Wednesday 1 January 2020

Trump apandwa na hasira Baada Ya Waandamanaji Kuuvamia ubalozi wa Marekani nchini Iraq na Kutaka Kuuchoma Moto

Rais Donald Trump wa Marekani ameonyesha kuchukizwa na  maandamano makubwa mbele ya ubalozi wa nchi hiyo huko Baghdad, mji mkuu wa Iraq lakini hata hivyo akaishia kusema anaamini  Iraq itatumia vikosi vyake vya usalama kuulinda ubaloz huo wa Marekani

Kauli hiyo ameitoa wakati ambapo anailaumu Iran kwa kuchochea vurugu hizo dhidi ya eneo lake. 

Wananchi wa Iraq ambao ni wafuasi wa wapiganaji wanaoungwa mkono na Iran waliandamana kwenye ubalozi wa Marekani siku ya Jumanne huku wakiimba nyimbo zinazosema ''Kifo cha Marekani,'' wakirusha mawe, wakivunja kamera za usalama pamoja na kulichoma moto eneo la mapokezi, wakilaani mashambulizi ya anga yaliyofanywa na Marekani.

Mashambulizi hayo yaliyofanyika Jumapili iliyopita yaliwaua wapiganaji wapatao 25 wa kundi la wanamgambo wa Kataeb Hezbollah. 

''Tunatarajia Iraq itavitumia vikosi vyake kuulinda ubalozi na tumearifiwa hivyo,'' ameandika Trump katika ukurasa wake wa Twitter. Trump amesema Iran itawajibika kikamilifu kwa machafuko hayo.


Mashambulizi ya Marekani yalikuwa ni kujibu shambulizi la roketi lililofanywa wiki iliyopita na kumuua mkandarasi mmoja wa Kimarekani katika kituo cha jeshi la Iraq, ambalo ni la karibuni kufnayika lililenga maslahi ya Marekani nchini Iraq. 

Hakuna kundi lolote lililodai kuhusika na shambulizi hilo, lakini vikosi vya usalama vya Marekani vimelishutumu kundi la Kataeb Hezbollah.
 
Trump amesema Marekani imejibu vikali shambulizi ambalo limemuua mkandarasi huyo na skwamba siku zote itafanya hivyo. 

Uhusiano kati ya Marekani na Iran umekuwa ukizorota tangu Marekani ilivyojiondoa kwenye mkataba wa kihistoria wa nyuklia wa Iran mwaka 2018 na kuweka vikwazo vipya.

Hii ni mara ya kwanza katika kipindi cha miaka kadhaa kwa waandamanaji kufanikiwa kuufikia ubalozi wa Marekani mjini Baghdad, uliopo kwenye eneo lenye ulinzi mkali maarufu kama Green Zone. 

Vikosi vya usalama ndani ya ubalozi huo walifyatua mabomu ya kutoa machozi kuwatawanya waandamanaji nje ya ubalozi huo. Imeripotiwa kuwa zaidi ya watu 20,000 walikusanyika nje ya ubalozi huo.


Share:

Waandamanaji wa Iraq wavamia ubalozi wa Marekani mjini Baghdad

Waombolezaji nchini Iraq wamekusanyika nje ya ubalozi wa Marekani mjini Baghdad kulaani mashambulio ya ndege za Marekani yaliyolenga vituo vya wanamgambo wa Kishia.

Waombolezaji hao walizingira ubalozi huo uliopo kwenye eneo lenye ulinzi mkali wakiwa wamebeba bendera za kundi la wanamgambo lenye ushawishi mkubwa.

Wakati huo huo, Saudi Arabia imewalaani wanamgambo wanaoungwa mkono na Iran kwa kuyashambulia majeshi ya Marekani yaliyoko nchini Iraq ambapo mkandarasi mmoja wa Marekani aliuliwa.

Wanamgambo hao walifanya mashambulio hayo wiki iliyopita. Marekani ilijibu kwa kuwashambulia kwa ndege wanamgambo hao wa Kataib Hezbollah Jumapili iliyopita. 


Wanamgambo hao wa Hezbollah walikishambulia kituo cha kijeshi cha Marekani nchini Irak Ijumaa iliyopita.

Hata hivyo Waziri Mkuu wa Iraq, Adel Abdul Mahdi ameilaani pia Marekani kwa kufanya mashambilio ya ndege yaliyolenga vituo vya wanamgambo wanaoungwa mkono na Iran. 


Amesema hatua ya Marekani inaweza kuitumbukiza zaidi Iraq katika vita vya kiwakala baina ya Marekani na Iran.


Share:

Rais Magufuli awatakia Watanzania heri ya mwaka Mpya 2020

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amewatakia Watanzania wote heri ya Mwaka mpya wa 2020 na kuwaomba waendelee kudumisha amani na upendo ili uwe mwaka wa maendeleo na ustawi kwa Taifa.

Mhe. Rais Magufuli ametoa salamu hizo jana  wakati akiagana na Maafisa na Askari Wanyamapori na Hifadhi ya Misitu wa Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo ambako alitembelea na kujionea vivutio vya utalii pamoja na wananchi wa Nyabugera na Muganza aliowasalimu wakati akiwa njiani kurejea nyumbani kwake Chato Mkoani Geita.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amepokea salamu za heri ya Mwaka Mpya wa 2020 kutoka kwa wananchi, viongozi mbalimbali wakiwemo Marais Wastaafu, Maaskofu na Masheikh ambao wamempongeza kwa kazi nzuri ya kuongoza nchi kwa mafanikio makubwa na wamemuelezea matarajio yao ya kufanikiwa zaidi katika mwaka ujao.

“Mhe. Rais wangu, Dkt. Magufuli, Bwana Yesu Asifiwe. Ninakupa hongera sana kwa wajibu mzito ulionao. Kwa neema ya Mungu tumejaaliwa kufikia siku ya mwisho kwa mwaka huu wa 2019. Mimi nakupongeza kwa jitihada zako nyingi za kuleta maendeleo kwa nchi yetu. Ninakuombea na kukutakia Mwaka Mpya 2020 wa heri na mafanikio makubwa. Uso wa Bwana uende nawe popote utakapokuwa” amesema Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dkt. Frederick Shoo.

Kabla ya kuondoka katika Hifadhi ya Taifa ya Kisiwa cha Rubondo, Mhe. Rais Magufuli amemshukuru Kamishna wa Uhifadhi wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) Dkt. Allan Kijazi, Maafisa na Askari wote wa hifadhi hiyo kwa mapokezi mazuri na juhudi kubwa zilizowezesha hifadhi hiyo kuvutia na amewahakikishia kuwa pamoja na kutoa shilingi Bilioni 2 za ujenzi wa kivuko cha kwenda hifadhi ya Kisiwa cha Rubondo, Serikali itatoa shilingi Milioni 200 za kuboresha barabara za hifadhi hiyo.

Baada ya kuvuka ziwa Victoria kwa kivuko cha MV Chato, Mhe. Rais Magufuli amekutana na wananchi wa Kasenda na kuelezea kutoridhishwa kwake na ukusanyaji wa mapato ya soko la dagaa na samaki la Kasenda baada ya kuelezwa kuwa makusanyo ya mapato ya soko hilo ni shilingi laki 5 kwa siku licha kuwa soko kubwa namba 2 kwa kuuza dagaa katika ukanda wa Ziwa Victoria.

Mhe. Rais Magufuli amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Chato, kufuatilia ukusanyaji wa mapato katika soko hili na kuchukua hatua za kudhibiti mianya ya upotevu wa mapato itakayobainika ili Halmashauri ya Wilaya ya Chato iweze kupata fedha zitakazosaidia kutatua kero za wananchi ikiwemo kuboresha mazingira ya soko hilo na ujenzi wa shule ya sekondari ya Nyabugera ambayo amechangia shilingi Milioni 5.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato Bw. Eliud Mwaiteleke kutangaza zabuni ya ujenzi wa barabara ya Kasenda - Muganza yenye urefu wa kilometa 2.2 ili ijengwe kwa kiwango cha lami kama alivyoahidi, na kwamba Serikali itatoa fedha za ujenzi wa barabara hiyo.

Mhe. Rais Magufuli pia amewasalimu wananchi wa Muganza, ambapo amewapongeza kwa maendeleo yaliyopatikana katika eneo hilo na amewahakikishia kuwa Serikali itaendelea kudhibiti matumizi mabaya ya fedha za umma ili iendelee kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo yenye manufaa kwa wananchi.

“Nchi hii ilikuwa inaliwa sana na majizi na mpaka sasa bado wapo, namuomba Mwenyezi Mungu aendelee kunipa uhai ili katika mwaka 2020 niendelee kuwatumbua majizi wote na fedha tutakazopata tuzipeleke kwenye miradi ya maendeleo kama ambavyo tumenunua ndege 11, tunajenga reli (standard gauge), tunatoa elimu bure na mengine mengi” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Rais Magufuli pia amemuonya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato Bw. Eliud Mwaiteleke kwa matumizi mabaya ya fedha yanayofanywa na halmashauri hiyo na ametaka dosari hizo zirekebishwe mara moja. “Nataka ujirekebishe, wananchi hawa wanateseka sana” amesisitiza Mhe. Rais Magufuli.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Chato


Share:

WAZIRI KIGWANGALLA : KULETA KIBURI NA JEURI KWENYE MAZINGIRA HAYA NI UPUMBAVU


Baada ya Rais John Magufuli kuagiza Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla pamoja na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Prof. Adolf Mkenda kumaliza tofauti zao vinginevyo atawaondoa, Kigwangalla ameibuka na kudai kuwa tayari walishamaliza tofauti zao na sasa hali ni shwari.

Kupitia akaunti yake ya Twitter na Instagram  amesema walishafanya kikao na Katibu Mkuu, Prof. Adolf Mkenda cha kumaliza tofauti zao.

“Kazi ya Urais ni ngumu sana, tulioteuliwa na Rais kumsaidia utendaji/usimamizi wa maeneo mbalimbali hatupaswi kumuongezea frustrations nyingine zaidi, sisi kwenye Wizara yetu, baada ya kikao na Chief Secretary tulimaliza tofauti zilizokuwepo na sasa hali ni shwari,” amesema Kigwangalla.

Ni imani na heshima kubwa sana kwako kuteuliwa kuwa Waziri kwenye nchi yako. Kwenye nchi ya watu milioni 60, kwa nini Hamisi KIGWANGALLA? Sijui. Ni neema na baraka za Mungu tu. Maana siyo kila mtu kwenye maisha yake atapata fursa ya kuhudumu kwenye serikali kama Waziri ama kama Katibu Mkuu kwenye serikali. Siibezi wala siwezi kuichezea fursa hii adhimu.

Ni kwa kuelewa ukweli huu na ushauri, mwongozo na maelekezo ya wakuu wa kazi, na watendaji wazoefu kwenye utumishi wa umma, kama Katibu Mkuu Kiongozi, tulikaa mimi na Katibu Mkuu wangu na kukubaliana kufungua ukurasa mpya wa mahusiano mazuri zaidi kwa manufaa ya nchi yetu.

Kuondolewa kwenye nafasi ya Uwaziri unaweza kuondolewa kwa sababu mbalimbali lakini kuondolewa kwa sababu watu wazima, tena viongozi, ambao mmepewa fursa ya kushauriwa, mmeshindwa kuelewana, ni upumbavu! Mimi siyo mpumbavu.

Kuleta kiburi na jeuri kwenye mazingira Haya ni upumbavu. Kwanza sisi waislam tunafundishwa kuwa wanyenyekevu, maana ‘kiburi’ ni sifa ya Mungu, siyo yetu wanadamu. Kufanya kiburi na jeuri ni upumbavu. Hekima ya Mungu ni kujishusha na kumshinda shetani.

Sina jeuri wala kiburi sababu nimelelewa vizuri na bibi yangu Mama Bagaile, na pia naogopa hasira za Mungu. Tumalizie haya masaa kwa amani! Happy New Year Good People. Nitaendelea kutoa darasa la mambo niliyojifunza 2019, na mipango yangu ya 2020.

Nipo jimboni nachunga ng’ombe wangu kidogo. Ningekuwa Dar ningemtembelea Prof. Mkenda kwa ajili ya picha tukigonga glass ili mjue tuko sawa 😀. Mhe. Rais yeye ana namna yake ya kupata taarifa zetu. Atazipata tu! 😀. Limeisha hilo au niongeze volume? 🤷🏾‍♂️ Wakatabahu Dkt. Hamisi KIGWANGALLA, MB., MNEC, WMU.
 


Share:

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatano January 1, 2020





















Share:

Tuesday 31 December 2019

Picha : MBUNGE MASELE ACHANGIA MILIONI 9 KUSAIDIA UJENZI WA SOKO LA NDALA, ZAHANATI YA MWAWAZA NA MASEKELO

Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele amechangia shilingi milioni 9 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa soko la kata ya Ndala,ujenzi wa zahanati ya Mwawaza na Masekelo katika Manispaa ya Shinyanga.


Akizungumza leo Jumanne Desemba 31,2019 wakati wa akiendelea na ziara yake ya kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika jimbo lake la Shinyanga Mjini ,Mhe. Masele amesema fedha hizo zitasaidia kuchochea maendeleo kwa wananchi.

“Kupitia fedha za Mfuko wa Jimbo la Shinyanga Mjini,naahidi kuchangia shilingi milioni tano kwa ajili ya kusaidia kumalizia ujenzi wa soko la Ndala,lakini pia shilingi milioni mbili kwa ajili kusaidia ujenzi wa zahanati ya Mwawaza na shilingi milioni mbili kwa ajili ya ujenzi wa zahanati ya Masekelo”,amesema Masele.

Akiwa katika kata ya Mwawaza Masele ambaye pia ni Makamu wa Kwanza wa Rais wa Bunge la Afrika (PAP),amesema serikali inaendelea kutekeleza miradi miradi mbalimbali ikiwemo ya barabara na maji ambapo tayari jumla ya shilingi milioni 400 zimeshapelekwa katika Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mjini Shinyanga (SHUWASA) kwa ajili ya kupeleka maji Mwawaza.

Katika hatua nyingine,Masele amewahimiza wakazi wa Mwawaza kulinda ardhi yao kwa kupima mashamba yao katika mfumo wa viwanja na kutunza hati za ardhi kwani ardhi ina thamani kubwa.

“Mji wa Shinyanga unapanuka,hapa Mwawaza imejengwa hospitali ya mkoa wa Shinyanga,naomba mpime ardhi yenu,mpate hati na siku mkiamua kuuza basi muuze kwa ridhaa yenu,sitaki kusikia mtu anawadhulumu ardhi yenu kwani kwenye baadhi ya maeneo kwenye jimbo nilihangaika kutatua migogoro ya ardhi kutokana na maeneo kutokuwa katika mpangilio mzuri”,ameeleza Masele.

Mhe. Masele akiwa ameambatana na Wajumbe wa kamati wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Shinyanga mjini,leo Desemba 31,2019 ametembelea kata tatu ambazo ni Mwawaza,Masekelo na Ndala.

ANGALIA PICHA HAPA CHINI
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele akizungumza katika kata ya Mwawaza leo Desemba 31,2019 na kuahidi kuchangia shilingi milioni mbili kusaidia ujenzi wa zahanati ya Mwawaza wakati akiendelea na ziara yake kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo katika jimbo lake la Shinyanga Mjini. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele akielezea mikakati mbalimbali inayofanywa na serikali kuwaletea maendeleo wananchi huku akiwaahidi wananchi wa Mwawaza kuwa huduma ya maji kutoka Ziwa Victoria imeanza kutekelezwa kwani tayari serikali imetoa shilingi milioni 400 ili kuwapatia huduma ya maji wananchi wa Mwawaza.
Wajumbe wa halmashauri wa Chama Cha Mapinduzi CCM kata ya Mwawaza wakiwa katika kikao na Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Masele.
Wajumbe wa halmashauri wa Chama Cha Mapinduzi CCM kata ya Mwawaza wakiwa katika kikao na Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Masele.
Katibu Msaidizi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Shinyanga mjini Rashid Mnunduma akizungumza wakati wa ziara ya Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele katika kata ya Mwawaza.
Diwani wa kata ya Mwawaza Juma Nkwabi akizungumza wakati wa ziara ya Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele.
Mwenyekiti wa CCM kata ya Mwawaza Dotto Mamboleo akisoma taarifa fupi ya Chama na serikali kata ya Mwawaza ambapo alizitaja changamoto wanazokabiliana nazo kuwa ni umeme,maji,barabara na zahanati.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele akizungumza katika kata ya Ndala leo Desemba 31,2019 na kuahidi kuchangia shilingi milioni tano kusaidia kukamilisha ujenzi wa soko la Ndala.Kulia ni Katibu Msaidizi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Shinyanga mjini Rashid Mnunduma,kushoto ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) wilaya ya Shinyanga Mjini Dotto Joshua. 
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM (UVCCM) wilaya ya Shinyanga Mjini Dotto Joshua akizungumza wakati wa ziara ya Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele katika kata ya Ndala.
Mwenyekiti wa UWT wilaya ya Shinyanga Mjini Shumbuu Katambi akizungumza wakati wa ziara ya Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele.
Afisa Mtendaji wa kata ya Ndala Lucas Magandula akisoma taarifa ya utekelezaji wa miradi mbalimbali katika kata ya Masekelo.
Wajumbe wa halmashauri wa Chama Cha Mapinduzi CCM kata ya Ndala wakiwa katika kikao na Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Masele.
Wajumbe wa halmashauri wa Chama Cha Mapinduzi CCM kata ya Ndala wakiwa katika kikao na Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Masele.
Soko la Ndala ambalo ujenzi wake bado haujakamilika ambapo Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele ameahidi kuchangia shilingi milioni 5 ili kukamilisha ujenzi huo.
Mwenyekiti wa CCM kata ya Ndala Rashid Mahene akizungumza wakati wa ziara ya Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele akizungumza na Wajumbe wa halmashauri wa Chama Cha Mapinduzi CCM kata ya Masekelo.
Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele akizungumza na Wajumbe wa halmashauri wa Chama Cha Mapinduzi CCM kata ya Masekelo ambapo aliahidi kuchangia shilingi milioni mbili kusaidia ujenzi wa zahanati ya Masekelo.
Katibu Msaidizi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Shinyanga mjini Rashid Mnunduma akizungumza wakati wa ziara ya Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele katika kata ya Masekelo.
Katibu wa CCM kata ya Masekelo Peter John akisoma taarifa ya utekelezaji wa ilani ya CCM katika kata ya Masekelo.
Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi CCM wilaya ya Shinyanga Mjini Esha Stima akizungumza wakati wa ziara ya Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele.
Katibu wa Mbunge Jimbo la Shinyanga Mjini Mwajuma Radhia akizungumza wakati wa ziara ya Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele.
Mwenyekiti wa CCM kata ya Masekelo Rashida Mahega akizungumza wakati wa ziara ya Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Julius Masele.
Wajumbe wa halmashauri wa Chama Cha Mapinduzi CCM kata ya Masekelo wakiwa katika kikao na Mbunge wa Jimbo la Shinyanga Mjini Mhe. Stephen Masele.
Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Share:

Yanga yamsimamisha Kaimu Meneja wao Dismas Ten




Share:
Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

Popular Posts

Unordered List

Pages

Blog Archive


Copyright © MASWAYETU BLOG | Powered by Blogger