Friday 3 July 2020

Picha : WANAFUNZI WALIOSOMA UHURU SEKONDARI WAMWAGA MISAADA KURUDISHA MAKALI YA SHULE YAO


Kiongozi Mkuu wa wanafunzi waliosoma Shule ya Sekondari Uhuru mwaka 2004, Masasi Marco akimkabidhi Katibu Mkuu wa Serikali ya Wanafunzi shuleni hapo, Ruth Joseph sehemu ya msaada kuboresha shule hiyo
Kiongozi Mkuu wa wanafunzi waliosoma Shule ya Sekondari Uhuru mwaka 2004, Masasi Marco akimkabidhi Katibu Mkuu wa Serikali ya Wanafunzi shuleni hapo, Ruth Joseph sehemu ya msaada kuboresha shule hiyo, wengine katika picha hiyo ni walimu wa shule hiyo.

Na Damian Masyenene - Shinyanga Press Club Blog
ILI kuhakikisha Shule ya Sekondari Uhuru iliyopo Manispaa ya Shinyanga mkoani humo inarejea katika makali yake kitaaluma, nidhamu na heshima iliyojengwa siku za nyuma, baadhi ya wadau mbalimbali waliowahi kusoma shuleni hapo wametoa msaada wa vifaa mbalimbali kukarabati baadhi ya majengo na fedha taslimu.

Umoja wa wanafunzi hao waliowahi kusoma shuleni hapo wamekabidhi fedha Sh 750,000/=, ndoo 18 za rangi kwa uongozi wa shule hiyo leo Julai 3, 2020 shuleni hapo, huku wakikutana na walimu wao wa zamani na kubadilishana mawazo na kuwapa mawaidha wanafunzi wanaoendelea na masomo katika shule hiyo.

Akikabidhi msaada huo, Kiongozi Mkuu wa wanafunzi waliosoma Uhuru Sekondari mwaka 2004, Misasi Marco alisema sehemu kubwa ya malengo yao ni kukusanyana na kuisaidia shule hiyo kutokana na wataalam mbalimbali waliozalishwa shuleni hapo mpaka sasa, kwani takwimu zinaonyesha idadi inafika wanafunzi 7,000 waliowahi kupita katika shule hiyo.

Marco amesema binafsi yuko tayari kutoa Sh 200,000 kwa mwanafunzi yeyote wa kidato cha nne katika shule hiyo atakayepata wastani wa kwanza (divion one) ya mwanzo kwenye mtihani wa taifa wa kuhitimu kidato cha nne mwaka huu.

"Japokuwa tumechelewa lakini tumeona kuna haja ya kuhamasisha wenzetu na kuweka mikakati na walimu namna ya kushiriki kuiboresha shule yetu," amesema.

Mmoja wa wanafunzi waliosoma shuleni hapo mwaka 2004, Estomine Henry ambaye kwa sasa ni Mratibu wa Klabu ya Waandishi wa Habari Mko wa Shinyanga (SPC), amewataka wanafunzi kudumisha nidhamu, kuzingatia masomo, kuweka ushindani chanya kwenye masomo ili kuipaisha shule yao kwani miaka ya nyuma shule hiyo ilisifika kwa ufaulu mzuri, heshima na bidii katika masomo.

Mwakilishi wa wanafunzi waliomaliza Uhuru Sekondari mwaka 1998, Nurah Kamuntu amesema tayari wameshashiriki katika kuiboresha shule hiyo kwa kupaka rangi madarasa, maabara na kufanya maboresho kwenye vyoo.

"Tuliwaza sana tutaifanyia nini shule yetu, ndipo tukaja na huu mpango wa kupaka rangi baadhi ya madarasa hapa shuleni na maabara, lakini pia tumeboresha vyoo na baadhi ya madarsa, hii yote ni kurudisha shukrani kwa jamii.....Shukrani hii ndogo tuliyoileta kwenu ni mwendelezo, je wewe (mwanafunzi) utarudisha shukrani ipi kwa shule yako," amesema.

Mkuu wa Shule ya Sekondari Uhuru, Victoria Nakiliaumi amesema wadau hao wanaboresha mazingira ya shule hiyo ili kuinua taaluma, ambapo amewataka wanafunzi wake kuhakikisha wanalikamilisha lengo hilo.

"Hawa wenzenu walikuwa na nidhamu sana na bidii katika masomo, lazima na nyinyi muendeleze na mpite katika mkondo huo," amesema.

Mmoja wa walimu wakongwe na maarufu shuleni hapo, Wilfred Masanja ambaye ni mtunzi wa wimbo wa shule hiyo, baada ya kukutana na wanafunzi wake wa zamani na kupewa fursa ya kuzungumza, amewataka wanafunzi kudumisha nidhamu, kujiunga na klabu mbalimbali zinazoanzishwa shuleni hapo mfano Klabu ya Mali Hai iliyokuwa ikitunza mazingira ili kuisaidia shule, pia akawataka wadau wengine kuendelea kuisaidia shule hiyo.

"Tuwe na makambi ya kujisomea kama ilivyokuwa utamaduni wa shule yetu, nawaomba sana msome kilichokuleta hapa ni kusoma mna walimu wazuri na wanafundisha kwa bidii, msaada ulioletwa tuutumie vizuri kazaneni na muda uliotolewa uwasaidie katika maisha yenu.

"Haya yanayozungumzwa ni ya kukufanya ujitambue na yachukueni kwa uchungu mkubwa ili iweze kuwasaidia katika safari yenu ya kimasomo," amesema.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Mtaa wa Miti Mirefu ilipo shule hiyo, Nassoro Warioba aliuomba uongozi wa shule kuendeleza mahusiano mazuri na wadau, huku akiwaomba wanafunzi hao wa zamani kuona uwezekano wa kulikamilisha jengo la maabara ambalo limejengwa na Serikali na sasa linahitaji kumaliziwa.

Katibu Mkuu wa Serikali ya Wanafunzi Shule ya Sekondari Uhuru, Ruth Joseph amewashukuru wote wanaoendelea kuisaidia shule yao, huku akisistiza kuwa kwa niaba ya wanafunzi wake wamepokea yale yote yaliyoelekezwa kwao na yatafanyiwa kazi ili kuhakikisha kwamba heshima ya shule hiyo inaendelea kudumishwa.
Kiongozi Mkuu wa wanafunzi waliosoma Shule ya Sekondari Uhuru mwaka 2004, Masasi Marco akizungumza shuleni hapo
Mratibu wa SPC, Estomine Henry akizungumza na wanafunzi.
Mkuu wa Shule ya Sekondari Uhuru, Victoria Nakiliaumi
Mwalimu Masanja akizungumza
Mwenyekiti wa Mtaa wa Miti Mirefu, Nassoro Warioba
Katibu Mkuu wa Serikali ya Wanafunzi Sekondari ya Uhuru, Ruth Joseph
Wanafunzi wakimshangilia mwalimu wa zamani wa shule hiyo, Wilfred Masanja
Katibu wa Serikali ya Wanafunzi Shule ya Sekondari Uhuru, Ruth Joseph akipokea msaada wa ndoo za rangi 
Mmoja wa waliosoma shule ya sekondari Uhuru mwaka 2004, Estomine Henry akitoa ujumbe kwa wanafunzi
Mkuu wa shule ya sekondari Uhuru, Victoria Nakiliaumi na wanafunzi wake wakipokea sehemu ya msaada huo
Mmoja wa wanafunzi waliosoma shuleni hapo mwaka 1998, Nurah Kamuntu akizungumza na wanafunzi.
Kiongozi Mkuu wa wanafunzi waliomaliza Uhuru Sekondari mwaka 2004, Misasi Marco akimkabidhi Sh 750,000 mkuu wa shule hiyo, Victoria Nakiliaumi
Mkuu wa Shule ya Sekondari Uhuru, Victoria Nakiliaumi akionyesha fedha alizopokea kutoka kwa wadau kuboresha mazingira ya shule hiyo
Baadhi ya vitu vilivyotolewa kama msaada kuboresha mazingira ya shule ya Sekondari Uhuru
Wanafunzi wakifuatilia tukio la kukabidhi msaada wa vifaa mbalimbali kuboresha shule yao
Mwalimu wa zamani wa shule hiyo, Wilfred Masanja alifika kujumuika na wanafunzi aliowafundisha
Mmoja wa wanafunzi waliohitimu shuleni hapo mwaka 1998, Nurah Kamuntu (kushoto) akiteta jambo aliyekuwa mwalimu wa shule hiyo
Mwenyekiti wa Mtaa wa Miti Mirefu, Nassoro Warioba naye alipata fursa ya kutoa shukrani za serikali ya mtaa.
Walimu wa Shule ya Sekondari Uhuru wakiwa katika picha ya pamoja na wadau waliojitokeza kusaidia shule hiyo
Wanafunzi wa Uhuru Sekondari wakisikiliza ujumbe
Wanafunzi wakifuatilia kwa ukaribu tukio la kukabidhi msaada wa vifaa mbalimbali
Wanafunzi wa shule hiyo
Wanafunzi wakifuatilia kwa umakini mkubwa ujumbe unaotolewa kwao
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Uhuru
Baadhi ya wanafunzi waliosoma shule hapo miaka ya nyuma wakiwa kwenye picha ya pamoja na walimu waliowafundisha
Share:

Stock, Forex, Crypto – Sales Agent

Job Summary This position has responsibility for driving foreign exchange sales revenue through high quality client servicing, strong internal partnerships, prospecting and strong sales process execution. Minimum Qualification: Bachelor Experience Level: Mid level Experience Length: 2 years Job Description TOPFX is an EU Investment Firm, specializing in Prime Brokerage Services that has appointed Top Earners Market as its exclusive […]

The post Stock, Forex, Crypto – Sales Agent appeared first on Udahiliportal.com.

Share:

TANESCO YATOA ELIMU JUU YA MATUMIZI BORA YA UMEME KWA WACHIMBAJI WA MGODI WA DHAHABU WA NHOLI WILAYANI BAHI


Mhandisi Mtafiti wa TANESCO, Aurea Bigirwamungu akitoa Elimu kwa Wachimbaji wadogowadogo wa Dhahabu katika Mgodi wa Nholi uliyopo wilayani Bahi juu ya matumizi bora ya Umeme
Mhandisi Mtafiti wa TANESCO, Aurea Bigirwamungu akisisitiza jamboa wakati wa kutoa Elimu kwa Wachimbaji wadogowadogo wa Dhahabu katika Mgodi wa Nholi uliyopo wilayani Bahi juu ya matumizi bora ya Umeme
Afisa Masoko TANESCO,Adelina Lyakurwa akizungumza na wachimbaji wadogowadogo wa Dhahabu katika Mgodi wa Nholi(hawapo pichani) uliyopo wilayani Bahi wakati wa kutoa elimu juu ya matumizi bora ya Umeme

Afisa Uhusiano Huduma kwa Wateja TANESCO Dodoma, Mariam Juma akieleza faida ya nishati ya umeme kwa wachimbaji wadogowadogo wa Dhahabu katika Mgodi wa Nholi (hawapo pichani) wakati wa kutoa elimu kwa juu ya matumizi bora ya umeme leo Wilayani Bahi
Baadhi ya Wachimbaji wadogowadogo wa Dhahabu katika Mgodi wa Nholi waliyojitokeza kupatiwa elimu juu ya matumizi bora ya Umeme kutoka kwa watendaji wa TANESCO leo Wilayani Bahi.
Afisa Masoko TANESCO Adelina Lyakurwa akiwa na Afisa Uhusiano Huduma kwa Wateja TANESCO Dodoma Mariam Juma wakionyesha kifaa cha umeme(umeter) kwa wachimbaji wadogowadogo wa Dhahabu katika Mgodi wa Nholi wilayani Bahi.
Katibu wa Mgodi wa Dhahabu wa Nholi Sebastian Aloyce (wakwanza kushoto) akizungumza kwa niaba ya wachimbaji wadogowadogo wa dhahabu katika mgodi huo na pembeni yake ni Meneja Mgodi Kulwa Limbu akimsikiliza kwa makini.
Watendaji wa TANESCO wakiwa katika picha ya pamoja na Wachimbaji wadogowadogo wa dhahabu katika Mgodi wa Nholi uliyopo wilayani Bahi baada ya kupatiwa elimu ya matumizi bora ya nishati ya Umeme.
Mhandisi Mtafiti TANESCO Aurea Bigirwamungu akikagua baadhi ya mitambo ya wachimbaji wadogowadogo wa Dhahabu wa Mgodi wa Nholi wilayani Bahi .
Wachimbaji wadogowadogo wa Mgodi wa Nholi wilayani Bahi wakiwa katika shughuli zao za uzalishaji.
Mwonekano sehemu moja wapo ya eneo la Mgodi wa Dhahabu wa Nholi wilayani Bahi
……………………………………………………….
. Na. Alex Sonna, Bahi Wachimbaji wadogowadogo wa dhahabu katika mgodi wa Nholi wilayani Bahi kupatiwa nishati ya umeme ndani ya miezi sita ili kuongeza uzalishaji katika mgodi huo. Kauli hiyo imetolewa leo na Mhandisi Mtafiti Aurea Bigirwamungu wakati wa kutoa elimu kwa wachimbaji wadogowadogo na wakazi wa kata hiyo kwa ajili ya matumizi bora ya umeme. 

 Mhandisi Bigirwamungu amesema kuwa mradi wa kuwafikishia nishati ya umeme wakazi hao utatekelezwa ndani ya miez sita ili kurahisisha shughuli za wajimbaji hao hasa katika uchenjuaji wa dhahabu na shughuli nyingine katika mgodi huo.

  Aidha Mhandisi Bigirwamungu amesema kuwa wachimbaji hao shughuli zao nyingi zinahitaji nishati ya umeme ili kuongeza uzalishaji katika ujimbaji wa dhahabu ambapo nishati hiyo itaweza kuinua kipato cha mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla. 

 “Ninaimani kubwa ndani ya miezi sita mradi huu utatekelezwa na kukamilika hivyo wakazi wa hapa watanufahika na kuongeza chachu katika uzalishaji na maendeleo yao ” ameweka wazi Mhandisi Bigirwamungu. 

 Lakini pia Mhandisi Bigirwamungu amesisitiza kuwa baada ya elimu hiyo wachimbaji hao wahakikishe wanatumia vifaa vilivyo bora hasa ambavyo havitumii umeme mwingi , lakin pia kuwa na matumizi mazuri ya umeme kila baada ya matumizi kuzima umeme huo.  

Naye Afisa Masoko Adelina Lyakurwa ametoa wito kwa wakazi hao kuchangamkia fursa ya kupata nishati ya umeme ili kuongeza uzalishaji katika shughuli zao za uchimbaji. 

 “Hivyo basi taratibu za kufanikiwa kupatiwa umeme ni kuhakikisha unapata fomu ya kuomba kupatiwa umeme, ukisha jaza fomu hiyo isainiwe na mkandarasi alafu irudishwe TANESCO na fanya kutandaza nyaya katika nyumba yako muda ukifika basi wewe ni kufungiwa umeme” amebainisha Lyakurwa.  

Aidha Lyakurwa ameongeza kwa Nishati hii ya umeme kwa wakazi hao wataunganishiwa nishati ya umeme kwa shilingi 27,000 tu. 

Kwa upande wake Afisa Uhusiano Huduma kwa Wateja TANESCO Dodoma Mariam Juma ameweka wazi kuwa lengo la kuwasogezea nishati ya umeme wakazi hao ni kuhakikisha wanatumia nishati hiyo kuchenjua dhahabu na shunguli nyinginezo katika mgodi huo ili kuongeza uzalishaji wa dhahabu katika mgodi huo na kuleta maendeleo kwa ujumla.  

Pia Mariamu amewashukuru wakazi wa kata hiyo kwa mwitiko waliyowapa na kusema kuwa elimu waliyopatiwa itakwa na manufaa kwao na kuleta tija kwao.

Kwa niaba ya wachimbaji na wananchi wa kata hiyo Meneja mgodi Kulwa Limbu ametoa changamoto ya wachimbaji hao kuwa wamekuwa wakitumia dizeli katika shughuli zao za uzalishaji wa dhahabu ambayo imekuwa ikuuzwa kwa bei ghali na kusababisha shughuli za mgodini kutotekelezwa ipasavyo. “Sisi tuko tayari kutumia nishati ya umeme hivyo nitoe wito kwenu watendaji wa TANESCO kuwa mradi huo uweze kukamilika ndani ya muda mliosema ili tuweze kunufaika na mradi huo kwa kuongeza uzalishaji ” ametoa rai

Share:

ZOEZI LA UTAMBUZI KAYA MASKINI MANISPAA YA SHINYANGA MPANGO WA TASAF KIPINDI CHA PILI LATANGAZWA RASMI...MAAFISA WATENDAJI WAKUTANA

Mratibu wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini - TASAF Manispaa ya Shinyanga Octavina Kiwone.

Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Mratibu wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini - TASAF Manispaa ya Shinyanga Octavina Kiwone amewataka Maafisa Watendaji wa Mitaa,vijiji na kata katika Manispaa ya Shinyanga kusimamia kwa uadilifu na umakini zoezi la utambuzi wa kaya maskini ambazo zitaingia kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini katika kipindi cha pili ulionza mwezi Juni,2020. 



Kiwone ametoa rai hiyo leo Ijumaa Julai 3,2020 wakati wa kikao kazi kilichokutanisha pamoja Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga kwa ajili ya kutoa maelekezo namna ya kutambua kaya maskini zitakazoingia kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini katika kipindi cha pili. 

Kiwone alisema utekelezaji wa Mpango wa Kunusuru kaya Maskini katika kipindi cha pili utakaodumu kwa kipindi cha miaka mitatu umeanza mwezi Juni 2020 ambapo zoezi la utambuzi katika Manispaa ya Shinyanga litafanyika kwa kipindi cha wiki mbili (kuanzia Julai 3 hadi Julai 20,2020). 

Alieleza kuwa zoezi la kutambua kaya maskini linalenga kaya maskini zilizosahaulika kwenye kipindi kilichopita lakini pia litahusisha mitaa na vijiji vyote katika Manispaa ya Shinyanga ambavyo havikuwepo kwenye mpango ambapo baada ya utambuzi huo wa awali ndipo serikali itajua inaenda kuhudumia walengwa wangapi na kutoa fedha kwa ajili ya kaya hizo. 

“Mpango huu wa kunusuru kaya maskini kipindi cha pili utagusa kata zote na Manispaa ya Shinyanga. Tunawasihi sana viongozi kwenye maeneo husika wasimamie zoezi hili kwa umakini na uadilifu mkubwa ili tupate kaya ambazo zina vigezo na zinastahili kuwepo kwenye mpango”,alisema Kiwone. 

“Hatutegemei kwenye eneo letu la Manispaa ya Shinyanga kupata kaya ambazo hazina sifa kuingia kwenye mpango. Kila mmoja atawajibika kwa nafasi yake kwa kufuata sheria, taratibu na kanuni zilizowekwa lakini pia watu wasifanye kwa matashi yao",alisema Kiwone. 

Alieleza kuwa ni haki ya kaya maskini kuhudumiwa siyo kwamba anapewa upendeleo ‘Favour’ au kwamba anapewa sadaka flani akibainisha kuwa hiyo ni fedha ya serikali inatakiwa iende kwa mtu stahiki na anayestahili kupata. 

Hata hivyo alisema baada ya utambuzi huo wa awali kufanyika kuna vyombo vingine vyenye dhamana vitarudi kwenye orodha ya kaya maskini zinakazopatikana ili kuhakiki kama waliopitishwa ni kweli ni kaya maskini zina vigezo na zinastahili kuingia katika mpango wa kunusuru kaya maskini. 

Alivitaja baadhi ya vigezo vinavyotakiwa katika mpango huo kuwa kaya zenye kipato duni zinazoshindwa kupata milo mitatu kwa siku,kaya yenye makazi duni, kaya yenye watoto wengi wanashindwa kuihudumia, kaya ambayo watoto wanashindwa kwenda shule kwa sababu hawana mahitaji ya shule au kwenda kliniki kwa sababu mbalimbali 

“Ni muda mzuri kwa wananchi pia kufahamu, wanapoitwa kwenye mikutano ya hadhara kwenye maeneo yao wafike ili wasikose haki yao ya msingi. 

Na kwa wananchi ‘makundi maalum’ ambao hawawezi kufika kwenye mikutano mfano watu wenye ulemavu,wazee maskini jamii iwataje. TASAF haiandikiwi mezani kupata orodha ya walengwa,orodha inapatikana kwenye mikutano ya hadhara,wakutambue kwamba wewe upo kwenye kaya maskini na mkutano uridhie kuwa kweli wewe ni kaya maskini”,alifafanua Kiwone.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Mratibu wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini - TASAF Manispaa ya Shinyanga Octavina Kiwone akizungumza katika kikao kazi kilichokutanisha pamoja Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga kwa ajili ya kutoa maelekezo namna ya kutambua kaya maskini zitakazoingia kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini katika kipindi cha pili kilichoanza mwezi Juni mwaka huu 2020 katika ukumbi wa Lewis Kalinjuna Manispaa ya Shinyanga leo Ijumaa Julai 3,2020 . Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mratibu wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini - TASAF Manispaa ya Shinyanga Octavina Kiwone akiwasisitiza Maafisa Watendaji wa Mitaa,vijiji na kata katika Manispaa ya Shinyanga kusimamia kwa uadilifu na umakini zoezi la utambuzi wa kaya maskini ambazo zitaingia kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini katika kipindi cha pili ulionza mwezi Juni,2020. 
Mratibu wa Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini - TASAF Manispaa ya Shinyanga Octavina Kiwone akiwasihi Maafisa Watendaji wa Mitaa,vijiji na kata katika Manispaa ya Shinyanga kusimamia kwa uadilifu na umakini zoezi la utambuzi wa kaya maskini ambazo zitaingia kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini katika kipindi cha pili ulionza mwezi Juni,2020. 
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa katika kikao cha kuelezwa namna ya kutambua kaya maskini zitakazoingia kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini katika kipindi cha pili. 
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa katika kikao cha kuelezwa namna ya kutambua kaya maskini zitakazoingia kwenye mpango wa kunusuru kaya maskini katika kipindi cha pili. 
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
Maafisa Watendaji wa kata,vijiji na mitaa katika Manispaa ya Shinyanga wakiwa ukumbini.
 Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger