Sunday 31 May 2020

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili May 31















Share:

Saturday 30 May 2020

Picha : RAIS MAGUFULI NA MARAIS WASTAAFU WAWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA OFISI ZA IKULU YA CHAMWINO DODOMA.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ameshika Chepe ili kuweka zege na Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benja min Mkapa kuashiria uwekaji wa jiwe la Msingi Ujenzi Ofisi za Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 30 Mei 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa ameshika Chepe ili kuweka zege na Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benja min Mkapa kuashiria uwekaji wa jiwe la Msingi Ujenzi Ofisi za Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 30 Mei 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamin Mkapa, Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete pamoja na Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere kuashiria uzinduzi wa Mitambo na magari yatakayotumika katika ujenzi wa Ujenzi Ofisi za Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 30 Mei 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamin Mkapa, Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete pamoja na Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere wakivuta utepe kuashiria uwekaji wa Jiwe la Msingi Ujenzi Ofisi za Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 30 Mei 2020.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na vijana wa JKT wanaojenga Ikulu ya Chamwino.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli pamoja Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi, Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamin Mkapa, Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete pamoja na Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere wakisikiliza maelezo kuhusu ujenzi wa Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere wakielekea kwenye uwekaji wa jiwe la msingi ujenzi wa Ofisi za Ikulu
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia bendi ya ya JKT mara baada ya hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi Ujenzi Ofisi za Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 30 Mei 2020.
Waandishi mbalimbali wa Habari wakiwa wameshika chepe ili kuweka zege kama ishara ya kuweka kumbukumbu kwenye jiwe la msingi Ujenzi Ofisi za Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma leo tarehe 30 Mei 2020.Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza jambo la Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete mara baada ya kuweka jiwe la msingi Ujenzi wa Ikulu ya Chamwino.PICHA NA IKULU



Share:

Riwaya Kali ya Kusisimua....SIN- Sehemu Ya Saba (07)

Mwandishi- EDDAZARIA G.MSULWA
Age-18+
Simu-0657072588(whatsapp) au 0768516188


ILIPOISHIA   
“Yaani sijui kwa nini uliaolewa na yule mzee”
“Ahaa ni maisha tu. Tumefika baba yangu”
Mrs Sanga alizungumza huku akisimamisha gari lake nyuma ya gari la Tomas alilo liacha kwenye maegesho ya ofisi za rafiki yake.
“Haya shuka, acha mimi niwahi nyumbani”
“Sawa mke wangu”
Tomas taratibu akafungua mlango wa gari la mrs Sanga na kushuka huku akiwa na mfuko wenye pesa. Mpelelezi mmoja akaanza kazi ya kumpiga picha Tomas bila ya yeye kufahamu. Huku mpelelezi mwengine akitoa ripoti kwa mkuu wao kwamba wamempata jambazi aliye mteka nabii Sanga.


ENDELEA
“Hakikisheni kwamba hamumpotezi mtuhumiwa”
“Sawa mkuu”
“Pia kuweni makini kumfatilia na ikiwezekana muweze kumkamata hata kabla hajafanya jambo lolote”
“Sawa sasa mkuu”
Tomas pasipo kujua chochote akaingia kwenye gari lake aina ya Toyota Prado Tx. Tomas akaanza kuondoka eneo hilo huku akiwa na furaha ya kujivunia milioni ishirini za bure, kwani makubaliano yake na watekaji ni kuwalipa milioni arobaini.
                                ***
“Mage Mkinga una ndugu?”
Sheby aliuliza huku akipunguza mwendo, kwani mbele yao kuna tuta refu kidogo.
“Hapana”
“Au unakwenda kwa shemeji?”
“Hakuna kitu kama hicho Sheby”
“Ila nini tena jamani?”
“Kuna mambo yangu nakwenda kuyafanya”
“Mmmmm….ila unaweza kunipa nafasi ya kuzungumza”
“Kuzungumza nini?”
“Ahaa….katika siku zote za maisha yangu, nimetokea kukupenda Mage, ila nilikuwa nina tafuta muda muafaka wa kuweza kukueleza hilo”
“Ila Sheby wewe si unaishi na mwanamke?”
“Ndio nina ishi naye tu, ila ukweli ni kwamba sina mapenzi naye”
“Acha uongo Sheby na yule dada alivyo mzuri, inakuwaje huna mapenzi naye?”
“Unaweza kuishi na mtu ila usimpende. Hivyo ni sawa na mimi, nina ishi naye tu ila ukweli ni kwamba simpendi”
“Inakuwaje una ishi na mwamke usiye mpenda?”
“Ana mimba yangu na hicho ndio kinacho mfanya kuwepo kwangu. Ila ingekuwa sio mimba wala nisinge kuwa naye”
“Sheby muogope Mungu.  Mpende mtoto wa watu usije ukamuumiza kwa chochote”
“Ila simpendi?”
“Sawa humpendi na mbaya ana kwenda kuwa mama wa mwanao. Hivyo mpende na kumuheshimu bwana”
“Haya bwana. Ila hata siku moja sijawahi kumuona shemeji yetu. Vipi?”
“Usijali utamuona”
“Ni nani?”
“Ahhaa….wewe si unataka kumuona. Utamuona siku itakapo fika”
“Haya bwana”
Safari ikazidi kusonga huku wakizungumza mambo mengi sana kuhusiana na maisha. Majira ya saa moja kasoro wakafika Mkinga. Magreth akatoa simu  yake na kupiga namba ya watekaji.
“Nimefika Mkinga”
“Upo na nani?”
“Dereva taksi”
“Muache hapo stendi na panda pikipiki na umpatie simu dereva wa pikipiki nitampatia maelekezo ya wapi anapaswa kukuleta”
“Sawa”
Simu ikakatwa.
“Nani huyo”
“Ni jamaa yangu. Ameniambia nikuache hapa kwa maana huko ninapo kwenda gari haiwezi kuingia. Nitapanda pikipiki, kisha nitapelekewa huko ninapo pahitaji”
“Sawa, kwa hiyo nikusubirie hapa kwa muda gani?”
“Hadi nitakapo rudi. Nipatie namba yako ya simu”
Sheby akamtajia Magreth namba yake ya simu. Magreth akashuka kwenye taksi hiyo. Waendesha pikipiki kama kawaida yao ya kumkimbilia mteja, ndivyo jinsi walivyo fanya kwa Magreth. Magreth akamchagua dereva mmoja kati ya watano walio mfata. Akapiga simu kwa watekeji.
“Mpatie dereva pikipiki simu”
Magreth akampatia dereva pikipiki simu. Baada ya kuelekezwa wapi ampeleke Magreth simu hiyo ikakatwa.
“Una pafahamu?”
“Ndio”
“Itakuwa kiasi gani?”
“Elfu kumi”
“Ni mbali sana?”
“Sio sana”
“Haya”
Magreth akapanda pikipiki na kuondoka eneo hilo la stendi. Ndani ya dakika arobaini na tano, wakafanikiwa kufika karibu kabisa na msitu huo. Magreth akashuka na kumlipa na dereva pikipiki akaondoka. Simu ya Magreth ikaita na kuipokea. Tembea hatua kumi mbele kisha kunja kushoto utaona gari nyeusi”
Magreth akaanza kutembea huku simu yake ikiwa sikioni mwake. Baada ya hatua hizo kumi akakunja kushoto na kuona gari nyeusi ikiwa imefichwa vichakani. Japo kigiza kimeanza kuingia ila hakuweza kuogopo kwa lolote kwani tayari amesha dhamiria kumuokoa nabii Sanga. Wanaume wawili walio zifunika sura zao wakatoka ndani ya gari hilo huku wakiwa na bastola mikononi mwao.
“Vua begi”   
Magreth akavua beigi hilo mgongoni na kulishika mkono wa kulia. Watekeji hao wakaanza kumpapasa mwili wake wote. Walipo hakikisha hana silaha wala kinasa sauti wakaichukua simu yake kisha wakamfunga kitambaa cheusi usoni mwake. Wakamuingiza ndani ya gari, ili kumchanganya Magreth asitambue ni wapi anapo elekea, wakaanza safari ya kurudi mjini. Walipo karibia na mjini, wakageuza gari na kuianza safari ya kurudi msituni huku gari hilo likiendeshwa kwa kasi sana. Wakafika msituni, wakamshusha Magreth kwenye gari, wakaongozana naye hadi kwenye chumba walipo muweka nabii Sanga.
                                ***

Wapelelezi hawa wakazidi kulifaafilia gari la Tomas kwa umakini sana. Tomas akatoa simu yake mfukoni, akatafuta namba ya Rama D, ambaye ndio kiongozi mkuu wa kikosi cha watekaji hao.
“Mzee baba”
“Niambie mwana”
“Vipi huyo boya ana endeleaje?”
“Yupo fresh, ana mbwela mbewle tu hapa”
“Chok** huyo. Sasa ni hivi mzee baba. Ninawaletea mpunga wenu muda huu”
“Muda huu?”
“Ndio”
“Fresh mwana, ni wewe ila kuwa makini”
“Usijali mwana nipo makini sana. Ila hakikisheni kwamba hamumpigi kwa maana bibie ana mbwela kishenzi”
“Ahahaa”
“Yaa nyinyi hakikisheni kwamba ana kuwa salama huyo mzee”
“Poa poa mwana, hilo halina tabu, kikubwa mpunga uwe mezani”
”Fresh mida”
“Poa”
Kitendo cha Tomas kukata simu, akastukia gari ndogo ikimpita kwa kasi na kupunguza mwendo hadi ikamlazimu na yeye kupunguza mwendo.
“Huyu msen** nini, anapunguzaje mwendo?”
Tomas alizungumza kwa hasira huku akipiga honi. Dereva wa gari hilo akaligeuza gari lake na kulifanya liifunge barabara nzima. Tomas akasimamisha gari lake na kushuka kwa hasira sana huku akimfaata dereva wa gari hilo.
“Wewe msen** umelewa nini?”
Tomas aliporomosha matusi. Wapelelezi hao wakashuka kwenye gari lao huku wakichomoa bastola zao. Kitendo hicho kikaanza kumtetemesha Tomas.
“Ka…kaaakkk…..ma…..”
Mpelelezi mmoja hakumpa nafasi Tomas ya kumalizia sentensi yake. Akampiga mtama mmoja matata na kumfanya arushwe juu kimo cha mbuzi na kuanguka mzima zima. Mpelelezi huyo akamgeuza Tomas na kumlaza kifudifudi. Akamuwekea kigoti cha shingoni huku akiichomeka bastola yake kiunoni mwake na kutoa pingu mfukoni mwake. Akaifunga mikono yake hiyo na kumnyanyua. Kitendo hicho kikamfanya Tomas atambue kwamba watu hao ni polisi na si majambazi kama alivyo hisi kwa mara ya kwanza.
“Munanikamata nini? Kosa langu ni nini?”
“Ushibitisho wa pesa upo hapa”
Mpelelezi ambaye alikuwa akikagua gari la Tomas alizungumza huku akitoa mfuko huo wenye milioni arobaini.
“Poa piga picha ushahidi kisha endesha gari lake na mimi nina muingiza huku. Una haki ya kukaa kimya, kila kitu utakwenda kukijua kituoni”
Mpelelezi huyo alizungumza huku akimuingiza Tomas, ndani ya buti ya Alteza na kuifunga. Akaingia ndani ya gari hilo, kisha wakageuza na kuanza safari ya kuelekea central Polisi.
                                ***
    Magreth akafunguliwa kitambaa alicho fungwa usoni mwake. Macho yake yakakutana na nabii Sanga, aliye kaa kwenye kiti huku pembeni yake wakiwa wamesimama watu wa wiwili wenye mitutu ya bunduki aina ya AK47. Akataka kumkimbilia na kumkumbatia, ila mtekaji mmoja akamzuia.
“Tunahitaji kuziona pesa”
Magreth akaliweka chini begi hilo na kulifungua. Vitita vya dola za Kimarekani, vikawafanya watekaji hao wawili walio kuwa karibu na begi hilo kutazamana. Kwa isharaha mkuu wao akamuagiza mmoja wao kuzimwaga pesa hizo juu ya meza. Vibunda hivyo vikamwagwa juu ya meza  na kuifanya mioyo ya watekaji hao kujawa na furaha.
“Kalete mashine”
“Sawa”
Mtekaji mmoja akatoka, baada ya dakika mbili akarudi akiwa na mashine ya kuheshabia pesa. Wakaanza kazi ya kuhesabu vibunda hivyo vya pesa. Ilipo timia dola elfu sitini, mkuu wao akampa mkono wa kumshukuru nabii Sanga.
“Unaweza kuzungumza chochote mzee”
“Ni nani ambaye amewapa oda ya kuniteka?”
“Ni kutoka kwa kijana wako Tomas ambaye ni dalali wako”
“Tomas?”
“Ndio na hapa ninavyo zungumza yupo njiani ana ileta milioni ishirini kwa ajili ya kazi tuliyo mfanyia.”
Nabii Sanga akakaa kimya huku akiisikilizia hasira jinsi inavyo utafuna moyo wake. Akanyanyuka kwenye kiti hicho huku macho yakitawaliwa na uwekundu. Muda wote Magreth yupo kimya akishuhudia jinsi nabii Sanga alivyo kasirishwa kwa kitendo hicho kibaya alicho fanyiwa.
“Ana kuja hapa eheee?”
“Ndio mzee”
“Sasa hiyo ni milioni mia na ishirini. Hizi ishirini anazo zileta chukueni na hiyo ishirini ya ziada aliyo zidi, hakikisheni muna mchinja mume nielewa?”
Kauli ya nabii Sanga ika mstua sana Magreth, ila hakuweza kufungua kinywa chake kwa maana hajajua ni makubaliano gani nabii Sanga ameingia na watekaji hao.
“Sawa mkuu”
“Tena nina hitaji mumkate kate kiungo kimoja baada ya kingingine na mumuambie kwamba mimi ndio nimetoa kazi hiyo”
“Sawa mzee”
“Na kuanzia hivi sasa, nitakuwa nina wapa kazi zangu. Nahitaji muzifanye kwa uhakika na sitaki kabisa mulegelege, kama muna taka pesa zaidi ya hii basi mushikamane na mimi sawa”
“Sawa, ila tunahitaji kukudhibitisha kwamba huto tusaliti. Wote hapa tumeingia kiapo cha damu hivyo na wewe tuna hitaji uingie kiapo cha damu”
“Hilo halina shida. Niambieni nifanye nini?”
Mmoja wao akatoa kisu. Wakamtazama Magreth, wakampa ishara ya kutoka ndani humo na Magreth akatii. Wakaufunga mlango wa chumba hicho. Wakavua vinyago vilivyo ficha sura zao.
“Mimi ninaitwa Rama D. Sisi sote ni watoto wa familia moja na mimi ndio kaka yao. Huyu anaitwa Selemani D. Huyu anaitwa Rashid D na huyu ni mdogo wetu wa mwisho ana itwa Abdalah D. Baba yetu alikuwa ni komandoo wa jeshi la nchi hii. Alitupa mafunzo toka tukiwa wadogo na tumekuwa ni professional wa mbinu za kijeshi. Tuna uwezo wa kufanya kila aina ya tukio hivyo karibu katika familia”
Rama D, alizungumza huku akimtazama nabii Sanga. Nabii Sanga alipo hakikisha kwamba amewakremisha sura zao vijana hao. Akajikata sehemu ndogo ya kiganja chake na akapewa kikopo cha kuiweka damu hiyo inayo mchuruzika kiganjani. Rama D na wadogo zake wakajikata na wao na damu zao wakaziweka katika kikopo hicho, ikiwa ni ishara ya muungano wa damu.
“Nimekaribia. Nina juana na watu wengi sana duniani. Nitahakikisha nina wawezesha kisilaha, kifedha na kila aina ya mbinu mpya nitawapatia kwa maana, hadi leo hii nimekuwa tajiri si kwamba ni Mungu amenibariki, ila nilitumia kila aina ya njia kuwa tajiri. Hivyo natambua shida kama hizi”
“Karibu sana.”
Baada ya nabii Sanga kukaribishwa katika familia hiyo. Rama D na wadogo zake, wakavaa vinyango vyao. Wakafungua mlango na kumuita Magreth ndani.
“Simu yako”
Selemani D, alizungumza huku akimkabidhi Magreth simu yake.
“Huyu mwanamke nina imani wote mume muona”
“Ndio”
“Hakikisheni kwamba hakuna anaye msogelea na kila anaye jaribu kumsogelea basi mnajua nini mna paswa kufanya”
“Tumekuelewa.”
Kutokana na Magreth sio mwana familia wao. Wakamfunga kitambaa machoni mwake, kisha wakainza safari ya kuelekea Mkinga mjini huku wakiwa pamoja na nabii Sanga ndani ya gari lao.
                                ***
    Tomas akatolewa ndani ya buti ya gari hilo. Kwa mwendo wa haraka, akaingizwa kwenye kituo hicho kikubwa cha polisi. Umaarufu wake wa udalali katika jiji hilo la Dar es Saalam, likawafanya baadhi ya askari kushangaa juu ya uwepo wake hapo kituoni. Ila kutokana  ameletwa na pingu mikononi mwao hapakuwa na hata mmoja aliye wazuia wapelelezi hao kumpeleka katika chumba cha mateso. Thomas akavuliwa nguo zake zote, akafunguliwa pingu za mikononi mwake na kufungwa minyororo mizito. Akaning’inizwa hewani huku mikono yake ikiwa imechanuliwa mithili ya Yesu alivyo sulubiwa msalabani. Wapelelezi hao wakamwagia maji mwilini mwake, kisha mmoja wao ahachukua nyaya mbili za umeme, zenye hasi na chanya. Akazigusanisha na zikaanza kutoa cheche cheche, zilizo mfanya Thomas kujawa na mshangao hata kabla ya kupachikwa na nyaya hizo mwilini.
“Ukijibu kwa usahihi basi adhabu hii huto ipata. Ila ukijibu kwa jeuri basi adhabu hii utakumbana nayo.”
Kauli ya mpelelezi ikamfanya Tomas macho kumtoka huku akiwa haelewi ni kosa gani lililo mfanya kukumbana na shurba zote hizo.
“YUPO WAPI NABII SANGA”
Mapigo ya moyo ya Tomas yakaanza kumdunda kwa kasi sana kwani hakutarajia kwamba, mpango wa siri alio upanga yeye na mrs Sanga utajulikana kirahisi namna hiyo.


 ITAENDELEA
Haya sasa nabii SANGA yupo huru na ametambua kwamba Tomas ndio muhusika wa kutekwa kake. Tomas yupo mikononi mwa polisi. Je akibanwa atafichua siri nzito ambayo hata polisi wakielezwa hawato iamini?. Nini kitatokea? Endelea kufaatilia kisa hiki cha kusisimua, usikose sehemu ya 08

 


Share:

Video Mpya : PILI NZALIA - MACHIMBO


Hii hapa ngoma mpya ya Pili Nzalia inaitwa Machimbo...
itazame hapa

Share:

Donald Trump aiwekea vikwazo China kufuatia sheria yake ya usalama Hong Kong

Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza kuweka vikwazo vipya dhidi ya China, akiituhumu tena kuhusika kwa maelfu ya vifo vilivyoptokana na ugonjwa hatari wa Covid-19.

Ametangaza pia kutokubaliana na sheria ya usalama wa China kwa Hong Kong ambayo imeendelea kuzusha wasiwasi mkubwa katika kimbo hilo linalojitawala.

Donald Trump ametekelza vitisho ambavyo amekuwa akitoa kwa siku kadhaa dhidi ya China.

Rais Trump amesema kuwa China imekiuka makubaliano ya uhuru wa Hong Kong kwa kupitisha sheria ya usalama wa Kitaifa. Nakala ambayo inaruhusu kurudi kwa vyombo vya usalama vya China kwa koloni la zamani la Uingereza na ambayo kwa wengi ni tishio kwa uhuru wa eneo hilo.

"Uchina inadai kulinda usalama wa kitaifa. Lakini ukweli ni kwamba Hong Kong ni eneo huru linalojitawala, lenye usalama na ambalolinaloendelea kuistawi kiuchumi na maendeleo mbalimbali. Uamuzi wa Beijing ni hatua ya kurudi nyuma. Uamuzi ambao unaimarisha uwepo wa China kwa mfumo wa usalama kwa eneo ambalo ni uhuru, "Rais wa Marekani amesema.

Uingereza, Japan, Canada, Australia na Marekani zimeelezea wasiwasi wao kuhusu sheria ya usalama wa China kwa Hong Kong. Uingereza imesema sheria hiyo inaweza kukandamiza mamlaka ya ndani ya Hong Kong.

Hisia mbalimbali zinazidi kutolewa kufuatia hatua ya bunge la China kuidhinisha mipango ya sheria tete ya usalama kwa Hong Kong. Waziri Mkuu wa China Li Keqiang amesema sheria hiyo mpya inalenga kuulinda mji wa Hong Kong, lakini Japan, Marekani, Canada, Australia na hata Marekani zimeikosoa hatua hiyo.

Katika taarifa ya nadra, punde tu baada ya sheria hiyo kupitishwa, wizara ya mambo ya nje ya Japan imeutaja mji wa Hong Kong kama mshirika muhimu zaidi. Yoshihide Suga ambaye ni waziri mwenye hadhi ya juu katika baraza la serikali la Japan amesema.


Share:

Kansela Angela Merkel akataa kuhudhuria mkutano wa G7 Marekani

Kansela Angela Merkel amekataa kuhudhuria mkutano wa kilele wa kundi la nchi 7 zenye uchumi wa juu zaidi duniani, G7, nchini Marekani mnamo mwezi Juni, kama ilivyopendekezwa na rais wa Marekani, Donald Trump.

Angela Merkel amesema hatohodhuria mkutano huo, kwa sababu ya janga la Corona, msemaji wa serikali ya Ujerumani amelithibitishia shirika la habari la AFP leo Jumamosi.

"Kwa leo, ukizingatia hali ya jumla ya janga la Corona, hawezi kukubali kusafari kwenda Washington," amesema msemaji wa serikali ya Ujerumani, akithibitisha habari ya chombo cha habari mtandaoni cha Politico kutoka Marekani.

"Ofisi ya kansela wa Ujerumani inamshukuru rais Trump kwa mwaliko wake kwenye mkutano wa G7," msemaji wa serikali ya Ujerumani ameongeza.

Bi Merkel, ndiye kiongozi wa kwanza wa kundi la G7 (Japan, Canada, Uingereza, Ufaransa, Ujerumani, Italia) kukataa rasmi mwaliko huu.

Umri wa Merkel, 65, ambaye pia ni sawa na ule wa Waziri Mkuu wa Japan Shinzo Abe, unamweka katika hatari kubwa ya kuambukizwa haraka janga la Covid-19.

Marekani ni nchi ya kwanza kuathirika zaidi duniani (zaidi ya watu 100,000 wamefariki dunia kwa Covid-19, huku watu Milioni 1.7 wakithibitishwa kuambukizwa virusi hivyo).

Ikulu ya White ilikuwa imetangaza mwanzoni mwa mwezi Machi kuwa inasitisha maandalizi ya mkutano huo, kwa sababu ya janga la Corona, kwa kuwaleta pamoja marais na viongozi wa serikali kutoka n-kundi la G7, ingependelea mkutano huo ufanyike kupitia video.

Lakini wiki iliyopita, Donald Trump alitangaza kwamba mkutano wa kilele wa kundi la G7 utafanyika mwezi wa Juni "katika Ikulu ya White House", ingawa kuna mikutano kadhaa ambayo inaweza kufanyika katika makazi ya rais ya Camp David, katika jimbo jirani la Maryland.


Share:

Baada ya vitisho, hatimaye Trump akata uhusiano na WHO

Rais Donald Trump wa Marekani ametangaza kukata uhusiano na Shirika la Afya Duniani WHO, akidai kuwa taasisi hiyo ya kimataifa ni kikaragosi cha China.

Katika kikao na waandishi wa habari katika Ikulu ya White House jana Ijumaa, Trump alirudia tuhuma zake dhidi ya shirika hilo akidai kwamba linaipendelea China, na eti lilishindwa kushughulikia ipasavyo janga la corona.

Aidha alitumia jukwaa hilo kuituhumu China kwa kusema Dunia inahitaji majibu kutoka kwa China juu ya virusi (vya corona)

Trump amechukua uamuzi huo chini ya wiki mbili baada ya kumuandikia barua Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Afya Dunia, Tedros Adhanom Gabrayesus ambapo alidai kuwa, "Marekani itaikatia misaada WHO kikamilifu iwapo haitapiga hatua kubwa za kujiboresha ndani ya siku 30 zijazo."


Share:

PICHA: Rais Magufuli akabidhi zawadi ya Ndege aina ya Tausi kwa Marais Wastaafu Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi Hati ya Makabidhiano ya zawadi ya Ndege aina ya Tausi 25 kwa Mama Maria Nyerere mjane wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kwa ajili ya kuwafuga katika Makazi yake, hafla hiyo fupi ilifanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi hati ya Makabidhiano ya ndege aina ya Tausi 25 kwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi kwa ajili ya kuwafuga katika makazi yake. Hafla ya Makabidhiano hayo imefanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi hati ya Makabidhiano ya ndege aina ya Tausi 25 kwa Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Benjamin Mkapa kwa ajili ya kuwafuga katika makazi yake. Hafla ya Makabidhiano hayo imefanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi hati ya Makabidhiano ya ndege aina ya Tausi 25 kwa Rais Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Kikwete kwa ajili ya kuwafuga katika makazi yake. Hafla ya Makabidhiano hayo imefanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi hao Wakuu wastaafu mara baada ya kuwakabidhi zawadi ya ndege aina ya Tausi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi, Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere pamoja na Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Benjamin Mkapa.

PICHA NA IKULU


Share:

Simbachawene: Serikali Ipo Katika Mchakato Kuhakikisha Mahabusu Nchini Wanafanya Kazi Magerezani Kama Wafungwa

Na Felix Mwagara, MOHA, Dar.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene amesema Serikali ipo katika mchakato wa kuhakikisha Mahabusu waliopo katika Magereza mbalimbali nchini wanaanza kufanya kazi kama ilivyokuwa kwa wafungwa.

Amesema mchakato huo ambao tayari umeanza, utakapo kamilika utaleta mapendekezo madhubuti ya jinsi gani ya kuwatumia mahabusu hao pamoja na wafungwa katika kufanya kazi za uzalishaji mali na kuhakikisha Jeshi hilo linajitegemea kikamilifu.

Akizungumza na Maafisa na Askari Magereza katika Magereza ya Segerea, Ukonga na Keko jijini Dar es Salaam, leo, kwa nyakati tofauti alipofanya ziara ya siku moja ya kusisitiza magereza yanajitegemea nchini, alisema ili binadamu ale lazima afanye kazi, na pia vitabu vitakatifu vinasisitiza hilo, hivyo mahabusu wanapaswa kufanya kazi kwa kuwa nao wanakula vyakula magerezani.

“Kuna mjadala mkubwa tunaendelea kuchakata kuhusu mahabusu waweze kufanya kazi, lakini lengo letu sio kuwafanyisha kazi za sulubu, au kazi zinazotweza utu wao, hapana, wao pamoja na wafungwa wana adhabu wanayoitumikia, tunataka kuwatumia katika kuzalisha, kwahiyo watafanya kazi kama watu wengine wanavyofanya kazi, hili naomba lieleweke,” alisema Simbachawene.

Aliongeza kuwa, “Mjadala unaendelea na tutakuja na majibu jinsi ya kuwatumia mahabusu na wafungwa, lakini tutakuja na majibu yenye mapendekezo tutashirikiana, lakini tunataka kuwatumia kwa nia njema ya kuzalisha, kama mnavyojua binadamu asipofanya kazi asile na imeandikwa katika vitabu vitakatifu, kama mtu umemfungia ndani alafu hafanyi kazi na anadai chakula na ajue kwamba asipofanya kazi hana haki ya kula, wewe umekuja ni mahabusu ili upeleke tonge hapa lazima uzalishe, huwezi kusema sifanyi kazi kwasababu ni mahabusu, hapana tutakulinda hata kwa bunduki utafanya kazi.”

Alisema lazima kuwepo na mtazamo mpana, mkubwa katika masuala ya kuzalisha na kujitegemea kwa Jeshi la Magereza, kwa ajili ya kuzalisha pamoja na kutatua matatizo mengine ndani ya Jeshi hilo ikiwemo kujenga nyumba, kulipa umeme pamoja na mahaitaji mbalimbali ya Jeshi hilo.

“Kama nilivyosema mjadala bado ni mkubwa kwa wafungwa na tunafahamu wapo chini ya Magereza, lakini hao wengine tumepewa tuwatunze wapo chini ya vyombo vingine, hivyo tunaendelea na mchakato wa kujadiliana kuhusu hilo, na ukikamilika tutawaletea majibu,” alisema Simbachawene.

Aliongeza kuwa, dhana ya Jeshi hilo kuzalisha na kujitegemea ni agizo la Amiri Jeshi Mkuu, Rais Dkt. John Magufuli kulitaka jeshi hilo kuzalisha kwa wingi ili kujitosheleza na kujitegemea.

Aidha, alilitaka Jeshi hilo kuhakikisha Magereza ya Mkoa wa Dar es Salaam yaanze kufanya kilimo cha mboga za majani na matunda pamoja na ubunifu wa uzalishaji mwingine katika mkoa huo, na magereza yaliyopo mikoani yaendelee na kilimo cha mpunga, mahindi, ufugaji pamoja na uzalishaji wa aina nyingine wanaoendelea nao katika maeneo yao.

Alisema kupitia uzalishaji mali huo utawezesha kupata fedha baada ya kuuza na kusaidia majukumu mengine ya Jeshi kuliko kutegemea fedha za matumizi mengine (OC) ambazo utolewa na Serikali kwa Jeshi hilo.

Pia Waziri Simbachawene amelitaka Jeshi hilo kuhakikisha wanahakiki mali zote za Jeshi ikiwemo mashamba yajulikane, na pia ijulikane yana hati au hayana, na mifugo ya Jeshi hilo ipo wapi na idadi yake ikiwa ni lengo la kutambua mali hizo na kuwekwa wazi kwasababu ni mali za umma.

Kwa upande wake Mkuu wa Magereza Mkoa wa Dar es Salaam, Kamishna Msaidizi wa Magereza (ACP), Solomon Urio, alimshukuru Waziri huyo kwa kufanya ziara katika Mkoa huo na kuwaomba viongozi mbalimbali nchini waweze kutembelea magereza ili waweze kujifunza na kujua kazi mbalimbali zinazofanywa na Jeshi mkoani humo.

“Tunakushukuru kwa kututembelea Mheshimiwa Waziri, na maelekezo uliyotaoa tutayafanyia kazi, na pia tunawaomba viongozi mbalimbali waweze kutembelea Magereza na kujua kazi mbalimbali tunazozifanya,” alisema ACP Urio.

Simbachawene amemaliza ziara yake ya siku moja kwa kutembelea magereza hayo, ambayo ni Gereza Kuu la Mahabusu Segerea, Gereza Kuu la Ukonga na Gereza la Mahabusu la Keko, ambapo katika ziara yake alipokua taarifa ya utendaji kazi kutoka kwa Wakuu wa Magereza hayo pamoja na kuahidi changamoto zao kufanyiwa.  


Share:

Picha : RAIS MAGUFULI AWAKABIDHI ZAWADI YA TAUSI MARAIS WASTAAFU WA TANZANIA




Ndege aina ya Tausi (Picha kutoka Maktaba)
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi Hati ya Makabidhiano ya zawadi ya Ndege aina ya Tausi 25 kwa Mama Maria Nyerere mjane wa Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere kwa ajili ya kuwafuga katika Makazi yake, hafla hiyo fupi ilifanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino Mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi hati ya Makabidhiano ya ndege aina ya Tausi 25 kwa Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi kwa ajili ya kuwafuga katika makazi yake. Hafla ya Makabidhiano hayo imefanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi hati ya Makabidhiano ya ndege aina ya Tausi 25 kwa Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Benjamin Mkapa kwa ajili ya kuwafuga katika makazi yake. Hafla ya Makabidhiano hayo imefanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimkabidhi hati ya Makabidhiano ya ndege aina ya Tausi 25 kwa Rais Mstaafu wa awamu ya nne Jakaya Kikwete kwa ajili ya kuwafuga katika makazi yake. Hafla ya Makabidhiano hayo imefanyika katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi hao Wakuu wastaafu mara baada ya kuwakabidhi zawadi ya ndege aina ya Tausi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza katika hafla hiyo fupi ya Makabidhiano ya zawadi ya ndege aina ya Tausi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimsikiliza Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete wakati akitoa neno la Shukrani kwa niaba ya Marais wenzake wastaafu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akifurahia jambo na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Dkt. Jakaya Kikwete mara baada ya hafla fupi ya Makabidhiano ya ndege aina ya Tausi katika Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwasili katika viwanja vya Ikulu ya Chamwino na Rais Mstaafu wa Awamu ya Pili Mzee Ali Hassan Mwinyi, Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere pamoja na Rais Mstaafu wa awamu ya Tatu Benjamin Mkapa. PICHA NA IKULU
Share:

FULL POWER , ZAT 50 NI SULUHISHO LA KUDUMU TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA UUME MDOGO



Sababu za upungufu wa nguvu za kiume na maumbile madogo ya uume


⇒Ngiri,

⇒Henia

⇒Kisukari

⇒Tumbo kujaa gesi

⇒Kutopata choo vizuri

⇒Utumiaji madawa kwa muda mrefu

⇒Unywaji wa pombe kupita kiasi

⇒Msongo wa mawazo 



⇮⇒Haya yote hupelekea mwili kutokuzalisha homoni ya gesrtogine au kuwa chache na kushindwa kupata mzunguko mzuri wa damu na vichocheo vingine kama madini ya zinki ambayo hukufanya kuwa na msisimko  na kufanya kuwa na muda  mrefu na nguvu za kutosha.



FULL POWER



⇨Ni dawa ya vidonge ya miti shamba inaongeza nguvu za kiume na kutibu kabisa tatizo hilo.



⇨Inaongeza hamu ya tendo la ndoa

⇨Inakufanya uchelewe kufika kileleni zaidi ya Dakika 30 na kurudia tendo zaidi ya mara nne na zaidi.


ZAT 50



⇨ Inarutubisha maumbile ya uume  na kunenepesha urefu nchi 6,unene sentimita 4


⇨Dawa hii ni ya kutibu kabisa tatizo hilo.

Pia tunatibu Magonjwa mengine Kama

Matatizo ya pumu,Bawasiri, vidonga vya tumbo,Kisukari,Magonjwa sugu ya zinaaa,Kaswende,U.T.I , kiuno,miguu kuwaka moto, Fangasi sehemu za Siri, kupunguza unene wa mwili,tumbo kuunguruma,kujaa gesi, matatizo ya uzazi kwa wanawake, kurutubisha mbegu za uzazi kwa akina baba, matatizo ya meno tunatibu bila kungoa

Kliniki yetu inapatikana Zanzibar, Dar es salaam na Shinyanga.

Wasiliana nasi kwa simu namba 071770 22 27
Share:

LIVE: Rais Magufuli Akiweka Jiwe La Msingi Ujenzi Ikulu Ya Chamwino

LIVE:  Rais Magufuli Akiweka Jiwe La Msingi Ujenzi Ikulu Ya Chamwino


Share:

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) Yatoa Bilioni 122.8

Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), imetoa Sh. bilioni 122.8 kwa vyuo na taasisi mbalimbali za elimu nchini kwa ajili ya ada, chakula na malazi ya wanafunzi wanaorejea vyuoni kuendelea na masomo Jumatatu.

Mkurugenzi wa HESLB, Abdul Razaq Badru, aliyasema hayo jana jijini Dodoma alipozungumza na waandishi wa habari.

Alibainisha kuwa, kati ya kiasi hicho, Sh. bilioni 63.7 ni kwa ajili ya chakula na malazi kwa wanafunzi 132,119 kupitia vyuo na taasisi za elimu 81 kwa kipindi cha miezi miwili kwanzia Juni Mosi hadi Julai 30, mwaka huu na kiasi kingine cha fedha ni malipo ya ada.

Alisema malipo ya robo ya nne ambayo ni ya mwisho kwa mwaka huu wa masomo, yatalipwa mwishoni mwa Julai mwaka huu.

Badru alisema kuwa katika kipindi cha wiki moja iliyopita kuanzia Mei 21 hadi Mei 29, mwaka huu, Sh. bilioni 59.1 zilipelekwa vyuoni kwa ajili ya ada za wanafunzi wanufaika ambazo zimelipwa kwa taasisi za elimu ya juu zaidi ya 70 nchini.

“Ni matumaini yetu kuwa fedha hizi zitavisaidia vyuo kutoa huduma bora kwa wateja wetu wapatao 132,119 waliopo katika taasisi za elimu mbalimbali nchini kote," alisema.

Vilevile, alisema tayari bodi imeshapeleka maofisa mikopo vyuoni kwa ajili ya kushughulikia mikopo ya wanafunzi.

Alisema wanafunzi wasiogope kurudi vyuoni kuendelea na masomo kwa sababu serikali imejipanga kwa kila kitu na kuwataka kuanza kuripoti kwa ajili ya kujisajili.

"Ninaomba wanafunzi wasiogope warudi shuleni, ili kuendelea na masomo kama ambavyo imetangazwa na serikali kuanzia Juni Mosi, mwaka huu," alisema.

Alisema usajili wa wanafunzi ulianza juzi na utaendelea hadi kesho, lakini watakaochelewa usajili utaendelea kufanyika Jumatatu.

Badru alisema Benki za biashara ziko tayari kwa ajili ya kusaidia mchakato wa malipo ya mikopo kwa wanafunzi wa vyuo.


Share:

Polisi Aliyemuua Kikatili Mmarekani Mweusi Ashitakiwa kwa Mauaji ya Bila Kukusudia

Afisa wa polisi anaetuhumiwa kwa mauaji ya kikatili ya  Mmarekani mweusi, George Floyd ametiwa mbaroni na kushtakiwa kwa kosa la mauaji   kufuatia kifo cha Raia huyo mweusi ambaye alimuua kwa kumkanyaga shingo na kumfanya akose pumzi

Hayo yanatokea katika kipindi ambacho mamlaka nchini  humo zimetangaza marufuku za kutotoka nje baada ya vurugu za maandamano ya siku tatu ambazo zimesababisha baadhi ya maeneo kuchomwa moto. 

Derek Chauvin, afisa wa polisi mzungu ambae alichukuliwa video, ikionesha kambana kwa kutumia goti shingoni, marehemu George Floyd kwa karibu dakika tisa, anashitakiwa kwa kusababisha kifo pasipo kukusudia


Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger