa mkulima na kikundi, kwa gunia zetu 12 kikundi kitapata faida kubwa itatusaidia kusomesha watoto na maandalizi ya mashamba kwa mwakani” alisema Bi. Christina mhasibu wa Mkombozi Group

“Mradi huu wa alizeti tuliofadhiliwa na REDESO umetupatia manufaa kwani mwaka jana tulipouza mafuta ya alizeti pesa zile zilitusaidia wanakikundi kwani tulikopeshana kwa lengo la kuanzisha miradi ya mtu binafsi wakati tusipokuwa na alzeti tukakopeshana pesa kila mtu 50,000 kwa liba ya 10% wapo waliolima pamba,karanga na hata mahindi pia na vinatusaidia”,alisema Mwenyekiti kikundi cha Tumani Bi.Elizabeth Bisha.

Mbali na hayo, Afisa maendeleo ya jamii kata ya Sakasaka wilayani Meatu mkoani Simiyu Bi. Mbuke Jaulula aliwataka akina mama wakulima wa vikundi vilivyoko katika kata hiyo kuendelea kuwapa wanawake na wanajamii wengine elimu juu ya ulimaji wa zao la alizeti licha ya kuwa linasitahimili ukame bali pia ni zao lenye faida kwa kutoa mafuta na hata chakula cha mifugo lakini pia kwa mwezeshaji wa kikundi hicho ambaye ni REDESO apate mrejesho mzuri dhidi ya matarajio yao wanayoyategemea baada ya kuwawezesha wanakikundi.

“Mwaka huu tumewezeshwa na REDESO mbegu bora za alizeti kwa vikunndi vinne na tumevuna gunia 2 hadi 3 kwa hekali kwa magunia ya debe 6 na tutanufahika pakubwa hivyo niwasihi wanajamii wa kata ya sakasaka hasa wanawake wa jamii hii ya kisukuma kwa kuwa bado kuna mila kandamizi, kupitia kilimo hiki tuwe na amasa zaidi ya ufugaji wa kisasa ikilinganishwa na kuwa tunaishi pembezoni mwa hifadhi na kukosa sehemu ya malisho kwa kulima zao hili tutapata chakula cha mifugo pia na hawatahangaika”aliongeza Bi. Jaulula.

Kwa upande wake Mratibu miradi na Meneja kutokea asasi isiyokuwa ya kiserikali REDESO inayofanya kazi wilayani Kishapu mkoani Shinyanga na baadhi ya kata za wilaya ya Meatu mkoani Simiyu Bw. Charles Buregeya amewapongeza wanakikundi hao huku akiwataka wasiridhike kwa mavuno hayo bali waendeleze bidii na jitihada katika uzalishaji ili waweze kufikia angalau gunia 7 hadi 8 kwa hekali moja kama inavyoshauliwa kitaalamu.

“Lakini pia kijasiriamali mmeonesha ukomavu kwani kuuza alizeti peke yake hautapata tija ukilinganisha na mafuta ila ninachotaka mkizingatie ni kuhakikisha mmeboresha uzalishaji,usindikaji na vifungashio ili tuweze kuingia kwenye ushindani na pia tuhakikishe tunatafuta masoko ili tuweze kuingia kwenye soko la ushindani, na pia shukrani kwa serikali kupitia maendeleo ya jamii kwa ushirikiano wanaotupatia”,alisema Buregeya.
Viongozi na wajumbe wa kikundi cha Mkombozi na Tumaini
Mratibu miradi na Meneja kutoka asasi isiyokuwa ya kiserikali REDESO inayofanya kazi wilayani Kishapu mkoani Shinyanga na baadhi ya kata za wilaya ya Meatu mkoani Simiyu Bw. Charles Buregeya akizungumza
Afisa maendeleo ya jamii kata ya Sakasaka wilayani Meatu mkoani Simiyu Bi. Mbuke Jaulula akizungumza
Afisa maendeleo ya jamii kata ya Sakasaka wilayani Meatu mkoani Simiyu Bi. Mbuke Jaulula na Mratibu miradi na Meneja kutoka asasi isiyokuwa ya kiserikali REDESO inayofanya kazi wilayani Kishapu mkoani Shinyanga na baadhi ya kata za wilaya ya Meatu mkoani Simiyu Bw. Charles Buregeya wakipiga picha ya pamoja na viongozi wa vikundi vya Mkombozi na Tumaini
Share:

TCRA YAIFUNGIA KWANZA TV KWA MIEZI 11

Kamati ya Maudhui ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imekifungia kituo cha Kwanza Online TV  kwa muda wa miezi kumi na moja (11) baada ya kusikiliza shauri la ukiukaji wa kanuni za utangazaji kufuatia taarifa iliyochapishwa katika ukurasa wake wa Instagram



Share:

MGODI WA WDL WATAKA KUUZWA KINYEMELA



Waziri wa Madini Doto Biteko akijipaka kitakasa mikono baada ya kupimwa joto kwenye mgodi wa Williamson Diamond Limited alipokuwa kwenye ziara yake Mwadui wilayani Kishapu mkoa wa Shinyanga.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjla akipimwa joto kabla hajaingia kwenye ukumbi wa mkutano katika mgodi wa Williamson Diamond Limited nyuma yake ni Mwenyekiti wa Tume ya Madini Prof. Idris Kikula.
Waziri wa Madini Doto Biteko akifafanua jambo kwenye kikao katika mgodi wa Williamson Diamond Limited uliopo Mwadui wilayani Kishapu mkoa wa Shinyanga


Baadhi ya washiriki walioshiriki kikao cha Waziri wa Madini katika mgodi wa Williamson Diamond Limited uliopo Mwadui wilayani Kishapu mkoa wa Shinyanga.


Baadhi ya washiriki walioshiriki kikao wa Waziri wa Madini katika mgodi wa Williamson Diamond Limited uliopo Mwadui wilayani Kishapu mkoa wa Shinyanga.

Waziri wa Madini Doto Biteko akizungumza jambo kwenye kikao katika mgodi wa Williamson Diamond Limited uliopo Mwadui wilayani Kishapu mkoa wa Shinyanga.

Waziri wa Madini Doto Biteko kushoto akiwa ameongozana na Katibu Mkuu Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjila mara baada ya kikao katika mgodi wa Williamson Diamond Limited uliopo Mwadui wilayani Kishapu mkoa wa Shinyanga.


Katibu Mkuu Wizara ya Madini Prof. Simon Msanjila akielekea kwenye gari mara baada ya kikao katika mgodi wa Williamsoni Diamond Limited uliopo Mwadui wilayani Kishapu mkoa wa Shinyanga.

Mkuu wa Wilaya ya Kishapu Nyabaganga Talaba akizungumza jambo kwenye kikao kilichofanyika katika mgodi wa Williamson Diamond Limited uliopo Mwadui wilayani Kishapu mkoa wa Shinyanga.


Muonekano wa mgodi wa madini ya Almasi wa Wiliamson Diamond Limited uliopo Mwadui wilayani Kishapu mkoa wa Shinyanga.



Na Tito Mselem ,Shinyanga 

Waziri wa madini Doto Biteko amesikitishwa na kitendo walichokifanya uongozi wa mgodi wa madini ya Almasi wa Williamson Diamond Limited (WDL), uliopo Mwadui katika wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga cha kutaka kuuza kinyemela mgodi huo bila  Serikali kupewa taarifa.



Hayo yamesemwa  Julai 5, 2020 na Waziri wa Madini Doto Biteko alipofanya ziara yake kwenye mgodi huo mara baada ya kuona matangazo ya kuuzwa kwa mgodi huo kwenye mitandao ya kijamii.



Waziri Biteko, alisema Serikali inaubia wa asilimia 25 katika mgodi wa WDL, haiwezekani utakekuuzwa bila mmbia wake kufahamu   kitendo hicho ni kukiuka taratbu na Sheria za nchi.



“Serikali inaubia wa asilimia 25 kwenye mgodi huu kama mnataka kuuza mgodi lazima mtoe taarifa serikalini na mpate kibali, kwa mantiki hiyo serikali inapaswa kuwaadhibu kwa kutaka kuuza mgodi bila kibali huko ni kuhujumu nchi,hivi mlituuliza serikali hatuna uwezo wa kununua mgodi na kuuendesha?,” alisema Waziri Biteko.



Kutokana na kitendo hicho, Waziri Biteko ameuagiza uongozi wa mgodi huo kufikia Julai 10 mwaka huu wawe wametoa maelezo kwa maandishi kueleza sababu za kutaka kuuza mgodi huo bila mmbia wake ambaye ni Serikali kujua na pia, kutoa taarifa ya kuwapunguza kazi wafanyakazi kisha kuwalipa nusu mshahara.



Alisema wafanyakazi waliopunguzwa kazi kwa kutumia kigezo cha ugonjwa wa Corona utaratibu uliotumiwa haufai na wao kama Wizara ya Madini hawakubaliani nao kutokana na kulipwa mishahara nusu jambo ambalo linawapa wakati mgumu na kusababisha migogoro isiyo ya lazima.



Aidha, Waziri Biteko, alisema sababu ambazo wanazitoa mgodi huo za kusitisha shughuli za uzalishaji na kutaka kuuza mgodi huo ni kushuka kwa bei ya almasi duniani iliyosababishwa na ugonjwa wa corona, ambapo alieleza kuwa sababu hizo hazina mashiko ila wawe wakweli kama wamefilisika ijulikane.



Waziri Biteko alisema sababu kubwa ambayo ingefanya mgodi huo kufungwa ni kushuka kwa uzalishaji na siyo uendeshaji, huku akihoji kama mgodi hauna fedha za kujiendesha wangesema badala ya kuweka matangazo kwenye mitandao mgodi unauzwa wakati serikali haina taarifa.

kwenda mitandaoni.



Kwa upande wake meneja mkuu wa mgodi huo Mhandisi Ayoub Mwenda, alikiri kuwa hawakutoa taarifa Serikalini juu ya kutaka kuuzwa kwa mgodi huo, huku akieleza kuwa walifunga mgodi huo April 8 mwaka huu kutokana na kushindwa kujiendesha na ameahidi kufuata maelekezo yote ambayo yametolewa na Waziri wa Madini.



Mhandisi Mwenda alisema walikuwa wanazalisha vizuri kabla ya mlipuko wa ugonjwa wa Corona ambapo kwa mchanga waliokuwa wameuzalisha walikuwa mbele kwa asilimia tatu na almasi walizokuwa wamezikusanya walikuwa mbele kwa asilimia 9.1kulingana na bajeti yao waliyokuwa wameiweka.



Alisema tatizo la Corona limeuathiri sana mgodi huo na kusimama kufanya shughuli za uzalishaji kutokana na kushuka bei ya masoko ya nje ambapo kabla ya Corona bei ilikuwa dola 246 kwa karati moja ambapo Machi mwaka huu waliuza karati moja dola 135 ambayo ilikuwa haiwezi kutosheleza gharama za uzalishaji.



Mkuu wa wilaya ya Kishapu Nyabaganga Talaba ameipongeza Wizara ya Madini kwa kazi nzuri wanazozifanya ambapo wamesaidia nchi kuingia katika uchumi wa kati.

Share:

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta Alegeza Masharti Ya Kukabiliana Na Corona

Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta amelegeza kwa kiasi fulani sheria kali zilizokuwa zimewekwa kwa ajili ya kukabiliana na maambukizi ya ugonjwa wa COVID-19

Akilihutubia taifa  hilo leo Jumatatu katika Jumba la Harambee jijini Nairobi, Rais Kenyatta ametangaza kuondoa marufuku ya safari ya watu kuingia au kutoka katika kaunti za Nairobi, Mombasa na Mandera kuanzia kesho Jumanne.

Hata hivyo amesema kuwa agizo la kutotoka nje kuanzia saa tatu usiku hadi saa kumi alfajiri litaendelea kuwepo kwa kipindi cha siku 30 zijazo.

Vile vile, Rais Uhuru Kenyatta amesema makanisa na misikiti itafunguliwa lakini waumini wasiozidi 100 ndio watakaoruhusiwa kuhudhuria ibada na kwa muda usiozidi saa moja. Shule za Jumapili na madrasa zitasalia kufungwa kwa muda wa siku 30.

Hali kadhalika Rais wa Kenya amesema safari za ndege za ndani ya nchini zitaanza Julai 15, huku zile za kimataifa zikitazamiwa kuanza Agosti Mosi, lakini kwa kufuata tahadhari za kiafya.


Share:

Makamu Wa Rais Mhe. Samia Amuwakilisha Rais Dkt. Magufuli Malawi

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na Rais wa Malawi Mhe. Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera  muda mfupi baada ya kusimikwa rasmi  kuwa Rais wa Jamhuri ya Malawi leo Julai 06,2020 kwenye Sherehe iliyofanyika katika Kambi ya Jeshi ya Kamuzu,  Lilongwe nchini Malawi.(Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)


Share:

Benard Membe Arudisha Kadi Ya Uanachama CCM

Aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya nje ya nchi wa Tanzania,na kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Benard Membe,amerejesha kadi ya uanachama wa Chama hicho.

Membe amerejesha kadi hiyo leo Jumatatu tarehe 6 Julai 2020 nyumbani kwake Rondo mkoani Lindi.

“Leo saa 6 na nusu mchana mimi na mke wangu nikisindikizwa na mamia ya wananchi wa Rondo, tumerejesha kadi zetu za CCM kwa wenyewe. Nimemwandikia KM (katibu mkuu) wa CCM kuhusu tukio hilo na kukishukuru chama kwa mema yote kilichonitendea. Nawatakia kila la heri viongozi na wanachama wote,” ameandika Membe kupitia ukurasa wake wa Twitter


Tarehe 28 Februari 2020, Kamati Kuu ya CCM ilitangaza kumfukuzwa uanachama Membe kwa madai amekuwa akikiuka taratibu na miongozo ya chama hicho



Share:

Nafasi ya Kazi katika Sekretarieti ya Jumuiya ya Madola




Share:

Rais Magufuli awasimamisha kazi viongozi wa polisi, Afisa Usalama kwa uzembe

Rais Magufuli ameagiza kusimamishwa kazi kwa Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Arumeru na Afisa Usalama wa Wilaya hiyo mkoani Arusha kwa kushindwa kutumiza majukumu yao.

Akizungumza wakati wa kuwaapisha viongozi aliowateua hivi karibuni, Rais Magufuli amesema kuwa viongozi hao wameshindwa kutimiza wajibu wao wa kukabiliana na dawa za kulevya, hadi maofisa kutoka makao makuu walipofika na kubaini uwepo wa kiwango kikubwa cha bangi.

Wakati huo huo, Rais Magufuli amempandisha cheo James Kaji kuwa Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya ambapo awali alikuwa akikaimu nafasi hiyo.

Akitangaza uamuzi huo wa kumthibitisha Kaji pamoja na kumuapisha, Rais Magufuli amesema anachotaka kuona ni matokeo ya kazi wanazofanya wasaidizi wake.


Share:

Monitoring & Evaluation Officer Job vacancy at Plan International

The Organisation Plan International is an independent development and humanitarian organisation that advances children’s rights and equality for girls. We believe in the power and potential of every child. But this is often suppressed by poverty, violence, exclusion and discrimination. And it’s girls who are most affected. Working together with children, young people, our supporters […]

The post Monitoring & Evaluation Officer Job vacancy at Plan International appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

RAIS DKT MAGUFULI AMEWAAPISHA VIONGOZI MBALIMBALI ALIOWATEUA IKULU CHAMWINO JIJINI DODOMA LEO


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha Bi. Mriam Perla Mbaga kuwa Katibu Tawala wa mkloa wa Simiyu kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Dodoma Julai 6, 2020
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha baada ya kumthibitisha Bw. James Kaji kuwa Kamishna Jenerali wa Mamlaka ya Udhibiti wa Dawa za Kulevya nchini (DCEA) kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Dodoma
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimuapisha wa Polisi Thobias Emir Andengenye kuwa Mkuu wa Mkoa wa Kigoma kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Dodoma
Wateuliwa wakila kiapo cha maadili ya Viongozi mbele ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Dodoma

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea baada ya kuwaapisha viongozi mbalimbali aliowateua  kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Dodoma
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akishuhudia Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Marco Gaguti akimuapisha Kanali Mathias Kahabi  kuwa Mkuu wa Wilaya ya Biharamulo kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Dodoma
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akishuhudia Mkuu wa Morogoro Mhe. Loatha Ole  Sanare akimuapisha Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Magereza (SACP) Ismail Twahir Mlawa kuwa Mkuu wa Wilaya ya Biharamulo kwenye haflailiyofanyika Ikulu Chamwino Dodoma
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akishuhudia Mkuu wa Mkoa wa Pwani akimuapisha Mhandisi Martine Ntemo kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kibaha kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Dodoma Julai 6, 2020

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea mara baada ya kuwaapisha viongozi aliowateuwa katika hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiondoka sehemu ya tukio baada ya kuwaapisha viongozi aliowateuwa katika hafla iliyofanyika Ikulu Chamwino Mkoani Dodoma
PICHA NA IKULU
Share:

IGP SIRO AWAPA MTIHANI WAKUU WA POLISI WILAYA NCHINI.

KAIMU Mkuu wa wilaya ya Pangani ambaye pia ni Mkuu wa wilaya ya Muheza Mhandisi Mwanasha Tumbo akizungumza jambo wakati wa ziara ya Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro kulia wilayani Pangani kushoto ni Mkuu wa Polisi wilaya ya Pangani Georgina Matagi
MKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Siro akizungumza na wadau wa maendeleo wilayani Pangani wakati wa ziara yake wilayani humo ambapo aliwashukuru kwa kufanikisha ujenzi wa kituo cha Polisi kushoto ni Kaimu Mkuu wa wilaya ya Pangani Mhandisi Mwanasha Tumbo ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Muheza na kulia ni Kamanda wa Polisi Mkoani Tanga Blasius Chatanda
 MKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro kulia akionyeshwa michoro mbalimbali ya kituo cha Polisi cha zamani wilayani Pangani na Mkuu wa Polisi wilaya ya Pangani (OCD) Georgina Matagi wakati alipokwenda kuwashukuru wasamaria wema wilayani humo waliojitolea ujenzi wa kituo cha Polisi ili kutokomeza uhalifu
 Sehemu ya wadau wa maendeleo wilayani Pangani wakimsikiliza kwa umakini Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro
Sehemu ya wadau wa maendeleo wilayani Pangani wakimsikiliza kwa umakini Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro

 MKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro kushoto akipata maelezo mapokezi wakati alipoingia kwenye kituo cha Polisi Pangani akiwa na kulia Mkuu wa Polisi wilaya ya Pangani (OCD) Georgina Matagi na Katibu Tawala wa wilaya ya Pangani Mwalimu Hassani Nyange


 MKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Simon Sirro akikitembelea kituo cha Polisi Pangani wakati alipokwenda kuwashukuru wasamaria wema kwa kujitokea kufanikisha ujenzi wa kituo cha Polisi kulia ni Mkuu wa Jeshi la Polisi wilaya ya Pangani (OCD) Georgina Matagi

MKUU wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro amewapa mtihani mkubwa wakuu wa Polisi wa wilaya nchini (OCD) ambao watakutwa kwenye maeneo yao hawajafanya jambo lolote la kimaendeleo atalazimika kuondokana nao kutokana na kwamba watakuwa hawana tija.

IGP Siro aliyasema hayo wakati alipofika wilayani Pangani kwa lengo la kuwashukuru wasamaria wema waliojitolea kufanikisha ujenzi wa kituo cha Polisi wilayani humo juhudi ambazo zimefanywa na Mkuu wa Polisi wa wilaya hiyo Georgina Matagi.

Alisema kwamba kazi kubwa iliyofanywa na Mkuu huyo wa Polisi wilaya kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo inapaswa kuigwa na wakuu wengine hapa nchini huku akiwataka kuacha kuwa watu wa kulialia bali wahakikishe wanakuwa wabunifu kwa kuiga mfano wa OCD wa Pangani.

“MaOCD msiwe watu wa kulia muwe wabunifu kuiga mfano wa Mkuu wa Polisi Pangani (OCD) huku akimtaka kuendelea hivyo hivyo kwa sababu kwani kuna ma ocd mawe hawafikirii namna ya kusaidia jeshi anachojua ni kumsubiri IGP ampelekee fedha…IGP yupo sawa,Amri Jeshi Mkuu yupo,wewewni ODC na RPC kuna vitu unaaweza kujiongeza kwa kuwatumia wadau werevu kuweza kusaidia”Alisema IGP Siro.

“Lakini pia OCD umenipa changmoto mimi niko smati sana sijua imekuwaje nikaisahau Pangani mpaka wewe bwana mdogo ukaja kufanya hii kazi nzuri hongera sana kwa kazi kubwa na nzuri ya kuhakikisha ujenzi huo unafanyika na kukamilika “Alisema

Aidha aliwashukuru wadau hao na OCD kwa kazi kubwa ya kulisaidia Jeshi la Polisi kujenga kituo hicho  huku akiwaambie kwamba walichokifanya kwa faida ya watanzania wote kwa kuacha alama ya kesho na kesho kutwa haupo watu watakukumbuka hivyo kwa niaba ya Rais niwashukur sana kwa kazi nzuri mliyofanya kituo hiki huku nyuma hahakikuwa hivi msione mmepoteza bali mmeongeza fursa.

Hata hivyo alisema kwamba kuna vitu ambavyo havijakamilika hivyo nitatoa milioni tano huku akiwaomba wadau wa maendeleo nchi nzima walisaidie Jeshi la Polisi kwa sababu usalama ndio kila kitu wanakwenda msikitini na kanisani kwa sababu ya usalama na usipokuwepo ni hatari hivyo kila mtu ambaye mungu amemjalia kipato akiona mahali kuna shida ya kituo cha Polisi asaidie,kwani vituo hivyo vitawasaidia.

Akizungumzia suala la usalama IGP Siro alisema suala hilo ni muhimu sana na ukishavurujika ni vigumu sana kuweza kuurudisha huku akitolea mfano watu wa  msumbuji kwa sabau usalama haupo hapa ni mpakani wakati wa uchaguzi watu  wenye nia mbaya wanaweza kuleta mambo ya hivyohovyo watoe taarifa wasimuamini kila mtu ni vuzuri wakavijulisha vyombo vya ulinzi na usalama.

Alisema kwamba wakati wa uchaguzi lolote linaweza kufanyika wabaya wetu wakachukua nafasi kufanya mambo maovu wanaweza kuingia hivyo niwaombe mkiona ya namna hiyo hakikisheni mnatoa taarifa kwenye vyombo vinavyohusika ili kuweza kufanyiwa kazi mambo hayo.

Hata hivyo alisema usalama watanzania walioukuta wajitahidi sana kuulinda huku akisema wachache wanaotaka kuleta figisufigisu watahakikisha wanashughulikiwa na kurudishwa kwenye mstari.

Awali akizungumza Kaimu Mkuu wa wilaya ya Pangani Mhandisi Mwanasha Tumbo ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Muheza alisema huo ni utekelezaji wa serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt John Magufuli kupitia CCM kwamba lazima askari wawe na maeneo mazuri ya kufanyia kazi na wananchi waweze kupata huduma nzuri wadau hao wamejitolea kwa kushirikiana na serikali kazi kubwa imefanyika
Share:

Mtandao Wa Maji Ruangwa Wamtua ‘wamtua Ndoo Mama Kichwani’

Na Mwandishi Wetu, MAELEZO
SERIKALI kupitia Wizara ya Maji imeendelea kutekeleza miradi mbalimbali ya maji katika maeneo ya mijini na vijijini kupitia Programu ya Maendeleo ya Sekta ya Maji kwa mujibu wa Sera ya Taifa ya Maji ya mwaka 2002.

Sera ya Taifa ya Maji ya mwaka 2002 inaelekeza kuwapatia wananchi waishio vijijini maji safi na salama katika umbali usiozidi mita 400 kutoka kwenye makazi yao, hatua inayolenga kuwaondelea changamoto mbalimbali ikiwemo maskini na magonjwa yanayosababishwa na maji.

Wizara ya Maji kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imeendelea kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi waishio vijijini kwa kujenga, kupanua na kukarabati miradi ya maji, lengo ikiwa ni kufikia asilimia 85 ya wananchi wanaopata huduma ya maji safi na salama katika maeneo ya vijijini ifikapo mwaka 2020.

Miradi ya Maji Vijijini inatekelezwa na Mamlaka za Serikali za Mitaa kwa kushirikiana na wananchi pamoja na sekta binafsi ambapo katika kuwapunguzia wananchi gharama, Serikali kwa kushirikiana na wadau inaandaa mifumo itakayofaa kusimamia na kuendesha miradi ya maji ikiwa ni pamoja na kuviimarisha Vyombo vya Watumiaji Maji.

Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa Mkoani Lindi inatekeleza miradi mbalimbali ya maji katika vijiji mbalimbali vya Wilaya hiyo hatua inayolenga katika kutoa huduma endelevu kwa wakazi waishio mijini na pembezoni mwa miji.

Wananchi wanaendelea kupata huduma ya maji safi na salama kutoka katika vyanzo vya Visima vifupi, Visima vya kati, Visima virefu ambavyo vimefungwa pampu za mikono, miradi ya maji bomba ya maporomoko na miradi ya maji ya kusukumwa na mitambo.

Tangu kuingia madarakani kwa Serikali ya Awamu ya Tano, hali ya upatikanaji wa huduma ya maji vijijini imeongezeka kutoka 38.5% mwaka 2015 hadi kufikia 51.20% kufikia mwezi Novemba, 2018 ikiwa ni ongezeko la 12.7% ambapo jumla watu 64,498 waishio vijijini wanapata huduma ya maji.

Miongoni mwa miradi hiyo ni pamoja na Mradi wa Maji wa Naunambe-Mpekenyera unaosimamiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kwa kushirikiana na Kamati za Vijiji vya Naunambe na Mpekenyera katika kuhakikisha kuwa Serikali inamtua mama ndoo kichwani na kumuondolea changamoto ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma ya maji.

Kufuatia juhudi kubwa zilizofanywa na Serikali ya Wilaya ya Ruangwa mradi huo ulikamilika mwezi Juni, 2018 na jumla wananchi 7,000 wameanza kupata maji na salama na kiasi Tsh. Milioni 828 zimetumika kwa ajili ya utekelezaji wa mradi huo, ikiwemo ununuzi wa vifaa mbalimbali ikiwemo mashine za kusafisha maji na miundombinu mbalimbali kwa ajili ya kurahisisha upatikanaji wa maji kutoka katika vyanzo na kuwafikia wananchi.

Akizungumza na Timu ya Maafisa Habari wa Idara ya Habari (MAELEZO) waliofanya ziara Wilayani humo, hivi karibuni, Katibu wa Mradi huo, Selemani Nyamiri anasema mradi huo ulianza kuibuliwa na wananchi mwaka 2010 kwa kaya mbalimbali katika vijiji hivyo kuchangishana fedha kwa ajili ya kuhakikisha mradi huo unatoa huduma endelevu ya maji katika vijiji hivyo vyenye wakazi zaidi ya 10,000.

‘Maji yaliyokuwa yakizalishwa katika chanzo cha Mpekenyeara yalikuwa yana chumvi sana, pia yalipatikana katika vyanzo visivyo safi na salama hivyo ilitulazimu kushirikiana na Halmashauri ya Wilaya kwa ajili ya kutumia mafundi na utaalamu wa ziada ili kuhakikisha kuwa maji yanarejea katika ubora wake’’

Nyamiri anasema kwa sasa kiwango cha chumvi katika maji hayo kimepungua na kufanya maji hayo kuwa na ubora wa matumizi kwa binadamu, ambapo watumiaji wanalazimika kuchangia gharama ya Tsh. 200 kwa kila ndoo, ikiwa ni fedha zinazokusanywa na kamati hiyo kwa ajili ya kufanya matengenezo na ukarabati wa miundombinu ya mradi.

Akifafanua zaidi anasema wananchi wa vijiji hivyo wataendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali katika kuboresha huduma za maendeleo ya jamii ikiwemo huduma ya maji ambapo wananchi wamekuwa na mwamko wa kusimamia uhifadhi wa maeneo ya vyanzo vya maji ili kufanya vijiji vyote vinapata maji ya uhakika.

Naye Mwenyekiti wa Kijiji cha Naunambe Bi. Amina Abdalla aliipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kupitia Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa kwa kusimamia utekelezaji wa mradi huo kwa kuwa umeondoa kero kwa akina mama wa vijiji hivyo waliokuwa wakisafiri umbali mrefu kutafuta huduma ya maji.

Bi. Rehema Mussa Mkazi wa Kijiji cha Mpekenyera alisema kwa kipindi cha nyuma hali ya upatikanaji wa huduma ya maji katika vijiji hivyo haikuwa ya kuridhisha, hususani wakati wa kipindi cha kiangazi na kuwalazimu wananchi wengi kutembea umbali wa kilometa 3 kufuata huduma ya maji katika vyanzo visivyo rasmi huku wakitembea na watoto migongoni.

‘Utekelezaji wa mradi huu ni mkombozi mkubwa sana kwetu wananchi wa Naunambe na Mpekenyera kwani kwa sasa shida ya maji imeisha, tunaipongeza Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Magufuli pamoja na juhudi kubwa zinazofanywa na Mbunge wetu wa Ruangwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa’’ alisema Rehema.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa, Andrea Chezue alisema hali ya upatikanaji wa maji katika Wilaya hiyo umefikia asilimia 55  huku kukisaliwa na maeneo machache ambayo yanakosa huduma ya maji ambapo Ofisi yake imekuwa ikiendelea na jitihada mbalimbali za kuhakikisha huduma ya maji inafikia walau asilimia 70 ifikapo mwishoni mwaka 2020.

‘Halmashauri ya Ruangwa inaendelea kutekeleza miradi mikubwa ya maji katika vijiji mbalimbali ikiwemo mradi wa maji wa Naunambe-Mpekenyera wananchi wanapata maji na wanafurahia huduma inayotolewa kwa mwaka 2019 pekee tulipata miradi minne ikiwemo mradi wa maji Kitandi na tayari tumeanza kufanya mawasiliano na Halmashauri ya Mtama kuhakikisha kuwa maji yanafikishwa katika vijiji jirani ikiwemo vijiji vya Nangumbu A na B’’ alisema Chezue.

Mwenyekiti wa Kamati ya Maji Kata ya Mandawa Rashid Mshamu anasema mradi wa maji mandawa unahuhudumia jumla ya vijiji 5 vya Nahanga, Chikundi, Mandawa Chini, Mchichili na Mtondo unaogharimu kiasi cha Tsh. Bilioni 1.7 zilizotolewa na Serikali, ambapo mradi huo unawanufaisha jumla ya watu 13,756.

Anaongeza kuwa mradi huo ulioasisiwa mwaka 1975 ulikuwa na miundombinu  chakavu na kusababisha kero kubwa kwa wananchi hususani wazee, wanawake na watoto ambapo walikuwa wanahangaika, ambapo Serikali iliamua kuufua mradi huo katika bajeti ya mwaka 2014/15.

Anasema kuwa kwa sasa mradi huo unaendelea vyema na huduma ya maji ni ya uhakika na wananchi wa vijiji hivyo wanalazimika kuchangia kiasi cha Tsh. 50 inayopelekwa katika mfuko wa maji wa kijiji hicho na kutumika kwa ajili ya ukarabati wa miundombinu ya mradi.

Miradi mingine ya maji inayotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Ruangwa ni pamoja na mradi wa maji Nanganga, mradi wa maji Likunja, mradi wa maji Namahema, mradi wa maji Chenjele, ambapo katika maeneo yote hali ya upatikanaji wa maji ni ya kurithisha.

Miradi mingine ni pamoja na ujenzi wa mradi wa maji katika kijiji cha Mibure, Namakuku na Namahema ambao tayari umekamilika na jumla ya watu 6,133 wananufaika, ambapo kiasi cha Tsh. Milioni 631,593,444.50 zimetumika.

Serikali imewekeza katika miradi ya maji mikubwa na midogo ili kufikisha huduma ya maji kwa wananchi, ambapo uwekezaji huo umeleta mabadiliko makubwa katika sekta mbalimbali nchini na maisha ya wananchi kwa ujumla.

Ili kuleta matokeo tarajiwa utekelezaji wa ujenzi wa miradi ya maji hapa nchini unahusisha ushirikiano baina ya serikali na sekta binafsi na pia wadau wa maendeleo kutokana na ukweli kuwa Serikali imeweka lengo la kufakisha huduma ya maji kwa asilimia 85 kwa upande wa wananchi.

MWISHO


Share:

VIDEO: Tigo yaongeza tahadhari kwa wateja wanaotembelea Banda lao SabaSaba

USALAMA KWANZA: Jinsi ambavyo #TigoSabasaba inachukua tahadhari mbalimbali uwapo ndani ya banda Ili kujikinga na maambukizi juu ya Covid-19 Tigo imechukua tahadhari mbalimbali ili uwepo katika banda la Tigo. Ni salama! Karibu ufurahie ofa na huduma msimu huu wa Tigo Sabasaba.


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger